chongoe
JF-Expert Member
- Mar 22, 2019
- 1,122
- 2,714
Habari zenu wakuu,
Mimi ni kijana ambaye kazi kubwa ni baharini; sio mvuvi ila mimi ni yule mshika usukani wa majahazi. Safari zangu ni za kupeleka mizigo tokea Mafia napeleka Kisiju au Zanzibar muda mwingine Kilwa, ndiyo kazi zangu. Nilitaka leo niwape story tu ninazokutana nazo hasa baharini maana mengi mno. Nitasimulia mawili mengine nitaendelea ikiwa nitaulizwa kwa mujibu wa story.
Story ya kwanza
Nakumbuka ilikuwa usiku natokea Kisiju naelekea Mafia, tupo safarini baada kupita kisiwa kimoja kinaitwa KOMA ndipo mauzauza yalipoanza. Kwa uzoefu wangu ndiyo mara ya kwanza kukutana na kioja kama kile wakati tunatembea baharini na jahazi ghafla mbele yetu ilitokea boti kubwa sana inakuja uelekeo wetu ilifika karibu kabisa mimi niljua wanatugonga; mara ghafla ikaturuka nzima mzima, kwa uoga wangu nilipiga kelele mpaka baadhi ya watu waliamka na kushtuka usingizini. Kuna mmoja wetu alivyoamka tu aliiona ile boti akaniuliza ile boti imetokea wapi nikamwambia ile imeturuka kimaajabu.
Hapa ndiyo maana nilipiga ukelele. Kusikia hivyo wale jamaa waliomka ikabidi watulie ghafla, ile boti ikawa inakuja uelekeo wetu nakutaka kutugonga; ilivyokaribia mule ndani ya jahazi yetu alikuepo mzee mmoja anaeishi Mafia. Sasa wakati boti inakaribia yule mzee alituambia tubaki kuwa kimya ghafla yeye akasimama sikujua kasema maneno gani ghafla nikaona boti inageuza kuelekea upande mwingine.
Zilichukua kama dakika mbili ile boti kupotea hatukuiona tena ndipo yule mzee akanambia usisafiri kama mwili wako mwepesi au acha kazi utakufa bure kumbe ile boti ilikuja kwa lengo la kutupoteza kuanzia ndio nikajitengeza sasa.
Story ya pili
Nilimpoteza ndugu yangu alikufa kwa ugonjwa wa kidole sababu yake wakati tunatokea Mafia tulipakia nazi za MZEE mmoja wakati wakudai nauli, yule mzee alikuwa hataki kulipa sasa alipo kuja kwangu dogo akawa ananisimulia huku anaonesha kidole kunipa ishara kwa yule mzee kuwa kagoma kulipa kumbe yule Mzee alkasirika baada kuona ananyooshewa kidole. Yule mzee akatamka kumwambia dogo hutanyoosha tena kidole; mimi nilidhani utani, dogo baada kufika jioni akaanza kuumwa na kidole siku ya tatu dogo akafariki. Hayo ndiyo nayopitia kwenye kazi yangu; yapo mengi ngoja nipumzike kwanza.
Sehemu ya Pili
Sehemu ya Tatu
Mimi ni kijana ambaye kazi kubwa ni baharini; sio mvuvi ila mimi ni yule mshika usukani wa majahazi. Safari zangu ni za kupeleka mizigo tokea Mafia napeleka Kisiju au Zanzibar muda mwingine Kilwa, ndiyo kazi zangu. Nilitaka leo niwape story tu ninazokutana nazo hasa baharini maana mengi mno. Nitasimulia mawili mengine nitaendelea ikiwa nitaulizwa kwa mujibu wa story.
Story ya kwanza
Nakumbuka ilikuwa usiku natokea Kisiju naelekea Mafia, tupo safarini baada kupita kisiwa kimoja kinaitwa KOMA ndipo mauzauza yalipoanza. Kwa uzoefu wangu ndiyo mara ya kwanza kukutana na kioja kama kile wakati tunatembea baharini na jahazi ghafla mbele yetu ilitokea boti kubwa sana inakuja uelekeo wetu ilifika karibu kabisa mimi niljua wanatugonga; mara ghafla ikaturuka nzima mzima, kwa uoga wangu nilipiga kelele mpaka baadhi ya watu waliamka na kushtuka usingizini. Kuna mmoja wetu alivyoamka tu aliiona ile boti akaniuliza ile boti imetokea wapi nikamwambia ile imeturuka kimaajabu.
Hapa ndiyo maana nilipiga ukelele. Kusikia hivyo wale jamaa waliomka ikabidi watulie ghafla, ile boti ikawa inakuja uelekeo wetu nakutaka kutugonga; ilivyokaribia mule ndani ya jahazi yetu alikuepo mzee mmoja anaeishi Mafia. Sasa wakati boti inakaribia yule mzee alituambia tubaki kuwa kimya ghafla yeye akasimama sikujua kasema maneno gani ghafla nikaona boti inageuza kuelekea upande mwingine.
Zilichukua kama dakika mbili ile boti kupotea hatukuiona tena ndipo yule mzee akanambia usisafiri kama mwili wako mwepesi au acha kazi utakufa bure kumbe ile boti ilikuja kwa lengo la kutupoteza kuanzia ndio nikajitengeza sasa.
Story ya pili
Nilimpoteza ndugu yangu alikufa kwa ugonjwa wa kidole sababu yake wakati tunatokea Mafia tulipakia nazi za MZEE mmoja wakati wakudai nauli, yule mzee alikuwa hataki kulipa sasa alipo kuja kwangu dogo akawa ananisimulia huku anaonesha kidole kunipa ishara kwa yule mzee kuwa kagoma kulipa kumbe yule Mzee alkasirika baada kuona ananyooshewa kidole. Yule mzee akatamka kumwambia dogo hutanyoosha tena kidole; mimi nilidhani utani, dogo baada kufika jioni akaanza kuumwa na kidole siku ya tatu dogo akafariki. Hayo ndiyo nayopitia kwenye kazi yangu; yapo mengi ngoja nipumzike kwanza.
Sehemu ya Pili
Sehemu ya Tatu