Simulizi: Mwanafunzi Mchawi (A Wizard Student)

Simulizi: Mwanafunzi Mchawi (A Wizard Student)

SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO

..DORICE alimshangaa Mumewe Mansoor kwa maneno yake. Machozi yalimlengalenga machoni mwake kisha akajiondoa kifuani kwa Mansoor na kujitenga kando.
"Vipi mke wangu?"
"Najuta Mansoor.. Najuta sana kukukubalia, sikujua kama hautakuwa mwaminifu kwa ahadi zako!" Alisema Dorice kwa hasira.

"Sina maana mbaya mke wangu mpenzi.. Usinielewe vibaya tafadhali...Nakupenda sana!"
"Unanipenda? Unanipenda nini uongo mtupu..!" Alisema Dorice kwa hasira huku machozi yakimshuka mashavuni mwake. Alijikuta anamchukia Mansoor kupita kiasi. Hakutaka hata kumsogelea karibu.
"Baby! Nimekuelewa basi naomba uwe na amani moyoni mwako" alisema Mansoor huku akimsogelea Dorice na kutaka kumkumbatia lakini Dorice alimsukumia kando Mansoor na kuongeza kilio chake.
"Sitaki uniguse mpaka utakaponiambia ni lini utatimiza ahadi yako"

"Baada ya wiki moja nitaitimiza ahadi yako..!" Alisema Mansoor kwa huzuni kwani alijua ni kiasi gani Dorice alimpenda Eddy na alijua kwamba endapo angemrudisha Dorice duniani basi angemsahau Yeye na kuponda raha na Eddy. Kila alipofikiria hilo Mansoor aliumia sana moyoni mwake. Hakutamani kumkosa Dorice lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kutunza uaminifu wa kutimiza ahadi yake.
"Una uhakika utanipeleka baada ya wiki moja?" Aliuliza Dorice akimtazama Mansoor.

"Ndio.. Usijali!" Mansoor alijibu kwa unyonge sana.
"Hapo umenifurahisha!" Alisema Dorice na kumkumbatia Mansoor.
"Lakini kabla haujaenda huko kuna kitu muhimu unatakiwa ufanye!" Alisema Mansoor akiwa bado amemkumbatia Doreen.
"Kitu gani?" Aliuliza Dorice.
Mansoor alimuachia Dorice kisha akanyoosha mkono wake na kumuonesha Dorice kiganja cha mkono wake. Kwa mshangao kidogo, Dorice akatazama kiganja cha Mansoor.
"Unaona nini hapa?"
"Sioni kitu.."
"Huoni kitu? Hebu tazama vizuri"
"Naona Pete" alijibu Dorice kwa mshangao.

*********
Eddy alimtazama kwa mshangao mlinzi wao. Alimkazia macho huku akimwomba msamaha kwa kumjibu vibaya hapo mwanzo.
"Usijali.. Najua matatizo yako yanakufanya uwe hivyo" alisema mlinzi.
"Sasa utanisaidiaje? Maana nateseka sana!"
"Nitakusaidia tu wala usiwe na haraka... "
"Lazima niwe na haraka Anko maana mpaka sasa hivi sijawahi hata kukojoa!"

"Mmh! Haraka zilimponza chura zikafanya awe na mabaka. Vuta subira tu maana umefanyiwa mchezo mbaya sana." Alisema mlinzi yule huku akijifunika vyema shuka lake na kujigesha ukutani ili amalizie usingizi wake. Lakini ghafla akapigwa Kofi zito shavuni, aliruka kama kuku aliyeona hatari. Kabla hajakaa sawa Kofi lingine zito lilitua shavuni kwake, akajishika shavu na kutazama kama alikuwa amechanika lakini haikuwa hivyo kwani hakukuwa na damu yoyote ile.

