Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,977
- Thread starter
- #61
Sehemu ya 11
“Fanyeni hata penzi la siri nina imani litakusaidia katika maisha yako.”
“Mmh! Nitajaribu kwa vile umeivunja ngome ya moyo wangu sina budi kukubaliana na wewe,” nilijikuta nikilegeza msimamo.
“Tena nakuomba mdogo wangu usiipoteze bahati hii. Hebu angalia jinsi Mungu alivyosikia kilio chako baada ya kukimbiwa na Beka.
“Tena amekwambia humpi mwili wako mpaka akamilishe alichokuahidi, Mungu akupe nini? Waache dada zako watakuja kuuanika wakati jua limekuchwa na kuutwanga mbichi.”
“Nilikuwa nawazo la kumshirikisha mama suala hili,” nilimweleza wazo langu la awali.
“Mwaija utaharibu kila kitu, kama una wasiwasi wa kugombana na ndugu zako mbebee mimba ule maisha. Tena mtoto anazaliwa akiwa na uhakika wa maisha yake tayari.
“Mwaija mizee kama hii ndiyo inatafutwa mjini, hela zao hazina chenji. Mdogo wangu kwangu mimi hata angekuwa mpenzi wa mama yangu mzazi, kama angenitangazia bingo kama hiyo nisingelaza damu.”
“Naweza kumkubalia lakini sijui kama yupo sawa?”
“Kivipi?”
“Kiafya, si unajua dada yangu mwingi wa habari, tusije chuma janga tulile wenyewe.”
“Mmh! Kweli hilo umenena mdogo wangu.”
“Kwa hilo utanisaidiaje?”
“Usimpe mwili wako labda mtumie kondomu.”
“Tukitumia kondomu mtoto tutampaje?”
“Sikiliza mdogo wangu hilo kwa sasa achana nalo, akiisha kutimizia kila kitu kwa jina lako. Sharti lako kubwa ili umpe mwili wako mwende kwanza mkapime.”
“Mmh! Dada nimekueleza itabidi nifanye hivyo.”
“Na majibu yake usiyacheleweshe ili asibadili uamuzi, si unajua wanawake tupo wengi wote tunataka hichohicho.”
“Nashukuru dada yangu kwa ushauri wako.”
Baada ya mazungumzo nilimpigia simu bwana wa dada kuwa nimemaliza kilichonichelewesha naye alinieleza atafika muda si mrefu.
Baada ya robo saa alifika kunichukua, kwa vile da Suzy alikuwa akikaa njiani kwenda kwetu, tuliondoka naye na kumteremshia njiani.
Baada ya kumteremsha da Suzy, tulibakia wawili kwenye gari, tulikwenda mwendo mfupi bwana wa dada alinisemesha akiwa ameangalia mbele.
“Mwaija za kazi?”
“Nzuri shemeji, shikamoo.”
“Marahaba, sasa wewe wasiwasi wako nini?” aliniuliza swali bila kunitazama.
“Wasiwasi! Wa nini?”
“Naona umeishaanza kuniogopa, nimekueleza lile ni ombi wala haliingiliani na mambo mengine.”
“Nikuogope kivipi?” sikumuelewa.
“Najua huniamini na kuona natumia turufu ya kukusaidia ili niweze kufanikisha mambo yangu. Lakini sivyo hivyo sina nia mbaya na wewe. Ningeweza kumpa mtu yoyote fedha niliyonayo lakini naamini kwako haitapotea.”
“Uliyosema nimekuelewa lakini sikuwa na maana hiyo. Nilikuwa na mazungumzo kidogo na da Suzy, nikaona nitakuchelewesha.”
“Niliyeamua kukuleta kazini na kukurudisha ni mimi wala sikulazimishwa na mtu.”
“Sawa, lakini kunipitia si adhabu, kama kuna dharura lazima tuambiane.”
“Nimekuelewa, ila nilipata wasiwasi, jana kuzungumza leo upatwe na dharura.”
“Walaa, wasiwasi wako siku zote wanadamu si wapangaji bali kila kitu hupanga wenyewe.”
“Ni kweli, vipi mzigo uliuona?”
“Ooh! Samahani kwa kuchelewa kushukuru, asante sana shemeji yangu,” nilijikuta nikiona aibu ya kuchelewa kutanguliza shukurani mapema.
“Usihofu ni kawaida, nia yangu siku moja uishi maisha kulingana na heshima yako.”
Nilijikuta nikipata kugugumizi cha kumpa jibu kuwa nimekubali, nilitaka mwenyewe kwanza aniulize kuliko kukurupuka.
Kwa vile tulikuwa tumekaribia maeneo ya nyumbani, nilishangaa siku ile kusimamisha gari mbali kidogo na nyumbani na kunigeukia kisha aliniita jina langu.
“Mwaija?”
“Abee.”
“Vipi, nina imani umepata muda wa kufikiria.”
“Nini?” nilijifanya sijui.
“Au basi,” shemeji naye alipindisha swali lake.
“Shemeji,” nilimwita huku nikimtazama usoni.
“Naam.”
”Wewe na dada mpoje?” nilimtupia swali.
“Kwa nini unauliza hivyo?”
“Jibu swali si sikuuliza swali.”
“Mwaija mbona hilo tulishalizungumza toka jana?”
“Sina maana ya unayofikiria ila jibu nililokuuliza.”
“Tulikuwa wapenzi.”
” Mlikuwa wapenzi, sasa hivi?”
“Si wapenzi tena.”
“Hilo halinihusu.”
“Ulikuwa unasemaje?”
“Nina imani tabia za dada unazijua vizuri?”
“Tabia zipi?”
“Za kutokuwa na mwanaume mmoja.”
“Ndiyo.”
“Nina imani katika starehe zenu kuna kipindi hamkutumia kinga.”
“Sina kumbukumbu hiyo, lakini sijawahi kukutana naye bila kinga.”
“Basi kupata uhakika tukapime.”
“Ili?”
“We si unataka kuzaa na mimi.”
“Mwaija mi nipo sawa mbona!”
“Sijakataa, ila muhimu tukapime, hata mimi najijua nipo sawa. Lakini kwa uhakika zaidi tukapime pamoja,” nilimwambia nami nipo tayari ili kumtoa hofu.
“Mmh! Sawa.”
“Mbona kama nakulazimisha?”
“Walaa nipo tayari.”
“Kwa hiyo tutakwenda lini?” nilimuuliza kumsikiliza.
“Siku yoyote utakayotaka.”
“Kesho ukinipitia wakati wa kutoka kazini.”
“Hakuna tatizo, Mwaija ila leo nitakushushia hapa sifiki kwenu.”
Ajabu siku ile mzee Sambi hakutaka kufika nyumbani kitu kilichonishtua sana.
“Vipi mbona leo hufiki nyumbani?”
“Sitakiwi.”
“Na nani?”
“Na dada yako.”
“Hutakiwi una maanisha nini?”
“Dada yako hataki nifike kwenu.”
“Kwa sababu gani?”
“Anasema yeye si mke wangu hivyo anahitaji uhuru.”
“Mmh! Sasa itakuwaje?”
“Kila kitu nimekihamishia kwako." "Tokea lini umekatazwa na dada kufika nyumbani?" "Leo inatimia wiki?" "Wiki! Muongo!”
“Kweli kabisa.”
“Mbona kila siku ulikuwa ukifika nyumbani?" "Sababu nilikuwa nakurudisha nyumbani pia nilizungumza na mama na dada yako mdogo." "Kwa hiyo itakuwaje?" "Basi tena, kama utakuwa tayari kuwa na mimi sitafika tena kwenu, tutajua tukutane wapi?”
“Tukutane wapi ili iweje?” nilishindwa kumuelewa tukutane ili iwe nini.
“Si kama unavyofikiri, nia kubwa kukutana baada ya kazi na kuzungumza kisha unarudi nyumbani kwenu.”
“Makubaliano yetu mpaka unipatie tulivyokubaliana na pia kwenda kupima, sasa habari hiyo inakuwaje?” pamoja na kuonesha dalili za kukubali lakini sikutaka kujirahisi.
“Kupima tunakwenda kesho, kwa vile nimekuahidi lazima nitafute kiwanja nikununulie na kuanzisha ujenzi.”
“Mmh! Hiyo si itakuwa kazi ya mwaka mzima?”
“Hapana ni ya miezi miwili, nilichokuwa nasubiri jibu lako tu.”
“Mi nimekubali.”
“Basi kila kitu niachie mimi, ungependa wiki hii uanze kuendesha gari lako?”
“Hapana nimalizie kwanza nyumba.”
“Basi Mwaija ndani ya miezi miwili utakuwa ndani ya nyumba yako.”
“Basi nikuache uwahi nyumbani.”
Niliagana na mzee Sambi aliyenipa elfu hamsini ya kupandia Bajaj japokuwa nyumbani hapakuwa mbali. Sikutaka kukodi Bajaj nilichepua kwa mguu hadi nyumbani.
Nilipofika dada alishtuka na kuniuliza:
“Vipi shemeji yako ndiyo kasusa?”
“Kwani vipi?”
“Achana naye kapewa lifti anataka kupiga mpaka honi.”
“Una maana gani?”
“Kumpa penzi mara moja kanigeuza mkewe, ooh! Nataka kukuoa ooh, nataka kuzaa na wewe nani kamwambia mi kiwanda cha kutotolea watoto.”
“Lakini dada yule jamaa ana fedha zake kwa nini usimkubalie.”
“Mwaija nawe msichana kama mimi hujapungukiwa kitu. We si mtu wa kuolewa mkubalie.”
“Dada nikimkubalia si utakasirika.”
“Mwaija nikasirike ili iweje?”
“Si tutakuwa tumechangia mwanaume mmoja.”
“Angekuwa mume wangu hapo kidogo afadhali, lakini mpita njia, wee kama katuma maombi mkubalie maisha yenyewe yapo wapi,” dada alisema kama alikuwa akijua nini kinaendelea.
“Mmh! Basi acha nikapumzike.”
“Haya mdogo wangu, kama katia timu kazi kwako hela zinamuwasha.”
“Dada baadaye basi.”
“Haya mdogo wangu.”
Niliagana na dada na kwenda chumbani kwangu kubadili nguo ili niende nikaoge. Baada ya kuoga na kula nilijilaza chali kama kawaida yangu mikono niliweka kichwani. Nilijikuta nikipata wazo la kumweleza dada kuwa mzee Sambi ananitaka kimapenzi.
Niliamini kutokana na maneno yake hawezi kushtuka lakini kwa upande wangu niliona ni mapema sana kumwambia jambo lile ambalo bado lilikuwa halijakamilika. Nilijiuliza nini hatima ya maisha yangu kama nitakuwa na mzee Sambi mwanaume mwenye mke.
Niliamua kufanya kwanza siri mpaka kila kitu kitakapokuwa wazi, kwa vile nilikuwa nimechoka na kazi usingizi haukuchelewa kunichukua.
***
“Fanyeni hata penzi la siri nina imani litakusaidia katika maisha yako.”
“Mmh! Nitajaribu kwa vile umeivunja ngome ya moyo wangu sina budi kukubaliana na wewe,” nilijikuta nikilegeza msimamo.
“Tena nakuomba mdogo wangu usiipoteze bahati hii. Hebu angalia jinsi Mungu alivyosikia kilio chako baada ya kukimbiwa na Beka.
“Tena amekwambia humpi mwili wako mpaka akamilishe alichokuahidi, Mungu akupe nini? Waache dada zako watakuja kuuanika wakati jua limekuchwa na kuutwanga mbichi.”
“Nilikuwa nawazo la kumshirikisha mama suala hili,” nilimweleza wazo langu la awali.
“Mwaija utaharibu kila kitu, kama una wasiwasi wa kugombana na ndugu zako mbebee mimba ule maisha. Tena mtoto anazaliwa akiwa na uhakika wa maisha yake tayari.
“Mwaija mizee kama hii ndiyo inatafutwa mjini, hela zao hazina chenji. Mdogo wangu kwangu mimi hata angekuwa mpenzi wa mama yangu mzazi, kama angenitangazia bingo kama hiyo nisingelaza damu.”
“Naweza kumkubalia lakini sijui kama yupo sawa?”
“Kivipi?”
“Kiafya, si unajua dada yangu mwingi wa habari, tusije chuma janga tulile wenyewe.”
“Mmh! Kweli hilo umenena mdogo wangu.”
“Kwa hilo utanisaidiaje?”
“Usimpe mwili wako labda mtumie kondomu.”
“Tukitumia kondomu mtoto tutampaje?”
“Sikiliza mdogo wangu hilo kwa sasa achana nalo, akiisha kutimizia kila kitu kwa jina lako. Sharti lako kubwa ili umpe mwili wako mwende kwanza mkapime.”
“Mmh! Dada nimekueleza itabidi nifanye hivyo.”
“Na majibu yake usiyacheleweshe ili asibadili uamuzi, si unajua wanawake tupo wengi wote tunataka hichohicho.”
“Nashukuru dada yangu kwa ushauri wako.”
Baada ya mazungumzo nilimpigia simu bwana wa dada kuwa nimemaliza kilichonichelewesha naye alinieleza atafika muda si mrefu.
Baada ya robo saa alifika kunichukua, kwa vile da Suzy alikuwa akikaa njiani kwenda kwetu, tuliondoka naye na kumteremshia njiani.
Baada ya kumteremsha da Suzy, tulibakia wawili kwenye gari, tulikwenda mwendo mfupi bwana wa dada alinisemesha akiwa ameangalia mbele.
“Mwaija za kazi?”
“Nzuri shemeji, shikamoo.”
“Marahaba, sasa wewe wasiwasi wako nini?” aliniuliza swali bila kunitazama.
“Wasiwasi! Wa nini?”
“Naona umeishaanza kuniogopa, nimekueleza lile ni ombi wala haliingiliani na mambo mengine.”
“Nikuogope kivipi?” sikumuelewa.
“Najua huniamini na kuona natumia turufu ya kukusaidia ili niweze kufanikisha mambo yangu. Lakini sivyo hivyo sina nia mbaya na wewe. Ningeweza kumpa mtu yoyote fedha niliyonayo lakini naamini kwako haitapotea.”
“Uliyosema nimekuelewa lakini sikuwa na maana hiyo. Nilikuwa na mazungumzo kidogo na da Suzy, nikaona nitakuchelewesha.”
“Niliyeamua kukuleta kazini na kukurudisha ni mimi wala sikulazimishwa na mtu.”
“Sawa, lakini kunipitia si adhabu, kama kuna dharura lazima tuambiane.”
“Nimekuelewa, ila nilipata wasiwasi, jana kuzungumza leo upatwe na dharura.”
“Walaa, wasiwasi wako siku zote wanadamu si wapangaji bali kila kitu hupanga wenyewe.”
“Ni kweli, vipi mzigo uliuona?”
“Ooh! Samahani kwa kuchelewa kushukuru, asante sana shemeji yangu,” nilijikuta nikiona aibu ya kuchelewa kutanguliza shukurani mapema.
“Usihofu ni kawaida, nia yangu siku moja uishi maisha kulingana na heshima yako.”
Nilijikuta nikipata kugugumizi cha kumpa jibu kuwa nimekubali, nilitaka mwenyewe kwanza aniulize kuliko kukurupuka.
Kwa vile tulikuwa tumekaribia maeneo ya nyumbani, nilishangaa siku ile kusimamisha gari mbali kidogo na nyumbani na kunigeukia kisha aliniita jina langu.
“Mwaija?”
“Abee.”
“Vipi, nina imani umepata muda wa kufikiria.”
“Nini?” nilijifanya sijui.
“Au basi,” shemeji naye alipindisha swali lake.
“Shemeji,” nilimwita huku nikimtazama usoni.
“Naam.”
”Wewe na dada mpoje?” nilimtupia swali.
“Kwa nini unauliza hivyo?”
“Jibu swali si sikuuliza swali.”
“Mwaija mbona hilo tulishalizungumza toka jana?”
“Sina maana ya unayofikiria ila jibu nililokuuliza.”
“Tulikuwa wapenzi.”
” Mlikuwa wapenzi, sasa hivi?”
“Si wapenzi tena.”
“Hilo halinihusu.”
“Ulikuwa unasemaje?”
“Nina imani tabia za dada unazijua vizuri?”
“Tabia zipi?”
“Za kutokuwa na mwanaume mmoja.”
“Ndiyo.”
“Nina imani katika starehe zenu kuna kipindi hamkutumia kinga.”
“Sina kumbukumbu hiyo, lakini sijawahi kukutana naye bila kinga.”
“Basi kupata uhakika tukapime.”
“Ili?”
“We si unataka kuzaa na mimi.”
“Mwaija mi nipo sawa mbona!”
“Sijakataa, ila muhimu tukapime, hata mimi najijua nipo sawa. Lakini kwa uhakika zaidi tukapime pamoja,” nilimwambia nami nipo tayari ili kumtoa hofu.
“Mmh! Sawa.”
“Mbona kama nakulazimisha?”
“Walaa nipo tayari.”
“Kwa hiyo tutakwenda lini?” nilimuuliza kumsikiliza.
“Siku yoyote utakayotaka.”
“Kesho ukinipitia wakati wa kutoka kazini.”
“Hakuna tatizo, Mwaija ila leo nitakushushia hapa sifiki kwenu.”
Ajabu siku ile mzee Sambi hakutaka kufika nyumbani kitu kilichonishtua sana.
“Vipi mbona leo hufiki nyumbani?”
“Sitakiwi.”
“Na nani?”
“Na dada yako.”
“Hutakiwi una maanisha nini?”
“Dada yako hataki nifike kwenu.”
“Kwa sababu gani?”
“Anasema yeye si mke wangu hivyo anahitaji uhuru.”
“Mmh! Sasa itakuwaje?”
“Kila kitu nimekihamishia kwako." "Tokea lini umekatazwa na dada kufika nyumbani?" "Leo inatimia wiki?" "Wiki! Muongo!”
“Kweli kabisa.”
“Mbona kila siku ulikuwa ukifika nyumbani?" "Sababu nilikuwa nakurudisha nyumbani pia nilizungumza na mama na dada yako mdogo." "Kwa hiyo itakuwaje?" "Basi tena, kama utakuwa tayari kuwa na mimi sitafika tena kwenu, tutajua tukutane wapi?”
“Tukutane wapi ili iweje?” nilishindwa kumuelewa tukutane ili iwe nini.
“Si kama unavyofikiri, nia kubwa kukutana baada ya kazi na kuzungumza kisha unarudi nyumbani kwenu.”
“Makubaliano yetu mpaka unipatie tulivyokubaliana na pia kwenda kupima, sasa habari hiyo inakuwaje?” pamoja na kuonesha dalili za kukubali lakini sikutaka kujirahisi.
“Kupima tunakwenda kesho, kwa vile nimekuahidi lazima nitafute kiwanja nikununulie na kuanzisha ujenzi.”
“Mmh! Hiyo si itakuwa kazi ya mwaka mzima?”
“Hapana ni ya miezi miwili, nilichokuwa nasubiri jibu lako tu.”
“Mi nimekubali.”
“Basi kila kitu niachie mimi, ungependa wiki hii uanze kuendesha gari lako?”
“Hapana nimalizie kwanza nyumba.”
“Basi Mwaija ndani ya miezi miwili utakuwa ndani ya nyumba yako.”
“Basi nikuache uwahi nyumbani.”
Niliagana na mzee Sambi aliyenipa elfu hamsini ya kupandia Bajaj japokuwa nyumbani hapakuwa mbali. Sikutaka kukodi Bajaj nilichepua kwa mguu hadi nyumbani.
Nilipofika dada alishtuka na kuniuliza:
“Vipi shemeji yako ndiyo kasusa?”
“Kwani vipi?”
“Achana naye kapewa lifti anataka kupiga mpaka honi.”
“Una maana gani?”
“Kumpa penzi mara moja kanigeuza mkewe, ooh! Nataka kukuoa ooh, nataka kuzaa na wewe nani kamwambia mi kiwanda cha kutotolea watoto.”
“Lakini dada yule jamaa ana fedha zake kwa nini usimkubalie.”
“Mwaija nawe msichana kama mimi hujapungukiwa kitu. We si mtu wa kuolewa mkubalie.”
“Dada nikimkubalia si utakasirika.”
“Mwaija nikasirike ili iweje?”
“Si tutakuwa tumechangia mwanaume mmoja.”
“Angekuwa mume wangu hapo kidogo afadhali, lakini mpita njia, wee kama katuma maombi mkubalie maisha yenyewe yapo wapi,” dada alisema kama alikuwa akijua nini kinaendelea.
“Mmh! Basi acha nikapumzike.”
“Haya mdogo wangu, kama katia timu kazi kwako hela zinamuwasha.”
“Dada baadaye basi.”
“Haya mdogo wangu.”
Niliagana na dada na kwenda chumbani kwangu kubadili nguo ili niende nikaoge. Baada ya kuoga na kula nilijilaza chali kama kawaida yangu mikono niliweka kichwani. Nilijikuta nikipata wazo la kumweleza dada kuwa mzee Sambi ananitaka kimapenzi.
Niliamini kutokana na maneno yake hawezi kushtuka lakini kwa upande wangu niliona ni mapema sana kumwambia jambo lile ambalo bado lilikuwa halijakamilika. Nilijiuliza nini hatima ya maisha yangu kama nitakuwa na mzee Sambi mwanaume mwenye mke.
Niliamua kufanya kwanza siri mpaka kila kitu kitakapokuwa wazi, kwa vile nilikuwa nimechoka na kazi usingizi haukuchelewa kunichukua.
***


Manfongo style