Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #81
SEHEMU YA 31
Nikavaa nguo na kutoka nnje ya nyumba ile ambapo nilimkuta yule mzee mwenye nyumba ile akiwa amekaa kwenye kiti cha mbao huku pembeni yake akiwepo binti mwenye afya mbovu sana akitwanga kitu ambacho sikukijua kwenye kinu! kwa mbali niliona watu wengine kila mmoja akiwa na kazi yake!...
ujio wangu pale nnje ulionesha kuwashitua watu wote waliokuwepo eneo lile wakawa wanasogea mmoja baada ya mwingine wakiwa wameshikwa na bumbuwazi!..
"ungepumzika kwanza afya yako itengemae, kaa hapa" alisema mzee yule huku akinipisha kiti ambacho alikuwa amekalia yeye! "hapana mzee, kaa tu! mimi niko sawa" nilijibu huku nikionekana kuwa na utimamu wa kutosha wa mwili, nikasogea na kukaa chini karibu na kile kiti chake "nadhani hamnijui, ningependa kwanza mnitambue kabla ya kukijua ambacho kimenileta kwenye mjini wenu" nilianza kujieleza lakini kabla sijafika mbali mzee yule alinikatisha "tunajua kila kitu kuhusu wewe, wewe ndiye ambaye hujui mengine kutuhusu! ila leo tutakueleza" alizungumza mzee yule nami nikakaa sawa kumsikiliza "najua unafahamu historia iliyopo kati ya wakazi wa mji huu na bwana Magugi.." Alianza kuzungumza nami nikakubali kwa kichwa kisha akaanza kuelezea kama sio yeye alieanza kwa kusema kuwa anajua kama naijua historia ile!..
akanielezea kila kitu kama ambavyo nilielezewa awali, lakini yeye alielezea mpaka maisha yalivyokuwa upande wa pili wa mlima baada ya kufika kwao "maisha hayakuwa mazuri kabisa, tulikuta ni eneo kame na lisilo na rutuba, hakukuwa na chochote cha kutuendeshea maisha zaidi ya ambavyo tulikuja navyo! Magugi alikuwa ametudanganya..
baada ya chakula kubaki kidogo, ilitubidi kukitoa chote kwa vijana kumi ili wao wapate nguvu na kwenda kutafuta kingi kwaajili ya wengine lakini walitakiwa kuwa makini wasiingie eneo la Muifufu na kuvunja mwiko tuliokuwa nao, vijana wale wakaenda na kufanya kazi ambayo waliagizwa, wakatafuta sana bila kupata chochote, mwishowe wakashauriana kuwa ni bora waingie Muifufu kuliko kuacha watu wote wa huku kijijini wafe na njaa!. kukatokea mabishano makili, wengine wakikubaliana na wazo hilo huku wengine wakipinga, hatimaye uamuzi ukaafikiwa kwamba kila mmoja afanye ambalo yeye aliona ni sahihi, hivyo vijana wanne wakarudi kijijini huku sita wakielekea eneo la Muifufu kutafuta chakula kwaajili ya waliobaki kwenye kijiji hiki wakiwa na hali mbaya sana kutokana na njaa...
"...basi wale vijana ambao waliamua kuvuka mpaka wa mlima kalingisi na kuingia eneo la Muifufu walilaanika na kugeuka kuwa Masokwe ambao wamekuokota na kukuleta hapa" alimaliza kunielezea mzee yule, nikashusha pumzi ndefu iliyoambatana na mshangao mkubwa juu ya historia ya sokwe ambao walinibeba kutoka mlimani mpaka pale kijijini "hivyo inamaana sokwe wale wanauwezo wa kutambua mambo?" niliuliza baada ya kushangazwa na kitendo cha sokwe wale kunipeleka pale nyumbani.
"ujio wako ulitabiriwa zamani sana na marehemu mzee Jafari ambaye alikuwa kiongozi wetu wakati huo na alikuwa na maono ya mbali, jamii hii imekuwa ikiishi maisha ya shida sana huku wakingojea ujio wako, hata masokwe wale wanatambua juu ya ujio wako ndio maana mara baada ya kukutambua walikuleta hapa haraka" alifafanua mzee yule namimi nikatumia nafasi ile kuwaelezea historia yangu yote ambayo inasababisha niwe pale na msaada ambao niliuhitaji sana kutoka kwao..
"kama ambavyo nimekueleza, sisi huwa hatuvunji ahadi, nadhani mpaka sasa unajua ubaya ambao unafuatia iwapo tutavunja kiapo ambacho tulikiweka. Kukusaidia kumuangusha Magugi bado ni kuvunja kiapo kwa maana tuliahidiana kutoshughulika na maisha yake kama akituacha tukaondoka Muifufu bila kutudhuru" aliongea mzee yule maneno ambayo yalielekea kunikwamisha, mapigo ya moyo yaka badilika ghafla na akili yangu ikawa inafanya kazi harakaharaka kujaribu kubuni namna ya kuwavutia watu wale ili kuungana nami katika kuuangusha utawala wa Magugi!..
"lakini tumekuwa tukiishi maisha ya kubahatisha kwa miaka mingi sana, jambo ambalo linatishia kutoweka kabisa kwa jamii hii, maana watu wanakufa kwa njaa. Tunahangaika sana kutafuta chakula na maji lakini tunapata kidogo sana kiasi cha kutoweza kututosheleza. Huu ni wakati wa kufanya maamuzi magumu na kuiweka hatma yetu mikononi mwako" aliongea tena mzee yule safari hii akiyarudisha matumaini yangu kwa kasi sana.
"sisi tutakusaidi ila ni lazima na wewe utusaidie. Kwakuwa nguvu kubwa ya Magugi ni msaada wa majini ambao ni sisi tulimtengenezea, basi tutaipunguza nguvu hiyo bila yeye kujua, baada ya hapo utafanya ambacho unataka kufanya ila malipo yetu sisi ni kifo cha Magugi ambacho kitavunja kiapo kilichopo kati yetu na yeye hata laana ambayo itatupata kwa kuvunja kiapo hicho itafutika papohapo" alielezea mzee yule nami nikamuelewa vizuri sana na kumsihi anisaidie na nitahakikisha maisha ya Magugi yanafikia mwisho kama malipo yangu kwao.
Nikavaa nguo na kutoka nnje ya nyumba ile ambapo nilimkuta yule mzee mwenye nyumba ile akiwa amekaa kwenye kiti cha mbao huku pembeni yake akiwepo binti mwenye afya mbovu sana akitwanga kitu ambacho sikukijua kwenye kinu! kwa mbali niliona watu wengine kila mmoja akiwa na kazi yake!...
ujio wangu pale nnje ulionesha kuwashitua watu wote waliokuwepo eneo lile wakawa wanasogea mmoja baada ya mwingine wakiwa wameshikwa na bumbuwazi!..
"ungepumzika kwanza afya yako itengemae, kaa hapa" alisema mzee yule huku akinipisha kiti ambacho alikuwa amekalia yeye! "hapana mzee, kaa tu! mimi niko sawa" nilijibu huku nikionekana kuwa na utimamu wa kutosha wa mwili, nikasogea na kukaa chini karibu na kile kiti chake "nadhani hamnijui, ningependa kwanza mnitambue kabla ya kukijua ambacho kimenileta kwenye mjini wenu" nilianza kujieleza lakini kabla sijafika mbali mzee yule alinikatisha "tunajua kila kitu kuhusu wewe, wewe ndiye ambaye hujui mengine kutuhusu! ila leo tutakueleza" alizungumza mzee yule nami nikakaa sawa kumsikiliza "najua unafahamu historia iliyopo kati ya wakazi wa mji huu na bwana Magugi.." Alianza kuzungumza nami nikakubali kwa kichwa kisha akaanza kuelezea kama sio yeye alieanza kwa kusema kuwa anajua kama naijua historia ile!..
akanielezea kila kitu kama ambavyo nilielezewa awali, lakini yeye alielezea mpaka maisha yalivyokuwa upande wa pili wa mlima baada ya kufika kwao "maisha hayakuwa mazuri kabisa, tulikuta ni eneo kame na lisilo na rutuba, hakukuwa na chochote cha kutuendeshea maisha zaidi ya ambavyo tulikuja navyo! Magugi alikuwa ametudanganya..
baada ya chakula kubaki kidogo, ilitubidi kukitoa chote kwa vijana kumi ili wao wapate nguvu na kwenda kutafuta kingi kwaajili ya wengine lakini walitakiwa kuwa makini wasiingie eneo la Muifufu na kuvunja mwiko tuliokuwa nao, vijana wale wakaenda na kufanya kazi ambayo waliagizwa, wakatafuta sana bila kupata chochote, mwishowe wakashauriana kuwa ni bora waingie Muifufu kuliko kuacha watu wote wa huku kijijini wafe na njaa!. kukatokea mabishano makili, wengine wakikubaliana na wazo hilo huku wengine wakipinga, hatimaye uamuzi ukaafikiwa kwamba kila mmoja afanye ambalo yeye aliona ni sahihi, hivyo vijana wanne wakarudi kijijini huku sita wakielekea eneo la Muifufu kutafuta chakula kwaajili ya waliobaki kwenye kijiji hiki wakiwa na hali mbaya sana kutokana na njaa...
"...basi wale vijana ambao waliamua kuvuka mpaka wa mlima kalingisi na kuingia eneo la Muifufu walilaanika na kugeuka kuwa Masokwe ambao wamekuokota na kukuleta hapa" alimaliza kunielezea mzee yule, nikashusha pumzi ndefu iliyoambatana na mshangao mkubwa juu ya historia ya sokwe ambao walinibeba kutoka mlimani mpaka pale kijijini "hivyo inamaana sokwe wale wanauwezo wa kutambua mambo?" niliuliza baada ya kushangazwa na kitendo cha sokwe wale kunipeleka pale nyumbani.
"ujio wako ulitabiriwa zamani sana na marehemu mzee Jafari ambaye alikuwa kiongozi wetu wakati huo na alikuwa na maono ya mbali, jamii hii imekuwa ikiishi maisha ya shida sana huku wakingojea ujio wako, hata masokwe wale wanatambua juu ya ujio wako ndio maana mara baada ya kukutambua walikuleta hapa haraka" alifafanua mzee yule namimi nikatumia nafasi ile kuwaelezea historia yangu yote ambayo inasababisha niwe pale na msaada ambao niliuhitaji sana kutoka kwao..
"kama ambavyo nimekueleza, sisi huwa hatuvunji ahadi, nadhani mpaka sasa unajua ubaya ambao unafuatia iwapo tutavunja kiapo ambacho tulikiweka. Kukusaidia kumuangusha Magugi bado ni kuvunja kiapo kwa maana tuliahidiana kutoshughulika na maisha yake kama akituacha tukaondoka Muifufu bila kutudhuru" aliongea mzee yule maneno ambayo yalielekea kunikwamisha, mapigo ya moyo yaka badilika ghafla na akili yangu ikawa inafanya kazi harakaharaka kujaribu kubuni namna ya kuwavutia watu wale ili kuungana nami katika kuuangusha utawala wa Magugi!..
"lakini tumekuwa tukiishi maisha ya kubahatisha kwa miaka mingi sana, jambo ambalo linatishia kutoweka kabisa kwa jamii hii, maana watu wanakufa kwa njaa. Tunahangaika sana kutafuta chakula na maji lakini tunapata kidogo sana kiasi cha kutoweza kututosheleza. Huu ni wakati wa kufanya maamuzi magumu na kuiweka hatma yetu mikononi mwako" aliongea tena mzee yule safari hii akiyarudisha matumaini yangu kwa kasi sana.
"sisi tutakusaidi ila ni lazima na wewe utusaidie. Kwakuwa nguvu kubwa ya Magugi ni msaada wa majini ambao ni sisi tulimtengenezea, basi tutaipunguza nguvu hiyo bila yeye kujua, baada ya hapo utafanya ambacho unataka kufanya ila malipo yetu sisi ni kifo cha Magugi ambacho kitavunja kiapo kilichopo kati yetu na yeye hata laana ambayo itatupata kwa kuvunja kiapo hicho itafutika papohapo" alielezea mzee yule nami nikamuelewa vizuri sana na kumsihi anisaidie na nitahakikisha maisha ya Magugi yanafikia mwisho kama malipo yangu kwao.