bioto
JF-Expert Member
- Oct 1, 2017
- 1,261
- 2,099
- Thread starter
- #21
Sehemu ya ishirini na moja
........Ilipoishia..........
"Humph Mimi namtaka Yule rafiki yako ambaye
aloniokoa kuna kitu natamani nimwambie tukiwa
wawili hivyo nahitaji msaada wako unikutanishe
nae" Lisa alijitetea
.......Tiririka nayo........
Humph alivyosikia hivyo akabaki na mshangao
maana ule ulikuwa ni mtihani ambao kwa mtazamo
wa kawaida si rahisi kukubaliana nao japo kwa
upande mwingine Humph aliona kama ndiyo muda
wa kumpata lisa.
"unataka kuonana nae lini na umwambie nini kwa
mfano maana hapatikani kiurahisi kama unavyoona
sasa ikibidi niagize nami nitafikisha ujumbe"
aliongea Humph akitarajia kuambiwa kile
kinachomsibu Lisa
"aaaah!! hapana hii ni siri yangu na yake Kama
hautaki kunisaidia basi yaishe" aliongea Lisa kwa
sauti iliyokata tamaa
Humph akajifikiria kwa sekunde kadhaa akaamua
akubali ombi la Lisa
"unakumbuka pale ambapo huwa tunakutana "
aliuliza Humph
"Wapi au pale katika lile daraja?" Lisa ailuliza nae
akijaribu kukumbuka eneo lile
"yap pale pale ndipo nitamwambia mkutane saa
moja usiku sawa" aliongea Humph
"Nitashukuru kama nikimuona" alijibu Lisa
★★★★★★★★★★★
Upande wa Sor mambo yalikuwa yamemwendea
kombo kila akibuni mbinu mpya inagundulika
mapema na Humph sasa muda huu alikuwa katika
pango moja kubwa akitafakari ni kitu gani cha
kufanya ili amtie adui yake mikononi.
Alifikiria sana ili apate njia mpya itakayo mtesa
vilivyo bwana mdogo Humph lakini suala
lililomuumiza hasa ni jinsi gani atakavyompata
maana watu wake wengi wanazidi kuteketea na pia
anatumia nguvu nyingi kuwatengeneza.
akiwa katika mawazo hayo ghafla akakumbuka
kuwa kuna kisiwa kimoja ambacho hakuna
binadamu mwenye uwezo wa kufika kule isipokuwa
wa jamii yao tu na endapo utatupwa huko ni shida
mtindo mmoja mpaka pale mauti itakapo kufika.
Sor aliafiki hilo wazo moja kwa moja na muda huo
huo akaanza kujipanga namna ya kumpeleka
Humph huko maana bila ujanja hawezi kufanikisha
azma yake.
★★★★★★★★★★★★★★★
Lisa alikuwa ameupara kweli kweli akiwa na shauku
ya kukutana na Humph pamoja na kijana ambaye
alimkomboa katika hatari nyingi zilizomkumba.
Alifika eneo la tukio nusu saa kabla,yote ni
kwasababu ya uhitaji wa moyo wake kuwa karibu na
mtu yule. Alikaa mno akisubiri mpaka wakati
mwingine alihisi huenda dakika zimeganda japo
hakuchoka hata chembe kusubiri kile alichoahidiwa.
Mvumilivu hula mbivu hatimaye muda uliwadia
lakini bado dalili yoyote haikujionesha kuwa Humph
au yule kijana anakuja.
Kumbe muda wote ambao Lisa anasubiri Humph
alikuwa amesimama mahali anamtazama jinsi
anavyohangaika kutoka sehemu moja kwenda
nyingine huku anaminya minya vidole vyake.
Humph hakuwa na amani juu ya kile ambacho
anaenda kuambiwa na alihisi wazi kuwa Lisa
atakuwa na mapenzi mazito moyoni mwake.
Humph alijishauri na mwisho akaamua liwalo na
liwe,akavuta kitambaa chake usoni na kofia yake
akaiweka vizuri kisha akaanza kusogea pale alipo
Lisa.
Lisa alimuona mtu akija kwa upande
wake,Hakumfikiria sana kama anaweza kuwa ni mtu
yule ampendae,baada ya Humph kusogea jirani
kabisa ndipo Lisa anamtambua na kwa kitendo cha
kustukiza anamrukia Humph kwa furaha naye
Humph bila kutegemea anamdaka kisha wanabaki
wanatazamana huku Lisa akitoa tabasamu la
ushindi.
Kwakuwa Humph alikuwa katika vazi lake la kazi
haikuwa rahisi kufahamika,Lisa anashushwa chini
taratibu kisha Humph anasogea jirani kabisa na
daraja lile akiwa na lengo la kuyatazama maji hii
ilikuwa ni kwa muonekano lakini akili yake ilimtuma
amuulize Lisa anakusudia nini bila kumtazama
usoni.
Lisa anaduwaa kwa muda akiangalia tukio
analolifanya Humph.Anaamua kumsogelea Humph
kwa mwendo wa madaha kulingana na viatu vya bei
kali alivyovaa.
Kabla Lisa hajamfikia Humph,Humph anaanza
kuzungumza kwa sauti nzito tofauti na ile sauti yake
iliyozoeleka masikioni mwa Lisa.
"Nimeambiwa na rafiki yangu wa karibu kuwa una
jambo la msingi unataka kuniambia,nipo hapa
kukusikiliza" Alifafanua Humph bila kugeuka nyuma
"Samahani kama nitakuwa nimekukwaza na
kukupotezea muda wako" Lisa akatulia kidogo
akimtazama Humph na kuendelea
"Naitwa Lisa na..na..na..?" akashindwa kumalizia
akashikwa na kigugumizi
Humph anautumia udhaifu huo wa Lisa kugeuka na
kumkazia macho ambayo yanawaka mwanga hafifu
usiotisha
"Mbona unasita Lisa niko hapa kwaajili yako nieleze
tu" Aliongea Humph kwa upole
Lisa akajipa moyo kuwa ni kheri kusema ukweli
kuliko kufa na maumivu moyoni ikiwa mtu
anayepaswa kuambiwa ukweli huo yu karibu nae na
ametahayari kumsikiliza kile akisemacho
"Usinifikirie vibaya ni moyo wangu nd'o umenituma
hili na hisia nzito nilizonazo kwako ni...." Kabla
hajamalizia kusema lile suala huku anaminya vidole
vyake kelele kubwa ikasikika kutoka upande wa pili
Ilikuwa ni sauti ya mwanamke akiomba
msaada,Humph bila kuchelewa akakurupuka na
kukimbilia eneo ambalo sauti imetokea.
Lisa alishindwa kumzuia Humph na pia kutokana na
kitendo cha Humph kuondoka eneo lile Lisa aliona
kuwa hajatendewa haki hata chembe kwani hakuwa
amemaliza kusema yaliyo moyoni mwake. Alibaki
amekaa pembeni ya daraja lile asijue nini cha
kufanya kati ya kumfuata Humph anakoenda au
amsubiri aone ni kipi kitakachotokea.
Humph alipofika eneo la tukio alishuhudia mama
mmoja akiwa anazunguka huku na kule mara ashike
kichwa nakuachia na wakati mwingine alikuwa
akipiga magoti pembeni ya bwawa linalopitisha
maji eneo lile.
Kwa ufahamu wa haraka Humph alitambua kuwa
kuna mtu ametumbukia katika bwawa lile.....
........Ilipoishia..........
"Humph Mimi namtaka Yule rafiki yako ambaye
aloniokoa kuna kitu natamani nimwambie tukiwa
wawili hivyo nahitaji msaada wako unikutanishe
nae" Lisa alijitetea
.......Tiririka nayo........
Humph alivyosikia hivyo akabaki na mshangao
maana ule ulikuwa ni mtihani ambao kwa mtazamo
wa kawaida si rahisi kukubaliana nao japo kwa
upande mwingine Humph aliona kama ndiyo muda
wa kumpata lisa.
"unataka kuonana nae lini na umwambie nini kwa
mfano maana hapatikani kiurahisi kama unavyoona
sasa ikibidi niagize nami nitafikisha ujumbe"
aliongea Humph akitarajia kuambiwa kile
kinachomsibu Lisa
"aaaah!! hapana hii ni siri yangu na yake Kama
hautaki kunisaidia basi yaishe" aliongea Lisa kwa
sauti iliyokata tamaa
Humph akajifikiria kwa sekunde kadhaa akaamua
akubali ombi la Lisa
"unakumbuka pale ambapo huwa tunakutana "
aliuliza Humph
"Wapi au pale katika lile daraja?" Lisa ailuliza nae
akijaribu kukumbuka eneo lile
"yap pale pale ndipo nitamwambia mkutane saa
moja usiku sawa" aliongea Humph
"Nitashukuru kama nikimuona" alijibu Lisa
★★★★★★★★★★★
Upande wa Sor mambo yalikuwa yamemwendea
kombo kila akibuni mbinu mpya inagundulika
mapema na Humph sasa muda huu alikuwa katika
pango moja kubwa akitafakari ni kitu gani cha
kufanya ili amtie adui yake mikononi.
Alifikiria sana ili apate njia mpya itakayo mtesa
vilivyo bwana mdogo Humph lakini suala
lililomuumiza hasa ni jinsi gani atakavyompata
maana watu wake wengi wanazidi kuteketea na pia
anatumia nguvu nyingi kuwatengeneza.
akiwa katika mawazo hayo ghafla akakumbuka
kuwa kuna kisiwa kimoja ambacho hakuna
binadamu mwenye uwezo wa kufika kule isipokuwa
wa jamii yao tu na endapo utatupwa huko ni shida
mtindo mmoja mpaka pale mauti itakapo kufika.
Sor aliafiki hilo wazo moja kwa moja na muda huo
huo akaanza kujipanga namna ya kumpeleka
Humph huko maana bila ujanja hawezi kufanikisha
azma yake.
★★★★★★★★★★★★★★★
Lisa alikuwa ameupara kweli kweli akiwa na shauku
ya kukutana na Humph pamoja na kijana ambaye
alimkomboa katika hatari nyingi zilizomkumba.
Alifika eneo la tukio nusu saa kabla,yote ni
kwasababu ya uhitaji wa moyo wake kuwa karibu na
mtu yule. Alikaa mno akisubiri mpaka wakati
mwingine alihisi huenda dakika zimeganda japo
hakuchoka hata chembe kusubiri kile alichoahidiwa.
Mvumilivu hula mbivu hatimaye muda uliwadia
lakini bado dalili yoyote haikujionesha kuwa Humph
au yule kijana anakuja.
Kumbe muda wote ambao Lisa anasubiri Humph
alikuwa amesimama mahali anamtazama jinsi
anavyohangaika kutoka sehemu moja kwenda
nyingine huku anaminya minya vidole vyake.
Humph hakuwa na amani juu ya kile ambacho
anaenda kuambiwa na alihisi wazi kuwa Lisa
atakuwa na mapenzi mazito moyoni mwake.
Humph alijishauri na mwisho akaamua liwalo na
liwe,akavuta kitambaa chake usoni na kofia yake
akaiweka vizuri kisha akaanza kusogea pale alipo
Lisa.
Lisa alimuona mtu akija kwa upande
wake,Hakumfikiria sana kama anaweza kuwa ni mtu
yule ampendae,baada ya Humph kusogea jirani
kabisa ndipo Lisa anamtambua na kwa kitendo cha
kustukiza anamrukia Humph kwa furaha naye
Humph bila kutegemea anamdaka kisha wanabaki
wanatazamana huku Lisa akitoa tabasamu la
ushindi.
Kwakuwa Humph alikuwa katika vazi lake la kazi
haikuwa rahisi kufahamika,Lisa anashushwa chini
taratibu kisha Humph anasogea jirani kabisa na
daraja lile akiwa na lengo la kuyatazama maji hii
ilikuwa ni kwa muonekano lakini akili yake ilimtuma
amuulize Lisa anakusudia nini bila kumtazama
usoni.
Lisa anaduwaa kwa muda akiangalia tukio
analolifanya Humph.Anaamua kumsogelea Humph
kwa mwendo wa madaha kulingana na viatu vya bei
kali alivyovaa.
Kabla Lisa hajamfikia Humph,Humph anaanza
kuzungumza kwa sauti nzito tofauti na ile sauti yake
iliyozoeleka masikioni mwa Lisa.
"Nimeambiwa na rafiki yangu wa karibu kuwa una
jambo la msingi unataka kuniambia,nipo hapa
kukusikiliza" Alifafanua Humph bila kugeuka nyuma
"Samahani kama nitakuwa nimekukwaza na
kukupotezea muda wako" Lisa akatulia kidogo
akimtazama Humph na kuendelea
"Naitwa Lisa na..na..na..?" akashindwa kumalizia
akashikwa na kigugumizi
Humph anautumia udhaifu huo wa Lisa kugeuka na
kumkazia macho ambayo yanawaka mwanga hafifu
usiotisha
"Mbona unasita Lisa niko hapa kwaajili yako nieleze
tu" Aliongea Humph kwa upole
Lisa akajipa moyo kuwa ni kheri kusema ukweli
kuliko kufa na maumivu moyoni ikiwa mtu
anayepaswa kuambiwa ukweli huo yu karibu nae na
ametahayari kumsikiliza kile akisemacho
"Usinifikirie vibaya ni moyo wangu nd'o umenituma
hili na hisia nzito nilizonazo kwako ni...." Kabla
hajamalizia kusema lile suala huku anaminya vidole
vyake kelele kubwa ikasikika kutoka upande wa pili
Ilikuwa ni sauti ya mwanamke akiomba
msaada,Humph bila kuchelewa akakurupuka na
kukimbilia eneo ambalo sauti imetokea.
Lisa alishindwa kumzuia Humph na pia kutokana na
kitendo cha Humph kuondoka eneo lile Lisa aliona
kuwa hajatendewa haki hata chembe kwani hakuwa
amemaliza kusema yaliyo moyoni mwake. Alibaki
amekaa pembeni ya daraja lile asijue nini cha
kufanya kati ya kumfuata Humph anakoenda au
amsubiri aone ni kipi kitakachotokea.
Humph alipofika eneo la tukio alishuhudia mama
mmoja akiwa anazunguka huku na kule mara ashike
kichwa nakuachia na wakati mwingine alikuwa
akipiga magoti pembeni ya bwawa linalopitisha
maji eneo lile.
Kwa ufahamu wa haraka Humph alitambua kuwa
kuna mtu ametumbukia katika bwawa lile.....