Xav Emmanuel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2018
- 215
- 316
SIMULIZI FUPI: MWALIMU WA ZAMU
MTUNZI: XAVERY LUOGA *AUTHOR XAV*
Namba: 0672493994
==================================
*********
Simulizi hii ni mwanga kwa kuendeleza Imani ya kumwabudu mungu aliye kweli.. pia ni ni funzo kwa watu ambao wanaacha tamaduni zao kwa kuzizarau au kwa namna moja au nyingine.
Pia haya ni baadhi tu ya mambo ambayo waalimu wanakutana nayo katika taaluma zao. Pengine si walimu tu, hata madaktari, na wengineo.
Tuungane katika simulizi hii fupi ya Mwalimu wa Zamu kupata funzo… Funzo la Maisha.
Karibu.
**********
SEHEMU: 01
Ilikuwa ni alfajiri ya mapema ambapo viungo vya mwili viliendelea kukumbushana majukumu yake, mdomo haukuacha kabisa kupanuka kuashiria unaitaji kupumua kwa nguvu zote, kupumua huko hukumbusha pia mikono kuwa inaitajika kusimama kwa ukakamavu na kuinuka, tena kwa kukunja ngumi huku mwingine ukienda kushoto na mwingine kwenda kulia. Kiuno nacho hakikuwa mbali katika kubinuka ili kuendana na kasi ya mdomo, mikono na miguu.
“Alhamdullilah!”, swala fupi ikatoka kinywani mwangu kuashilia sipo mbali sana Mungu. Hakuna aliyekosea kusema kuwa mimi ni Muislam tena Muislam aliyekomaa kwa kuangalia tu jina langu.
“Yusuph Athumani” Jina hili linamaanisha Baba Muislam, Mama Muislam; Nilitabasamu.
Baada ya muda nikaupa ubongo nafasi ngeni ya kutabasamu kwa kukumbuka baadhi ya kumbukumbu wakati nipo chuo, na maandalizi yote ya safari kutoka Dodoma hadi Songea. Ubongo nao haukuitupa nafasi hiyo kwa kutaja neno UDOM; kila baada ya nukta.
Kuna mda nilikaa kushangaa kwa nini neno hilo limekuwa mzizi katika mawazo yangu, lakini kushangaa huko kulijibiwa vizuri na ubongo. “University of Dodoma” Ubongo ukaishia kunijibu hivyo na kutoweka.
Nilikumbuka kuwa hata safari hiyo ya kutoka Dodoma kwenda Songea ilikuwa ni sababu ya neno UDOM. Ni kweli kabisa nilikua nimetumwa kufanya moja ya majukumu ya mafunzo yangu ya ualimu. Yaani mafunzo ya ufundishaji wa vitendo.
Basi harakati za hapa na pale zikaendelea, hatimaye nikafanikiwa kumaliza kila kitu kwa kujiandaa, angali sehemu ambayo ilikuwako shule nilikua bado siijui vizuri, lakini jina na maeneo ilipo nilishaelekezwa tayari, kilichobaki ni kuchoma tu pesa kwa dereva bodaboda kunifikisha sehemu husika.
“Naenda Ruvuma Sekondari”, nilitoa maelezo hayo na sikuulizwa kitu zaidi ya kupanda na safari ikaanza, dakika tano tu nilifika eneo la shule.
Nilipokelewa kwa shangwe na vumbi la kutosha, lote lilitaka kung’ang’ania mwili wangu. Miti iliyolala ikasimama na kunionea huruma, barabara nayo ikatanuka kwa kiasi chake kuacha njia kubwa ya mimi kupita.
Nilihisi furaha kupitiliza kwa baadhi ya salamu nyingi kutoka kwa wanafunzi, nyingi zikiwa za lugha ya Kiswahili, hizo nilivunga kuitikia, ila za lugha ngeni nilipatwa na shauku ya kuzijulia hali,
“Good Morning! how are you?”. Huku uso wa bashasha uliojaa nizamu ya ugeni ukisogea machoni mwa wanafunzi.
Nilitulia sehemu ambayo juu ya jengo hilo kuliandikwa neno UTAWALA. Ndio nilisimama hapo, niende wapi mimi kuku mgeni?. Nilikuwa mimi na begi langu lililosheheni makatasi ya kulipo sehemu ya kazi.
Nilitulia kama dakika sita hivi bila kutikisika, kwani nilizubaa kuangalia wanafunzu ambao wengi wao walivaa hijabu zao nyeupe ‘pee’ na kuendelea na shughuli zao za usafi. Walikuwa bize kweli kufanya usafi huku wengine wakikata majani, wengine kufagia na wengine kumwagilia maua.
“Eti kaka samahani!, kwa tunaofika leo utaratibu upoje?”, sauti nyepesi ilinishitua katika dimbwi la mawazo na kukaa sawa kama askari aliye fanyiwa ziara ya kushitukiza na mkuu wake wa kazi. Alikuwa ni mwanamke.
“ah ah… khoonho konhooo” nilikohoa kidogo kwa kujiweka sawa kisha kujibu.
“Sijajua!, kwa maana na mimi naripoti leo!” nilijibu huku macho yangu yakiendelea kuchambua uzuri wa mwanamke yule mgeni katika mboni yangu. Alikuwa na asili yake kwa kweli.
“Mmmh!, Oky!. ko nawe wa TP e?, Chuo gani mwalimu?”. Maswali mengine yakafuata kutoka kwa mwanamke yule ambaye naye alikuwa mgeni kama mimi.
“Yahp, natokea huko Dodoma, Chuo Kikuu cha Dodoma”. Nilijibu, nikikuna kichwa kidogo na kumtazama.
“Oh wow!, aya sawaa, mi wa UD..!” hakumalizia kauli yake akapokea salamu ya mwanafunzi na mazungumzo mengine yakaendelea, wakaongezeka na waalimu wengine saba na kuwa jumla yetu kufikia waalimu tisa tulioripoti siku hiyo.
Walimu walioajiliwa shule hiyo walitupokea vizuri kwani walijua kwa majuma machache tutakayo kuwa shuleni hapo, tutakuwa tunawapunguzia baadhi ya majukumu ya ufundishaji, na uhudumu shule.
Tulipokelewa na mkuu wa shule pamoja na makamu wake na kufanyiwa semina fupi inayohusu mienendo na falsafa za shule hiyo. Hakuna alichotuficha mkuu wa shule, alituambia yote japo mengine alitubinya, aliyasema kwa hofu.
“Wazazi wa watoto ni wakali kweli…….., mjitahidi kulinda hasira zenu……..” mkuu wa shule licha ya kuongea mambo mengi sana ya kujenga lakini alikomea sehemu hii kwa malizia maneno hayo mawili ambayo hakuyatolea ufafanuzi zaidi ya kuongea kimkato tu na kumkaribisha mwalimu mkuu msaidizi.
“Kama nilivyojitambulisha mwanzo, Mwalimu Kunambi Michael ndio jina langu, yote yameshaongelewa na mkuu, nategemea utekelezaji tu.”, mwalimu huyu alikuwa na ushawishi wa maneno wa aina yake, aliongea kisomi bila kipindapinda. Alikuwa mwepesi wa kutumia lugha.
Baada ya kumalizika kwa semina tukakabidhiwa waalimu wa masomo na majukumu ya hapa na pale yakiendelea. Tukawa rasmi waalimu wanafunzi kwa mafunzo ya vitendo.
***********
Labda kabla sijaendelea kusimulia ndugu wasikilizaji, hii ni simulizi iliyojaa visa vingi ndugu zangu, iliyo na lengo ya kuelimisha uma kuwa si kila sehemu ya kuingia kichwa kichwa, maana kila sehemu kuna utamaduni na mienendo yake iliyolenga kuimalisha jamii hiyo katika kila mipaka……..
INAENDELEA….
KUMBUKA:
Baadhi ya matukio, sehemu na watu katika simulizi hii ni ya kweli. Lakini simulizi ni ya kutungwa na haina uhusiano wowote hule kati ya matukio mengi ya humu na uhalisia wa sehemu yenyewe. Karibu katika mwendelezo….
Sent using Jamii Forums mobile app
MTUNZI: XAVERY LUOGA *AUTHOR XAV*
Namba: 0672493994
==================================
*********
Simulizi hii ni mwanga kwa kuendeleza Imani ya kumwabudu mungu aliye kweli.. pia ni ni funzo kwa watu ambao wanaacha tamaduni zao kwa kuzizarau au kwa namna moja au nyingine.
Pia haya ni baadhi tu ya mambo ambayo waalimu wanakutana nayo katika taaluma zao. Pengine si walimu tu, hata madaktari, na wengineo.
Tuungane katika simulizi hii fupi ya Mwalimu wa Zamu kupata funzo… Funzo la Maisha.
Karibu.
**********
SEHEMU: 01
Ilikuwa ni alfajiri ya mapema ambapo viungo vya mwili viliendelea kukumbushana majukumu yake, mdomo haukuacha kabisa kupanuka kuashiria unaitaji kupumua kwa nguvu zote, kupumua huko hukumbusha pia mikono kuwa inaitajika kusimama kwa ukakamavu na kuinuka, tena kwa kukunja ngumi huku mwingine ukienda kushoto na mwingine kwenda kulia. Kiuno nacho hakikuwa mbali katika kubinuka ili kuendana na kasi ya mdomo, mikono na miguu.
“Alhamdullilah!”, swala fupi ikatoka kinywani mwangu kuashilia sipo mbali sana Mungu. Hakuna aliyekosea kusema kuwa mimi ni Muislam tena Muislam aliyekomaa kwa kuangalia tu jina langu.
“Yusuph Athumani” Jina hili linamaanisha Baba Muislam, Mama Muislam; Nilitabasamu.
Baada ya muda nikaupa ubongo nafasi ngeni ya kutabasamu kwa kukumbuka baadhi ya kumbukumbu wakati nipo chuo, na maandalizi yote ya safari kutoka Dodoma hadi Songea. Ubongo nao haukuitupa nafasi hiyo kwa kutaja neno UDOM; kila baada ya nukta.
Kuna mda nilikaa kushangaa kwa nini neno hilo limekuwa mzizi katika mawazo yangu, lakini kushangaa huko kulijibiwa vizuri na ubongo. “University of Dodoma” Ubongo ukaishia kunijibu hivyo na kutoweka.
Nilikumbuka kuwa hata safari hiyo ya kutoka Dodoma kwenda Songea ilikuwa ni sababu ya neno UDOM. Ni kweli kabisa nilikua nimetumwa kufanya moja ya majukumu ya mafunzo yangu ya ualimu. Yaani mafunzo ya ufundishaji wa vitendo.
Basi harakati za hapa na pale zikaendelea, hatimaye nikafanikiwa kumaliza kila kitu kwa kujiandaa, angali sehemu ambayo ilikuwako shule nilikua bado siijui vizuri, lakini jina na maeneo ilipo nilishaelekezwa tayari, kilichobaki ni kuchoma tu pesa kwa dereva bodaboda kunifikisha sehemu husika.
“Naenda Ruvuma Sekondari”, nilitoa maelezo hayo na sikuulizwa kitu zaidi ya kupanda na safari ikaanza, dakika tano tu nilifika eneo la shule.
Nilipokelewa kwa shangwe na vumbi la kutosha, lote lilitaka kung’ang’ania mwili wangu. Miti iliyolala ikasimama na kunionea huruma, barabara nayo ikatanuka kwa kiasi chake kuacha njia kubwa ya mimi kupita.
Nilihisi furaha kupitiliza kwa baadhi ya salamu nyingi kutoka kwa wanafunzi, nyingi zikiwa za lugha ya Kiswahili, hizo nilivunga kuitikia, ila za lugha ngeni nilipatwa na shauku ya kuzijulia hali,
“Good Morning! how are you?”. Huku uso wa bashasha uliojaa nizamu ya ugeni ukisogea machoni mwa wanafunzi.
Nilitulia sehemu ambayo juu ya jengo hilo kuliandikwa neno UTAWALA. Ndio nilisimama hapo, niende wapi mimi kuku mgeni?. Nilikuwa mimi na begi langu lililosheheni makatasi ya kulipo sehemu ya kazi.
Nilitulia kama dakika sita hivi bila kutikisika, kwani nilizubaa kuangalia wanafunzu ambao wengi wao walivaa hijabu zao nyeupe ‘pee’ na kuendelea na shughuli zao za usafi. Walikuwa bize kweli kufanya usafi huku wengine wakikata majani, wengine kufagia na wengine kumwagilia maua.
“Eti kaka samahani!, kwa tunaofika leo utaratibu upoje?”, sauti nyepesi ilinishitua katika dimbwi la mawazo na kukaa sawa kama askari aliye fanyiwa ziara ya kushitukiza na mkuu wake wa kazi. Alikuwa ni mwanamke.
“ah ah… khoonho konhooo” nilikohoa kidogo kwa kujiweka sawa kisha kujibu.
“Sijajua!, kwa maana na mimi naripoti leo!” nilijibu huku macho yangu yakiendelea kuchambua uzuri wa mwanamke yule mgeni katika mboni yangu. Alikuwa na asili yake kwa kweli.
“Mmmh!, Oky!. ko nawe wa TP e?, Chuo gani mwalimu?”. Maswali mengine yakafuata kutoka kwa mwanamke yule ambaye naye alikuwa mgeni kama mimi.
“Yahp, natokea huko Dodoma, Chuo Kikuu cha Dodoma”. Nilijibu, nikikuna kichwa kidogo na kumtazama.
“Oh wow!, aya sawaa, mi wa UD..!” hakumalizia kauli yake akapokea salamu ya mwanafunzi na mazungumzo mengine yakaendelea, wakaongezeka na waalimu wengine saba na kuwa jumla yetu kufikia waalimu tisa tulioripoti siku hiyo.
Walimu walioajiliwa shule hiyo walitupokea vizuri kwani walijua kwa majuma machache tutakayo kuwa shuleni hapo, tutakuwa tunawapunguzia baadhi ya majukumu ya ufundishaji, na uhudumu shule.
Tulipokelewa na mkuu wa shule pamoja na makamu wake na kufanyiwa semina fupi inayohusu mienendo na falsafa za shule hiyo. Hakuna alichotuficha mkuu wa shule, alituambia yote japo mengine alitubinya, aliyasema kwa hofu.
“Wazazi wa watoto ni wakali kweli…….., mjitahidi kulinda hasira zenu……..” mkuu wa shule licha ya kuongea mambo mengi sana ya kujenga lakini alikomea sehemu hii kwa malizia maneno hayo mawili ambayo hakuyatolea ufafanuzi zaidi ya kuongea kimkato tu na kumkaribisha mwalimu mkuu msaidizi.
“Kama nilivyojitambulisha mwanzo, Mwalimu Kunambi Michael ndio jina langu, yote yameshaongelewa na mkuu, nategemea utekelezaji tu.”, mwalimu huyu alikuwa na ushawishi wa maneno wa aina yake, aliongea kisomi bila kipindapinda. Alikuwa mwepesi wa kutumia lugha.
Baada ya kumalizika kwa semina tukakabidhiwa waalimu wa masomo na majukumu ya hapa na pale yakiendelea. Tukawa rasmi waalimu wanafunzi kwa mafunzo ya vitendo.
***********
Labda kabla sijaendelea kusimulia ndugu wasikilizaji, hii ni simulizi iliyojaa visa vingi ndugu zangu, iliyo na lengo ya kuelimisha uma kuwa si kila sehemu ya kuingia kichwa kichwa, maana kila sehemu kuna utamaduni na mienendo yake iliyolenga kuimalisha jamii hiyo katika kila mipaka……..
INAENDELEA….
KUMBUKA:
Baadhi ya matukio, sehemu na watu katika simulizi hii ni ya kweli. Lakini simulizi ni ya kutungwa na haina uhusiano wowote hule kati ya matukio mengi ya humu na uhalisia wa sehemu yenyewe. Karibu katika mwendelezo….
Sent using Jamii Forums mobile app