Mlinzi yule akatazama huku na kule lakini hakuona Mtu aliyempiga makofi Yale mazito yaliyotua shavuni kama radi wakati wa mvya Kali.
"Vipi Anko?"
"Ah.. Hanna kitu.. Niko sawa tu.."
"Mbona umeruka sana?"
"Usijali Eddy.. Mimi nimeaga kwetu Musoma.. Niliwaaga wajita wenzangu..!" Alisema Mlinzi huku akisikilizia maumivu makali ya vibao alivyopigwa.
"Sikuelewi Anko ."
"Nimeaga.. Hakuna wa kunichezea!" Alizidi kuropoka mlinzi yule kisha akatulia kimya. Mawazo tele yakamjaa kuhusu vibao vile alivyopigwa kiuchawi. Aliwaza sana kwani alikuwa ana zindiko kubwa sana, sasa kwanini apigwe vile wakati ana kings anayoiamini? Alijiuliza sana bila kupata jibu.

Kulipambazuka kabisa, kimwanga kidogo cha jua kilianza kuchomoza kwa mbali. Wakati huo Mr Alloyce alikuwa kwenye gari take kuelekea msituni alikopotelea Mama Eddy.
Kichwani mwake alifikiria sana jinsi ya kutatua matatizo yanayoikumba familia yake. Hakupata njia kamili ya kuweza kutatua matatizo yake.

Aliendesha gari kwa mwendo wa SAA moja na nusu hatimaye akawasili kwenye eneo alilotakiwa kufika, akashuka kwenye gari na kuangaza macho yake huku na kule kuona kama atamwona mkewe.

******
"Amka mama Pamela kuna jambo nataka nikuambie"
"Bwana utaniambia asubuhi"
"Huu ndo muda mzuri wa kukuambia lakini kama hutaki basi.. " Alisema baba Pamela kwa sauti ya utulivu sana . Licha ya ubishi aliokuwa nao mama Pamela katika suala la kuamka lakini ilimbidi tu aamke ili amsikilize mume wake. Kwani alijua huenda ana jambo muhimu anataka kumueleza wakati ule.
"Niambie basi mume wangu!" Alisema mama Pamela huku akipiga miayo ya uchovu wa usingizi.
"Asubuhi ya Leo nina safari kikazi.."
"Unaenda wapi?" Aliuliza mama Pamela.
"Naenda Arusha mke wangu... Nilitemea nikuambie Jana ila uliniudhi mpaka nikashindwa kukuambia"
"Mmh! Utakaa muda gani?"
"Mwezi mmoja!"
"Mwezi mzima? Mbona mrefu hivyo?"
"Ndio hivyo mke wangu ni masuala ya kazi tu, sina jinsi"
"Imekuwa ghafla!"
"Ndio nimepewa taarifa juzi jioni, lakini...."
"Lakini nini?" Alishtuka mama Pamela
"Nikiondoka tu, na huyo mgeni wako atoke hapa nyumbani kwangu"

Alisema Baba Pamela kwa sauti ya msisitizo sana akidhihirisha kuwa alimaanisha kile alichokisema.
"Baba Pamela utaniudhi.. Sitaki maudhi yako na hiyo roho mbaya yako"
"IPO siku utafahamu kwanini nasema hivo.. Kaa vizuri na Mungu utafahamu mengi!" Alisema Baba Pamela kisha akajifunika vizuri na kulala ili aamke baada ya nusu saa.

Mama Pamela alibaki na mawazo mengi sana ila katu hakuwa tayari kumwacha Doreen aende zake. Alimwonea huruma binti yule kwani alishamwambia historian nzima ya maisha yake.' Mime wangu sijui yukoje siku hizi.. Ana roho mbaya.. Simfukuzi ng'oo Doreen. Mtoto ana adabu tena mstaarabu' aliwaza Bi Carolina.

Asubuhi na Mapema Baba Pamela alijiandaa na kuwahi uwanja wa ndege, Bi Carolina alimsindikiza mumewe hadi uwanja wa Songwe Airport Kisha akamuaga.
"Ila tekeleza nilichokuambia"
"Sawa !" Alijibu Bi Carolina kisha akaingia kwenye gari na kuondoa gari kuelekea nyumbani kwake.
Haukupita muda mrefu Bi Carolina alitia timu nyimbani kwake, akapaki gari na kuingia ndani. Lakini alipoingia ndani alikutana na hali ya utofauti.

Itaendelea.....
 
Babu niunge katika hii thread mana mm hapa jaman bado mgeni san'aaa.
Jana kwanza imenipotea nikapata tabu kweli kuipata hadi nikakata tamaa kabisa na Leo hii ndo yaja tena nimefurahi sana.
Asinicheke mtu mm APA mgeni bado ktk jukwaa hili.
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Babu niunge katika hii thread mana mm hapa jaman bado mgeni san'aaa.
Jana kwanza imenipotea nikapata tabu kweli kuipata hadi nikakata tamaa kabisa na Leo hii ndo yaja tena nimefurahi sana.
Asinicheke mtu mm APA mgeni bado ktk jukwaa hili.
Hii thread iwekee nyota... any comments utakuwa unapata notifications. . So babu akituma utaona tu..
 
Babu niunge katika hii thread mana mm hapa jaman bado mgeni san'aaa.
Jana kwanza imenipotea nikapata tabu kweli kuipata hadi nikakata tamaa kabisa na Leo hii ndo yaja tena nimefurahi sana.
Asinicheke mtu mm APA mgeni bado ktk jukwaa hili.
Tayari ushajiunga mkuu. Kama unatumia jf app utaikuta sehemu imeandikwa subcribe.
 
Babu lete ubuyu.... Hadithi inazidi kuwa tamu
 
Asanateni wana jf.
Hakika na enjoy sana hii App kwa kusoma na kujifunza mangi...be blessed guys!
 
  • Thanks
Reactions: Lee
SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO

..DORICE alimshangaa Mumewe Mansoor kwa maneno yake. Machozi yalimlengalenga machoni mwake kisha akajiondoa kifuani kwa Mansoor na kujitenga kando.
"Vipi mke wangu?"
"Najuta Mansoor.. Najuta sana kukukubalia, sikujua kama hautakuwa mwaminifu kwa ahadi zako!" Alisema Dorice kwa hasira.

"Sina maana mbaya mke wangu mpenzi.. Usinielewe vibaya tafadhali...Nakupenda sana!"
"Unanipenda? Unanipenda nini uongo mtupu..!" Alisema Dorice kwa hasira huku machozi yakimshuka mashavuni mwake. Alijikuta anamchukia Mansoor kupita kiasi. Hakutaka hata kumsogelea karibu.
"Baby! Nimekuelewa basi naomba uwe na amani moyoni mwako" alisema Mansoor huku akimsogelea Dorice na kutaka kumkumbatia lakini Dorice alimsukumia kando Mansoor na kuongeza kilio chake.
"Sitaki uniguse mpaka utakaponiambia ni lini utatimiza ahadi yako"

"Baada ya wiki moja nitaitimiza ahadi yako..!" Alisema Mansoor kwa huzuni kwani alijua ni kiasi gani Dorice alimpenda Eddy na alijua kwamba endapo angemrudisha Dorice duniani basi angemsahau Yeye na kuponda raha na Eddy. Kila alipofikiria hilo Mansoor aliumia sana moyoni mwake. Hakutamani kumkosa Dorice lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kutunza uaminifu wa kutimiza ahadi yake.
"Una uhakika utanipeleka baada ya wiki moja?" Aliuliza Dorice akimtazama Mansoor.

"Ndio.. Usijali!" Mansoor alijibu kwa unyonge sana.
"Hapo umenifurahisha!" Alisema Dorice na kumkumbatia Mansoor.
"Lakini kabla haujaenda huko kuna kitu muhimu unatakiwa ufanye!" Alisema Mansoor akiwa bado amemkumbatia Doreen.
"Kitu gani?" Aliuliza Dorice.
Mansoor alimuachia Dorice kisha akanyoosha mkono wake na kumuonesha Dorice kiganja cha mkono wake. Kwa mshangao kidogo, Dorice akatazama kiganja cha Mansoor.
"Unaona nini hapa?"
"Sioni kitu.."
"Huoni kitu? Hebu tazama vizuri"
"Naona Pete" alijibu Dorice kwa mshangao.

*********
Eddy alimtazama kwa mshangao mlinzi wao. Alimkazia macho huku akimwomba msamaha kwa kumjibu vibaya hapo mwanzo.
"Usijali.. Najua matatizo yako yanakufanya uwe hivyo" alisema mlinzi.
"Sasa utanisaidiaje? Maana nateseka sana!"
"Nitakusaidia tu wala usiwe na haraka... "
"Lazima niwe na haraka Anko maana mpaka sasa hivi sijawahi hata kukojoa!"

"Mmh! Haraka zilimponza chura zikafanya awe na mabaka. Vuta subira tu maana umefanyiwa mchezo mbaya sana." Alisema mlinzi yule huku akijifunika vyema shuka lake na kujigesha ukutani ili amalizie usingizi wake. Lakini ghafla akapigwa Kofi zito shavuni, aliruka kama kuku aliyeona hatari. Kabla hajakaa sawa Kofi lingine zito lilitua shavuni kwake, akajishika shavu na kutazama kama alikuwa amechanika lakini haikuwa hivyo kwani hakukuwa na damu yoyote ile.

Mlinzi yule akatazama huku na kule lakini hakuona Mtu aliyempiga makofi Yale mazito yaliyotua shavuni kama radi wakati wa mvya Kali.
"Vipi Anko?"
"Ah.. Hanna kitu.. Niko sawa tu.."
"Mbona umeruka sana?"
"Usijali Eddy.. Mimi nimeaga kwetu Musoma.. Niliwaaga wajita wenzangu..!" Alisema Mlinzi huku akisikilizia maumivu makali ya vibao alivyopigwa.
"Sikuelewi Anko ."
"Nimeaga.. Hakuna wa kunichezea!" Alizidi kuropoka mlinzi yule kisha akatulia kimya. Mawazo tele yakamjaa kuhusu vibao vile alivyopigwa kiuchawi. Aliwaza sana kwani alikuwa ana zindiko kubwa sana, sasa kwanini apigwe vile wakati ana kings anayoiamini? Alijiuliza sana bila kupata jibu.

Kulipambazuka kabisa, kimwanga kidogo cha jua kilianza kuchomoza kwa mbali. Wakati huo Mr Alloyce alikuwa kwenye gari take kuelekea msituni alikopotelea Mama Eddy.
Kichwani mwake alifikiria sana jinsi ya kutatua matatizo yanayoikumba familia yake. Hakupata njia kamili ya kuweza kutatua matatizo yake.

Aliendesha gari kwa mwendo wa SAA moja na nusu hatimaye akawasili kwenye eneo alilotakiwa kufika, akashuka kwenye gari na kuangaza macho yake huku na kule kuona kama atamwona mkewe.

******
"Amka mama Pamela kuna jambo nataka nikuambie"
"Bwana utaniambia asubuhi"
"Huu ndo muda mzuri wa kukuambia lakini kama hutaki basi.. " Alisema baba Pamela kwa sauti ya utulivu sana . Licha ya ubishi aliokuwa nao mama Pamela katika suala la kuamka lakini ilimbidi tu aamke ili amsikilize mume wake. Kwani alijua huenda ana jambo muhimu anataka kumueleza wakati ule.
"Niambie basi mume wangu!" Alisema mama Pamela huku akipiga miayo ya uchovu wa usingizi.
"Asubuhi ya Leo nina safari kikazi.."
"Unaenda wapi?" Aliuliza mama Pamela.
"Naenda Arusha mke wangu... Nilitemea nikuambie Jana ila uliniudhi mpaka nikashindwa kukuambia"
"Mmh! Utakaa muda gani?"
"Mwezi mmoja!"
"Mwezi mzima? Mbona mrefu hivyo?"
"Ndio hivyo mke wangu ni masuala ya kazi tu, sina jinsi"
"Imekuwa ghafla!"
"Ndio nimepewa taarifa juzi jioni, lakini...."
"Lakini nini?" Alishtuka mama Pamela
"Nikiondoka tu, na huyo mgeni wako atoke hapa nyumbani kwangu"

Alisema Baba Pamela kwa sauti ya msisitizo sana akidhihirisha kuwa alimaanisha kile alichokisema.
"Baba Pamela utaniudhi.. Sitaki maudhi yako na hiyo roho mbaya yako"
"IPO siku utafahamu kwanini nasema hivo.. Kaa vizuri na Mungu utafahamu mengi!" Alisema Baba Pamela kisha akajifunika vizuri na kulala ili aamke baada ya nusu saa.

Mama Pamela alibaki na mawazo mengi sana ila katu hakuwa tayari kumwacha Doreen aende zake. Alimwonea huruma binti yule kwani alishamwambia historian nzima ya maisha yake.' Mime wangu sijui yukoje siku hizi.. Ana roho mbaya.. Simfukuzi ng'oo Doreen. Mtoto ana adabu tena mstaarabu' aliwaza Bi Carolina.

Asubuhi na Mapema Baba Pamela alijiandaa na kuwahi uwanja wa ndege, Bi Carolina alimsindikiza mumewe hadi uwanja wa Songwe Airport Kisha akamuaga.
"Ila tekeleza nilichokuambia"
"Sawa !" Alijibu Bi Carolina kisha akaingia kwenye gari na kuondoa gari kuelekea nyumbani kwake.
Haukupita muda mrefu Bi Carolina alitia timu nyimbani kwake, akapaki gari na kuingia ndani. Lakini alipoingia ndani alikutana na hali ya utofauti.

Itaendelea.....
Nzuri
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA

....BI CAROLINA alipiga hatua za taratibu kuelekea sebuleni lakini hali iliyokuwemo ndani mle ilizidi kumshangaza kwani alisikia harufu Kali na mbaya ya kitu kuungulia. Alifika sebuleni lakini hakukuta Mtu yeyote, akaamua kwenda jikoni.

Alipoingia jikoni tu, alipiga chafya tatu mfululizo kutokana na moshi mzito ulioambatana na harufu Kali sana uliotawala jikoni mle. Aliisogelea mpaka sehemu ya kupikia akagundua moto uliwashwa na kuna kitu kilichomwa. Akaangalia sufuria zote lakini hakukuta kitu chochote, akabaki na mshangao.
"Doreen!" Aliita Bi Carolina akiwa ameshika mkono kiunoni.
"Abee mama!" Sauti ya Doreen ilisikika kutoka chumbani.
"Njoo huku jikoni"

Bila ya kuchelewa Doreen alifika jikoni kule na kumkuta Bi Carolina akiwa ameshika kiuno akimsubiri kwa hamu amuulize kilichotokea.
"Abee mama" aliitikia Doreen kwa adabu sana.
"Nini kimetokea huku jikoni?"
"Nisamehe mama... Nilitaka kupika.. Ila kwa bahati mbaya nikaunguza kwani sijui kutumia jiko la gesi." Alijitetea Doreen huku akitia huruma sana.

"Ulitaka upike nini asubuhi yote hii?"
"Nili...nilikuta maziwa.. Nyama kwenye friji nikataka nipike.."
"Mara maziwa mara nyama.. Mbona sikuelewi? Haya ulipikia sufuria gani?" Bi Carolina alishindwa kumuelewa Doreen ila kutokana na ugeni aliokuwa nao hakuweza kumfokea sana kwa kuhofu kuwa atajisikia vibaya.
"Nilichukua nyama... Sufuria ilipoungua sana nikaamua kuiosha.." Alisema Doreen akidai kutetemeka kwa woga.
"Sawa ila usirudie tena.. Nitakufundisha jinsi ya kupikia jiko la gesi.."
"Sawa mama" alisema Doreen kwa sauti ya upole iliyojaa hekima ya viwango vya juu.
"Sawa mwanangu nenda kaendelee na kazi zako"

Doreen alitoka jikoni mle na kuelekea chumbani kwake. Alichukua kimfuko cheusi kidogodogo kisha akafungua na kuutoa ungaunga mweusi. Kisha akaweka kiganjani na kusogelea kila kona ya chumba kile na kuupuliza kwa midomo yake. Alifanya hivyo mpaka unga ule ilipoisha, akasogelea kitanda chake na kukaa.

"Hapa sasa nimemaliza kazi... Mpaka huo moshi uishe nitakuwa nimefanikiwa kabisa." Alisema Doreen akitabasamu kwani ule moshi uliotapakaa ndani mle ulisababishwa na Doreen. Alikuwa amechoma dawa ambayo ingewafanya wakaaji wa nyumba ile kumpenda Doreen kupita kiasi, na wasingeweza kumfukuza hata iweje mpaka pale atakapoamua kuondoka yeye mwenyewe.

Aliangalia SAA yake ya mkononi ilikuwa tayari ni saa nne na nusu asubuhi. Doreen alisikia sauti ya Bi Carolina ikimwita. Akatii wito na kumfuata Bi Carolina.
"Abee mama" aliitikia kwa heshima.
"Umeoga?"
"Bado"
"Kaoge unywe chai."
"Sawa mama"
Doreen alitoka sebuleni pale na kwenda bafuni kuoga. Alipomaliza alipaka mafuta na kuvaa tena nguo alizokuwa amevaa kabla ya kuoga kisha akaenda sebuleni. Akamkuta Bi Carolina akiwa amekaa huku akitazama televisheni.
"Mbona umevaa nguo chafu?"
"Sina zingine"

"OK.. Baadae tutaenda Mwanjelwa ukatafute nguo za kuvaa.. Sasa hivi nenda ukanywe chai.." Alisema Bi Carolina.
"Sawa mama.. Vipi kuhusu Dada Pamela?" Aliuliza Doreen.
"Atakuja si muda mrefu.. Ameniambia yupo njiani. Baada ya kumwambia hivyo ghafla mlango ukagongwa . Akaingia msichana mmoja mrefu kiasi, mweupe, matiti yenye ukubwa kiasi, kiuno chembamba kama sindano na makalio makubwa kama milima miwili iliyopangana vyema. Wote walishtuka kidogo.
"Ah Pamela kumbr ulikuwa jirani tu.. Tumekuongelea sasa hivi hapa.."

"Sikuwa mbali"
"Karibu sana" alisema Bi Carolina wakati huo Pamela alikuwa akiketi sofani na kuweka pembeni mkoba wake. Kwa muda wote huo Doreen alikuwa akimtazama Pamela katika maeneo ya kifuani.
"Shkamoo Dada Pamela" alisalimia Doreen
"Marhaba hujambo? Wewe ndo Doreen?"
"Ndio.." Aliitikia Doreen huku akimgeukia mama Pamela "kumbe una mtoto mzuri namna hii?" Alisema.
Bi Carolina na Pamela walicheka tu.
"Huyu ndo mwanangu mpenzi... Yuko peke yake kama Tanzanite..." Alisema Mama Pamela huku akicheka.
Doreen aliwaacha wakiendelea na mazungumzo kisha yeye akaenda chumba cha kulia chakula (dinning). Moyoni mwake alifurahi sana kwani kwa uzuri aliokuwa nao Pamela titi lake lilifaa sana kwa kazi ya Doreen.

********


Dorice aliitazama Pete ya Mansoor kwa mshangao kwani hakujua lengo kamili la Mansoor kutaka kuitazama Pete ile.
"Umeitazama vizuri Pete hiyo?"
"Ndio"
"Hii Pete, si kama Pete za kawaida, ina nguvu nyingi sana ambayo inazidi nguvu za kaeaida." Alisema Mansoor kisha akakohoa kidogo ili kusafisha koo lake kisha akaendelea.

"Pete hii nilipewa na babu yangu ambaye anaishi mbali sana katika sayari nyingine kabisa, alinipa kwaajili ya ulinzi wangu binafsi kwasababu alikuwa ananipenda. Na Mimi nitakupa wewe pete hii kwasababu nakupenda sana, ili ikusaidie katika kumuokoa mtu umpendae sana." Alisema Mansoor huku akimtazama Dorice. Dorice aliendelelea kumsikiliza kwa umakini sana Mansoor.
"Pete hii ni ya ufalme wangu pale nitakapopewa ufalme na mama yangu... Wewe kwasababu ni mke wangu utakuwa malkia..."
"Nini?"

