Simulizi: Mji

Simulizi: Mji

ILIPOISHIA...
Tina hakujua kabisa kuwa mimi nilikuwa ni mfuasi
wa shetani laiti angenigundua basi asingedhubutu
kujenga ukaribu na mimi, Sikutaka mtu hata mmoja
ajue siri zangu hivyo nilipanga kumuua mtu yoyote
ambaye atagundua siri zangu. Wahenga huwaga
wanasema ukizoeana sana na mbwa iko siku
atakufata hadi msikitini, Hii kauli iliweza
kujidhihilisha kutoka kwa Tina ambaye alikuja
kuniletea seke seke kubwa.
SASA ENDELEA....Mimi na Tina tulizoeana sana yani
tulikuwa ni marafiki wakubwa kupita maelezo, Tina
kidogo alikuwa amekolea kwenye dini hivyo kila
siku ya jumapili ilikuwa ni lazima ahudhulie kanisani,
Alinishawishi na mimi niende kanisani kwao kusali
lakini nilimwambia kuwa dini yangu ni tofauti na
yake hivyo siwezi kuingia kanisani, Tina
hakunilazimisha sana kwani naye pia hakuwa
mkamilifu kwenye dini, kuna siku alikuwa anaenda
lakini kuna siku nyingine alikuwa haendi. Mimi na
Tina tulikuwa na tabia ya kutembeleana majumbani
kwetu, Nilikuwa nina uwezo wa kushinda kwa Tina
siku nzima hata Tina alikuwa na uwezo wa kushinda
kwangu siku nzima japo nilikuwa makini sana
kumchunga Tina asije akaingia kwenye kile chumba
maalumu na kuzigundua siri zangu, Kuna siku moja
nilikuwa nimetoka kwenda kwenye mizunguko
yangu, ilikuwa ni mizunguko ya kawaida tu ambayo
haikuwa na umuhimu wowote, Nikiwa barabarani
natembea simu yangu ya mkononi aina ya Samsung
j8 iliita, Niliichomoa kwenye mkoba wangu wa pinki
ili niangalie jina la mpigaji, Sikushangaa sana baada
ya kuona Tina ndiye aliyekuwa ananipigia lakini
nilivyoipokea ile simu nilijikuta natetemeka mwili
mzima, Tina alinipigia ile simu huku akinieleza ya
kwamba yupo nyumbani kwangu amekuja
kunitembelea lakini ameshangaa kuona milango ya
nyumba yangu iko wazi, Ile kauli ya Tina ya milango
kuwa wazi iliniogopesha sana nikajawa na hofu
isiyoelezeka, Niliamua kumwambia Tina asiingie
ndani lakini kwasababu Tina alikuwa amenizoea
sana aliamua kuhoji kwa nini asiingie ndani, Mimi
niliendelea kumsisitiza aondoke nyumbani kwangu,
Nilimsikia Tina akicheka sana huku akiniambia kuwa
nitamkuta sebuleni kwangu anaangalia Runinga,
Niliona kuendelea kuongea na Tina ni kupoteza
muda hivyo niliamua kukata simu ili nirudi nyumbani
kwangu kabla mambo hayajaharibika, Siku iyo
ilikuwa ni kama siku ya mkosi kwangu kwani hata
daladala ambayo nilikuwa nimepanda ilikuwa
inatembea mwendo wa taratibu sana hadi nikawa
namfokea dereva atuwahishe, Foleni nayo ilikuwa ni
kubwa sana barabarani, Niliogopa sana akili yangu
ilikuwa inamuwaza Tina kwasababu nilihisi huenda
akawa ameingia kwenye kile chumba ambacho
nikikuwa nimehifadhi vichwa vya wanaume ambao
niliwaua. Baada ya kusota sana kwenye foleni
takribani nusu saa hatimaye nilifanikiwa kurudi
nyumbani, Nilikuta mlango wa nje umefungwa,
Nilipoangalia kwenye kibaraza niliona viatu vya kike
vipo chini, Moyo wangu ulinipasuka sana nikajua
dhahiri Tina anaweza kuwa amegundua siri zangu,
Kabla ya kuingia ndani nilijiwazia sana lakini
nikaikumbuka ahadi yangu ya kwamba mtu yoyote
ambaye atagundua siri zangu lazima afe, Hivyo kwa
vyovyote Tina ilikuwa ni lazima afe. Niliufungua
mlango na kuingia ndani, Nilikuta Runinga yangu
ikiwa imewashwa bila mtu yoyote kuitazama,
Sikujaji sana nilitembea kuelekea kwenye kile
chumba changu maalumu chenye vichwa vya
binadamu, Sikuamini macho yangu baada ya kukuta
kile chumba kipo wazi huku Tina akiwa ameanguka
chini na kupoteza fahamu, Nilimnyanyua taratibu
nikamuingiza ndani ya kile chumba kisha
nikamfungia ndani yake, Baadhi ya vichwa vilikuwa
vimeoza na kuharibika huku vikitoa harufu kali,
Vichwa vingine vilikuwa vimebakia mifupa tu yani
nyama zote zilikuwa zimeoza na kuisha. Nilimfunga
Tina kamba mikononi na miguuni ili akizinduka
asiweze kukimbia, Sikuishia apo kwani nilimuwekea
matambala mdomoni ili asije akapiga kelele, Baada
ya kufanya vile nilimuona Tina akifumbua macho
kutoka kwenye usingizi mzito ambao alikuwa
amelala, Nilitoka ndani ya kile chumba haraka sana
nikawa nasubilia ifike saa saba usiku ili nikafanye
jambo la kikatili kwa Tina.
Saa saba ilivyofika nilirudi ndani ya kile chumba
nikiwa nimeshikilia kile kinu changu kikubwa huku
ndani yake kukiwa kuna mkasi na kisu kikubwa,
Tina alionekana kunishangaa sana huku akiwa
amejawa na uoga mwingi kwani alionekana
akiweweseka kutaka kujiokoa lakini ilikuwa ni
vigumu kwasababu nilikuwa nimemfunga kamba na
kumziba mdomo. Nilipanga kumkata tina viungo
vyake vyote na kuvitwanga kwenye kile kinu, Sikuwa
na huruma hata kidogo linapokuja swala la kuondoa
uhai wa mtu.
 
ILIPOISHIA....
Saa saba ilivyofika nilirudi ndani ya kile chumba
nikiwa nimeshikilia kile kinu changu kikubwa huku
ndani yake kukiwa kuna mkasi na kisu kikubwa,
Tina alionekana kunishangaa sana huku akiwa
amejawa na uoga mwingi kwani alionekana
akiweweseka kutaka kujiokoa lakini ilikuwa ni
vigumu kwasababu nilikuwa nimemfunga kamba na
kumziba mdomo. Nilipanga kumkata tina viungo
vyake vyote na kuvitwanga kwenye kile kinu, Sikuwa
na huruma hata kidogo linapokuja swala la kuondoa
uhai wa mtu.
SASA ENDELEA....Nilimuangalia Tina kwa macho
makavu kabisa, muda huo kitu ambacho nilikuwa
ninakiwaza ni kuua tu, Tina alitamani kuniambia
jambo lakini sauti haikuweza kumtoka kwasababu
nilikuwa nimemziba na matambala mdomoni,
Nilichukua kile kisu nikawa na lengo lakumchinja
Tina, Nilivyokisogeza kisu maeneo ya shingo
nilimuona Tina akiangaika sana kana kwamba kuna
kitu alikuwa anataka kuniambia, Kwa hasira niliamua
kumtoa Tina yale matambala mdomoni nikiwa na
lengo la kumsikiliza kitu ambacho anataka
kuniambia, Nakumbuka Tina aliongea maneno
makali sana huku machozi yakimtililika, Maneno ya
Tina yalipenya vizuri kwenye masikio yangu,
Yalikuwa ni maneno ambayo yalinifanya niingiwe na
huruma kiasi, Huruma ambayo sikuwahi kuwa nayo
kabla, Tina alielezea jinsi tulivyokuwa marafiki
tulioshibana, Tina hakutaka kabisa kufa hata kidogo
hivyo aliniomba nisimuue huku akiniahidi kuitunza
ile siri bila kumwambia mtu mwingine, Niliinua
shingo ya Tina nikiwa na lengo lakumchinja lakini
huwezi amini kwa mara ya kwanza nilishindwa
kufanya hivyo, Roho ya huruma dhidi ya Tina ilinijia,
Nilishindwa kabisa kupitisha kile kisu kwenye
shingo ya Tina. Ni kama kuna kitu kiliniingia
kichwani nikakitupa kile kisu huku nikiilaumu nafsi
yangu kwa kitendo cha kushindwa kumuua Tina,
Niliamua kumuacha tina akiwa salama lakini
nilimpa onyo kali sana, Nilimwambia yale mambo
aliyo yaona ndani ya kile chumba changu maalumu
ibakie kuwa siri yake kwani akimueleza mtu yoyote
basi atapata upofu wa milele, Baada ya kumuonea
Tina huruma niliamua kumfungulia zile kamba ila
nilimruhusu kuondoka mida ya asubuhi. Siku
iliyofuata Leandro luciker alinitokea na kunifokea
vikali kuhusu kile kitendo nilichokifanya cha
kumuacha Tina akiwa hai, Leandro luciker aliniambia
kuwa kile ni kitendo cha hatari sana kwenye maisha
yangu kwani hakuna binadamu ambaye anaweza
kukaa na siri ya kutisha kama ile kwa muda mrefu,
Nilimtoa wasiwasi Leandro luciker nikamwambia
asijali kwani Tina hawezi kutoa ile siri kwasababu
nimempa adhabu ya kumuweka upofu endapo
ataitoa ile siri. Maisha yaliendelea kama kawaida
Tina akapunguza ukaribu kwangu kwani alikuwa
ananifahamu fika ya kwamba mimi nilikuwa mtu
mkatili tena mfuasi wa shetani, Sikumjali sana Tina
kwani kitu nilichokuwa nimemwambia ni kuitunza
siri aliyoweza kuigundua ndani ya chumba changu
maalumu. Siku zilivyozidi kusonga mbele nilianza
kuona utofauti kutoka kwa Tina kwasababu nilianza
kuona wahubiri mbali mbali wakiwa wanakuja kusali
nje ya nyumba ambayo Tina alikuwa anaishi, Kile
kitendo kilinikera sana kwasababu kwa asilimia
kubwa kilikuwa kinanivurugia mipango yangu ya
kiuchawi ambayo nilikuwa ninaipanga kila siku,
Niliamua kumpa Tina onyo kuhusu wale wahubili
lakini Tina aliniambia kuwa wale wahubiri walikuwa
ni watu wa jumuhiya yake ya kusali hivyo ilikuwa ni
ngumu kwa yeye kuwazuia wasije pale kwenye
nyumba aliyokuwa anaishi. Niliamua kuvumilia kwa
muda lakini nilianza kushindwa kabisa kwani yale
mahubiri yalionekana kuwa na nguvu sana,
Asikuambia mtu kuna wahubiri wanapiga neno, Japo
dunia ya sasa hivi wahubiri wengi ni waongo lakini
wale wahubiri waliokuwa wanakuja kwa Tina
walikuwa wana upako wa ukweli kutokana na
matukio ambayo yalikuwa yananitokea. Kuna siku
mida ya usiku nikiwa nimetoka kwenye shughuri
yangu ya kiuchawi nilianza kuhisi mwili wangu
ukiniwasha, Mwanzoni muwasho ulianza taratibu
lakini kadri muda ulivyokuwa unazidi ule muwasho
uliongezeka maradufu, Mwili wangu uliniwasha sana,
Nilijikuna hadi ngozi ya mwilini ikawa inachunika,
Nilianza kuangaika ndani ya ile nyumba yangu
nikiitaji msaada wa kuondoa ule muwasho,
Nilikimbia hadi jikoni nikajipaka majivu lakini ndio
kama nilikuwa nimemwagia mafuta kwenye moto
kwani muwasho uliongezeka maradufu, Ungenionea
huruma kwa jinsi nilivyokuwa najikuwa, Ilikuwa ni
kama mtu amenitupia furushi la upupu, Kipindi
naangaika nilisikia sauti kwenye nyumba ya jirani
zikiwa zinapamba moto, Kwa mbali nilisikia kama
mahuburi yanaendelea, Kwa usiku ule ilikuwa ni
vigumu kuamini kama maombi yalikuwa yanafanyika
lakini kiukweli ni kwamba Tina alikuwa amepanga
kuniangamiza kabisa kwasababu siku iyo wahubiri
wengi walikuwa wamefurika nyumbani kwake
wakiwa wanafanya maombi. Yale maombi
yalivyopungua na muwasho mwilini mwangu ulikuwa
unapungua, Nilitokea kumchukia Tina kwasababu
alionekana dhahiri kuwa alipania kupambana na
mimi, Asubuhi kulivyokucha nilikuwa namuogopa
sana Tina, Ujasiri wangu wote ulionekana kupungua
kwa kasi, Wale wahubiri hawakuacha kuja kwa Tina,
Nilikuwa ninakimbilia ndani kujificha pindi
nilipokuwa ninawaona wale waumini. Yale
mapambano yalionekana kunishinda ikabidi
nimueleze Leandro luciker jinsi nilivyokuwa
ninateswa na maombi ya wale wahubiri, Leandro
Luciker alinikasirikia sana akaniambia kuwa kitendo
cha kumuacha Tina mzima lilikuwa ni kosa kubwa
sana kulitenda. Leandro luciker aliamua kuingilia
kati lile jambo aliniambia nimuachie lile swala
apambane nalo. Nilifurahi sana kuona Leandro
luciker ameonesha nia ya kunisaidia hivyo nilikuwa
nimerejewa na furaha upya, Hatukuongelesha tena
na Tina kwani nilitokea kumchukia, Nilitamani
kumuua kabisa lakini nilikuwa ninashindwa. Baada
ya wiki moja kupita kuna tukio la kushangaza
lilizuka mtaani, Nikiwa ndani nimejipumzisha
nilisikia sauti nyingi zikipiga kelele nje ya nyumba
yangu, Nilipochungulia dilishani niliona kuna mtu
anapigwa mithili ya mwizi, Niliamua kutoka ili
nishuhudie lile tukio lakini nilishtuka baada ya kuona
Leandro luciker anapigwa mawe huku akiwa
amevalia mashuka meusi, Pembeni ya wale watu
alikuwepo mtu mmoja ambaye mkononi alikuwa
ameshikilia biblia, Kumbe kipindi Tina na waumini
wenzake wanafanya maombi Leandro luciker alitaka
kuwajaribu na kwa bahati mbaya akajikuta
anazidiwa nguvu na kuonekana akiwa kwenye
muonekano wa mtu anayewanga, kwa macho yangu
nilimshuhudia Leandro luciker anapigwa mawe hadi
kufa japo yule mtu aliyeshikilia biblia alikuwa
anawazuia raia wenye hasira kali wasimuue lakini
ilishindikana. Moyoni nilijisikia vibaya lakini ilibakia
ni mimi na Tina. Tina alikuwa anatamani kunitaja
lakini alikuwa anahofia kuwa kipofu, Kwa masikio
yangu nilimsikia Tina akiongea kwenye ule umati wa
watu kuwa anataka kumtaja mtu mwingine ambaye
ni mshirikina mkubwa, Kwa yale maneno ilionesha
dhahiri Tina alikuwa amenilenga mimi.
 
ILIPOISHIA...
Tina alikuwa anatamani kunitaja lakini alikuwa
anahofia kuwa kipofu, Kwa masikio yangu nilimsikia
Tina akiongea kwenye ule umati wa watu kuwa
anataka kumtaja mtu mwingine ambaye ni
mshirikina mkubwa, Kwa yale maneno ilionesha
dhahiri Tina alikuwa amenilenga mimi.
SASA ENDELEA....Niliamua kurudi ndani haraka
nikiwa na lengo lakuondoka lile eneo kwasababu
nilihisi muda siyo mwingi mambo yatanibadilikia na
mimi. Kipindi naingia ndani ya nyumba yangu
nilisikia sauti za watu wakipiga kelele huku
wakiikaribia nyumba ambayo nilikuwa ninaishi,
Nilivyojaribu kuchungulia kwenye uwazi wa mlango
niliona kundi kubwa la raia wenye hasira kali likiwa
linakuja uelekeo wa nyumba yangu, Kwa mbali
nilimuona Tina akiwa anapapasa kama mtu
asiyeweza kuona, Akili ilinicheza nikajua Tina
alikuwa amevujisha siri ambayo alikuwa anaifahamu
kuhusu mimi, Nilikimbia ndani zaidi nikaingia
chumbani mwangu kisha nikajipaka unga mweupe
mwili mzima, Nilivyomaliza kujipaka ule unga
nilinena maneno ya kichawi kisha nikajibanza
kwenye kona ya ukuta wa chumbani mwangu,
Haikupita muda watu wengi walivamia ndani ya
nyumba yangu huku wakipekua kila sehemu, Watu
wengine waliingia hadi chumbani ambamo nilikuwa
nimejificha lakini walikuwa hawana uwezo
wakuniona ila mimi ndiye niliyekuwa na uwezo
wakuwaona, Wale watu walikuwa wameshikilia
silaha za jadi huku wakiongea maneno makali,
Maneno ambayo yalilenga kuniangamiza mimi
Halima. Nilianza kunyata taratibu nikitoka nje ili
niikimbie ile nyumba, Nilifanikiwa kutoka nje lakini
kitendo cha kutoka nje nilihisi mwili wangu unawaka
moto kwasababu nilimuona Tina akiombewa na
wale wahubiri tena kwa nguvu sana, Sikuamini
baada ya kumshuhudia Tina akiona tena. Miujiza
iliyokuwa inatendeka kwenye lile eneo ilinitisha sana
nikaamua kutimua mbio. Nakumbuka nilifanikiwa
kuondoka ule mtaa wa mwembe nikaenda mbali
zaidi, Baada ya kutembea sana nilifanikiwa kufika
sehemu ambayo sikuhifahamu vizuri kwasababu
sikuwa mwenyeji. Kwakuwa nilikuwa nina pesa kiasi
niliamua kwenda kupata chakula kwenye moja ya
hoteli ndogo ambayo ilikuwa inapatikana maeneo
yale, Muda huo nilikuwa nimeshajifuta ule unga
mweupe ambao nilikuwa nimejipaka hivyo nilikuwa
katika hali ya kawaida, Nilipojaribu kumuuliza
muhudumu aliyenipatia chakula alinijibu kuwa
nilikuwa nipo katika mtaa wa korogwe, Baada ya
kuambiwa vile nilimalizia kula kisha nikaanza
kuondoka kuelekea eneo ambalo sikuwa
nikilifahamu, Nilivyokuwa njiani niliwaza mengi
sana, Nilijiuliza ni wapi ninaelekea lakini sikupata
jibu la uhakika. Siku iyo sikuwa na sehemu ya
kwenda hivyo niliamua kujihifadhi kwenye moja ya
jumba bovu ambalo lilikuwa halijaisha vizuri,
Sikuogopa giza la aina yoyote kwasababu nilikuwa
ni mfuasi wa shetani hivyo giza lilikuwa ni nuru
yangu, Kipindi nimejilaza ndani ya like jumba
nilisikia sauti mbili zikivutana, Sauti moja ilikuwa
inaniita ikimaanisha nirudi ndani ya mji wa laana ila
sauti ya pili ilikuwa inanihamasisha mambo ya
wokovu, Nilishtuka kutoka usingizini kwani nilihisi
ile ndoto yaweza kuwa na maana kubwa sana.
Huwezi amini kwani nilivyoshtuka niliweza
kumshuhudia mtu ambaye sura yake ilikuwa
haionekani akiwa amesimama mbele yangu, Yule
mtu alikuwa amevalia vazi jeupe lililokuwa linang'aa
mithili ya dhahabu, Nilitaka kukimbia lakini yule mtu
alitoa sauti ya ngurumo huku aniniambia kuwa mimi
ni mteule ambaye ninahitajika sana nikafanye jambo
la kuwakomboa wana wa Mungu waliopotea,
Nilishangazwa na ile kauli ya yule mtu aliyenitokea
kwani mimi nilikuwa ni mtu mchafu zaidi ambaye
nilizungukwa na dhambi ya kila aina. Yule mtu
baada ya kunena yale maneno alipotea mithili ya
upepo nikabaki mwenyewe natafakali. Yani Halima
mimi nilihitajika nikalieneze neno kwa wana wa
Mungu waliojawa na dhambi wakati nilikuwa
mchafu wa kutupwa na mbaya zaidi jina langu
lilikuwa lipo upande wa pili wa dini, Hilo jambo
halikuniingia akilini hata kidogo.
 
ILIPOISHIA....
Sikuamini kabisa yani Halima mimi nilihitajika
nikalieneze neno kwa wana wa Mungu waliojawa na
dhambi wakati nilikuwa mchafu wa kutupwa na
mbaya zaidi jina langu lilikuwa lipo upande wa pili
wa dini, Hilo jambo halikuniingia akilini hata kidogo.
SASA ENDELEA....Baada ya kutafakari kwa muda
mrefu usingizi ulinipitia tena nikashtuliwa asubuhi na
sauti za watu waliokuwa wanakatiza pembezoni
mwa ile nyumba ambayo nilikuwa nimejificha,
Niliamua kuinuka haraka haraka ili niondoke katika
lile eneo. Nilitembea kwa muda mrefu ndani ya ule
mtaa wa korogwe huku nikiyawaza yale maneno ya
yule mtu aliyenitokea usiku wa jana. Kuna muda
nilikoswa koswa kugongwa na piki piki ambayo
ilikuwa inakatiza barabarani, Yule aliyekuwa
anaendesha piki piki alinitukana matusi makali
ambayo yaliniuma lakini sikumjibu kwasababu mimi
ndiye niliyekuwa nina kosa, Sikuwa muangalifu pindi
nilipokuwa nakatiza barabarani ndio mana ilibakia
kidogo yule dereva wa pikipiki anigonge. Nilikuwa
natembea barabarani huku nikilia japo sikutoa sauti
lakini machozi yalikuwa yananitililika, Moyo wangu
uliniuma sana pindi nilipofikilia maisha ambayo
nilikuwa ninayaishi mkoani Simiyu kabla ya kuwa
mfuasi wa shetani, Kiukweli kwa kipindi kile
nilikuwa nina mipango mizuri ambayo ilikuwa ni
kuolewa na kuishi maisha ya furaha na mume
wangu lakini ndoto zile zote zilikatizwa na bibi
yangu ambaye alinisababishia matatizo makubwa
sana. Niliamua kujifuta yale machozi na mkono
wangu wa kulia kisha nikapanga kujisalimisha
sehemu husika ili nipumzike kwani maisha ya
kumtumikia shetani yalikuwa yamenichosha,
Sikutaka tena kuwa mtumwa wa shetani,
Nilipokatiza upande wa pili wa barabara niliona
kikundi kikubwa cha watu kikipita huku kinaimba
nyimbo mbali mbali za kusifu na kuabudu jina la
mwenyezi mungu, Kile kikundi kilikuwa kimevalia
sare za njano kama waimba kwaya, Wananchi nao
walikuwa nyuma wakikisindikiza kile kikundi huku
wakiwasapoti kwa kuimba nyimbo zao, Niliamua
kuwafata wale watu kwa nyuma nikiwa na lengo la
kufahamu sehemu ambayo walikuwa wanaelekea,
Safari yao iliishia kwenye uwanja mkubwa wa mpira
ambao ulikuwa umefungwa spika kubwa ambazo
ziliweza kutoa sauti za muhusika ambaye alikuwa
anaongea, Ule uwanja ulikuwa umefurika watu wengi
sana, Nilifikiri inaweza kuwa mkutano wa raisi lakini
haikuwa vile kwasababu raisi hakuwepo eneo lile,
Nilipoangalia vizuri kwa mbele niliweza kuona
jukwaa kubwa huku kwa juu yake amesimama
mwanaume mmoja aliyekuwa anaongea kwa sauti
kubwa, Maneno ya kwanza ambayo niliyasikia
maeneo yale yalikuwa yanasema (BWANA YESU
ASIFIWE), Hayo maneno yalionekana kuwa tofauti
na mimi kabisa siyo kwamba sikuyapenda bali
misingi ya dini yangu ilikuwa haiendani nayo hata
kidogo, Nilihisi lile halikuwa eneo sahihi kwa ajili
yangu, Nilianza kurudi nyuma taratibu ili niondoke
mahala pale, Kipindi naondoka kuna mtu
nisiyemfahamu alinishika bega akaniambia maneno
ambayo yaliniweka njia panda, Yule mtu alionekana
kunifahamu sana kwani aliniita kwa jina langu kamili
kisha akanisihi nisiondoke nibakie eneo lile ili
niweze kufunguliwa, Nilimshangaa sana yule mtu
lakini kabla sijaongea kitu chochote yule mtu
alinipotea kwenye mazingira ya kutatanisha. Yale
maneno ya yule mtu yalionekana kuniingia kiasi
kwani zoezi la kuondoka nilighairi kisha nikaanza
kujisogeza karibu kabisa na lile jukwaa ambalo
alikuwa amesimama mtu ambaye alijulikana kama
mchungaji, Safari hii sikuangalia utofauti wa dini
yangu wala nini, Nilijikuta napata hamu ya
kumsikiliza yule mchungaji ambaye siwezi kumtaja
jina lake kutokana na sababu za usalama wa maisha
yangu. Yule mchungaji alihubiri maneno mazuri
yakumtumikia Mwenyezi Mungu kisha akaanza
kurudisha watu waliokuwa wamechukuliwa kiuchawi
yani misukule, Lile jambo la misukule lilinifanya
niwe makini kulifatilia, Misukule mingi sana
ilirejeshwa kwenye hali ya kawaida. Yule mchungaji
aliendelea kuhubiri kwa nguvu hadi nikahisi yale
maombi yananilenga mimi kwani mwili wangu
ulianza kufa ganzi huku nikiishiwa nguvu taratibu,
Nilishangaa kuona yule mchungaji akiongea kuhusu
kuuteketeza Mji wa laana huku akisema kuwa huo ni
mji ambao ulikuwa upo sehemu za siri sana, mji
ambao watu wake wamelaaniwa kwa laana ambazo
wanazitenda, Baada ya mchungaji kuongea yale
maneno nilianguka chini kama mzigo nikiwa
sijielewi hata kidogo, Sikufahamu kitu
kilichoendelea lakini nilikuja kushtuka na kujikuta
nipo juu ya jukwaa huku mchungaji akinipa kipaza
sauti nitoe ushuhuda wa matukio yaliyonitokea,
Nikijikuta naropoka maneno mazito bila kusita,
Niliongea mambo yote niliyoyatenda huko nyuma
hadi ule umati wa watu ukawa unatahamaki, Kila
mtu alishangaa ule ushuhuda wangu. Yule
mchungaji alinishika kichwani kisha akaniambia kwa
damu ya Yesu mwana wa kondoo nimetakaswa na
kuwa kiumbe kipya, Yule mchungaji aliongea mbele
ya ule umati wa watu kwamba atanichukua na
kunifanya niwe mfuasi wa Kumtukuza mwenyezi
Mungu maisha yangu yote. Baada ya kuombewa na
dini ambayo haikuwa upande wangu nilihisi
nitakuwa kwenye mstari mnyoofu wa kuyatenda
mema lakini kilichokuja kunitokea kilifanya niache
kumuamini mtu yoyote juu ya uso huu wa dunia.
Roho inaniuma halima mie, Kwanini lakini maisha
yangu yalikuwa vile, Kwenye kimbilio napo
panageuka kuwa sehemu chungu kwangu, kama
nitakuwa nimekosea naomba nisamehewe lakini
nitaweka wazi kila kitu ambacho kilinikuta baada ya
kuchukuliwa na yule mchungaji.
 
ILIPOISHIA....
Roho inaniuma Halima mie, Kwanini lakini maisha
yangu yalikuwa vile, Kwenye kimbilio napo
panageuka kuwa sehemu chungu kwangu, kama
nitakuwa nimekosea naomba nisamehewe lakini
nitaweka wazi kila kitu ambacho kilinikuta baada ya
kuchukuliwa na yule mchungaji.
SASA ENDELEA....Nakumbuka baada ya kutoka
kwenye maombi pale uwanjani niliweza kuongozana
na yule mchungaji ambaye alinipeleka hadi kanisani
kwake na kunitambulisha kwa waumini wake,
Niliweza kufundishwa mambo mengi sana
yaliyokuwa yanahusiana na ukristo hadi nikafanikiwa
kuijua ile dini vizuri, Maisha ya wokovu yalitokea
kunipendeza kwani sikupata tena misukosuko
kutoka katita jamii ya kichawi, Yule mchungaji
alinikabizi kwa mmoja wa waumini wake ambaye
alikuwa anajulikana kwa jina la Eda, Niliishi na Eda
kwenye misingi ya dini kwani tulikuwa tunasifu na
kuabudu kila siku huku tukijaribu kufundishana tabia
njema ambazo tulihisi ni tabia za kupendeza. Kitu
ambacho nilishindwa kubadilisha ilikuwa ni jina
hivyo niliendelea kutumia jina langu halisi la Halima
japo nilikuwa nimeingia katika ukristo. Mimi na Eda
tulifanya vitu vingi vya kuliendeleza kanisa la yule
mchungaji kwa kiufupi tulikuwa tumebobea kwenye
dini, Ilikuwa ni ngumu kuniamini kuwa nilikuwa nina
asili ya uislamu. Nilibadilika kabisa kitabia nikawa
mtu wa kuchukia maovu, nilijaribu kuzieneza habari
ya uzima kila mahara japo nilikuwa nakutana na
ugumu kwasababu watu wengi waishio Tanga
walikuwa hawauamini ukristo ila nilijitahidi kadri ya
uwezo wangu kulitangaza jina la bwana, Sikuangalia
utofauti wa dini za watu lakini mimi nilichoangalia ni
namna ya kuwaonya watu wasifanya maovu. Baada
ya miezi kadhaa kupita Eda alianza tabia ya kuwa
kila ikifika saa nne usiku ananiacha chumbani
mwenyewe na kuelekea kwenye nyumba moja wapo
ambayo alikuwa anapendelea kuishi yule mchungaji
mkuu, Nilijaribu kumuhoji Eda kitu ambacho
anafuata kwenye ile nyumba lakini Eda aliniambia
kuwa huwa anaenda kufanya maombi na mchungaji,
Sikufikilia vibaya bali nilihisi ni jambo la heri
kushiliki maombi na mchungaji. Ile tabia ya Eda
iliendelea vile vile hadi nikawa nimeizoea,
Nakumbuka kuna siku nikiwa nimelala niliota ndoto
ambayo ilikuwa inafumbo kubwa sana, Fumbo
ambalo lilikuwa linamuhitaji mwanafunzi mwenye
uwezo mkubwa kulitatua, Nilimuota yule mtu
ambaye alinitokea kwenye lile jumba bovu miezi
kadhaa iliyopita, Yule mtu niliyemuota alikuwa
anaongea kwa sauti ya masikitiko akinikumbusha
kwenda kuitangaza injili ya bwana, Yule mtu
aliniambia kwa nini ninapoteza muda kwa mambo
ambayo hayanifai hata kidogo, Baada ya yule mtu
kuongea yale maneno alitoweka. Nilishtuka kutoka
kwenye ile ndoto nikasali kwa nguvu zangu zote
kisha nikalala. Siku tatu mbeleni baada ya kuota ile
ndoto Eda aliniambia ninaitwa na mchungaji kwenye
ile nyumba ambayo huwa anapenda kwenda kusali
naye, Nakumbuka ilikuwa ni mida ya saa nne usiku,
Nilijiweka kiheshima kisha nikaelekea kwenye ile
nyumba ambayo haikuwa mbali sana na nyumba
ambayo tulikuwa tunaishi na Eda, Nilivyofika ndani
ya ile nyumba nilimkuta mchungaji akiwa ameketi
mezani huku akionesha kutabasamu, Nilijaribu
kumuuliza mchungaji kitu alichoniitia lakini yule
mchungaji aliinuka kisha akanisogelea karibu na
kuniuliza ya kwamba Eda hajanitaarifu kitu chochote,
Nilishindwa kuelewa ile kauli yake, Nikiwa natafakali
kitu cha kufanya, Yule mchungaji alinishika sehemu
ambayo ilikuwa ni kama udhalilishaji kwenye mwili
wangu, Sikuamini kabisa mambo ambayo yalikuwa
yanataka kutokea, Kumbe kile ndio ambacho Eda
huwa anakuja kufanya na yule mchungaji kila ifikapo
saa nne usiku. Sikuwa tayari kujidhalilisha tena
kwani nilikuwa nimeshaamua kuwa mtu mwema
hivyo sikutaka kufanya uchafu mwingine maishani
mwangu, Nilimkatalia yule mchungaji lile swala lake
la kushiriki ngono na mimi, Huwezi amini yule
mchungaji alitaka kunibaka kwa nguvu lakini
nilimshinda na kutoka nje ya nyumba yake, Nilirudi
kwa Eda huku nikiwa nina hasira nyingi, Nilimlaumu
Eda kwa upuuzi ambao alikuwa anaenda kuufanya
na yule mchungaji, Eda aliniangalia kwa muda kisha
machozi yakaanza kumtililika, Eda aliamua
kunielezea sababu iliyokuwa inafanya agawe mwili
wake kwa yule mchungaji ambaye nilianza kumuona
kama mchungaji wa uongo. Eda aliniambia hakuwa
na baba wala mama, Yule mchungaji alimchukua
Eda kutoka mitaani kwa lengo la kumlea kwenye
misingi ya kidini lakini mwisho wa siku alikuwa
anamtumia kingono kila siku, Eda hakuweza kupinga
kwasababu kula yake na kuvaa kulimtegemea yule
mchungaji. Eda alivyomaliza kuongea Roho yangu
iliniuma sana nikamwambia Eda afunge macho
tusali. Tulisali kwa pamoja ili kukemea ule uchafu
lakini tukiwa katikati ya maombi ilisikika sauti ya
mtu ikitukejeli, Ile sauti ilisikika ikisema
(MMEMALIZA KUSALI?).
 
ILIPOISHIA....
Eda alivyomaliza kuongea roho yangu iliniuma sana
nikamwambia Eda afunge macho tusali. Tulisali
kwa pamoja ili kukemea ule uchafu lakini tukiwa
katikati ya maombi ilisikika sauti ya mtu ikitukejeli,
Ile sauti ilisikika ikisema(MMEMALIZA KUSALI).
SASA ENDELEA...Niliendelea na maombi huku
nimefumba macho yangu nikiwa najaribu kuipotezea
ile sauti ili nisiisikie masikioni mwangu, Kumbe Eda
baada ya kuisikia ile sauti alisitisha maombi akawa
anahofu juu ya ile sauti ambayo ilisikika bila
kuonekana mtu aliyekuwa ameitoa. Baada ya
kumaliza maombi yangu nilifumbua macho yangu
nikawa namuangalia Eda kwa ujasiri wa hali ya juu,
Niliongea kwa nguvu nikimaanisha mtu aliyeitoa ile
sauti ajitokeze kama kweli anajiamini. Huwezi amini
hazikupita dakika nyingi yule mchungaji alitokea
ghafla maeneo ya pembezoni kwa ukuta huku
amevuta mdomo wake kwa kukasirika, Eda
uvumilivu ulimshinda akawa anaogopa hadi
akazimia kwa lile tukio alilolishuhudia, Muda huo
mkononi nilikuwa nimeshikilia kitabu kitakatifu(bibl
ia) nikijaribu kusali kumkemea yule mchungaji wa
uongo ambaye alijitokeza akiwa kwenye muonekano
wa tofauti kidogo kwani alikuwa kwenye umbile la
nusu binadamu nusu nyoka, kuanzia kiunoni kwenda
juu alikuwa ana umbile la kibinadamu lakini kutoka
kiunoni kwenda chini alikuwa ana umbile la nyoka,
Meno yake mawili ya mbele yalikuwa
yamechongoka mithili ya misumali mikubwa
iliyokuwa mikali, Muonekano wa yule mchungaji wa
uongo ulikuwa unatisha sana ndio maana Eda
alizimia. Nilijitoa kwa ajili ya kumtumikia mwenyezi
Mungu hivyo uoga ulikuwa mbali na mimi japo kuna
muda nilikuwa napata wasiwasi ila niliendelea
kukemea kwa nguvu zangu zote hadi jasho likawa
linanitililika mithili ya maji. Yule mchungaji wa
uongo alikuwa ananisogelea kwa karibu akiwa hana
wasiwasi wowote juu yangu, Alinisogelea kwa
karibu huku akiwa ametanua mdomo wake ili
aning'ate maeneo ya shingoni lakini kitendo cha
kunigusa tu kilimsababishia matatizo makubwa
ambayo sizani kama atayasahau, Yule mchungaji wa
uongo alivyojaribu kunigusa alipigwa na kitu kama
shoti ya umeme hadi akarushwa kwa nyuma na
kujigonga kwenye ukuta wa kile chumba, Niliona ile
ndio njia nzuri ya kumuangamiza kabisa kwani
niliendelea kuomba kwa nguvu, Nilipiga maombi ya
haja hadi yule mchungaji wa uongo akaanza kulia
huku akibadilika kwenye maumbo mbali mbali,
Nakumbuka alibadilika na kufanana na wanyama
mbali mbali kama vile mbuzi, mbwa na paka,
Mwishoni akabadilika kuwa katika umbo ambalo
nahisi ndio lilikuwa umbo lake halisi kwani
alibadilika na kuwa kiumbe cheusi sana kilichokuwa
kina mapembe kichwani huku kimebabuka mwili
mzima, Kucha zake za mikononi na miguuni
zilikuwa ni ndefu, meno yake mdomoni yalikuwa ni
mengi mithili ya mamba. Maombi ni silaha tosha
kwa wote wamuabudio Mola aliyetuumba kwani
kwa nguvu zangu za kawaida nisingeweza
kumshinda yule kiumbe wa ajabu aliyekuwa
amejivisha umbile la binadamu lakini kwa uwezo wa
maombi niliweza kuvishinda vile vita vya kiroho.
Kile kiumbe kililia sana pale chini kikiugulia
maumivu kisha kikaanza kupotea kwa kupuputika
mithili ya umande unavyopotea mida ya asubuhi.
Baada ya dakika chache nilibakia mimi na Eda tu
mdani ya kile chumba chetu, Mchungaji wa uongo
alipotea kwenye mazingira ya kutatanisha, Niliamua
kumpepea Eda ambaye alizinduka kutoka kwenye ile
hali ya kuzimia akawa anashangaa asijue nini
kilikuwa kimetokea, Nilimwambia kuwa
tumevishinda vita vya kiroho hivyo asiwe na
wasiwasi wowote. Siku zilivyozidi kusonga mbele
yule mchungaji wa uongo hakuonekana tena kila
mtu akawa anaongea lake, Niliamua kuwaeleza
waumini juu ya ushetani wa yule mchungaji jambo
ambalo lilipingwa vikali na waumini wa lile kanisa
ambao walikuwa wanamuamini yule mchungaji
kama mtu sahihi wakuwaponya. Nilijikuta najiingiza
kwenye matatizo makubwa kwa kumsema vibaya
yule mchungaji ambaye alikuwa anaaminika kwa
waumini wake ambao alikuwa amewapumbaza
macho.
 
ILIPOISHIA....
Nilijikuta najiingiza kwenye matatizo makubwa kwa
kumsema vibaya yule mchungaji ambaye alikuwa
anaaminika kwa waumini wake ambao alikuwa
amewapumbaza macho.
SASA ENDELEA....Nilijaribu kuwaeleza kwa kina
wale waumini ya kwamba yule hakuwa mchungaji
wa kweli bali alikuwa ni shetani lakini mimi ndiye
niliyeonekana mbaya, Kitu kilichoniuma zaidi ni
kwamba baadhi ya waumini walianza kunikosoa na
kuniita mimi mpagani kutokana na muonekano
wangu ambao kwa kiasi kikubwa ulikuwa ni
muonekano wa kiislamu, Kama kuna siku roho
iliniuma zaidi basi siku iyo niliyoitwa mpagani ndio
niliumia zaidi, Nilishindwa kuelewa wale ni watu wa
aina gani wasiokubali kuelezwa ukweli. Baadhi ya
viongozi wa dini waliokuwa chini ya yule mchungaji
wa uongo aliyetoweka waliamua kuchukua ile nafasi
ya kuliendeleza kanisa lakini kwa kiasi kikubwa
nilikuwa ninatengwa kwani mambo mengi ya kanisa
yalikuwa yananipita bila kushirikishwa, Ile hali
sikuipenda hata kidogo, Kwanini nitengwe na kanisa
wakati nilikuwa ni mmoja wa waumini wa lile
kanisa, Niliamua kumuomba Eda ushahuri kuhusu
lile jambo kwani Eda pekee ndiye aliyekuwa ananipa
ushirikiano. Eda alinipa ushauri ambao sikuwa tayari
kuupokea hata kidogo, Eda aliniambia kama
nikiweza ni vyema nikaondoka kwenye jumuiya ya
lile kanisa kisha nichague kutafuta jumuiya nyingine
au nirudi kwenye dini yangu ambayo nilizaliwa nayo.
Kwa kifupi maisha yangu yalikuwa yamejawa na
utata mkubwa sana, Utata huo ulianza kwenye
maisha ya kawaida hadi kwenye dini, Nilikuwa
nimeshachanganya dini mbili kwa wakati mmoja
lakini dini ya ukristo ilikuwa imenikaa vyema kuliko
hata dini ambayo ndiyo ilikuwa asili yangu. Kitu
kilichokuwa kinanipa nguvu mimi ni kwamba Mungu
wetu ni mmoja, Uwe muislamu au mkristo lakini
wote tumamuabudu Mungu mmoja hivyo utofauti wa
dini haukuwa na nafasi kwangu hata kidogo. Baada
ya kuona kanisa zima lina ninyanyapaa niliwaza sana
ila mwisho niliukumbuka ushauri wa Eda nikaona
ndio muda muafaka wa kuutumia, Nilipanga
kuondoka ndani ya ile Jumuiya ili nikatafute jumuiya
ambayo itanipa ushirikiano wa kutosha. Usiku
nilikusanya nguo zangu vizuri nikazikunja kwenye
begi ili kesho yake niondoke mahala pale lakini
nikiwa ninapanga nguo zangu mkojo ulinibana sana
nikaamua kwenda kukojoa, Nilikojoa salama
nikamaliza lakini pindi nilipokuwa ninarudi ndani
niliona kwa mbali kama kuna mtu ananiita, Yule mtu
alikuwa kwenye muonekano wa mavazi meupe, Yule
mtu hakuonekana usoni vizuri kwasababu ya giza
ambalo lilikuwa limetanda, Nilitaka kusita kumfata
lakini kwakuwa nilikuwa ninajiamini niliamua
kumfata ili nimfahamu, Kumbe kipindi namfata yule
mtu alikuwa anarudi kwa nyuma, Mimi bado
nilikuwa namfata huku akili yangu ikiwa ni kama
imepooza kwasababu nilikuwa ninamfata yule mtu
bila kujua madhala ambayo yanaweza kunikuta.
Niliamua kuongea kwa nguvu nikiashiria yule mtu
aliyevalia mavazi meupe asimame, Yule mtu kweli
alisimama huku amenigeuzia mgongo, Alikuwa
amegeukia kwa mbele. Sikushtuka hata kidogo
nilikuwa ninapiga hatua kumsogelea ili nifahamu
alikuwa ni mtu wa aina gani. Huwezi amini yule mtu
aliponigeukia nilijikuta ninaanguka chini huku
nikijawa na hofu moyoni mwangu, Ile hofu
ilinipunguzia ujasiri wangu ambao huwa ninautumia
kwenye magumu, Yule mtu alikuwa anabadilika
badilika sura yake, Ile sura yake ilibadilika na
kuonesha sura zote za wanaume ambao niliwahi
kuwaua na kuwakata vichwa vyao kipindi cha
nyuma. Nikiwa nimeanguka chini yule mtu alinijia
kwa kasi kubwa akawa ananikaba shingoni huku
akitoka damu mdomoni kwake, Nilikabwa sana hadi
sauti ikawa haitoki, Niliyakodoa macho yangu
ambayo muda huo yalikuwa mekundu mithili ya mtu
aliyekuwa amevuta bangi. Kwakweli hadi leo
napumua ni mengi sana nimepitia Halima mie hadi
dunia siitamani.
 
ILIPOISHIA....
Nikiwa nimeanguka chini yule mtu alinijia kwa kasi
kubwa akawa ananikaba shingoni huku akitokwa
damu mdomoni kwake, Nilikabwa sana hadi sauti
ikawa haitoki, Niliyakodoa macho yangu ambayo
muda huo yalikuwa ni mekundu mithili ya mtu
aliyekuwa amevuta bangi. Kwakweli hadi leo
napumua ni mengi sana nimepitia Halima mie hadi
dunia siitamani.
SASA ENDELEA....Nikiwa bado nimekabwa maeneo
ya shingoni na yule mtu nisiyemfahamu, Niliokota
kipande cha jiwe nikampiga nacho kichwani, Yule
mtu aliniachia kisha akaanza kucheka sana, Mimi
muda huo nilikuwa nimeshikilia shingo yangu huku
nikikohoa kwa nguvu, Yule mtu aliendelea kucheka
kisha akapotea maeneo yale, Nilishindwa kuelewa
alikuwa ni nani na kwanini alikuwa amenijia mimi
pekee, Kwakuwa nilikuwa nina amini katika Imani
niliamua kupiga magoti pale pale chini nikaomba na
kukemea juu ya lile tukio la kutisha lililokuwa
limenipata. Nilivyomaliza kukemea nilirudi moja
kwa moja hadi mdani ya kile chumba ambacho
nilikuwa ninaishi na Eda, Nilijaribu kumuuliza Eda
kama alikuwa amesikia chochote kutoka nje lakini
Eda alisema hakuwa amesikia chochote,
Nilishangaa sana yani Eda hakusikia chochote
pamoja na kelele zote ambazo nilikuwa nimezitoa
kule nje pindi nilipokuwa nimekabwa na yule mtu
wa ajabu. Ilibidi nilale hadi ilipofika alfajili nikaamka
mapema bila hata kumuaga Eda kisha nikaanza
safari ya kuondoka kutoka kwenye ile jumuiya ya
kanisa ambayo ilikuwa inanitenga. Nakumbuka
nilianza safari mida ya Saa kumi alfajiri,Nilipanga
kwenda mbali sana ili nijiepushe na wale waumini
ambao hawakutaka kunipa ushirikiano hata kidogo,
Kitu kilichokuwa kinanipa wasiwasi ni kwamba
nilikuwa sijui sehemu gani niende kwa kuwa sikuwa
na mtu mwingine ambaye nilikuwa nina mfahamu.
Nilitembea hadi nilipofika sehemu moja ambayo
kulikuwa kuna kibanda chakavu nikaamua
kupumzika ili kujikinga na jua ambalo lilikuwa ni
kali sana, Nilitoa kitabu changu kitakatifu nikawa
najaribu kupitia baadhi ya mistari iliyokuwa inanipa
nguvu ya kufanya mema ya kupendeza, Baada ya
kukisoma sana kile kitabu kitakatifu niliona haina
haja ya kuyakimbia matatizo, Niliona ni vyema
nirudi kwenye lile kanisa ili nijaribu kueneza neno
ambalo lina ukweli ndani yake, Kitu kilichonipa
ujasiri ni mistari ambayo ilikuwa ndani ya kile kitabu
kitakatifu. Nilihisi kabisa lazima kutakuwa kuna watu
wabaya wanaliendesha lile kanisa na kuwapotosha
waumini wengi, Niliamua kukamata begi langu
nikaanza safari ya kurejea nilipotoka, Kwakuwa
ilikuwa ni mida ya saa mbili asubuhi niliamua
kupitiliza moja kwa moja hadi kwenye jengo la
kanisa ambalo ndio huwa linatumiwa kwa ajiri ya
maombi, Nilijipenyeza nyuma nyuma hadi nikawa
nimefanikiwa kuingia ndani ya lile kanisa hususani
viti vya nyuma, Uzuri ni kwamba ile sehemu ambayo
nilikuwa nimekaa ilikuwa ina waumini wapya hivyo
hawakuweza kunigundua kuwa mimi ndiye ambaye
kanisa lilikuwa limenitenga. Kwa mbele kabisa kuna
msaidizi wa mchungaji aliyepotea alikuwa
anaendelea kuendesha sala, Yule msaidizi alikuwa
amezungukwa na wenzake wapatao watano,
Waumini wengi walionekana kuyafurahia yale
maombi kasoro mimi pekee ambaye kuna kitu
nilihisi hakipo sawa, Ulipofika muda wa kuwaombea
watu, Niliweza kushuhudia mambo ya kushangaza
kwa macho yangu, Yule msaidizi wa mchungaji na
wenzake walikuwa wanawarushia watu vitu
vilivyofanana na unga wa kijivu, Ule unga ulikuwa
ukiwamwagikia watu wanaanguka chini na
kupandisha mashetani, Ni mimi pekee ambaye
nilikuaa ninalishuhudia lile tukio kwasababu waumini
wengine wao walikuwa kwenye hali ya kawaida bila
kushtuka. Sikupendezwa na ile hali hata kidogo.
Niliinuka kutoka eneo ambalo nilikuwa nimekaa
nikaanza kusogea mbele huku mkononi nimeshikilia
Biblia yangu. Watu wengi walikuwa wananishangaa
kwani hawakupendezwa na ujio wangu, Hata Eda
pia alishtuka baada ya kuniona kwasababu alikuwa
ameamini kuwa nilikuwa nimeshaondoka mahala
pale. Nilipania kuwapinga wale viongozi wa dini
ambao walikuwa wanatumia nguvu za giza.
 
ILIPOISHIA....
Niliinuka kutoka eneo ambalo nilikuwa nimekaa
nikaanza kusogea mbele huku mkononi nimeshikilia
Biblia yangu. Watu wengi walikuwa wananishangaa
kwani hawakupendezwa na ujio wangu, Hata Eda
alishtuka baada ya kuniona kwasababu alikuwa
ameamini kuwa nilikuwa nimeshaondoka mahala
pale. Nilipania kuwapinga wale viongozi wa dini
ambao walikuwa wanatumia nguvu za giza.
SASA ENDELEA....Nilifanikiwa kufika mbele kabisa
bila kuwajali watu ambao walikuwa wananishangaa,
Minong'ono ya watu ilikuwa ni mingi mule kanisani
kila mmoja akionesha kuchukizwa na kile kitendo
changu cha kuwasogelea viongozi wa kanisa,
Sikuonesha kutetereka hata kidogo bali nilikuwa
nimejivika ujasiri wa hali ya juu. Wale viongozi wa
dini walivyoniona walishtuka wakawa wananiangalia
kwa jicho la hasira, Mimi pia nilikuwa nawaangalia
kwa macho makavu huku nikipiga neno kimoyo
moyo, Nilikamata vizuri kitabu changu kitakatifu
nikaanza kukemea huku nikiwageukia wale viongozi
wa dini, Muda huo kanisa zima lilikuwa kimya
likiangalia lile tukio ambalo lilikuwa linaendelea.
Mwenyezi Mungu hakika ni muweza wa yote kwani
nilijikuta najawa na nguvu za kiroho ambazo
zilinisaidia kwa kiasi kikubwa kupingana na wale
viongozi wa dini ambao walikuwa wanatumia nguvu
za kishirikina kuwaponyesha watu. Sikuchoka hata
kidogo, muda wote nilikuwa nakemea hadi nikawa
kama nimeweuka, Wale viongozi wa dini baada ya
kuona nakaribia kuwashinda walitaka kukimbia
kwani walikuwa wanaugulia maumivu kama vile ya
kuchomwa moto, Baada ya kuwakemea sana
mwisho wa siku wale viongozi wapatao sita
walibadilika kutoka katika umbile la binadamu na
kuwa umbile la viumbe ambavyo vilikuwa vinatisha
sana. Vile viumbe vya kutisha vilikuwa vyote
vimelala chini huku vikitokwa na mapovu meupe
mdomoni, Kulitokea tafrani kubwa sana ndani ya
kanisa kwani baadhi ya waumini uvumilivu
uliwashinda wakaanza kukimbia kutoka nje ya lile
jengo la kanisa, Kila mtu hakuamini macho yake
kwani vile viumbe vilikuwa vinatisha sana kuanzia
sura hadi miili yao, Siku iyo nilikemea sana hadi
vile viumbe vikapotea bila kujulikana sehemu
ambapo vilikimbilia. Nilivyomaliza kukemea
nilijikuta naanguka chini kwa kukosa nguvu lakini
nilijitahidi nikajinyanyua kisha nikawasihi watu
wasikimbie, Watu wenye mioyo mepesi walikimbia
lakini wale walio na mioyo migumu walibakia
wakawa wananisikiliza, Ilibidi niwaeleze kwa kina
kuwa wale hawakuwa wachungaji bali vilikuwa ni
viumbe vya kishetani ambavyo vilikuja duniani
kuwateketeza watu, Niliwasihi waumini wafunge na
kusali kila siku kwani kwenye dunia hii kuna mengi
sana yanatokea ambayo ni ya kutisha. Nilifurahi
sana baada ya kuona waumini wananisapoti kwani
kila mmoja kuanzia siku ile alianza kuniamini. Eda
pia alifurahi kwa kiasi kikubwa baada ya kuona
nimetenda mambo makubwa ambayo yalikuwa
yanapendeza kwa macho ya kila mwenye uhai.
Baada ya siku kadhaa kupita nilipendekezwa kuwa
kiongozi wa kanisa lakini sikuwa tayari. Sikukataa
kwa ubaya bali niliona siyo jambo zuri kwa
mwanamke kuwa kiongozi wa kanisa wakati
wanaume walikuwepo hivyo ilibidi mwanaume
mmoja ambaye alikuwa amekolea kwenye dini
achaguliwe kuwa kiongozi wa lile kanisa, Mimi
nilibaki kuwa muumini wa kawaida kama walivyo
waumini wengine, Moyoni nilifurahi sana kuona
nimefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwateketeza
waumini wa uongo lakini akilini mwangu kuna
jambo moja ambalo lilikuwa linanikosesha usingizi.
Kila siku nilikuwa nawaza jinsi ya kuutokomeza Mji
wa Laana kwasababu ndio mji ambao ulikuwa
unazalisha mashetani wengi kuja kuiharibu dunia.
Kilichofanya niwaze kuuteketeza Mji wa laana ni
matendo ambayo tulikuwa tunayafanya kipindi cha
nyuma tulipokuwa kwenye mji huo, Vitendo vya
mapenzi ya jinsia moja, vitendo vya kula nyama za
watu, vitendo vya kuharibu ujauzito wa watu na
vitendo vya kuwalisha binadamu nyama za watu,
Hakika hivyo vitendo viliniumiza nafsi yangu,
Niliamua kujitoa kwa ajili ya kumtumikia Mola
wangu hivyo nilikuwa tayari kuuteketeza ule mji japo
sikujua ni kwanamna gani nitafika kwenye ule mji.
 
ILIPOISHIA....
Kilichonifanya niwaze kuuteketeza Mji wa laana ni
matendo ambayo tulikuwa tunayafanya kipindi cha
nyuma tulipokuwa kwenye mji huo, Vitendo vya
mapenzi ya jinsia moja,Vitendo vya kula nyama za
watu, vitendo vya kuharibu ujauzito wa watu na
vitendo vya kuwalisha binadamu nyama za watu,
Hakika hivyo vitendo viliniumiza nafsi yangu,
Niliamua kujitoa kwa ajili ya kumtumikia Mola
wangu hivyo nilikuwa tayari kuuteketeza ule mji japo
sikujua ni kwanamna gani nitafika kwenye ule mji.
SASA ENDELEA....Siku zilizidi kusonga mbele ,
Moyoni nikiwa bado nina ahadi ambayo nilitamani
kuikamilisha haraka ipasavyo. Muda mwingi
nilikuwa najaribu kuvuta kumbu kumbu ili niweza
kutambua vizuri jinsi ya kurudi kwenye ule mji wa
laana lakini hali bado ilikuwa inashindikana,
Mawazo yalinijaa sana hadi Eda akawa anajaribu
kuniuliza tatizo ambalo linaniumiza kichwa,
Nilimueleza Eda ya kwamba ninataka
Nikauangamize mji wa laana kwasababu ndio
lilikuwa chimbuko la mashetani yaliyokuwa yanakuja
kuiteketeza dunia. Eda aliwaza kwa kina kisha
akaniambia ya kwamba kuna habari ashawahi
kuzisikia huko nyuma kwamba kuna kitabu kilikuwa
cha ajabu sana, Kile kitabu kilisadikika ya kwamba
kilikuwa kina uhalisia na mambo ambayo
yameandikwa ndani yake, jina la kitabu icho Eda
aliniambia kilikuwa kinaitwa (KARIBU MJI WA
LAANA), Baada ya Eda kuongea vile nilikumbuka
mbali sana kwani jana la kitabu lilikuwa siyo geni
masikioni mwangu, Nakumbuka kitabu hicho ndiyo
kilinifanya nifike mji wa laana bila kujitambua.
Nakumbuka nilimuhoji Eda kuhusu jinsi ya kukipata
hicho kitabu lakini Eda alisema naye pia haelewi,
Tulikuwa kwenye mtihani mzito sana wa kupata kile
kitabu ambacho kingeniwezesha kurudi tena mji wa
laana ili nikapambane na jamii ya kishetani ambayo
niliamini ilikuwa inapatikana ndani ya ule mji.
Shughuri ilikuwa ni jinsi ya kukipata kile kitabu,
Niliamua kuachana na zile habari kwa muda lakini
sikukata tamaa moja kwa moja, Niliingia mtaani na
kuanza kuhubiri mahubiri ya kuwajenga watu,
Nashukuru kwa kiasi kikubwa nilifanikiwa
kwasababu safari hii watu wengi walitokea
kunikubali, Hata wale waliokuwa wabishi waliniunga
mkono wakawa wananisapoti kwa kitendo ambacho
nilikuwa ninafanya , Nilitembea mitaa karibia yote ya
mkoa wa Tanga huku nikilitangaza neno, Jua
lilikuwa linanichoma lakini sikujali hata kidogo mimi
muda wote nilikuwa nimeshikilia Biblia yangu
mkononi huku nikilieneza neno takatifu. Kuna siku
nilikuwa katika mtaa ambao kwa jina siwezi
kuukumbuka vizuri kwasababu ni miezi mingi sana
imepita, Nilikuwa kwenye ule mtaa kwa lengo la
kutangaza utukufu wa Bwana, Nakumbuka siku iyo
nilihubiri kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa nane
mchana bila kuchoka, Mahubiri yangu mengi
yalikuwa yanafanyika sehemu ambazo hazikuwa
rasmi, Ninavyosema sehemu ambazo siyo rasmi
simaanishi sehemu za ovyo bali namaanisha ni
sehemu ambazo hazikuwekwa mahususi kwa ajili ya
mahubiri mfano masokoni na barabarani. Ilivyotimia
saa nane niliamua kutafuta sehemu ambayo
nilipanga kula chakula, Nilifanikiwa kupata sehemu
ambayo ilikuwa na mazingira mazuri ya usafi kisha
nikaagiza chakula changu lakini kabla ya kula alikuja
mwanaume ambaye simfahamu akakaa kwenye kiti
cha mbele tukawa tunaangalia, Yule mwanaume
hakuagiza kitu chochote bali alikuwa akiniangalia
kwa makini usoni hadi nikaanza kumtilia mashaka,
Nilitaka nihame ile meza lakini roho ya kijasiri
ikaniambia nikimuamini Muumba hakuna kitakacho
nitetelesha. Baada ya ukimya wa muda mrefu yule
mwanaume aliamua kuongea, Aliongea sauti
ambayo ilikuwa inajirudia rudia, Nilijaribu
kuwaangalia watu wengine kama walikuwa
wanaisikia ile sauti ya yule mwanaume lakini
walikuwa wanaendelea na mambo yao, Sikuteteleka
nikawa namsikiliza yule mwanaume kitu
anachoniambia, Yule mwanaume alianza kuongea
maneno ambayo yalinishangaza kwa kiasi kikubwa
hadi nikabaki najishangaa mimi mwenyewe,
Sikuamini kabisa ya kwamba dunia hii tunayoishi
ndiyo iko vile kwasababu maneno aliyoyaongea
yalikuwa ni kama ufafanuzi wa mji wa laana.
 
MJI WA LAANA-30(MWISHO)
MTUNZI-SHADU
TELL-0677884981
ILIPOISHIA....
Yule mwanaume alianza kuongea maneno ambayo
yalinishangaza kwa kiasi kikubwa hadi nikabaki
najishangaa mimi mwenyewe, Sikuamini kabisa ya
kwamba dunia hii tunayoishi ndiyo iko vile
kwasababu maneno aliyo yaongea yalikuwa ni kama
ufafanuzi wa mji wa laana.
SASA ENDELEA....Ni maneno mengi sana yule
mwanaume aliyaongea lakini siwezi kuyakumbuka
yote, Namnukuu kwa baadhi ya maneno yake
ambayo hayawezi kufutika kichwani mwangu hadi
siku naingia kaburini....."Najua unaitwa Halima, Ni
mengi sana umeyapitia, Ulikuwa mchafu tena
usiyetamanika lakini kwa Damu ya aliye hai
ukapewa nafasi ya kutubu makosa yako, Nafurahi
kuona umejirekebisha na kuwa mtu mwema ambaye
unasaidia kuwaeleza watu wengine kila siku kuhusu
ukuu wa Mola, Najua una hamu ya kujua mimi ni
mtu gani lakini napenda kukuambia ya kwamba
mimi siyo mtu wa kawaida kama uwazavyo bali
mimi ni mmoja wa wateule walioandaliwa makazi
mema mbinguni kwa Baba, Mimi ni malaika
ambaye ndiye niliyepewa jukumu la kukulinda na
kukuhesabia matendo yako tangu ulipo zaliwa hadi
siku ambayo utaingia kaburini. Nilikuwa nakulilia
sana kipindi ulipokuwa unatenda maovu lakini
ulikuwa hauna uwezo wa kuniona, Leo nimejitokeza
mbele yako nikiwa katiki umbo hili la binadamu ili
usiwe na wasiwasi kwasababu hakuna mwanadamu
yoyote ambaye ataona maumbile yetu sisi wateule
wa Bwana hadi siku ya kiama, Pia najua una hamu
kubwa ya kuuteketeza mji wa laana, Ni kazi kubwa
sana unajipa Halima, Kazi ambayo yakuhitaji
kujengeka zaidi kiroho ili uweze kutimiza azima
yako ambayo umeipanga. Ningependa nikufafanulie
halima kitu ambacho haukifahamu kuhusu mji wa
laana, Huu ni mji ambao zamani ulikuwa ni mji
mwema ambao ulibarikiwa kwa kila kitu lakini kwa
tamaa za wanadamu wakaamua kuuharibu huu mji,
Najua unafikiri labda huu mji ni sehemu ambayo ipo
mahala fulani pasipojulikana lakini ukweli ni
kwamba Mji wa laana ni dunia hii hii unayoishi, Yale
yaliyokuwa yanakutokea yalikuwa ni kiini macho ili
usiweze kuujua ukweli kuhusu hii dunia ndio maana
ulikuwa unaamini ya kwamba mji wa laana ni
sehemu ambayo ipo mahala fulani, Ninachokuomba
Halima usirudie tena maovu ambayo ulishawahi
kuyafanya uko nyuma, kama umeamua kuokoka
naomba uishikilie dini ili mwisho wako uwe mwema
kwasababu yakubidi utambua hadi sasa bado
unaishi kwenye mji wa laana(Dunia) hivyo chaguzi
ni yako kama utakubali kufata mambo ya kilaana
yaliyopo duniani au utaamua kuendelea kumtumikia
Muumba wako. Dunia ya leo imekuwa Mji wa laana
kwasababu ya matendo ya kilaana yanayotendeka,
Naumia sana kwa jinsi dunia hii inapoelekea yani
inafika hatua wanaume wanaoana wao kwa wao,
wanawake pia hivyo hivyo, watu wanauana ovyo,
makanisa na misikiti inaendeshwa kwa nguvu za
giza, Shikilia neno Halima usirudie makosa
tena".....Ni maneno ya yule mwanaume aliyekuwa
anaongea kwa sauti ya kujirudia rudia huku machozi
ya damu yakimtiririka, Yule mwanaume alivyomaliza
kuongea aliinuka kisha mwanga mkali ulimuangaza
akatoweka bila kuonekanana machoni mwa watu
wengine huku akiwa ameniachia maneno mazito.
Niliona ni miujiza kwani kwa asilimia kubwa yule
mwanaume alikuwa ni mmoja wa malaika
aliyenitokea kwenye umbile la kibinadamu, Ilibidi
niachane na zile habari za kuuwazia mji wa laana
kwani ukweli nilikuwa nimeshaambiwa ya kwamba
mji wa laana ni dunia hii ambayo tunaishi. Miaka
ilizidi kusonga mbele nikawa sitokewi tena na
mambo ya kutisha, Niliishi maisha ya furaha na ya
kumpendeza Mungu. Nilifanikiwa kumpata
mwanaume wa ndoto yangu ambaye alikuwa
anaitwa Samson. Namshukuru Mungu kwani hadi
leo bado nipo na Samson ambaye tunapendana
sana na pia tumefanikiwa kupata mtoto mmoja wa
kike aitwaye Helisa. Maisha ya familia yangu yapo
katika misingi ya kidini hivyo ningekuomba na wewe
pia ujaribu kuishi maisha ya Kumpendeza mwenyezi
Mungu kwani mambo ambayo nimeyapitia bila
uwezo wake basi ningekuwa nimeshafariki muda
mrefu, Siyo kwamba mimi ninafaa bali ni mapenzi
yake Mungu baba, Kuna muda nikikumbba mambo
ya nyuma machozi yananitililika lakini najikaza na
kumshukuru Mungu kwa kuniokoa na ule ushetani
ambao nilikuwa nao. Hata nikifa leo naomba
Historia ya maisha yangu iwe fundisho kwa kizazi
kijacho.
****MWISHO****
 
MJI WA LAANA-30(MWISHO)
MTUNZI-SHADU
TELL-0677884981
ILIPOISHIA....
Yule mwanaume alianza kuongea maneno ambayo
yalinishangaza kwa kiasi kikubwa hadi nikabaki
najishangaa mimi mwenyewe, Sikuamini kabisa ya
kwamba dunia hii tunayoishi ndiyo iko vile
kwasababu maneno aliyo yaongea yalikuwa ni kama
ufafanuzi wa mji wa laana.
SASA ENDELEA....Ni maneno mengi sana yule
mwanaume aliyaongea lakini siwezi kuyakumbuka
yote, Namnukuu kwa baadhi ya maneno yake
ambayo hayawezi kufutika kichwani mwangu hadi
siku naingia kaburini....."Najua unaitwa Halima, Ni
mengi sana umeyapitia, Ulikuwa mchafu tena
usiyetamanika lakini kwa Damu ya aliye hai
ukapewa nafasi ya kutubu makosa yako, Nafurahi
kuona umejirekebisha na kuwa mtu mwema ambaye
unasaidia kuwaeleza watu wengine kila siku kuhusu
ukuu wa Mola, Najua una hamu ya kujua mimi ni
mtu gani lakini napenda kukuambia ya kwamba
mimi siyo mtu wa kawaida kama uwazavyo bali
mimi ni mmoja wa wateule walioandaliwa makazi
mema mbinguni kwa Baba, Mimi ni malaika
ambaye ndiye niliyepewa jukumu la kukulinda na
kukuhesabia matendo yako tangu ulipo zaliwa hadi
siku ambayo utaingia kaburini. Nilikuwa nakulilia
sana kipindi ulipokuwa unatenda maovu lakini
ulikuwa hauna uwezo wa kuniona, Leo nimejitokeza
mbele yako nikiwa katiki umbo hili la binadamu ili
usiwe na wasiwasi kwasababu hakuna mwanadamu
yoyote ambaye ataona maumbile yetu sisi wateule
wa Bwana hadi siku ya kiama, Pia najua una hamu
kubwa ya kuuteketeza mji wa laana, Ni kazi kubwa
sana unajipa Halima, Kazi ambayo yakuhitaji
kujengeka zaidi kiroho ili uweze kutimiza azima
yako ambayo umeipanga. Ningependa nikufafanulie
halima kitu ambacho haukifahamu kuhusu mji wa
laana, Huu ni mji ambao zamani ulikuwa ni mji
mwema ambao ulibarikiwa kwa kila kitu lakini kwa
tamaa za wanadamu wakaamua kuuharibu huu mji,
Najua unafikiri labda huu mji ni sehemu ambayo ipo
mahala fulani pasipojulikana lakini ukweli ni
kwamba Mji wa laana ni dunia hii hii unayoishi, Yale
yaliyokuwa yanakutokea yalikuwa ni kiini macho ili
usiweze kuujua ukweli kuhusu hii dunia ndio maana
ulikuwa unaamini ya kwamba mji wa laana ni
sehemu ambayo ipo mahala fulani, Ninachokuomba
Halima usirudie tena maovu ambayo ulishawahi
kuyafanya uko nyuma, kama umeamua kuokoka
naomba uishikilie dini ili mwisho wako uwe mwema
kwasababu yakubidi utambua hadi sasa bado
unaishi kwenye mji wa laana(Dunia) hivyo chaguzi
ni yako kama utakubali kufata mambo ya kilaana
yaliyopo duniani au utaamua kuendelea kumtumikia
Muumba wako. Dunia ya leo imekuwa Mji wa laana
kwasababu ya matendo ya kilaana yanayotendeka,
Naumia sana kwa jinsi dunia hii inapoelekea yani
inafika hatua wanaume wanaoana wao kwa wao,
wanawake pia hivyo hivyo, watu wanauana ovyo,
makanisa na misikiti inaendeshwa kwa nguvu za
giza, Shikilia neno Halima usirudie makosa
tena".....Ni maneno ya yule mwanaume aliyekuwa
anaongea kwa sauti ya kujirudia rudia huku machozi
ya damu yakimtiririka, Yule mwanaume alivyomaliza
kuongea aliinuka kisha mwanga mkali ulimuangaza
akatoweka bila kuonekanana machoni mwa watu
wengine huku akiwa ameniachia maneno mazito.
Niliona ni miujiza kwani kwa asilimia kubwa yule
mwanaume alikuwa ni mmoja wa malaika
aliyenitokea kwenye umbile la kibinadamu, Ilibidi
niachane na zile habari za kuuwazia mji wa laana
kwani ukweli nilikuwa nimeshaambiwa ya kwamba
mji wa laana ni dunia hii ambayo tunaishi. Miaka
ilizidi kusonga mbele nikawa sitokewi tena na
mambo ya kutisha, Niliishi maisha ya furaha na ya
kumpendeza Mungu. Nilifanikiwa kumpata
mwanaume wa ndoto yangu ambaye alikuwa
anaitwa Samson. Namshukuru Mungu kwani hadi
leo bado nipo na Samson ambaye tunapendana
sana na pia tumefanikiwa kupata mtoto mmoja wa
kike aitwaye Helisa. Maisha ya familia yangu yapo
katika misingi ya kidini hivyo ningekuomba na wewe
pia ujaribu kuishi maisha ya Kumpendeza mwenyezi
Mungu kwani mambo ambayo nimeyapitia bila
uwezo wake basi ningekuwa nimeshafariki muda
mrefu, Siyo kwamba mimi ninafaa bali ni mapenzi
yake Mungu baba, Kuna muda nikikumbba mambo
ya nyuma machozi yananitililika lakini najikaza na
kumshukuru Mungu kwa kuniokoa na ule ushetani
ambao nilikuwa nao. Hata nikifa leo naomba
Historia ya maisha yangu iwe fundisho kwa kizazi
kijacho.
****MWISHO****

Safi sana... Bonge la story...

Chapter Closed...



Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom