Simulizi: Msegemnege

Ndo maana una Uandishi mzuri Somo la Kiswahili sijui Fasihi umelisoma vizuri nawe umekuwa mwalimu 😂Umenikumbusha Secondary.
Asili yake ni neno SEGEMNEGE

Segemnege ni KIELEZI

Kielezi huelezea kitendo (KITENZI) jinsi kilivyo fanyika.

Mf.

Nourhan anatembea "taratibu"

Neno ANATEMBEA ni 'kitenzi' (kitendo)

Neno TARATIBU ni 'kielezi', kwa kwa mukhtadha husika anaelezewa jinsi Nourhan anavyotembea.

Msegemnege ni vivyohivyo kielezi, na maana yake kwa maneno mengine ni 'Shaghalabaghala', 'a~bila mpangilio', 'hovyo hovyo', nk.

---

Tangia alivyomuacha mke wake wa kwanza, mambo yake yanaenda segemnege.

---

Simulizi hii ni msegemnege

(m) hapo nimeongezea kuvunisha tu!

Kama vile baadhi ya watu wa Tanga, Mombasa na Zanzibar wavumishavyo maneno...

mf.

Meli => Jimeli...
Honda => Jihonda...

kama vile baadhi ya watu wa kanda ya ziwa wavumishavyo maneno...

mf.

Baiskeli => Libaiskeli
Moyo wangu umekudondokea => Limoyo langu limekudondokea

Kama vile watu wa kanda ya magharibi wavumishavyo maneno kwa kudunisha...

Hela => Kahela

Simu yake nzuri => kasimu kake kazuri.

Bila kuwasahau baadhi ya watu wa nyanda za juu kusini...

Sanduku => Gusanduku

Nyumba kubwa => Gunyumba gukubwa

Nk

___
Bila shaka umepata mwanga.
 
Sasa Kuna ubaya gani kuuliza swali
Simulizi ya kubuni haina uhalisia hivyo kulikuwa hakuna haja ya kuuliza unasoma unamezea kwakua ni simulizi sio uhalisia.
 

Attachments

  • Screenshot_20230703-161747.jpg
    Screenshot_20230703-161747.jpg
    152.7 KB · Views: 50
Shuleni kiswahili darasa zima kilikuwa kinatupa tabu.

Tuliathiriwa na muingiliano wa lugha (lahaja) nne hivi kwa wakati mmoja kwa eneo moja.

Kitaturu, Kisukuma, Kinyiranba, Kinyisanzu.

Wakati mwingine walimu ilikuwa inabidi wachanganye na kilugha kidogo tupate kielewa.

R. I. P. Mwl. 'Gudu' & Igumi.

Walitujenga sana.

Kiswahili kilianza kunyooka nilivyoenda Lindi hahahhaaa

Lakini nikaathirika tena na herufi 'N'

Lakini nilipoanza kuishi Dar ndio kikaanza kukaa sawa, neno juzi nikawa nalisema juzi badala ya jjjuzi hahahahha.

Maisha haya!

Ukanda wa Pwani ukanyoosha kiswahili changu ingawaje bado si sanifu kivile.
 
Happy Birthday.

Ukisoma unaona maisha ya watoto baada ya wazazi kufariki.

Hasa kifo kama hicho ambapo watoto wote walikuwa bado hawajaweza kusimamia kwa miguu yao.

Na usumbufu wa mahakama ni tatizo lingine

Nitarudi kuendelea kusoma.

Keki ni wapi huko?
Maisha ya uyatima ni tabu sana hususani wasimamizi wa mirathi wakiwa wenye kudhulumu.
 
Tupio la IX - Omari

“Ilikuwa, siku ya Jumanne, asubuhiii,
Nataka kwenda kaziniii,
Ulipotamka neno kuwa, umechokaaa,
Kuishi na mimiii!

Kosa gani, ewe Faulataaa,
Sikupata jibu lingiineee,
Ila, sikutaki eee,
Sikutaki tuuu!

Kuchunguza, kuchunguza, kumbeee,
Umempata bwana awezaye kumiliki maisha yakooo,
Kunishinda mimiii!

Ama kweli ooo,
Maradhi yote ugua,
Lakini kuchacha,
Usiombeeee!...”


Yalikuwa maneno yamtokayo kijana Omari akiimba wimbo huku akitembea ufukweni kandokando ya bahari ya Hindi eneo la Kawe Dar es Salaam.

Omari ni mtoto wa uswahilini Ukwamani Kawe, amezaliwa Lugalo na kukulia hapo Ukwamani. Hakubahatika kuendelea na masomo ya sekondari baada ya kumaliza shule ya msingi Mzimuni iliyopo Kawe miaka mitatu iliyopita hivyo alikuwa akijishughulisha na kazi za ‘deiwaka’ maeneo ya ufukweni kwa Kawe beach club hadi maeneo ya Msasani beach.

Wazazi wake wote wawili wapo hai, baba mwanajeshi na mama anajishughulisha na kuuza ‘genge’ nyumbani kwao maeneo ya Ukwamani. Kutokana na pato dogo la wazazi wake na maisha yao kwa ujumla Omari hakutaka kwenda Sekondari bali alitamani kazi ya Daladala. Baba yake alikuwa mlevi wa kupindukia, hata kazini kwake wanamstahi tu kwakuwa amebakisha mwaka mmoja kustaafu akiwa na rank ya ‘lance corporal’ (V moja).

Huenda ilikuwa ni stress ya kutopata watoto wengine licha ya jitihada nyingi na minong’ono hapo mtaani kwake inasemekana hata huyo Omari ni mtoto wa askari mwenzie.

Omari alijiegesha kwenye daladala moja itokayo Kawe kwenda Mtongani lakini baada ya miezi michache daladala hiyo uliuzwa na kufanya awe mpiga debe kwa muda mrefu na hatimaye akaamua aishie kufanya kazi za ufukweni mwa bahari.

Tayari Omari alikuwa ameanza kujihusisha na masuala ya mapenzi kama ilivyo kwa watoto wengi uswahilini wa umri huo, na siku chache zilizopita aliachwa na mpenzi wake binti wa mtaani kwao kwa sababu ya ufukara wake hususani baada ya kuacha kazi ya daladala.

Wimbo huo wa ‘Kuchacha kubaya’, ulioimbwa na Juwata Jazz Band, uilikuwa unamfariji Omar wakati akirandaranda ufukweni akisubiri ‘vyombo’ virudi kutoka kuvua samaki ili apate ‘deiwaka’ mbalimbali ikiwemo kubeba samaki, kuwaadaa samaki kwa ‘kuwapaa’ na kuwatoa utumbo tayari kwa kupewa mteja wa rejereja kama kitoweo nk. Sasa kwa bahati siku hiyo maji yalikuwa ‘yametoka’ na sehemu kubwa ya ardhi ya bahari ilikuwa kavu (kavu ile ya ubichi-bichi wake na maji sehemu sehemu). Sasa vyombo vilikuwa vinaishia mita kadhaa kutoka ufukweni, jambo liliowafanya wateja na wadau mbalimbali kuvifuata vyombo huko huko na kufanya ‘uchuuzi’.

Sasa wakati Omari naye akielekea kufuata chombo kilichofika muda si mrefu, ndipo alipoona kitu kama chupa ndogo hivi iliyofungwa vema. Chupa hiyo ilikuwa inaelea kwenye ‘kidimbwi’ cha maji yaliyo ‘kupwa’.

“Hee!” alishangaa Omari.

“Sijui kichupa gani hiki mbona kipo hivi…” alijiuliza.

Kichupa kile kilikuwa cha kuhifadhia kinywaji baridi lakini mtindo wa chupa ile ilikuwa ni nadra sana kupatikana nchini.

“Isije ikawa ni chupa zile za majini (viumbe) kama kwenye simulizi mbalimbali za kale…” alijisemea huku akikiokota.

Kwa kuwa ilikuwa chupa yenye kuangaza (transparent), aliweza kuona ndani kuna nini…

“Mmmh, kuna karatasi, sijui imeandikwa nini, ngoja kwanza niwahi kazi nitaifungua baadaye…” alijisemea na kukiweka katika kikapu cha ‘ukindu’ alichokuwa nacho.

Omari aliendelea na kazi na kusahau kufungua kile kichupa hadi jioni alipokuwa anafunga kazi na kuandaa kitoweo alicho ‘tomoa’ kwa wavuvi ili apeleke nyumbani.

Kitendo cha Omari kuwa kila siku analeta kitoweo aina ya samaki nyumbani ilifanya mama yake apate unafuu kwa kuwa mumewe pesa zote alikuwa akimalizia kwenye madeni ya pombe, isingekuwa kupewa maelekezo ya kuchukuwa posho ya chakula kila siku fulani ya mwezi pale kambini, hali yao ingekuwa mbaya zaidi. Hivyo Omari alikuwa na jukumu kubwa la kutafuta fedha na kumsaidia mama yake pale nyumbani. Na bado yeye alikuwa akiishi hapo hapo kwa mama na baba yake, nyumba ambayo walifanikikiwa kuinunua mara baba yake alivyopata marupurupu baada ya kutoka Sudan kwenye fatiki maalum wakati huo.

Wakati akiendelea kuwaandaa samaki wake ndipo alikiona kile kichupa na akakichukuwa ili kukiangalia vizuri.

“Kumbukaa ee Faulata,
Kila mpanda ngazi hushukaaa,
Usidanganyikeee, usidanyanyikee ooo wee dada…”


Mrindimo wa wimbo ule alioamka nao tangia asubihi akiimba na kujifariji ukamrudia na akawa anauimba kwa kwa sauti ya chini kama kawaida yake huku akiendelea kuiangalia ile chupa kabla ya kuifungua…

“Nisikilize kwa makini,
Haya ninayo kuambiaa,
Kuibuka na kuchacha eee,
Mola ndio mpangaji wa yote…”

“Ama kweliooo, maradhi yote uguaaa, lakini kuchacha usiombeee”

“Ngazi hiyo wamepanda wengi,
Na sasa wameshukaaa,
Nakuruhusu uendeee
Utaiona Duniaaeee…”

“Ama kwelioo, maradhi yote uguaa, lakini kuchacha usiombeee”


“Umekuwa mzigo wa moto,
Haubebeki wala haushikiki,
Nakuruhusu uendeee
Utaiona Duniaaeee…”

“Ama kwelioo, maradhi yote uguaa, lakini kuchacha usiombeeee”


Aliendelea kuimba huku akimalizia kwa kuigiza mirindimo ya gitaa ya ‘solo’, mara ‘ridhim’ mara ‘trumpet’ mara ‘saxafone’ ilimradi tu apate ladha anayoitaka katika kujifariji.

Wakati akiichunguza ile chupa kwa makini, huku akiwa na wasiwasi asije akaokota chupa yenye Jini ndani yake ndio akaona karatasi nyeupee iliyofunga kwa ustadi na akawa ana shauku ya kutaka kuona nini kimo ndani ya ile karatasi.

Akafanya hima kumaliza kazi ya kuwaadaa samaki wake kisha akarudi hadi kwao uswahilini Ukwamani na kumkabidhi mama yake samaki wale, kisha akasafisha kapu lake kama kawaida na akaingia chumbani kwake na kuifungua ile chupa…




Inaendelea…
 
Tupio la X - Zawadi

Ilipoishia

Alipotoka nje ya mlango wa chumbani kwake, Vai Kwa mbali aliona mtu mzima mwamamke akiwa amejitanda khanga akitoka, lakini aliona mgongo tu na wala hakusikia vishindo vya nyao za kutembea, na kabla ya yule mtu tupotelea mlangoni aligeuka nyuma na wakakutanisha macho…


Sasa endelea…


La haula, ilikuwa ni sura ya mama yake…

“Mama!” aliita Vai kwa sauti ya juu…

Yule mama alirudisha uso wake mbele na kutokomea kupitia mlangoni pasi na mlango kufunguliwa.

Sauti ile ya Vai ilimfanya mama Rose kushtuka kutoka usingizini na kuamka na kuja kwenye ‘korido’ ya nyumba ambako ndipo sauti ile iliposikika ikitokea..

“Kuna nini mama Junior!” Aliuliza mama Rose alipmuona Vai akiwa amesimama na kuduwaa…

Vai akanyoosha tu mkono kule mlangoni huku akisema mama! Huku akiwa Analia…

“Hebu tulia kwanza, nini kimetokea na kwa nini usiku huu uka hapa ‘ukumbini’ peke yako, mtoto yuko wapi?!” Mama Rose aliuliza mfululizo akiwa na shauku ya kutaka kujuwa kulikoni.

Alipotulia, Vai alianza kuelezea…

“Nilifanya maombi ili Mungu anioneshe huyo kiumbe anayekuja kumbadilisha nepi mtoto mimi nikiwa nimepitiwa na usingizi, na leo ndio nimemuona…” alisema Vai akiwa bado amesimama.

“Hebu twende sebuleni kwanza tukae unieleze vizuri.” Mama Rose alisema.

“Ni sura ya mama! Ni mama kabisa yule…” alisema Vai huku akiwa na kwikwi ya kulia

“Mtoto yuko wapi?” Mama Rose alirudia swali la awali.

“Junior yupo ndani amelala, na amebadilishwa nepi na zingine zimefuliwa, zimewekwa kwenye besini…”

“Enhe!?” alichagiza mama Rose kutaka kujua zaidi…

“Ndio, nimeona sura ya mama, nilikuwa nimelala, nimepitiwa na usingizi, lakini kwa bahati nzuri nikashtuka ili nimkague mtoto asije akawa amejilowesha sana, ndio nikagundua nepi ni kavu kabisa, nilipoangalia kwenye beseni, nikakuta nepi zote chavu zimefuliwa, na wakati huo huo nilisikia sauti kama ya mlango ukijifunga ndipo kwa haraka nikatoka kuja ukumbini kuangalia ni nani …” alimeza mate kisha akaendelea…

“… ndio nikamwona mtu mwanamke amejitanda ushungi wa khanga na akitembea bila kishindo chini kuelekea kule mlango wa kutokea nyuma ya nyumba, sasa kabla ‘hajaishia’ si akageuka kuniangalia…”

“Enhe!” mama Rose alichagiza…

“Ndio tukakutanisha macho na nikaona sura ni ya mama, yani mama yangu kabisa bi Mariam…” Vai alianza kulia tena…

“Basi mama Junior usilile, hebu nyamaza na simama tusali…” Alisema mama Rose kwa sauti ya kumfariji.
---

Mwanzo wa kadhia ya maajabu haya, Vai alidhani ni mpangaji wake ndio ana mauza uza hayo, lakini baada ya uchunguzi wake akajiridhisha pasi na shaka kuwa si yeye mama Rose mwenye kuleta mauza-uza hayo.

Walianza kuimba nyimbo za ‘kuabudu’ kisha wakaanza kusali na kuomba kwa ‘kukemea’, ingawaje walikuwa hawapayuki.

Walitumia muda mrefu katika maombi hayo hadi mtoto Rose alipokuwa akilia na kuita mama, mama!

Walihimitisha ibada yao hiyo ya dharura kisha kila mmoja alirudi chumbani kwake kuendelea kuutafuta usingizi maana bado kulikuwa hakujacha.

“Inakuwaje nione sura ya mama wakati yeye nilishamzika…” Alijiuliza Vai wakati anajaribu kuutafuta usingizi ‘uliopaa’.

“Au ni Malaika katika sura ya mama…!” aliendelea kujiuliza

“Au ni mizimu wa mama!?”

“Au ni mchawi aliyejigeuza sura kuwa kama ya mama?!”

“Au ni Pepo lililojivesha sura ya mama!?”

Aliendelea kutafakari weee hatimaye usingizi ukampitia hadi asubuhi aliposikia Junior akilia kwa kutaka kunyonya.

Akampatia haki yake na yeye akaendelea kulala na akapitiwa na usingizi mzito hadi kukakucha kabisa.
---


Asubuhi hiyo wakati mama Rose akifua na Vai akianika nepi za mwanawe, wakamwona yule binti aliyekuja siku ile katika Kanisa la mama Mchugaji.

Ilikuwa siku ya Jumapili ambapo kwa kuchelewa kuamka kwao walipanga waende misa ya pili Roman kisha jioni waende kule KKKT badala ya kwa mama Mchungaji.

“Shikamoo!” ilikuwa sauti ya yule binti.

Alikuwa amevaa nguo safi tu ila zimefubaa, hali iliyomtambulisha kuwa ametoka katika familia isiyojiweza kifedha. Sauti yake ilikuwa nyembamba kama ilivyo kwa mabinti ambao hawajavunja ungo.

“Marhaba” walijibu kwa pamoja kisha mama Rose akasema…

“Karibu binti, karibu ndani…”

Yule binti akajibu… “Asantee, lakini nitakaa hapa hapa nje, si mlikuwa mnataka kwenda kanisani, basi twendeni wote…”

Mama Rose na mama Junior wakaangalina kisha mama Junior akasema…

“Sisi tumechelewa leo na tulipanga tuende kule Roman misa ya pili halafu baadaye ndio tuende kanisa la wokovu…”

Yule binti akasema… “Sawa, basi nawasubirini, lakini nilikuwa nataka niwaoneshe kitu…”

Mama Rose, akamuuliza…

Kwani wewe unaitwa nani? Mtoto wa nani na unatokea maeneo gani?

Wakati huo Vai alikuwa ameingia ndani kumchukulia kigoda yule binti ili apate kuketi.

Kabla yule binti hajaanza kujibu maswali, Vai alikuwa amesharudi na kumkaribisha…

“Karibu ukae, sisi tunamaliza sasa hivi, eee ulisema unataka kutuonesha kitu!?...”

Yule binti akaketi kisha akaanza kusema…

“Mimi naitwa Zawadi, natokea nyumba ya tano kutokea hapa, siyo mwenyeji sana huku, nililetwa wiki ile ambayo Jumapili yake nikaja Kanisani, nimeletwa kuja kumsaidia dada kazi za ndani maana yeye ana mtoto mchanga…”

“Dada yako anaitwa nani? Na uliletwa kutokea wapi?..” Mama Rose alimuuliza tena…

“Dada anaitwa Mama Rajabu na mimi kwetu ni Iringa Gangilonga, dada na mume wake wao kwao ni Tanga…”

Vai na mama Rose wakaangaliana kisha mama Rose akasema…

“Aaa kumbe unakaa kwa mama ustadhi…!!!” kisha akaendelea..

“Kwa hiyo mama ustadhi sio ndugu yako kabisa…!?”

“Eee, siyo dada wa kuzaliwa, ila namwita tu dada…”

Mama Junoir akashusha pumzi na kumuuliza…

“Sasa mbona siku ile ulinipa mtoto kisha ukaondoka Kanisani bila hata kuaga?”

“Niliaga mbona na wote mliitikia?” alijibu Zawadi.

Mama Rose na Vai wakaangaliana tena kisha wakaguna kwa ndani ndani.

“Eee ulisema unataka utuoneshe kitu, kitu gani hicho?...” Vai aliuliza na wakati huo alikuwa ameshamaliza kazi zake za udobi.

“Ndiyo, nilitaka niwaoneshe kitu Kanisani kule kwa mama mchungaji…” alijibu Zawadi.

“Hebu ngoja kwanza…” Vai alisema, kisha akamshauri Mama Rose akaoge yeye kwanza wakati wao wanakunywa chai kisha akitoka bafuni nay eye Vai aende kujimwagia maji.

Wakaingia ndani kupata kifungua kinywa…

Baada ya mama Rose na Vai wote kuwa wameoga kukawa na mazungumzo ya pamoja na yule mtoto.

Zawadi aliwaeleza kuwa alidhani wanaenda kule Kanisa la mama Mchungaji ili awaoneshe kitu lakini kwakuwa tayari walishapanga ratiba zao basi aliamua awasubiri ili waende wote huko Roman.

“Eti, mama Rose, au twende tu na huyu binti kule kwa mama Mchungaji!?..” Vai aliuliza… kisha mama Rose akasema…

“Ingawaje tumechelewa lakini bado watakuwa wanaendelea na ibada, si unajuwa wale wanachukuwa muda mrefu hadi kumaliza, basi tujiandae twende…”

Baada ya muda mchache wakawa tayari na watoto wao kisha wakafunga milango ya nyumba na kuanza safari ya kwenda Kanisani kwa mama Mchungaji…


Itaendelea…
 
Tupio la XI – The Jonathan Company Limited

Ilipoishia


Kikao kilihitimishwa kwa sisi kupewa ‘business card’ za Mheshimiwa Jaji, Gavana na Afande nasi tukawapa namba zetu ambapo walizisevu moja kwa moja kwenye simu zao na Hakimu alisisitiza baada ya wiki moja tusikose kufika NMB makao makuu kwani huku kuna kila kitu chetu na kwamba atafuatilia kujua kama kuna changamoto yoyote tutakayopata.

Sasa endelea…

Siku zilipita, na hatimaye ikafika Jumatatu ambapo ndio ilikuwa siku ya kwenda benki. Queen na Alex walikuwa wamejiandaa vyema kwa changamoto yoyote itakayo jitokeza kule benki na wote siku hiyo walikuwa wamevalia nadhifu baada ya Queen kumlazimisha sana Alex anunue nguo mpya na Queen alisimamia hilo.

Kutokea dawati la huduma kwa wateja, walipokelewa vizuri na kueleza shida yao ya kutaka kumuona meneja wa wateja, wakaambiwa wasubiri kwenye viti kwani wakati huo meneja husika alikuwa ana mgeni ofisini kwake.

Baada ya kusubiri kama nusu saa hivi tukaitwa.

Alex anaelezea…

Tukaoneshwa mlango wa kuinga na tukakaribishwa na meneja huyo kwa tabasamu zuri.

“Karibuni niwasaidie…” alisema yule dada Meneja

Queen tulikubaliana kuwa yeye ndiye atakuwa mzungumzaji mkuu hadi pale yeye akitaka mimi niongee ndipo niseme kitu…

“Ahsante dada, mimi naitwa Queen Jonathan na huyu hapa ni ndugu yangu anaitwa Alex Jonathan…” Alisema Queen.

“Oooh, karibuni sana, hebu subiri kidogo…” akaitikia yule meneja kana kwamba alikuwa anafahamu kitu kisha akainua simu yake ya mezani.

“…Boss, Jonathan Company is here…, Okay, okay, yes, in a second.” Akakata simu.

Aliongea yule Meneja kwa kunong’ona sana kiasi kwamba usipokuwa makini huwezi kujua hata ameongea kitu gani kisha akatuambia tumfuate naye akanyanyuka na kutuongoza katika ofisi nyingine…

Nilibahatisha kusoma mlangoni wakati tunaingia maana mimi nilikuwa wa mwisho kuingia tukitanguliwa na Meneja aliyetuongoza akitumia kitu kama kadi hivi kuruhusu milango kufunguka, tukapitia kwenye sehemu kuna ‘scanner’ ya mwili na kuturuhusu kuendelea…

“DCEO Corporate Banking” ni maandishi niliyoyasoma pale mlangoni. ..

“Karibuni..” Alisema yule dada Meneja aliyetuongoza…

“Sir, here is Mister Alex and Miss Queen...” aliongea tena yule dada meneja kisha akatugeukia na kutuambia suala letu litashughulikiwa hapo.

“Karibuni vijana, eee, mimi naitwa (akataja jina) ni msaidizi wa CEO …” akavuta droo na kutoa folder lenye mafaili kadhaa na kisha akawasha tarakilishi yake ya mezani na kuanza kubofya.

“Ahsante, mimi naitwa Queen Jonathan na huyu mdogo wangu anaitwa Alex Jonathan…”

“Nashukuru kuwafahamu, na habari zenu ninazo, karibuni sana.” Tukaitikia pale wote “Ahsante”

Sekunde chache mlango wa ofisi ile ukafunguliwa na akaingia dada aliyevalia sare maalum akituletea chai.

Ofisi ilikuwa kubwa, nzuri yenye hadhi ya kuitwa ofisi ya CEO.

“Karibuni, kuna chai, kahawa, maziwa, milo na cocoa…” alisema yule dada mhudumu huku akisubiri majibu yetu ili ajue ataandaeje…

“Nipatie Kahawa ya maji pekee…” alisema dada

“Nami nipatie maziwa yenye cocoa…” nilisema.

Tukamiminiwa viywaji vyetu pale na tukaanza kunywa tukisindikizia na sambuza ndogo ndogo nzuri na biskuti.

“Nipatieni vitambulisho vyenu vya Taifa…” alisema yule DCEO. Nikatoa changu na kumpa dada ambaye yeye ndiye akasimima kumpelea DCEO yule ambaye meza yake ilikuwa mita tatu hivi kutoka tulipokuwa tumeketi.

Hali ya ubaridi mkali mle ndani na utulivu uliokuwepo ilifanya nihisi njaa ya chai kuliko kawaida kitu kilichopelekea kujiongezea maziwa na kuweka milo na kahawa kwa pamoja safari hii.

“Queen, njoo uweke kidole hapo kwenye biometric (finger print reader)” alisema yule DCEO na pia ikawa hivyo ilipofika zamu yangu.

“Well well, sasa nimesha thibitisha kuwa ninyi ndio wahusika halisi katika suala hili,… malizeni kunywa chai kisha mnijulishe tuendelee…” alisema tena.

Kwa hamu tuliyokuwa nayo tukamaliza fasta chai na dada akasema…

“Tupo tayari baba”

DCEO akasimama na kutuamuru tumfuate ambapo tuliingia chumba kingine hapo hapo na ilionekana ni chumba cha mikutano kwa mandhari ya mpangilio wa meza, viti, sehemu ya ‘presentation display’ nk.

“Karibuni sana, hiki ni chumba cha mikutano yangu na wateja, hapa sasa tutaelewana vizuri…”

Akabofya kuwasha tarakilishi mpakato ilikuwepo pale meza kuu na ‘boom’, display ikaonekana kule kwenye ubao maalum ukutani.

DCEO akaanza kuongea…

“Eeee kuna mirathi yenu katika benki yetu lakini pia katika sehemu nyingine kama wosia unavyosema…”

“Awali ya yote poleni sana kwa kupoteza wazazi wenu…”

Aliendelea kuongea pale wee huku sisi tukisikiliza kwa makini, aliongea kwa kusoma wosia sentesi kwa sentensi na mgawanyo wa mali. Ajabu ni kwamba wasia ambao sisi tulisomewa mahakama ya mwanzo ulikuwa mfupi tofauti na huu ambao tulikuwa tunauona kwa macho yetu jinsi ulivyoandikwa kwa hati ya baba. Aidha mirathi kwa upande wa mama haukuwa mrefu zaidi ya mgawanyo tu wa hela zilizokuwa benki kwenye akaunti yake.

Sehemu ya wosia wa baba ilikuwa inasomeka hivi…

- Pesa zilizopo benki ya CRDB (TZS & UDS), NBC (TZS) , EXIM (USD) pamoja na STANBIC Bank (EURO & USD) zote zihamishiwe kwenye benki ya NMB, kisha zifunguliwe akaunti mbili (Corparate) moja ya Queen Jonathan Ngonyani na nyingine ya Alex Jonathan Ngonyani ambapo akaunti hizo ziwe za USD pekee. Jumla ya fedha hizo mpaka naandika wosia huu ni ka ifuatavyo:-

CRBDTZS - 79,xxx,xxx
CRDBUSD - 563,xxx
NBCTZS - 894,xxx,xxx
EXIMUSD – 270,xxx,xxx
STANBICUERO – 355,xxx
STANBICUSD – 350,xxx

-Pesa zilizopo benki ya NMB akaunti ya biashara zigawanywe nusu kwa nusu kisha wapewe Queen Jonathan Ngonyani na Alex Jonathan Ngonyani wafunguliwe akauti za biashara, hadi naandika wasio huu jumla ya yake zipo TZS 1,832,xxx, xxx/- pia washauriwe wafungue akaunt za akiba NMB ambapo waweke fedha kiasi.

Kuna hisa katika makampuni matatu ambapo hisa hizo zigawanywe nusu kwa nusu kisha umiliki uhamie kwa majina ya Queen Jonathan Ngonyani na Alex Jonathan Ngonjani :-
  • Kampuni ya uwekezaji A 3%
  • Kampuni ya mtandao wa simu A TZ 5%
  • Kampuni ya uwekezaji B 1%
DCEO yule alikuwa anatusomea taratibu ili tuelewe na huku sisi wenyewe tukiona maandishi yenye hati ya baba yetu yakipita kwenye display iliyokuwepo mbele…

Wasio ulikuwa mrefu na wenye maelekezo na maelezo mengi, sote mimi na dada tulikuwa tunastaajabu utajiri ambao baba alikuwa nao na wala hatukujuwa wala hakuonesha kuishi katika hali ya ukwasi kiasi kile.

Moyoni tukiwa na furaha, lakini na maswali yasiyo na majibu pia kichwa tuliendelea kufuatilia maelezo ya DCEO.

“Eee kwa jinsi hiyo, yote hayo, kwa maana ya mgawanyo wa mirathi kwa upande wa baba yenu na upande wa mama yenu yameshafanyika, na akaunt zenu zitakuwa tayari punde si punde…” kisha akabofya kitufe fulani na baada ya dakika chake akaingia afisa mmoja wa benki, tulimtambua kwa sare zake, alikuja na camera na atakupiga picha kisha akaondoka.

Alituonesha pia pesa zilizokuwemo kwenye benki yake NMB, ambapo zilitofautiana kidogo na zile zilizomo kwenye wosia kwa kuongezeka kila akaunti. Pia akapiga simu kwenye benki zingine zenye akaunti za marehemu na kuomba apatiwe statement kwa mujibu wa amri ya mahakama kama tulivyomsikia akiongea, ambapo punde si punde zilikuja ‘printout’ kutoka kwenye printer na soft copy zilionekana kwenye display, nako hapakuwa na mabadiliko ya viwango vya fedha kama ilivyooneshwa kwenye wosia.

“Received, reeived received… proceed with bank transfer as ordered by BoT, you may check authentic of the source…, okay, …, Okay, transfer confirmed…”

Aliongea yule DCEO kwa lugha zao za kibenki wakifanya miamala ambayo sasa tulijuwa inaingia kwenye akaunt zetu.

“Kama mnavyosikia, hela zenu zote zinahamishiwa hapa, kisha ninyi mtakuwa huru kufungua akauti sehemu nyingine katika benki yoyote, lakini kwanza tulitaka kulimaliza zoezi hili mara moja ili muanze umpya mkiamua, lakini itakuwa vyema tukiendelea kufanya kazi nanyi Jonathan Company.

Siku hiyo ndio tulijua kuwa marehemu baba alikuwa ana ‘Private Company’ iitwayo Jonathan Company Ltd iliyokuwa inajishughulisha na mambo mbalimbali kama tulivyoonesha Memorandum and Article of Association ya kampuni hiyo na hisa zote za kampuni hiyo iliamriwa na wosia ziende kwa dada Queen.

Hadi inafika saa tisa alasiri tulikuwa tayari tumeshakabidhiwa kadi zetu za Corporate, fedha kiasi tulihamishia kwenye akaunti za akiba ambazo sote mimi na dada Queen tulikuwa nazo za hapo NMB na zoezi la uhamishaji umiliki wa kampuni Queen aliambiwa aende Brela kwa ajili ya kukamilisha utaratibu, na kuhusu hisa za uwekezaji katika kampuni alizowekeza baba ilibakia kipengele cha kuweka sahihi tu.

Alituruhusu kwenda mapumziko mafupi lakini alitutaka turudi tena benki baada ya saa moja…

“Saa kumi mrudi hapa, milango itakuwa imefungwa kwa wateja waliopo nje lakini mkifika waonesheni walinzi hizo kadi zenu mpya mtafunguliwa, kuna sehemu nataka niwasindikize…”

Tulitoka mle ndani tukiwa hatuna hata njaa, sijui kwa sababu ya ile chai nzito ama kwa sababu ya utajiri wa ghafla ili mradi tulikuwa na furaha na tulitembea kuelekea restaurant ya jirani kupata chakula cha mchana.

“Dada mimi sisikii njaa hata!” Nilisema wakati tunaingia cafeteria fulani iliyopo kwenye kituo cha kuuzia mafuta.

“Hata mimi Alex, sisikii njaa japo nilionja tu ile kahawa na sambusa kidogo” tukacheka kiasi na kuketi mle mghahawani.

Itaendelea...
 
Tupio la XI – The Jonathan Company Limited

Ilipoishia


Kikao kilihitimishwa kwa sisi kupewa ‘business card’ za Mheshimiwa Jaji, Gavana na Afande nasi tukawapa namba zetu ambapo walizisevu moja kwa moja kwenye simu zao na Hakimu alisisitiza baada ya wiki moja tusikose kufika NMB makao makuu kwani huku kuna kila kitu chetu na kwamba atafuatilia kujua kama kuna changamoto yoyote tutakayopata.

Sasa endelea…

Siku zilipita, na hatimaye ikafika Jumatatu ambapo ndio ilikuwa siku ya kwenda benki. Queen na Alex walikuwa wamejiandaa vyema kwa changamoto yoyote itakayo jitokeza kule benki na wote siku hiyo walikuwa wamevalia nadhifu baada ya Queen kumlazimisha sana Alex anunue nguo mpya na Queen alisimamia hilo.

Kutokea dawati la huduma kwa wateja, walipokelewa vizuri na kueleza shida yao ya kutaka kumuona meneja wa wateja, wakaambiwa wasubiri kwenye viti kwani wakati huo meneja husika alikuwa ana mgeni ofisini kwake.

Baada ya kusubiri kama nusu saa hivi tukaitwa.

Alex anaelezea…

Tukaoneshwa mlango wa kuinga na tukakaribishwa na meneja huyo kwa tabasamu zuri.

“Karibuni niwasaidie…” alisema yule dada Meneja

Queen tulikubaliana kuwa yeye ndiye atakuwa mzungumzaji mkuu hadi pale yeye akitaka mimi niongee ndipo niseme kitu…

“Ahsante dada, mimi naitwa Queen Jonathan na huyu hapa ni ndugu yangu anaitwa Alex Jonathan…” Alisema Queen.

“Oooh, karibuni sana, hebu subiri kidogo…” akaitikia yule meneja kana kwamba alikuwa anafahamu kitu kisha akainua simu yake ya mezani.

“…Boss, Jonathan Company is here…, Okay, okay, yes, in a second.” Akakata simu.

Aliongea yule Meneja kwa kunong’ona sana kiasi kwamba usipokuwa makini huwezi kujua hata ameongea kitu gani kisha akatuambia tumfuate naye akanyanyuka na kutuongoza katika ofisi nyingine…

Nilibahatisha kusoma mlangoni wakati tunaingia maana mimi nilikuwa wa mwisho kuingia tukitanguliwa na Meneja aliyetuongoza akitumia kitu kama kadi hivi kuruhusu milango kufunguka, tukapitia kwenye sehemu kuna ‘scanner’ ya mwili na kuturuhusu kuendelea…

“DCEO Corporate Banking” ni maandishi niliyoyasoma pale mlangoni. ..

“Karibuni..” Alisema yule dada Meneja aliyetuongoza…

“Sir, here is Mister Alex and Miss Queen...” aliongea tena yule dada meneja kisha akatugeukia na kutuambia suala letu litashughulikiwa hapo.

“Karibuni vijana, eee, mimi naitwa (akataja jina) ni msaidizi wa CEO …” akavuta droo na kutoa folder lenye mafaili kadhaa na kisha akawasha tarakilishi yake ya mezani na kuanza kubofya.

“Ahsante, mimi naitwa Queen Jonathan na huyu mdogo wangu anaitwa Alex Jonathan…”

“Nashukuru kuwafahamu, na habari zenu ninazo, karibuni sana.” Tukaitikia pale wote “Ahsante”

Sekunde chache mlango wa ofisi ile ukafunguliwa na akaingia dada aliyevalia sare maalum akituletea chai.

Ofisi ilikuwa kubwa, nzuri yenye hadhi ya kuitwa ofisi ya CEO.

“Karibuni, kuna chai, kahawa, maziwa, milo na cocoa…” alisema yule dada mhudumu huku akisubiri majibu yetu ili ajue ataandaeje…

“Nipatie Kahawa ya maji pekee…” alisema dada

“Nami nipatie maziwa yenye cocoa…” nilisema.

Tukamiminiwa viywaji vyetu pale na tukaanza kunywa tukisindikizia na sambuza ndogo ndogo nzuri na biskuti.

“Nipatieni vitambulisho vyenu vya Taifa…” alisema yule DCEO. Nikatoa changu na kumpa dada ambaye yeye ndiye akasimima kumpelea DCEO yule ambaye meza yake ilikuwa mita tatu hivi kutoka tulipokuwa tumeketi.

Hali ya ubaridi mkali mle ndani na utulivu uliokuwepo ilifanya nihisi njaa ya chai kuliko kawaida kitu kilichopelekea kujiongezea maziwa na kuweka milo na kahawa kwa pamoja safari hii.

“Queen, njoo uweke kidole hapo kwenye biometric (finger print reader)” alisema yule DCEO na pia ikawa hivyo ilipofika zamu yangu.

“Well well, sasa nimesha thibitisha kuwa ninyi ndio wahusika halisi katika suala hili,… malizeni kunywa chai kisha mnijulishe tuendelee…” alisema tena.

Kwa hamu tuliyokuwa nayo tukamaliza fasta chai na dada akasema…

“Tupo tayari baba”

DCEO akasimama na kutuamuru tumfuate ambapo tuliingia chumba kingine hapo hapo na ilionekana ni chumba cha mikutano kwa mandhari ya mpangilio wa meza, viti, sehemu ya ‘presentation display’ nk.

“Karibuni sana, hiki ni chumba cha mikutano yangu na wateja, hapa sasa tutaelewana vizuri…”

Akabofya kuwasha tarakilishi mpakato ilikuwepo pale meza kuu na ‘boom’, display ikaonekana kule kwenye ubao maalum ukutani.

DCEO akaanza kuongea…

“Eeee kuna mirathi yenu katika benki yetu lakini pia katika sehemu nyingine kama wosia unavyosema…”

“Awali ya yote poleni sana kwa kupoteza wazazi wenu…”

Aliendelea kuongea pale wee huku sisi tukisikiliza kwa makini, aliongea kwa kusoma wosia sentesi kwa sentensi na mgawanyo wa mali. Ajabu ni kwamba wasia ambao sisi tulisomewa mahakama ya mwanzo ulikuwa mfupi tofauti na huu ambao tulikuwa tunauona kwa macho yetu jinsi ulivyoandikwa kwa hati ya baba. Aidha mirathi kwa upande wa mama haukuwa mrefu zaidi ya mgawanyo tu wa hela zilizokuwa benki kwenye akaunti yake.

Sehemu ya wosia wa baba ilikuwa inasomeka hivi…

- Pesa zilizopo benki ya CRDB (TZS & UDS), NBC (TZS) , EXIM (USD) pamoja na STANBIC Bank (EURO & USD) zote zihamishiwe kwenye benki ya NMB, kisha zifunguliwe akaunti mbili (Corparate) moja ya Queen Jonathan Ngonyani na nyingine ya Alex Jonathan Ngonyani ambapo akaunti hizo ziwe za USD pekee. Jumla ya fedha hizo mpaka naandika wosia huu ni ka ifuatavyo:-

CRBDTZS - 79,xxx,xxx
CRDBUSD - 563,xxx
NBCTZS - 894,xxx,xxx
EXIMUSD – 270,xxx,xxx
STANBICUERO – 355,xxx
STANBICUSD – 350,xxx

-Pesa zilizopo benki ya NMB akaunti ya biashara zigawanywe nusu kwa nusu kisha wapewe Queen Jonathan Ngonyani na Alex Jonathan Ngonyani wafunguliwe akauti za biashara, hadi naandika wasio huu jumla ya yake zipo TZS 1,832,xxx, xxx/- pia washauriwe wafungue akaunt za akiba NMB ambapo waweke fedha kiasi.

Kuna hisa katika makampuni matatu ambapo hisa hizo zigawanywe nusu kwa nusu kisha umiliki uhamie kwa majina ya Queen Jonathan Ngonyani na Alex Jonathan Ngonjani :-
  • Kampuni ya uwekezaji A 3%
  • Kampuni ya mtandao wa simu A TZ 5%
  • Kampuni ya uwekezaji B 1%
DCEO yule alikuwa anatusomea taratibu ili tuelewe na huku sisi wenyewe tukiona maandishi yenye hati ya baba yetu yakipita kwenye display iliyokuwepo mbele…

Wasio ulikuwa mrefu na wenye maelekezo na maelezo mengi, sote mimi na dada tulikuwa tunastaajabu utajiri ambao baba alikuwa nao na wala hatukujuwa wala hakuonesha kuishi katika hali ya ukwasi kiasi kile.

Moyoni tukiwa na furaha, lakini na maswali yasiyo na majibu pia kichwa tuliendelea kufuatilia maelezo ya DCEO.

“Eee kwa jinsi hiyo, yote hayo, kwa maana ya mgawanyo wa mirathi kwa upande wa baba yenu na upande wa mama yenu yameshafanyika, na akaunt zenu zitakuwa tayari punde si punde…” kisha akabofya kitufe fulani na baada ya dakika chake akaingia afisa mmoja wa benki, tulimtambua kwa sare zake, alikuja na camera na atakupiga picha kisha akaondoka.

Alituonesha pia pesa zilizokuwemo kwenye benki yake NMB, ambapo zilitofautiana kidogo na zile zilizomo kwenye wosia kwa kuongezeka kila akaunti. Pia akapiga simu kwenye benki zingine zenye akaunti za marehemu na kuomba apatiwe statement kwa mujibu wa amri ya mahakama kama tulivyomsikia akiongea, ambapo punde si punde zilikuja ‘printout’ kutoka kwenye printer na soft copy zilionekana kwenye display, nako hapakuwa na mabadiliko ya viwango vya fedha kama ilivyooneshwa kwenye wosia.

“Received, reeived received… proceed with bank transfer as ordered by BoT, you may check authentic of the source…, okay, …, Okay, transfer confirmed…”

Aliongea yule DCEO kwa lugha zao za kibenki wakifanya miamala ambayo sasa tulijuwa inaingia kwenye akaunt zetu.

“Kama mnavyosikia, hela zenu zote zinahamishiwa hapa, kisha ninyi mtakuwa huru kufungua akauti sehemu nyingine katika benki yoyote, lakini kwanza tulitaka kulimaliza zoezi hili mara moja ili muanze umpya mkiamua, lakini itakuwa vyema tukiendelea kufanya kazi nanyi Jonathan Company.

Siku hiyo ndio tulijua kuwa marehemu baba alikuwa ana ‘Private Company’ iitwayo Jonathan Company Ltd iliyokuwa inajishughulisha na mambo mbalimbali kama tulivyoonesha Memorandum and Article of Association ya kampuni hiyo na hisa zote za kampuni hiyo iliamriwa na wosia ziende kwa dada Queen.

Hadi inafika saa tisa alasiri tulikuwa tayari tumeshakabidhiwa kadi zetu za Corporate, fedha kiasi tulihamishia kwenye akaunti za akiba ambazo sote mimi na dada Queen tulikuwa nazo za hapo NMB na zoezi la uhamishaji umiliki wa kampuni Queen aliambiwa aende Brela kwa ajili ya kukamilisha utaratibu, na kuhusu hisa za uwekezaji katika kampuni alizowekeza baba ilibakia kipengele cha kuweka sahihi tu.

Alituruhusu kwenda mapumziko mafupi lakini alitutaka turudi tena benki baada ya saa moja…

“Saa kumi mrudi hapa, milango itakuwa imefungwa kwa wateja waliopo nje lakini mkifika waonesheni walinzi hizo kadi zenu mpya mtafunguliwa, kuna sehemu nataka niwasindikize…”

Tulitoka mle ndani tukiwa hatuna hata njaa, sijui kwa sababu ya ile chai nzito ama kwa sababu ya utajiri wa ghafla ili mradi tulikuwa na furaha na tulitembea kuelekea restaurant ya jirani kupata chakula cha mchana.

“Dada mimi sisikii njaa hata!” Nilisema wakati tunaingia cafeteria fulani iliyopo kwenye kituo cha kuuzia mafuta.

“Hata mimi Alex, sisikii njaa japo nilionja tu ile kahawa na sambusa kidogo” tukacheka kiasi na kuketi mle mghahawani.

Itaendelea Jumamosi panapo majaaliwa.
JBourne59 kwenye ubora wako haujawai kosea
 
Back
Top Bottom