JBourne59
JF-Expert Member
- Jan 17, 2020
- 941
- 8,569
JF huwa ni moja ya sehemu zangu za kujiburudisha hususani kwa ‘ID’ hii. Kwa kuwa nimepata muda kidogo wa kuandika na tarehe ya leo ni kumbukumbu yangu ya siku ya kuzaliwa, nimeona nianze kuwaletea simulizi iitwayo “Msegemnege”.
MSEGEMNEGE
Ni simulizi ya kubuni.
Haina uhalisia wowote.
---
Msegemnege
Tupio la I – Alex.
Alex alikuwa akiishi na wazazi wake nyumba za mamlaka ya bandari eneo la Masaki, Tour Drive, mita kadhaa kabla ya kufika Sea-Cliff Hotel. Lakini baada ya wazazi wake kufariki alifukuzwa kwenye nyumba hiyo ya Masaki, yeye na dada yake wakahamia uswahilini Manzese kwa ‘mfuga mbwa’ sehemu ambayo iliendana na hali yao wakati huo na palikuwa jirani na chuo alichokuwa akisoma Alex.
Alex ni kijana asiye na majivuno wala maringo hata wakati wa uhai wa wazazi wake ambao walikuwa wana ukwasi wa kutosha kibongobongo, hakuwa mtu mwenye kujikweza. Mama yake alikuwa mfanyakazi wa mamlaka ya bandari na baba yake alikuwa mfanyabiashara. Baba yake na mama yake waliuwawa katika tukio la ujambazi. Ujambazi ambao uliacha maswali mengi kwa kitengo cha upelelezi cha Polisi kwani kwenye gari waliokuwa wakitokea mjini kurudi nyumbani walishambuliwa eneo la makutano ya ‘tour drive’ na ‘Tumbawe road’ na katika upekuzi kwenye gari walilokuwa wakitumia marehemu, kulikutwa kiasi fulani cha hela kwenye droo ya gari pamoja na vitu vingine vya thamani kwenye kiti cha nyuma ikiwemo tarakirishi mpakato Hp moja na vishikwambi viwili aina ya ‘Surface’. Hii iliashiria kuwa halikuwa tukio la ujambazi wa kawaida bali kuna jambo lipo nyuma ya tukio hilo. Hii ilikuwa ni takribani miaka mitano iliyopita na upelelezi ulikuwa bado haujakamilika.
Alex alikuwa ni mtoto wa kiume pekee wa mzee Jonathan na Miriam ambao katika maisha yao ya ndoa walibahatika kupata watoto wawili, wa kwanza akiwa wa kike aitwaye Queen ambaye habari zake tutaziona huko mbele, lakini kwa upande wa Alex yeye alikuwa anapenda mambo ya urubani na kufanya wazazi wake wampeleke kuanza mafunzo ya urubani katika chuo cha Taifa cha usafirishaji (NIT) ambapo akiwa mwaka wa pili ndipo wazazi wake wakafariki na kukatisha masomo yake miezi kadhaa baadaye kwa kukosekana kwa ada na hela za kulipia mafunzo kwa vitendo.
Alex hakuwa na jinsi bali kujiingiza katika biashara ndogo ndogo za kimachinga. Aliuza vocha, akauza karanga, akauza viatu vya ‘kulenga’, aliuza matunda ya msimu ili mradi kila alichoona kinafaa yeye alifanya ili aweze kujikimu. Kwa kuwa alikuwa anapenda kusoma, alikusanya fedha na kudahiliwa tena chuo cha IFM kwa masomo ya usimamidhi wa fedha na kwa bahati nzuri alipata mkopo kwa asilimia mia moja. Pamoja na kusoma lakini pia hakuacha kufanya biashara ndogo ndogo akiwa Chuoni IFM.
Kama ilivyo kawaida ya vijana wa vyuo, Alex naye alikuwa na rafiki wa kike ambaye wanafahamiana kwa muda mrefu tangia Alex alipokuwa akiishi Masaki ingawaje alimuacha madarasa matatu nyuma wakati huo. Walipo kutana IFM wakaanzisha uhusiano wa kimapenzi na walikuwa wanapendana ingawaje sasa Alex hakuwa kama vile alivyokuwa wakati wazazi wake wakiwa hai. Alikuwa anavaa kawaida tu siyo kama zamani, hakuwa na chombo cha usafiri, kwa ujumla maisha yalikuwa ya kuunga-unga.
Miezi michache baada ya uhusiano wao, Emilia aliona bora atafute mwanafunzi mwingine ili aachane na Alex maana Emmy alikuwa na marafiki zake ambao mabwana zao walikuwa vizuri kiasi cha kumfanya Emmy kuanza kumdharau Alex licha ya kujua historia yake.
Siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa Emilia ndiyo ilikuwa chaguo zuri kwake kumuacha Alex mbele ya marafiki zake kwenye sherehe fupi iliyofanyika kwenye bustani ya moja ya Hotel Kubwa maarufu iliyopo jirani na hapo chuo.
Neema, Rachel, Margareth, Lidya, Zaituni na Laura ndio walikuwa marafiki wa Emilia ambapo tayari walikuwa viwanja vya Hyatt Regency pamoja na mabwana zao ambapo Emmy sasa alikuwa na bwana mpya aitwaye John.
SMS
“Alex, uko wapi?” – Aliandika Emmy
“Nipo Library” – Alijibu Alex.
“Chukuwa boda fasta njoo hapa Hyatt Regency Hotel” - aliandika tena Emmy.
“Dakika sifuri” – alijibu Alex asijue hili wala lile, kumbe maskini ndio anaenda ‘kupigwa kibuti mubashara’ mbele za watu.
Baada ya dakika chache Alex akawa Mapokezi pale hotelini, akamtumia text msg Emmy, “Upo room ipi mie nipo hapa receiption”
“Hapana sipo room, zunguka huku uwanjani kuna party fupi, umesahau leo ni birthday yangu?!”
Kutokana na mchanganyiko wa mambo tangia Alex apoteze wazazi wala hakuwa tena anakumbuka tarehe ya kuzaliwa ya Emmy. Hivyo ni kama alishtukizwa tu.
Alex akaenda moja kwa moja hadi huko uwanjani ambako alikuwa watu wakifurahi na kunywa huku kila mmoja akiwa amekaa na mpenzi wake ‘including’ Emmy.
Ghafla Emmy akamuacha John na kwenda kumpokea Alex na kumbusu kiaina na kumkaribisha kwenye party.
Hakuna katika rafiki zake Emmy aliyekuwa anajuwa kuwa Alex ameitwa ili apigwe kibuti mbele zao.
Watu walikuwa wanendelea kuburudika na vinywaji na mziki kwa mbali kisha sauti ikasikika…
“Jamani nina tangazo…” Emmy alisema.
“Nina furaha kutimiza miaka kadhaa leo (aliitaja) na kwamba leo ninatengana rasmi na Alex na kuanza rasmi uhusiano na John…”
Alex alipigwa na butwaa, akaachama mdomo wazi, na kupata ububu wa ghafla…
Rafiki zake Emmy wote nao wakashangaa na mmoja akasema…
“Emmy, unafanya nini !!??” – Zai alisema kwa kumshangaa Emmy.
Emmy naye akajibu kuwa ndiyo hivyo kama mlivyosikia, kisha akamfuata John na kumkumbatia na kumbusu.
Wakati huo Alex bado alikuwa ameduwaa asijue la kufanya huku mikono yake akiwa amejishika kichwa.
“We Emmy, kwa nini unamfanyia hivi Alex?, Alex anakupenda sana, na unajuwa jinsi anavyo kupambania, unajua fika kuwa pato lake sasa hivi ni dogo lakini amepambana na kukufanyia mengi makubwa na hivi karibuni amekununulia simu nzuri latest…” Alisema Laura.
“Simu ndio nini, kwa nini ning’ang’anie Samsung wakati nimepata Iphone, chukuwa lisimu lako hili…” Emmy alijibu na kumtupia simu Alex ambapo kwa kuzubaa ilimpiga kifuani na kuanguka chini.
Alex hakuiokota. Akageuka na kuanza kuondoka huku akiwa na mawazo tele.
---
Alex alitarajia kumuoa Emmy, ilikuwa ni faraja yake maana wanafahamiana kwa muda mrefu na kwamba Emmy alikuwa anajuwa historia ya Alex na hali aliyokuwa nayo mwanzo, hivyo Alex alidhani amepata wa kumfariji.
Aliondoka huku machozi yaki mlenga-lenga na alikuwa amejiinamia huku anatembea alitoka mle hotelini ili achukue bodaboda kuelekea IFM.
Huku nyuma Zai aliiokota ile simu na kuanza kuikagua…
“Mmmmh, lakini wewe Emmy wewe,…” alisema Zai.
“Wewe nini!, kama unamtaka wewe mfuate…” alimaliza Emmy.
Zai akaangaliana na bwana ‘ake kisha akamtupia tena maneno Emmy…
“Kumbe ulishaifuta kila kitu, lakini ona sasa umeipasua kioo…”
Emmy alionekana kuto kujali na kuendelea kugigida kinywaji na ‘party’ iliendelea japo si kwa muda mrefu tena baada ya pale.
Ilikuwa siku ya Ijumaa mida ya alasiri, Alex akiwa Hostel za IFM kwa rafiki yake Boniface, akiwa amejilaza kwenye kitanda akitafakali kilichotokea, mara ghafla meseji ikaingia kwenye simu yake. Hakutaka hata kuifungua…
Alimshirikisha Bony suala hilo na Bony alimtia moyo na kumshauri amfute moyoni mwake na ndio itakuwa tiba ya kuvunjika kwa moyo alikokupata baada ya tukio lile.
Bony ndiye aliyekuwa rafiki yake mkubwa Alex pale chuoni, na ‘alimbeba’ kwa malazi (hostel) siku amabazo Alex alikuwa hawezi kurudi nyumbani kwake Manzese.
Sasa kabla ya kumuaga Bon ili arudi home Manzese, aliamua kusoma ile sms na kukuta imeandikwa hivi…
Ndugu Alex Jonathan na bi Queen Jonathan, shauri lenu la mirathi limefikia hitimisho, hivyo mnatakiwa mfike bila kukosa Mhakama ya Mwanzo Sinza siku ya Jumatatu saa mbili asubuhi bila kukosa kwa ajili ya kukamilisha taratibu zingine. – Hakimu Mkazi, Mahakama ya Mwanzo Sinza.
Ghafla sura ya Alex ikakunjuka na furaha moyoni ikarudi, maana ni zaidi ya miaka minne shauri lao linazungushwa na Mahakama na hawakuwa na ‘connection’ wala fedha za kuhonga kitu kilichofanya shauri lao kupigwa kalenda kila siku wakienda na kisha ‘kupotezewa’.
Inaendelea…
MSEGEMNEGE
Ni simulizi ya kubuni.
Haina uhalisia wowote.
---
Msegemnege
Tupio la I – Alex.
Alex alikuwa akiishi na wazazi wake nyumba za mamlaka ya bandari eneo la Masaki, Tour Drive, mita kadhaa kabla ya kufika Sea-Cliff Hotel. Lakini baada ya wazazi wake kufariki alifukuzwa kwenye nyumba hiyo ya Masaki, yeye na dada yake wakahamia uswahilini Manzese kwa ‘mfuga mbwa’ sehemu ambayo iliendana na hali yao wakati huo na palikuwa jirani na chuo alichokuwa akisoma Alex.
Alex ni kijana asiye na majivuno wala maringo hata wakati wa uhai wa wazazi wake ambao walikuwa wana ukwasi wa kutosha kibongobongo, hakuwa mtu mwenye kujikweza. Mama yake alikuwa mfanyakazi wa mamlaka ya bandari na baba yake alikuwa mfanyabiashara. Baba yake na mama yake waliuwawa katika tukio la ujambazi. Ujambazi ambao uliacha maswali mengi kwa kitengo cha upelelezi cha Polisi kwani kwenye gari waliokuwa wakitokea mjini kurudi nyumbani walishambuliwa eneo la makutano ya ‘tour drive’ na ‘Tumbawe road’ na katika upekuzi kwenye gari walilokuwa wakitumia marehemu, kulikutwa kiasi fulani cha hela kwenye droo ya gari pamoja na vitu vingine vya thamani kwenye kiti cha nyuma ikiwemo tarakirishi mpakato Hp moja na vishikwambi viwili aina ya ‘Surface’. Hii iliashiria kuwa halikuwa tukio la ujambazi wa kawaida bali kuna jambo lipo nyuma ya tukio hilo. Hii ilikuwa ni takribani miaka mitano iliyopita na upelelezi ulikuwa bado haujakamilika.
Alex alikuwa ni mtoto wa kiume pekee wa mzee Jonathan na Miriam ambao katika maisha yao ya ndoa walibahatika kupata watoto wawili, wa kwanza akiwa wa kike aitwaye Queen ambaye habari zake tutaziona huko mbele, lakini kwa upande wa Alex yeye alikuwa anapenda mambo ya urubani na kufanya wazazi wake wampeleke kuanza mafunzo ya urubani katika chuo cha Taifa cha usafirishaji (NIT) ambapo akiwa mwaka wa pili ndipo wazazi wake wakafariki na kukatisha masomo yake miezi kadhaa baadaye kwa kukosekana kwa ada na hela za kulipia mafunzo kwa vitendo.
Alex hakuwa na jinsi bali kujiingiza katika biashara ndogo ndogo za kimachinga. Aliuza vocha, akauza karanga, akauza viatu vya ‘kulenga’, aliuza matunda ya msimu ili mradi kila alichoona kinafaa yeye alifanya ili aweze kujikimu. Kwa kuwa alikuwa anapenda kusoma, alikusanya fedha na kudahiliwa tena chuo cha IFM kwa masomo ya usimamidhi wa fedha na kwa bahati nzuri alipata mkopo kwa asilimia mia moja. Pamoja na kusoma lakini pia hakuacha kufanya biashara ndogo ndogo akiwa Chuoni IFM.
Kama ilivyo kawaida ya vijana wa vyuo, Alex naye alikuwa na rafiki wa kike ambaye wanafahamiana kwa muda mrefu tangia Alex alipokuwa akiishi Masaki ingawaje alimuacha madarasa matatu nyuma wakati huo. Walipo kutana IFM wakaanzisha uhusiano wa kimapenzi na walikuwa wanapendana ingawaje sasa Alex hakuwa kama vile alivyokuwa wakati wazazi wake wakiwa hai. Alikuwa anavaa kawaida tu siyo kama zamani, hakuwa na chombo cha usafiri, kwa ujumla maisha yalikuwa ya kuunga-unga.
Miezi michache baada ya uhusiano wao, Emilia aliona bora atafute mwanafunzi mwingine ili aachane na Alex maana Emmy alikuwa na marafiki zake ambao mabwana zao walikuwa vizuri kiasi cha kumfanya Emmy kuanza kumdharau Alex licha ya kujua historia yake.
Siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa Emilia ndiyo ilikuwa chaguo zuri kwake kumuacha Alex mbele ya marafiki zake kwenye sherehe fupi iliyofanyika kwenye bustani ya moja ya Hotel Kubwa maarufu iliyopo jirani na hapo chuo.
Neema, Rachel, Margareth, Lidya, Zaituni na Laura ndio walikuwa marafiki wa Emilia ambapo tayari walikuwa viwanja vya Hyatt Regency pamoja na mabwana zao ambapo Emmy sasa alikuwa na bwana mpya aitwaye John.
SMS
“Alex, uko wapi?” – Aliandika Emmy
“Nipo Library” – Alijibu Alex.
“Chukuwa boda fasta njoo hapa Hyatt Regency Hotel” - aliandika tena Emmy.
“Dakika sifuri” – alijibu Alex asijue hili wala lile, kumbe maskini ndio anaenda ‘kupigwa kibuti mubashara’ mbele za watu.
Baada ya dakika chache Alex akawa Mapokezi pale hotelini, akamtumia text msg Emmy, “Upo room ipi mie nipo hapa receiption”
“Hapana sipo room, zunguka huku uwanjani kuna party fupi, umesahau leo ni birthday yangu?!”
Kutokana na mchanganyiko wa mambo tangia Alex apoteze wazazi wala hakuwa tena anakumbuka tarehe ya kuzaliwa ya Emmy. Hivyo ni kama alishtukizwa tu.
Alex akaenda moja kwa moja hadi huko uwanjani ambako alikuwa watu wakifurahi na kunywa huku kila mmoja akiwa amekaa na mpenzi wake ‘including’ Emmy.
Ghafla Emmy akamuacha John na kwenda kumpokea Alex na kumbusu kiaina na kumkaribisha kwenye party.
Hakuna katika rafiki zake Emmy aliyekuwa anajuwa kuwa Alex ameitwa ili apigwe kibuti mbele zao.
Watu walikuwa wanendelea kuburudika na vinywaji na mziki kwa mbali kisha sauti ikasikika…
“Jamani nina tangazo…” Emmy alisema.
“Nina furaha kutimiza miaka kadhaa leo (aliitaja) na kwamba leo ninatengana rasmi na Alex na kuanza rasmi uhusiano na John…”
Alex alipigwa na butwaa, akaachama mdomo wazi, na kupata ububu wa ghafla…
Rafiki zake Emmy wote nao wakashangaa na mmoja akasema…
“Emmy, unafanya nini !!??” – Zai alisema kwa kumshangaa Emmy.
Emmy naye akajibu kuwa ndiyo hivyo kama mlivyosikia, kisha akamfuata John na kumkumbatia na kumbusu.
Wakati huo Alex bado alikuwa ameduwaa asijue la kufanya huku mikono yake akiwa amejishika kichwa.
“We Emmy, kwa nini unamfanyia hivi Alex?, Alex anakupenda sana, na unajuwa jinsi anavyo kupambania, unajua fika kuwa pato lake sasa hivi ni dogo lakini amepambana na kukufanyia mengi makubwa na hivi karibuni amekununulia simu nzuri latest…” Alisema Laura.
“Simu ndio nini, kwa nini ning’ang’anie Samsung wakati nimepata Iphone, chukuwa lisimu lako hili…” Emmy alijibu na kumtupia simu Alex ambapo kwa kuzubaa ilimpiga kifuani na kuanguka chini.
Alex hakuiokota. Akageuka na kuanza kuondoka huku akiwa na mawazo tele.
---
Alex alitarajia kumuoa Emmy, ilikuwa ni faraja yake maana wanafahamiana kwa muda mrefu na kwamba Emmy alikuwa anajuwa historia ya Alex na hali aliyokuwa nayo mwanzo, hivyo Alex alidhani amepata wa kumfariji.
Aliondoka huku machozi yaki mlenga-lenga na alikuwa amejiinamia huku anatembea alitoka mle hotelini ili achukue bodaboda kuelekea IFM.
Huku nyuma Zai aliiokota ile simu na kuanza kuikagua…
“Mmmmh, lakini wewe Emmy wewe,…” alisema Zai.
“Wewe nini!, kama unamtaka wewe mfuate…” alimaliza Emmy.
Zai akaangaliana na bwana ‘ake kisha akamtupia tena maneno Emmy…
“Kumbe ulishaifuta kila kitu, lakini ona sasa umeipasua kioo…”
Emmy alionekana kuto kujali na kuendelea kugigida kinywaji na ‘party’ iliendelea japo si kwa muda mrefu tena baada ya pale.
Ilikuwa siku ya Ijumaa mida ya alasiri, Alex akiwa Hostel za IFM kwa rafiki yake Boniface, akiwa amejilaza kwenye kitanda akitafakali kilichotokea, mara ghafla meseji ikaingia kwenye simu yake. Hakutaka hata kuifungua…
Alimshirikisha Bony suala hilo na Bony alimtia moyo na kumshauri amfute moyoni mwake na ndio itakuwa tiba ya kuvunjika kwa moyo alikokupata baada ya tukio lile.
Bony ndiye aliyekuwa rafiki yake mkubwa Alex pale chuoni, na ‘alimbeba’ kwa malazi (hostel) siku amabazo Alex alikuwa hawezi kurudi nyumbani kwake Manzese.
Sasa kabla ya kumuaga Bon ili arudi home Manzese, aliamua kusoma ile sms na kukuta imeandikwa hivi…
Ndugu Alex Jonathan na bi Queen Jonathan, shauri lenu la mirathi limefikia hitimisho, hivyo mnatakiwa mfike bila kukosa Mhakama ya Mwanzo Sinza siku ya Jumatatu saa mbili asubuhi bila kukosa kwa ajili ya kukamilisha taratibu zingine. – Hakimu Mkazi, Mahakama ya Mwanzo Sinza.
Ghafla sura ya Alex ikakunjuka na furaha moyoni ikarudi, maana ni zaidi ya miaka minne shauri lao linazungushwa na Mahakama na hawakuwa na ‘connection’ wala fedha za kuhonga kitu kilichofanya shauri lao kupigwa kalenda kila siku wakienda na kisha ‘kupotezewa’.
Inaendelea…