"Unashangaa nini? Sina njia nyingine ya kukusaidia mbali na hii.. Kama upon tayari nitakupa pete hii na utakuwa na uwezo mkubwa sana wa kijini... Utarudi duniani na utafanya kila unalotaka..." Alisema Mansoor. Maneno yake yalikuwa mazuri masikoni mwa Dorice ingawa yalimpa utata wa kiwango cha juu alijiuliza maswali mengi kichwani mwake juu ya suala la umalkia. Lakini akayapotezea maswali yake kwani alitamani sana kurudi duniani kumuokoa mpenzi wake Eddy na kwenda kwa wazazi wake ambao hakuwaona kwa muda mrefu.
"Sawa... Nipe tu..!" Alisema Dorice akionesha kukubali masharti ya Mansoor.

"Nitakupa Mke wangu lakini kuna jambo muhimu unalotakiwa kuzingatia pindi utakapokuwa na hii pete"
"Jambo Gani?" Dorice alishtuka.
"Hii ni pete ys heshma sana, ambayo haihitaju uchafu wa aina yoyote.. Kwahiyo ukiivaa na kwenda Nayo duniani hutakiwi kufanya mapenzi na mwanaume mwingine zaidi yangu Mimi!" Alisema Mansoor huku akimtazama mkewe kwa macho yaliyoonesha msisitizo kwa kile alichokizungumza.

"Mmh!" Aliguna Dorice kwani alikuwa na wazo la kumsaliti Mansoor pindi atakaporudi duniani. Na alikuwa na lengo la kutorudi tena katika himaya ile ya majini. Hivyo basi masharti ya pete ile yalikuwa magumu sana kwake na kumuweka katika wakati mgumu sana.
"Mbona unaguna?"
"Kwani hakuna msaada mwingine mbali na hiyo pete" aliuliza Doreen
"Upo!"
"UPI.. Nipe msaada mwingine Mansoor tafadhali"
"Unataka njia nyingine?"
"Ndio.." Alijibu Dorice haraka.

**********

Mr Aloyce alitembeatembea katika eneo lile akimsubiri mkewe atokeze lakini muda ukazidi kwenda Vila kuona dalili yoyote. Mr Aloyce alianza kukata tamaa ya kumpata mkewe akahisi huenda alikuwa anadanganywa tu. Akataka kuondoka lakini moyo wake ulisita sana baada ya kuumbuka msemo usemao "atafutaye hachoki, akichoka keshapata" akaamua kuwa mvumilivu kwani siku zote mvumilivu hula mbivu.

Ajasogelea eneo tulivu lenye nyasi fupi kisha akaketi pale. Mawazo mengi yalifurika kichwani mwake, "nimekuwa mtumwa... Mtumwa wa nguvu za giza hii hali mpaka lini? Kila siku yanaibuka mapya... Mmh! Yote hii ni kwasababu ya Eddy.. Ila sipaswi kumlaumu" alijiwazia Mr Alloyce huku machozi yakimtiririka.

Ghafla upepo mkali ulianza kupuliza eneo lile na kumwondoa mawazoni Mr Aloyce. Alinyanyuka pale chini na kutazama juu lakini hakuona chochote.

Upepo ukazidi kupuliza kwa kasi sana mpaka miti ikaanza kuyumbayumba. Miti iliyumba kwa kasi sana na ile isiyo na nguvu ikaanguka. Mr Aloyce aliogopa sana.
Baada ya upepo ule radi Kali zikapiga mfululizo, zikazidi kumtisha Mr Aloyce. Alipiga hatua kuelekea kwenye gari yake ili akajifiche mle maana hali ilitishs lakini ghafla akasikia sauti ya kilio kikali.

"Nisaidie mume wangu.. Nisaidiee!" Mr Aloyce alishtuka sana kwani sauti ile aliijua fika. Ilikuwa ni sauti ya mkewe mpenzi. Akabaki amesimama wima kama mlingoti ili asubiri kitakachoendelea.
Akiwa bado amesimama alishtushwa na kitu kikipita miguuni mwake, akatulia kimya huku akipiga jicho kutazama kilikuwa kitu gani.

"Mamaaa" mr Aloyce alipiga ukunga kwa woga na hofu baada ya kuonana uso kwa uso na chatu aliyekuwa akijiviringa kwa kasi mwilini mwake.

Itaendelea.....
 
Mbona upande wa shuleni hatuadithiwi tena.. naona vipande vya shuleni havipo kbsaaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom