the_legend
JF-Expert Member
- Jan 14, 2019
- 1,612
- 7,110
Mtoto wa Baba Paroko : SEHEMU YA KWANZA
Erick Amuona Lucia Kwa Mara Ya kwanza
“Amani ya Kristu iwe nawe” “Iwe nawe pia” walikuwa ni Eric na Lucia wakipeana mikono ya amani katikati ya ibada ya mkesha wa Noeli Parokia ya Mavurunza Kimara Jijini Dar es salaam. Padre Masunga alisisitiza waumini wapeane mikono ya amani kwa kumaanisha na kuwa kama kuna mtu anajua ana chuki na mwenzake basi ni wakati wa kuombana msamaha kwani haitakuwa na maana waumini kusherehekea kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo huku wakiwa na chuki na visasi na majirani zao. Padre Masunga alisisitiza kuwa waumini wasalimiane kwa kujuliana hali tena kwa tabasamu.
Lucia, msichana mrembo sana mzuri kwa sura na umbo alikuwa akisalimiana na Eric kijana mtanashati tena mseminari. Lucia alikuwa na nywele ndefu za rangi ya blond, macho yake yalijaa kope nyingi utadhani ameongezea na za bandia alikuwa hawezi kumtazama mtu usoni kwa sekunde tatu kwa jinsi alivyojaa haiba na aibu.Alikuwa ni mrefu na mwenye umbo la wastani lakini cha mno kuhusu Lucia aliweza sana kujua kuvaa na kujipamba ilikuwa ni kawaida sana yeye kupita na kila mtu wa kike na wa kiume kumwangalia na kumpenda.Hakika alivutia sana kwa macho.
Eric alimpa mkono wa amani Lucia na ghafla alijikuta moyo wake unakwenda mbio kwa jinsi mkono wa Lucia ulivyokuwa laini. Lucia alimtazama machoni Eric kwa kuibia kisha aliangalia chini kwa aibu kama kawaida yake. Eric aliendelea kuushika mkono wa Lucia bila kuuachia, haikuwa kawaida kwani mtu hutakiwa kumshika mkono na baada ya kusalimiana hutakiwa kumwachia na kumsalimia mtu mwingine. Lucia alikuwa amekaa dawati la nyuma ya Eric.Baada ya sekunde kadhaa Eric aliuachia ule mkono wa Lucia na kuendelea kusalimia waumini wengine. Kisha ibada ikaendelea.
Ibada iliendelea huku akili ya Eric ikiwa imehama. Eric alikuwa ni mwanafunzi wa seminari kubwa ya Kipalapala Tabora. Alikuwa akiendelea na masomo yake ya upadre na sasa alikuwa likizo. Katika maisha yake Eric hakuwa amewahi kukutana na mwanamke kimwili. Ni kijana alielelewa kwenye familia yenye maadili sana na hakika hakuwahi kuwa na mahusiano na mwanamke ya kimapenzi japo mara nyingi alikuwa akiingia kwenye vishawishi hivyo. Eric siku zote aliamini padre hutakiwa kuwa mtakatifu na kuwa kwa kazi ile ya uchungaji anayoitaka ambayo hairuhusu kuoa alijitahidi sana kutojiingiza kwenye mahusiano ya kingono.
Ibada ilikuwa ikiendelea lakini Eric akili yake haikuwa pale. Alishindwa kuelewa nini kinatokea akilini mwake, inakuwaje anashindwa kuzingatia ibada mara tu baada ya kumuona Lucia.Wakati hayo yakiendelea Lucia nae alikuwa akitafakari kuhusu Eric kumng’ang’ania mkono wake bila kumsemesha chochote. Hakuwa akimjua Eric na kama ni mwanafunzi wa u padre lakini nae akili haikumtulia.
Ilipofika muda wa watu kwenda kupokea sakramenti Eric aliwahi sana ili aweze kurudi mapema na kukaa kumtazama Lucia. Wakati Lucia akiwa anarudi ndipo Eric aliweza kumtazama vizuri na kwa umakini. Mapigo ya moyo ya Eric yalikuwa yakienda kwa kasi sana. Lucia nae bila kujua alimtupia macho Eric na kujikuta anapoteza hatua na kutaka kudondoka. Eric hakuweza kujizuia alichukua karatasi iliyokuwa ndani ya misale yake (Kitabu kinachoonyesha masomo ya siku hiyo) akaandika “Naitwa Eric ningependa kuongea nawe baada ya Ibada kama hutojali.Asante” alipomaliza alikikunja na kutafakari namna ya kumpa Lucia alieketi nafasi ya nyuma yake.
Wakati akitafakari ulikuwa umefika muda wa kutoa sadaka ya pili hivyo vikapu vya sadaka vilikuwa vikipita kwenye viti unaweka sadaka halafu unampa mwenzako nae akimaliza anampa mwengine hivyo hivyo. Eric akaona hapo ndio muda wa kupenyeza ujumbe wake.Alipokipokea kikapu akaweka sadaka kisha badala ya kumpa wa pembeni yake yeye akageuka akampa Lucia kikapu lakini mkono mmoja akiwa ameshika kile kikaratasi akamshikisha Lucia vyote. Haraka Lucia akang’amua kuwa ule ujumbe ulikuwa wake hivyo akaweka sadaka kwenye kikapu na kumpa wa pembeni yake na kubaki na ule ujumbe. Baada ya dakika kadhaa kupita kwa siri Lucia alifungua kile kikaratasi na kusoma ule ujumbe. Mapigo ya moyo yalimwenda mbio kwani alianza kuhisi nini kitafuata na yeye hakuwa akimjua mwanaume mpaka umri ule. Lucia ndio kwanza alikuwa amejiunga na Chuo kikuu mwaka wa kwanza shahada ya Sheria.
Wakati hayo yakiendelea padre Masunga alisimama na kutoa tangazo kuwa katika ibada ile wapo vijana waliopo seminari wanaosomea u padre na angependa waumini wawafaham kwani ndio mapadre wao wa kesho. Vijana watatu walisimama lakini Eric hakusimama. Hakusimama kwa makusudi kwani kwa anachotaka kuongea na Lucia hakutaka kabisa Lucia ajue kama yeye anasomea u padre. “Nilimwona Eric hapa amekaa wapi mbona simwoni kusimama” alikuwa ni padre Masunga akimwita Eric asimame huku akizungusha shingo kumtafuta alipokaa. Haraka Eric alisimama kwa aibu. Waumini waliwapigia makofi na kisha walikaa.
Baada ya ibada Eric alihitajika kwenda kuonana na padre lakini yeye alitoka haraka ili amuwahi Lucia pale nje. Alipofika nje alimwona Lucia akiwa anatoka nje ya kanisa na alianza kumsogelea ili amsalimie lakini alipomkaribia Lucia alimkwepa na hakupokea mkono wake aliokuwa ameunyoosha tayari kumsalimia Lucia. Eric aligeuka na kumuona Lucia akiingia ndani ya Land Rover Discovery series 4 likiendeshwa na baba yake kisha likaondoka. “Eric padre anakutafuta” ilikuwa ni sauti ya Stanley rafiki wa Eric na mseminari mwenzake ikimwita kumtaarifu kuwa padre Masunga ana mwita Sakrestia (Chumba wanachotumia padre kujiandaa kabla na baada ya ibada). Eric alishtuka na kuanza kukimbia kuelekea sakrestia.
the Legend☆
Erick Amuona Lucia Kwa Mara Ya kwanza
“Amani ya Kristu iwe nawe” “Iwe nawe pia” walikuwa ni Eric na Lucia wakipeana mikono ya amani katikati ya ibada ya mkesha wa Noeli Parokia ya Mavurunza Kimara Jijini Dar es salaam. Padre Masunga alisisitiza waumini wapeane mikono ya amani kwa kumaanisha na kuwa kama kuna mtu anajua ana chuki na mwenzake basi ni wakati wa kuombana msamaha kwani haitakuwa na maana waumini kusherehekea kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo huku wakiwa na chuki na visasi na majirani zao. Padre Masunga alisisitiza kuwa waumini wasalimiane kwa kujuliana hali tena kwa tabasamu.
Lucia, msichana mrembo sana mzuri kwa sura na umbo alikuwa akisalimiana na Eric kijana mtanashati tena mseminari. Lucia alikuwa na nywele ndefu za rangi ya blond, macho yake yalijaa kope nyingi utadhani ameongezea na za bandia alikuwa hawezi kumtazama mtu usoni kwa sekunde tatu kwa jinsi alivyojaa haiba na aibu.Alikuwa ni mrefu na mwenye umbo la wastani lakini cha mno kuhusu Lucia aliweza sana kujua kuvaa na kujipamba ilikuwa ni kawaida sana yeye kupita na kila mtu wa kike na wa kiume kumwangalia na kumpenda.Hakika alivutia sana kwa macho.
Eric alimpa mkono wa amani Lucia na ghafla alijikuta moyo wake unakwenda mbio kwa jinsi mkono wa Lucia ulivyokuwa laini. Lucia alimtazama machoni Eric kwa kuibia kisha aliangalia chini kwa aibu kama kawaida yake. Eric aliendelea kuushika mkono wa Lucia bila kuuachia, haikuwa kawaida kwani mtu hutakiwa kumshika mkono na baada ya kusalimiana hutakiwa kumwachia na kumsalimia mtu mwingine. Lucia alikuwa amekaa dawati la nyuma ya Eric.Baada ya sekunde kadhaa Eric aliuachia ule mkono wa Lucia na kuendelea kusalimia waumini wengine. Kisha ibada ikaendelea.
Ibada iliendelea huku akili ya Eric ikiwa imehama. Eric alikuwa ni mwanafunzi wa seminari kubwa ya Kipalapala Tabora. Alikuwa akiendelea na masomo yake ya upadre na sasa alikuwa likizo. Katika maisha yake Eric hakuwa amewahi kukutana na mwanamke kimwili. Ni kijana alielelewa kwenye familia yenye maadili sana na hakika hakuwahi kuwa na mahusiano na mwanamke ya kimapenzi japo mara nyingi alikuwa akiingia kwenye vishawishi hivyo. Eric siku zote aliamini padre hutakiwa kuwa mtakatifu na kuwa kwa kazi ile ya uchungaji anayoitaka ambayo hairuhusu kuoa alijitahidi sana kutojiingiza kwenye mahusiano ya kingono.
Ibada ilikuwa ikiendelea lakini Eric akili yake haikuwa pale. Alishindwa kuelewa nini kinatokea akilini mwake, inakuwaje anashindwa kuzingatia ibada mara tu baada ya kumuona Lucia.Wakati hayo yakiendelea Lucia nae alikuwa akitafakari kuhusu Eric kumng’ang’ania mkono wake bila kumsemesha chochote. Hakuwa akimjua Eric na kama ni mwanafunzi wa u padre lakini nae akili haikumtulia.
Ilipofika muda wa watu kwenda kupokea sakramenti Eric aliwahi sana ili aweze kurudi mapema na kukaa kumtazama Lucia. Wakati Lucia akiwa anarudi ndipo Eric aliweza kumtazama vizuri na kwa umakini. Mapigo ya moyo ya Eric yalikuwa yakienda kwa kasi sana. Lucia nae bila kujua alimtupia macho Eric na kujikuta anapoteza hatua na kutaka kudondoka. Eric hakuweza kujizuia alichukua karatasi iliyokuwa ndani ya misale yake (Kitabu kinachoonyesha masomo ya siku hiyo) akaandika “Naitwa Eric ningependa kuongea nawe baada ya Ibada kama hutojali.Asante” alipomaliza alikikunja na kutafakari namna ya kumpa Lucia alieketi nafasi ya nyuma yake.
Wakati akitafakari ulikuwa umefika muda wa kutoa sadaka ya pili hivyo vikapu vya sadaka vilikuwa vikipita kwenye viti unaweka sadaka halafu unampa mwenzako nae akimaliza anampa mwengine hivyo hivyo. Eric akaona hapo ndio muda wa kupenyeza ujumbe wake.Alipokipokea kikapu akaweka sadaka kisha badala ya kumpa wa pembeni yake yeye akageuka akampa Lucia kikapu lakini mkono mmoja akiwa ameshika kile kikaratasi akamshikisha Lucia vyote. Haraka Lucia akang’amua kuwa ule ujumbe ulikuwa wake hivyo akaweka sadaka kwenye kikapu na kumpa wa pembeni yake na kubaki na ule ujumbe. Baada ya dakika kadhaa kupita kwa siri Lucia alifungua kile kikaratasi na kusoma ule ujumbe. Mapigo ya moyo yalimwenda mbio kwani alianza kuhisi nini kitafuata na yeye hakuwa akimjua mwanaume mpaka umri ule. Lucia ndio kwanza alikuwa amejiunga na Chuo kikuu mwaka wa kwanza shahada ya Sheria.
Wakati hayo yakiendelea padre Masunga alisimama na kutoa tangazo kuwa katika ibada ile wapo vijana waliopo seminari wanaosomea u padre na angependa waumini wawafaham kwani ndio mapadre wao wa kesho. Vijana watatu walisimama lakini Eric hakusimama. Hakusimama kwa makusudi kwani kwa anachotaka kuongea na Lucia hakutaka kabisa Lucia ajue kama yeye anasomea u padre. “Nilimwona Eric hapa amekaa wapi mbona simwoni kusimama” alikuwa ni padre Masunga akimwita Eric asimame huku akizungusha shingo kumtafuta alipokaa. Haraka Eric alisimama kwa aibu. Waumini waliwapigia makofi na kisha walikaa.
Baada ya ibada Eric alihitajika kwenda kuonana na padre lakini yeye alitoka haraka ili amuwahi Lucia pale nje. Alipofika nje alimwona Lucia akiwa anatoka nje ya kanisa na alianza kumsogelea ili amsalimie lakini alipomkaribia Lucia alimkwepa na hakupokea mkono wake aliokuwa ameunyoosha tayari kumsalimia Lucia. Eric aligeuka na kumuona Lucia akiingia ndani ya Land Rover Discovery series 4 likiendeshwa na baba yake kisha likaondoka. “Eric padre anakutafuta” ilikuwa ni sauti ya Stanley rafiki wa Eric na mseminari mwenzake ikimwita kumtaarifu kuwa padre Masunga ana mwita Sakrestia (Chumba wanachotumia padre kujiandaa kabla na baada ya ibada). Eric alishtuka na kuanza kukimbia kuelekea sakrestia.
the Legend☆

