Simulizi: Mji

Simulizi: Mji

bioto

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2017
Posts
1,261
Reaction score
2,099
SIMULIZI-MJI WA LAANA-1
MTUNZI-SHADU
TELL-0677884981
UTANGULIZI.....
Kila mwanadamu ana mitihani ya kidunia ambayo
inaweza kumkatisha tamaa ili asifikie malengo yake
ambayo alikuwa amejipangia, kuna baadhi ya watu
huwa wanafikia hatua ya kutaka kujiua kabisa
wakizania ndiyo njia sahihi ya kukabiliana na
matatizo yao ambayo yanakuwa yamewasumbua
kwa muda mrefu bila kupata ufumbuzi. Matatizo
yanaweza kumfanya mwanadamu afikie hatua ya
kujuta kwa nini alizaliwa, wengine huwa
wanamkufuru Mwenyezi Mungu kwa sababu tu ya
matatizo waliyonayo. Matatizo hayo hayo ndiyo
yaliyopelekea leo hii niwe katika haya maisha
ambayo sikuwahi kuwaza kama nitaweza kuja
kuyaishi, Kwa majina naitwa Halima Ramadhani
kinoko, Ni mtoto wa mwisho kwenye familia ya
watoto watano, Sikuweza kufaidi malezi ya wazazi
wangu kwani niliambiwa na ndugu zangu wakaribu
ya kwamba wazazi wangu walishafariki kipindi cha
nyuma, kipindi ambacho nilifikisha miezi kumi.
Malezi yangu mengi nililelewa na bibi katika kijiji
cha Busamuda wilaya ya Maswa mkoani simiyu,
Nilipokuwa mdogo sikuweza kutambua umuhimu
wa wazazi kwakuwa sikuwa na akili ya kujitambua
vizuri, Bibi yangu alijitahidi kunihiza nisome sana ili
nije kumsaidia kwasababu wale kaka zangu wannne
walionitangulia hawakuonekana kumjali bibi, hata
mimi pia hawakuwa wananijali kwasababu ilipita
miaka takribani mitatu bila kuonekana pale kijijini,
Lile jambo lilimuumiza sana bibi yangu hivyo akawa
ananisisitiza kila siku nisome kwa bidii ili baadae
nije kuwa msaada mkubwa kwake. Nilivyofika
darasa la nne ndio nilianza kuona umuhimu wa
kuwa na wazazi kwani siku za maafari ya kishule
wanafunzi wenzangu wengi walikuwa wamekuja na
wazazi wao lakini kwangu hali ilikuwa tofauti,
sikuwa na mzazi hata mmoja, hakuwepo baba wala
mama ila mtu pekee ambaye nilikuwa namtegemea
kwa kipindi kile alikuwa ni bibi yangu aliyekuwa
anajulikana kwa jina la bibi kidawa, sikujuwa kwa
nini walikuwa wanamuita jina la bibi kidawa lakini
niliona watu wengi tu wamezoea kumuita hilo jina,
Nilipata uchungu kila nilipokuwa nawaona rafiki
zangu wakifurahi pamoja na wazazi wao, Bibi
alikuwa anajaribu kunifariji kila siku ili nisiweze
kuwawaza wazazi wangu lakini ilikuwa ni ngumu
sana, haikuwa kitu rahisi kuacha kuwawaza wazazi
wangu ambao sikubahatika japo kuwaona sura zao.
Niliendelea na elimu yangu ya msingi hadi
nilipomaliza darasa la saba. Mtihani wa taifa ambao
tulikuwa tumeufanya ulikuwa ni mgumu sana hivyo
sikuona miujuza yoyote ya kufaulu, Kitu ambacho
nilikuwa nakiwaza ni kupata mwanaume wakunioa
kwani wasichana wengi ambao walikuwa
wanamaliza darasa la saba katika kile kijiji cha
Busamuda walikuwa lazima waolewe, Ni wasichana
wachache sana ambao walikuwa wanapata nafasi ya
kuendelea na kidato cha kwanza. Baada ya matokeo
kutoka sikuwa miongoni mwa wanafunzi
waliochaguliwa kuendelea na elimu ya juu hivyo
nilibaki nyumbani nikiwa nasubilia mwanaume
wakuja kunioa. Sikuwa msichana mkubwa sana
lakini kwa miaka ile kumi na nne ambayo nilikuwa
nayo ilitosha kabisa kuwavutia wanaume wengi
ambao walikuwa wananitongoza kila kukicha,
Nilipata wakati mgumu sana kuchagua mwanaume
wakuweza kumkubalia kwasababu karibia wote
walionifata walionekana kuwa na maneno matamu
tena yakuvutia, wengine walikuwa wanadiliki kabisa
kumwaga machozi wakiahidi watanioa na
kuniendeleza kielimu. Baada ya kufanya uchunguzi
wa kutosha jina la Edger niliona ndio linafaa, kwani
Edger alionekana kuwa mwanaume wakujali sana,
Nilijaribu kumjibu ovyo kwa kumpima ili nijue kama
alikuwa na malengo na mimi lakini Edger
hakuoneshwa kukera na maneno yangu, Aliendelea
kila siku kunishawishi nikubali ombi lake la kuwa
wapenzi. Baada ya kumchunguza Edger kwa muda
mrefu mwishoni niliamua kumkubalia Edger lakini
kabla ya kufanya mambo mengine nilimuomba kitu
cha kwanza aje kwa bibi yangu(bibi kidawa)
kujitambulisha, Edger hakuwa na hiyana alikuja hadi
nyumbani kwa bibi akajitambulisha na kueleza kila
kitu ambacho alikuwa amekipanga juu yangu, Kwa
upande wangu nilifurahi sana kwani Edger aliongea
kwa nidhamu ya hali ya juu huku akijiamini. Baada
ya Edger kuongea vile nilimuona bibi akikasirika
huku akikunja sura, Kwa macho yangu mimi Halima
niliweza kumuona bibi yangu akimtemea makohozi
Edger huku akimwambia aondoke haraka kabla
hajachukua uamuzi mwingine, Nilistajabishwa na lile
jambo nikaamua kumuuliza bibi kwa nini amefanya
vile lakini bibi aliniangalia kwa macho ya hasira na
kusema hataki kumuona mwanaume mwingine akija
kuongea ujinga pale nyumbani kwake. Roho iliniuma
sana lakini sikuwa na lakufanya, Edger aliondoka
nyumbani huku akiwa amesikitishwa sana na kile
kitendo cha kutemewa makohozi na bibi yangu. Kila
siku nilikuwa namsumbua sana bibi kuhusu swala la
mimi kuolewa kwasababu nilikuwa bado ni
msichana mbichi na wanaume wengi wenye nia
ukiachana na Edger walikuwa wanazidi kujitokeza
lakini bibi alikataa kata kata. Bibi hakutaka niolewe
wala hakuwa na lengo lakunitafutia kitu cha kufanya
hivyo muda mwingi nilikuwa nipo nyumbani nikiwa
nimekaa tu bila kufanya kitu chochote. Kuna siku
niliamua kuvunja ukimya na kumuuliza bibi kwa nini
alikuwa hataki niolewe, Kwa kuwa ilikuwa ni saa
mbili usiku bibi aliamua kuwasha kibatari kisha
akaketi kwenye kigoda na kuanza kuongea, bibi
aliongea maneno ambayo hayakuniingia kabisa
akilini mwangu..."Siyo kwamba sitaki uolewe halima
bali nina lengo kubwa sana na wewe, ukiolewa
utakuwa umeharibu kila kitu, siku zangu za kuishi
duniani zinahesabika hivyo ni wewe pekee ndiye
ninayeona unafaa kubeba hii mikoba halima"...alion
gea bibi ambaye alikuwa anatafuna ugoro wake,
Nilihisi bibi huenda akawa amechanganyikiwa kwani
yale maneno ambayo aliniambia yalikuwa
yameniweka njia panda, Nilivyojaribu kumuuliza bibi
vizuri kuhusu lile jambo aliloliongea, Bibi aliamua
kuniweka wazi kuwa mimi ndiye niliyekuwa
nimechaguliwa kuridhi mikoba yake ya uchawi,
kumbe bibi yangu alikuwa ni mchawi tena mchawi
mwenye nyazifa kubwa sana katika serikali ya
kichawi. Sikuwa tayari kukubaliana na bibi kwani
niliuogopa sana uchawi lakini kitendo cha kukataa
ile mikoba ya bibi kiliweza kunisababishia matatizo
makubwa ambayo yalinitesa sana.
 
ILIPOISHIA....
Bibi aliamua kuniweka wazi kuwa mimi ndiye
niliyekuwa nimechaguliwa kurithi mikoba yake ya
uchawi, kumbe bibi yangu alikuwa ni mchawi tena
mchawi mwenye nyazifa kubwa katika serikali ya
kichawi. Sikuwa tayari kukubaliana na bibi kwani
niliogopa sana uchawi lakini kitendo cha kukataa ile
mikoba ya bibi kiliweza kunisababishia matatizo
makubwa ambayo yalinitesa sana.
SASA ENDELEA....Nilipogundua kuwa bibi yangu ni
mchawi nilianza kupanga mikakati ya kutoroka pale
kijijini busamuda na kukimbilia mbali kabisa,
sikutaka kumshirikisha mtu yoyote juu ya lile jambo
la mimi kutoroka kwasababu nilihisi nikimshirikisha
mtu anaweza kuniharibia mipango yangu, Nilipanga
hadi siku ya kutoroka bila hata bibi yangu kujua,
Sikufikilia kabisa sehemu gani ambayo ningefikia
endapo nitatoroka pale kijijini lakini nilichowaza
mimi ni kutoroka na kumuacha bibi peke yake kwa
kuwa nilikuwa nimeshamgundua ya kwamba ni
mchawi, mbaya zaidi alikuwa anataka anirishishe
mikoba ya uchawi jambo ambalo sikuwa nimeliafiki
hata kidogo. Kila siku bibi hakusita kunihamasisha
nikubaliane na swala la kurithi mikoba yake ya
uchawi, ilifikia muda akawa ananipa vitisho vikali ya
kwamba nisipokubali kurithi mikoba basi mizimu
itaniadhibu vikali, Niliogopa sana lakini niliona ni
vyema nijitenge mbali na bibi kwani nilihisi huenda
ndiyo itakuwa suluhu la kukwepa ile mikoba ya
uchawi. Kuna siku niliamua kujiweka sawa ili
nimtoroke bibi, nakumbuka ilikuwa ni siku ya
jumatatu saa tano usiku bibi akiwa amelala fofofo
niliamua kuinuka kwa kunyata kutoka kwenye
chumba changu kisha nikachukua furushi la nguo
zangu ambazo nilikuwa nimeziandaa mchana kwa
ajili ya kumtoroka bibi, Nilifanikiwa kutoka nje ya
kile chumba ambacho nilikuwa ninalala lakini giza
la nje lilinitisha, Giza lilikuwa ni kali mno na pia
sauti za fisi pamoja na mbwa mwitu zilisikika kwa
mbali zikipiga kelele, Nilitaka kurudi ndani ili
nikalale lakini nilipofikiria masuala ya kurithi mikoba
ya uchawi niliingiwa na hofu mpya nikaamua kuanza
kupiga hatua kwa kunyata taratibu ili nisiweze
kusikika, Ule usiku wa kutisha sitausahau kwani
ulikuwa ni usiku ambao uliniogopesha sana kitu
kibaya zaidi nilikuwa mwanamke hivyo roho ya
ujasiri ilikuwa mbali na mimi, Nilikuwa natembea
huku naangaza kushoto na kulia ili kutambua kama
kuna hatari inataka kunikaribia, Mikononi sikuwa na
silaha yoyote ya kunilinda zaidi ya furushi langu la
nguo, Nilivyofika umbali mrefu nilihisi kama kuna
vishindo vizito vikikimbia kuja upande wangu,
Mapigo yangu ya moyo yalinienda kasi mno, nilihisi
huenda ni kiumbe kikali kinataka kunidhuru usiku
ule hivyo niliamua kupanda juu ya mti mrefu kiasi ili
kuinusuru roho yangu, vile vishindo vilisogea hadi
chini ya ule mti ambao nilikuwa nimeupanda,
sikuweza kuona kitu kilichokuwa kinatoa vile
vishindo kwasababu giza lilikuwa nikali sana, kitu
nilichoweza kukisikia pale chini ni muungurumo
mkali wa kiumbe ambacho sikuweza kukifahamu,
Baada ya dakika kadhaa vile vishindo pamoja na ule
muungurumo ulipotea lile eneo likabaki kimya.
Nilipokuwa juu ya ule mti nilianza kujilaumu sana
kwa nini nimetoroka nyumbani kwa bibi kwasababu
nilikuwa naogopa sana, Niliogopa kupita maelezo,
sikujua ni jambo gani lakufanya pale juu ya mti,
sikuwa na mtu wakumuomba msaada zaidi ya
kumuomba Mola wangu. Nilivyoona hali imekuwa
shwari niliamua kushuka juu ya ule mti huku
natetemeka nikiwa tayari kuendelea na safari yangu,
Nilitaka asubuhi inikute nikiwa mbali na kile kijiji
cha busamuda hivyo nilijitahidi kadri ya uwezo
wangu wa kutembea ili nifike mbali, Siku iyo ndiyo
niliyoamini usiku ulikuwa unaficha mambo mengi
ambayo ukiwa umelala hauwezi kuyatambua.
Nilivyofika umbali mrefu kiasi niliweza kulishuhudia
jambo ambalo lilifanya nishikwe na bumbuwazi,
Japokuwa giza lilikuwa totoro lakini niliweza kuona
kikundi cha watu wengi sana wakiwa kwenye
msururu uliojumuisha wake kwa waume, Wale watu
walikuwa wamejifunga mashuka meupe huku
wakiimba nyimbo zao ambazo kwa upande wangu
sikuweza kuzielewa hata kidogo, Ule msururu wa
wale watu ulikuwa ni mrefu sana lakini watu wanne
waliokuwa wanaongoza ule msafara walikuwa
wamebeba jeneza juu kana kwamba wanaelekea
kuzika, Ile hali iliniogopesha sana yani watu
wanaenda kuzika giza nene kama lile, kwa nini
wasisubili hadi asubuhi itimie ndio wazike, Ni moja
ya maswali ambayo nilijiuliza nikiwa bado
nimesimama nikiwaangalia wale watu, Niliishiwa
hata nguvu za kujificha hivyo muda wote nilikuwa
nimesimama nikiwa natokwa jasho jingi mithili ya
maji, Wale watu hawakuonesha kunijali sana kwani
walikuwa wapo bize huku wakiendelea kuimba lakini
mtu mmoja miongoni mwa ule msafara aligeuka
nyuma na kuniona, Alivyoniangalia tu alimshika
mwezie mkono kichwani kwa haraka kisha msafara
wote ukapotea, Sikuweza kuona tena ni wapi
wameelekea, Hapo ndipo nilipochanganyikiwa zaidi
ikabidi nikimbie kama kichaa huku nikiwa sielewi
wapi niendapo, Katika kimbia kimbia yangu
nilijikuta navamia kichaka kimoja cha miba ambayo
ilinichoma sana, Nilipata uchungu mkali hadi nikawa
nalia mwenyewe, Miba mingi ilinichoma maeneo ya
mapajani na kwenye tumbo, Nilijichomoa vipisi vya
miba ambavyo vilikuwa vimeninasa nikaanza
kujikokota huku nikihisi maumivu ya kuchomwa na
ile miba, Hakika ule usiku niliteseka sana, mambo
ya kutisha ambayo niliyashuhudia yaliweza kabisa
kunifanya niwe muoga, Kuna muda nilikuwa nasikia
sauti za watu wakiongea lakini nilikuwa siwaoni,
Nilivyozidi kuchanja mbuga nilihisi kuna mtu
ananivuta blauzi yangu kwa nyuma hivyo niliamua
kugeuka haraka kwa uoga ili nimuone mtu ambaye
ananivuta lakini sikuona kitu chochote, Nikiwa
mwingi wa taharuki nilihisi nimebanwa na mikono ya
mtu ambaye alikuwa haonekani, Nilijaribu kujinasua
lakini ilikuwa haiwezekani, Yule mtu alinibana sana
hadi pumzi zikaanza kuniishia, Niliishiwa pumzi
kabisa nikawa nimelegea nisijue nini lakufanya,
Nilivyojaribu kutoa sauti haikutoka, Nikabaki
nimekodoa macho huku nikihisi maumivu makali
mwilini mwangu, Yale maumivu niliyoyapata
yalipelekea nipoteze fahamu zangu. Baada ya pale
sikujua kilichoendelea lakini Asubuhi nilijikuta nipo
sehemu tofauti, Sikuweza kujilaumu kutokea ile
sehemu kwasababu kwa ule usiku uliopita ilikuwa ni
ngumu kuelewa sehemu ambayo nilikuwa ninaenda,
Kitu kilichonishangaza ni kwamba tangu nizaliwe
sikuwahi kukutana na sehemu ambayo ilikuwa
inafanana na ile ambayo nilikuwa nimetokea.
 
ILIPOISHIA....Baada ya kupoteza fahamu zangu
sikujua kilichoendelea lakini asubuhi nilijikuta nipo
sehemu tofauti, sikuweza kujilaumu kutokea ile
sehemu kwasababu kwa ule usiku uliopita ilikuwa ni
ngumu kuelewa sehemu ambayo nilikuwa ninaenda,
Kitu kilichonishangaza ni kwamba tangu nizaliwe
sikuwahi kukutana na sehemu ambayo ilikuwa
inafanana na ile ambayo nilikuwa nimetokea.
SASA ENDELEA.....Ile sehemu ilionekana kuwa na
utulivu mwingi sana, hakuonekana mtu yoyote
kukatiza lile eneo, sikuwa na budi nilianza kuongoza
mbele huku nikifata njia ambayo sikujua ilikuwa
inaelekea wapi, Nakumbuka kwa kukadilia
nilitembea kwa muda wa masaa takribani matatu
bila kukutana na mtu yoyote, Ile njia niliyokuwa
nakatiza ilikuwa imezungukwa na vichaka vya
wastani hivyo nilikuwa ninatembea huku nikijaribu
kuchukua tahadhali, Kichwani nilikuwa nimebebelea
furushi langu la nguo ambazo niliona zinaanza kuwa
mzigo kwangu. Jua lilivyokuwa limezidi ilibidi
nijisogeze kwenye kivuli ili nijikinge na lile jua kali,
njaa pia ilikuwa ni kali lakini kilichonisaidia ni
miogo ya kuchemsha ambayo nilikuwa
nimeibebelea kwenye lile furushi langu la nguo,
Nilikula ile miogo kiasi nikashushia na maji ambayo
nilikuwa nimeyachukua pia kwenye chupa ya
wastani. Nilitembea sana bila kukutana na mtu
njiani hadi nikaanza kuhisi huenda nipo kwenye
ulimwengu ambao hakukuwa na mtu mwingine
anayeishi zaidi yangu, Kwa uoga ilibidi niite kwa
sauti ya kuomba msaada kama kuna mtu atanisikia
lakini hakuna aliyeijibu ile sauti yangu zaidi ya sauti
za ndege ambao walishtuliwa na ile sauti yangu.
Nilivyoona lile furushi langu la nguo limekuwa
mzigo mzito niliamua kuchambua baadhi ya nguo
kisha zingine nikazitupa ili kupunguza ule mzigo,
Ilibidi nichukue nguo chache tu, nakumbuka nilibeba
sketi zangu mbili na tisheti za juu zipatazo nne,
Baada ya kutembea umbali mrefu nilijikuta natokeza
mwisho wa ile njia niliyokuwa napita, Nilishangaa
kwa mbele kuna njia zipatazo nne zimeungana na
ile njia yangu, Nilikuwa kwenye wakati mgumu
kwani sikuelewa ni upande upi wa njia ambao
ninatakiwa niufate kwani njia zilikuwa
zimegawanyika sehemu nne, Baada ya kuumiza
sana kichwa niliamua kwenda upande wa kulia
ambao nilihisi ndio njia sahihi ya kunipeleka hadi
njia kuu ambayo itafanya nikimbie mbali kabisa na
kile kijiji cha busamuda, Kijiji ambacho nilitokea
kukichukia kwa sababu ya bibi yangu ambaye
alitaka anirishishe mikoba ya uchawi. Nilitembea
mwendo mfupi kwa mbali nikawa namuona kama
mtu amesimama huku akiwa hatingishiki, sikuweza
kumtambua kwa urahisi kwasababu alikuwa umbali
mrefu sana kutoka eneo ambalo mimi nilikuwepo,
Nilitaka kusita kusonga mbele ili nirudi nilikotoka
lakini nafsi myingine ikaniambia yaweza kuwa yule
alikuwa mtu mwema hivyo niliamua kuzidi
kimsogelea kwa karibu ili nimuombe msaada wa
kunisaidia kunitoa ndani ya kile kimsitu kidogo
ambacho kilikuwa kinanichanganya, Kitu cha
kushangaza ni kwamba kadri nilivyokuwa nazidi
kumsogelea yule mtu ndio nilikuwa nina uona
utofauti uliokuwa umejificha juu yake, Alikuwa
amejifunika shuka nyeusi mwili mzima huku
amejiinamia chini akiwa anaonesha ishara ya kulia,
Mkononi alikuwa ameshikilia mkongoja ule wa
wazee ambao hawawezi kutembea vizuri, Sura yake
alikuwa ameiinamisha chini kwaiyo kumuona ilikuwa
inanipa tabu, lakini hadi pale moyo wangu ulikuwa
tayari umejawa na hofu kubwa sana, Nilijaribu
kumuongelesha yule mtu huku nikiwa nimesimama
hatua kama kumi kutoka eneo alilokuwa ameinama
lakini yule mtu hakunijibu zaidi ya kuinua sura yake
juu na kuniangalia kwa macho yaliyokuwa yamejawa
na machozi mengi ya damu, Moyo wangu ulidunda
pigo moja kuu baada ya kuushuhudia uso wa bibi
yangu niliyekuwa nimemkimbia, Ndio alikuwa ni bibi
yangu kabisa tena alionekana kujawa na hasira hadi
macho yake yalikuwa yamejawa na machozi ya
damu, Mwili wangu wote ulikufa ganzi nikaishiwa
hata nguvu za kukimbia. Ilikuwa ni kawaida kabisa
ya mwili wangu kuishiwa nguvu pindi ninapokutana
na kitu cha kutisha au kuogopesha kwa ghafla.
Nilimuona bibi yangu akinisogelea kwa karibu huku
mkononi ameshikilia kitu kilichokuwa kinadunda
mithili ya moyo wa binadamu ambao ulikuwa
unafanya kazi ukiwa nje ya mwili, Niliogopa zaidi
baada ya kuona kile kitu kinadunda huku kinavuja
damu zilizokuwa zinaruka kwa nguvu sana kama vile
mtu anaubinya, Bibi alikula kipande kidogo cha ule
moyo akawa anataka kunirisha na mimi, Sikuwa
tayari kuula ule moyo uliofanana na moyo wa
binadamu kwani niliogopa sana lakini kitendo
changu cha kuishiwa nguvu kilionekana kumpatia
bibi urahisi wa kufanya chochote anachokitaka,
muda wote nilikuwa nimesimama bila hata
kutingishika, kitu kilichokuwa kinafanya kazi kwenye
mwili wangu ulikuwa ni mfumo mzima wa fahau
pekee kwani niliweza kuona na kusikia kila kitu
kilichokuwa kinaendelea kwenye lile eneo, Bibi
yangu alianza kunisogezea ule moyo uliokuwa
unadunda ili niule lakini kabla hajaniingizia
mdomoni ilipiga radi moja kubwa sana tena kwa
sauti kali hadi Bibi alishtuka na kusitisha zoezi la
kunirisha ule moyo, Haikupita muda mvua kubwa
iliyo ambatana na radi ilianza kunyesha kwa wingi
sana, Ile mvua ilisababisha nirejewe na nguvu zangu
upya kisha nilimsukuma bibi akawa ameanguka
chini, Ule moyo ambao bibi alikuwa ameushikilia
ulianguka kwenye kidimbwi cha maji kisha yale
maji yakabadilika rangi na kuwa meusi sana,
Niliona bibi akianza kulalamika huku akiwa anajitupa
tupa huku na kule, Niliona ile ndio ilikuwa nafasi
yangu ya pekee yakujikomboa kutoka kwenye hatari
ile hivyo nilichomoka mbio, Sikukumbuka hata
kubeba kile kifurushi changu cha nguo chache,
Nakumbuka nilikimbia sana hadi nikawa nahema juu
juu kama mwizi aliyekoswa koswa na wananchi
wenye hasira kali. Safari hii nilijikuta nakoteza
sehemu yenye barabara kubwa ambayo ilikuwa ya
vumbi, lile vumbi la ile barabara lilibadilika na kuwa
tope la kaki kutokana na mvua kubwa ambayo
ilikuwa inaendelea kunyesha, Nilivyofika barabarani
nikiwa nimechafuka matope kila sehemu ya mwili
wangu nilikuwa nikikimbia kuelekea mbele huku
nikimuomba Mwenyezi Mungu anisaidie kuniokoa
katika hatari ile ambayo ilikuwa imeniandama.,
Mwanga wa jua ulianza kufifia ikiashilia ya kwamba
Giza lilikuwa tayari limeanza kuingia, Hatimaye giza
lilinikuta bado nipo ndani ya kile kimsitu ambacho
nilikuwa sikijui vizuri, Kwa kuwa nilikuwa nimechoka
ilibidi niwe natembea pembezoni mwa ile barabara
iliyojaa matope huku nikiwa naomba lipite gari
lolote ambalo nitaliomba msaada, Ombi langu kama
ni vile lilikuwa limesikilizwa kwa muda sahihi kwani
baada ya muda mfupi niliona basi kubwa likiwa
linapita kwenye ile barabara, Ilibidi nianze kupunga
mikono yangu huku nikipiga kelele za kuomba
msaada, Nilivyoona haitoshi niliamua kukata majani
ya miti na kuanza kunyoosha juu, Ilinibidi nisimame
katikati ya barabara na kuamza kupiga yowe ya
kulisimamisha lile basi, Mwendo wa lile basi
ulikuwa ni mkali sana kwani hata dereva pamoja na
kunimulika taa lakini hakupunguza mwendo niliona
mwendo wa lile basi ukiongezeka maradufu nikajua
dhahiri lile basi litanigonga ila chakushangaza
liliweza kusimama mbele yangu bila kunigonga,
Sikuelewa yule dereva alikuwa na ujuzi gani
wakusimamisha gari kwa breki ya haraka namna ile,
Sikupoteza muda nilikimbia moja kwa moja hadi
kwenye mlango wa kuingia ndani ya lile basi
nikaufungua na kuingia ndani, Kwa wenge lililokuwa
limenipata sikuweza hata kumuongelesha mtu
yoyote ila mimi nilipitiliza nikaenda kukaa siti
ambayo ilikuwa wazi, Abiria nao walionekana kuwa
bize kwani ilionesha dhahiri walikuwa wamechoshwa
na safari, Dereva pia hakuniongelesha chochote
kwani aliwasha lile basi na kuanza safari upya.
Nilivuta pumzi nzito kuashiria kuushusha mzigo
mzito uliokuwa kifuani mwangu, Nilihisi sasa
nakikimbia kijiji cha busamuda, Kijiji ambacho
nilipanga kukisahau katika maisha yangu, Baada ya
ukimya wa muda mrefu ilibidi nimuulize jirani
ambaye nilikuwa nimekaa naye kwenye siti ya
upande mmoja, Yule jirani yangu hakunijibu kitu
zaidi ya kukaa kimya bila kuongea, Ilibidi na mimi
nikae kimya kwasababu sikutaka kuendelea kuongea
na mtu ambaye hakutaka kuongea na mimi. Basi
lilipofika umbali mrefu lilisimama kwa ghafla kama
kawaida yake, Nikamuona dada mmoja mrefu
mweupe akiwa anainuka kutoka sehemu yake
aliyokuwa amekaa kisha akatoka ndani ya lile basi
kwa kupitia ubavuni mwa lile basi, alipitia sehemu
ambapo hapakuwa na mlango hali iliyofanya
nipigwe na butwaa huku macho yakinitoka kwa
mshangao, dereva wa lile basi aliwasha gari safari
ikawa inaelekea kusipojulikana, wasiwasi uliniingia
upya nikaanza kumuogopa hata jirani yangu ambaye
alikuwa hataki kuongea na mimi. Sijui ni nini
kilinituma niangalie chini ya lile basi kwani
nilichokutana nacho kiliweza kunifanya nijute
kulipanda lile basi, Mimi halima niliweza kushuhudia
abiria karibia wote walio ndani ya lile basi wakiwa
na kwato za ng'ombe miguuni mwao huku juu ya
zile kwako kukiwa na manyoya mengi.
 
ILIPOISHIA....
Dada mmoja ndani ya lile basi aliinuka na kupitia
ubavuni mwa lile basi, alipitia sehemu ambapo
hapakuwa na mlango hali iliyofanya nipigwe na
butwaa huku macho yakinitoka kwa mshangao,
dereva wa lile basi aliwasha gari safari ikawa
inaelekea kusipojulikana, wasi wasi uliniingia upya
nikaanza kumuogopa hata jirani yangu ambaye
alikuwa hataki kuongea na mimi. Sijui ni nini
kilinituma niangalie chini ya lile basi kwani
nilichokutana nacho kiliweza kunifanya nijute
kulipanda lile basi, mimi halima niliweza kushuhudia
abiria karibia wote walio ndani ya lile basi wakiwa
na kwato za ng'ombe miguuni mwao huku juu ya
zile kwato kukiwa na manyoya mengi.
SASA ENDELEA....Niliamua kujikausha kimya
kwenye ile siti niliyokuwa nimekaa, Mwendo wa lile
basi uliongezeka kupita kiasi mithili ya kimbunga,
Kuna muda hadi nilihisi lile basi litapinduka hivyo
nilikuwa nikitetemeka kwa uoga lakini wale abiria
wengine hawakuonekana kujali kitu chochote, wao
muda mwingi walikuwa kimya ndani ya lile basi
kana kwamba walikuwa hawashtushwi na ule
mwendo mkali wa basi. Baada ya mwendo mrefu
hatimae nilianza kuona kila abilia akifuka moshi
uliokuwa unafanana na majivu, Abiria mmoja baada
ya mwingine alianza kupotea kimiujiza ndani ya lile
basi hadi nikabaki mimi peke yangu na dereva huku
mwendo wa basi ukiwa bado mkali sana. Kufumba
na kufumbu dereva naye alikuwa ametoweka ndani
ya lile basi hivyo nilikuwa nimebaki peke yangu
nikiwa sijui nini lakufanya, Nilianza kupiga kelele za
kuomba msaada kwani nilikuwa nakiona kifo mbele
yangu, Lile basi lilikimbia kwa kasi likaacha njia na
kwenda kugonga mti mkubwa pembezoni mwa ile
barabara Lakini cha ajabu sikuweza kupapa jeraha
lolote zaidi ya kujikuta nipo juu ya ungo uliokuwa
chini ya ule mti, Kumbe nilikuwa nimepanda basi la
wachawi, Na mambo yale yote yaliyonitokea ndani
ya lile basi ndiyo mambo ambayo wachawi huwa
wanayafanya pindi wanapokuwa wanasafiri kutoka
eneo moja kwenda lingine mida ya usiku. Nilijinasua
kutoka kwenye ule ungo ambao ulikuwa
umezungushiwa hirizi nyingi kisha nikaanza kusonga
mbele, Uzuri ni kwamba kulikuwa kumeanza
kukucha kwaiyo nilikuwa ninaona vizuri sehemu
ambayo nilikuwa ninaelekea, Nilitembea mwendo
mfupi hadi nilipotokea kwenye makazi ya watu,
Kiukweli sikuweza kuitambua kabisa ile sehemu
yenye makazi hivyo nilikuwa ninatembea huku
nikiangaza huku na kule kama nitaona kitu
kinachoweza kunitambulisha ule mtaa ambao
nilikuwa nimetokea lakini bado sikufanikiwa
kuutambua ule mtaa, Sikujua nianzie wapi
kwasababu hakuna mtu ambaye nilikuwa
ninamfahamu, Nilivyokuwa bado nimezubaa alikuja
kijana mmoja pembeni yangu na kuanza
kuniongelesha, Yule kaka aliniuliza maswali mengi
kwani alijuwa dhahiri nilikuwa mgeni kwenye ule
mtaa, Nilitaka kujifanya mwenyeji lakini upande
mwingine niliamua kuwa muwazi kwa yule kaka
kuwa mimi ni mgeni kwenye ule mtaa, Niliamua
kufanya vile ili nipate msaada kutoka kwa yule kaka
kwasababu kwa kipindi kile ndiye mtu ambaye
niliona anaweza kunisaidia kwakuwa akili yangu
ilikuwa ni kama imechanganyikiwa kutokana na
mambo ya kishetani ambayo nilikuwa
nimeyashuhudia. Pamoja na yule kaka kujikuta
mkarimu kwangu kumbe alikuwa ana kitu chake
alichokipanga juu yangu, Kumbe alikuwa
amenitamani kimapenzi hivyo alitumia ugeni wangu
kama njia ya kujipatia kitu ambacho alikihitaji
kutoka kwenye mwili wangu. Sura ya yule kaka
ilionekana kuwa ya kistaarabu sana lakini moyo
wake ulikuwa wa kikatili, Ninayokueleza mpenzi
msomaji ni ya kweli kabisa kwani usiku ulivyofika
nilipata sana shida kutoka kwa yule kwake, Alikuwa
amenipa hifadhi kwenye chumba chake lakini
nilishangaa kumuona akinilazimisha kufanya naye
mapenzi, Nilipojaribu kumgomea alianza kunipiga
vibao pamoja na ngumi usoni, Nilijisikia maumivu
maeneo aliyokuwa ananipiga hadi nikaamua
kumuacha afanye anachokitaka, Niliona ni bola
ninusuru roho yangu kuliko kuendelea kuumizwa
kwa kitu kidogo japo sikuridhia kufanyiwa kile
kitendo, Kipindi yule kaka anafanya mapenzi na
mimi nilikuwa nahisi maumivu makali kama ya
tumbo la hedhi, Nilijaribu kujirudisha kwa nyuma ili
nipunguze maumivu lakini yule kaka alikuwa anazidi
kunibana kwa nguvu pale kitandani kwake, Sikuhisi
raha hata kidogo ila kitu nilichokuwa napata ni
maumivu makali sana, Yule kaka alikuwa anaendelea
kufanya kwa nguvu lakini nilianza kushtuka baada ya
kumuona yule kaka akikoroma kama vile mafua
yamemkamata, Haikupita muda niliona damu
zimenijaa kifuani mwangu, kwa uoga nilihisi kifua
changu kimechanika lakini haikuwa hivyo bali yule
kaka ndiye aliyekuwa anavuja damu mdomoni,
Haikupita muda akaanza kutetemeka kama vile
anakata roho, Niliogopa sana kuona mtu anataka
kufia kifua mwangu, ikabidi nimsukume pembezoni
huku nikipiga kelele kwa wingi, Hauwezi kuamini
nilifungua mlango nikatoka nikiwa uchi wa mnyama
na kuanza kukimbia kama kichaa huku nikipiga
kelele nyingi. Milango ya nyumba nyingi ilikuwa
imefungwa na hakuonekana hata mtu mmoja kutoka
nje licha ya kelele nilizokuwa nimezipiga, Ilisikika
sauti moja tuu ikiongea na hata sikujua imetoka
wapi....(RUDIII NYUMBANIIIIII, KARIBIA
NITAKUFAAA)....Ni sauti iliyokuwa inajirudia rudia
ikinihimiza nirudi nyumbani, Nilishindwa kuelewa
nyumbani wapi ile sauti ilikuwa inanihimiza nirudi,
Nikiwa nipo nje huku nikitetemeka mwili mzima
niliweza kushuhudia watu wafupi sana kwa kimo
wakiingia kwenye kile chumba ambacho nilimuacha
yule kaka aliyekuwa anatokwa na damu mdomoni,
Wale watu wafupi walikuwa wapatao watatu,
Hawakupita kwenye mlango wa kawaida wa nyumba
bali walipitia kwenye pembe ya ukuta ambayo
ilikuwa haina mlango, Baada ya muda walitoka
ndani ya ile nyumba wakiwa wamebebelea maiti ya
yule kaka, Wale watu walisogea na ile maiti hadi
pale nilipokuwa nimesimama wakaanza kunizunguka
huku wakipiga miruzi, Walinizunguka mara saba
kisha wakapotea, Baada ya kulishuhudia lile jambo
nilianguka chini mzima mzima, Nilihisi mwili wangu
kuwa wa baridi sana, Hakika nilikuwa nayashuhudia
mambo makubwa sana ambayo kila kukicha
yalikuwa yanatokea upande wangu.
Asubuhi kulivyo pambazuka nilijipata nipo
hospitalini huku nimetundikiwa drip ya maji, Sikujua
pale Hospitalini nimefikaje, Nilishtuka baada ya
kumuona dokta anakuja upande wangu huku
ameshikilia sindano ambayo ndani yake niliona ina
dawa ya maji ambayo ilifanana kabisa na damu,
Nilipata uoga nikaamua kuchomoa ile drip ya maji
kisha nikakamata ile sindano na kumchoma nayo
yule dokta nikaanza kukimbia kutoka ndani ya ile
hospitali, Kiufupi akili yangu haikuwa sawa hata
kidogo, Nilikuwa nimechanganyikiwa kwa mauza
uza ambayo yalikuwa yamenitokea. Nilikimbia sana
ndani ya ile hospitali ili nitoke nje kwa nyuma
nilishangaa kuona watu wote ndani ya ile hospitali
wakinikimbiza. Walinzi, Madaktari, Pamoja ma
wagonjwa wengine wote waliungana wakaanza
kunikimbiza, lilikuwa ni jambo la ajabu sana ndani
ya ile hospitali, Mbio zangu ziliishia sakafuni baada
ya kukanyaga kopo ambalo lilifanya niteleze na
kuangukia vyombo vya pale hospitalini. Niliona kila
mtu miongoni mwa lile kundi lililokuwa
linanikimbiza akiwa ameshikilia sidano mkononi
akiwa na lengo lakunichoma nayo.
 
ILIPOISHIA....
Walinzi, madaktari pamoja na wagonjwa wengine
waliungana wote wakaanza kunikimbiza, lilikuwa ni
jambo la ajabu sana ndani ya ile hospitali, mbio
zangu ziliishia sakafuni baada ya kukanyaga kopo
ambalo lilifanya niteleze na kuangukia vyombo vya
pale hospitalini. Niliona kila mtu miongoni mwa lile
kundi lililokuwa linanikimbiza akiwa ameshikilia
sindano mkononi akiwa na lengo la kunichoma
nayo.
SASA ENDELEA.....Niliingiwa na uoga uliopitiliza,
Nilitamani niinuke ili niendelee kukimbia lakini mwili
wote ulikuwa umekufa ganzi. Kitu cha kushangaza
kadri wale watu walivyokuwa wananisogelea kwa
karibu walikuwa wanapungua idadi hadi akabakia
mtu mmoja aliyekuwa amevalia vazi jeupe safi
lisilokuwa na doa hata sehemu moja, Kwa lile vazi
alilokuwa amelivaa ilionesha dhahiri alikuwa ni
daktari japo sikuwa nimeiona sura yake kabla. Yule
mtu alikuwa ananiongelesha lakini sikuweza kusikia
hata neno moja kwasababu masikio yangu yalikuwa
ni kama yameziba kwaiyo muda mwingi nilikuwa
nikimuangalia usoni, Haikuchukua muda
nikanyanyuliwa kutoka pale chini na yule mtu kisha
akanipeleka kwenye chumba ambacho kilikuwa
tofauti na kile nilichowekwa mara ya kwanza.
Nilivyokuwa ndani ya kile chumba fahamu zangu
zilianza kunirejea upya hivyo nilikuwa nina uwezo
wakusikia na kuelewa kila kitu ambacho nilikuwa
ninaongeleshwa. Nakumbuka nilihojiwa kwa muda
mrefu na yule daktari akiwa na lengo la kufahamu
matatizo yaliyonikabiri hadi niwe katika ile hali
ambayo haikuwa ya kawaida. Nami bila kuficha
nilieleza kuanzia mwanzo hadi mwisho kuhusu
matatizo yaliyo nikumba, Yule daktari aliyekuwa na
jinsia ya kiume alikuwa kwenye mshangao mzito
baada ya kusikia mambo ambayo nilimueleza.
Ukimya ulitawala kwa dakika takribani moja ndani
ya kile chumba kisha yule daktari akanipa wazo
ambalo kwa upande mwingine niliona linaweza
kuwa msaada mkubwa kwangu, Yule daktari
aliniambia ni vyema nikajaribu na upande wa pili wa
shilingi akimaanisha niende kwa mganga maana
swala langu lilikuwa linahusiana na mambo ya
kishirikia, Nilimkubalia lakini sikuwa hata na pesa
ya kumlipa mganga hivyo bado nilikuwa kwenye
mtihani mzito. Yule daktari sijui alikuwa na roho ya
aina gani kwani alinipatia kiasi cha shillingi elfu
arobaini akaniambia kitanisaidia kumlipa mganga,
Alinielekeza hadi sehemu ambayo anapatikana
mganga aliyebobea kwenye mambo ya kutatua
matatizo ya kishirikina. Baada ya kukabidhiwa ile
pesa sikupoteza muda nilimuaga yule daktari
nikaanza safari ya kuelekea sehemu ambayo
mganga alikuwa anapatikana, Sikutaka hata kupitia
sehemu ya kula chakula japo njaa ilikuwa inaniuma,
mimi kitu nilichokuwa ninakiwaza ni kwenda kwa
mganga ili aweze kuniondolea ile misuko suko
ambayo ilikuwa inaniandama kila kukicha, Ile
sehemu ambayo mganga alikuwa anapatikana
ilikuwa ni mbali sana kutoka kwenye ile hospitali,
Yani ilikuwa ni simiyu vijijini kabisa tena vile vijiji
vya ndani kabisa ambavyo vipo mbali na mji,
Sikukata tamaa niliamua kutembea kwa miguu
kuelekea kwa mganga, Kitu kilichonisaidia ni
kwamba nilikuwa mwanamke niliyekulia vijijini hivyo
kama kutembea umbali mrefu nilishatembea sana
kipindi nilipokuwa ninaenda kuchota maji katika
visima ambavyo vilikuwa vinapatikana mbali na kijiji
chetu kile cha busamuda. Nilitumia masaa sita
nikawa nimefika eneo ambalo nilielekezwa na
daktari, Halikuwa eneo lingine bali eneo la mganga
wa kienyeji, Sikuweza kupotea kwasababu nilikuwa
ninatembea huku nikijaribu kuwauliza wapita njia
wachache ambao nilikuwa ninapishana nao njiani.
Safari yangu iliishia nje ya kijumba kilichokuwa
kimeezekwa kwa nyasi kavu huku kikiwa
kimezungushiwa matambala mekundu na meusi kila
upande, Nje ya kile kijumba lilikuwa limepaki gari
binafsi aina ya Landcruza, lile jambo lilinishtua kiasi
lakini sikutaka kujali sana, Nilisogea hadi kwenye
mlango wa kile chumba nikabisha hodi nikiomba
kuingia ndani lakini ukimya ulikuwa umetawala,
Nikaamua kubisha tena hodi lakini safari hii niliona
kijana ambaye alikuwa amevalia suti akitoka ndani
ya kile chumba huku mkononi ameshikilia kimfuko
cheusi, Yule kijana alipitiliza na kile kimfuko kuingia
kichakani, sikujua ni nini alikuwa ameenda kufanya
kichakani na kile kimfuko, Nikiwa bado nashangaa
ilisikika sauti kutoka ndani ya kile chumba ikiashilia
niingie ndani, Niliamua kufunua pazia jekundu
lililokuwa limewekwa mlangoni kisha nikaingia
ndani, Mule ndani ya kile chumba kulikuwa kuna
harufu mbali mbali za udi na marashi mengine
ambayo yalikuwa ni makali sana, Nilimkuta babu wa
makamo ambaye ndiye alikuwa mganga, Aliniambia
nikae kwenye ngozi ya ng'ombe ambayo ilikuwa
imetandikwa chini huku pembezoni kukiwa na vibuyu
vingi vyeusi, Mganga alianza kunieleza kitu
kilichonipeleka kwake kabla hata sijamuelezea shida
yangu, Sikushangaa sana kwani ni kawaida kabisa
kwa baadhi ya waganga kuwa na uwezo
wakutambua shida ya mtu hata kama bado
hawajaelezewa. Yule mganga aliniambia tatizo langu
ni lakawaida kama nitakuwa makini kufata maelezo
yake, Alinipatia kimfuko cheusi akaniambia niende
nikakifukie kwenye kichaka cha jirani na eneo lile
kisha nikimaliza nitemee mate lile eneo. Nilifanya
kama mganga alivyoniambia nikawa namuuliza
gharama ya ile dawa aliyonifanyia, Yule mganga
alicheka sana kisha akaniambia haitaji chochote
kutoka kwangu kwani amenifanyia bule kama
mwanae, Nilihisi labda alishajua hali yangu ngumu
niliyonayo ndiyo mana hakutaka hata shilingi kumi
kutoka kwangu, Nilipokuwa najiandaa kuondoka
nilimuona yule kaka wa mwanzo niliyepishana naye
kwa mganga akirudi kutoka kule kichakani,
Sikumzingatia sana nilianza kutembea kwa miguu
kuianza safari ya masaa kadhaa ya kurudi
nilipotoka. Yule kaka aliingia kwenye lile gari la
Landcruza akaja kulisimamisha mbele yangu,
Alinipatia lifti ya bule kwakuwa naye alikuwa anapita
njia ambayo nilikuwa ninapita, Njiani nilikuwa kimya
sana huku nikiwaza hatima ya maisha yangu, Hata
yule kaka hakuonekana kuwa muongeaji sana, muda
wote alikuwa siriazi akiendesha gari lake kwa
makini, Kama ujuavyo wanawake tulivyokuwa
wadhaifu kwa wanaume hususani pale nyota zetu
zinapokuwa zinashabiana, Kuna muda tulijikuta
tunakutanisha macho yetu kitu ambacho ni kama
kilisisimua mwili wangu, Nilikwepesha macho
yangu haraka kwa aibu, Ile iliweza kusaidia
kutufanya tuanze kuongea ndani ya lile gari,
Tuliongea mambo mengi sana mimi na yule kaka
ambaye aliniambia anaishi Mwanza lakini shida
aliyokuwa nayo ndiyo ilimfanya atoke Mwanza hadi
Simiyu kuja kuonana na yule mganga, Huo ndio
mwanzo wa kuzoeana na yule kaka ambaye kwa jina
aliniambia anaitwa Steven, Kwakuwa nilikuwa sina
sehemu ya kufikia Steven aliamua kuondoka na
mimi hadi Mwanza ambapo alipanga kunipa kazi ya
ndani, Kazi ambayo kwa upande wangu niliifurahia
japo sikujua kuwa kuna mambo mengi ya
kustajabisha ninaenda kukutana nayo ndani ya jiji la
Mwanza.
 
Kitu kipya Safi mkuu tupo pamoja ubarikiwe
 
ILIPOISHIA....
Tuliongea mambo mengi sana mimi na yule kaka
ambaye aliniambia anaishi Mwanza lakini shida
aliyokuwa nayo ndiyo ilimfanya atoke Mwanza hadi
simiyu kuja kuonana na yule mganga, Huo ndio
mwanzo wa kuzoeana na yule kaka ambaye kwa jina
aliniambia anaitwa Steven, Kwakuwa nilikuwa sina
sehemu ya kufikia Steven aliamua kuondoka na
mimi hadi Mwanza ambapo alipanga kunipa kazi ya
ndani, Kazi ambayo kwa upande wangu niliifurahia
japo sikujua kuwa kuna mambo mengi ya
kustajabisha ninaenda kukutana nayo ndani ya jiji la
Mwanza.
SASA ENDELEA....Tulivyofika jijini Mwanza,
Tuliongozana na Steven hadi sehemu ambayo
alikuwa anaishi. Steven alikuwa ameoa mke mmoja
ila hawakuwa na mtoto kwaiyo mke wa Steven
alivyoniona nimeongozana na mume wake hadi pale
nyumbani kwake alitaka kuleta shida lakini Steven
alisimama kama mwanaume halisi akanitetea kisha
akamueleza mke wake kuwa mimi ndiye mfanyakazi
wa ndani ambaye kila siku alikuwa anamsumbua
amtafutie mtu wa kumsaidia kazi za nyumbani,
Baada ya muda mrefu wa majibizano hatimae mke
wa Steven aliamua kushusha jazba na kuniruhusu
niingie ndani kwake, Kitu kilichomuondoa hofu mke
wa Steven ni muonekano wangu ambao nilikuwa
nao, Nilikuwa katika muonekano wa kishamba sana
hata kwa uzuri nilikuwa nimezidiwa tena mbali na
mke wake Steven. Nilioneshwa sehemu ya kwenda
kuoga nikaoga vizuri kisha nikaoneshwa chumba
ambacho nitakuwa ninalala. Siku iliyofata nilianza
kuoneshwa sehemu za kuwa nafanya usafi,
nikapewa pamoja na masharti ya Pale nyumbani na
mke wake Steven ambaye alikuwa anaitwa Anitha.
Siku za mwanzoni nilipata shida kwasababu nilikuwa
nakosea kila ninachofanya lakini siku zilivyokuwa
zinazidi kusonga ndio nilikuwa nafahamu taratibu
jinsi ya kupangilia kazi ambazo zilikuwa ni jukumu
langu pale nyumbani, Steven alikuwa si mtu wa
kushinda sana nyumbani, Yeye alikuwa anaondoka
alfajiri kisha anarudi usiku sana hivyo kumuona
ilikuwa ni ngumu sana, Nilichokipenda kwenye ile
nyumba ya Steven ni kwamba mke wake(Anitha)
hakuwa na roho mbaya japo kwenye makosa
hakusita kunifokea, Anitha hakuonesha kunitenga
hata kidogo, alinichukulia kama mdogo wake hivyo
tulikuwa tunapata hata muda wa kujadili mambo
yetu ya wanawake. Kila kukicha nilijitahidi kufanya
kazi kwa bidii huku nikiepuka uzembe katika kazi,
Ujio wangu kwenye ile familia ya Steven ulionekana
kufurahiwa zaidi na mke wake kwasababu nilikuwa
namsaidia kazi nyingi sana pale nyumbani. Sikujua
Steven na Anitha walikuwa wana kazi gani japo
muda mwingi anitha alikuwa anashida nyumbani, Ila
kuna baadhi ya siku alikuwa akiniaga huku akisema
anaenda kazini, Sikutaka sana kuingilia maisha ya
mabosi wangu hivyo sikupenda kuwauliza kazi
ambazo walikuwa wanazifanya, Mwezi wa kwanza
ulivyokatika nililipwa laki moja kama mshahara
wangu, Siku iyo baada ya kupokea laki moja
nilifurahi sana. Kwa kuwa sikuwa mwenyeji mdani
ya jiji la mwanza niliamua kumuomba mke wa bosi
wangu(Anitha) anisindikize hadi sehemu wanapouza
nguo ili nikanunue japo baadhi ya nguo za kunikidhi
kwaskuwa sikuwa na nguo nyingi. Tulienda katika
soko la mlango mmoja lililopo kata ya mbugani
wilaya ya nyamagana, Hatukuchukua muda mwingi
sana kwa kuwa hatukuwa tunaishi mbali sana na
wilaya ya nyamagana,Nilinunua nguo kadhaa
ambazo nilihisi zilikuwa zinanifaa ila nguo za ndani
ndio ambazo nilizingatia sana kwani kipindi hicho
nakumbua nilikuwa na pea mbili tu za nguo ya
ndani. Mke wa bosi wangu yeye alinunua gauni
moja ambalo lilikuwa na bei kubwa sana kisha
tukarejea nyumbani. Baada ya siku kadhaa ugomvi
mkubwa uliibuka ndani ya nyumba kati ya Steven na
Anitha, Ugomvi ambao ulisababishwa vitu vya
thamani kuvunjwa, Sikujua chanzo cha ule ugomvi
kilikuwa ni nini lakini nilimsikia Anitha akimshtumu
Steven kuwa hataki kumpatia mtoto, Muda huo
ugomvi unatokea ilikuwa ni usiku kama mida ya saa
sita hivyo niliamua kunyata taratibu hadi kwenye
mlango wa chumba cha Steven na Anitha kisha
nikaanza kusikiliza maongezi yao, Niliweza kumsikia
Anitha akilalamika sana kuhusu swala la mtoto ila
Steven alikuwa akimwambia kuwa wawe na subira
kwasababu mtaalamu wa simiyu aliwaambia siku
siyo nyingi watapata mtoto, Akili yangu ndiyo
iliweza kufunguka na kuelewa jambo ambalo
lilimfanya Steven awepo kule simiyu kwa mganga,
Kumbe Steven alikuwa anahitaji mtoto. Kama tendo
la ndoa Steven na Anitha walishashiriki sana bila
mafanikio ya kupata mtoto ndio mana Steven
aliamua kwenda kwa mganga.
Baada ya wiki chache kupita tangu ule ugomvi
utokee, Anitha alianza kuonesha dalili za kuwa
mjamzito hivyo Steven alifurahi sana, Ile mimba
ilionekana kumsumbua sana Anitha kwakuwa ilikuwa
ndio mimba yake ya kwanza, Steven aliamua
kumpeleka anitha Hospitali ambapo alilipa gharama
zote za anitha kuangaliwa hadi siku atakayo
jifungua, Steven alifanya vile kwasababu Anitha
alikiwa anapata sana tabu pindi alipokuwa nyumbani
hivyo aliona ni vyema awe karibu na madaktari ili
wawe wanamuhudumia matatizo yatakayokuwa
yanajitokeza.
Baada ya Anitha kupelekwa hospitali Nilibaki mimi
na Steven nyumbani, Sikuwa muoga sana kuhusu lile
swala kwakuwa nilikuwa najua dhahiri ya kwamba
Steven ni mtu mpole sana wala hana mambo ya
tamaa za wanawake, lakini kiukweli nilichokizania
kilikuwa kipo tofauti sana. Kwa upande mmoja au
mwingine naweza kusema mtu mwenye makosa
naweza kuwa ni mimi kwasababu siku ya jumamosi
nilimaliza kazi zangu mapema sana pale nyumbani,
Nikaamua kwenda kuoga ili kujiweka sawa,
Kwakuwa nilikuwa nimetumia bafu la nje kuoga basi
niliamua kujifunga kanga yangu nikiwa ninaelekea
ndani kubadilisha nguo zangu, Kumbe kipindi napita
kuingia chumbani kwangu Steven hakuwa mbali na
lile eneo hivyo aliweza kujawa na tamaa juu yangu,
Nikiwa najipaka mafuta nilishtuka baada ya kuona
mtu akiingia chumbani kwangu bila kubisha hodi,
Nilivyogeuka kuangalia nilikutana na Steven ambaye
alikuwa anatabasamu bila aibu, Nilikimbilia shuka
langu nikajifunika kuustiri mwili wangu, Nilijaribu
kumsihi Steven asinifanyie kile kitendo lakini Steven
hakuyasikiliza maneno yangu, Alinikumbatia huku
akinichezea kifuani, Mwanzoni nilikiwa najitahidi
kumkwepa lakini mwishoni nilizidiwa kabisa, Ile
ilitokana na kitendo cha kukaa muda mrefu bila
kufanya mapenzi hivyo steven alikuwa ni kama
amekutana na kitu kibichi kabisa, Ile siku sitaisahau
maishani mwangu mimi Halima kwani Steven
alinichezea sana, Nikiwa kitandani nimelegea kabisa
nilihisi kitu kigumu cha moto kikipita kati kati ya
mapaja yangu hali iliyonifanya nishtuke kwa hofu,
Steven alinibana vilivyo hadi akamaliza haja zake,
Japo kuwa nilikuwa nimeumia lakini siku iyo
nilifurahia sana. Steven aliniambia ile ibakie siri
baina yangu na yeye, Nami nilimuambia sitamueleza
Anitha wala mtu yoyote kuhusu lile jambo.
Miezi tisa ilivyopita anitha alijifungua mtoto wa kike,
Nyumba nzima tulijawa na furaha sana baada ya
kuona Anitha kapata mtoto. Yule mtoto alilelewa
vizuri hadi alipofikia miaka ya kunyweshwa uji,
Jukumu la kumnywesha uji lilikuwa juu yangu
kwasababu nilikuwa ndiye mfanyakazi wa ndani
kwenye ile nyumba, Anitha aliamua kumuita
mwanaye jina la saadani hata Steven alilikubali hilo
jina, Saadan akiwa na umri wa miaka mitatu alianza
kuonesha maajabu ndani ya ile nyumba. Mambo
aliyokuwa anayafanya yalikuwa si mambo
yakawaida hata kidogo.
 
ILIPOISHIA....
Yule mtoto alilelewa vizuri hadi alipofikia miaka ya
kunyweshwa uji, Jukumu la kumnywesha uji lilikuwa
lipo juu yangu kwasababu nilikuwa ndiye mfanyakazi
wa ndani kwenye ile nyumba, Anitha aliamua
kumuita mwanaue jina la Saadani hata Steven
alilikubali hilo jina, Saadani akiwa na umri wa miaka
mitatu alianza kuonesha maajabu ndani ya ile
nyumba. Mambo aliyokuwa anayafanya yalikuwa si
mambo yakawaida hata kidogo.
SASA ENDELEA...Yule mtoto alimaarufu kama
Saadani alianza kuwa wa tofauti sana, Huo utofauti
nilianza kuugundua mimi pekee, Sio Steven wala
Anitha walioweza kuugundua ule utofauti wa mtoto
wao(Saadani). Nakumbuka kuna siku Steven na
Anitha waliondoka nakuniacha mimi pamoja na
Saadani nyumbani, waliniambia nimuhudumie vizuri
kwani wao hawatachelewa kurudi wanaenda kwenye
kikao cha mkutano wa kamati, Nilikubaliana nao
nikawa nimebaki na Saadani huku nikijaribu
kumpatia maziwa ili anywe kwakuwa siku iyo
alikuwa ni msumbufu sana, Saadani hakutulia muda
wote alikuwa analia sana, Nilijuta kuachiwa yule
mtoto, Nilitamani mama yake arudi mapema ili aje
kumbembeleza lakini haikuwa hivyo, Yalipita
takribani masaa matano Saadani akiwa bado analia
kwa nguvu, Nilihisi huenda joto linamsumbua hivyo
niliamua kwenda kumuandalia maji ili nimuogeshe,
Nilimuacha Saadani akiwa kwenye kochi huku akilia
lakini nilivyorudi baada ya kumuandalia maji ya
kuoga nilishtuka sana baada ya kukutana na kitu
cha ajabu, Sikumkuta tena Saadani ile sehemu bali
nilimkuta bibi kizee mmoja wa makamo aliyekuwa
anatoa sauti ya Saadani, Moyo wangu ulilipuka pigo
moja kubwa kisha nikawa kama nimepigwa na
bumbuwazi, Kwa uoga wa hali ya juu nilikimbia
kutoka sebuleni hadi nje ya ile nyumba ambayo
ilikuwa imezungushiwa ukuta wa gharama.
Sikufanikiwa kutoka nje kabisa ya lile geti nikawa
nimekutana tena na yule bibi kizee, Safari hii
alikuwa halii kama mtoto ila alikuwa anatoa sauti ya
ghurumo kali, Kilichonisaidia ni kwamba Kabla yule
bibi kizee hajafanya kitu chochote, Honi ikitokea nje
ililia ikiashilia geti likafunguliwe, Kufumba na
kufumbua yule bibi kizee alipotea mahala pale,
Nikaenda kufungua geti huku natetemeka sana,
Steven na Anitha waliniuliza kitu gani kimenisibu
lakini sikuweza kuongea, Nilikuwa nanyoosha kidole
kenye ile sehemu ambayo bibi kizee alikuwa
amepotea, Anitha hakupoteza muda alikimbilia
ndani kwenda kumuangalia mtoto kama yupo
salama, Na kweli baada ya muda mfupi alitoka nje
akiwa amemkumbatia Saadani, Nilishangaa
kumuona Saadani akiwa anafurahi yani hakuonekana
kama alikuwa analia muda mfupi uliopita. Baada ya
kumuona Saadani wazo la yule bibi kizee lilinipotea
kichwani mwangu, Nilikuwa nakumbuka kilichotokea
muda mfupi uliopita lakini wazo la kuwaambia
wakina Steven na Anitha halikiwepo kabisa. Hata ile
hali ya kutetemeka haikuwepo tena nikabaki
najishangaa pale getini, Ilibidi Steven na Anitha
waachane na mimi wakaingia ndani baada ya kuona
sieleweki. Ile siku ilipita bila tatizo lingine
kujitokeza lakini hofu yangu kwa yule mtoto Saadani
bado ilikuwepo japo mdomo wangu ulikuwa mzito
sana kuwaeleze wazazi wake ya kwamba yule
hakuwa mtoto wa kawaida kama wajuavyo. Anitha
alimpenda sana Saadani kwa kuwa ndio alikuwa
mtoto wake wa pekee, kiukweli Saadani hakuwa
mtoto wa kawaida bali alikuwa ni jini, Tena alikuwa
jini aliyekuwa anapenda sana damu na nyama.
Saadani aliniweka kwenye kifungo kizito sana kwani
mimi pekee ndiye niliyekuwa nimemgundua hivyo ile
siri alitaka nikae nayo siku zote, Hakutaka niropoke
kwa mtu yoyote ndani ya ile nyumba. Wazazi wake
wakiwa nyumbani huwa anakuwa mtoto wa kawaida
lakini wakiondoka anabadilika na kuwa katika umbo
la bibi kizee, Muda mwingi alikuwa anataka
nimletee nyama ambazo zilikuwa mbichi, Sikuwa na
jinsi nilikuwa nafanya hivyo kwakuwa Steven alikuwa
anatoa pesa nyingi sana, Zile pesa Steven alikuwa
anazitoa bila hata yeye mwenyewe kujijua kama
anatoa pesa nyingi kiasi kile, Vitu pekee ambavyo
nilikuwa ninapenda kumnunulia Saadani ni Nyama
mbichi na damu za ng'ombe ambazo nilikuwa
nazifata machinjioni, Kwa siku Saadani alikuwa
anakunya takribani lita tatu za damu, Hali ilikuwa
inatisha sana, Niliogopa kupita maelezo, Nilitamani
kusema lakni vitisho wa Saadani vilinifanya niogope
kutoa ile siri kwa kuhofia kupoteza maisha yangu.
Siku za mwisho wa wiki Familia nzima tulikuwa
tunajumuika pamoja nyumbani tukijadiliana mambo
tofauti tofauti, Anitha hakuacha kabisa kuwa karibu
na Saadani kwani muda mwingi alikuwa akicheza na
mtoto wake huyo, Nilimuangalia Anitha kwa
masikitiko makubwa sana kwasababu nilijua kabisa
yule siyo mtoto bali ni jini. Niliamua kuondoka pale
Sebuleni ambapo niliwaacha Steven, Anitha na
mtoto wao(Saadani) wakiwa wanaangalia vipindi vya
muziki nikaingia ndani ya chumba cha Steven,
Sikujua ni nini kilichonipeleka kule chumbani lakini
nilijikuta tu nimeingia ndani ya kile chumba, Nilienda
moja kwa moja kwenye droo ya Steven nikaanza
kupekuwa, Kipindi napekua ile droo niliweza
kukiona kitabu kidogo kilichokuwa kimeandikwa
KARIBU MJI WA LAANA, Sikuwa mpenzi sana wa
kusoma simulizi lakini jina la kile kitabu lilinivutia,
Niliamua kukichukua kile kitabu ili nifahamu mambo
yaliyozungumziwa ndani yake, Nilikiiba kile kitabu
kwa siri sana nikaenda kukificha chumbani mwangu.
Nilisubili hadi ilivyofika saa sita usiku nikachukua
kile kitabu ili nikisome. Nilivyokuwa nakisoma kile
kitabu nilikuwa nasikia kama sauti zikiniita kwa
nguvu, Zilikuwa ni sauti kama za watu wengi
waliokuwa wananiita kwa kupokezana.
 
ILIPOISHIA....
Kipindi napekuwa ile droo ya Steven niliweza
kukiona kitabu kidogo kilichokuwa kimeandikwa
(KARIBU MJI WA LAANA), Sikuwa mpenzi sana wa
kusoma simulizi lakini jina la kile kitabu lilinivutia,
Niliamua kukichukua kile kitabu ili nifahamu mambo
yaliyozungumziwa ndani yake, Nilikiiba kile kitabu
kwa siri sana nikaenda kukificha chubani kwangu.
Nilisubili hadi ilivyofika saa sita usiku nikachukua
kile kitabu ili nikisome. Nilivyokuwa nakisoma kile
kitabu nilikuwa nasikia kama sauti zikiniita kwa
nguvu, Zilikuwa ni sauti za watu wengi waliokuwa
wananiita kwa kupokezana.
SASA ENDELEA....
Zile sauti zilinishtua sana ikabidi nisitishe zoezi la
kukisoma kile kitabu ambacho niliona kama
kinanichanganya, Kwa uoga wa hali ya juu niliamua
kujifunika shuka langu huku nikiziba masikio ili
nisiweze kuzisikia zile sauti, Pamoja na kufanya vile
lakini bado haikusaidia kwani zile sauti ndio
ziliongezeka tena safari hii zilikuwa zinasikika karibu
kabisa na kitanda ambacho nilikuwa nimelala, Siku
iyo niliogopa sana nikawa nimepanga kukikucha
niondoke kwenye ile nyumba kwasababu nilishaanza
kuona utofauti ndani ya ile nyumba ya Steven. Ghafla
nikiwa bado nimejifunika shuka kitandani nilihisi
kuna mtu ananishika maeneo ya bega, Apo ndipo
nilichanganyikiwa kabisa, Kwa uoga niliokuwa nao
ilibidi nifunue lile shuka kisha nikapiga kelele za
kuomba msaada, Nilivyoangaza huku na kule
sikuona mtu yoyote ndani ya kile chumba, Jasho
jingi lilikuwa likinitililika mithili ya mtu aliyetoka
kuogelea mtoni. Kile kitabu nilichokuwa nimekiiba
kwenye droo ya Steven kilikuwa kimeanguka chini,
Nilivyokiangalia vizuri kilikuwa ni kama kinawaka
moto lakini cha ajabu kilikuwa hakiungui, Ilinibidi
nifungue mlamgo wa chumba changu kisha
nikakimbia kwa nguvu kuelekea kwenye chumba
ambacho Steven na Anitha walikuwa wanalala,
Nilifanya vile ili nikawaombe msaada kutokana na
mauza uza ambayo yalikuwa yamenitokea usiku ule.
Kipindi nakimbia nilishangaa kuona taa za nyumba
nzima zikiwa zinawaka na wakati ulikuwa ni usiku
mnene, Nilivyoangalia vizuri kwenye ubavu wa ukuta
niliona alama ya viganja vya damu kana kwamba
kuna mtu alikuwa anatembea kwenye ukuta kwa
kutumia viganja vya mikono yake, lile jambo
lilifanya niongeze kasi hadi nikafanikiwa kufika
mlangoni mwa chumba cha Steven na Anitha,
Nilibisha hodi kwa nguvu sana huku nikiongea kwa
kulia lakini hakuna mtu aliyefungua mlango, Nilijua
huenda wamezidiwa na usingizi hivyo niliamua
kuchukua chuma kizito nikaanza kuupiga ule mlango
nikiwasihi wafungue lakini bado ukimya ulitawala,
Nikiwa bado nimesimama nje ya chumba cha kina
Steven na Anitha nilisikia sauti za watu zikiwa
zinaimba kutokea kwenye korido, Nyimbo ambazo
walikuwa wanaziimba zilikuwa ni nyimbo za
mazishi. Kiukweli mimi Halima nilichanganyikiwa
sana, Moyo wangu wa kike tena ulio dhahifu ulijawa
na uoga uliopitiliza, Niliamua kuvunja kitasa cha kile
chumba ambacho Steven na Anitha walikuwa
wanalala nikaingia kwa nguvu ndani, Oh Mungu
wangu nilijikuta nadondosha kile chuma nilichokuwa
nimekishikilia na kuanza kutapika kwa mfululizo
baada ya kukuta Steven na Anitha wameuawa kifo
kibaya sana, Kitanda kizima kilikuwa kimelowana
damu zilizokuwa zinachuruzika hadi kwenye sakafu,
Maandishi mengi yaliyo andikwa kwa dama
yalikuwa yametapakaa kwenye kuta ya kile chumba,
Maandishi yale yalikuwa yameandikwa kwa herufi
kubwa yakisomeka (KARIBU MJI WA LAANA).
Sikutaka kuyazingatia sana yale maandishi nikawa
natoka ndani ya kile chumba huku nikiwa
natetemeka. Nilivyotoka nje tu ya kile chumba
nilishangaa kukutana na kundi kubwa la watu
waliokuwa wamevalia mavazi mekundu yenye ishala
ya alama kama ya pembe tatu kwenye vifua vyao,
Sikuelewa kwa usiku ule lile kundi kubwa kiasi kile
tena ndani ya nyumba ya Steven lilikuwa limetokea
wapi, Ilibidi nianze kurudi nyuma huku nikiwasihi
wasiniue, Wale watu hawakujali kilio changu kwani
wao walikuwa wanaendelea kuimba zile nyimbo zao
za mazishi huku wakiwa wananisogelea taratibu
kabisa, Miongoni mwa lile kundi alikiwepo yule bibi
kizee ambaye alikuwa anajigeuza na kujifanya mtoto
mdogo(Saadani), Nyuso nyingi za wale watu
waliokuwa wananisogelea zilionekana kunawili sana,
Wanawake walionekana kuwa wazuri tena waliokuwa
wanavutia, hata wanaume nao walionekana kuwa
katika muonekano wa utanashati. Sikujua kabisa nini
la kufanya kuweza kujiokoa katika ushetani ule
ambao ulikuwa umeniandama, Swala la kusali na
kuomba ili mwenyezi Mungu aniokoe halikuwepo
kabisa akilini mwangu hivyo muda mwingi nilikuwa
ninalia kama mtoto mdogo, Wale watu waliovalia
mavazi mekundu walivyonisogelea kwa karibu
kabisa walisimama wakaacha kuimba, Waliinamisha
vichwa vyao kwa muda wa sekunde kadhaa kisha
mzee mmoja ambaye alikuwa ni kiongozi wao
alinisogelea na kuanza kuniongelesha, Aliniambia
mambo mengi sana ambayo nilikuwa
nimeshayafanya huko nyuma, Mbaya zaidi
akanikumbushia yale mambo ya bibi yangu
aliyoniambia nilisi mikoba yake, Yule kiongozi wao
aliniambia ya kwamba kukana kwangu kupokea
mikoba ya bibi yangu kuliwakasirisha sana hivyo
ndio maana wameamua kunifata kwa nguvu ili
wanipeleke kwenye mji wao ambao walipenda kuiita
mji wa laana kutokana na hanasa nyingi ambazo
walikuwa wanazifanya ndani ya huo mji. Yule mzee
alivyomaliza kuongea alinichapa kofi moja zito
upande wa kushoto wa shavu langu hali iliyofanya
mdomo wangu uwe mzito kufunguka, Baada ya
muda niliona jeneza jeusi likisogezwa mbele yangu,
Sikujua lile jeneza limefikaje pale kwa haraka namna
ile, Yule mzee aliniamrisha niingie ndani ya lile
jeneza akinisihi ndiyo tunaelekea katika mji wa laana
ila niliogopa sana nikawa nakataa kuingia ndani ya
lile jeneza huku nikilia kumuomba anisamehe, Yule
mzee alivyoona nagoma kuingia ndani ya jeneza
kwa hiari yangu alichukua kifimbo kidogo
akanichapa nacho kwenye maeneo yangu ya
makalio huku akiongea maneno ambayo sikuwa
nikiyaelewa, Baada ya muda nilianza kujisogeza
taratibu karibu na lile jeneza ili niingie ndani, Nilipo
liangalia vizuri niliona kuna mwanaume ambaye
alikuwa amelala ndani ya lile jeneza tena mtupu
kabisa bila nguo hata moja, Mbaya zaidi alikuwa
anaonekana tayari ameshafariki kwani alikuwa
ameharibika sana, Sikujua yule mzee akili yangu
alikuwa ameifanyaje kwasababu nilikuwa najiandaa
kuingia ndani ya lile jeneza bila kujali kama kuna
maiti ambayo ilikuwa imeharibika.
 
ILIPOISHIA....
Baada ya muda nilianza kujisogeza taratibu karibu
na lile jeneza ili niingie ndani, Nilipo liangalia vizuri
nilioma kuna mwanaume ambaye alikuwa amelala
ndani ya lile jeneza tena mtupu kabisa bila nguo
hata moja, Mbaya zaidi alikuwa anaonekana tayari
ameshafariki kwani alikuwa ameharibika sana,
Sikujua yule mzee akili yangu alikuwa ameifanyaje
kwasababu nilikuwa najiandaa kuingia ndani ya lile
jeneza bila kujali kama kuna maiti ambayo ilikuwa
imeharibika.
SASA ENDELEA....Nilianza kuingia mdani ya lile
Jeneza huku akili yangu ikiwa ni kama
imehamishwa kutoka maeneo yale, Niliweza
kulaliana na ile maiti ambayo ilikuwa imeharibika
sana kisha lile jeneza lilijifunga kwa nguvu, Hapo
ndipo akili ya kawaida iliponijia upya nikawa nasikia
harufu mbaya sana, Nikiwa ndani ya lile jeneza
nilianza kupiga kelele huku nikiligonga kila mahala
ili lifunguke lakini halikuweza kufunguka, Ile maiti
ilikuwa inanyofoka nyama kila nilipokuwa nabanana
nayo, Vipisi vingi vya nyama ya ile maiti vilikuwa
vinaganda kwenye mwili wangu huku vikitoa harufu
kali. Sikujua kitu kilichokuwa kinaendelea nje ya lile
jeneza ambalo nilikuwa nimewekwa ila nilihisi kama
linanyanyuliwa juu huku kwa mbali nikisikia watu
wakiimba nyimbo za kwenda kuzika, Moyo wangu
ulijawa na hofu kubwa sana, Giza nene ndio
lililokuwa limetawala ndani ya lile jeneza, Nikiwa
bado napiga kelele nilisikia mtikisiko mkubwa sana
hadi nikawa nimejigonga kwenye ubavu wa lile
jeneza, Ule mtikisiko ulisababisha niikandamize kwa
nguvu zaidi ile maiti niliyofungiwa nayo ndani ya lile
jeneza, Ule mkandamizo ulisababisha ile maiti
igawanyike mithili ya nyanya iliyo gandamizwa na
kiganja cha mkono, Nakumbuka Nililia sana hadi
machozi yakaniishia, Baada ya muda nilihisi vitu
kama mchanga vikitupwa juu ya lile jeneza, Hapo
ndipo wasi wasi uliponiingia tena na kuhisi
ninazikwa mzima. Hazikupita dakika nyingi nikawa
sisikii tena sauti ya kitu chochote, Sikusikia sauti ya
mchanga ikimwagika wala sauti ya mtu yoyote
kama ilivyokuwa awali, Jasho jingi lilianza
kunitiririka ndani ya lile jeneza huku nikiwa sioni
chochote kwasababu kulikuwa kuna giza zito, Lile
joto ambalo nilikuwa nalihisi sikuwahi kulihisi kabla
sijawekwa mule ndani ya lile jeneza, Nilijua dhahiri
tayari nimeshafukiwa kwenye kaburi ingali bado
nipo hai, Roho ili iuma sana kuona naelekea kufa
kifo ambacho sikuwahi kukiwaza, Nilikuwa nina
ndoto nyingi sana za kimaisha lakini niliona kabisa
ndoto zangu zinaenda kupotea kama moshi uvumao
angani.Nguvu zilianza kuniisha nikawa
nanyong'onyea mwili wangu, Hakika ninavyo
zungumzia adhabu za kabuli basi inabidi unielewe
kuwa ni mbaya sana, Sijui kwa maiti huwa adhabu
ya kaburi anaihisi vipi ila kwa mimi ambaye
nilikuwa nimezikwa mzima nilihisi ni kali sana tena
zenye mateso yaliyopitiliza, Nilitamani wazazi wangu
ambao sikupata bahati ya kuwaona wawepo mbele
yangu niwaombe msaada wa kunisaidia mimi mtoto
wao Halima ambaye nilikuwa nateswa bila hatia
yoyote, Huwezi amini nilikuwa navuta pumzi kwa
tabu sana huku nikiwaita wazazi wangu waniokoe
lakini hakusikika mtu yoyote aliyenijibu, Nilikuwa ni
mimi na ile maiti ambayo nilikuwa nimeilalia ndani
ya lile jeneza, Sikuona kitu chochote kilichohusiana
na mji wa laana ambao wale watu waliovalia nguo
nyekundu waliniambia wananipeleka, Niliishiwa
nguvu kabisa kwa kukosa hewa safi nikawa nasubili
roho iache mwili wangu, Nikikumbuka yale mambo
machozi yananitililika kwa wingi hadi naishiwa
nguvu ya kuendelea kusimulia, Nilikuwa msichana
wa kawaida ambaye nilitakiwa kuishi maisha ya
furaha lakini uchawi wa bibi ndio ulisababisha
niyapitie yale, Oh Mungu wangu siku ile ndio nilihisi
kwa mara ya kwanza maumivu ambayo mtu hupitia
pindi roho inapokuwa inatengana na mwili, Nikiwa
hoi taabani nilihisi pumzi zinanikata huku pua zangu
zikijilazimisha kupumua kwa tabu, Nilihisi kitu
kikilazimisha kupita kifuani mwangu huku
kikinichoma kwa ncha kali kama sindano,
Nilipambana na ile hali huku nikiwa natupa mikono
na miguu huku na kule, Kiu kilibana sana tena kile
kiu nakumbuka hakikuwa cha kawaida kwani
kilipelekea koromeo langu likauke sana, Yale
maumivu yalikuwa ni makali sana, Giza lilitanda
kwenye uso wangu, Taswira ya matendo yangu yote
mazuri na mabaya ilianza kuoneka mbele ya uso
wangu, Ile taswira iliyotokea ilikua inanionesha nipo
sehemu yenye njia panda mbili, Njia moja ya
kushoto ilikuwa imejaa watu waliokuwa wamevaa
nguo za heshima huku wakiimba na kusifu jina la
Mwenyezi Mungu, Njia ya pili ya kulia ilikuwa
imejaa watu waliokuwa wamevalia nguo zisizo na
maadili, Wanawake walikuwa wamevaa vimini huku
mikononi wameshikilia chupa za bia, Wanaume
walikuwa wamevalia nguo za kubana hali
iliyowafanya wafanane kabisa na wanawake,
Nilisimama kwenye zile njia panda kwa muda kisha
nikaamua kwenda upande wa kushoto nikiwa
nimevalia vazi langu jekundu. Kumbuka hayo
mambo yote yalikuwa yananitokea kwenye taswira
kipindi ambacho roho yangu ilikuwa inataka
kuuacha mwili ndani ya lile jeneza ambalo nilikuwa
nimefukiwa nalo. Baada ya ile taswira kupotea
nilivuta pumzi moja kubwa mapafu yangu yakawa
yanabana kwa maumivu makali ambayo yalikuwa
yanazidi maumivu yote ulimwenguni, Ghafla ile maiti
ambayo nilikuwa nayo mule kwenye jeneza
ilifumbua macho yake yaliyokuwa yanang'aa sana
kisha ikaanza kunipulizi hewa mdomoni mwangu, Ile
ndio ilikuwa pona pona yangu ya kuaga dunia,
kwani baada ya kupuliziwa ile hewa nguvu zilirudi
upya kwenye mwili wangu, Nilishangaa kuona lile
jeneza linavutwa kwa kupanda juu, Kipindi
linapandishwa juu nilianza kuzisikia tena zile sauti
za wale watu waliokuwa wanaimba nyimbo za
mazishi, Safari hii nyimbo zao zilikuwa ni za
kusherekea kwani hakuna aliyesikika akiimba
nyimbo za mazishi tena, Lile jeneza lilijifungua
lenyewe baada ya kuwa limefika juu kabisa kutoka
kule chini lilipokuwa limefukiwa, Nilianza kutoka
ndani ya lile jeneza huku nikiwa nashangiliwa sana
na wale watu, Kitu cha ajabu ile maiti ambayo
nilizikwa nayo haikuwepo tena bali zilionekana pesa
nyingi zikiwa ndani ya lile jeneza. Nilishtuka baada
ya kuona nimetokea sehemu ambayo ilikuwa ni ya
kipekee, Sehemu ambayo kulikuwa kuna kila kitu
ambacho unakihitaji, Yule mzee ambaye alikuwa
mdiye kiongozi aliamua kunipatia vazi jekundu lenye
nembo ya pembe tatu, Ile sehemu ilikuwa ni kama
mji uliovutia hata kuutazama kwa macho. Muda huo
akili yangu ilikuwa imeshabadilika na kuwa kama ya
ile jamii, Lakini mambo mengi ambayo yalikuwa
yanatokea kwenye ule mji niliotokea yalikuwa
yananishangaza kwani yalikuwa ni mambo ya aibu,
tena yalikuwa mambo ambayo hayakutakiwa
kuzungumziwa hata kidogo.
 
ILIPOISHIA....
Muda huo akili yangu ilikuwa imeshabadilika na
kuwa kama ya ile jamii, Lakini mambo mengi
ambayo yalikuwa yanatokea kwenye ule mji
niliotokea yalikuwa yananishanga kwani yalikuwa ni
mambo ya aibu tena yalikuwa mambo ambayo
hayakutakiwa kuzungumzwa hata kidogo.
SASA ENDELEA....Nikiwa nimezubaa huku
nikiendelea kutafakari uzuri wa ule mji niliotekea,
Walikuja wanawake wawili upande wangu wakawa
wananivuta mikono kwa utaratibu kuelekea mbele ya
Hekalu moja ambalo lilionekana limezungushiwa
dhahabu kila mahala, Nami sikubisha nilianza
kupiga hatua nikiwa nimeongozana na wale
wanawake wawili, Hakika ule mji ulikuwa
unapendeza tena sana, Sikuwahi kufikilia hata siku
moja kama kuna siku ninaweza kutokea sehemu
kama ile, Sehemu ambayo karibia nyumba zake
nyingi zilikuwa zimejengwa kwa dhahabu iliyokuwa
inavutia, Kipindi ninatembea kuelekea kwenye lile
Hekalu walionekana watu wengi wakiwa
wananishangilia sana, Na mimi kwakuwa sikuwa na
akili zangu kamili nilianza kuwapungia mkono kama
ishara ya kukubali wanishangilie, Kila mtu aliye
onekana maeneo yale alikuwa amevaa vazi jekundu
lililokuwa na alama ya pembe tatu, Baada ya muda
Nilijikuta tayari nipo ndani ya lile Hekalu ambalo
kwa ndani lilikuwa kimya sana, Nikiwa nimesimama
pamoja na wale wanawake wawili ghafla zilianza
kusikika kelele za matarumbeta zikipulizwa kwa
wingi kutoka kwenye kila kona ya lile Hekalu, Kitu
kilichonishangaza ni kwamba watu waliokuwa
wanapiga yale matarumbeta nilikuwa siwaoni ila
zilikuwa zinasikika sauti tu, Zile sauti za
matarumbeta zilivyoacha kupiga wale wanawake
wawili waliinamisha vichwa vyao chini kama
wanasujudia kitu kisha wakawa wanarudi nyuma
kwa kuhesabu hatua, Mimi muda huo nilikuwa
sielewi ni nini kinaendelea kwani muda wote
nilikuwa nawashangaa wale wanawake wawili,
Haikupita muda mrefu mbele yetu ulitokeza mwanga
mkali uliosababisha nikinge macho yangu, Ule
mwanga ulivyopungua niliweza kuonana na kitu
ambacho tangu nizaliwe ndiyo ilikuwa mara ya
kwanza kuonana nacho, Hakikuwa kitu kingine bali
ni kiumbe ambaye alikuwa anataka kufanana na
Popo kwa muonekano wa haraka haraka, Yule
kiumbe alikuwa ni mkubwa wa umbo huku mwilini
mwake akiwa na manyoya mengi kiasi, Mwili wake
haukutofautiana sana na mwili wa binadamu, Mimi
nikiwa nimeingiwa na uoga kiasi niliwaona wale
wanawake wawili wakikisogelea kile kiumbe bila
hofu yoyote kisha wakainama tena chini yake na
kuanza kumsujudia, Walifanya vile kwa muda mfupi
kisha wakatoka ndani ya lile Hekalu na kuniacha
mimi peke yangu nikiwa nimesimama huku sielewi
nini la kufanya, Yule kiumbe alinisogelea kwa karibu
kabisa akawa ananinusa nusa maeneo ya usoni na
kichwani, Kipindi ananinusa nilikuwa nasikia harufu
kali sana, Ilikuwa ni kama harufu ya mzoga, Yani
alikuwa ananuka hadi pua zangu zikawa zinauma
kutokana na harufu ambayo alikuwa anatoa yule
kiumbe. Kitu kingine kilichokuwa kinanitia hofu ni
kwamba yule kiumbe alionekana kuwa uchi wa
mnyana , Mwili wake ulionekana kuwa kama
mchanganyiko wa biadamu na mnyama tena aina ya
popo. Nikiwa nimesimama nilikuwa ni kama
nimepumbazwa kwa muda kwani Yule kiumbe
alikuwa ananivuta mkono kunipeleka sehemu
ambayo ilikuwa imejitenga ndani ya lile Hekalu,
Nililazwa kwenye eneo ambalo lilikuwa linataka
kufanana kama kitanda, Yule kiumbe alinivua lile
vazi jekundu nikabaki mtupu nikiwa nimelala chali,
Nilimuona anakamata mkononi kitu cha chuma
ambacho kwa mbele kilikuwa chekundu kama vile
kilikuwa kimepitishwa kwenye moto, Nilikuwa kama
nimepararaizi kwani hata nguvu za kujiinua sikuwa
nazo kwaiyo muda wote nilikuwa namuangalia yule
kiumbe kitu anachotaka kunifanyia, Kile chuma cha
moto kilinyanyuliwa kikawa kinaletwa kwenye paji
langu la uso kisha kikagandamizwa, Nilihisi
maumivu makali hadi nilipiga kelele lakini sauti
haikutoka, Yule kiumbe hakuishia apo alipitisha kile
chuma tena kwenye ziwa langu la kushoto tena kwa
nguvu sana, Yale maumivu yalikuwa makali sana
kwani ziwa langu liliungua hadi likaweka alama
nyeusi, Yale maumivu niliyo yapata yalifanya hadi
kichwa changu kiume sana., Niliumia zaidi wakati
kile chuma cha moto kilivyopitishwa chini ya kitovu
kwenye eneo ambalo lilikuwa karibu kabisa na njia
ya kutolea mkojo, Hapo ndipo nilipiga kelele hadi
sauti ikatoka, Nililia sana hadi mwili wangu wote
ukajawa na jasho lililokuwa linanitiririka kwa wingi.
Baada ya kunifanyia vile yule kiumbe alipotea
kwenye mazingira ya kushangaza kisha mlango wa
lile Hekalu ulifunguka wakaingia wale wanawake
wawili wakiwa wamejawa na furaha, Walinikaribia
wakiwa wameshikilia kikombe kilichokuwa na dawa
kisha wakaanza kunipaka kwenye majeraha ambayo
nilikuwa nimeyapata. Wale wanawake walivyomaliza
kunipaka ile dawa sikusikia tena maumivu lakini
nilibakiwa na chapa za maandishi sehemu ambazo
yule kiumbe alinipitishia chuma cha moto. Nilianza
kuingiwa na wasi wasi baada ya kuona wale
wanawake wawili wananifanyia mambo ambayo
yalikuwa ni mambo ya kunidhalilisha, Yalikuwa ni
mambo ambayo kwa mimi mtoto wa kike nilitakiwa
nifanyiwe na mwanaume lakini nilishangaa kuona
wale wanawake wawili ndio walikuwa wananifanyia,
Sitamani kuelezea yale mambo kwani kila
nikiyakumbuka naingiwa na simanzi, Hakika wale
wanawake wawili walinifanyia vitendo vichafu sana,
Muda mwingi wao walikuwa wanafurahia kana
kwamba wapo na mwanaume ila kwa upande
wangu nilikuwa nachukia sana kwani kushiriki
vitendo vya mapenzi na mwanamke mwenzangu
nilikichukulia kama kitendo cha laana. Baada ya
wale wanawake kurizika na lile tendo walilonifanyia
waliamua kunitoa ndani ya lile Hekalu hadi nje
ambapo nilikuta kuna watu wengi wamelizunguka
lile Hekalu huku wakishangilia. Sikuelewa ni nini
walichokuwa wanashangilia ila nilichukuliwa na
mmama mmoja ambaye alinieleza jinsi ya kuishi na
ile jamii, Yule mama aliniambia nisiogope kitu
chochote kwani nitapata kila nitakacho ndani ya ule
mji ambao ulionekana kuwa mji wa utajili. Taratibu
nilianza kuzoea mazingira ya ule mji nikawa naanza
kufata tamaduni zao ambazo zilikuwa ni za kipekee,
Kitu kingine kilichokuwa kinanishangaza ni kwamba
wanaume walikuwa wananiogopa sana, hawakutaka
hata kidogo kujiweka karibu yangu, Watu ambao
walikuwa wanajenga ukaribu kwangu walikuwa ni
wanawake wenzangu hadi ile hali ikaanza kunipa
mashaka. Ilibidi nimuulize yule mama aliyenifunza
tamaduni za kule kwanini wanaume wananiogopa,
Yule mama alinijibu ya kwamba wanaume
wananiogopa kwasababu nilikuwa nimewekwa
chapa ya mapenzi ya jinsia moja na Mungu wao
hivyo haikutakiwa hata kidogo kufanya mapenzi na
wanaume ndio mana wanajitenga mbali na mimi
wakihofia kudhurika, Hapo Ndipo nilipojitambua ya
kwamba nilikuwa sihitajiki kufanya mapenzi na
mwanaume, Maisha yangu mengi yalikuwa ni ya
kushiriki mapenzi na wanawake wenzangu,
mwanzoni nilikuwa napata shida ila mwishoni
nikajikuta naanza kuzoea na kuona wanawake
wenzangu ndio bola kuliko wanaume, Hakika ule
ulikuwa ni ushetani uliopitiliza. Ndani ya ule mji
tulikuwa hatufanyi kazi yoyote lakini tulikuwa
tunakula na kusaza, Hayo ndiyo yalikuwa maisha
yangu mapya ndani ya mji ambao ulijulikana kwa
jina la (MJI WA LAANA), Jina langu la halima
lilianza kupata umaarufu mkubwa sana ndani ya ule
mji kutokana na matendo yangu ambayo yalikuwa
yanawavutia zaidi wanawake wenzangu. Nilifanya
uchafu wa kila aina. Baada ya kuishi ndani ya ule
mji kwa miaka kadhaa hatimaye muda wa
kutambika uliwadia, Na ilikuwa ni lazima mtu
mmoja ateuliwe kwa ajili ya kupoteza maisha yake
ili ile jamii ya laana iendelee kuishi, Kula zilipigwa
ya nani atolewe kafara, Kwa bahati mbaya kula
nyingi zilinipendekeza mimi ndiyo niuawe kwa ajili
ya wengine kupona, Watu wengi walionipigia kura
walikuwa ni wanaume kwani hawakutaka niendelee
kuwepo kutokana na ile chapa ambayo nilikuwa
nimewekewa na Mungu wao. Sikuwa tayari kutolewa
kafara, Nikapanga kutoroka ili nikimbilie mbali zaidi
bila ya kujua kipi kitanikuta.
 
ILIPOISHIA....
Watu wengi walionipigia kura walikuwa ni wanaume
kwani hawakutaka niendelee kuwepo kutokana na
ile chapa ambayo nilikuwa nimewekewa na Mungu
wao. Sikuwa tayari kutolewa kafara, Nikapanga
kutoroka ili nikimbilie mbali zaidi bila ya kujua kipi
kitanikuta.
SASA ENDELEA....Ile siku ya kunitoa kafara iliwadia,
Kila mtu kwenye ile jamii ya laana alionekana
kufurahia ile kafara ambayo ilikuwa inaenda
kutolewa lakini kwa upande wangu sikuwa tayari
kupoteza maisha yangu hivyo kichwani mwangu
nilikuwa tayari nimeshaweka mikakati yangu vizuri
namna ya kukwepa ile kafara. Kawaida ya ule mji
wa laana ni kwamba mtu ambaye huwa anatolewa
kafara huwa na furaha kuzidi watu wengine wote
kwani ilikuwa imeaminishwa kuwa mtu anayetolewa
kafara ndiye bola kuliko wengine waliobakia lakini
kwa upande wangu sikuwa na furaha hata kidogo
muda mwingi nilikuwa mpole na mwenye huzuni
tele, Nakumbuka nilifungiwa kwenye chumba kidogo
ambacho kilikuwa kizuri sana, Nililetewa chakula
kingi na vinyaji vya kila aina kwasababu ndiyo
walikuwa wananiaga wakiamini ile ndiyo ilikuwa
safari yangu ya mwisho. Ndani ya kile chumba
nilifungiwa peke yangu bila kuwepo na mtu
mwingine, Sikuwa na hamu ya kula chakula hivyo
kile chakula nilichowekewa sikukila hata kidogo,
Baada ya muda mrefu kupita mlango wa kile
chumba nilichokuwa nimefungiwa ulifunguka
akaingia mdada mmoja ambaye alikuwa ni kama
mpenzi wangu kwani kipindi chote cha nyuma ni
yeye ambaye nilikuwa ninashiriki naye mapenzi ya
jinsia moja, Yule mdada aliingia akaufunga mlango
kwa komeo kisha akaanza kunililia, Aliniambia ya
kwamba hakupenda mimi mpenzi wake nitolewe
kafara lakini hakuwa na namna inabidi kafara
ifanyike kwa masilahi ya wakazi wote wa mji wa
laana, Sikushangaa yule dada kuniita mimi mpenzi
wake kwani michezo mingi ya kiuhasherati
nilishafanya naye hivyo niliona ni jambo la kawaida
japo moyoni nilikuwa nina simanzi zito. Yule dada
aliniambia amekuja kuniaga mara ya mwisho kwaiyo
alikuwa anataka kushiriki na mimi ule uchafu ambao
tulikuwa tunaufanya siku za nyuma, Kwakua ilikuwa
ni mida ya asubuhi niliamua kumkubalia ili nitimize
hazma yangu ambayo nilikuwa nimeipanga, Nilikuwa
nimepanga kutoroka asubuhi iyo iyo kabla mida ya
saa sita usiku haijafika kwani hiyo mida ndiyo
ambayo hutumiwa kutoa kafara, Kipindi nafanya
mapenzi ya jinsia moja na yule dada niliamua
kumvizia kwa siri nikamsukuma kwa nguvu hadi
akajigonga ukutani na kudondosha funguo za kile
chumba chini, Nilijuta kufanya kile kitendo kwani
yule dada alivyoanguka chini alipasuka kichwani
akawa anavuja damu ngingi, Pale pale yule dada
alibadilika kutoka katika umbo la msichana na kuwa
kiumbe cha ajabu tena cha kutisha, Sura yake
ilikuwa inatisha sana kwani macho yake yalikuwa
yamefumba huku mdomoni yakichomoza meno
makubwa, Ngozi yake ilikuwa ni ya mabaka
mabaka, Pale ndipo nilipojua ya kwamba watu wa
ule mji walikuwa ni mashetani waliovalia umbo la
binadamu. Kwa ujasiri wa hali ya juu niliokota
kipande cha mbao nzito kilichokuwa ndani ya kile
chumba nikamponda nacho yule dada kichwani hadi
kichwa kikawa hakitamaniki, Niliamua kufungua
mlango kwa tahadhali kubwa nikawa natoka nje
huku naangaza kila kona, Nilishangaa kujiona nipo
sehemu ambayo hakuna mtu hata mmoja, yali kile
chumba ni kama kilikuwa kimetengwa sehemu ya
mafichoni ambapo hakuruhusiwa mtu mwingine
kuingia. Nilijikongoja taratibu nikiwa naelekea eneo
ambalo lilionekana kuwa na njia iliyo nyooka,
Nilitembea kwa haraka kiasi hadi pale nilipoona
watu wengi kiasi wakiwa wamevalia mavazi
mekundu huku wakiimba kwa furaha kuja kwenye
upande wa chumba ambacho nilikuwa
nimehifadhiwa, Ilinibidi nibadilishe njia nikapita
upande wa kusini na kuanza kukimbia kwa nguvu,
Nilikimbia sana hadi nilipofika sehemu ambapo
sikuweza kupafahamu lakini ilikuwa ni sehemu
ambayo hapakuonekana mtu yoyote, Muda huo
ilikuwa bado ni asubuhi hivyo mwili wangu
haukuchoka sana, Nilipofika sehemu moja ambayo
kilikuwa ni kama kakichaka kakutengenezwa niliona
kuna kitu ndani ya kile kichaka kwani kile kichaka
kilikuwa kinacheza cheza, Niliogopa sana ikanibidi
nisogee kwa makini kuchungulia kitu ambacho
kilikuwa kimejificha ndani ya kile kichaka, Nilishtuka
baada ya kumkuta msichana wa kawaida kabisa
akiwa ndiye amejificha kwenye kile kichaka, Yule
msichana aliniambia na mimi niiname kujificha
kwani naye alikuwa na lengo la kutoroka kwenye ule
mji la laana, Kwa namna moja au nyingine nilifurahi
kuona nimepata mtu wa kusaidiana naye ili
kutoroka, Kilichonipendeza zaidi yule msichana
alikuwa anazijua njia za kutoroka kwani alikuwa pia
anaujua uchawi wa kuutumia ili tusiweze kuonekana
kwa watu wengine ndani ya ule mji la laana. Ilibidi
niwe namfatisha yule msichana kila sehemu
ambayo alikuwa anapita, Tulitembea hadi tulipofika
sehemu ambayo ilikuwa inaonesha ni kama mwisho
wa ardhi kwani kulikuwa kuna wingu zito limeziba
hivyo ilikuwa siyo rahisi kuona kitu kilichokuwepo
mbele, Yule msichana alinipatia vitu vyeusi kisha
akaniambia nivitafune huku nikiwa nimefumba
macho yangu, Vile vitu ambavyo nilikuwa nimepewa
nivitafune vilikuwa vichungu sana ila niliamua
kujikaza kikavitafuna vyote. Nilivyomaliza kutafuna
huku nimefumba macho nilihisi napaa kabisa lakini
yule dada alikuwa ananisisitiza nisifumbue macho
yangu hata kidogo, Nilijitahidi kufumba kwa nguvu
macho yangu lakini uoga ulikuwa unazidi kuniingia
kwasababu huwezi amini nilikuwa najiona nipo
hewani, tena anga la mbali kabisa hali ambayo
ilikuwa inanitia mashaka, Sijui ni kitu gani kilinituma
nifumbue macho yangu kwasababu kitu
kilichonitokea pindi nimefumbua macho kilikuwa ni
kitu cha kushangaza, Nilijikuta naangukia kwenye
moja ya paa la nyumba ambalo lilinitelezesha hadi
chini kabisa nikiwa nipo juu ya ungo huku mwilini
nikiwa sina hata nguo moja, Nilikuwa uchi kabisa
juu ya ungo ambao ulikuwa umeanguka chini, Kwa
mbali angani nilimuona yule msichana ambaye
alinisisitiza nisimbue macho yangu akiwa anaishia
na ungo wake, Haikuchukua muda ghafla wananchi
wa ile sehemu ambayo nilikuwa nimeanguka
walianza kujazana huku wakiwa wamenizunguka,
Wale wananchi walikuwa ni raia wa kawaida kabisa
tofauti na wale wa mwanzo ambao walikuwa
wanavalia mavazi mekundu yenye alama ya pembe
tatu. Nilivyoanguka pale chini sikuwa na nguvu za
kuinuka ili nikimbie kwani ni kama dawa za yule
msichana niliyetoroka naye kwenye mji wa laana
zilikuwa zimeishiwa nguvu pindi nilipofungua
macho, wananchi wengi walikuwa wamefika eneo la
tukio wakiwa wananishangaa, baadhi yao wenye
hasira kali walikuwa wameshikilia matofali,
mapanga na fimbo nzito wakiwa na lengo la
kunihukumu wakiniita mchawi. Nilitandikwa sana
kwa fimbo huku baadhi yao wakiwa wananipiga na
mawe kama wanaua nyoka, Akili zangu za kawaida
zilirudi nikawa napiga kelele huku nikilia
nikiwaomba wasiniue mimi siyo mchawi. Siku iyo
nilipigwa sana kwani kwa jinsi nilivyokuwa ulikuwa
hauwezi kunitazama mara mbili kwasababu mwili
nzima ulitapakaa damu.
 
ILIPOISHIA....
Wananchi wengi walikuwa wamefika eneo la tukio
wakiwa wananishangaa, baadhi yao wenye hasira
kali walikuwa wameshikilia matofali, mapanga na
fimbo nzito wakiwa na lengo la kunihukumu
wakiniita mchawi. Nilitandikwa sana kwa fimbo
huku baadhi yao wakiwa wananipiga kwa mawe
kama wanaua nyoka, Akili zangu za kawaida zilirudi
nikawa napiga kelele huku nikilia nikiwaomba
wasiniue mimi siyo mchawi. Siku iyo nilipigwa sana
kwani kwa jinsi nilivyokuwa ulikuwa hauwezi
kunitazama mara mbili kwa sababu mwili mzima
ulitapakaa damu.
SASA ENDELEA...Kipindi nipo chini nikiwa hoi
kutokana na kipigo ambacho nilikuwa nimepigwa
nilisikia sauti kwa mbali ikiwaamuru wale wananchi
wenye hasira kali waache kunipiga lakini wale
wananchi hawakusikia hata kidogo walikuwa
wanaendelea kunipiga kama mwizi aliyeiba vitu vya
thamani, Ulisikika mlio wa bunduki ambao
ulisababisha kila mtu aliye kwenye lile eneo kutimua
mbio, Ile ndio ilikuwa pona pona yangu kwani japo
uso wangu ulikuwa umevimba kutokana na kipigo
lakini niliweza kuwaona maaskari wawili waliofika
karibu yangu kisha wakanifunga pingu huku
wakinikokota kuelekea kwenye defender(gari lao la
kipolisi), Walinirusha kama mzoga kwenye lile gari,
Sikuweza kuhisi maumivu mengine kwani mwili
wangu ulikuwa umekufa ganzi kabisa, Sikuelewa jina
la ule mtaa wala mkoa ambao nilikuwa nipo na
wala sikujua sehemu ambapo wale maaskari
walikuwa wananipeleka, Nilipokuwa ndani ya like
gari lao nilikuwa nimeishiwa nguvu, Nilikuwa nipo
hoi sana hadi nikajuta kuzaliwa kwani niliona napitia
mateso makali sana yaliyokuwa yananiumiza kila
kukicha. Macho yangu yalifumba kwa mara nyingine
nikawa naona ukungu mwingi ukitanda usoni
mwangu, Sikuelewa kitu kilichofuata kwani nilikuwa
ni kama nimezimia, Nilikuja kushtuliwa na maji ya
baridi ambayo nilikuwa nimemwagiwa mwilini
mwangu huku nikiwa kwenye chumba ambacho
kilikuwa kina dirisha dogo kwa juu, Nilikurupuka
huku nikihema juu juu kama vile nilikuwa
ninakimbizwa, Nilipojicheki mkononi nilikuwa nina
pingu huku mwilini nimevalishwa mavazi ya njano
ikiashilia nilikuwa tayari mimi ni mfungwa, Mbele
yangu alikuwa amesimama askari wa kike aliyekuwa
ana sura ya kikatiri, Yule askari ndiye aliyenimwagia
maji ya kunishtua kutoka kwenye ile hali ya kuzimia,
Yule askari hakuongea maneno mengi ila
alinionesha chumba changu ambacho nitakuwa
ninalala kisha akanifungulia pingu mikononi, Roho
iliniuma sana kuona nipo kwenye chumba ambacho
kilikuwa kimezungushiwa nondo, Nilijiuliza maswali
mengi sana ambayo sikupata jibu, Nilishangaa kwa
nini nimepelekwa kufungwa haraka haraka kiasi kile
bila hata kufanyika uchunguzi wa kubaini makosa
ambayo niliyatenda. Sikuwa na jinsi niliamua kutulia
huku nikiwa sijui nini hatima ya maisha yangu
ambayo kila kukicha yanakuwa na misuko misuko
isiyo pungua. Kawaida ya lile gereza wafungwa
walikuwa wanapangwa wawili wawili kwenye
chumba kimoja, Mimi nilikuwa nimepangwa na
msichana wa kiarabu ambaye alikuwa anajua
kiswahili, Yule msichana alionekana kuwa mzoefu
wa lile gereza na pia alionekana kana kwamba
alikuwa ameishi maisha mengi mule gerezani kwani
hakuonekana kuwa na hofu hata kidogo, Ilibidi
nimuelezee yule msichana wa kiarabu mambo
ambayo yamenikuta hadi nipo mule gerezani, Yule
msichana alishangaa sana kwani hakuwahi kusikia
kabla mtu akifungwa kwa kesi ya uchawi, Ilibidi yule
msichana anitie moyo kisha akaniambia nisiwe na
wasi wasi kama nilifungwa kwa bahati mbaya basi
ipo siku nitatoka na kurudi uraiani tena, Ilibidi
nimuulize yule msichana maswali mengi ambayo
nilitamani kuyajua, Bila hiyana yule msichana
ambaye alikuwa anaitwa Hudati aliniambia kuwa lile
gereza lilikuwa linaitwa Gereza mlonge, Lilikuwa ni
moja ya gereza kubwa la kike lililokuwa linapatikana
mkoani Tanga, Nilivyosikia habari za Tanga
nilishtuka sana, Sikuamini masikio yangu kwa kile
nilichokisikia kuwa nilikuwa ndani ya Tanga, Yani
kumbe kipindi nimesafiri na ule ungo kutoka Mji wa
laana nilikuja kuangukia Tanga, Niliogopa sana ila
nikaamua kujikaza, Nilijaribu kumuuliza tena Hudati
kitu kilichofanya afungwe mule gerezani, Hudati
alicheka kiasi kisha akaniambia yeye alimuua
mpenzi wake kutokana na wivu wa mapenzi hivyo
alikuwa amehukumiwa kifungo cha maisha gerezani.
Maisha ndani ya lile gereza mlonge yalikuwa
magumu sana kwani chakula kilikuwa ni kidogo
hivyo muda mwingi wafungwa walikuwa
wanagombania, Wasichana wababe ndio walikuwa
wanafaidika na kile chakula kwani walikuwa
wanatunyanyasa sana sisi ambao tulikuwa wapole,
Kitu nilichokipenda ndani ya lile gereza mlonge ni
kwamba Hudati alikuwa ni miongoni mwa wafungwa
wababe hivyo muda mwingi nilikuwa natumia kivuli
chake kufaidika, Hudati hakutaka nionewe kabisa
hata kidogo, Alikuwa yupo radhi kupigana hata na
wafungwa watano pindi atakaponiona naonewa,
Taratibu ndani ya lile gereza la mlonge nilianza
kuishi maisha ya raha, Maisha ambayo yalikuwa
siyo ya kunyanyasika kutoka kwa wafungwa
wenzangu. Kitu ambacho kilikuwa kinanishinda
ndani ya lile gereza ni harufu mbaya ya vyumba
ambavyo tulikuwa tunalala kwani tulikuwa
tunajisaidia haja kubwa na ndogo kwenye ndoo
ambazo zilikuwa zimewekwa kwenye kila chumba
cha wafungwa, Ile hali iliniuma sana yani tulikuwa
tunaishi kama wanyama wa porini ambao walikuwa
wanajisaidia sehemu ambayo wanalala, Iyo ndiyo
ilikuwa hali halisi ambayo ilinitokea ndani ya gereza
mlonge, Kuna kipindi nilikuwa nikikaa naanza
kuwaza ni heri ningepokea mikoba ya bibi ya uchawi
kwani kukataa kwangu kurithi ile mikoba ndiyo
kulinisababishia matatizo na mikosi yote ile,
Sikujua kama yule bibi yangu alikuwa mzima au
alikuwa tayari ameshafariki kwani ilikuwa imepita
muda mrefu sana tangu nilivyo ondoka mkoani
Simiyu. Magereza ya wanawake ni magereza
ambayo huwa yana mambo mengi sana ambayo
huwa siyo yakupendeza hata kidogo, Nikiwa kule
gerezani mlonge nilipitia matukio mengi ambayo
sikuweza kuyaepuka, Kwani siku zilivyokuwa
zinasonga mbele Hudati alianza kunitamani
kimapenzi kitu kibaya zaidi alianza kunijengea wivu
hadi kwa wafungwa wengine ambao walikuwa rafiki
zangu, Hudati bila aibu alinitamkia kuwa
amenipenda na yupo radhi kunifanyia chochote
nitakachokitaka, Kauli ya Hudati haikunishtua sana
kwani yale mambo nilisha yafanya sana kule kwenye
mji wa laana lakini niliitaji kuyasahau. Hudati
alinilazimisha sana hadi mwisho wa siku niliamua
kuwa mpenzi wake, Ninavyo zungumza hivi inabidi
unielewe kuwa Hudati alikuwa ni mwanamke
mwenzangu, Kila kitu kilichokuwa kwenye mwili
wake ndiyo nilikuwa nacho mimi lakini kwa tamaa
zetu za miili tulijikuta tunaingia kwenye uchafu wa
kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja, Najua wengi
wenu mtanihukumu na kunichukia kutokana na
matendo ambayo nilikuwa ninayafanya lakini
usiombe usingiziwe kosa kisha upelekwe gerezani,
Nakuapia ukirudi kutoka kifungoni utakuja kuniambia
kuwa mambo ambayo ninakueleza yapo na bado
yataendelea kuwepo kila siku magerezani. Penzi
langu na Hudati lilikuwa ni tamu sana ilifikia muda
mimi pia nikawa namuonea wivu Hudati pindi
nikimuona na msichana mwingine, Kila ikifika usiku
ilikuwa ni lazima tufanye uchafu wetu kabla ya
kulala, Kumbe tuliokuwa tunafanya vile vitendo vya
kiuhasherati hatukuwa sisi tu bali karibia gereza
zima lilikuwa linajihusisha na mapenzi ya jinsia
moja, Ile hali ilisababishwa na hamu ya mapenzi
ambayo wafungwa wengi tulikuwa tunayo na
ukizingatia tulikuwa ni wanawake. Zile taarifa za
kuhusu wafungwa kusagana ndani ya gereza mlonge
ziliwafikia hadi wakuu wa gereza ambao
walichukizwa na zile taarifa, Onyo kali lilitolewa kwa
yoyote atakayebainika kushiriki mapenzi ya jinsia
moja. Maaskari magereza waliamua kutufanyisha
kazi ngumu ambazo zilisaidia kutupunguzia hamu za
mapenzi kutokana na uchovu ambao tulikuwa
tunaupata, Ile ilisaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza
ule mchezo mchafu, Hata mimi na Hudati hatukuwa
na hamu tena yakushiriki ule uchafu japo tuliendelea
kuishi kama mke na mume. Ndani ya lile gereza la
mlonge uliingia utaratibu ambao ulikuwa
unatushangaza sana wafungwa wengi kwani kila
wiki wafungwa kadhaa walikuwa wanachukuliwa na
maaskari magereza kwa kisingizio kuwa wanaenda
kufanyiwa ukaguzi wa miili yao, Kitu cha ajabu
walikuwa wakiondoka hawarudi hali ambayo ilikuwa
inatupa wasi wasi wafungwa wengi, Kuna siri kubwa
sana ambayo ilikuwa inahusiana na wale wafungwa
ambao walikuwa wanachukuliwa bila kurudishwa,
Siri ambayo nilikuja kuigundua kipindi ambacho
nilikuwa ni mmoja wa wafungwa ambao walikuwa
wamechukuliwa kwa kisingizio cha kwenda
kufanyiwa ukaguzi.
 
ILIPOISHIA....
Kuna siri kubwa sana ilikuwa inahusiana na
wafungwa ambao walikuwa wanachukuliwa bila
kurudishwa, siri ambayo nilikuja kuigundua kipindi
ambacho nilikuwa ni mmoja wa wafungwa ambao
walikuwa wamechukuliwa kwa kufanyiwa ukaguzi.
SASA ENDELEA....Tulipakizwa kwenye gari kubwa
nikiwa miongoni mwa wafungwa ambao tulikuwa
tumechukuliwa kisha safari kutoka ndani ya lile
gereza ilianza, Safari ambayo hatukujua dhumuni
lake hasa ni lipi japo wengi tuliamini kuwa ni safari
ya kwenda kufanyiwa ukaguzi wa miili yetu,
Sikumbuki idadi kamili ya wafungwa ambao
tulikuwa tumepakiwa ndani ya lile gari lakini kwa
haraka haraka tulikuwa ni kama wafungwa
tusiopungua ishirini, Lile gari ambalo tulipakizwa
lilitembea umbali mrefu huku tukiwa tumefungiwa
kwa ndani, Hatukuweza kuona kwa nje kwa sababu
lilikuwa ni gari aina ya basi ambalo lilikuwa
limefungwa vioo vyake, ilikuwa ni vigumu kuona kitu
ambacho kipo kwa nje hivyo tulikuwa tunasafirishwa
kama vipofu, Baada ya safari ndefu hatimaye lile
gari lilisimama huku kila mfungwa akiwa na hamu
ya kutaka kuona kitu ambacho kilikuwa kipo nje la
lile basi, Hudati alikuwa ni mmoja wa wafungwa
ambaye tuliungana naye, Hudati alikuwa karibu
yangu huku akijaribu kuniongelesha mambo mbali
mbali, Tukiwa hatuelewei hili wala lile mlango
ulifunguliwa kisha tukashushwa chini tukiwa
tumepagwa kwenye mstari mmoja mrefu, Wafungwa
wengi tulishtuka baada ya kujikuta tumeletwa
kwenye eneo ambalo halikuonekana kuwa salama
hata kidogo, Lilikuwa ni eneo ambalo lilifanana
kabisa na uwanja wa vita kwani sehemu nyingi
zilikuwa zinafuka moshi, Tuliweza kuwaona
maaskari wengi sana wakiwa wamewafunga kamba
wafungwa ambao walikuwa wamechukuliwa kutoka
gerezani siku za nyuma, Tukiwa tunatahamaki
alisogea askari mmoja pembeni yetu na mnyororo
mrefu akaanza kutufunga mikono yetu, Wafungwa
wenye mioyo mepesi walianza kulia huku wakiomba
warudishwe gerezani walikotolewa. Siku iyo
tulikusanywa wote tukafungiwa kwenye chumba
ambacho kilikuwa kikubwa, Hatukupewa chakula
wala maji hadi kulivyokucha, Asubuhi tuliamshwa
kwa mijeredi iliyotua kwenye migongo yetu,
Tulijizoa zoa huku minyororo ikituumiza mikononi
lakini wale maaskari hawakutujali kabisa,
Tulisogezwa hadi kwenye eneo ambalo lilikuwa liko
wazi, mfungwa mmoja wetu alikuwa amechoka sana
hadi akawa anashindwa kuvumilia, muda mwingi
alikuwa anaanguka chini, Askari mmoja wa kiume
mwenye sura nyeusi alimsogelea akamfungua
nyororo kisha akamsogeza mbele kama hatua tano
na kumpiga risasi zipatazo sita kifuani, Hapo ndipo
tulijawa na uoga uliopitiliza, Hata Hudati alilia pia
pamoja na ujasiri wake, Yule askari alituambia tukae
kimya akawa anatishia kutupiga risasi, Ile sehemu
ilikua inatisha yani muundo wake ulikuwa ni kama
kambi iliyoathiliwa na vita kwani kulikuwa kuna
nyumba kadhaa zilizokuwa zimeharibiwa na
mabomu, Pia ile sehemu ilikuwa imezungushiwa
nyaya ngumu kuzunguka wigo wake. Tulivyokuwa
tumesimama kwenye ule uwanja alikuja mtu mmoja
ambaye mkononi alikuwa ameshikilia panga kali,
Yule mtu alikuwa amekuja pia na begi kubwa
ambalo lilikuwa lipo katika muundo wa nailoni,
Maaskari watano waliongezeka kwenye lile eneo
huku wakiwa wamesogeza kitu kilichofanana na
meza nzito, Pale pale mfungwa wa mbele
alifunguliwa minyororo akasogezwe kwenye ile
meza huku kichwa chake kimeinamishwa kwenye ile
meza, Hauwezi kuamini yule mfungwa alikatwa
kichwa kwa ule upanga mkali kisha akanyofolewa
baadhi ya viungo vyake kama vile matiti na figo,
Yule mtu aliyemchinja yule mfungwa mwenzetu
alifungua begi lake akaweka kichwa, matiti na figo
za yule msichana(mfungwa mwenzetu), Niliogopa
sana moyo ukawa unanidunda kwa kasi, Siyo mimi
peke yangu niliyekuwa ninaogopa bali wafungwa
wote walikuwa wanaogopa huku wakilia kwa kuhofia
kupoteza maisha yao, Hakuna kitu kinachouma
kama kufa huku unajiona, Lile zoezi la kukata
vichwa liliendelea hadi walipomfika Hudati ambaye
alikuwa mbele yangu, Mimi nilikuwa mtu wa pili
kutoka mwisho, Hudati alilia sana huku
akining'ang'ania ili asipelekwe kwenye ile meza
ambayo ilikuwa imetapakaa damu, Nilimuonea
huruma Hudati kwani nilijua baada ya yeye kufa
nitafatia mimi, Hudati alipigwa na kitako cha
bunduki kichwani baada ya kuleta ubishi, Hatimaye
akasogezwa kwenye ile meza huku kichwa chake
kimelazwa kwenye meza kwa ajili ya kukatwa,
Sikuweza kuvumilia kwa jinsi Hudati alivyokuwa
anatapa tapa huku kiwili wili chake kikiwa
kimetengana na kichwa. Oh mimi halima hadi
napata kuyaelezea haya roho inaniuma sana, sisi
binadamu ni wanyama hatarishi sana tena tusio na
huruma hata kidogo, Hudati alikuwa anatapa tapa
kama kuku aliyekatwa kichwa, Roho ya Hudati
ilionekana kuwa ngumu kukatika kwani alitapa tapa
kwa muda mrefu huku damu zikiruka kutoka kwenye
mirija ya shingoni mwake, baada ya muda kupita
Hudati alitulia akanyofolewa viungo vyake ambavyo
viliwekwa kwenye mabegi mengine ambayo
yakikuwa yameongezwa. Ilifika zamu yangu, Nikiwa
muoga wa hali ya juu, Nililia hadi machozi yakawa
yameisha machoni mwangu, Sikuwa na ujanja lile
panga lilivyonyanyuliwa juu niliamua kusali sara
yangu ya mwisho kimoyo moyo nikiwa tayari
nimekubalia kufa kwani nilikuwa nimeshachoka na
mateso ya duniani, Nilijua nitahisi maumivu makali
lakini nilijipa moyo ya kuwa baada ya muda
sitasikia maumivu kwani nitatulia kama wenzangu
waliokuwa wamechinjwa tayari, Nikiwa
nimekubaliana na hali halisi nilishangaa kumuona
yule mchinjaji anashangaa kana kwamba kuna kitu
anakiangalia kwa mbele, Ile kutahamaki kilipita
kimbunga kikali ambacho kilisababisha kila mtu
ajifiche kuokoa maisha yake, Ule ndio ulikuwa
usalama wangu kwani na mimi kwa kuwa nilikuwa
nimefunguliwa minyororo niliamua kukimbia mbio ili
nijinasue kwenye mauaji yale, Kile kimbunga
kilikuwa ni kikali sana, kwani kilileta uharibifu
mkubwa kwenye lile eneo. Katika kimbia kimbia
yangu nilijikuta nadondoka kwenye shimo ambalo
lilikuwa ni andaki, Nilijibanza kwenye ile sehemu
hadi kimbunga kilivyopita, Nikiwa kwenye lile andaki
nilipata kuwasikia wale maaskari wakiongea na yule
mchinjaji ya kwamba biashara yao imeenda vizuri
japo kimbunga kilitaka kuwaharibia, Hapo ndipo
nilipogundua kuwa viungo vya wale wafungwa
waliokuwa wamechinjwa vilikuwa vinaenda kuuzwa
kama sehemu ya biashara, Roho iliniuma sana
kuona binadamu tumekuwa wakatili kiasi kile.
Nilijificha kwenye lile andaki hadi ikipofika usiku,
Nilijikaza nikajitoa kwenye lile andaki kwasababu
sikusikia sauti za mtu yoyote akiongea hivyo nilihisi
maaskari watakuwa wameondoka wote,
Nilichungulia kwenye upenyo mdogo ambao ulikuwa
kwenye lile andaki, Giza lilikuwa ni kali sana, Hivyo
sikuweza kuona kitu chochote lakini nilivyo angalia
vizuri niliona kitu cha ajabu, Niliona kama watu
wakigombania zile maiti za wafungwa, Nilishtuka
baada ya kushuhudia lile tukio, Uoga uliniingia kwa
wingi nikawa natetemeka mwili mzima, Wale watu
waliokuwa wanazila zile maiti hawakuwa watu wa
kawaida kwani kwa muonekano wao walikuwa
wanawaka waka huku wakiwa na sura za kutisha
sana, Ilinibidi nijirudishe kwenye lile andaki kwa
umakini lakini kipindi najirudisha nilikanyaga udongo
ambao ulianguka na kusababisha sauti ambayo
ilimshitua mmoja wa wale watu waliokuwa wanakula
zile maiti, Yule mtu alianza kusogelea lile eneo
ambalo nilikuwa nimejificha.
 
ILIPOISHIA....
Wale watu waliokuwa wanakula zile maiti hawakuwa
watu wa kawaida kwani kwa muonekano wao
walikuwa wanawaka waka huku wakiwa na sura za
kutisha sana, Ilinibidi nijirudishe kwenye lile andaki
kwa umakini lakini kipindi najirudisha nilikanyaga
udongo ambao ulianguka na kusababisha sauti
ambayo ilimshtua mmoja wa wale watu waliokuwa
wanakula zile maiti, Yule mtu alianza kusogelea lile
eneo ambalo nilikuwa nimejificha.
SASA ENDELEA....Nilijikausha kimya chini ya lile
andaki huku nikiziba pua zangu pamoja na mdomo
ili nisiweze kutoa hewa ambayo ingeweza kumshtua
yule mtu wa ajabu ambaye alikuwa amelikalibia lile
andaki, Yule mtu alisogea kwa karibu akawa
anachungulia kwenye uwazi wa lile andaki ambalo
nilikuwemo, Nilikuwa naogopa sana hadi
nikajikojolea kutokana na uoga ambao nilikuwa nao
siku iyo, Yule mtu aliangaza kwa makini kwenye lile
andaki na ghafla akageuka kurudi kwa wenzake,
Sikujua ni kitu gani kilimfanya arudi kwa wenzake
lakini nilihisi huenda hakuwa ameniona ndio mana
hakutaka kufatilia sana chini ya lile andaki ambalo
nilikuwa nimejificha. Zilivyopita dakika kadhaa
sikusikia sauti ya kiumbe chochote kwenye lile
eneo, Nilitamani kutoka nje ya andaki ili niangaze
lakini uoga niliokuwa nao ulikuwa hauelezeki,
Ilinibidi nijibanze ndani ya lile andaki hadi ilipofika
alfajili ndiyo niliamua kutoka huku nikiwa na
wasiwasi, Niliangaza kulia na kushoto bila kumuona
mtu yoyote kisha nikaamua kukimbia bila kuangalia
nyuma, Nilikimbia sana nikiwa nimevalia yale
mavazi ya kifungwa, Nilipita njia ambazo
sikuzifahamu lakini kitu nilichoamini ni kwamba
nilikuwa nipo ndani ya jiji la Tanga, Baada ya
kukimbia umbali mrefu niliamua kuzivua zile nguo
za kifungwa nikawa nimebakiwa na nguo za ndani
tu, Niliamua kufanya vile ili kujiondolewa hatari ya
kujulikana kama mfungwa niliyetoroka, Kitu
kilichosaidia ni kwamba sehemu nilizokuwa ninapita
hazikuwa na mtu hata mmoja ambaye nilikuwa
napishana naye, Yani kwa kifupi zilikuwa ni sehemu
za mbali sana, Nilitembea kwa miguu takribani siku
tatu bila kuona mji wowote, Njaa na kiu vilinitesa
lakini nilijikaza kama mwanamke shupavu nikawa
naendelea kusonga mbele huku nikiomba nikutane
na mtu yoyote ambaye atanipatia msaada. Kwa
bahati nzuri ndani ya ile siku ya tatu mida ya
mchana nilikutana njiani na mama ambaye alikuwa
amejitwisha kikapu chake kichwani, Yule mama
alihisi mimi ni chizi kwa muonekano wangu jinsi
nilivyokuwa kwasababu nilikuwa nimevaa nguo za
ndani pekee, Niliamua kumdanganya yule mama ya
kwamba kuna vijana walikuwa wanataka kunibaka
ndio mana sina nguo yoyote, Yule mama alinionea
huruma akanipatia kanga yake ambayo nilijifunga
lubega, Hakuishia apo alinipatia na kibuyu cha
maziwa ambacho alikuwa amekibebelea kisha
tukaachana kila mtu akaendelea na safari zake,
Moyoni nilijisikia amani nikamshukuru sana yule
mama kwa wema alionitendea mtu asiyenifahamu.
Baada ya kuuliza uliza sana nilifanikiwa kufika
maeneo ya Tanga mjini kama mida ya saa nne
usiku, Sikuwa na mtu ambaye nilikuwa namfahamu
pale Tanga mjini hivyo sikuwa na sehemu ya
kwenda kulala, Nilipanga kulala kwenye mabaraza
ya maduka ya watu, Kile kibuyu cha maziwa
nilichopewa na yule mama mpita njia kiliisha
nikawa nahisi njaa upya, Niliamua kwenda kuomba
kwa wauza chakula kama wanaweza kunipa mabaki
ya chakula lakini wote walinikatalia, Hapo ndipo
nilipo mkumbuka yule mama mkarimu aliyenisaidia
kibuyu cha maziwa. Niliamua kuzunguka mitaani
nikitafuta sehemu ambayo naweza kupata japo
makombo ya chakula ili nilirizishe tumbo langu
ambalo lilionekana kulalamika kwa njaa kali, Katika
pita pita zangu nilitokea eneo ambalo lilionekana
kuwa na jengo moja kubwa ambalo kwa juu lilikuwa
limeandikwa (MIAMI CLUB), Yale maneno yaliyo
andikwa kwenye lile jengo yalikuwa yanang'aa kwa
rangi nyekundu, Nilivyo angalia nje ya lile jengo
niliona kuwa watu wengi wakiendelea na mambo
yao, Gari za kifahari nyingi zilikuwa pia zimepaki nje
ya lile jengo ambalo lilionekana kama jengo la
starehe. Kitu kilichonishangaza ni mavazi ambayo
wanawake wenzangu walikuwa wameyavaa,
wanawake wengi nje ya lile jengo walikuwa
wamevaa nusu uchi, Ninavyokuambia nusu uchi
inabidi uelewe ya kwamba nusu ya mwili wao
ilikuwa wazi bila kustiliwa na kitu chochote,
Nilijisikia vibaya kwani wale wanawake walionekana
kufurahia ule muonekano wao, Isitoshe
nilivyowachunguza vizuri niligundua walikuwa
wanafanya biashara ya kuuza miili yao nje ya ule
ukumbi wa starehe. Niliamua kusogea umbali
kidogo kutoka kwenye lile eneo nikiwa na lengo la
kuomba pesa kwa mtu yoyote atakayepita karibu
yangu ili nikanunue chakula, Kumbuka wakati huo
bado nilikuwa nimejifunga lubega, Wanawake wengi
waliokuwa wamevalia nusu uchi walikuwa
wananipita huku wakinishangaa kwa jinsi
nilivyokuwa nimevaa, Najua wengi walikuwa
wamenihisi nimetoka kijijini lakini mimi sikuwajali
hata kidogo, Na wala sikuwaonea aibu nilikuwa
nawaomba japo wanipe elfu moja nikanunue
chakula, Wengi wao walinijibu majibu mabaya sana,
Mbaya zaidi wengine walifikia hatua ya kunitukania
wazazi wangu, Nilijisikia vibaya sana kama
mwanamke ila niliamua kuyavumilia yote. Nikiwa
nimejiinamia huku machozi yakinitililika nilihisi kuna
mtu ananishika kichwa akiniashiria nisimame,
Nilivyo nyanyua kichwa changu nilikutana na kijana
ambaye nilikuwa simfahamu, Alikuwa ni kijana
mrefu kiasi ambaye alionekana kuwa mtanashati,
Yule kijana aliniuliza tatizo langu, Nami bila kusita
nilimwambia kuwa nilikuwa nina njaa na wala
sikuwa na sehemu ya kulala, Yule kijana aliamua
kunisaidia usiku ule kwani alikuwa amekuja na gari
lake, Aliamua kurudi kwa marafiki zake waliokuwa
wamesimama kando kidogo akawa anawaaga,
Sikusikia maongezi yao vizuri lakini kwa mbali
nilimsikia yule kijana akiwaambia wenzake ya
kwamba anaenda kula kuku wa kijijini kwasababu
kuku wa mjini amewachoka, Ile kauli iliniweka njia
panda lakini baada ya kutafakali sana niliweza
kuielewa, Yule kijana alimaanisha anaenda kulala na
mimi mwanamke wa kijijini kwasababu wanawake
wa mjini alikuwa amewachoka, Nilitaka kusita
kuondoka nae lakini nilihisi nitakosa msaada usiku
ule na sikuwa na sehemu ya kwenda, Yule kijana
alinipakiza kwenye gari lake tukawa tunaondoka,
Moyoni nilipanga kutoshiriki penzi na yule kijana
kwasababu ya chapa ambayo nilikuwa nimewekewa
chini ya kitovu kipindi kile nilipokuwepo Mji wa
laana, Ile chapa ilikuwa ni kama onyo lakutokufanya
mapenzi na mwanaume hivyo sikutaka kumuua
kijana wa watu. Wanaume ni watu wabishi na wenye
tamaa sana kwani huwezi amini tulivyokuwa ndani
ya lile gari yule kijana alikuwa ananilazimisha
tufanye mapenzi ndani ya gari lake.
 
ILIPOISHIA....
Yule kijana alinipakia kwenye gari lake tukawa
tunaondoka, Moyoni nilipanga kutoshiriki penzi na
yule kijana kwasababu ya chapa ambayo nilikuwa
nimewekewa chini ya kitovu kipindi nilipokuwepo
ndani mji wa laana, Ile chapa ilikuwa ni kama onyo
lakutofanya mapenzi na mwanaume hivyo sikutaka
kumuua kijana wa watu. Wanaume ni watu wabishi
na wenye tamaa sana kwani huwezi amini
tulivyokuwa ndani ya lile gari yule kijana alikuwa
ananilazimisha tufanye mapenzi ndani ya gari lake.
SASA ENDELEA....
Sikutaka kabisa yule kijana ashiriki ngono zembe na
mimi ndani ya lile gari, Nilijitahidi kadri ya uwezo
wangu kumzuia asifanya kile kitendo ambacho
kilikuwa hatarishi kwa upande wake, Kila
nikimkumbuka yule kijana huwa namuombea
apumzike kwa amani kutokana na kulazimisha kitu
ambacho hakujua madhara yake, Kama ujuavyo
wanawake hatuna nguvu za kutosha kuweza
kupingana na wanaume, Yule kijana alinilazimisha
kwa nguvu huku akinipandisha kanga yangu kwa
juu, Nilijitetea kadri ya uwezo wangu lakini
nilishindwa kabisa kujinasua kwa yule kijana
ambaye alionesha nia kabisa yakutaka kushiriki
ngono zembe na mimi, Sijui wanaume muda
mwingine wanakuwa ni viumbe wa aina gani
kwasababu waking'ang'ani kitu huwaga wanataka
kutimiza bila kutambua athari zilizopo mbele yao,
Mambo mengine ya aibu siwezi kuyaelezea yote
lakini kitu nachokumbuka ni kwamba yule kijana
alienda mishindo miwili kisha akaanza kutetemea
huku akishikilia kolomeo lake, Niliogopa sana usiku
ule, kwakuwa gari lilikuwa limepakiwa pembezoni
mwa barabara niliamua kutoka haraka huku
nikikimbia kukwepa ushahidi, kitu nilichokumbuka ni
kubeba pochi ya yule kijana ambayo ilikuwa ina
pesa nyingi, Kifo cha yule kijana kiliniogopesha
japo nilitegemea kitatokea kutokana na ile chapa
niliyokuwa nayo, Ile chapa ilikuwa inaniruhusu
kushiriki mapenzi ya jinsia moja na wanawake
wenzangu tu, Sikutakiwa kabisa kushiriki ngono na
mwanaume ndio maana vijana karibia wawili
waliojaribu kushiriki ngono na mimi walikuwa
wamefariki vifo vya ghafla. Zile pesa nilizozichukua
kutoka kwa yule kijana ziliweza kunisaidia kununua
nguo ambazo nilizitumia kuustiri mwili wangu,
Nakumbuka ile pochi ilikuwa ina kama laki sita
ambazo niliamua kuzitumia vizuri, Kitu cha kwanza
nilitafuta chumba cha kupanga Tanga mjini maeneo
ya Donge, Sikuishia apo niliamua kujifanyia biashara
zangu ndogo ndogo za kuniingizia kipato, Niliamua
kuuza karanga pamoja na mahindi ya kuchoma,
Kipindi hicho nilikuwa tayari nimeshakuwa msichana
mkubwa kabisa ambaye nilikuwa na uwezo wa
kujiendesha kwenye biashara bila matatizo yoyote,
Mwanzoni nilikuwa napata sana tabu kwenye ile
biashara yangu lakini nilipofanya kwa muda mrefu
nilianza kupata wateja wengi, Taratibu nikaanza
kuingiza kipato ambacho kilikuwa kinanikidhi
kuendesha maisha yangu, Kila siku sikuacha
kumuombea yule kijana aliyekufa ndani ya gari
apumzike mahara pema peponi kwasababu bila
yeye nisingepata ule mtaji wa laki sita ambao
ulionekana kubadilisha maisha yangu kwa kiasi
kikubwa. Nilipata wateja wengi sana hasa hasa
wanaume kwani walionekana kuvutiwa na mimi zaidi
kuliko biashara yangu, Mimi pia nilikuwa nawapa
ushirikiano wakutosha kwa kubadilishana mawazo
lakini sikuwa tayari kuwakubalia maombi yao
ambayo walikuwa wanataka tuwe wapenzi, Sikutaka
kabisa kuendelea kuwapoteza vijana wasiokuwa na
hatia, Kila siku nilikuwa napata vishawishi vya
wanaume lakini nilijaribu kuvikwepa siyo kwamba
sikuwapenda bali sikutaka wafe kwa ajili yangu.
Duniani hakuna mwanamke mbaya hata kidogo,
Kwakuwa nilikuwa naingiza pesa nzuri niliamua
kununua vipodozi kwa ajili ya kujiremba ili nami
nipendeze kama wanawake wenzangu, Lile lilikuwa
kosa kubwa sana kulifanya kwani ilikuwa ni kama
nimewaambia wanaume waanze tena kunitongoza,
Safari hii nilitongozwa sana hadi nikawa nachukia,
Wanaume walionifata walikuwa ni wengi sana ila
kuna mmoja ambaye yeye alionesha nia ya dhati
kabisa ya kuishi na mimi kwani alikuwa ananiambia
mipango mizuri ambayo angeifanya na mimi pindi
tukiishi pamoja kama mke na mume, Yule kaka
alionekana kuwa mstarabu sana na wala hakuwa na
mbwembwe nyingi kama wanaume wengine, Hisia
za mapenzi ni mbaya sana, Sura ya yule kaka
ilikuwa inanijia ndotoni kila nikilala, Nilianza
kumpenda kwasababu hisia zangu za mapenzi
zilikuwa zimevutwa kwake, Nilijizuia kutokumpenda
lakini nilikuwa nashindwa, Nilisha yashuhudia
machozi ya wanaume wengi lakini chozi la yule
kaka akinililia niwe wake lilinifanya mimi pia nilie na
kumwambia nimekubali kuwa wake, Nilishindwa
kujizuia kabisa kumkatalia, Mapenzi yana nguvu
sana hasa wawili mkipendana kwa dhati,
Nilimkubalia yule kaka lakini nilimwambia
hatutafanya mapenzi hadi siku akiwaona wazazi
wangu, Niliamua kumwambia vile ili kumuepusha na
kifo kaka wa watu aliyevutiwa na mimi.
****Yule kaka kwa majina alijulikana kama Rama
Suleimani, Alikuwa ni mfanyakazi wa benki moja
iliyopo ndani ya jiji la tanga, hakufanikiwa kuwa
tajiri sana bali alikuwa ana utajiri wa kawaida,
Alikuwa amejenga nyumba nzuri ya vyumba vitano,
Pia alikuwa amefanikiwa kununua gari ndogo aina ya
Alteza. Siku ambayo alinikaribisha kwake kwenda
kumtembelea sikuamini kwa jinsi alivyokuwa
amejipanga kimaisha, Nilifurahi nami pia nilimleta
sehemu ambayo nilikuwa nimepanga, Hakufurahia
sana maisha ambayo nilikuwa ninayaishi hivyo
aliamua kunishawishi tukaishi pamoja nyumbani
kwake, Kwakuwa tulikuwa ni wapenzi sikuona ubaya
wowote niliamua kuhamia nyumbani kwake moja
kwa moja, Nikawa naishi kama mke wake,
Tulipendana sana na Rama, Nilideka kama mtoto
akanidekeza, Rama hakutaka kabisa niwe na huzuni
hata kidogo hivyo muda mwingi alinifanyia kila kitu
nikichokitaka. Mwaka mzima ulikatika bila kushiriki
tendo la ndoa na Rama, hakuna mtu aliyemlaumu
mwenzie kwasababu tulishakubaliana kabla hivyo
Rama ilimbidi avumilie japo kuna muda nilikuwa
namuonea huruma kwasababu nilijua kabisa
namnyima haki yake ya msingi lakini nilimnyima ili
kuokoa maisha yake. Mwaka wa pili ulivyoanza
Rama aliamua kuniambia nimpeleke kwa wazazi
wangu ili akawaone na kujitambulisha kabisa,
Nilikuwa mbishi kumueleza Rama ukweli ila kuna
siku Rama alikasirika akaniambia mimi ni msaliti
ndio maana sitaki kumwambia ukweli kuhusu
sehemu ambayo wazazi wangu walikuwa wanaishi,
Yale maneno yaliniuma sana nikaanza kumueleza
Rama ukweli wa maisha yangu niliyopitia hadi nipo
mbele yake nikiwa mzima, Niliamua kuumwaga
ukweli wote kuanzia siku ambayo bibi alitaka
kunirishisha mikoba ya uchawi, Nikamueleza pia na
habari zote za mji wa laana pamoja na chapa
ambayo nilikuwa nimewekewa chini ya kitovu karibu
kabisa na sehemu zangu za siri, Niliamua kutoboa
siri ili kama kunifukuza basi anifukuze kuliko
kuendelea kuishi maisha ya kumdanganya kaka wa
watu. Nilivyomaliza kuongea Rama alikuwa mdomo
wazi alihisi ni kama nimemuelezea sinema. Rama
alipigwa na butwaa kutokana na habari
nilizomuelezea, Kitu kilichomgusa zaidi ni habari za
Mji wa laana, Rama hakuamini kama mji wa laana
ulikuwepo, Kwani aliingia chumbani kisha akatoka
na kitabu cha simulizi ambacho kilikuwa kina jina la
mji ambao nilikuwa nimemuelezea, Siwezi kumtaja
mwandishi wa kile kitabu kwasababu alikuwa
ameshafariki siku nyingi zilizopita, Na kifo chake
kilikuwa ni kifo cha utatanishi, Nilivyokiona kile
kitabu nilimwambia Rama akitupe haraka kwani
nilimkumbuka Steven ambaye alifariki miaka kadhaa
iliyopita nyuma, Chanzo cha kifo chake kilitokana na
kile kitabu kilichoandikwa KARIBU MJI WA LAANA.
Nilikuwa kama chizi kwani nilikuwa nampigia kelele
Rama akitupe kile kitabu, Rama alinituliza
akaniambia kuwa kile ni kitabu tu hakina maajabu
yoyote japo simulizi yake ni ya kutisha ambayo
ilimshinda kumaliza kuisoma. Rama hakujua
madhara ya kile kitabu kwani alikua ni kama
amefufua mashetani ambayo yalikuwa yametulia
kwa muda, Kile kitabu cha KARIBU MJI WA LAANA
kilikuwa ni kitabu cha ajabu chenye uhalisia wa
habari zilizokuwa zimeandikwa ndani yake, Matukio
ya kutisha na ukatili wa hali ya juu yaliibuka tena.
Oh Mola wangu naomba unitie nguvu kwa haya
ninayoenda kuyaelezea kwani nilipanga kuyasema ili
kuwafungua watu wote kabla sijawa marehemu.
 
ILIPOISHIA....
Kile kitabu cha KARIBU MJI WA LAANA kilikuwa ni
kitabu cha ajabu chenye uhalisia wa habari
zilizokuwa zimeandikwa ndani yake, Matukio ya
kutisha na ukatili wa hali ya juu yaliibuka tena. Oh
mola wangu naomba unitie nguvu kwa haya
ninayoenda kuyaelezea kwani nilipanga kuyasema ili
kuwafungua watu wote kabla sijawa marehemu.
SASA ENDELEA....
Rama alikuwa hanielewi kabisa kuhusu onyo ambalo
nilikuwa nimempa lililohusiana na kile kitabu
ambacho nilitokea kukiogopa sana, Rama
alinisogelea kwa karibu akanishika kwa nguvu huku
akiniongelesha maneno ambayo nilikuwa siyasikilizi
hata kidogo, Mawazo yangu mengi yalikuwa ni juu
ya kitabu ambacho kwa wakati huo Rama alikuwa
amekiweka pembeni, Rama alifanikiwa kunituliza
huku akiniaminisha kuwa kile kitabu hakikuwa na
kitu chochote cha ajabu, Alinishikisha hadi
mikononi, Niliogopa sana lakini nilijitahidi kukishika,
Hakuna chochote kilichotokea kwa muda ule hadi
nikawa nashangaa, Rama alinicheka sana akawa
ananiita mimi muoga, Nilijaribu kumsihi Rama
asichukulie mzaha kwani mambo ambayo nilikuwa
nimemueleza yalikuwa ni ya kweli kwa asilimia
zote. Ilibidi Rama akirudishe kile kitabu kwenye
kabati dogo ambalo ndio anapopenda kukihifadhi,
Siku iyo sikutaka kuwa mbali na Rama kwani kila
sehemu Rama alipokuwa anaenda nilikuwa nipo
nyuma yake, Ilifikia muda hata akiwa anaenda
chooni nilikuwa namsubili mlangoni, Nilifanya vile
kutokana na uoga niliokuwa nao. Rama alikuwa
ananishangaa sana kwa uoga ambao nilikuwa ninao
siku iyo lakini hakuonesha kuchukia, Pamoja na
Rama kutokuwa na hofu yoyote kuhusu kile kitabu
lakini zile habari nilizompa za mji wa laana
zilionekana kumuingia vilivyo kwani mara nyingi
alikuwa ananidadisi akitaka nisadiki kama zile
taarifa ni zakweli au nilikuwa nimebuni,
Nilimwambia Rama kuwa sikubuni wala kuongeza
chumvi hata moja kwenye maneno ambayo
nimemueleza, Rama aliwaza sana kwa kina kisha
akanipa chaguzi mbili akimaanisha nichague moja
wapo, Chaguzi ya kwanza ilikuwa inahusiana na
mambo ya kwenda kwa mashehe kuombewa ili
niondolewe kile kifungo cha kutokufanya mapenzi na
mwanaume, Chaguzi ya pili ambayo Rama alinipa
ilikuwa ni ya kwenda kwa mganga wa kienyeji.
Wazo la kwenda kwa mganga sikuliafiki hata
kidogo, Niliona mganga hana uwezo wa kutatua
tatizo ambalo ninalo, Niliamua kumwambia Rama
anipeleke kwa shehe ambaye anasifika kwa
utaalamu wa kutatua matatizo sugu yanayowatesa
watu, Rama alikuwa anahaha kumtafuta shehe
ambaye ni mtaalamu, Baada ya kuzunguka huku
akiulizia kila kona hatimaye alifanikiwa kuelezewa
habari za shehe jumbe.
****Shehe jumbe alikuwa ni shehe maalufu pale
Tanga hususani katika mtaa wa Utamuni uliokuwa
unapakana na mtaa wetu wa Donge, Shehe Jumbe
alikuwa ni mtaalamu wa kuondoa mizumu pamoja
na mashetani ambayo huwa yanawavaa watu. Rama
alivyoniambia habari za shehe Jumbe nilifurahi sana
nikaona kabisa naenda kutatuliwa matatizo yangu,
Tuliongozana wote kwa pamoja na Rama hadi
nyumbani kwa Shehe Jumbe ambaye alikuwa
anaishi peke yake, Shehe Jumbe alitupokea vizuri
akatupa dawa za kufukiza ndani kisha akatutajia
siku ambayo inabidi tumfate nyumbani kwake kwa
ajili ya kuondoa ile alama ya chapa ambayo alisema
ndiyo alama ambayo inawaua wanaume pindi
wanavyoshiriki mapenzi na mimi. Nilisubili kwa
hamu hadi siku ikawadia, Hatukuachana na Rama
kwani wote wawili tulirudi tena kwa Shehe Jumbe
tukiwa na hamu ya kufanikiwa kwa jambo ambalo
lilionekana kuwa kikwazo kizito upande wangu.
Nakumbuka ilikuwa ni siku ya Ijumaa, Siku ambayo
Rama hakwenda kazini kwa ajili yangu, Tulivyofika
mtaa wa Utamuni, tuliongoza moja kwa moja hadi
kwenye nyumba ya Shehe Jumbe. Tulibisha sana
hodi siku iyo bila Shehe Jumbe kutukaribisha ndani,
Tuliamua kukaa nje tukimsubili kwa muda wa
masaa mawili tukiamini huenda shehe Jumbe
ametoka kidogo, Masaa mawili yalipita bila shehe
Jumbe kuonekana, Nilianza kukasirika japo
sikuonesha usoni, Nilihisi kama vile shehe Jumbe
ametudharau kwasababu tulikuwa tumefika muda
muafaka ambao alituambia tufike lakini yeye
hakuonekana pale maeneo ya nyumbani kwake.
Nilisimama na kwenda kugonga mlango kwa mara
nyingine, Sijui nini kilinituma nifungue ule mlango
kwa sababu nilichokiona ndani kilinifanya nigande
kwa dakika moja huku nikitetemeka bila kuongea
hata neno moja, Sikuamini macho yangu kumuona
shehe ambaye alikuwa anasifika kwa sifa za kuzuia
mashetani akiwa amelala sakafuni huku damu
zikimtiririka maeneo ya puani na mdomoni, Shehe
jumbe alikuwa ametobolewa maeneo ya kifuani huku
akiwa kama amechomolewa moyo wake,
Nilishindwa kujizuia nikajikuta naanza kutapika kwa
wingi hali iliyomshtua Rama ambaye alikuja haraka
hadi pale mlangoni kunijulia hali, Rama alihisi
huenda nimeshikwa na tumbo la kuhara lakini
alivyoangalia chini ya sakafu alishtuka pia, Ikabidi
tuondoke kwa haraka lile eneo kwani ilishakuwa
hatarishi, Kifo cha Shehe Jumbe kilikuwa ni kifo cha
kushtajabisha, Kitu kilicho tushangaza ni jinsi
alivyokuwa ameuliwa kwa kutolewa moyo,
Hatukujua kabisa nani aliyefanya lile tukio. Tulirudi
hadi nyumbani wote wawili tukiwa tumejawa na
wasiwasi mwingi kwenye nafsi zetu. Usiku
haukulalika kabisa kila mtu alikuwa macho akijaribu
kumuomba mungu wake kwa jinsi awezavyo.
Sikumuongelesha Rama wala Rama
hakuniongelesha mimi, muda wote tulikuwa
tunaangaliana bila kuongea neno lolote, Wanaume
huwa wanasifika kwa ujasili lakini siku iyo Rama
alikuwa kama mwanamke kwani alikuwa akipitiwa
hata na mende mguuni anaruka kwa uoga, Matukio
ya usiku ule yalikuwa yanafurahisha lakini sikuwa
hata na hamu ya kucheka, Nakumbuka tuliogopa
kabisa kwenda hata chooni hivyo tulijisaidia haja
ndogo mule mule chumbani, Hakuna aliyemlaumu
mwenzie kwasababu tukio lililomtokea shehe jumbe
Lilikuwa limetutisha sana. Siku zilivyozidi kukatika
Rama akawa ameanza kunitilia mashaka kwani
alikuwa ameshanichoka na hakutaka kabisa kuishi
na mimi tena lakini alikuwa anashindwa anifukuze
vipi, Niliweza kuligundua hilo kwasababu ule ukaribu
wake na mimi ulipungua akawa hanijali tena,
Tukawa tunaishi kwenye nyumba moja kama
wapangaji wawili tusiofahamiana, Lile jambo
liliniumiza lakini ilinibidi nivumilie kwasababu
maisha yangu kwa muda ule yalikuwa
yanamtegemea Rama. Siwezi kumtupia Rama
lawama nyingi kwasababu kwa upande wake alihisi
alikuwa yupo sahihi lakini kitu Rama alichokuwa
amekosea ni kile kitendo cha kutaka kuniua akihisi
mimi ndiye mshirikina ndani ya nyumba yake.
Baada ya kununiana kwa miezi kadhaa ndani ya
nyumba, Rama aliamua kurudisha ukaribu upya,
Ukaribu ambao ulikuwa ni wa kukatisha maisha
yangu, Nakumbuka nikiwa natoka kuoga Rama
alikuwa chumbani akiwa amekaa kwenye kitanda
huku akitabasamu kwa furaha, Nilifurahi sana
kumuona Rama kwenye hali ile, Niliamua kugeuka
kwenye kioo kikubwa na kumpa Rama mgongo ili
nijipake mafuta, Kile kioo siwezi kukisahau hata
kidogo kwani ndio kilikuwa mkombozi wangu,
Huenda bila kile kioo basi leo hii nisingepata pumzi
ya kuyasimulia haya, Kupitia kile kioo niliweza
kumuona Rama akiwa ameshikilia kisu akiwa
anakuja kwa kasi ili anichome nacho, Nilijikuta
nampisha kwa nguvu hali iliyosababisha Rama
akivamie kile kioo na kujikwaruza, Kwakuwa
nilikuwa napigania roho yangu sikuangalia kama
Rama alikuwa ni mpenzi wangu wala nini, Kwa
haraka nilichomoa kipande cha nondo kilichokuwa
kimening'inia nikampiga nacho Rama kwa nguvu
kichwani, Nilimpiga sana kama vile ninaua mdudu
hatarishi, Sijui ujasiri ule niliutoa wapi kwani
nilimponda Rama kichwani na ile nondo hadi
kichwa chake kikawa kinavuja damu kwa wingi,
Nilikuwa nimeua kwasababu Rama hakutingishika
tena, Niliyaogopa yale mauaji japo niliyatekeleza
mwenyewe, Nikiwa najiandaa kukimbia nilishangaa
kumuona mtu akiwa kafanana na Rama amesimama
mlangoni huku akicheka sana. Ilikuwa ni kama
mauza uza maana Rama mmoja alikuwa yupo chini
amefariki tayari lakini Rama mwingine alikuwa
amesimama mlangoni huku akicheka sana tena
akiwa hana hata jeraha mwilini.
 
ILIPOISHIA....
Niliyaogopa yale mauaji japo niliyatekeleza
mwenyewe, Nikiwa najiandaa kukimbia nilishangaa
kumuona mtu akiwa kafanana na Rama amesimama
mlangoni huku akicheka sana. Ilikuwa ni kama
mauza uza maana Rama mmoja alikuwa yupo chini
amefariki tayari lakini Rama mwingine alikuwa
amesimama mlangoni huku akicheka sana tena
akiwa hana hata jeraha mwilini.
SASA ENDELEA....Nikiwa sielewi kitu gani nifanye,
Yule Rama aliyekuwa amesimama mlangoni
aliendelea kucheka huku akiisogelea maiti yake
mwenyewe ambayo ilionekana imelala chini,
Alivyoisogelea ile maiti yake pale chini aliiangalia
kwa muda kiasi kisha akachovya damu yake kidogo
akailamba mdomoni mwake, Mwili wangu ulikuwa
umepigwa na ganzi mithili ya kitu kilichogandishwa
na barafu hivyo nilibakia nikiangalia tu lile jambo
lilivyokuwa linaendelea. Baada ya muda yule mtu
aliyefanana kabisa na Rama alibadilika sura yake
akawa kwenye sura ya mtu mwingine, Tena safari
hii alikuwa ametokea kwenye sura ya mtu ambaye
sikuwahi kumuona kabla, alikuwa amejivalia vazi
jekundu mwili mzima, Nilivyo yaangalia yale mavazi
yake hayakutofautiana na mavazi ambayo walikuwa
wanapendelea kuvaa wale watu waliokuwa wanaishi
kwenye ule mji wa laana ambao nilishawahi kuishi
kipindi cha nyuma, Yule mtu alinisogelea kwa karibu
huku akiwa makini sana akawa ananiongelesha
lugha ambayo sikuweza kuielewa kabisa, Baada ya
muda mfupi kupita ile maiti halisi ya Rama ambaye
nilikuwa nimemuua mimi kwa kumpiga na nondo
kichwani ilibadilika na kuwa mchanga mweupe
uliofanana kabisa na mchanga wa fukwe za bahari,
Nilishindwa kuelewa kabisa kwa nini ile maiti
ilibadilika na kuwa mchanga, Nikiwa nashangaa
nisijue nini lakufanya yule mtu alinishika mkono
wangu wa kushoto akawa ananivuta ili nimfate
sehemu anayoenda, Niliamua kumfata japo sikujua
kama ile ilikuwa ni akili yangu au alikuwa
amenibadilisha, Nilimfata nyuma nyuma hadi
tukafika ndani ya choo cha ile nyumba ambayo
nilikuwa ninaishi na Rama kabla hajawa marehemu,
Kumbuka muda huo sikuwa na nguo hata moja
mwilini kwani yale matukio yalikuwa yamenitokea
kipindi kile nimetoka kuoga, Tulivyokuwa kule
chooni yule mtu alianza kunipaka unga mweupe
mwilini mwangu nikawa nafanana na misukule,
Baada ya kumaliza kunipaka ule unga tulikaa ndani
ya kile choo kwa muda mrefu hadi ilipofika usiku,
Nikiwa vile vile uchi wa mnyama yule mtu alinivuta
mkono tukawa tunatoka ndani ya ile nyumba ya
marehemu Rama, Yule mtu alikuwa ni kama
anaiendesha akili yangu kwasababu muda wote
nilikuwa ninafata mambo ambayo ananieleza.
Sikujali kama nilikuwa uchi wala nini mimi nilikuwa
ninafata maelezo ambayo alikuwa ananipatia, Yule
mtu alikuwa ananitembeza mtaani nikiwa uchi lakini
hakuna mtu aliyekuwa anatuona japo sisi tulikuwa
tunawaona, Iyo ilijidhihirisha kwasababu muda
mwingi watu ambao tulikuwa tunapishana nao
karibu walikuwa bize na mambo yao bila
kutuongelesha wala kututilia mashaka. Nilimfata
yule mtu nyuma yake hadi tulipofika maeneo ya
makaburini, Muda huo ilikuwa ni usiku sana kwani
giza lilikuwa limetanda kila mahala, Tulivyofika
makaburini yule mtu alinilaza juu ya kaburi moja
ambalo lilioneka kuwa chakavu, Na mimi bila ubishi
nilijilaza huku nimenyoosha miguu yangu nikiwa
naangalia kwa juu, Baada ya kunilaza juu ya lile
kaburi yule mtu alinisogelea kwa juu na kuanza
kuning'ata ziwa langu la kushoto, Nilikuwa nahisi
maumivu makali lakini sikuweza kumzuia
kwasababu akili yangu alikuwa anaiendesha yule
mtu, Ziwa langu la kushoto lilitafunwa hadi likabakia
kipisi, damu nyingi zilikuwa zinanivuja upande wa
ziwa langu ambalo lilikuwa limeng'atwa, Maumivu
ambayo nilikuwa ninayahisi yalikuwa hayaelezeki
hata kidogo kwani yalikuwa ni makali sana. Baada
ya kunifanyia vile yule mtu aliinuka juu yangu
akachukua unga wake mweupe kisha akanipaka
kwenye lile ziwa ambalo alikuwa amelitafuna,
Maumivu yaliniisha haraka sana, Nikawa sihisi tena
maumivu hata nilivyojishika kwenye lile ziwa langu
la kushoto nilishangaa kuona limerudi kwenye hali
yake ya kawaida kwani halikuonekana tena kuwa na
jeraha lolote. Yule mtu alininyanyua kutoka juu ya
lile kaburi ambalo alikuwa amenilaza kisha
akanipiga kofi dogo maeneo ya usoni, Baada ya
kupigwa lile kofi nilitapika nyama ambazo zilikuwa
mbichi kisha nikarudiwa na akili zangu za kawaida.
Nilishtuka nikataka kukimbia lakini yule mtu
aliyekuwa amevalia mavazi mekundu alinishika
mkono kwa nguvu akaniambia nitulie kwasababu
kuna mengi anataka anieleze, Kwa uoga ulioniingia
nilitaka kumchomoka ili nimkimbie lakini yule mtu
alinipiga kofi lingine kwenye makalio yangu hali
iliyofanya ninyong'onyee mwili mzima na kuanguka
chini, Nilihisi kichwa kikiniuma sana. Sifahamu ni
kitu gani kiliendelea kwakuwa fahamu zangu
zilikuwa zimekata lakini asubuhi kulivyokucha
nilijikuta nipo ndani ya chumba ambacho kilikuwa
kinavutia, Kile chumba kilikuwa kina runinga ya
kisasa pamoja na vitu vingine vya thamani,
Nilipoangalia pembeni ya kitanda ambacho nilikuwa
nimelala nilishangaa kumuona yule mtu ambaye
alikuwa amenipeleka makaburini usiku wa jana yake,
Yule mtu alikuwa makini akiniangalia usoni huku
akiwa anataka kuniambia jambo fulani, Siku iyo
hakuwa na yale mavazi mekundu bali alikuwa
amevaa suti yake vizuri. Yule mtu aliniambia
nisiogope ila nitege masikio yangu vizuri
kumsikiliza mambo ambayo anataka kunieleza. Yule
mtu ambaye alikuwa ni mwanaume wa makamo
alijielezea kwa majina anaitwa Leandro luciker ni
mmoja wa wafuasi wa shetani ambaye ametumwa
kutoka katika mji wa laana kuja kunipatia majukumu
ambayo ninatakiwa niyatekeleze, Aliniambia ya
kwamba kwasababu nilikuwa nimekwepa kutolewa
kafara ili watu wengine ndani ya mji wa laana waishi
basi mtawala wa ule mji aliamua kuniambia
ninatakiwa nimtumikie kwa kufata masharti ambayo
anayataka, Masharti yenyewe yalikuwa ni magumu
sana kwani Leandro luciker aliniambia inabidi
maisha yangu niwe naishi kwa kuua ili watu waishio
ndani ya mji wa laana waweze kuishi kwa kunywa
damu za watu ambao nitakuwa ninawauwa.
Nilijifikilia sana mwisho wa siku niliamua
kukubaliana na mawazo ya Leandro ila nilimuuliza
kwanini maisha yangu yamekuwa na misukosuko
kiasi kile, Leandro aliniambia kuwa bibi yangu
alikuwa ni mmoja wa washirika wazuri wa mji wa
laana lakini kitendo chake cha kushindwa
kunishawishi vizuri nirithi mikoba yake ya uchwawi
ndio kilisababisha niingie kwenye misukosuko yote
ile ambayo imenitokea. Leandro aliniambia ilikuwa
ni misukosuko ambayo nilikuwa nimepewa
makusudi ili kunikomaza kiakili na kinafsi. Na kweli
kama kuua nilikuwa nimeshaua watu kadhaa hivyo
damu za watu hazikuonekana kitu cha ajabu
kwangu. Kwa mara ya kwanza nikajikuta nakubali
kuwa mfuasi wa shetani. Sijui Leandro alinifanyia
kitu gani kwenye akili yangu kwani nilikuwa ni
mwanamke muuaji tena niliyekuwa sina huruma hata
kidogo. Tuliagana na Leandro ambaye alipotea
kama upepo ndani ya kile chumba na kuniacha
mwenyewe. Nilianza zoezi la kutafuta watu wa
kuwaua ili ninywe japo damu kwasababu
nakumbuka nilikuwa nina hamu sana ya kula nyama
za watu pamoja na damu. Niliona njia pekee ya
kupata watu ni kujifanya kahaba kisha nikaenda
meneo maarufu ya kujiuza. Kupitia ile biashara ya
kujiuza niliwaua wanaume wengi sana ambao kwa
idadi siwezi kuwakumbuka. Sikupenda kuelezea
jinsi nilivyokuwa nawaua wale wanaume ambao
walikuwa wananinunua ili wakanitumie kingono
lakini ninaona ni vyema niwaeleze ili kuwakomboa
kaka zetu na baba zetu ambao wanaendelea na
tabia ya kununua makahaba ambao wanajipanga
barabarani usiku wa manane.
 
ILIPOISHIA....
Kupitia ile biashara ya kujiuza niliwaua wanaume
wengi sana ambao kwa idadi siwezi kuwakumbuka.
Sikupenda kueleza jinsi nilivyokuwa nawaua wale
wanaume ambao walikuwa wananinunua ili
wakanitumie kingono lakini ninaona ni vyema
niwaeleze ili kuwakomboa kaka zetu au baba zetu
ambao wanaendelea na tabia ya kununua makahaba
ambao wanajipanga barabarani usiku wa manane.
SASA ENDELEA...Mkoa wa Tanga ulikuwa ni moja
kati ya mikoa ambayo watu wake wanapenda
starehe sana. Wakazi wengi wa mkoa ule wa Tanga
walionekana kuwa na rafudhi kama ya kipemba,
Hata muonekano wao pia haukutofautiana sana na
watu waliokuwa wanatokea pemba, Sikuwa nikifanya
kazi yoyote ndani ya Tanga lakini Leandro luciker
alikuwa akinitokea kimiujiza na kunikabidhi pesa
nyingi sana ambazo nilizitumia kukodi nyumba moja
kubwa ambayo nilikuwa ninaishi peke yangu.
Nakumbuka mara nyingi Leandro alikuwa akinitokea
usiku wa saa saba huku akinisisitizia kuwa inabidi
nianze kazi rasmi ya kumwaga damu, Nilimkubalia
nikamuahidi asiwe na wasiwasi kwani siku siyo
nyingi nitaingia viwanja vya starehe ili nikawapate
wanaume walio walafi wa wanawake. Kwakuwa
Mkoa wa Tanga ulikuwa ni maarufu kwa miziki ya
baikoko basi niliamua na mimi kujichanganya
kwenye ile miziki nikiwa nimevalia mavazi ambayo
yalionesha nusu ya mwili wangu wazi, Ile baikoko
ilikuwa inafanyika maeneo ya Mianzini, Hilo eneo
lilikuwa ni eneo maarufu kwa starehe ndani ya Mkoa
wa Tanga, Ule mziki wa baikoko ulianza mida ya
saa moja usiku, Watu wengi sana walikusanyika
eneo lile wakiwa na lengo lakupata burudani kutoka
kwa wadada ambao walikuwa na kazi ya kukatika
huku kanga zao walizovaa zikiwa zimelowanishwa
kwa maji, Ilikuwa ni zaidi ya laana, Usikubali hata
siku moja mtoto wako wa kike au wa kiume akuage
kwenda kwenye miziki ya baikoko kwani atajifunza
tabia nyingi chafu ambazo zitamuharibia taswira
yake yote ya maisha, Wale wadada waliokuwa
wanacheza walifikia hadi hatua ya kukatikia chupa
za bia huku wakiwa wamelowana chapa chapa mwili
mzima, Mimi sikuonekana kuwajali sana kwani
niliamua kutafuta eneo ambalo walikuwa wanauza
vinywaji nikanunua bia kadhaa na kuanza kunywa
peke yangu, Baada ya muda mfupi kuna kijana wa
kiume alikuwa amekuja pembeni ya sehemu
ambayo nilikuwa nimekaa akaagiza na yeye kinywaji
chake, Kwakuwa ilikuwa ni sehemu kubwa kiasi basi
kila mmoja wetu alipata nafasi ya kuagiza kinywaji
chake akipendacho akakiweka kwenye meza na
kuanza kunywa, Akili yangu ilikuwa inajua kabisa
kuwa yule kijana ndio atakuwa mtu wa kwanza wa
kufungulia ukurasa wa mauaji kwenye orodha mpya
ambayo nimeiandaa lakini kitu cha kushangaza yule
kijana hakuniongelesha hata neno moja kwani muda
mwingi alikuwa bize akinywa kinywaji chake cha
aina ya safari lager, Zilipita dakika kama kumi bila
kuongeleshana na yule kijana nikaamua kuanza
kumtega kwa kupandisha kimini changu juu hadi
nguo ya ndani ikawa inaonekana lakini yule kijana
hakuonekana kabisa kupagawa na mimi hadi
ikafikia hatua nikahisi huenda yule kijana ni hanisi,
Baada ya muda yule kijana alimaliza kunywa bia
yake akainuka na kuondoka zake, Moyoni niliumia
sana kuona nimempoteza mtu wa kwanza kumuua
lakini nilihisi ile haikuwa bahati yangu hivyo
niliamua kuendelea kutega lile eneo ili wanaume
wengine wanase, Na kweli haikuchukua muda
akatokea baba wa makamo ambaye alikuja kwa
mbwembwe nyingi sana lile eneo ambalo nilikuwa
nimekaa, Yule baba alikuwa hana haya hata kidogo
kwani pamoja na umri wetu kuwa umetofautiana
sana lakini aliamua kujichetua akili huku akiongea
ovyo kutoka a na bia ambazo alikuwa amekunywa,
Kitu cha kwanza alichonifanyia baada ya kufika lile
eneo ni kunishika makalio huku akimuagiza waita
aongeze bia, Kimoyo moyo nilifurahi kuona
nimempata mtu wa kwenda kumuua, Tuliongea
maongezi mengi sana na yule baba kisha tukawa
tumekubaliana tukalale wote hadi asubuhi,
Tulipanda kwenye bajaji hadi maeneo ya Mwembe,
Hayo maeneo ndiyo ambayo nilikuwa nimekodi
nyumba kubwa, Yule baba hakunitilia mashaka hata
kidogo ila muda mwingi alionekana kuwa na papara
za kutaka kufanya mapenzi kwani tulivyofika
sebuleni alinisukumiza kwenye kochi kubwa akiwa
anataka kufanya kile kitendo cha ngono pale pale
sebuleni, Niliamua kumtuliza mzuka nikamshawishi
hadi tukaingia chumbani, Kabla ya yote nilijifanya
kumwabia avae kinga kisha anipatie laki moja kama
pesa ya kulala na mimi usiku mzima, Yule baba
alionekana kuwa mtu mzito serikalini kwani
alinipatia laki moja haraka bila kuchelewesha muda,
Kuona haitoshi aliamua kuniongeza kiasi cha shilingi
laki mbili akimaanisha alikuwa anataka nimpatie
hadi kinyume na maumbile kwasababu ndani ya
mkoa wa Tanga ulikuwa ni mchezo ambao
umezoeleka kwa wanawake kufanya hivyo vitendo
hususani wanawake wanaojiuza. Masikini yule baba
wa watu tamaa zake za ngono zilimponza kwani
kitendo cha kuniingilia tu kilisababisha aanze
kukohoa kama vile amekabwa na kitu, Hakuchukua
muda akaanza kutokwa na damu sehemu zake zote
ambazo zilikuwa wazi, kwa jinsi alivyokuwa
ungeweza kuzani alikuwa anaumwa ebola lakini
haikuwa hivyo, Yule baba aliweweseka kwenye kifua
changu hadi akatulia kimya, Niliinuka nikiwa
nimelowana damu ambazo zilitoka kwenye mwili wa
yule baba kisha nikachukua kisu kikali na kukata
baadhi ya viungo vyake ambavyo niliambiwa na
Leandro luciker nivihifadhi kwenye chumba
kimojawapo ambacho nitakichagua, Nakumbuka
viungo ambavyo nilimkata yule baba vilikuwa ni
kichwa chake pamoja na uume wake, Kichwa
nilienda kukihifadhi kwenye chumba nilichokiteua
kisha uume wa yule baba niliula ukiwa mbichi
kabisa, Nilikuwa ni muuaji ambaye ulikuwa hauwezi
kunizania hata kidogo, Kwa kifupi nilikuwa mfuasi
wa shetani ambaye nilikuwa ninaongozwa na
Leandro luciker, Baada ya kufanya yale mauaji
nilichukua unga mweupe nikakinyunyuzia kiwili wili
cha yule baba kikapotea ndani ya ile nyumba,
Chumba kilirudi kwenye hali ya usafi wa hali ya juu
kana kwamba hakukuwa na mauaji yaliyotendeka.
Niliendelea na ule mchezo wa kujiuza ili niwapate
wanaume wengi, Kwakiasi kikubwa nilifanikiwa
kwani idadi ya vichwa vya watu nilivyovifungia ndani
ya kile chumba changu maalumu ilikuwa kubwa
sana, Hao wanaume niliowaua hakuna hata
mwanume mmoja niliyemuonea huruma pindi
alipokuwa anakata roho, sana sana nilifurahia vifo
vyao. Baada ya kufanya mauaji ya wanaume kwa
muda mrefu hatimaye Leandro luciker alinitokea
tena akaniambia ya kwamba nisitishe zoezi la kuua
wanaume kwani idadi yao iliyokuwa inatakiwa ndani
ya mji wa laana imetosha, Leandro luciker
aliniambia ni muda muafaka wa kugeukia
mahospitalini hasahasa kwenye wodi za wamama
wajawazito. Inaniuma sana jamani, Nayaelesa haya
huku machozi yakinitililika hasa hasa nikizikumbuka
sauti za vitoto vichanga zikinililia, Naomba ewe
mwanamke mwenzangu usinichukie mimi halima
kutokana na mambo ambayo niliyafanya, kama
ulikuwa ni mjamzito na mimba yako ikaharibika basi
tambua kwa kiasi kikubwa mimi halima ndiye
niliyeweza kuwa kikwazo kikubwa kwenye ujauzito
wako. Nilifanya mauaji makubwa sana kwenye
hospitali mbali mbali ndani ya mkoa wa Tanga.
Sitakuficha hata kitu kimoja nitakueleza kila kitu
nikichokifanya kwenye mahospitali.
 
ILIPOISHIA....
Nina yaeleza haya huku machozi yakinitililika hasa
hasa nikizikumbuka sauti za vitoto vichanga
zikinililia, Naomba ewe mwanamke mwenzangu
usinichukie mimi halima kutokana na mambo
ambayo niliyafanya, kama ulikuwa ni mjamzito na
mimba yako ikaharibika basi tambua kwa kiasi
kikubwa mimi halima ndiye niliyeweza kuwa
kikwazo kikubwa kwenye ujauzito wako. Nilifanya
mauaji makubwa sana kwenye hospitali mbali mbali
ndani ya mkoa wa Tanga. Sitakuficha hata kitu
kimoja nitakueleza kila kitu nilichokifanya kwenye
mahospitali.
SASA ENDELEA....
Nilihuzuria wodi nyingi za wamama wajawazito kwa
siri sana bila kuonekana, Kitu kilichofanya
nisionekane ni dawa ambazo nilikuwa ninazipaka
mwilini mwangu kwaiyo nilikuwa ninapita kwenye
wodi mbali mbali nikiwa sina wasi wasi wowote.
Mauaji yangu ya kwanza kabisa yalikuwa ni ya
mama mmoja na mtoto wake mchanga ambaye
hakufanikiwa hata kidogo kuufaidi mwanga wa jua.
Siku iyo niliingia kwenye moja ya hospitali ambayo
ilikuwa haipo mbali sana kutoka ile sehemu ya
Mwembe ambayo nilikuwa ninaishi, Niliingia
kiuchawi ndani ya ile Hospitali mida ya usiku
mnene, Nilivyofanikiwa kuingia ndani nilienda moja
kwa moja kwenye wodi maalumu ya kulazwa
wamama wajawazito ambao siku zao za kujifungua
zilikuwa zinakaribia, Siwezi kutaja jina la ile hospitali
kutokana na sababu za kiusalama lakini kitu
ninachoweza kukuelezea ni matukio ambayo
niliyatenda kwa usiku ule, Nilivyokuwa ndani ya ile
wodi ya wajawazito niliona wamama kadhaa wakiwa
wamelazwa kwenye vitanda tofauti tofauti,
Nilitembea kwenye kila kitanda kilichopo ndani ya
ile wodi bila kuonekana nikiwa naangalia mjamzito
wa kuanza naye. Baada ya kuzunguka kwa muda
nilifika kwenye kitanda ambacho alikuwa amelala
mama mmoja ambaye alionekana kuchoka sana
kutokana na mimba ambayo ilikuwa inamsumbua,
Nilivutiwa sana na yule mama kwasababu ya tumbo
lake ambalo lilikuwa limetuna sana. Niliamua
kuchukua vifaa vya upasuaji ambavyo nilikuwa
nimevihifadhi kwenye begi la mgongoni kisha
nikawa tayari kuanza kazi ya kumpasua tumbo yule
mama ili nichukue kichanga alichokuwa amekibeba
tumboni, Kabla sijafanya tukio lolote yule mama
alianza kujigeuza huku akipiga makelele kiasi ya
kuomba msaada, Zile kelele hazikuhusiana na mimi
kwasababu hakuwa ameniona bali zilikuwa ni kelele
za kulalamikia tumbo lake, Haikupita muda daktari
wa zamu aliingia ndani ya ile wodi kwa ajili ya
kumsaidia yule mama, Muda huo mimi nilikuwa
nimesimama pembeni ya kile kitanda cha wagonjwa
bila kuonwa na mtu yoyote, Baada ya yule mama
kupewa huduma aliacha kupiga kelele akawa
ametulia bila tatizo lolote, Yule daktari alivyoondoka
nilichukua kitu kilichofanana na udi kisha
nikakichoma moto, Kile kitu kilitoa moshi
mwekundu ambao ulienea kwenye ile wodi nzima,
baada ya muda wajawazito wote wakawa
wamepitiwa na usingizi mkali, Niliona ndio muda
muafaka wa kuanza kazi yangu kwani nilichukua
kifaa aina ya mkasi na kisu chembamba nikaanza
kulichana tumbo la yule mama kwa umakini ili nitoe
kichanga, Nilifanikiwa kuchana kabisa tumbo la yule
mama hadi utumbo ukawa umemwagika kwa
pembeni, Nilivuta kile kichanga ambacho kilikuwa
kimebakiza miezi kadhaa kizaliwe nikakiweka
kwenye begi langu kikiwa tayari kimeshafariki,
Mikono yangu ililowa damu nyingi sana lakini
sikuonekana kuhofia kitu chochote, Baada ya
kufanya lile tukio nilipotea kiuchawi ndani ya ile
hospitali nikarudi nyumbani kwangu nikiwa tayari
nimeshaiba kichanga kimoja, Usiku ule ule
sikupoteza muda nilichukua kinu changu kidogo
nikakiweka kile kichanga kisha nikaanza kukitwanga
kama vile natwanga mboga ya kisamvu, Nilitwanga
sana hadi nyama za yule kichanga zikalainika sana
mithili ya nyama za ng'ombe, Nilivyomaliza kufanya
ule ukatili nilichukua sufuria nikaiweka ile nyama
kisha nikaifunika, Ilikuwa imetimia saa nane usiku
giza likiwa bado kali, Leandro luciker alinitokea tena
akachukua lile sufuria ambalo niliweka nyama za
kile kichanga kisha akapotea nalo, Siku hiyo
Leandro luciker alinipongeza sana kwa kazi mzuri
ambayo nilikuwa nimeifanya. Siku ambayo ilifata
nilihamia hospitali nyingine ambayo nilifanikiwa
kuiba watoto wachanga wapatao kumi ambao
walikuwa wamezaliwa siku iyo, Wale watoto
niliwaiba kiuchawi kwani nilivizia mama zao
walipojifungua nikawachukua haraka na kuwaachia
mama zao mizoga ya watoto wa mbwa ambao kwa
macho yao ya kawaida wao waliona ni watoto wao
wamefariki, Kama kawaida vile vitoto vichanga
vikiwa hai niliviweka kwenye kinu tayari kwa
kuvitwanga, Siku iyo nilichukua kinu kikubwa nikawa
nawatwanga watatu watatu, Nilitwanga bila huruma
hata kidogo nikafanikiwa kujaza nyama zao kwenye
sufuria lililokuwa kubwa, Leandro luciker bila
kuchelewa alinitokea mida ile ile akabeba lile
sufuria kwa ajili ya kuondoka zake, Mara nyingi
alikuwa ananiaga na kuniambia anapeleka zile
nyama kwenye ule mji wa laana, Niliamua kumuuliza
wanaenda kuzifanyia nini lakini Leandro luciker
alicheka kidogo akachota baadhi ya nyama zilizopo
kwenye lile sufuria akazila kisha akaniambia
wanaenda kuziweka kwenye makopo maalumu
kisha wanazipeleka kwenye masuparmarket
makubwa ambayo yanauza nyama za makopo ili
wapate wafuasi wengi kwani yoyote ambaye anakula
zile nyama basi anakuwa ni mmoja wa wafuasi wa
mji wa laana. Mpenzi msomaji wa huu ushuhuda
ninaokupa ningependa unisikilize kwa makini
kwakuwa mimi niliyapitia hayo yote, Usipendelee
kula nyama ambazo zinahifadhiwa kwenye makopo
kwasababu nyama nyingi huwa ni za binadamu
wenzetu, Si maanishi usile nyama lakini pindi
unapokula jaribu kuwa makini sana kwasababu
mimi nilikuwa ni mmoja wa watu ambao tulihusika
kwa kiasi kikubwa kuwalisha watu wengi nyama za
vitoto vichanga. Matukio ya mimba kuharibika na
vifo vya watoto wachanga yalikuwa ni mengi sana,
Kila mtu mtaani alikuwa anaongea kuhusu la kwake,
Mimi pia nilikuwa najifanya kusikitika kuhusiana na
yale matukio wakati mimi ndiye nilikuwa
mtekelezaji wa ule unyama. Kama unavyojua hakuna
sehemu ambapo majirani wanakosekana kwani hata
lile eneo ambalo nilikuwa nimekodi nyumba
kulikuwa kuna majirani ambao nilikuwa nimepakana
nao, Nilizoeana na majirani wachache hususani
dada mmoja ambaye alikuwa anaitwa Tina lymo.
Tina lymo alikuwa anamiliki saluni ndogo ya kike
ambayo ilikuwa inamuingizia kipato chake cha
halali, Kwakweli Tina alikuwa ni mwanamke
mchakalikaji ambaye alitokea kunizoea sana,
Pamoja na yale mazoea ya Tina lakini sikumruhusu
kabisa kuingia kwenye kile chumba ambacho
nilikuwa nimehifadhi vichwa vya wanaume wengi
ambao nilikuwa nimewaua, Baadhi ya vichwa
vilikuwa vimeisha nyama na kubakia mafuvu. Tina
hakujua kabisa kuwa mimi nilikuwa ni mfuasi wa
shetani laiti angenigundua basi asingedhubutu
kujenga ukaribu na mimi, Sikutaka mtu hata mmoja
ajue siri zangu hivyo nilipanga kumuua mtu yoyote
ambaye atagundua siri zangu. Wahenga huwaga
wanasema ukizoeana sana na mbwa iko siku
atakufata hadi msikitini, Hii kauli iliweza
kujidhihilisha kutoka kwa Tina ambaye alikuja
kuniletea seke seke kubwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom