Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Ahsante sana kwa maoni na mtazamo wako, wazo la kutoa movie hata baadhi ya member wengine wameshauri hivyo.

Ila si jambo jepesi, gharama zake ni kubwa hasa kama unataka tamthilia ifike kwa walaji ikiwa na viwango vya 2022, kama stori ilivyo Kunatakiwa Shots na scenes zote ziwe kali, kwa mfano boss awe boss kweli kweli, magari makali, vituo vya polisi kama ni police post iwe hivyo kama ni central, iwe hivyo, lakini pia wahusika nao ni wengi sana,

Yaani movement zote, from 2011 to 2013 ,huku locations zisiwe za kujibana , kumbuka Kuna riwaya na visa vipo humu jamiiforums ni Kali na zenye kuvutia, lakini baada ya wahusika kutoa movie au tamthilia hazikuwa na mvuto kama ilivyo simulizi.

Nikiri wazi hapa Tanzania,kunako bongo movie Kuna vipaji haswa, vya watunzi na waandishi lakini kazi zao Mara nyingi zinakosa .bajeti, bajeti, bajeti,.

Waigizaji mahiri,
Locations nzuri,

Mfano Mimi na madam tulikuwa tunakutana kwenye migahawa tofauti tofauti hivyo inatakiwa hata kwenye tamthilia iwe hivyo hivyo jambo ambalo kivitendo ni ngumu.

Hii inataka mzigo wa kutosha kuiandaa.

Yote kwa yote niwape pongezi wanaoguswa Kila mtu kwa namna yake , tuenjoy simulizi maana ipo hatua za mwisho

Uzuri simulizi inajisimulia yenyewe kwenye vitu vilivyonitokea, nipo tayari kujibu maswali yenu.
kwenye hii movie mimi ntakua esta
 
  • Thanks
Reactions: ADK
Mimi ntakuwa yule boss aliye kutana na jamaa kimasihala
 
SEHEMU YA MWISHO......(FINAL)

Kwa wenye kuamini Dini na madhehebu yao, au hata wanaoamini sehemu wanazozijua, wote kwa pamoja tuweke IMANI kwa MUNGU mmoja maana yupo na anatenda.

Maisha yaliendelea, familia zilifurahi huku Kila kitu kikiwa kwenye mpango sahihi kabisa

Mume wangu, unajua kama tarehe 17 mwezi huu, ndiyo siku yako muhimu wewe kuripoti kazini?
(akimaanisha tarehe 17 ya mwezi wa kwanza mwaka 2013).

Usijali mke wangu, najua sana, najua hilo, ila bado wiki nzima ujue. nilimjibu.

Sawa, ningekuwa na uwezo ningekufungia ndani usitoke kabisa, maana najua huko kuzurura kwako unaweza kuyazua huko ukaja kukatisha ndoto zako, nimechoka masuala yasiyokuwa na maana.
alilalamika.

(Nikicheka)
Ajali haina kinga mke wangu, hata nikikaa hapahapa lolote linaweza kutokea bado nikakatisha ndoto zangu, kikubwa ni kumuomba MUNGU ili atufatufanyie wepesi na kunyoosha mapito yetu. Nilimjibu.

Amina, basi piga magoti nikuombee maana hiyo kazi ni ya muhimu kwangu kuliko hata wewe,. aliniomba nifanye hivyo.

Kwa kumridhisha kutokana na Imani yake niliweza kufanya hivyo ili tu nisilete mgongano Kati yetu.
Baada ya kumaliza yale maombi mafupi , nilimpigia Rose ili tukutane maana alikuwa ananyanyasa sana moyo wangu.

Ndugu msomaji, kazi niliyopata kwa sasa hakujua mtu yeyote zaidi ya mke wangu na Rose.
Rose anajua kwakuwa ni mmoja wa wahusika walionipigania kule, ila yeye hakuwa na Imani juu ya Mimi kufanya kazi pale, maana Mara nyingi alikuwa akiniuliza akitaka kuhakikisha, kama taratibu zimekamilika.

Na Mimi sikutaka kumwambia na kutapika yote, kuhusu ile kazi kwani, licha ya kuwa nilishakamilisha vitu vingi lakini bado niliamini kwa asilimia tisini tu, hivyo kumwambia mtu na kujimaliza Kisha mpango wako ukakwama, sijui utaeleza nini.

Lakini nilichogundua ni kwamba penzi letu na Rose, Lilianza kufifia yaani lile penzi moto moto sikuliona tena yote haya yalisababishwa na Mimi kutokuwa na uhakika na kazi.

Nakumbuka tulikutana kwenye mgahawa mmoja Mimi na yeye nikaagiza Chakula ili wakati maongezi yakiendelea tupate kuburudika naye.

Hivi my, kwanini unapenda kuharibu pesa hivyo, Mimi naona Bora hata uagize soft drinks tu inatosha, hakuna haja ya sisi kutumia gharama kubwa, alisema huku akimaanisha.

Nilimtazama nikimshangaa maana hawezi sema yale na hajawahi kusema jambo lile, hela hatoi mfukoni mwake kwanini zimuume?

Kwani baby Kuna tatizo, sioni kama ni vitu vya gharama kiasi hicho. niliuliza.

Ujue lazima tu nikwambie ukweli, Daniel (akinitaja kwa jina mithili ya shambaboy)
Wewe huna uhakika wa kazi, na kama ujuavyo hii ni January huwa Kuna ugumu fulani ambao unasumbua hivyo kuheshimu pesa ni suala muhimu sana,. aliweka kituo.

Kwanini unasema sina uhakika wa kazi, Ina maana huwa huniamini ninayokwambia? nishakwambia nimeambiwa niliripoti tarehe fulani, Cha ajabu nini my, au kama Kuna jambo unalijua nambie maana hata wakati naachishwa kazi kule, wewe na mdogo wako mlikuwa mnajua na msiniambie, Sasa basi hamna kuficha nambie Nini umekisikia. niliongea kiume huku nikikaza uso mtoto wa kike hawezi niletea dharau.

Akuuuh, sijasikia lolote toka kwa mtu yeyote, hata Yale ya tetesi za wewe kufukuzwa kazi, aliniambia mdogo wangu, ila zilisikika kama tetesi hatukuwa na uhakika Hadi pale ilipotokea kweli. kama nimekukwaza nisamehe, aliongea huku akiwa anavuta mkoba wake uliokuwa mezani na kuuweka mapajani ili kama ikitokea lolote iwe rahisi kuondoka.

Vyakula vililetwa muda mwingi sana nikaanza kula kwa kujilazimisha huku hasira nazo hazikuwa nyuma kutokana na demu anavyonichukulia poa.

Alipoona nakula naye akaanza kula nadhani alikuwa ananisindikiza tu ila hakuwa tayari kula na mimi,

Rose alibadilika sana.

Siyo Rose yule ambaye huwa haoni aibu kufanya chochote akiwa na Mimi, tulikuwa tukilishana mithili ya mapenzi ya under 23 age. alikuwa anafumua nywele zake Kisha ananiambia nimsuke basi kwakuwa siwezi tunajikuta tunafurahishana huku akinirudisha kwenye utoto,
Lodge zingekuwa zinaongea zina mengi zinashuhudia huku vyumba vikikosa ya kuongea kama samaki
Ndani ya maji.

Leo hii Rose hataki nimsogelee wala kumgusa, nikiuliza kwanini, anasema lazima tujiheshimu. Kweli hakuna lenye mwanzo likakosa mwisho, lakini mbona huu mwisho kwangu umekuja mapema? nilijiuliza huku Chakula nacho kikipungua ladha sababu ya mawazo.

My tumekaa hapa, naona husemi umeniitia nini, maana nina haraka ujue sisi madaktari shughuli zetu huwa zina mabadiliko hivyo usishangae nikapigiwa simu muda wowote. aliongea huku akiwa busy na simu.

Nachojua Mimi na yeye tukiitana huwa hakuna sababu, yaani ukimwita njoo atakuja wala haulizi ulichomwitia, lakini Leo hii anataja niseme shida yangu! Ama kweli kanichoka.

Sina sababu maalum, ila furaha yangu nikukuona tu , we mwenyewe unatambua hilo. nilijibu huku nikimtazama kwa makini nikiusoma uso wake,.

Ahaaa ok, kama ni hivyo sawa, bila shaka umeshaniona, unaweza kuniruhusu niende? aliuliza

Mbona mapema hivyo my, kwanini tusikaekae kidogo, na tukitoka twende (nikitaja jina la lodge fulani)

Samahani yaani leo wala sijisikii vizuri sana, nashangaa mwenzangu mawazo hayo unayapata wapi, mwaka mpya umeingia huu, kule kwenye duka langu la dawa mkataba mpya wa kulipia lile eneo unatakiwa .

Hela zinazotakiwa pale, si haba pia hapa sijaja na gari kwasababu nimeliacha kwa fundi ili afanye marekebisho hela aliyonitajia ni MUNGU tu anajua yaani Sina msaada wowote ule, aliongea kwa kulalamika .

Akaendelea.....
Hivyo usione kama nakudharau ni kwamba navurugwa na vitu hivyo hapo. akaweka kituo.

Nilimwangalia Kisha nikacheka kidogo, maana mtu ambaye hakupendi ana Kila sababu ya kutaka muachane.huku nikijiuliza Kodi anayodaiwa huko dukani kwanini imsumbue, kwani duka au biashara yake haina faida, kusema huwa hapigi hesabu kuhusu TRA, Mtaji aliowekeza, faida zinazopatika, gharama za pango na makorokoro kibao kwani huwa hajui. Nilijiwazia moyoni.

Basi kwa maana hiyo , Mimi nimeridhika nashukuru kwa kutenga muda na nafasi ya kuonana na wewe, MUNGU akupe moyo huo huo. niliongea kimtego.

Usijali, nakupenda sana my, usinifikirie vibaya. alijibu shortcut huku akiondoka.

Si kawaida kuagana ndani ya mgahawa huwa ni lazima tusindikizane kidogo Kisha tunaachania mbele ila kwa siku hiyo ikawa tofauti.

Nilitoka nikichanja mbuga , huku moyo uliniuma kwani nilikuwa najua Rose anataka tuachane na Mimi sikuwa tayari kwani nilimpenda ile kumpenda sana, beautiful girl, English figure, na nywele nyingi Peruvian hair, ningemwachaje,

Achilia hayo kubwa zaidi ni Binti msomi, mwenye Elimu yake, mwenye kazi yake, nani anamrubuni my love Rose, mtu anayeongea kisomi huwa anapangilia maneno, kapata malezi Bora ya pande mbili, namuachaje jamaniiii.

Ni mshauri mzuri, ananiheshimu na kuiheshimu familia yangu. ana moyo wa huruma Kila unachomweleza huwa anakipokea na kutoa ushauri usioumiza, Sasa namwachaje Rose .

Ni Ms***e gani anataka kuniovertake achukue hii Mali. Aaaaaa weweee sitakubali.

Au ni masuala ya Kodi na gari lake yanamuumiza, ukute ni vitu hivyo kweli vitafanya nimkose Kisha akachukuliwa na mafioso wa hapa mjini.

Ngoja nitafanya kitu nauza shamba langu la huko kisemvule ili najua sikosi hela ndefu, nitahakikisha Rose hachomoki mikononi mwangu.

Ila shamba hapana, ekari kumi na kitu nauzaje kizembe? Ule ni urithi wa wanangu.

Au nikamsaundishe wife nimwambie nahitaji kama milioni moja Kuna jambo nakamilisha halafu, si nitarudisha ? halafu nimpe Rose naamini atalipa kupunguza matatizo yake. Kisha penzi litarudi upya .

Mmmh ila usawa huu kutoa jiwe moja uongo, wanawake huwa hawaridhiki hawa.

Nilijiuliza na kujijibu mwenyewe.

Nilifika nyumbani huku nikipokelewa na wife vikorokoro nilivyonunua na Mimi nikimpokea mtoto huku nikicheka cheka naye.

Mke wangu ujue siku zinavyosogea huyu mtoto anazidi kuchukua sura yangu, yaani huyu simuiti mwanangu Bali pacha wangu. sipati picha miaka hiyo tukikwaruzana Mimi na wewe , atavyokuja kunikoromea huku akinitisha.nilitania

Unapenda sana kusema mmefanana ila namuomba MUNGU mfanane sura siyo akili na maamuzi yako. Maana mume wangu kama ingekuwa siyo Elimu yako, napata picha ya maisha ambayo tungeishi. aliongea kwa kumaanisha.

Kila kitu hupangwa na MUNGU ukute ningekuwa Sina Elimu ningekuwa na good life zaidi , yaani circle of life ione hivyo hivyo mke wangu.nilijibu huku tukitaniana mambo mbalimbali, nilifurahi kwani ilinipunguzia machungu ya Rose.

Siku zilikimbia na kukatika huku tarehe husika ya Mimi kuripoti kazini ikifika, nakumbuka siku hiyo ya jumatatu nilifika kazini na kukabidhiwa ofisi yangu huku taratibu zingine zikiendelea kukamilika. hatimaye nikawa mfanyakazi rasmi wa taasisi yenye heshima nchini. Huku nikipewa na gari kwaajili ya kurahisisha mizunguko yangu maana kazi niliyopata huku neno kwenda mkoani lilikuwa ni jambo la kujiandaa kwani ni muda wowote na saa yeyote.

Penzi la kulazimisha Kati yangu Mimi lilirudi japo siyo kama zamani , maana penzi hili watu kukaa wiki nzima bila kutafutana ilikuwa kawaida tu.

Tuliachana vipi na Rose......

Nakumbuka Kuna siku moja , Rose Rose nilimpigia simu kuwa kesho ijumaa weekend inavyoingia tuonane, alikubali kuwa hakuna shida.
Kweli baada ya kesho kufika nilitegemea kuwa hii leo tutaonana ili tukamwagilie moyo, mimi na yeye, chaajabu Kuna muda kama saa kumi na moja alinipigia simu akidai tuahirishe tu lile zoezi, maana Kuna dharula mama yake anaumwa sana.

Nikamwambia kama ni hivyo basi nifike tu nije nimuone mama, alikataa kwa kusema si jambo jema , maana haitaleta picha nzuri.

(Na hili nililileta humu Kuna Uzi unasema hivi

"UJINGA NILIOWAHI KUUFANYA KULILIA PENZI LA MCHEPUKO "

Sasa endelea.....

Basi baada ya kunikatalia nisifike, niliamua kumrushia kiasi cha laki moja na nusu kama mwanaume uliyepokea taarifa ya ugonjwa lazima ujiongeze, alishukuru huku, Mimi Ahadi yangu ya kwenda viwanja ikiwa pale pale.

nilimchukua jamaa mmoja ambaye huwa tunaongoza sehemu nyingi tukachagua kiwanja kizuri tukaenda kufika pale, nilichokiona kilinishangaza sana kwani nilimuona Rose akiwa kimahaba na kijamaa fulani huku wakiwa kwenye mahaba mazito sana.

Aisee baada ya macho kugongana nilipata hasira sana, tena mno nikataka kuanzisha ugomvi lakini mchizi wangu alinisihi.

Dani braza, utaharibu ujue kwanza wewe una mke , vipi shemeji akija kusikia umeanzisha ugomvi sababu ya mchepuko utajidharaulisha bro acha, aliongea yule jamaa yangu huku akinishika mkono na kuondoka eneo lile.

Tulibadilisha kiwanja, huku tayari nikiwa nimevurugwa maana nilimpenda kupitiliza hivyo niliumia sana kwa aliyonifanyia.

Naam baada ya hapo hakuna aliyemtafuta mwenzake , na penzi likafika mwisho.

Nikarudisha UPENDO kwa familia yangu huku matukio ya mikosi kwa upande wangu yakipungua , nikizidi kupiga kazi huku wigo wa kujuana na watu wakubwa, wazito na kujua mambo mengi vikizidi kupanuka.
Kweli watu ni mtaji.

Hii ni tamati kwenye simulizi hii, nimeamua kushare na wanajamvi simulizi hii ili ,
Tuburudike na tujifunze mambo mbalimbali, kwa waliokata TAMAA wakae wakijua siku yao ipo kwani hakuna maisha magumu.

Bali Kuna mapito magumu.

Jack Daniel member wa jamiiforum.
 
SEHEMU INAYOFUATA.................... Nilirudi nyumbani usiku wa manane, nikalala kupunguza usingizi, niliamshwa na mke wangu Huku nikigundua ni saa mbili na robo na robo.

Pole mume wangu , naona mkukumkuku wa jana ulikuchosha sana, kaoge ili uje tunywe chai.

Niliingia bafuni nikajiswafi Kisha nikatoka sikutaka hata kusubiri chai badala yake, nilimweleza wife kwa kifupi huku nikiwahi kwa mke wa Shedy.

Sikumkuta mtu yeyote zaidi ya watoto, nikajua Hawa wapo kituoni, nilifika kituoni nikawakuta watu wengi majirani na mke wa Shedy, wakiwa wamenyongea sana.
Niliwasalimia huku nikigundua wanahisi labda nilifanya makusudi kuchelewa, kumbe nilipitiwa tu.

Nawahitaji wahusika wa Shedrack , wanifuate, aliamuru afande Fulani mwenye cheo Cha juu.

Tuliingia kwenye chumba fulani, huku tukiwa watu watano askari wa sita akiwa kazungukwa na maaskari wadogo wenye silaha.

Naitwa afande (jina kapuni)naomba tufahamiane, watu walitaja majina huku wakitaja uhusiano wao wapo vipi na mtuhumiwa, zamu yangu na ya mwisho ilifika, nikataja jina huku afande akiniangalia sana,

Huyu mtu umefahamiana muda gani, aliniuliza,

Kwakweli afande labda waulize wengine swali hilo,huyu Mimi nimecheza naye utotoni, nilijibu huku akionesha kuridhika,

Jamani nimewaita hapa kwasababu, tulikuwa tunasubiri upelelezi ukamilike ilu tujue mtuhumiwa anafunguliwa kesi ya aina gani,

Huyu baada ya kuhojiwa kakiri kuwa ni kweli walikuwa wanajaribu kuvunja duka moja ambapo walikuwa wanne ndipo risasi ilipomkuta mwenzao akafariki pale pale huku wao wakikimbia, hivyo kwa kushirikiana na raia wema waliotutajia hao wahalifu, walipo tukafanikisha kuwanasa mtu pekee aliye tusumbua ni huyu shedy kwani huyu kakamatiwa mkoani kabisa.

Lakini pia, watuhumiwa wote wanakabiliwa na kesi ya jinai na si ya mauaji kama taarifa ya awali ilivyodai,. aliweka kituo

Binafsi nilifurahi kama ni kesi ya jinai maana iliwezekana kumdhamini japo Mimi nilijitoa,

Afande aliendelea.....

Hivyo taratibu za dhamana mtapewa maana Kuna vitu vya kiintelijensia tunakamilisha. mnaweza kwenda, tuliruhusiwa huku wote tukitoka nje na kuwaeleza wenzetu kwa kifupi Kisha tukapanda daladala kuja nyumbani kwa Shedy.

Tulikaa kikao na majirani huku michango ikiendelea na pole nyingi za kinafiki,

Wewe bwana Daniel tunakuomba uwe kiongozi kwenye hili suala la mwenzetu, aliyepatwa na matatizo. aliongea jamaa mmoja.

Hapana haitawezekana kwasababu Mimi mwenyewe nina matatizo hivyo nimekuja tu kwakuwa hili la mwenzangu ni zito. lakini pia sitakuwepo kwenye orodha ya wadhamini badala yake nitatoa kiasi Cha pesa kwa kadri ya uwezo wangu pale pesa itakapohitajika,

simu ya Rose iliita, alipiga ikabidi nitoke chemba, nikaipokea.
Tukasalimiana.

My mbona kimya hivyo, unajua fika siwezi kukutafuta kwasababu ya mipaka tuliyojiwekea, vipi Kuna shida gani.aliongea kwa kulalamika Rose.

Hapana mpenzi wangu, kwanza nisamehe sana, pili Kuna matatizo, Kuna ndugu yangu ana kesi na mpaka muda huu yupo mahabusu na Mimi nipo kwake na wanafamilia wengine tukijadili namna ya kumtoa. nilimfahamisha Rose.

Sawa, ila my Dad kasema kapata dharula kidogo hivyo katoa maelekezo kule kuwa utaenda, hivyo unachotakiwa kufanya ni kujiandaa ili wakakupe maelekezo. aliweka kituo

Sawa, naomba niache kidogo nitakupigia tuongee vizuri maana nahitajika kwenye kikao,

Sawa Wala usijali, alijibu Rose mchepuko wangu, napenda kumwita 3D kwasababu alinionesha UPENDO wa kweli japo Kuna muda alinigeuka, fuatilia stori Hadi mwisho.

Nilirudi kwenye kikao huku watu wote wakinitaka niwe mstari wa mbele kwenye process ya dhamana, ikabidi niwakatae kwa kuwapa maneno haya.......

Huyu mtuhumiwa naweza kusema namfahamu vizuri kuliko wengi wetu hapa bahati nzuri shemeji yangu unalitambua hili. hivyo Mimi ushauri wangu na mtazamo wangu niwe muwazi na mkweli, hili suala lazima litafika mahakamani, hivyo kutakuwa na usumbufu mwingi na dharula za hapa na pale, lakini mtambue hapohapo na Mimi lazima nitakuwa nahitajika kusukuma gurudumu la maisha kwenye vibarua vyetu nikitafuta mkate wa kila siku,

Hivyo basi nashauri wapatikane watu wengine,ili tugawane majukumu huku Mimi nikibeba jukumu la kuisaidia familia ya ndugu yangu itakapokwama kwa lolote , huku nikiwa bega kwa bega na nyinyi. nilijitetea.

Huyu kijana Mimi nimemwelewa vizuri sana, yaani anamaanisha wapatikane watu wengine wawe wadhamini huku yeye mchango wake ni kuilisha familia , jamani hamuoni bado mtu kafanya uungwana.? aliongea mzee mmoja huku wengi wakionesha kumuunga mkono. Wakajitokeza watu watakaokuwa tayari kwa dhamana Mara ripoti kutoka polisi itakapotoka. niliacha kiasi cha pesa, tukaagana nikaondoka mchana ule.

Ndugu wasomaji,
Kama Shedy angekamatwa kwa kosa lingine ningekuwa first line kwenye kumdhamini lakini alikuwa anakabiliwa na kesi ya ujambazi, wizi, unyang'anyi, nisingejitumbukiza kwenye hayo makusudi hasa ukizingatia sikuwa na kazi wakati huo,

Haya ni makusudi, maisha haya ukamwibie mtu kweli?
Hata siamini kwa yule jamaa yangu sikuwahi kumfikiria kuwa ana haya mawazo,

Nilikuwa nampongeza kwa hustlers zake huku nikimuiga baadhi ya vitu .
Kweli moyo wa mtu kichaka
Kinachomsumbua jamaa yangu kwenye maisha ni TAMAA. ana TAMAA mbaya, asione kitu Cha mtu, akihitaji kutimiza malengo yake atalazimisha hata pasipo wezekana.

Hebu tufanye ametoka na yupo uraiani kwa skendo yake ilivyosambaa, si atakufa hata kwa kuviziwa Huyu, ataishije hapa mjini , Nilijiwazia moyoni huku nikikaribia kufika nyumbani .

Eenhee za utokako , maana hata Chakula hukutaka kula ukawa juujuu tu, kama aliyeko ndani ni mwanao wa kumzaa, alihamaki mke wangu.

Mama Jack, ujue jamaa ana kesi nzito na ile Sijui kama atachomoka yaani nyundo zinamuhusu kabisa, nilimwambia

Kwani kakutwa na hatia gani yule, aliuliza mke wangu.

Kesi ya unyang'anyi, tena uchunguzi bado unaendelea, na dhamana wamekataa wanadai Kuna vitu wanaweka sawa, kuna nini hapo, lengo wanataka aende mahakamani, Sasa maisha yenyewe haya na watoto alionaoooooh, ujue inafikirisha mke wangu? na hapo tumetoka kwenye kikao cha kifamilia namba ya kumnusuru jamaa.

Kama kawaida yako , upo mstari wa mbele kusaidia watu , sisemi usisaidie mtu, ila shedy ni mshenzi sana, kipindi upo ndani, nahangaika na tumbo langu, hakujali yeye na mkewe , cha ajabu alikuja kwangu nilidhani anataka kunisaidia kumbe msaada wenyewe hadi alale na mimi yaani mume wangu Sijui una moyo wa aina gani , kwanini usiwaache wapambane wenyewe, hapo tu huna kazi umefukuzwa, lakini bado tu unajiona waweza kuwa msaada wa mtu . aliweka kituo

Wewe nani kakwambia nimefukuzwa kazi. niliuliza nikiwa serious.

Weweeee mjini hapa mtu atakunyima Chakula siyo maneno, ni jana tu nilivyotoka kwenye msaada wa wazungu, ESTA kaniambia Kila kitu. ooh naenda kuonana na boss wangu Mara nini, yaani wewe boss wako kakuponza na ukute hujasingiziwa, na nikawa nashangaa maana Kila nikiuliza sababu ya kusimama kazi ni nini unaniambia vitu havina hata mashiko.haya tuishi baba, tena huna kazi ni fursa nzuri kuhudhuria kesi ya shedy, ambaye alikuwa ananing'iniza miguu kwenye baa yake pindi upo mahabusu huku akinipigia hesabu alale na Mimi.

Leo hii zamu yake kuwa mahabusu, wewe tena hata kula hutaki unawaza rafiki yako yupo ndani, mwache mwache aozee ndani si mwizi?

Ohhh namalizia fence mke wangu, tutanunua gari, nani wa kununua gari , mume wangu huyuhuyu? Hela zenyewe unapata kama homa za vipindi, sisi ni masikini na tutakufa masikini. aliongea mke wangu Huku akishusha freestyle kiasi chakunikasirisha.

Mke wangu Mimi naamini wema haulipwi kwa ubaya, Mimi wala sipo mstari wa mbele kwenye kesi yake badala yake nimebaki kama mshauri tu Wala usinihisi vibaya, nilijishusha maana tayari pengine tungezua mengine mke wangu alikuwa kapaniki Sana.

Weweeee umefukuzwa kazi umenificha, hili utaniambia ukweli?
Ila nikukumbushe tu kuwa kwenda kwenda huko unaweza Kuta mnaswekwa ndani mkitafsirika kama wezi wenzake,. aliongea mke wangu Huku nikigundua heshima yangu ishaanza kushuka, mke wangu hajawahi Wala kuthubutu kunitamkia maneno kwa kujiamini vile. Acha pesa iitwe pesa ukiikosa, mtu anaweza kudai talaka Bila sababu .

Nilikula Chakula Kisha nikampigia Rose, tuongee kuhusu masuala ya kazi, alinielewesha vizuri sana huku akinitahadharisha kuwa nisiwaangushe yeye na baba yake.

Siku za kukumbuka kuzaliwa kwa kristo zilikaribia huku kipande hiki nikiwa Sina wasiwasi kwani akiba nilikuwa nayo, lakini pia matumaini ya kazi iliyoko mbele yangu, yalitosha kushusha Presha japo sikuwa na uhakika wa asilimia mia moja.

Nilikata simu ya Rose nikampigia ESTA lengo nimchane kwanini kuniingilia kwenye familia yangu.?
Akapokea simu.

My huyooo jamani umenikumbuka?
Mbona unakuwa kimya hivyo, huwa unaahidi utanipigia lakini kimya kinakuwa kingi mno baba, aliongea kwa kubana pua akilazimisha sauti ya kitoto.

Sasa wewe , inakuwaje kumwambia mke wangu maneno ya kufukuzwa kazi kwangu, kwanini ufanye hivyo kulikuwa na ulazima gani? niliuliza kwa ukali,.

Eee eeeeeeh baba hasira zako peleka hukoo, kwani kazi si umefukuzwa kweli kwani uongo? alijibu kijeuri huku nikijiona kama Nina mkosi mbona hakuna anayeniheshimu hata ESTA ananipandishia,?

Wewee jiheshimu tena, jua unaongea na nani au hujui kuwa we ndiyo chanzo Cha kufukuzwa kazi au huyo shoga yako hakukwambia chanzo Cha Mimi kutolewa pale.

Wewe Daniel vipi, umesahau kama kazi uliyofanya ulilipwa, Sasa jua kuwa ulichagua kazi ya usuluhishi kuliko kazi yako muhimu, hivyo usitafute mchawi, Wala kutafuta pa kufia sawa baba ........

Niliamua kukata simu huku, nikigundua mwanamke akipaniki siyo wa kubishana naye lakini pia ESTA kwa Sasa wanaiva sana na madam kifupi yupo upande wenye nguvu.
PESA, PESA, PESA.

Alamski.

Itaendelea..........................
Armed robbery kumbe ina dhamana? Sema ina mafunzo tupo pamoja mwamba Tolonino
 
So huo msemo binafsi hua siuamini sana naamin katika mipango
Sio lazima ufanye kazi kwako. Lakini nikuulize swali Moja. Ulivyokuwa umerelax Ina Mana Kama labda ungemaliza ukarelax bila hata ya kuzunguka bado tu ungeupata ama ulitokana na kuzunguka kwako. Iko ivi Kuna kupanda mbegu iote Sasa wakati wa mavuno ukifika.

Iyo ku relax Ni sawa when your set up ikifika sip kuwa hustle zako la hasha Ni set up imekuja Ni kuachia trigger umeua mnyama na sio kupigapiga risasi kisa unazo nyingi
 
Tunashukuru mno mkuu Ila Rose hajawahi kukutafuta ama kujua kuwa ulipata kule kazi. Nadhani rose alikupenda ukiwa na qualities fulani ama subjectively Ila sio objectively.
Ila nakusihi sijui Kama ungelimtafuta ama Kama ulimtafuta ukamshukuru hata kwa kumtoa 2M Mana sehemu kubwa mno Ali play part. So usitumie nayeye Mana mapenzi huwa Ni animals insticts,inner voice/feelings,yaani huwa automatically,is like subconscious mind inavyofanya kazi like reflex action,ama huwa Ni intuition,Kama haipo ama ikahamia kwa mwingine usimlaumu Mana unaweza inajieleza Ile rationally ama by your logic, reasoning, concious brain unapiga mistari wapi hakuelewi Mana intuition iko kwa mwingine yaani lizard brain ndio inam control mtu hata hajui Ni kwa Nini kampenda mwingine wewe kakuacha. Yaani huwa Ni emotions na kwa vile sie Ni emotions creatures we rationalize our emotions. Yaani tunafanya kitu kwa emotions baadaye ndio tunakuja kuzi reason emotions zetu kuwa nikifanya hivi kwa sababu ya hivi na hivi.
Hii elimu ya emotions Ni biological things so Zina nguvu mno.

Aliyekupenda hutumii nguvu Sana mkuu. Mke wangu siku ya kwanza kuniona namie sijawahi kumuona nikamkubali naye akanikubali akaenda kuita baba yake tukamsalimia nikamwambia kuwa wazee wenzake watakuja kuongea naye mkuu. Hebu imagine mie nilielezwa kuwa familia fulani nenda Kuna binti ulimpenda uoe kule hakuna shida,mpaka saivi nashukuru Mungu nimempata mke mzuri mie ndiye smt namzingua.


Ila big up mno kila la heri in your life
 
SEHEMU YA MWISHO......(FINAL)

Kwa wenye kuamini Dini na madhehebu yao, au hata wanaoamini sehemu wanazozijua, wote kwa pamoja tuweke IMANI kwa MUNGU mmoja maana yupo na anatenda.

Maisha yaliendelea, familia zilifurahi huku Kila kitu kikiwa kwenye mpango sahihi kabisa

Mume wangu, unajua kama tarehe 17 mwezi huu, ndiyo siku yako muhimu wewe kuripoti kazini?
(akimaanisha tarehe 17 ya mwezi wa kwanza mwaka 2013).

Usijali mke wangu, najua sana, najua hilo, ila bado wiki nzima ujue. nilimjibu.

Sawa, ningekuwa na uwezo ningekufungia ndani usitoke kabisa, maana najua huko kuzurura kwako unaweza kuyazua huko ukaja kukatisha ndoto zako, nimechoka masuala yasiyokuwa na maana.
alilalamika.

(Nikicheka)
Ajali haina kinga mke wangu, hata nikikaa hapahapa lolote linaweza kutokea bado nikakatisha ndoto zangu, kikubwa ni kumuomba MUNGU ili atufatufanyie wepesi na kunyoosha mapito yetu. Nilimjibu.

Amina, basi piga magoti nikuombee maana hiyo kazi ni ya muhimu kwangu kuliko hata wewe,. aliniomba nifanye hivyo.

Kwa kumridhisha kutokana na Imani yake niliweza kufanya hivyo ili tu nisilete mgongano Kati yetu.
Baada ya kumaliza yale maombi mafupi , nilimpigia Rose ili tukutane maana alikuwa ananyanyasa sana moyo wangu.

Ndugu msomaji, kazi niliyopata kwa sasa hakujua mtu yeyote zaidi ya mke wangu na Rose.
Rose anajua kwakuwa ni mmoja wa wahusika walionipigania kule, ila yeye hakuwa na Imani juu ya Mimi kufanya kazi pale, maana Mara nyingi alikuwa akiniuliza akitaka kuhakikisha, kama taratibu zimekamilika.

Na Mimi sikutaka kumwambia na kutapika yote, kuhusu ile kazi kwani, licha ya kuwa nilishakamilisha vitu vingi lakini bado niliamini kwa asilimia tisini tu, hivyo kumwambia mtu na kujimaliza Kisha mpango wako ukakwama, sijui utaeleza nini.

Lakini nilichogundua ni kwamba penzi letu na Rose, Lilianza kufifia yaani lile penzi moto moto sikuliona tena yote haya yalisababishwa na Mimi kutokuwa na uhakika na kazi.

Nakumbuka tulikutana kwenye mgahawa mmoja Mimi na yeye nikaagiza Chakula ili wakati maongezi yakiendelea tupate kuburudika naye.

Hivi my, kwanini unapenda kuharibu pesa hivyo, Mimi naona Bora hata uagize soft drinks tu inatosha, hakuna haja ya sisi kutumia gharama kubwa, alisema huku akimaanisha.

Nilimtazama nikimshangaa maana hawezi sema yale na hajawahi kusema jambo lile, hela hatoi mfukoni mwake kwanini zimuume?

Kwani baby Kuna tatizo, sioni kama ni vitu vya gharama kiasi hicho. niliuliza.

Ujue lazima tu nikwambie ukweli, Daniel (akinitaja kwa jina mithili ya shambaboy)
Wewe huna uhakika wa kazi, na kama ujuavyo hii ni January huwa Kuna ugumu fulani ambao unasumbua hivyo kuheshimu pesa ni suala muhimu sana,. aliweka kituo.

Kwanini unasema sina uhakika wa kazi, Ina maana huwa huniamini ninayokwambia? nishakwambia nimeambiwa niliripoti tarehe fulani, Cha ajabu nini my, au kama Kuna jambo unalijua nambie maana hata wakati naachishwa kazi kule, wewe na mdogo wako mlikuwa mnajua na msiniambie, Sasa basi hamna kuficha nambie Nini umekisikia. niliongea kiume huku nikikaza uso mtoto wa kike hawezi niletea dharau.

Akuuuh, sijasikia lolote toka kwa mtu yeyote, hata Yale ya tetesi za wewe kufukuzwa kazi, aliniambia mdogo wangu, ila zilisikika kama tetesi hatukuwa na uhakika Hadi pale ilipotokea kweli. kama nimekukwaza nisamehe, aliongea huku akiwa anavuta mkoba wake uliokuwa mezani na kuuweka mapajani ili kama ikitokea lolote iwe rahisi kuondoka.

Vyakula vililetwa muda mwingi sana nikaanza kula kwa kujilazimisha huku hasira nazo hazikuwa nyuma kutokana na demu anavyonichukulia poa.

Alipoona nakula naye akaanza kula nadhani alikuwa ananisindikiza tu ila hakuwa tayari kula na mimi,

Rose alibadilika sana.

Siyo Rose yule ambaye huwa haoni aibu kufanya chochote akiwa na Mimi, tulikuwa tukilishana mithili ya mapenzi ya under 23 age. alikuwa anafumua nywele zake Kisha ananiambia nimsuke basi kwakuwa siwezi tunajikuta tunafurahishana huku akinirudisha kwenye utoto,
Lodge zingekuwa zinaongea zina mengi zinashuhudia huku vyumba vikikosa ya kuongea kama samaki
Ndani ya maji.

Leo hii Rose hataki nimsogelee wala kumgusa, nikiuliza kwanini, anasema lazima tujiheshimu. Kweli hakuna lenye mwanzo likakosa mwisho, lakini mbona huu mwisho kwangu umekuja mapema? nilijiuliza huku Chakula nacho kikipungua ladha sababu ya mawazo.

My tumekaa hapa, naona husemi umeniitia nini, maana nina haraka ujue sisi madaktari shughuli zetu huwa zina mabadiliko hivyo usishangae nikapigiwa simu muda wowote. aliongea huku akiwa busy na simu.

Nachojua Mimi na yeye tukiitana huwa hakuna sababu, yaani ukimwita njoo atakuja wala haulizi ulichomwitia, lakini Leo hii anataja niseme shida yangu! Ama kweli kanichoka.

Sina sababu maalum, ila furaha yangu nikukuona tu , we mwenyewe unatambua hilo. nilijibu huku nikimtazama kwa makini nikiusoma uso wake,.

Ahaaa ok, kama ni hivyo sawa, bila shaka umeshaniona, unaweza kuniruhusu niende? aliuliza

Mbona mapema hivyo my, kwanini tusikaekae kidogo, na tukitoka twende (nikitaja jina la lodge fulani)

Samahani yaani leo wala sijisikii vizuri sana, nashangaa mwenzangu mawazo hayo unayapata wapi, mwaka mpya umeingia huu, kule kwenye duka langu la dawa mkataba mpya wa kulipia lile eneo unatakiwa .

Hela zinazotakiwa pale, si haba pia hapa sijaja na gari kwasababu nimeliacha kwa fundi ili afanye marekebisho hela aliyonitajia ni MUNGU tu anajua yaani Sina msaada wowote ule, aliongea kwa kulalamika .

Akaendelea.....
Hivyo usione kama nakudharau ni kwamba navurugwa na vitu hivyo hapo. akaweka kituo.

Nilimwangalia Kisha nikacheka kidogo, maana mtu ambaye hakupendi ana Kila sababu ya kutaka muachane.huku nikijiuliza Kodi anayodaiwa huko dukani kwanini imsumbue, kwani duka au biashara yake haina faida, kusema huwa hapigi hesabu kuhusu TRA, Mtaji aliowekeza, faida zinazopatika, gharama za pango na makorokoro kibao kwani huwa hajui. Nilijiwazia moyoni.

Basi kwa maana hiyo , Mimi nimeridhika nashukuru kwa kutenga muda na nafasi ya kuonana na wewe, MUNGU akupe moyo huo huo. niliongea kimtego.

Usijali, nakupenda sana my, usinifikirie vibaya. alijibu shortcut huku akiondoka.

Si kawaida kuagana ndani ya mgahawa huwa ni lazima tusindikizane kidogo Kisha tunaachania mbele ila kwa siku hiyo ikawa tofauti.

Nilitoka nikichanja mbuga , huku moyo uliniuma kwani nilikuwa najua Rose anataka tuachane na Mimi sikuwa tayari kwani nilimpenda ile kumpenda sana, beautiful girl, English figure, na nywele nyingi Peruvian hair, ningemwachaje,

Achilia hayo kubwa zaidi ni Binti msomi, mwenye Elimu yake, mwenye kazi yake, nani anamrubuni my love Rose, mtu anayeongea kisomi huwa anapangilia maneno, kapata malezi Bora ya pande mbili, namuachaje jamaniiii.

Ni mshauri mzuri, ananiheshimu na kuiheshimu familia yangu. ana moyo wa huruma Kila unachomweleza huwa anakipokea na kutoa ushauri usioumiza, Sasa namwachaje Rose .

Ni Ms***e gani anataka kuniovertake achukue hii Mali. Aaaaaa weweee sitakubali.

Au ni masuala ya Kodi na gari lake yanamuumiza, ukute ni vitu hivyo kweli vitafanya nimkose Kisha akachukuliwa na mafioso wa hapa mjini.

Ngoja nitafanya kitu nauza shamba langu la huko kisemvule ili najua sikosi hela ndefu, nitahakikisha Rose hachomoki mikononi mwangu.

Ila shamba hapana, ekari kumi na kitu nauzaje kizembe? Ule ni urithi wa wanangu.

Au nikamsaundishe wife nimwambie nahitaji kama milioni moja Kuna jambo nakamilisha halafu, si nitarudisha ? halafu nimpe Rose naamini atalipa kupunguza matatizo yake. Kisha penzi litarudi upya .

Mmmh ila usawa huu kutoa jiwe moja uongo, wanawake huwa hawaridhiki hawa.

Nilijiuliza na kujijibu mwenyewe.

Nilifika nyumbani huku nikipokelewa na wife vikorokoro nilivyonunua na Mimi nikimpokea mtoto huku nikicheka cheka naye.

Mke wangu ujue siku zinavyosogea huyu mtoto anazidi kuchukua sura yangu, yaani huyu simuiti mwanangu Bali pacha wangu. sipati picha miaka hiyo tukikwaruzana Mimi na wewe , atavyokuja kunikoromea huku akinitisha.nilitania

Unapenda sana kusema mmefanana ila namuomba MUNGU mfanane sura siyo akili na maamuzi yako. Maana mume wangu kama ingekuwa siyo Elimu yako, napata picha ya maisha ambayo tungeishi. aliongea kwa kumaanisha.

Kila kitu hupangwa na MUNGU ukute ningekuwa Sina Elimu ningekuwa na good life zaidi , yaani circle of life ione hivyo hivyo mke wangu.nilijibu huku tukitaniana mambo mbalimbali, nilifurahi kwani ilinipunguzia machungu ya Rose.

Siku zilikimbia na kukatika huku tarehe husika ya Mimi kuripoti kazini ikifika, nakumbuka siku hiyo ya jumatatu nilifika kazini na kukabidhiwa ofisi yangu huku taratibu zingine zikiendelea kukamilika. hatimaye nikawa mfanyakazi rasmi wa taasisi yenye heshima nchini. Huku nikipewa na gari kwaajili ya kurahisisha mizunguko yangu maana kazi niliyopata huku neno kwenda mkoani lilikuwa ni jambo la kujiandaa kwani ni muda wowote na saa yeyote.

Penzi la kulazimisha Kati yangu Mimi lilirudi japo siyo kama zamani , maana penzi hili watu kukaa wiki nzima bila kutafutana ilikuwa kawaida tu.

Tuliachana vipi na Rose......

Nakumbuka Kuna siku moja , Rose Rose nilimpigia simu kuwa kesho ijumaa weekend inavyoingia tuonane, alikubali kuwa hakuna shida.
Kweli baada ya kesho kufika nilitegemea kuwa hii leo tutaonana ili tukamwagilie moyo, mimi na yeye, chaajabu Kuna muda kama saa kumi na moja alinipigia simu akidai tuahirishe tu lile zoezi, maana Kuna dharula mama yake anaumwa sana.

Nikamwambia kama ni hivyo basi nifike tu nije nimuone mama, alikataa kwa kusema si jambo jema , maana haitaleta picha nzuri.

(Na hili nililileta humu Kuna Uzi unasema hivi

"UJINGA NILIOWAHI KUUFANYA KULILIA PENZI LA MCHEPUKO "

Sasa endelea.....

Basi baada ya kunikatalia nisifike, niliamua kumrushia kiasi cha laki moja na nusu kama mwanaume uliyepokea taarifa ya ugonjwa lazima ujiongeze, alishukuru huku, Mimi Ahadi yangu ya kwenda viwanja ikiwa pale pale.

nilimchukua jamaa mmoja ambaye huwa tunaongoza sehemu nyingi tukachagua kiwanja kizuri tukaenda kufika pale, nilichokiona kilinishangaza sana kwani nilimuona Rose akiwa kimahaba na kijamaa fulani huku wakiwa kwenye mahaba mazito sana.

Aisee baada ya macho kugongana nilipata hasira sana, tena mno nikataka kuanzisha ugomvi lakini mchizi wangu alinisihi.

Dani braza, utaharibu ujue kwanza wewe una mke , vipi shemeji akija kusikia umeanzisha ugomvi sababu ya mchepuko utajidharaulisha bro acha, aliongea yule jamaa yangu huku akinishika mkono na kuondoka eneo lile.

Tulibadilisha kiwanja, huku tayari nikiwa nimevurugwa maana nilimpenda kupitiliza hivyo niliumia sana kwa aliyonifanyia.

Naam baada ya hapo hakuna aliyemtafuta mwenzake , na penzi likafika mwisho.

Nikarudisha UPENDO kwa familia yangu huku matukio ya mikosi kwa upande wangu yakipungua , nikizidi kupiga kazi huku wigo wa kujuana na watu wakubwa, wazito na kujua mambo mengi vikizidi kupanuka.
Kweli watu ni mtaji.

Hii ni tamati kwenye simulizi hii, nimeamua kushare na wanajamvi simulizi hii ili ,
Tuburudike na tujifunze mambo mbalimbali, kwa waliokata TAMAA wakae wakijua siku yao ipo kwani hakuna maisha magumu.

Bali Kuna mapito magumu.

Jack Daniel member wa jamiiforum.
Naamini sa hivi utakuwa hata KATEKISITA Kanisani je Ester ulimchakata au ndio iliishia pale
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom