bioto
JF-Expert Member
- Oct 1, 2017
- 1,261
- 2,099
- Thread starter
- #61
Sehemu ya pili
.....Ilipoishia.......
Hatimaye Walitoka wote na kufika wodini,Humph
akiwa kitandani anaweweseka huku Mara kwa Mara
akimtaja Sor,Mama Humph akamkumbatia mumewe
machozi yakizjdi kumtoka kwa uchungu.
.......Shuka nayo.........
Ukweli Ni kwamba alimuonea Huruma mno
mwanaye.
Lisa alirudi nyumbani kwao akiwa mpweke
ajabu,mawazo yalimtafuna mwili mzima,hata taxi
aliyopanda hakukumbuka kulipa baada ya
kufikishwa kwao. Dereva alishuka upesi na
kumfuata akiwa nusu akikimbia na nusu kutembea.
Kabla Lisa hajaingia getini mwa nyumba yao
akasikika dereva akiita kwa nguvu
"Binti!,Binti!" Lisa hakugeuka alizidi kuendelea na
safari
"Hela yangu vipi we binti?" Dereva alimvuta Lisa
blauzi huku akiuliza kwa ghadhabu
"Hela gani?,we nani kwanza?" Lisa alionekana
kumshangaa yule dereva ambaye sasa sura ilianza
kutengeneza matuta ya hasira.
"Kwani hii gari uliyopanda ni ya baba yako eti
wewe?" Dereva alihoji kwa hasira huku akimtikisa
Lisa ambaye hakuwa akijali kitu,hali iliyopelekea
mzozo mkali baina yao.
Mlinzi wa getini kwa akina Lisa alitoka nje mbio
mbio na kuanza kuamua kesi ile asiyoijua ndipo
Lisa akapata upenyo wa kuingia ndani akimuachia
mlinzi kasheshe ile..
Mpaka asubuhi Lisa alikuwa na kazi ya kuitazama
picha ya Humph biila kupata majibu ya kile
anachokiwaza. Alivyoona kumekucha akajiandaa na
kuelekea hospitali,alimkuta mama wa Humph akiwa
pale usiku mzima ulimuishia pale bila kujali chakula
wala kutafuta mahali sahihi pa kulala.
Alifika na kumuamsha taratibu mpaka
akaamka,baadaye waliingia wodini baada ya
kuruhusiwa kwenda kumtazama Humph.
Lisa aliketi kitandani na kumshika Humph kichwani.
"Dokta amesema mchana atakuwa ameshaamka
hivyo usiwe na shaka sawa mwanangu" mzee Kasai
alimwambia Lisa
"Sawa baba" Lisa alijibu
Mchana unafika Humph anafumbua macho taratibu
Lisa anawahi kumshika mkono na kutabasamu
lakini Humph haoneshi hata dalili ya
kutabasamu,Dokta Alex anaingia na manesi wawili
baada ya kuitwa
"Mfanyieni utaratibu wa kula" alizungumza Dokta
Alex wakati amemaliza na kumcheki Humph.
"Usiwe na hofu binti rafiki yako ni mzima kabisa na
baadaye ataruhusiwa,jitahidi kuwa naye karibu
maana vitu vingi hakumbuki hapo alipo tuliweka
kumbukumbu ya vitu vichache"
"Dokta Alex alimwambia Lisa na kumfanya aduwae
kidogo na kutambua kitu kipya kuwa Humph
hakutabasamu kwasababu hamkumbuki.
Baada ya Humph kuruhusiwa na kurudi nyumbani
Lisa alikuwa naye karibu mno kwa kila kitu lakini
kwa Humph haikuwa hivyo yeye alimchukulia
kawaida tu.
Lisa hakuona shida,wakati wameketi pamoja Lisa
aliamua kuanzisha maongezi ili kumuweka sawa
Humph.
" Hey,um! Nilisahau kujitambulisha toka awali
uliponiona,naitwa Lisa ni rafiki pekee wa karibu
kwako nikiamanisha "girlfriend" wako tangu tukiwa
tunasoma sekondari" Lisa aliongea huku akiminya
vidole vyake
"Ongeza Sauti kidogo mdada sijakusikia vyema"
Humph alijibu kwa pozi huku akiondoa (spika
ndogo za masikioni) earphone.
"Naitwa Lisa Ni mpenzi wako wa siku nyingi" Lisa
alijibu akiwa ameanza kukasirika kutokana na tabia
mpya aliyokuwa nayo Humph
"Mmh! Mpenzi tena,aaah! Sidhani,mbona sijawahi
kuwa na mpenzi,wewe Ni wa wapi labda?" Humph
akauliza kwa madoido akionesha wazi
kutomfahamu Lisa kiundani.
Lisa akatoka mbio analia mlangoni akapishana na
mama yake Humph lakini hakumsemesha,licha ya
mama Humph kujaribu sana kumuita Lisa bado
haikusaidia
"Umemfanya nini mtoto wa watu?" Ilikuwa Ni kauli
ya kwanza ya mama Humph baada ya kuingia ndani
na kumuuliza Humph
"Sijui,mi' amejitambulisha kuwa ni mpenzi
wangu,nikamuuliza wa wapi maana sijawahi kuwa
na mpenzi,ndipo akachukia na kutimua mbio huku
akilia" Humph alijibu bila wasiwasi Ni kama alikuwa
akiongea na rafikiye.
"Umeonesha dharau kubwa sana mbele yake,yule
msichana amejitoa kwa hali na mali isitoshe Ni wa
kwako kwa muda mrefu sasa haukupaswa
kumfanyia vile,hakustahili kwa kweli" mama Humph
alilalama
"Mama simfahamu yule binti na sitokaa nimfahamu
kamwe,na kama Ni wangu kwanini asiwemo karika
kumbukumbimu zangu za kila siku" Humph alisema,
mama Humph na mumewe pamoja na familia nzima
waliapa kukaa kimya kuhusu matatizo ya Humph ili
yasijirudie hivyo hawakuthubutu kusema lolote
"Kamuombe msamaha,mjinga mkubwa wee!"
Humph akainuka huku akiongea "sijamkosea mimi "
Mama Humph akaishia kutikisa kichwa tu huku
akionekana kutofurahia tabia mpya ya Humph
iliyotokana na kufutwa kumbukumbu zake
zilizoondoka na mambo mengi mno,mpaka wazazi
wake alikuwa akiwachukulia kama jamaa wa
kawaida walio karibu yake.
鈽呪槄鈽匤ourney to the falling Mountain鈽呪槄鈽?
鈽呪槄鈽匰afari ya mlima unaoanguka鈽呪槄鈽?
"Habari za asubuhi hii ndugu wanachuo,nafurahi
kufika siku hii ambayo imerejea tena mbele
yetu,kwa wale wageni wa mwaka wa kwanza yaani
wanachuo wapya hawalitambui suala hill na itakuwa
Ni Mara yao ya kwanza kulisikia" Akatulia kidogo
Mkuu wa chuo msaidizi akitafakari usikivu wa
wanachuo kwa muda kisha akaendelea
"Tuna mashindano mbalimbali ambayo huendeshwa
na kufanyika nje ya chuo chetu yakijumuisha vyuo
vingi vinavyotuzunguka,na kawaida yetu huwa
tunafanyia mashindano haya katika kisiwa cha
falling mountain (mlima unaoanguka) pia tutakuwa
na utalii wa muda katika milima yake na misitu pia
inayosemekana kubeba utajiri mkubwa pamoja na
kishamiri maajabu mengi ya kihistoria"
Wanachuo wote wakalipuka kwa shangwe nyingi
lakini mkuu wa chuo msaidizi hakuwa amemaliza
hivyo akanyoosha mikono kuwanyamazisha
wanachuo wote
"Hatuna muda mwingi,kesho safari itaanza na
niseme tu poleni kwa kuwastukiza,natumaini
mtajiandaa kuanzia sasa" alimalizia Mkuu wa chuo
msaidizi na kuwaacha wanachuo wote wakilipuka
kwa shangwe nyingi ikiwemo Humph
Lisa hakuwa na furaha hata kidogo mbaya zaidi
alimuona Humph alivyoifurahia safari ile ikiwa si
kawaida yake kabisa.
"Mambo mdada" Lisa akistukia akisalimiwa na
alipogeuka aliduwaa kuona ni Humph,akabaki
kujiuliza ni saa ngapi mtu yule amemfikia lakini
ukweli ulibaki kuwa muda alioutumia kuzama katika
dimbwi la mawazo ndiyo muda alioutumia Humph
kufika pale.
"Poa tu" Lisa alikumbuka kuijibu salamu ya Humph
lakini akiwa mnyonge mno
"Samahani,ulisema u nani vile?" Humph aliuliza
akiwa anatazama huku na kule
"Lisa" Lisa alijibu kwa mkato huku akimtazama
vyema Humph ambaye hakujua kama binti huyo
alikuwa akimuangalia.
"Sikia binti,Jana nusura mama apasuke ulivyotoka
unalia,sasa Fanya yaishe maana hapendi kabisa
nikichokifanya kwako" Humph alisema akiwa
anamuangalia binti mmoja aliyekuwa
anatabasamu,macho yao yakagongana
"Yameisha toka Jana Humph" Lisa alijibu akiwa
hana amani
"Poa,alafu nimempenda yule mdada sijui anaitwa
nani?,hey! Vipi unamfahamu hata kwa jina labda?"
Humph alimuuliza Lisa akiwa bado anamtazama
yule binti.
Lisa hakuvumilia ule upuuzi ulioonekana dhahiri
kuwa ni dharau kutoka kwa Humph,akaamua
kuondoka kimya kimya.
Humph anakuja kugeuka baada ya kukosa
jibu,anamkosa Lisa pale alipokuwa
amesimama,akaangaza huku na kule asimuone
kutokana na uwingi wa wanachuo.
.....Ilipoishia.......
Hatimaye Walitoka wote na kufika wodini,Humph
akiwa kitandani anaweweseka huku Mara kwa Mara
akimtaja Sor,Mama Humph akamkumbatia mumewe
machozi yakizjdi kumtoka kwa uchungu.
.......Shuka nayo.........
Ukweli Ni kwamba alimuonea Huruma mno
mwanaye.
Lisa alirudi nyumbani kwao akiwa mpweke
ajabu,mawazo yalimtafuna mwili mzima,hata taxi
aliyopanda hakukumbuka kulipa baada ya
kufikishwa kwao. Dereva alishuka upesi na
kumfuata akiwa nusu akikimbia na nusu kutembea.
Kabla Lisa hajaingia getini mwa nyumba yao
akasikika dereva akiita kwa nguvu
"Binti!,Binti!" Lisa hakugeuka alizidi kuendelea na
safari
"Hela yangu vipi we binti?" Dereva alimvuta Lisa
blauzi huku akiuliza kwa ghadhabu
"Hela gani?,we nani kwanza?" Lisa alionekana
kumshangaa yule dereva ambaye sasa sura ilianza
kutengeneza matuta ya hasira.
"Kwani hii gari uliyopanda ni ya baba yako eti
wewe?" Dereva alihoji kwa hasira huku akimtikisa
Lisa ambaye hakuwa akijali kitu,hali iliyopelekea
mzozo mkali baina yao.
Mlinzi wa getini kwa akina Lisa alitoka nje mbio
mbio na kuanza kuamua kesi ile asiyoijua ndipo
Lisa akapata upenyo wa kuingia ndani akimuachia
mlinzi kasheshe ile..
Mpaka asubuhi Lisa alikuwa na kazi ya kuitazama
picha ya Humph biila kupata majibu ya kile
anachokiwaza. Alivyoona kumekucha akajiandaa na
kuelekea hospitali,alimkuta mama wa Humph akiwa
pale usiku mzima ulimuishia pale bila kujali chakula
wala kutafuta mahali sahihi pa kulala.
Alifika na kumuamsha taratibu mpaka
akaamka,baadaye waliingia wodini baada ya
kuruhusiwa kwenda kumtazama Humph.
Lisa aliketi kitandani na kumshika Humph kichwani.
"Dokta amesema mchana atakuwa ameshaamka
hivyo usiwe na shaka sawa mwanangu" mzee Kasai
alimwambia Lisa
"Sawa baba" Lisa alijibu
Mchana unafika Humph anafumbua macho taratibu
Lisa anawahi kumshika mkono na kutabasamu
lakini Humph haoneshi hata dalili ya
kutabasamu,Dokta Alex anaingia na manesi wawili
baada ya kuitwa
"Mfanyieni utaratibu wa kula" alizungumza Dokta
Alex wakati amemaliza na kumcheki Humph.
"Usiwe na hofu binti rafiki yako ni mzima kabisa na
baadaye ataruhusiwa,jitahidi kuwa naye karibu
maana vitu vingi hakumbuki hapo alipo tuliweka
kumbukumbu ya vitu vichache"
"Dokta Alex alimwambia Lisa na kumfanya aduwae
kidogo na kutambua kitu kipya kuwa Humph
hakutabasamu kwasababu hamkumbuki.
Baada ya Humph kuruhusiwa na kurudi nyumbani
Lisa alikuwa naye karibu mno kwa kila kitu lakini
kwa Humph haikuwa hivyo yeye alimchukulia
kawaida tu.
Lisa hakuona shida,wakati wameketi pamoja Lisa
aliamua kuanzisha maongezi ili kumuweka sawa
Humph.
" Hey,um! Nilisahau kujitambulisha toka awali
uliponiona,naitwa Lisa ni rafiki pekee wa karibu
kwako nikiamanisha "girlfriend" wako tangu tukiwa
tunasoma sekondari" Lisa aliongea huku akiminya
vidole vyake
"Ongeza Sauti kidogo mdada sijakusikia vyema"
Humph alijibu kwa pozi huku akiondoa (spika
ndogo za masikioni) earphone.
"Naitwa Lisa Ni mpenzi wako wa siku nyingi" Lisa
alijibu akiwa ameanza kukasirika kutokana na tabia
mpya aliyokuwa nayo Humph
"Mmh! Mpenzi tena,aaah! Sidhani,mbona sijawahi
kuwa na mpenzi,wewe Ni wa wapi labda?" Humph
akauliza kwa madoido akionesha wazi
kutomfahamu Lisa kiundani.
Lisa akatoka mbio analia mlangoni akapishana na
mama yake Humph lakini hakumsemesha,licha ya
mama Humph kujaribu sana kumuita Lisa bado
haikusaidia
"Umemfanya nini mtoto wa watu?" Ilikuwa Ni kauli
ya kwanza ya mama Humph baada ya kuingia ndani
na kumuuliza Humph
"Sijui,mi' amejitambulisha kuwa ni mpenzi
wangu,nikamuuliza wa wapi maana sijawahi kuwa
na mpenzi,ndipo akachukia na kutimua mbio huku
akilia" Humph alijibu bila wasiwasi Ni kama alikuwa
akiongea na rafikiye.
"Umeonesha dharau kubwa sana mbele yake,yule
msichana amejitoa kwa hali na mali isitoshe Ni wa
kwako kwa muda mrefu sasa haukupaswa
kumfanyia vile,hakustahili kwa kweli" mama Humph
alilalama
"Mama simfahamu yule binti na sitokaa nimfahamu
kamwe,na kama Ni wangu kwanini asiwemo karika
kumbukumbimu zangu za kila siku" Humph alisema,
mama Humph na mumewe pamoja na familia nzima
waliapa kukaa kimya kuhusu matatizo ya Humph ili
yasijirudie hivyo hawakuthubutu kusema lolote
"Kamuombe msamaha,mjinga mkubwa wee!"
Humph akainuka huku akiongea "sijamkosea mimi "
Mama Humph akaishia kutikisa kichwa tu huku
akionekana kutofurahia tabia mpya ya Humph
iliyotokana na kufutwa kumbukumbu zake
zilizoondoka na mambo mengi mno,mpaka wazazi
wake alikuwa akiwachukulia kama jamaa wa
kawaida walio karibu yake.
鈽呪槄鈽匤ourney to the falling Mountain鈽呪槄鈽?
鈽呪槄鈽匰afari ya mlima unaoanguka鈽呪槄鈽?
"Habari za asubuhi hii ndugu wanachuo,nafurahi
kufika siku hii ambayo imerejea tena mbele
yetu,kwa wale wageni wa mwaka wa kwanza yaani
wanachuo wapya hawalitambui suala hill na itakuwa
Ni Mara yao ya kwanza kulisikia" Akatulia kidogo
Mkuu wa chuo msaidizi akitafakari usikivu wa
wanachuo kwa muda kisha akaendelea
"Tuna mashindano mbalimbali ambayo huendeshwa
na kufanyika nje ya chuo chetu yakijumuisha vyuo
vingi vinavyotuzunguka,na kawaida yetu huwa
tunafanyia mashindano haya katika kisiwa cha
falling mountain (mlima unaoanguka) pia tutakuwa
na utalii wa muda katika milima yake na misitu pia
inayosemekana kubeba utajiri mkubwa pamoja na
kishamiri maajabu mengi ya kihistoria"
Wanachuo wote wakalipuka kwa shangwe nyingi
lakini mkuu wa chuo msaidizi hakuwa amemaliza
hivyo akanyoosha mikono kuwanyamazisha
wanachuo wote
"Hatuna muda mwingi,kesho safari itaanza na
niseme tu poleni kwa kuwastukiza,natumaini
mtajiandaa kuanzia sasa" alimalizia Mkuu wa chuo
msaidizi na kuwaacha wanachuo wote wakilipuka
kwa shangwe nyingi ikiwemo Humph
Lisa hakuwa na furaha hata kidogo mbaya zaidi
alimuona Humph alivyoifurahia safari ile ikiwa si
kawaida yake kabisa.
"Mambo mdada" Lisa akistukia akisalimiwa na
alipogeuka aliduwaa kuona ni Humph,akabaki
kujiuliza ni saa ngapi mtu yule amemfikia lakini
ukweli ulibaki kuwa muda alioutumia kuzama katika
dimbwi la mawazo ndiyo muda alioutumia Humph
kufika pale.
"Poa tu" Lisa alikumbuka kuijibu salamu ya Humph
lakini akiwa mnyonge mno
"Samahani,ulisema u nani vile?" Humph aliuliza
akiwa anatazama huku na kule
"Lisa" Lisa alijibu kwa mkato huku akimtazama
vyema Humph ambaye hakujua kama binti huyo
alikuwa akimuangalia.
"Sikia binti,Jana nusura mama apasuke ulivyotoka
unalia,sasa Fanya yaishe maana hapendi kabisa
nikichokifanya kwako" Humph alisema akiwa
anamuangalia binti mmoja aliyekuwa
anatabasamu,macho yao yakagongana
"Yameisha toka Jana Humph" Lisa alijibu akiwa
hana amani
"Poa,alafu nimempenda yule mdada sijui anaitwa
nani?,hey! Vipi unamfahamu hata kwa jina labda?"
Humph alimuuliza Lisa akiwa bado anamtazama
yule binti.
Lisa hakuvumilia ule upuuzi ulioonekana dhahiri
kuwa ni dharau kutoka kwa Humph,akaamua
kuondoka kimya kimya.
Humph anakuja kugeuka baada ya kukosa
jibu,anamkosa Lisa pale alipokuwa
amesimama,akaangaza huku na kule asimuone
kutokana na uwingi wa wanachuo.