bioto
JF-Expert Member
- Oct 1, 2017
- 1,261
- 2,099
- Thread starter
- #41
Sehemu ya arobaini
★★Ilipoishia★★
Kwakuwa kila mtu alikuwa na shauku ya kutaka
kusikia kile ambacho kilimkuta Humph hawakusubiri
walianza na maswali ya moja kwa moja.
★★★Endelea nayo★★★
"Enheee!! tuambie mwenzetu ilikuwaje mpaka
ukapotea dume zima hivyo" aliuliza Sifa kwa utani
"mmmh! sifa maswali gani hayo kwa kaka yako"
aliingilia mama yao
"Sasa mama nisimuulize wakati Mimi nilikuwa
nimemkumbuka jamani kila muda nilikuwa peke
yangu tu eeeeh!" aliongea Sifa kwa sauti ya kudeka
"Aya kwani nd'o nimesema uanze kulia,ndiyo baba
ulikuwa wapi siku zote hizi?" mama wa Humph
aliamua naye kupigilia msumari kwa Humph
mzee Mandevu alimuangalia Humph kwa jicho lile
la usiseme chochote na Humph akawa ameelewa
hivyo akajifanya Kama mtu anayefikiria jibu japo ni
kweli maswali Yale yalimrudisha masaa machache
nyuma alipokuwa katika kisiwa cha giza.
Mzee Mandevu aliutumia mwanya ule wa Humph
kujifanya amezama katika mawazo lukuki na
kulimaliza swali kiakili
"Jamani nafikiri mnaiona hali ya mgonjwa jinsi ilivyo
maana ni dakika hizi hizi ametoka kuzinduka na
hatuwezi kufahamu ni mambo mangapi aliyoyapitia
huko alikotoka hivyo nawaombeni muwe wapole
walau mgonjwa wetu apumzishe akili ndipo
tumuhoji akiwa ametulia au nimesema vibaya
wajameni" mzee Mandevu alimaliza kwa mtindo huo
na kuwarushia swali la mtego
"Hapana mzee wangu upo sahihi kabisa itabidi
tumuache apumzike kwanza na badae tutapata
wasaa mzuri wa kuongea naye." alijibu mama wa
Humph akionesha kukubaliana na wazo la mzee
Mandevu
"Sawa sawa nadhani sasa twende sebuleni
tumuachie kamda kidogo apumue" aliongea mzee
Mandevu kwa uchangamfu
★★★★★★★★★★
Sor alihesabu kuwa ni siku ya tano mpaka muda ule
na kwa bahati mbaya zaidi kile kisiwa kiliitwa
kisiwa cha giza yote ni kwasababu mtu aliye nje ya
kisiwa kile hata awe na nguvu kiasi gani hawezi
kutazama yanayoendelea mle ndani ya kisiwa.
Sor alikuwa na furaha isiyo kifani maana aliamini
kuwa hakuna mtu anayeweza kuepuka mateso
yanayopatikana katika kisiwa kile,alienda moja kwa
moja mpaka
katika njia za upenyo alizojitengenezea yeye
mwenyewe wakati anaingia kisiwani mle bila
kutambulika na mtu yeyote.
Kama kawaida Sor alifanikiwa kuingia ndani ya
kisiwa kisha kwa kutumia nguvu alizojaaliwa
akaanza kumtafuta Humph mahali alipojifia,Alitafuta
sana lakini hakuambulia chochote.
Sor alipofika sehemu Fulani alipagawa kukuta watu
wakiwa wamekufa isipokuwa mmoja tu aliyekuwa
anaugulia maumivu ya mwishoni ili aungane na
wenzake walipokwenda
Sor alifika na kuwaangalia kwa makini watu wale
kitendo cha kumshika yule wa mwisho ambaye
hakuwa amekufa alipigwa shoti iliyosababishwa na
radi ile waliyopigwa kwani bado ilikuwa ikiendelea
kuzunguka mwilini mwao.
Alistuka sana baada ya kupigwa na ile shoti
akaanza kujiuliza ni kwanini watu wale wafe kirahisi
vile ikiwa hakuna mtu ambaye ananguvu ya
kuwasambaratisha isipokuwa yeye na watu wa
karibu sana na mfalme enzi zile japo tayari
walishapoteza maisha
lakini pia alitambua kwamba kwa siku ambazo
humph alikaa mle kisiwani ni wazi kuwa macho
Yale hayakuwa na nguvu tena kwani muhusika
hakuweza kuzimudu kutokana na majanga
yaliyomkumba ndani ya kisiwa kile.
Akiwa na mawazo Yale ya msimu yaliyokiharibu
kichwa chake ghafla kuna kit anakiwaza ilikuwa ni
karne kadhaa enzi za tawala zao.
Na papo hapo akakumbuka matukio mengi mno
yaliyo wahi kupita huko nyuma ikiwemo watu wenye
nguvu za kila aina walizojaaliwa na baadhi ya vita
walivyowahi kupambana na mwisho katika matukio
hayo yote
akili yake ikatua kwa mzee mmoja ambaye enzi
hizo alimvutia mno kwa mitindo yake ya upambanaji
na umaridadi wake lakini kubwa zaidi alikumbuka
jinsi ambavyo mzee huyo mwenye ndevu nyingi
pindi ni kijana
alipomsaidia wakati wa vita alipotaka kuuwawa kwa
kuwapiga wapinzani wake radi iliyotengeneza shoti
Fulani baada ya kuwapiga watu wale na kuwajeruhi
vibaya.
"mmmh! haiwezekani hata kidogo ina maana yule
Mandevu bado anaishi mpaka Leo hapana,ni kitu
kisichowezekana hata kidogo ngoja" alijiongelea Sor
akiwa haamini kilichotokea
Aliinama chini ya mwili mmoja usiokuwa na uhai
akafanya anavyojua kisha akaushika kifuani,matukio
yote yaliyotokea nyuma wakati Humph amejiegesha
pembeni ya jiwe akiwa hoi
Pia aliona jinsi watu wale wa ajabu walivyoanza
Kumsogelea Humph pale pale akaiona radi moja
matata ikipiga na kumshusha mtu,Sor akarudia lile
tukio na kuliwekea umakini hakika alifanania na
mpelelezi mmoja makini mno
Sor akaona haitoshi ni kama vile hakumuona vizuri
mtu yule aliyeshushwa na radi ya ajabu akaamua
kujiingiza katika tukio hilo na kukaa jirani kabisa na
radi ile ilipomshushia mtu yule japo pale awali
Humph aliona ni radi tu ya kawaida hakujua kama
ilimshusha mzee Mandevu.
Sor alibaki ametoa macho baada ya kumuona mzee
Mandevu akishushwa na radi ile kwa maringo tele
japo ilishuka kwa kasi na fujo zote,Hakuishia hapo
bakuli lake lilibaki wazi bila kufungwa(mdomo).
Alimfahamu vyema mtu yule hakuwahi kuwa na
utani hata chembe hasa anapotetea mahali
anapoamini kuwa anatenda haki,pia aliujua uwezo
wake fika kuwa kama unataka kupambana naye ni
lazima uwe umeshasaini kifo chako yote ni
kwasababu mzee Mandevu hakujua neno huruma
kwa adui yake na alia mini kuwa usipommaliza adui
yako basi atakumaliza wewe mwenyewe.
Kwa mara ya kwanza Sor anakiri kuwa vita
imemshinda baada ya kushuhudia kila kitu
kilichofanywa na mzee mpaka anapoondoka na
Humph.Sor alikaa chini akijiuliza nini hatima yake
kwani toka yeye alipoasi kwa mfalme na kuanza
kupambana naye ndipo walipokosana na mzee
Mandevu kisa tu mzee Mandevu alikuwa akimsaidia
mfalme Sangu.
Sor alibaki amelegea kwa mtindo huo tena
kilichommaliza zaidi ni pale ambapo alilikumbuka
jeshi lake lililoteketezwa na Humph kila alipojaribu
kuunda jeshi jipya.Kiukweli Sor alikuwa amepatikana
haswaa tena si kitoto ila kiutu uzima zaidi
★★Ilipoishia★★
Kwakuwa kila mtu alikuwa na shauku ya kutaka
kusikia kile ambacho kilimkuta Humph hawakusubiri
walianza na maswali ya moja kwa moja.
★★★Endelea nayo★★★
"Enheee!! tuambie mwenzetu ilikuwaje mpaka
ukapotea dume zima hivyo" aliuliza Sifa kwa utani
"mmmh! sifa maswali gani hayo kwa kaka yako"
aliingilia mama yao
"Sasa mama nisimuulize wakati Mimi nilikuwa
nimemkumbuka jamani kila muda nilikuwa peke
yangu tu eeeeh!" aliongea Sifa kwa sauti ya kudeka
"Aya kwani nd'o nimesema uanze kulia,ndiyo baba
ulikuwa wapi siku zote hizi?" mama wa Humph
aliamua naye kupigilia msumari kwa Humph
mzee Mandevu alimuangalia Humph kwa jicho lile
la usiseme chochote na Humph akawa ameelewa
hivyo akajifanya Kama mtu anayefikiria jibu japo ni
kweli maswali Yale yalimrudisha masaa machache
nyuma alipokuwa katika kisiwa cha giza.
Mzee Mandevu aliutumia mwanya ule wa Humph
kujifanya amezama katika mawazo lukuki na
kulimaliza swali kiakili
"Jamani nafikiri mnaiona hali ya mgonjwa jinsi ilivyo
maana ni dakika hizi hizi ametoka kuzinduka na
hatuwezi kufahamu ni mambo mangapi aliyoyapitia
huko alikotoka hivyo nawaombeni muwe wapole
walau mgonjwa wetu apumzishe akili ndipo
tumuhoji akiwa ametulia au nimesema vibaya
wajameni" mzee Mandevu alimaliza kwa mtindo huo
na kuwarushia swali la mtego
"Hapana mzee wangu upo sahihi kabisa itabidi
tumuache apumzike kwanza na badae tutapata
wasaa mzuri wa kuongea naye." alijibu mama wa
Humph akionesha kukubaliana na wazo la mzee
Mandevu
"Sawa sawa nadhani sasa twende sebuleni
tumuachie kamda kidogo apumue" aliongea mzee
Mandevu kwa uchangamfu
★★★★★★★★★★
Sor alihesabu kuwa ni siku ya tano mpaka muda ule
na kwa bahati mbaya zaidi kile kisiwa kiliitwa
kisiwa cha giza yote ni kwasababu mtu aliye nje ya
kisiwa kile hata awe na nguvu kiasi gani hawezi
kutazama yanayoendelea mle ndani ya kisiwa.
Sor alikuwa na furaha isiyo kifani maana aliamini
kuwa hakuna mtu anayeweza kuepuka mateso
yanayopatikana katika kisiwa kile,alienda moja kwa
moja mpaka
katika njia za upenyo alizojitengenezea yeye
mwenyewe wakati anaingia kisiwani mle bila
kutambulika na mtu yeyote.
Kama kawaida Sor alifanikiwa kuingia ndani ya
kisiwa kisha kwa kutumia nguvu alizojaaliwa
akaanza kumtafuta Humph mahali alipojifia,Alitafuta
sana lakini hakuambulia chochote.
Sor alipofika sehemu Fulani alipagawa kukuta watu
wakiwa wamekufa isipokuwa mmoja tu aliyekuwa
anaugulia maumivu ya mwishoni ili aungane na
wenzake walipokwenda
Sor alifika na kuwaangalia kwa makini watu wale
kitendo cha kumshika yule wa mwisho ambaye
hakuwa amekufa alipigwa shoti iliyosababishwa na
radi ile waliyopigwa kwani bado ilikuwa ikiendelea
kuzunguka mwilini mwao.
Alistuka sana baada ya kupigwa na ile shoti
akaanza kujiuliza ni kwanini watu wale wafe kirahisi
vile ikiwa hakuna mtu ambaye ananguvu ya
kuwasambaratisha isipokuwa yeye na watu wa
karibu sana na mfalme enzi zile japo tayari
walishapoteza maisha
lakini pia alitambua kwamba kwa siku ambazo
humph alikaa mle kisiwani ni wazi kuwa macho
Yale hayakuwa na nguvu tena kwani muhusika
hakuweza kuzimudu kutokana na majanga
yaliyomkumba ndani ya kisiwa kile.
Akiwa na mawazo Yale ya msimu yaliyokiharibu
kichwa chake ghafla kuna kit anakiwaza ilikuwa ni
karne kadhaa enzi za tawala zao.
Na papo hapo akakumbuka matukio mengi mno
yaliyo wahi kupita huko nyuma ikiwemo watu wenye
nguvu za kila aina walizojaaliwa na baadhi ya vita
walivyowahi kupambana na mwisho katika matukio
hayo yote
akili yake ikatua kwa mzee mmoja ambaye enzi
hizo alimvutia mno kwa mitindo yake ya upambanaji
na umaridadi wake lakini kubwa zaidi alikumbuka
jinsi ambavyo mzee huyo mwenye ndevu nyingi
pindi ni kijana
alipomsaidia wakati wa vita alipotaka kuuwawa kwa
kuwapiga wapinzani wake radi iliyotengeneza shoti
Fulani baada ya kuwapiga watu wale na kuwajeruhi
vibaya.
"mmmh! haiwezekani hata kidogo ina maana yule
Mandevu bado anaishi mpaka Leo hapana,ni kitu
kisichowezekana hata kidogo ngoja" alijiongelea Sor
akiwa haamini kilichotokea
Aliinama chini ya mwili mmoja usiokuwa na uhai
akafanya anavyojua kisha akaushika kifuani,matukio
yote yaliyotokea nyuma wakati Humph amejiegesha
pembeni ya jiwe akiwa hoi
Pia aliona jinsi watu wale wa ajabu walivyoanza
Kumsogelea Humph pale pale akaiona radi moja
matata ikipiga na kumshusha mtu,Sor akarudia lile
tukio na kuliwekea umakini hakika alifanania na
mpelelezi mmoja makini mno
Sor akaona haitoshi ni kama vile hakumuona vizuri
mtu yule aliyeshushwa na radi ya ajabu akaamua
kujiingiza katika tukio hilo na kukaa jirani kabisa na
radi ile ilipomshushia mtu yule japo pale awali
Humph aliona ni radi tu ya kawaida hakujua kama
ilimshusha mzee Mandevu.
Sor alibaki ametoa macho baada ya kumuona mzee
Mandevu akishushwa na radi ile kwa maringo tele
japo ilishuka kwa kasi na fujo zote,Hakuishia hapo
bakuli lake lilibaki wazi bila kufungwa(mdomo).
Alimfahamu vyema mtu yule hakuwahi kuwa na
utani hata chembe hasa anapotetea mahali
anapoamini kuwa anatenda haki,pia aliujua uwezo
wake fika kuwa kama unataka kupambana naye ni
lazima uwe umeshasaini kifo chako yote ni
kwasababu mzee Mandevu hakujua neno huruma
kwa adui yake na alia mini kuwa usipommaliza adui
yako basi atakumaliza wewe mwenyewe.
Kwa mara ya kwanza Sor anakiri kuwa vita
imemshinda baada ya kushuhudia kila kitu
kilichofanywa na mzee mpaka anapoondoka na
Humph.Sor alikaa chini akijiuliza nini hatima yake
kwani toka yeye alipoasi kwa mfalme na kuanza
kupambana naye ndipo walipokosana na mzee
Mandevu kisa tu mzee Mandevu alikuwa akimsaidia
mfalme Sangu.
Sor alibaki amelegea kwa mtindo huo tena
kilichommaliza zaidi ni pale ambapo alilikumbuka
jeshi lake lililoteketezwa na Humph kila alipojaribu
kuunda jeshi jipya.Kiukweli Sor alikuwa amepatikana
haswaa tena si kitoto ila kiutu uzima zaidi
