Simulizi: Mpaka Kieleweke

Abdallahking

JF-Expert Member
Mar 19, 2018
3,983
10,804
26171301_135461037136046_3406855638411712926_o.jpg


Simulizi: MPAKA KIELEWEKE
Mwandishi: NIRA SAIRE

Imeletwa kwenu na: BURE SERIES

SEHEMU YA 1

Nilikuwa nimeongozana na mke wangu tukitokea dukani eneo lile la ugenini nikiwa busy kwenye simu yangu huku nikiongea na mke wangu ambaye alikuwa nyuma yangu akinisemesha hili na lile. Mara nikagundua hali isiyo ya kawaida, mke wangu alikuwa kimya ghafla.. nikageuka haraka kutaka kujua nini kilimfanya awe kimya namna ile lakini cha ajabu sikumuona mke wangu. "khaaa, kabaki wapi huyu mwanamke?" nilijikuta nikiuliza kwa sauti ilhali nilijua fika kuwa nilikuwa peke yangu eneo lile lenye kiza cha kutosha.

Uamuzi nilioufikia haraka ni kuamua kurudi nyuma kujaribu kumtafuta huku nikimpigia simu kwa maana nakumbuka alitoka nyumbani na simu yake. kitu cha ajabu simu yake iliita nyuma yangu baada ya kuwa nimetembea hatua chache tu, niligeuka nikaufuata muito ule wa simu ambao nilikuwa nikiujua kuwa ni wa simu ya mke wangu... kweli ilikuwa simu ya mke wangu ikiwa pale chini ikiendelea kuita, nilishikwa na bumbuwazi kwa sekunde chache nisijue hata cha kufanya kisha nikaiokota ile simu na kuanza upya safari ya kurudi eneo lile la madukani kujaribu kuona kama naweza kumuona mke wangu.



Nilitembea huku nikiangaza huku na huko nikiamini pengine ningemuona mke wangu lakini mpaka nafika eneo lile la maduka sikuwa nimemuona.

Nikajaribu kuvuka eneo lile na kuangalia maeneo ya mbele zaidi ila sikumuona.

Akili ikaniambia labda atakuwa amekwenda nyumbani, nikakimbia mpaka nyumbani ila mlango ulikuwa umefungwa kama ambavyo tuliuacha, mke wangu hakuwepo na funguo alikuwan azo yeye. Sikuwa na sehemu nyingine ya kumuangalia kwa maana tulikuwa hata hatujazoeana na majirani.

Moja kwa moja nikaenda mpaka duka lile ambalo tulikuwa tumenunua bidhaa dakika chache zilizopita kwani ndilo duka pekee ambalo tulikuwa tukinunua kwa muda wote wa siku tatu tangu tuhamie mji ule. Hata muuzaji wa duka lile tulikuwa tumeanza kuzoeana hivyo sikuwa na mtu mwingine wa kumfuata wakati ule zaidi yake.

“samahani Mangi” nilianza kumsemesha mara baada ya mteja aliyekuwa akamuhudumia kuondoka... “aisee mke wangu hajafiaka hapa?” niliuliza nikilingojea jibu kwa hamu huku nikitamani awe na chochote cha kusema ambacho kingesaidia kumpata mke wangu kwa maana hofu kubwa ilikuwa imeniingia tayari.. Mangi alionekana kunishangaa kidogo kisha akauliza..

“wewe si umeondoka hapa na mke wako hata dakika kumi hazijaisha?” kufika hapo nikachoka kabisa na kujikuta nikikaa kwenye benchi ambalo lilikuwa nnje pale dukani. Mwili wangu ulikuwa ukitetemeka kiasi ambacho kilimshangaza Mangi ambaye wakati huo alikuwa akijaribu kunisemesha lakini hata sikumbuki alikuwa anaongea nini kwa maana akili yangu hata haikuwa pale na wala sijui ilikuwa wapi.

Kugutuka nilimuona Mangi akiwa amesimama mbele yangu pamoja na watu wengine ambao walionekena kuwa wenyeji wa eneo lile wakitaka kujua nini kilikuwa kimetokea.

“Kijana hebu tueleze hali ambayo imetokea pengine tunaweza kusaidiana mawazo na jambo likawa jepesi” aliongea mzee mmoja wa makamo ambaye sikumfahamu ila moja kwa moja nikajua Mangi alimuita ili kuja kusaidia baada ya kuniona katika hali ile isiyoeleweka.

Nilijikaza nikawasimulia mkasa uliotokea, wakati naendelea kuongea watu walikuwa wanazidi kuongezeka.. mpaka namaliza kuongea kulikuwa na kundi kubwa sana, wake kwa waume.

“Jamaniiiii hali hii mpaka lini?” ilikuwa sauti ya mama mmoja mtu mzima ambaye alikuwepo akisikiliza maelezo yangu, kauli ile iliniacha njia panda.. inamaana matukio ya namna hii ni ya kawaida kutokea eneo lile? Nilikuwa nikijiuliza. Watu

ambao walikuwepo pale pia hawakuonekana kujiuliza ni wapi alipotelea mke wangu badala yake walionekana kunionea huruma.

Pemebeni nilimuona mzee yule ambaye alinitaka kuwaelezea ambacho kilinisibu akishauriana na wanaume wengine watatu kisha wakaja pale nilipo..

“Tumpelekeni kwa mzee Miale” aliongea yule mzee, wakanisaidia kunyanyuka na safari ya kuelekea kwa mzee Miale ambaye sikujua ni nani wala tunaenda kufanya nini kwake ikaanza.

Kwakweli nilikuwa nimechanganyikiwa nikajikuta nafuata kila ambacho naambiwa bila hata kuhoji.

Tulifika kwa mzee Miale tukabisha hodi na kupokelewa na mama mtu mzima kidogo.

“Karibuni jamani, kwema?” alitukaribisha mama yule akiwa na mshtuko nadhani ilitokana na wingi wa watu ambao tulikuwa tumeongozana nao.

“Sio kwema sana shemeji, huyu bwana tumemkuta?” aliongea mzee mmoja kwa niaba ya kundi lile.

“Hapana, huyu bwana ameenda kwenye

shughuli zake huko Michese ila atarudi asubuhi” alijibu yule mama ambaye nilikuwa nimegundua kuwa alikuwa mke wa mzee Miale. Yule mzee ambaye tulikuja naye akamchukua yule mama wakakaa kando kidogo na kuongea, nadhani alikuwa akimuhadithia kilichonikuta. Baada ya muda mfupi wakasogea ambapo tulikuwa tumesimama na yule mama akaongea..

“Pole kwa yaliyokukuta mwanagu, jikaze ndio ukubwa huo” akanitazama, nikaitikia kisha akaendelea..

“Sasa wewe nenda kapumzike kesho mida ya
 
SEHEMU YA 2

saa mbili uje mzee atakuwepo” aliongea yule mama nami nikaitikia.

Tukaondoka njiani tukigawanyika kila mmoja akishika njia ya kuelekea kwake mpaka nikabaki na vijana wawili ambao tuliendelea kuongozana..

“Pole sana kaka, mimi ni jirani yako bwana, nakaa ile nyumba yenye rangi ya kijani kulia mwa pale kwako” aliongea mmoja wa wale vijana wenzangu huku mwingine akituaga na kufuata njia ambayo ilimuhusu.

“Asante aisee” nilimjibu tukaendelea na safari huku nikijaribu kudodosa juu ya ambacho anadhani kitakuwa kimempata mke wangu.

“Mimi ni mbumbumbu juu ya hili kama ulivyo wewe, ukifika kwa yule mzee kesho nadhani unaweza kupata majibu mazuri” alinijibu wakati huu tukiwa tumefika kwangu tukaachana.

Nilitembea hatua chache kuelekea ulipo mlango wa kuingilia nikakumbuka kuwa mlango ulikuwa umefungwa na funguo alikuwa nazo mke wangu, nikafikiri kwa muda na kisha kuamua kuwa kama simu iliachwa pale basi pengine na funguo ipo maeneo yale ila sikuiona kwakuwa kulikuwa na giza, hivyo nikaamua kurudi eneo lile nikaitafute kwa kutumia tochi ya simu ya mke wangu ambayo ilikuwa na mwanga mzuri tu.

Saa kwenye simu ilikuwa inaonesha kuwa ni majira ya saa sita kasorobo usiku, nikatembea polepole kuelekea eneo ambalo alipotelea mke wangu, nikafika na kuwasha tochi ya simu kisha nikaanza kuangaza kuitafuta funguo ya mlango wa nyumbni kwangu lakini nilishtushwa sana na ambacho nilikiona kama hatua tatu mbele ya ambapo nilikuwa nimesimama, zilikuwa ni nguo za mke wangu......

Nilisogea mpaka zilipokua zile nguo nikazikagua na kugundua kweli zilikuwa nguo za mke wangu, tena zote mpaka za ndani, niliogopa sana na kuanza kuhofia ambacho kilikuwa kimempata mke wangu kipenzi.

Wakati naendelea kumulika nikaiona na funguo ambayo ndio chanzo hasa cha mimi kwenda eneo lile wakati ule, nikaiokota pamoja na nguo za mke wangu na kuanza safari ya kuelekea nyumbani.

Nilifika nyumbani nikafungua mlango na kuingia ndani kisha nikajilaza chali kitandani, nilikuwa nimechoka sana kuanzia mwili mpaka akili, nikachukua simu yangu na kupiga namba za baba yangu, niliamini ni mtu pekee ambaye angeweza kunifaa kwa wakati ule kama ambavyo amenifaa mara zote ninapohitaji msaada wake wa kimawazo...

Simu ile iliita kwa muda lakini haikupokelewa, nikaangalia saa na kugundua ilikuwa saa sita na robo usiku, bila shaka atakuwa usingizini na mara zote huiweka simu yake silent anapolala.

Niliachana na kupiga simu nikajaribu kulala lakini haukuwa usingizi wa maana, akili yote ilibaki macho ikijaribu kuvuta upya taswira ya tukio zima ambalo lilikuwa limetokea...

Nilijikuta nikiamini tukio lile lilikuwa likihusika na masuala ya kishirikina, mambo ambayo sikuwa na uzoefu nayo hata kidogo, niliishia kuyasikia tu kwa watu.

Hali ikawa hivyo usiku kucha, kila saa nikijaribu kuangalia saa yangu nikitamani kukuche nianze hatua za kumtafuta mke wangu...

Sasa saa ilionesha kuwa ilikuwa saa 11 na dakika 5 alfajiri, simu yangu ikiwa inaita, nilikurupuka haraka nikaichukua na kumuangalia mpigaji, alikuwa ni baba yangu, ambaye nadhani ndio alikuwa anaamka na kukuta “missed call” yangu ile ya usiku mnene. Nilipokea haraka haraka na kuanza kuongea na baba ambaye moja kwa moja alijua kuna tatizo kutokana na kumpigia muda ule ambao si muda wa kupeana salamu za kawaida.

Nilimuelezea baba kila kilichokuwa kimetokea naye akashangazwa sana na hali ile, alikaa kimya kwa muda, nadhani alikosa chochote cha kusema kisha akaongea “Jikaze mwanangu, kukicha nenda kwa huyo mzee ukaone kama atakuwa na msaada wowote, mimi nitaondoka na basi la kwanza hapa nadhani majira ya saa saba mchana tutakuwa pamoja” tukaagana, akakata simu nami nikajiinua kutoka pale kitandani ambapo sikuweza kupata usingizi usiku kucha.

Nikaingia bafuni, nikajimwagia maji ili kuchangamsha mwili tayari kwa kwenda kwa mzee Miale, wakati nikiwa nakoga nikajiuliza kwanini sikuwa nimeripoti tukio lile katika kituo cha polisi, nikajiona nilikuwa mzembe hivyo nikaoga haraka haraka kisha nikatoka na kuvaa, safari ya kuelekea kituo cha polisi ikaanza kwa kutumia pikipiki yangu, wakati huo ilikuwa ni majira ya saa 12 za asubuhi nikaamini nitawahi kurudi na kwenda kwa Mzee miale kwa wakati.

Nilifika kituoni nikajitambulisha na kuelezea kilichotokea, askari walichukua maelezo yangu wakayaandika na kuniruhusu kuondoka, nilishangazwa kuona hawakulichukulia jambo lile kama jambo kubwa sana, sasa niliamini tukio langu halikuwa la kwanza katika jamii ile. Nikaondoka na kuelekea kwa mzee Miale.

Nilifika nikapokelewa na mzee ambaye umri wake ulionekana kuwa si chini ya miaka 70, ambaye nilimkuta amekaa peke yeke kwenye kiti cha kizee pale nje, “Shikamoo mzee, sijui wewe ndo mzee Miale?” nilisalimia akaitikia nikamuuliza na swali ambalo alilijibu kwa kukubali kuwa ndio yeye, nami nikajitambulisha na akanitambua haraka kwa maana alikua tayari ameshaelezwa juu yangu, alinichukua tukaingia ndani kisha akaanza kunieleza juu ya ambacho kimemtokea mke wangu, akianzia kunipa historia ya miaka mingi sana iliyopita...
 
SEHEMU YA 3





“Zamani eneo hili lilikuwa ni himaya ya wachawi wenye nguvu kubwa sana, wachawi kutoka maeneo mbalimbali walikuja katika eneo hili na kujifunza taaluma hiyo kisha wakatoka wakiwa na uwezo mkubwa sana.

Wachawi hao walikwenda kwenye maeneo yao na kuwa wasumbufu katika jamii, na kama nilivyokueleza walikuwa na nguvu sana hivyo mbinu za kupambana nao hazikuwa zikifanikiwa. Ulifikia wakati watawala wa maeneo mbalimbali walikutana na kujaribu kushauriana nini kifanyike juu ya wachawi ambao walikuwa kero kubwa kwa wananchi wa himaya zao, tawala zile zikakubaliana kuwa eneo hili ambalo ndilo lilikuwa makao makuu ya shughuli hizo haramu liteketezwe lote, mipango ikapangwa wakishirikiana na waganga wa kienyeji ambao walikuwa na mbinu za ziada na ikabainika siku ambayo wachawi wote hukutana katika eneo lile, wakaamua kuitumia siku hiyo kwenda kuwateketeza wote, lakini kwa bahati mbaya habari zikavuja na kuwafikia wachawi wale ambao waliutumia uchawi wao kujikinga, wakajenga himaya yao ndani ya eneo hili kisha wakafanya zindiko kubwa kuhakikisha himaya yao hiyo haitokuwa ikionekana na mtu yeyote, hivyo watu wale waliokwenda kwa ajili ya kuwateketeza walikuta mji huu hauna mtu hata mmoja, ikabidi wataalamu ambao walikua nao wapige ramli na kugundua nini kilikua kimetokea, wakagundua zindiko hilo la wachawi hivyo nao wakafanya ufundi wao kuzuia himaya hiyo ya siri ibaki hukohuko na isiingiliane na himaya hii, kisha wakafanya utaalamu mwingine ili watu wa himaya hiyo ya siri wasizaliane wakiamini watakuwa wakifa bila kuzaliana hatimaye himaya hiyo itatoweka..



Maisha yakaenda hivyo kwa muda kidogo lakini baadae watu wa himaya ile ya kichawi wakapata namna ya kuwa wanapenya na kuja himaya hii mara chache.

Baadae wakaamua kuwa ikitokea mtu amekufa himayani mwao basi hutoka nje ya himaya yao na kumchukua mtu mwingine ili aende kuziba nafasi ile, lakini ilikuwa ngumu sana kwa mtu ambaye ametokea huku nje kuishi kama ambavyo wao walitaka hivyo wakaja kugundua njia nyepesi na kumfanya mtu awe wa kule (mtu wao) na kisha aishi kama wao ni mtu huyo kuzaliwa katika ardhi yao, kwa kua hawakuweza kuzaliana kutokana na laana ile ya wazee wa zamani wakaamua kua wawe wanakuja huku na kukamata wanawake wajawazito kisha wanawapeleka katika ardhi yao ili mtoto akazaliwe katika ardhi yao na kisha hua wa kwao kabisa..”

alitulia kidogo akaniuliza.

“Ni kweli mkeo alikuwa mjamzito??”, nami nikamjibu kua ni kweli, mke wangu alikuwa na ujauzito wa miezi miwili.

Sasa nilikuwa nimejua nini kilikuwa kimempata mke wangu.

“Nawezaje kumpata mke wangu mzee?” nilimuuliza mzee Miale huku moyoni nikiwa nasali kuwe na njia ya kufanikisha hilo......





Mzee Miale aliniangalia kwa upole kisha akasema “watu kutoka dunia yetu hii huwa hawaingii mji ule wa siri ingawa wa kutoka kule huja huku, unadhani mkeo atarudije ukizingatia habari ambayo nimekueleza?”

Kauli za mzee Yule zilizidi kunichanganya nikajiona kama nilipoteza muda kuja pale. Nilijikuta machozi yakinitiririka bila kizuizi chochote mzee yule akinishuhudia bila hata ya kuwa na msaada wa kunipa.. “huu ni uonevu, bora wangechukua kingine chochote lakini sio mke wangu” niliongea kwa hasira, mzee miale akanitazama kwa masikitiko kisha akaongea “jikaze tu mwanangu, utafanya nini sasa?” nilianza kuichoka ile kauli ya nijikaze ambayo nilikuwa nimeisikia mara nyingi sana toka kumpoteza mke wangu kipenzi siku chache tu baada ya ndoa yetu, niliona kama watu wale waliokuwa wakinitaka nijikaze walikuwa hawaelewi ni kiasi gani nilikuwa nikiumia.

“nitahakikisha nampata mke wangu kwa gharama yoyote, sikubali hata kidogo nasema, nitapambana mpaka kieleweke” nilisema huku nikisimama , machozi yalikuwa yamenifika shingoni. Mzee Miale alinisihi kuwa mtulivu lakini sikuwa nikitaka tena hata kumsikiliza kwa maana niliona msaada wake ulikuwa umeishia pale kwenye kunijuza mahali ambapo mke wangu angeweza kuwepo wakati ule. Nilimuaga nikaondoka na kuelekea kazini kwangu ambapo nilitegemea kukutana na rafiki yangu bwana Anthon Matovu ambaye nilitegemea tunaweza kushauriana na kujua pa kuanzia, kwa kutumia pikipiki yangu haikunichukua muda sana nikawa nimefika kazini na kukutana na bwana Matovu nikamuomba tutoke kidogo ofisini kwa ajili ya mazungumzo mazito kidogo, naye akatii tukatoka na kwenda kukaa kwenye glosary ambayo ilikuwepo pale karibu tukakaa na nikamuelezea tatizo kubwa ambalo lilikuwa likinikabili.

Habari ile ilimshangaza na yeye ila akashauri twenda kwa mtaalamu wa masuala haya ya kienyeji ambaye alikuwa akimfahamu. Nilijaribu kumueleza kuwa jambo hili pengine lisingeweza kutatuliwa na mtaalamu huyo ila akasisitiza kuwa mzee huyo anayepatikana kijiji cha Ihihi ni mjuzi hasa na lazima atalimudu jambo lile. Tukakubaliana kwenda Kijiji hicho kesho yake asubuhi.
 
SEHEMU YA 4

Tukarudi ofisini, nikafanya utaratibu wa kuomba likizo ya dharura, nikaomba likizo ya miezi mitatu bila malipo nikijieleza kuwa na matatizo ya kifamilia ambayo yanahitaji muda wa kutosha kuyatatua na nikafanikiwa.

Nilirudi nyumbani nikajipikia chakula na kukaa kujaribu kula lakini sikuweza, niliyaona maisha yangu kuwa magumu bila mke wangu pale nyumbani, nilitamani tu kesho ifike nipelekwe huko kwa huyo mganga nikaone kama anaweza kunisaidia kumpata mke wangu.

Wakati huo nilipata ujumbe mfupi wa simu toka kwa baba ambaye alikuwa akinijulisha kuwa alikuwa amekaribia kufika stendi ya mabasi nami ikanibidi kwenda kumpokea. Nilimpokea baba tukaenda nyumbani ambapo tulikaa nikamuelezea ambapo nilikuwa nimefikia katika harakati za kumtafuta mke wangu, tukakubaliana kuwa kesho yake tungeenda pamoja kwa mganga huko Ihihi.

Tuliongea mengi, sana sana alikua akinifariji na kunitaka nijikaze kiume akiamini kuwa hili litaisha salama na mke wangu atarudi kuishi nami.

Kutokana na uchovu baba alitangulia kuchoka akaniaga na kwenda kulala akiniacha mimi nikiangalia TV ingawa kwa kweli hata sikuwa nikiona nini kilikuwa kikiendelea kwa maana akili yangu hata haikuwa pale. Majira ya saa 7 usiku nilihisi kuchoka nikaamua kwenda chumbani kujipumzisha, nilifika nikajitupa kitandani kama nilivyokuwa na kupitiwa na usingizi.

Nilishtuka kutoka usingizini kutokana na upepo mkali ambao ulikuwa ukivuma mule chumbani, upepo ule ulifikia kusukuma vitu vyepesi vikaanguka na vingine kugongana mpaka kukawa kuna hali ya kelele mule chumbani, niliamka haraka nikakaa kitandani na kusikilizia hali iliyokuwa ikiendelea, mara chumba kilijazwa na mwanga mkali sana ingawa taa haikuwa ikiwaka, mwanga ule ulitosheleza kuona kila kitu mule ndani kama vile ilikuwa mchana.

Kwenye pembe mojawapo ya chumba kile nilimuona mtu akiwa amechuchumaa nikashituka sana, ilibaki kidogo nikimbie lakini mtu yule aliamka pale haraka sana akasimama akiuziba mlango, ili nisitoke maana kupita ilikuwa ni lazima nimtoe yeye pale mlangoni.. “kama unataka kumpata mkeo tulia na unisikilize kwa makini” aliongea mtu yule ambaye alikuwa ni mzee kiasi. Ingawa nilikuwa bado naogopa nilijikaza na kukaa kitandani kwa upole. “mimi ndo mtu pekee ambaye naweza kukusaidia kufika alipo mkeo kwenye dunia hii” aliongea mtu yule akinisogolea kwa tahadhari kubwa. “tafadhali nisaidie kumpata mke wangu, niko tayari kufanya chochote ili kuonana tena na mke wangu” nilisema katika hali ile ya uoga na mtu yule akawa amefika kabisa mbele yangu na sasa niliweza kuiona hata sura yake ambayo ilikuwa ya mtu wa kawaida tu, wala haikuwa ikitisha. “kumpata mkeo inakupasa kuwa jasiri sana, ni lazima uingie MUIFUFU” alielezea mzee yule. “MUIFUFU ndo wapi mzee wangu?” niliuliza kwa shauku ya kutaka kujua nini napaswa kufanya ili kumpata mke wangu, nilikuwa tayari kwa lolote. “Muifufu ni mji wa siri ambao upo ndani ya mji huu, huko ndiko mkeo aliko” alisema mzee nami nikaelewa kuwa alikuwa akiuzungumzia mji ambao nilielezewa kuuhusu na Mzee Miale. “niko tayari mzee wangu, nawezaje kufika huko” niliongea nikionesha nia thabiti ya kwenda sehemu hiyo kwa kua ndiko aliko mke wangu na mwanangu ambaye yuko tumboni ambaye sikutaka kabisa aishi maisha ya huko kwa mashetani. Mzee yule aliniangalia akatabasamu, kisha akaongea “kwenda Muifufu sio jambo la mchezo, wengi ya wanaoishi huko ni wachawi na ili kufanikiwa ndani ya mji ule ni lazima na wewe uwe mchawi” aliongea mzee yule ambaye bila shaka na yeye alikuwa mchawi. Nilishituka sana nikawaza kuhusu mimi kuwa mchawi na nikaingiwa na uoga lakini baada ya kukumbuka kua ndio njia pekee ya kumrudisha mke wangu kwenye maisha yetu ya pamoja nilijikuta nikijibu.. “niko tayari mzee wangu, niko tayari kwa chochote”







Yule mzee aliniangalia kwa utulivu kisha akasema "nakuachia siku nzima ya kesho kufikiria kama kweli uko tayari kwa hili" kisha akaanza kurudi kinyumenyume na giza likarudi kama ilivyokuwa awali

"NGOJAAAAAAA USIONDOKEEEEEE" Nilisema kwa sauti baada ya kugundua kuwa mzee yule alikuwa anaondoka.. "ongea haraka, napaswa kuondoka hapa

kabla anga halijafunga" aliongea nami nikaendelea ingawa sikuelewa alikuwa na maana gani kuhusu anga kufungwa "niko tayari mzee, tunavyozidi kuchelewa napata mashaka juu ya hali ya mke wangu huko

aliko" nilisema kwa hali ya kubembeleza, kwakweli sikuhitaji muda zaidi wa kufikiria nilikuwa tayari kufanya chochote. "mkeo ni

mjamzito, tena mimba yenyewe ndo kwanza ina miezi miwili, wanawake

wajawazito huwa wanaishi kama malkia huko Muifufu, huwa hawapati shida

yoyote ingawa wana maisha kama ya kinyonga" aliongea na mwishowe

akaishia kunichanganya tena, "maisha kama ya kinyonga? una maana

gani?" nilijikuta nikipata swali lingine na kumuuliza tena...
 
SEHEMU YA 5

"hilo nitakuelezea wakati mwingine, kuna miezi saba kabla mkeo hajajifungua na ndani ya wakati wote huo atakuwa na maisha ya amani sana, ila wazo la kwenda kwa mganga kesho uliondoe kabisa kwa maana uchawi wa huku si kitu kulinganisha na uchawi wao, ukienda kwa mganga akafanya chochote

watagundua kama unawafuatilia na hapo wataanza kukufuatilia kila hatua

na mipango yetu yote itajilikana kisha hakuna ambacho utaweza kufanya... KWAHERI" Alimaliza kuongea akamalizia na kuaga bila kunisikiliza.. "HAPANAAAA, SUBIRIIIII" nilisema haraka nikitaka

kumuuliza zaidi angalau hata nijue nawezaje kumpata iwapo nitamuhitaji

tena lakini upepo kama ambao ulivuma wakati anakuja ukavuma tena na kisha kukawa kimya sana, nikaamka kwa kasi na kwenda kuwasha taa kisha nikaangaza huku na huko ndani ya chumba lakini nilikuwa pekeyangu ndani ya chumba kilichovurugiza kama vile wamepita ng'ombe maeneo yale.

Sikuwa na chakufanya zaidi ya kutoka chumbani nikaenda kumuamsha baba

na kumuelezea juu ya ambacho kimetokea, baba aliniambia kuwa alisikia nikiwa naongea na mtu akadhani nilikuwa naongea na simu kwa maana ilikuwa ikisikika sauti yangu bila ya ambaye naongea naye.

Tulishauriana na baba kuhusu kwenda ama kutokwenda kwa mganga kesho

yake, mimi nilikuwa nikishauri tusiende lakini baba alikuwa anasisitiza twende kwakuwa yeye hakumuamini mzee yule ambaye aliingia chumbani kwangu "vipi kama mzee huyo ni kundi lilelie la wachwawi waliomchukua mkeo na sasa anakutisha ili tusiende kwa mganga huyo

kwakuwa wanajua nguvu zake?" baba aliuliza swali ambalo kwakweli lilikuwa swali la msingi, kwa kiasi fulani nikaona yuko sahihi. Lakini nilikuwa naogopa pia kwenda kwa mganga yule kwamaana kama maneno aliyoyasema mzee yule ni yakweli basi nitakuwa napoteza nafasi ya kumpata mke wangu. Mwisho tulikubaliana kuwa asubuhi tukamuone mzee Miale labda anaweza akawa anajua kitu chochote juu ya mzee yule aliyenitokea chumbani.

nikaachana na baba na kurudi chumbani ambapo sikuweza kupata usingizi, nikachukua laptop yangu na kuanza kuperuzi kwenye internet.

Wakati nikiendelea kuperuzi nikiwa sina kitu maalumu ambacho nimekilenga nikakumbuka kauli ya mzee yule kuwa maisha ya mke wangu ni kama ya kinyonga, nikajiuliza mdudu yule mbaya wa sura ana kipi kinachofanana na maisha ya mke wangu, kitu pekee ambacho najua ni maarufu kuhusu kinyonga ni kuwa ana uwezo wa kuiga rangi yoyote aitakayo je mke wangu amefikia huko? nikajikuta nikiingia google na kusearch juu ya maisha ya kinyonga. Baada ya dakika 5 tu nilijikuta nimekipata ambacho nilikuwa nakitafuta, sehemu hii ni sehemu ambayo

ilikuwa ikielezea kuwa kinyonga huwa akizaa anakufa na mtoto anaishi..

Nikakumbuka maneno ya mzee yule kuwa kabla ya kuzaa mke wangu ataishi kama malikia kwakuwa ana mimba, nikaelewa kuwa ukinyonga utampata pale atakapozaa kwa maana atakufa yeye na kubaki mtoto, uoga ukaongezeka maradufu, nikatamani wakati huo ningekuwepo alipo mke wangu niweze

kumuokoa kwenye dhahama ile lakini halikuwa jambo lililo ndani ya uwezo wangu, nikaishia kujifariji kuwa bado kuna miezi saba mpaka kufikia wakati huo.



Ilikuwa majira ya saa mbili asubuhi nikiwa nimekaa na baba kwenye kasebule kale kadogo cha mzee Miale tukimsubiri aje baada ya kupokelewa na mjukuu wake na kuambiwa kuwa babu alikuwa akioga!,

tulisubiri kwa dakika kama kumi kisha mzee Miale alijumuika nasi na mazungumzo yakaanza kwa kumtambulisha baba yangu kisha nikamuelezea juu ya ujio wa mzee yule wa usiku pamoja na maonyo yake.

Taarifa ile ilionekana kumshitua mzee Miale ambaye aliniuliza maswali mbalimbali nami nikayajibu kisha akaonekana kugundua kitu..

"Huyo aliyekuja kwako ni Mnaro,mtoto wa mzee Magugi ambaye ni matwala wa

Muifufu" baba alinitazama kisha akanambia "si nilikwambia? wote hawa

ni kitu kimoja" lakini mzee Miale akamkatisha "hawa sio kitu kimoja

hata kidogo, Mnaro amemuasi baba yake kitambo sana na kukimbia Muifufu" alisema mzee Miale kisha akaendelea, "Inasemekana Mnaro na baba yake bwana Magugi wana ugomvi wa masuala ya kimapenzi, Magugi alipora binti ambaye Mnaro alikuwa akimpenda toka utotoni na kumfanya mke wake wa 28, Mnaro alimuomba sana baba yake kumuachia mke huyo tu na ahangaike na wengine wote waliobaki kama angewahitaji ila baba yake alikataa akidai kuwa iwapo Mnaro angeishi na mwanamke yule angekuwa

mdhaifu sana juu ya mwanamke huyo na hata kutawaliwa na hatimaye kutoa siri ambazo watu wa Muifufu hawazijui isipokuwa Magugi na mwanaye

Mnaro ambaye alikuwa akimuandaa kuja kuwa kiongozi wa Muifufu baadae.
 
SEHEMU YA 6

Kutokana na hasira za kunyang'anywa ambacho alikuwa akiona ni haki yake Mnaro alifanya jaribio la kumuua baba yake ambalo lilishindikana kisha akakimbia Muifufu, askari wa mzee Magugi kutoka Muifufu walikuja mara kadhaa kwenye ardhi hii kumtafuta Mnaro lakini hawakufanikiwa, pengine ni kutokana na mbinu nyingi ambazo alikuwa

nazo kwa kuwa baba yake alimfundisha mengi akimuandaa kuja kumrithisha

uongozi, hivyo Mnaro hakuwahi kuonekana toka wakati huo lakini naamini ni yeye ambaye alikuja kwako usiku kwa maana hakuna mtu mwingine ambaye anajua habari za Muifufu zaidi yake" mzee Miale alimaliza maelezo yale na mara ikasikika sauti ambayo haikujulikana ilikotokea

ikisema "na kama baba yangu angejua kuwa kuna mtu anaijua historia yake

namna hii basi usingekuwa hai mzee Miale"

sote tukakaa kimya na kuisikiliza sauti ile ambayo iliendelea,

“Nimekuwemo ndani ya ardhi hii nikiishi maisha ya upweke kwa muda mrefu lakini nikiwa na ndoto kubwa ya kuja kutawala Muifufu. Tumaini pekee la kufanikisha mpango wangu ni kumtorosha mpenzi wangu ambaye kwa sasa anaishi kama mke wa baba yangu. Kabla ya kwenda kufanya jaribio la kumuua baba yangu niliongea na na mwanamke yule nikamwambia ambacho nataka kufanya kwaajili ya mapenzi yetu na ambacho nitafanya iwapo nisipofanikiwa, tukakubaliana kuwa endapo nisipofanikiwa yeye ataolewa na baba yangu na kuigiza kama mke mwema mpaka hapo mimi

nitakapofanikiwa kwenda kumchukua huku wakati wote akiyasoma mazingira ya baba yangu na kupata njia ambayo itatuwezesha kuuangusha utawala wake wa kikatili ndani ya Muifufu, baba yangu anaamini mwanamke yule amefutwa kumbukumbu zote kwenye kichwa chake kama ambavyo hufanywa wakazi wote wa Muifufu lakini akili ya mwanamke huyo iko sawa na anakumbuka kila kitu kwa maana niliikinga vilivyo kabla ya kukimbia Muifufu” sauti ile ilinyamaza kwa muda wa sekunde kumi na tano nami nikauliza huku nikiwa sijui kama mtu yule bado yupo ama ameondoka

tayari “kwahiyo watu wote wa huko Muifufu hufutwa kumbukumbu kwenye

akili zao?” sauti ile ikajibu.. “ndio, hata ukikutana na mke wako leo hawezi kukumbuka wewe ni nani, hakuna kitu hata kimoja ambacho anakumbuka zaidi ya kuamini kuwa Magugi ndio kila kitu katika maisha yake na anapaswa kuishi kumfurahisha yeye, yani Magugi ni mungu huko Muifufu”.... alielezea bwana yule ambaye nilikuwa nikijua sasa kuwa

alikuwa akiitwa Mnaro.

“Bwana wewe kwani uko wapi na kwanini

hatukuoni?” baba yangu naye alipata swali la kuuliza na akajibiwa..

“Niko mbali sana na hapo mlipo, ingawa naweza kuwaona na kuituma sauti

yangu mpaka hapo mlipo” iliongea sauti ile nami nikapata shauku ya kujua jambo nikauliza “unaweza kuona na kupeleka sauti mpaka Muifufu?”

nikajibiwa “ndio ninao uwezo huo ingawa huwa naishia kuangalia nini kinaendelea huko Muifufu lakini huwa situmi sauti kwamaana huwa sitaki baba yangu ajue kama huwa naona kinachoendelea huko na kwa kutuma sauti atajua mara moja. “tafadhali niangalizie kama mke wangu yuko salama huko” nilijikuta nimetoa ombi na sauti ikanijibu

“nadhani ingekuwa bora uangalie na umuone mwenyewe”.....




“Nitashukuru sana kama utanisaidia kwa hilo” nilijibu huku sauti yangu ikionyesha waziwazi kiherehere cha kutaka jambo hilo litokee haraka. “kifaa kinachoniwezesha kutekeleza jambo hilo kiko hapa kwangu na hakiwezi kutoka hapa, itakubidi uje huku ili uweze kuona” ilielezea sauti ya mzee yule nami nikamjibu “haina shida mzee, nielekeze nije sasa hivi” ... “huwezi kufika kwangu mpaka mimi nikulete, nitakuja kukuchukua usiku kama kweli uko tayari” ilisema ile sauti nami nikakerwa kidogo na tabia ile ya kutaka kila jambo lichelewe kutendwa, nikajikuta nimeuliza kwa mara nyingine “kwani hauwezi kuja kunichukua asubuhi hii nikaja huko?” sauti ile ikatulia kwa muda kisha ikanijibu “kua mchawi kunataka subira, kuna mambo mengi ya kuyafanya kwa upole na ukiwa na haraka kama hii yako utajikuta umepoteza kila kitu, kama kweli unataka kuwa mchawi jifunze hilo” hapo nikakumbuka tena kuwa napaswa kua mchawi, jambo ambalo hata sijui litafanikishwaje. “kwanini ni lazima awe mchawi ila kutekeleza haya majukumu?” safari hii ni baba ambaye aliuliza.. “kwa sababu bila ya kua mchawi hatoweza kufanya chochote ndani ya Muifufu, atakuwa anajipeleka kuuawa tu. Ili kufanikiwa anapaswa kuwa mchawi, tena mchawi hasa ili aweze kushindana na wachawi wa huko wenye uwezo mkubwa mno” baba akauliza tena “ wewe ni mchawi tayari, kwanini usitusaidie tu mara moja kwa hili?” sauti ile ikajibu, tena ilionesha kukasirshwa kama sio kuchoshwa na maswali yale.. “naona kama tunarudi nyuma kila baada ya kupiga hatua moja, kua mchawi sio jambo kubwa kama ambavyo ninyi mnaliona!
 
SEHEMU YA 7

Ni swala la kujua tu mbinu na kuzitumia, sio lazima uanze kuua au kuwangia watu, kila mtu anaamua jinsi ya kuutumia ujuzi anaoupata!. Ndio maana nikasema nakuachia siku nzima ya leo kisha kesho utafanya maamuzi” sauti ile ilitulia nasi tukawa kimya, baadae nikavunja ukimya “mimi niko tayari mzee, wala haina haja ya kungoja kesho ili nifanye maamuzi” sauti ile ikacheka kisa ikasema “tumerudi nyuma tena, jifunze kuwa na subira kama kweli unataka kuwa mchawi, tutaonana usiku” kisha kimya kikatawala.

Tulibaki pale tukiwa tumeduwaa, hakuna ambaye alikuwa akiongea! Nadhani kila mmoja alikuwa akijaribu kuwaza na kuwazua kama ambavyo nilikuwa nikifanya mimi. “Bado mna mpango wa kwenda kwa mganga?” mzee Miale alivunja ukimya na mimi nikamuangalia baba kama ishara ya kumtupia yeye swali hilo ili afanye maamuzi baada ya ambacho tumekiona.. “tujifunze kuwa na subira” alijibu baba akiigiza ile sauti tukacheka kisha tukaaga na kuondoka.

Usiku wa siku hiyo tulikuwepo nyumbani mapema, tukala na kuingia vyumbani mwetu! Yalikuwa kama majira ya saa tatu na sikuwa na usingizi hata kidogo, nilikuwa na hofu kidogo huku nikimgoja mzee yule nikiwa sina uhakika kama atakuja ama laa!..

Sijui hata saa ngapi nilipitiwa na usingizi ila nilikuja kujikuta nikiisikia sauti ya mtu ikiniita kwa mbali kama naota vile, niliposhituka nilijikuta katika mzingira ambayo sikuwa nikiyajua. Mbele yangu alikuwa amesimama mtu ambaye sikuwa nimewahi kumuona! Alikuwa ni mwanume wa makamo tu, hakuwa mzee wala hakuwa kijana. “karibu bwana, hapa ndipo ambapo napatikana” aliongea bwana yule lakini ilikuwa ni sauti ile ambayo ilitutembelea kwa mzee Miale na hata ambayo alikuja nayo mzee aliyenifuata nyumbani! “wewe ni Mnaro?” niliuliza baada ya kuhisi kuwa alikuwa yeye “ndio” alijibu kwa kifupi nami nikashangaa kwa maana sio yeye ambaye alikuja kwangu usiku ule. “na yule mzee ambaye alikuja kwangu alikuwa nani?” niliuliza naye akanijibu huku akiwa ameshughulika kufanya shughuli ambazo hazikueleweka, alikuwa akihamisha hamisha vitu kama vile ambaye alikuwa akikipanga upya chumba kile ambacho kilijaa makorokoro.. “nilikuwa ni mimi pia” akawa amenichanganya lakini akaendelea na kunipa mwanga “ninao uwezo wa kuonekana kama kijana, kama mzee, kama mtoto, kama mwanamke au hata kama mnyama yoyote yule” sasa alikuwa amesogeza mbele yangu kitu kama beseni kubwa sana ambalo lilikuwa limetengenezwa kwa matirio kama ya mbao hivi, kuangalia ndani ya beseni lile kulikuwa kuna kimiminika cha rangi nyekundu. “sasa ni wakati wa kumuona mkeo” aliongea mzee yule nami nikayalengesha macho yangu zaidi ndani ya beseni lile lakini hakukuwa na chochote ambacho kilionekana! Lakini akaanza kunyunyizia ungaunga ambao ulikuwa ukionekana kama majivu kisha akachukua kipande cha kitambaa na kuanza kukisemea maneno kisha akanikabidhi, nilipokiangalia vizuri niligundua kuwa kilikuwa kipande cha nguo ambayo aliivaa mke wangu siku ile ambayo alipotea, nikashangaa nguo ile aliipata wapi mzee yule kwa maana nilijua kua nguo ile ilikuwa nyumbani. “ili kumuona mtu hapa unatakiwa kuweka humo nguo yake ambayo aliivaa na haijafuliwa, ukitaka kumuona mkeo weka humo kipande hicho cha nguo yake” alisema yule mzee nami nikauliza “lakini mbona nguo yake iko nyumbani?” yule mzee akaniangalia kisha akaniuliza baadala ya kunijibu “kwani wewe ulikuwepo hapa? Haukuwa nyumbani?” nikabaki bila jibu wala swali lingine la kuuliza kisha nikawa nakiingiza kitambaa kile ndani ya kimimkinika kile ambacho nilianza kudhani kuwa kilikuwa damu. Mara niliona kimiminika kile kikianza kuchemka polepole, huku kikiongeza kasi ya kuchemka kadri muda ulivyozidi kwenda na mara kikaanza kuzunguka ndani ya beseni lile kubwa la mbao kisha nikaona kama macho yangu yanavutwa ndani ya beseni lile nikawa najaribu kujivuta kurudi nyuma lakini sikuweza kushindana na nguvu ile nikajiona kama ambaye napoteza fahamu!......

Akili iliporudi sawa nikajikuta nimesimama katika mazingira ambayo sikuwa nikiyajua, kulikuwa na miti mingi sana kama pori fulani hivi kisha nikasikia sauti ikiniita nyuma yangu, nilipogeuka nikakutana na sura ya Mnaro lakini kitu cha ajabu kilikuwa ni kichwa tu kikielea hewani bila kiwiliwili, kitu kingine cha kushangaza ilikuwa ni mchana wakati nilikuwa nikikumbuka vyema kabisa kuwa dakika chache zilizopita nilikuwepo kwa Mnaro na ilikuwa ni usiku. “tembea ukifuata njia hiyo unayoiona mbele yako kisha utakuwa umetoka nje ya pori hili na utakutana na nyumba za watu na watu mbalimbali wakifanya kazi zao kama kawaida, pita kote mpaka utakapokuta nyumba ambayo mlango wake ukiwa umetandwa na mwanga mkubwa, ingia hapo utamkuta mkeo, lengo ni kumuona na sio kumsemesha.
 
SEHEMU YA 8

Ukiongea umeharibu kila kitu, sawa?” kilielekeza kichwa kile cha Mnaro baada ya mimi kuwa nimegeuka kufuata sauti yake aliponiita nami nikaitikia kwa kukubali kisha nikauliza “sasa watu hao ambao nitawakuta wakiwa wanaendelea na shughuli zao hawatonisumbua?” kichwa cha Mnaro kikajibu.. “sisi hatupo hapa, tuko huko kwenye dunia yetu ya kawaida hivyo hakuna ambaye anakuona, ila ukiongea watakusikia” alimaliza kutoa maelezo nami nikaridhika na kuanza safari ya kufuata ile njia ambayo ilikuwa inanitoa nje ya pori lile kwa maelezo ya Mnaro.

Nilifanikiwa kutoka ndani ya pori lile na kwa mbali nikaanza kuziona nyumba, zilikuwa nyumba za kizamani sana, yani yalikuwa kama mazingira ya kijijini au sehemu ambayo haijaendelea sana. Nilianza kusikia sauti za watu na mifugo ikilia, kilikuwa ni kijiji kikubwa chenye shughuli mbalimbali. Watu wa eneo lile walionekana kuwa ni wachapakazi kila mmoja akiwajibika panapomuhusu. Nilipita nikiwavuka watu wote wale lakini sidhani kama kuna ambaye alikuwa akioniona kwa maana hakuna hata mmoja ambaye alikuwa akiniangalia ingawa nilikuwa nikiwapitia mbele yao kabisa, nikawa nikitembea nikijaribu kuitafuta nyumba ambayo mlango wake una mwanga lakini sikuiona, nikazidi kwenda mbele mpaka nikakaribia kukata tamaa lakini nikaona nyumba moja kubwa ambayo mlango wake ulikuwa wazi lakini kulikuwa na nuru kali kiasi cha kunifanya kushindwa kuona ndani yake, nikaamini Mnaro alimaanisha nyumba ile nami nikaenda na kuingia kwenye mlango ule, baada ya kuvuka mlangoni ndani hakukuwa na mwanga mkali sana nikaona watu wakiwa wamekaa kwenye mkeka eneo lile la wazi wakila chakula, nikazidi kusogea karibu na kugundua kuwa walikuwa wamekaa juu ya ngozi ya mnyama ambaye sikumjua, nilipojaribu kuwatazama vizuri nikagundua kuwa mmoja wao alikuwa mke wangu..

Alikuwa anakula kwenye sahani ya peke yake ingawa wengine walikuwa wakila kwenye sinia moja , nikasogea karibu zaidi nikaona alikuwa anakula wali na nyama ambayo sikujua ni ya mnyama gani, pembeni yake pia kulikuwa na sahani yenye matunda, niliweza kugundua kulikuwa na ndizi, machungwa na matunda mengine sikuyajua. Alikuwa na maji ya kunywa pia kwenye kikombe kikubwa cha mbao. Nilikuwa nimeduwaa nikimuangalia akila kwa upole nikaingiwa na huruma sana nikitamani nimchukue na kuondoka naye. Nikatembea kwa kasi mpaka pale alipo na kutaka kumshika mkono kumnyanyua lakini sikuweza kukamata mkono wake, mkono wangu ulikuwa ukiuvuka wake kama moshi unavyopita mbele ya mtu, roho ikaniuma sana na wakati huu machozi yalikuwa yakinitoka nikafungua mdomo wangu na kutaka kumwambia tuondoke “mke wa...” kabla sijamalizia nikakabwa kabali kubwa ya shingo....





Nilijitahidi kupambana na kabali ile ambayo ilikuwa ikinivuta nyuma lakini sikuwa na ubavu wa kukabiliana na nguvu kubwa namna ile, nikajikuta nikiburuzwa kama kiroba cha mchele kutoka eneo lile, machozi yalikuwa yakinitoka kuona kwa mara nyingine namkosa mke wangu....... tena mara baada ya kuonana naye kwa muda mfipi bila hata kupata wasaa wa kuongea naye angalau neno moja. Nilitamani angalau ningemjuza kuwa napambana kwa ajili yake na sitokubali mpaka nifanikiwe lakini haikuwepo hata nafsi ya kufikisha ujumbe huo baadala yake nikajikuta nikipoteza fahamu.

Nilipokuja kuzinduka nilikuwa pale ndani kwa Mnaro nikiwa nimelala chini kwenye kijumba kile kisicho na sakafu huku yeye akiwa amenisimamia huku amejishika kiuno. “ulitaka kufanya nini sasa?” alihoji Mnaro kwa ukali sauti yake ikiambatana na kitetemeshi cha uoga. “unajua ni muda gani nimetumia kupanga namna ya kumtoa Sauda mikononi mwa Mgugi?, kwanini unataka kuharibu kila kitu ndani ya dakika tano tu za kukuamini?” aliendelea kuhoji mfululizo wa maswali Mnaro akionekana kukerwa hasa na tukio nililolifanya akiamini lilielekea kukata matumaini ya kumpata huyo Sauda ambaye niligundua kuwa ndiye yule mpenzi wake ambaye aliolewa na baba yake. Wakati wote huu niliamua kuwa mpole kwa maana hata sikujua niseme nini, kumuona mke wangu mbele ya macho yangu baada ya kumpoteza muda wote ule kulinichanganya hata kunifanya nisifikirie vizuri nikabaki na wazo moja tu ambalo ni kurudi naye katika maisha ambayo tumeyazoea bila kujali hatari za jaribio lile, sasa akili ilikuwa imerudi mahala pake na kujiona kweli nilikuwa nimeharibu na kukosa hata neno la kujitetea.

“hebu nenda kwanza nyumbani ukakue ili kichwa xhako kiweze kukumbuka mafunzo kisha tutaendelea” aliongea tena Mnaro kauli ambayo ilinikata kata maini, nilikuwa nimepata uhakikaka sasa kuwa bwana Mnaro anaweza kunisaidia kumpata mke wangu mara baada ya kuniwezesha kufika alipo. Jambo pekee ambalo nilikuwa nikilitaka kwa wakati ule ni mipango ya haraka kuelekea kumtoa mke wangu katika himaya ile ya wachawi na sio kuahirisha tena hili zoezi.
 
SEHEMU YA 9

“usifanye hivyo ndugu yangu, najua nimekosea sana ila nimejifunza tayari..” nilisema huku nikijiburuza kurudi nyuma pale chini nilipokaa kwa maana Mnaro alikuwa akinisogelea, lakini ghafla nilimuona akiwa amekwishanifikia na kunishika kwenye paji langu la uso huku akinong'ona maneno ambayo sidhani kama yalikuwa katika lugha ya kiswahili kisha nikapoteza fahamu.



Nilipokuja kushtuka nilikuwa nimelala pale kitandani kwangu kama nilivyokuwa kabla ya kujikuta kule kwa Mnaro, nikajiuliza ilikuwa ndoto ya aina gani ile kwa maana ilikuwa ni kama mambo ambayo nilikuwa nikiyashuhudia kweli, haikufanana na ndoto nyingine ambazo nilikuwa nikiziota maisha yangu yote, nikaamka na kwenda kujitizama kupitia kioo cha dressing table ambayo ilikuwemo mule chumbani na kushangaa kujiona nikiwa nimetapakaa vumbi kama ambaye nilikuwa nikigalagala kwenye mchanga, mwili wangu pia ulikuwa ukitokwa jasho la kutosha kama ambalo nilikuwa nalo kule ndotoni, nikaamini hii haikuwa ndoto bali ni matendo ambayo yametokea kweli, nikazidi kujutia kiendo ambacho nilikuwa nimekifanya na kumuudhi Mnaro, nilianza kuona matumaini ya kumpata mke wangu yakififilia gizani, nikaumia sana.

Nikatoka na kwenda kumgongea mlango baba akaamka tukaelekea sebuleni ambapo tulikaa nikamuelezea ambacho kilikuwa kimetokea, mpaka namalizia kumuelezea nilishindwa kujizuia na kujikuta nikilia kama mtoto, niliona kama nilikuwa nimejirudisha nyuma mimi mwenyewe na sasa sina jinsi ya kufika tena ambako nilikuwa nimefikia. “huyu bwana anaonekana anakutegemea sana, yeye ana shida kama ambavyo wewe una shida na ili kutatua shida zenu ni wazi kuwa mnategemeana. Ninaamini atarudi tu kwako baada ya hasira zake kuisha” baba alisema akijaribu kunifariji na kweli kwa mara nyingine alifanikiwa kurudisha matumaini yangu angalau kwa kiasi kidogo. Tulibaki pale tukiongea, sambamba na kupanga na kupangua mpaka kukakucha ndipo tukaamu kurudi vyumbani mwetu kufidia usingizi ambao tulikuwa tumeupoteza.



Nilishtuliwa na kishindo kikubwa sana ndani ya chumba cghangu ambacho sikujua kimetokea wapi, nikastuka na kuamka harakahataka na kukaa kitandani huku macho yangu yakiangaza ndani ya chumaba kujaribu kuona kama naweza kukiona ambacho kilisababisha mshindo ule. Nilipatwa na mstuko mkubwa sana baada ya kukiona ambacho kilikuwepo pembeni ya kitanda changu. Alikuwa mnyama mwenye ukubwa wa ndama, alikuwa na sura ya mmbwa lakini pua yake ilikuwa ni kama ya ng'ombe, sikuwahi kumuona mnyama wa aina ile. Mnyama yule akawa ananisogelea polepole nami nikasimama juu ya kitanda huku nikonesha hishara ya kumfukuza kama vile nafukuza kuku “shiii! Shiiii!” lakini mnyama yule hakuonesha hata dalili ya kuogopa baadala yake akawa anatoa muunbgurumo mdogo kama ambao mmbwa huwa anautoa kuonya” nikajaribu kuhama upande wa kitanda naye akahama kunikinga nisitoroke, nikarudi upande uleule ambao ndipo ulipo mlango wa kutokea nnje ya chumba kile naye akawahi kunikinga kwa mbele kwa mara nyingine. Nikaamua kuruka kupita juu yake ili niuwahi mlango na kukimbilia nnje lakini nikatua vibaya na kuumia kifundo cha mguu wangu wa kushoto nikakitahidi kujikongoja kuuelekea mlango lakini kasi yangu ilikuwa ndogo kutokana na maumivu nikajikuta nikivutwa na mnyama yule ambaye alikuwa ameng'ata kwenye suruali yangu karibu na kiunoni, mnyama yule alikuwa na nguvu sana akaniburuza na kunirudisha karibu na kitanda yeye akawa upande ule wa mlangoni kwa mara nyingine.

Nikakimbia mpaka kwenye dressing table ambapo kulikuwa na kistuli nikakibeba na kugeuka nacho ili kukitumia kama silaha dhidi ya mnyama yule lakini nikakutana na Mnaro uso kwa uso akiwa ametoa tabasamu.

Nikashusha pumzi na kukiweka kile kistuli chini nikiwa nimekasirishwa na ujio ule wa bwana Mnaro, nikatembea kwa kuchechemea kutokana na maumivu ya mguu nikakaa kitandani. “Muifufu kuna wanyama na matukio mengi zaidi ya kutisha, huna nafasi ya kuwa muoga kama unataka kwenda huko” aliongea Mnaro huku akija pale nilipokaa akachuchumaa na kuugusa mguu ulea ambao ulikuwa na maumivu, akatulia kidogo kama ambaye anausikilizia kisha akatoa kamkoba cha ngozi ambacho ulikuwa amekibeba na kutoa majani fulani ambayo yalikuwa yamenyauka kisha akayatafuna na kutemea mkononi kwake halafu akaanza kunipaka kuzunguka kifundo cha mguu wenye maumivu huku akisema vineno vya kilugha kwa kunong'ona, mara mguu ule ukapatwa na hali ya umoto kama uliowekwa karibu na jiko la mkaa kisha maumivu yote yakapotea. Nilishangaa sana, kutokana na kuwa mwanamichezo najua jishi ambavyo maumivu ya kifundo cha mguu yanavyochukuaga muda mrefu lakini yeye alitibu ndani ya sekunde chache tu...

“huu ni mwezi wa 6, mwezi ambao Mgugi huchagua mke mwingine kila mwaka, mwaka huu kuna uwezekana mkubwa sana wa mkeo kuchaguliwa kwa maana Magugi ameonesha waziwazi kuwa anavutiwa naye” alielezea Mnaro habari ambazo sikutamani kuzisikia katika maisha yangu yote, nikajikuta napatwa na wasiwasi mara kumi zaidi ya ambao nilikuwanao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom