Simulizi: Laana Za Maiti

Simulizi: Laana Za Maiti

Shunie

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2016
Posts
157,400
Reaction score
465,165
Mtunzi ally Katalambula

Sehemu ya 01

Kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniacha hai mpaka leo hii kwa niliyoyafanya naamini sikufaa kuwa hai mpaka leo hii. Nina imani alifanya hivi ili niweze kuyasema mazito yaliyomoyoni mwangu ambayo yamekuwa mateso makuu ya moyo wangu kila kukicha.

Watu wananiona nina maisha mazuri ambayo nao wanayatamani, wananiona nacheka wakidhani nafurahia maisha. Lakini moyoni nina majuto makubwa kwa yote niliyoyafanya ambayo haikutakiwa kufanywa na mwanadamu mwenye akili timamu kama mimi.

Kama kungekuwa inawezekana maiti wakatoka juu ya kaburi ili kuonana nao basi ningepita magoti kuwaomba msamaha kwa vitendo viovu nilivyowafanyia ambavyo havikistahili tamaa ya fedha ndiyo iliyonipelekea kuyafanya yote hayo. Kila ninapoyafiria moyo hukosa amani na kutamani nizikwe nikiwa hai.

Maiti ni mwili unaotakiwa kuheshimiwa kwa vile hauna uhai hivyo unatakiwa kuhifadhiwa vizuri kabla ya kuzikwa na baada ya matayalisho yote uhifadhiwa kwa kuzikwa.

Lakini niliwageuza mradi wa kunipatia kipato ambacho kilinifanya nionekane mtu mbele ya watu bila kujua utajiri wangu nimeupata kwa njia gani.
Kama watu wangejua nilivyoupata utajiri wangu hakuna hata mmoja ambaye angenisogelea. Wapo ambao wangeweza hata kuniua kwa kunipima mawe. Kwani nilikuwa nanuka ubaya ambao naamini hata nionge vipi au nijipake mafuta yenye harufu gani uvundo nilionaohauwezi kutoka mpaka nafukiwa ardhini.

Najiuliza kwa Mungu nina adhabu gani ambayo inanisubiri kwa niliyotafanya ya kuwadhalilisha viumbe vyake alivyovitoa uhai kwa tamaa ya fedha.Nina imani toba yangu kwake hugeuka kelele ambazo asingependa kuzisikia.

Nimekuwa kila siku nikikesha nikiomba huku hela zangu zikiliwa na waganga wa jadi ambao waligeuka kimbilo langu kila mambo yaliponichachia.

Sina furaha ya mali niliyonayo kila usiku ukiingia kwangu umekuwa mateso makubwa ambayo yananifanya uchukuie usiku kwani huna nakesha bila kulala kwani kila nikifumba macho hutokewa na vitu vya ajabu sivijui ni vya dunia gani ambavyo hunitisha huku vikiyatama maisha yangu.

Narudia kama maiti wanaweza kufufuka hata kwa dakika tano basi ningewaomba msamaha kwa yote niliyomtendea kwa kutembea kwa magoti hata kuyasaga kwenye mawe kokoto au mimba yenye nchi kali ili wajue najuta kwa yote niliyowafanyia. Majuto moyoni mwangu ni makubwa naamini moyo wangu huvuja kila nikiyakumbuka.

Wanasema msamaha wa kwanza ni kwa yule uliyemkosea na kisha kwa muumba wako ambaye humalizia kwa vile hawezi kukusamehe bila kusamehewa na uliyemkosea ambaye ataendelea kuwa na kinyongo. Kama watu hau wangekuwa hai ningekwenda kuwaomba msamaha lakini wote ni marehemu na niliwafanyia yale wakiwa wafu hivyo ilikuwa vigumu kuwaomba msamaha.

Najua utajiuliza utajiri wangu niliupataje na kwa kazi gani, nakuomba uandamane na mimi ujue baadhi ya siri nzito za kutisha zilizopo chini ya jua. Kwa jina naitwa Mawazo Bwezeka. Nimezaliwa miaka 49 iliyopitanikiwa mtoto wa sita kati ya watoto kumi na tatu wa mzee Bwezeka.

Naweza kusema baba yangu alikuwa na utajiri wa watoto lakini tuliokosa elimu, maisha yetu yalikuwa ya kubahatisha kilichotusaidia kilikuwa kilimo kwani vijana wote kila asubuhi tulikwenda shambani kulima na kurudi jioni. Maisha yaliendelea huku tukiwa hatuna nyumba wala mbele.

Nakumbuka kuna rafiki yangu tuliyekuwa naye kijiji kimoja alikwenda mjini, kuna kipindi alirudi kwao huku akionesha kubadilika kwa mavazi na mwonekano. Kwa vile alikuwa mtu wangu wa karibu nilitaka kujua siri ya mabadiliko yake. Alinielezea jinsi mjini watu wanavyopata pesa.

“Mawazo, hizi nguvu ukizitumia mjini unaweza kujenga nyumba na kununua gari.”

“Kivipi?” nilimuuliza.
“Kule nguvu ndiyo kila kitu, kuna kazi nyingi ukifika utaona mwenyewe kuliko kuendelea kukaa kijijini.”
Nilikubaliana naye kwa vile baada ya kuondoka Kijijini aliporudi aliweza kuwajengea nyumba ya matofari na bati wazazi wake.

Hali ile ilinipa na mimi nguvu ya kwenda mjini.Niliamini kabisa kama ningemuomba ruhusa baba asingenikubalia kwa vile nilikuwa kipenzi chake hivyo asingekubali kuwa mbali naye.
 

Attachments

  • 20191226_051032.jpg
    20191226_051032.jpg
    47.5 KB · Views: 55
LAANA ZA MAITI

SEHEMU YA 02

Niliamini kabisa kama ningemuomba ruhusa baba asingenikubalia kwa vile nilikuwa kipenzi chake hivyo asingekubali kuwa mbali naye.

Kingine hakutaka watoto wake kwenda mjini kwani kulikuwa na sifa mbaya ya kuharibika tabia na kuiga za watu wa huko ambako wengi wao ni walevi na wizi wakati vitu hivyo kijiji vipo kama kawaida. Sikutaka kumuaga baba kwenda mjini nilipanga kutoroka.

Siku ya rafiki yangu Somati kurudi mjini, niliondoka naye baada ya kuuza mbuzi wa nyumbani kwa beirahisi ili nipate nauli bila idhini ya mmiliki ambaye ni baba yetu. Tulitimkia mjini na kufikia kwa rafiki yangu, wakati huo alikuwa na mke na mtoto mmoja na alikuwa amepanga chumba na sebule.

Nilianza maisha kwa kulala sebuleni kwa muda wa wiki moja, baadaye aliniombea kulala na watoto wa kiume wa mwenye nyumba. Niliyaanza maisha katika jiji kubwa ambalo kwangu kila nilichokiona kilikuwa kigeni. Rafiki yangu Somati alikuwa akifanya kazi ya ulinzi kwenye godauni moja.

Kwa vile mimi nilikuwa sijapitia mafunzo ya mgambo, alinitafutia kazi ya kulinda shamba la mtu lilikuwa lipo nje kidogo ya mji ambako kulikuwa na mifugo ambako nilifanya kazi ya kulinda na kukatia majani na kufanyia usafi mabanda. Mwanzo nilitegemea mshahara ambao haukuwa mkubwa kwa wakati huo lakini kwa vile sikuwahi kukamata fedha kama zile kwangu kwa wakati huo niliona kubwa.

Baada ya kuzoea maeneo yale nilianza kuuza mayai na maziwa kwa wanakijiji kwa bei nafuu na kujikuta nikipata kipato kikubwa kiasi tofauti na mshahara. Hata wakati wa kwenda nyumbani rafiki yangu Somati nilimpatia pesa nyingiawapelekee wazazi wangu.

Aliporudi alinipa shukurani za wazazi wangu japokuwa niliondoka bila kuwaaga. Somati alinieleza kuwa wazazi wangu wamefurahi sana kwa zawadi nilizowapelekea, pia walinionya nisifanye kazi zozote zisizo za halali na kama nitakosa kazi basi nirudi kijijini.
Upande wangu niliamini kwa kazi ile lazima niyabadili maisha ya familia yangu kwa kuwajengea nyumba ya kisasa kama aliyowajengea Somati familia yake.

Nilipanga kipato nitakachokipata nitawasaidia wazazi wangu kulimisha mashamba na kuwapumzisha na kilimo cha kila kukicha kiguu na njia. Nilifajirika kupata salamu nyumbani na kuonesha wazazi wangu hawakuwa na kinyongo chochote kwangu japokuwa niliwatoroka.

Niliamini dua zao njema ni mafanikio yangu katika maisha. Mwaka ulikatika nikiendelea na kazi yangu ya ulinzi ambao uliyabadili maisha yangu kiasi cha kununua kiwanja kwa siri kwani niliogopa tajiri yangu kujua angenifukuza kazi kwa kujua namwibia.

Bahati mbaya rafiki yangu kipenzi Somati alisimamishwa kazi baada ya kutokea wizi sehemu wanayolinda.Ilibidi rafiki yangu atumie pesa nyingi kutika kuhonga ili kuizima kesi ile. Mpaka anapona kifungo alikuwa amebakia na kiasi kidogo cha fedha, ilibidi aanze maisha ya kubangaiza.

Baada ya muda maisha ya Somati yalianza kuyumba na kumweka kwenye wakati mgumu, wakati huo alikuwa na mke na watoto wawili. Ilikuwa kama katupiwa gundu(mkosi) kila alilofanya lilikwenda kombo ikafikia hatua hata ya kulala na njaa na familia yake.

Ilibidi afunge safari mpaka kijiji kwangu kuja kunieleza hali yake ya maisha ilivyomwelemea. Kwa kweli roho iliniuma sana na kuona ule ndiyo muda wa kuonesha shukrani zangu kwake kwa kuniwezesha kuwa na maisha ya nafuu. Nilimwahidi kumsaidia rafiki yangu kwa nguvu zangu zote.

Kwa vile siku ile aliyokuja nilikuwa nimeuza mazao niliyokuwa nikilima mwenyewe na pia nilikuwa nimeuza mayai. Nilimpatia mihogo, viazi matunda mayai maziwa na pesa za matumizi.Somati alinishukuru sana kwa kumsaidia katika kipindi kigumu, nilimwambie yale ni malipo kwa kunitoa kijijini.

Tuliendelea na maisha ya kusaidizana kwa kipindi kirefu mpaka rafiki yangu aliponieleza amepata kazi ya ulinzi katika hospitali kubwa jijini. Nilishukuru Mungu rafiki yangu kupata kazi kwani niliamini hata akili yake ingetulia. Tuliendelea na maisha yetu huku ushirikiano ukiwa mkubwa.

Kwa vile nami nilikuwa ni haja zangu kama mwanaume shababi niliweza kumpata msichana mmoja ambaye tulianzisha uhusiano kupelekea kumpatia ujauzito uliomfanya ahamie shambani kwangu. Baada ya muda alijifungua mtoto wa kikeambaye nilimpa jina la mama yangu mzazi Kaotote.

Namshukuru Mungu maisha yaliendelea huku rafiki yangu naye akiwa ametulia kwenye kazi yake. Siku zote hakuna mtu anayefurahi mafanikio ya mtu, kuna watu walipeleka maneno ya uongo kwa tajiri yangu kuwa nauza maziwa na mayai. Mwenye mali alifanya uchunguzi na kunikamata.

Baada ya kukamatwa nauza mali ya tajiri nilifukuzwa kazina kurudi mjini, kwa vile nilikuwa akiba yangu niamini nitaweza kupambana wakati nasubiri kupata kazi nyingine. Rafiki yangu alinieleza nisiwe na wasiwasi kwa vile yeye muda ule alikuwa yupo vizuri nilitakiwa kutulia kutafuta kazi.

Nilipanga chumba na kununua baadhi ya vitu vya ndani, kwanza nilinunua godoro, viti vya ndani ndoo sufulia chache sahani. Tuliyaanza maisha na mwenetu huku nikitafuta kazi ya kufanya. Wakati huo rafiki yangu alikuwa akiendelea na kazi yake ambayo mimi niliamini ni ya ulinzi.
Lakini ajabu kwa muda wa miezi sita toke aanze kazi ya ulinzi katika hospitali ile aliweza kujenga jumba moja kubwa la gharama.

Nilijiuliza anapata mshahara kiasi gani, kiasi cha kujenga jumba kumbwa ndani ya uzito wa matofari na umeme juu na ndani ya jumba kulikuwa na kila kitu cha gharama.

Lazima nishukuru rafiki yangu kupata mafanikio, kwani vyumba alivyokuwa amepanga aliniachia na kila kitu cha ndani. Pia alinipia kodi ya miaka miwili huku akinieleza nisiwe na wasiwasi ninapopata matatizo nisiogope kumfuata. Maisha ya Somati yalibadilika haraka sana.

Nilikuwa najiuliza kazi ya ulinzi tu ndiyo iliyoyabadili maisha yake, nilikuwa na wasiwasi huenda anatumika kuivusha madawa hivyo naye kupata gawio lake. Haukupita muda Somati alinunua daladala(DCM) mbili na teksi mbili. Nilijikuta nikiwa na maswali yasiyo na majibu
 
Sehemu ya 03

Nilikuwa najiuliza kazi ya ulinzi tu ndiyo iliyoyabadili maisha yake, nilikuwa na wasiwasi huenda anatumika kuivusha madawa hivyo naye kupata gawio lake. Haukupita muda Somati alinunua daladala(DCM) mbili na teksi mbili. Nilijikuta nikiwa na maswali yasiyo na majibu.

• Kitu ambacho rafiki yangu Somatihakukisahau kilikuwa kuhakikisha ananiangalia kwa ukaribu, kila siku alinipa elfu kumi akikosa elfu. Nami nikijikuta naishi maisha kama nafanya kazi japokuwa sikufurahishwa na maisha ya kumtegemea mtu. Nami nilihangaika kutafuta kazi lakini mambo yalikuwa magumu.

• Kila baada ya mwezi rafiki yangu alifanya mabadiliko makubwa kwa kununua gari la kutembelea la gharama.Siku moja nilikosa uvumilivu na kumuuliza rafiki yangu ametumia njia gani kuyabadili maisha yake kwa haraka hivyo.
• “Rafiki yangu hapa mjini lazima akili ifanye kazi ya ziada.”

• “Sawa, nifundishe na mimi.”
• “Kazi ninayoifanya utaiweza?” swali la rafiki yangu ilinishtua sana na kuwaza mbali sana, mawazo yangu yalinipelekalabda ni jambazi anayetumia siraha kuwapora watu kazi ambayo sikuwa radhi kuifanya.

• “Akili, kazi ya ulinzi inishindenimeweza kulinda porini nishindwe mjini tena kazi yako kufungua mlango na kukagua watu,” nilijibu kwa kujiamini.

• “Mawazo, kazi ya ulinziniliiacha muda mrefu huu ni mwezi wa tisa unakatika.”
• “Unataka kuniambia mambo yote unayofanya ni kwa ajili ya kazi hiyo ya ulinzi tu?”
• “Wewe ni rafiki yangu ambaye sasa ni zaidi ya ndugu.”

• “Ni kweli.”
• “Nina imani mwanzo nilikuficha sikutaka ujue kazi yangu, lakini sina budi leo kukueleza.”
• Kauli ile ilifanya mapigo ya moyo yaende kazi kujiuliza jamaa anataka kuniambia kitu gani.

• “Ndiyo.”
• “Najua kazi ninayofanya itakushtua lakini nimejifunza katika maisha usichague kazi ambayo mwenzako anaweza kuifanya.” Alitulia kidogo kumeza mate na kuendelea kusema.
• “Mawazo nafanya kazi kuhudumia maiti Mochwari.”

• “Eti?” Niliuliza kama sikusikia alichokisema.
• “Unashtuka nini?”
• “Sishtuki ila naona kama sikusikia vizuri.”

• “Sasa hivi nafanya kazi chumba cha maiti (mochwari).”
• “Mmh!” nilijikuta nikiguna huku nimeshikilia tama.

• “Unaguna nini?”
• “Mmh! Kazi ya kutunza chumba cha maiti si mchezo yataka akili zilizofyatuka.”

• “Siyo kufyatuka.”
• “Nasikia kazi ile ni ngumu maiti inaweza kuamka au nasikia huwa kuna vitu vya ajabu hutokea kwenye chumba hicho wewe unavikabilije?”
• “Nimekueleza tokea mwanzo, kazi anayoiweza mwenzako basi wewe isikushinde.”

• “Sawa lakini kazi hiyo mmh!”
• “Ya kawaida kama kazi nyingine ngumu mwanzo ukiizoea nakuhakikishia utaipenda.”

• “Utani huo yaani mtu anaipenda kazi ya kuhudumia maiti?” sikuamini.
• “Ndiyo, mbona ya kawaida tu kama kazi nyingine.”
• “Somati unanitania hiyo siyo kazi iliyokuingia kipato kikubwa kuna kazi nyingine.”

• “Mawazo yako tu, tena nimekumbuka kesho alfajiri njoo hospitali ukifika njoo moja kwa moja chumba cha maiti utanikuta kuna kitu nitakupatia ukae nacho mimi nitakipitia kwako.”

• “Mmh! Sawa, sasa hiyo kazi ya Mochwari inahusiana vipi na uwezo wako wa kifedha?” bado nilikuwa sijapata jibu la kuniridhisha.

• “Ukija kesho utajua kila kitu.”
• “Sawa.”
• Sikutaka kuuliza zaidi nilikaa kimya na kusubiri hiyo kesho alfajiri niweze kuujua uwezo wake wa kifedha anaupataje.
 ***

• Siku ya pili nilidamka saa kumi za usiku na kujiandaa, wakati huo rafiki yangu alikuwa ameninunulia baiskeli ya kisasa. Nilianda baiskeli yangu kuelekea hospitali, nilitumia dakika arobaini kufika hospitali. Baada ya kuingia ndani ya hospitali nilielekeachumba cha maiti.

• Kutoka getini hadi chumba cha maiti lazima uzunguke majengo wa wodi, nilitembea taratibu huku nikiwa siamini. Nilipokaribia chumba cha maiti mochwari kwa pembeni ya mlango wa kuingilia chumba cha maiti kulikuwa na kiti kuonesha ni cha rafiki yangu, kabla sijafika mlangoni kiti kile.

• Nilishtushwa na sauti ya kitu kikisukumwa nilipoangalia upande wa sauti inapotokea niliona kitanda kikisukumwa kuelekea kwenye mlango wa mochwari, Nilipoangalia vizuri niligundua walikuwa wakiupeleka mwili wa mtu aliyefariki kwa ajili ya kuuhifadhi kabla ya kuchukuliwa na familia yake.

• Walikuwa wauguzi wawili wa kike walipofika mlangoni waligonga, baada ya dakika chache mlango ulifunguliwa na kumwona rafiki yangu Somati ambaye aliwasaidia kukisukuma kitanda kukiingiza ndani kilichokuwa na mwili wa mtu aliyeonekana amefariki usiku wa kuamkia siku ile.

• Baada ya dakika kama kumi hivi wauguzi walitoka na kitanda kitupu kurudi wadini.Baada ya dakika kama kumi nyingine Somati alitoka akiwa na sigara mkononi, alikaa kwenye kiti chake na kuvuta taratibu.

Nilisogea karibu yake na kushtuka kuniona.
“Aah! Mawazo karibu.”
• “Asante.”
• Nilipomwangalia vizuri niligundua koti alolikuwa amevaa lilikuwa na damu.
• “Nina imani utaamini sasa kazi yangu, hiki ni chumba cha kuhifadhia maiti.”

• “Mmh! Mbona koti ulilovaa lina damu?”
• “Mmh! Leo ndugu yangu kumeletwa maiti kumi na mbili za ajali ya Hiace, hivi nilikuwa na kazi ya kuzipanga kwani zingine hazitamaniki ukiziangalia kama una moyo mdogo huli nyama kwa mwezi mzima.”
• “Mmh! Unajua siamini naona kama nipo ndotoni.”

• “Ndoto za nini, hapa ndugu yangu hapa ndipo panaponipa jeuri yote hiyo.”
• “Kwani mshahara wake kiasi gani?”
• “Lakini mbili.”
• “Lakini mbili?”

• Nilishtuka kusikia mshahara wake lakini mbili, kwa muda aliokuwa kazini mshahara wake bila matumizi yoyote kama angeuweka ni shilingi milioni moja na laki mbili. Lakini maisha ya rafiki yangu yalikuwa zaidi ya milioni mia moja na zaidi. Lakini sikutakiwa kuuliza swali kwa vile nilielezwa niendepale muda ule ili nijue kipi kimempa jeuri ya kufanya anavyotaka.

• “Yaani mimi hapa moyo unanitetemeka unawezaje kuzizoea maiti?”
• “Kuzizoea kivipi kwani kuna muda wa kuzungumza nazo? Mwanadamu akiisha lala utakapo mweka huna kazi nyingine mpaka muda wa watu watakapokuja kuchukua ndugu yao au asiye na ndugu kuchukuliwa na jiji kwa ajili ya kwenda kuwahifadhi.”

• “Mmh! Lakini yataka moyo.”
• “Nina imani tunaongelea nadhalia kuliko vitendo, hebu ingia ndani uione kazi yangu.”

• Japo moyo ulikuwa ukitetemeka nilikubali kufuatana na Somati hadi ndani chumba cha maiti ambacho kilikuwa kikitisha kutokana hali ilivyokuwa ndani. Chini kwenye sakafu kulikuwa na maiti zaidi ya kumi zilizopata ajali zilikuwa zimefunikwa shuka lililokuwa limelowa damu.

• Somati alichukua tambala na ifafio mrefu na kuifuta damu iliyokuwa ikitoka katika maiti zile kisha alisogea karibu na kufunua ile shuka kidogo nikimbie ilikuwa maiti ya mwanaume aliyekuwa amefumuka kichwa kwa ajali.

Nilihisi kichefuchefu kutokana na harufu hali ya damu mbichi.
• “Mbona hawa wapo chini?” nilijikaza na kumuuliza.

• “Nafasi katika droo zimejaa, pia hizi zinazovuja damu huwezi kuziweka kwenye kabati, zinawekwa chini ili kuziacha zivuje damu kisha baadaye zinaziwekwa katika friji.”

• “Huogopi?”
• “Nimekuambia kazi yoyote anayoifanya mwanadamu mwenzako usikubali ikushinde.”

“Kwa siku unapokea maiti ngapi?”
• “Hakuna idadi maalumu kwa vile sina mawasiliano na anayepanga kifo anachukua roho ngapi kwa siku.”

• Kutokana harufu kali ya Mochwari ambayo ilinifanya nijisikie kama nataka kufa baada ya kujiona kama sipumui nilimwomba tutoke nje ya chumba kile kwani kila muda nilikuwa najisikia vibaya tofauti na mwenzangu yeye alikuwa katika hali ya kawaida.

Tulitoka nje ya chumba cha maiti huku nikiziacha pua zangu kuvuta hewa safi baada ya kuwa kwenye hali mbaya. Baada ya kutulia Somati aliniambia:
 
Sehemu ya 04

Tulitoka nje ya chumba cha maiti huku nikiziacha pua zangu kuvuta hewa safi baada ya kuwa kwenye hali mbaya. Baada ya kutulia Somati aliniambia:
“Nina imani umeiona kazi yangu?” alisema huku akifungua kichupa kidogo cha kinyagi na kunywa kidogo.

“Nimeiona lakini bado naona maluweluwe.”
“Ya nini?”
“Bado siamini kazi hii ya mshahara wa laki mbili uwe kwenye hali uliyonayo kwa sasa.”

“Nitakujibu jioni, la muhimu chukuahuu mzigo niliokuitia nitaukuta kwako.”
Kwa vile sikuhitajikuwa eneo lile kutokana na hali yangu kubadilika kwani toka nilivyoiona maiti iliyopata ajali nilikosa amani moyoni mwangu. Nilijiuliza Somati ana moyo mgumu kiasi gani kuziona maiti kama kitu cha kawaida.

Nilichukua mzigo alionipa na kuondoka zangu kurudi nyumbani huku njiani nilijiuliza kama mimi kuona mtu mmoja tu nimechanganyikiwa nilijiuliza kama ningewaona wote kumi sijui ingekuwa kwenye hali gani, kila dakika nilihisi kichefuchefu na kutema mate ovyo.
Nilipofika nyumbani kwa vile nilitoka usikuusiku nilioga na kupanda kitandani, usingizi haukuchelewa kunichukua.

Usingizini niliiota ile maiti moja kati ya kumi niliyooneshwa na Somati ya mtu aliyopata ajali. Nilijikuta nikiweweseka na kupiga kelele kitu kilichomshtua mke wangu.
“Vipi mume wangu leo una nini?”
“Ha..ha..pana,”nilijikuta nikibabaika huku akitweta na jasho kumtoka.

“Kwani mume wangu umeota nini?” Mke wangu aliniuliza huku akiwa amesimama pembeni ya kitanda. Macho yangu yalikutana na mwanga mkubwa wa nje kuonesha kumekucha kitambo, nilijiuliza nimepiga kelele kiasi gani.
“Kwani umesikia nini?” nilimuuliza mke wangu.

“Nilikuwa nje sauti yako kama umekutana na shetani imenitisha sana na kuingia nimekukuta akihema huku jasho likikutoka hebu niambie umeona nini mume wangu,” mke wangu alinibembeleza kwa shauku ya kutaka kujua nimeota nini.

“Niliota nataka kugongwa na treni,” nilitengeneza uongo ili kuficha kilichonitisha usingizini.
“Pole mume wangu.”
“Asante.”

Mke wangu aliniletea maji ya kunywa ili kuipoza hofu, baada ya kunywa maji, nilimuuliza mke wangu:
“Muda huu ni saa ngapi?”

“Saa nne asubuhi.”
“Ooh! Kumbe nimelala sana.”
“Labda uchovu wa kudamka alfajiri.”
“Vipi shemeji amekuja?”

“Mmh! Sijamuo...”
Mazungumzo yetu walikatishwa na hodi iliyokuwa ikibishwa mlangoni, mke wangu alikwenda hadi mlango wa sebuleni na kumsikia akisema:

“Karibu shemeji.”
Kauli ya kukatibishwa mgeni ilininyanyua kitandani na kukaa, nilitulia kwa muda mpaka mkewe wangu alipokuja kunieleza.
“Mume wangu shemeji amekuja.”

Sikutaka kuuliza shemeji gani kwa vile mtu aliyekuwa amezoeleka kwangu ni rafiki yangu Somati, nilinyuanyuka nikiwa nimejifunga kanga ya mke wangu na kutoka chumbani, nilimkuta Somati amejaa tele sebuleni.

“Karibumzee.”
“Asante, za muda?”
“Mmh! Nzuri.”
“Mbona umelala sana?”
“Si unajua nilitoka usiku.”

“Tuachane na hayo, naomba ule mzigo.”
Nilikwenda chumbani na kuchukua mfuko alionipa Somati na kumpelekea, baada ya kupokea na kuingiza mkono kwenye mfuko ule na kutoa bunda la noti na kunikabidhi.

“Za nini?” nilimuuliza.
“Za kwako kwa kazi uliyoifanya.”
“Kazi! Kazi gani?” nilishtuka.
“Kwani umeamka saa ngapi?”
“Usiku.”

“Ukaenda wapi?”
“Nikaja kwako.”
“Basi ndiyo kazi uliyofanya leo.”
“Asante.”
“Basi mi’ nikuache upumzike tutaonana jioni.”
“Sawa, unataka kuniambia zote hizo ni pesa?”

“Ina maana hukuziangalia?”
“Walaa, sikuwa na idhini ya kupekua.”
“Ni pesa, na hii ndiyo biashara inayoyabadili maisha yangu.”
“Duh! Sasa pale una biashara gani?”
“Tutazungumza jioni.”
“Sawa.”

Somati aliaga na kuondoka na kuniacha nimekaa sebuleni pesa zangu mkononi, nilinyanyuka na kurudi chumbani. Nilipofika chumbani nilifungua burungutu nililopewa na Somati na kuzihesabu noti zile. Sikuamini zilikuwa shilingi milioni moja taslimu.

Nilijiuliza kama burungutu moja ni milioni moja mule kwenye mfuko zipo kiasi gani. Nilijikuta nikiwa na maswali yasiyo na jibu juu ya fedha nyingi kiasi kile ambazo nilikwenda kuzichukua kwa Somati. Nilijiuliza kuna biashara gani iliyopo pale hospitali.

Kutokana na kuchanganyikiwa na kiasi kikubwa cha fedha nilijikuta nimesahau niliyokutana nayo mochwari na kubakia moja la rafiki yangu kupata kiasi kikubwa cha fedha huku nami nikiingusa milioni kwa mara ya kwanza. Nilijikuta nikiwa na shauku ya kutaka kujua rafiki yangu anapataje kiasi kikubwa cha fedha wakati kule mochwari hakuna biashara yoyote.

Mazingira ya kazi yake hayakuonesha dalili zozote ya kuwa na kitu cha kumuingia fedha nyingi kiasi kile. Lakini niliamini majibu ya maswali yangu nimeyapata kwa Somati mwenyewe jioni ya siku hiyo. Nilijikuta mwenye mawazo mengi juu ya matumizi ya fedha niliyopewa na rafiki yangu.

Nilimwita mke wangu na kumwelea kuwa nimepewa fedha na Somati, akiwa katika hali ya kutoamini wingi wa fedha alinipa ushauri wa kununua kiwanja. Wazo la mke wangu nililiunga mkono na kupanga kutafuta kiwanja kwa ajili ya kujenga nyumba angalau chumba na sebule.

Pamoja na mipango yote bado akili yangu ilikuwa kwenye fumbo la kutaka kujua Somati anapata wapi fedha nyingi kama ile na kwa biashara gani. Nilijikuta nikikosa raha kusubiri kujua siri ya fedha za rafiki yangu. Mwanzo nilidhani labda ana fedha za ndagu kutokana na jinsi alivyokuwa akijiweka.

Somati alikuwa halingani na uwezo wake wa kifedha, gari zake alikuwa akipanda mkewe na watoto yeye alikuwa akipanda mpaka sehemu kuanzia hapo hupanda daladala mpaka kazini.

Lakini nilipofika kazini kwake na mzigo alionipa ulibadiliwazo la kutumia ndagu. Niliamini kama si ya haramu nami lazima nijiunge naye ili niyabadili maisha yangu ambayo muda wote yalikuwa tegemezi kwa kumtegemea rafiki yangu. Nilisubiri muda ufike nipate jibu la fumbo langu.

***
Siku zote jioni kabla ya kuingia kazini tulikuwa tunakaa pamoja mpaka saa mbili usiku ndipo huondoka kwenda kazini na mimi kurudi nyumbani. Muda huo huwa tunazungumza mengi huku tukipata vinywaji vikali japo sikuwa mnywaji kama Somati lakini nami nilikuwa mwanachama.

Toka mambo ya Somati kuwa mazuri alikuwa akinywa pombe kali, lakini jibu la unywa pombe kali nililipata ilitokana na kazi yake ambayo kama una moyo mdogo huwezi kuifanya. Kwangu siku moja nilichanganyikiwa mpaka kuota mchana bila kunywa pombe unaweza kutoka mbio.

Lakini siku ile tulipokutana nilikuwa nataka kujua kule mochwari anafanya biashara gani iliyokuwa ikimuingizia kipato kikubwa kiasi kile.Pia nilitaka kujua kipi kilichomvutakufanya kazi ngumu kama ile ambayo kwa mtu kama yeye mpaka kuikubali.

Kwa kweli nilivyokuwa nikimfahamu Somati na kazi niliyomuona anaifanya haikuwa rahisi kukubali mara moja. Lakini aliamini siku ile ningepata majibu ya maswali yasiyo na jibu yaliyouzunguka ubongo wangu. Kama kawaida tulikutana sehemu yetu lakini siku hiyo tulikaa meza ya pembeni tofauti na tuliyoizoea.
Kama kawaida tuliagiza vinywaji vyetu kwa mimi kuagiza bia na mwenzangu kuagiza konyagi kubwa.

Kila mmoja alimimina kinywaji chake kwenye glasi na kunywa taratibu, lakini Somati alikunywa glasi nzima kwa mtindo wa tarumbeta kisha alirudisha glasi tupu juu ya meza na alitikisa kichwa kuonesha imefika sehemu yake huku mishipa ya kichwa ikimsimama na macho kugeuka rangi.

Alifuta mdomo kwa kiganja cha mkono na kuniangalia kwa macho makali kitu kilichonitisha na kunifanya nimuulize.
“Vipi, mbona hivyo?”

“Mmh! Imefika kwenyewe, unajua rafiki yangu kila siku nakueleza kazi anayoifanya mwanadamu mwenzako wewe usikushinde. Mwanzo nilikuwa na mawazo kama yako lakini nilikutana na mtu mmoja aliyenibadili akili yangu na kuwa na mtazamo mwingine kabisa ambao nataka na wewe kuanzia leo ubadili mtazamo wa mawazo yako na kuhamia dunia ya upambanaji.

“Najua uwezo wangu wa kipesa umekushangaza kwa vile nimelipuka kama bomu, pia leo alfajiri kuna kitu umekiona ambacho najua kimekuchanganya sana?”

“Ni kweli, unajua mpaka sijui pale kuna biashara gani yenye kukuingia fedha nyingi kiasi kile pia uliwezaje kuipata lkazi kama ile na nini kilikusukuma kuifanya kazi ile?”
Kabla ya kujibu Somati alicheka kidogo na kupuga funda la konyagi bila kuitia kwenye glasi na kusema:

“Kwanza ningependa kukueleza mwanadamu tumeumbwa na moyo wa uoga ambao umekuwa siku zote ukiturudisha nyuma katika kutafuta mafanikio. Lakini amini siku zote mwanadamu akiondoa woga mafanikio huwa usoni mwake. Kwa kweli wakati nikiwa nafanya kazi ya ulinzi nilikuwa nakutana na watu wengi.

“Baada ya matatizo ya kikazi na kukaa benchi, nashukuru rafiki yangu hukunitupa ndiyo maana leo nipo pamoja na wewe sitakuacha katika hali yoyote kwa vile nafahamu umuhimu wako kwangu.Si wewe tu wapo watu niliowasaidia wakati nikiwakazini kabla ya kusimamishwa.

“Nakumbuka nilikutana na jamaa yangu mmoja Titonilikuwa nikifanya naye kazi siku za nyuma ambaye naye alifukuzwa kama sisi. Baada ya kufukuzwa hakuacha kutupitia washkaji zake pale alipokuwa hana kitu nasi tulimtoa kiaina. Baada ya muda alipotea ghafla, hatukujua amekwenda wapi.

Baada ya miaka miwili kukatika wakati huo nipo benchi, siku moja jirani yangu kulikuwa na msiba, mimi nilikuwa mmoja wa watu tuliofuata mwili wa marehemu hospitali. Tulipofika chumba cha kuhifadhia maiti nilishtukakumkuta rafiki yangu Timo akiwa ndiye mhudumu wa chumba cha maiti.

Kilichonishangaza alikuwa mtu mwenye afya nzuri na kitambi juu, aliponiona alishtuka na kunishangaa nilivyokuwa kwani nilipoteza haiba ya zamani niliyokuwa nayo wakati nina kazi nilipungua na kuwa kama mgonjwa. Baada kutupatia mwili wa marehemu tuliyemfuata aliniita pembeni na kuniuliza kulikoni au naumwa.

Sikumficha nilimweleza kila kitu kilichonitokea kama kilichomkuta yeye, alinionea huruma na kunipa pole. Aliniuliza kama bado nipo nilipokuwa nakaa zamani nilimweleza bado nipo pale ila nilikuwa nina mpango wa kukirudisha chumba kimoja baada ya mambo kuwa magumu kila kukicha.

Bila kutegemea alinieleza nimsubiri, alikwenda ndani na kutoka na bahasha ya kaki aliyonipa na kunieleza akitoka kazini atakuja tuzungumze.Niliipokea bila kujua kuna nini japo mawazo yangu yalinipelekea labda kuna pesa. Tuliuchukua mwili wa marehemu na kuupeleka msibani kwa ajili ya maandalizi ya mazishi jioni ya siku ile.

Kwa vile tulikuwa tunazika jioni nilirudi nyumbani mara moja huku nikiwa na shauku kujua kwenye bahasha kuna nini.Nilipoingia ndani niliifungua bahasha, nilishtuka kukuta kuna shilingi laki mbili taslimu. Huwezi kuamini nami nilishtuka kama wewe kwani mtu kunipa laki mbili kipindi kile tena afya yake ilikuwa nzuri na kitambi juu tofauti na pale tulipokuwa pamoja kazini.

Nilimpa mke wangu pesa ya kula kisha nilirudi msibani huku nikiwa na hamu ya kuonana na rafiki yangu. Muda mwingi nilikuwa mtu wa mawazo juu ya hali ya rafiki yangu Timo pia kufanya kazi yenye kutisha kama ile ya kuhudumia maiti. Mwanzo hata mimi nilikuwa naogopa maiti pengine kushinda hata wewe.

Lakini nilibadilishwa mawazo na kuiona kazi ya mochwari ni kazi kama kazi nyingine na maiti wanahitaji kuhudumiwa na wanadamu na si malaika japo ilikuwa vigumu, lakini maneno ya ujasiri niliyopewa yaliondoa woga moyoni mwamngu na leo nina maisha mazuri kama unayoyaona.

Basi nilikuwa msibani lakini mawazo yote kwa rafiki yangu,” rafiki yangu Somati aliendelea kunieleza sababu zilizomwingiza kwenye kazi ya hatari kama ile wakati mimi nilikuwa najua yeye ni mlinzi.

“ Basi rafiki yangu, majira ya saa moja na nusu usiku Tito alifika nyumbani, nilimpokea na hakuwa mgeni nyumbani kwani alipokuwa na shemeji yako naye alimshangaa jinsi alivyokuwa kwani alikuwa na afya nzuri yenye kuonesha maisha mazuri. Kwa hali aliyokuja naye Tito ilionesha maisha hayana fomula.
Baada ya muda aliomba tusogee pembeni kwa mazungumzo, tulikwenda kwenye grosary iliyokuwa jirani.

Tulitafuta meza ya pembeni ambayo ilikuwa imejitenga na nyingine.
Tuliagiza vinywaji mwenzangu aliagiza konyagi mimi niliagiza bia, baada ya ukimya mfupi huku tukiendelea kunywa, Tito aliniita jina langu.

“Somati.”
“Naam.”
“Kwanza pole kwa matatizo.”
“Asante, ni sehemu ya maisha ya mwanadamu.”

“Ni kweli, lazima nami nirudishe shukurani zangu kwenu, waswahili wanasema kipande cha muhogo wakati wa njaa si sawa na biriani wakati umeshiba.Kidogo mlichonisaidia wakati nikiwa na shida si sawa na nilichokupa leo. Nina imani ulishtuka kupotea kwangu ghafla?”

“Ni kweli, wazo langu nilijua labda umepata kazi na upo bize ndicho tulichokuwa tukiomba wote siku moja mwenzetu uwe na maisha mazuri.”

“Ni kweli, lakini amini usiamini nilijiona nimegeuka ombaomba hivyo nikaona kama nawasumbua pili hata mimi niliona kama hadhi yangu inapungua. Nikaona kuna umuhimu wa kurudi kijiji. Kuna siku niliwaomba fedha kuwa mke wangu anaumwa, ile pesa mliyonipa ndiyo niliyofanya nauri ya kurudi kijijini mimi na familia yangu.

“Kwa kweli maisha ya kijijini yalikuwa magumu sana hasa nikizingatia niliisha zoea mjini. Lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kujipanga upya ili nirudi mjini na kuiacha familia yangu kijijini ili nije peke yangu.

Maisha ya kijiji ilikuwa kila kukicha afadhali ya jana, lakini sikuwa na jinsi kwani hata pesa ya nauli ilikuwa tatizo.
“Siku moja nilikutana na mzee mmoja jirani yetu aliyekuwa akiishi mjini, alishangaa kuniona nipo kijijini wakati tulishawahi kukutana mjini.

Hali aliyonikutana nayo ilikuwa ikisikitisha nlikuwa nimebakia mfupa na ngozi.Aliniuliza nina mpango gani na maisha yangu.
“Nilimweleza nikipata fedha ningerudi mjini kwani kuendelea kuwa kijijini ni kupoteza dira ya maisha.

Yule mzee alisema anaweza kunipa nauli lakini mjini nitafanya kazi gani? Nilimweleza yoyote nikifika mjini sitachagua kwa muda ule. Basi alinieleza kuwa kuna nafasi moja ya kazi kama nikiweza nitaondoka naye siku ya pili. Kwa kweli kauli ile ilikuwa faraja kubwa moyoni mwangu.

“Nilimshukuru yule mzee kwa kuwona kama Mungu wa duniani japosikujua ni kazi gani nakwenda kuifanya. Kutokana na muonekano wake niliamini kazi yake ni nzuri, baada ya makubaliano niliagana na familia yangu kuwa nimepata kazi mjini.Familia yangu ilifurahi na kuwaeleza baada ya hali kutulia ningewafuata.

“Siku ya pili niliondoka na mzee Kubo hadi mjini ambako tuliwasilia majira ya saa mbili usiku na kufikia kwake. Alikuwa na nyumba kubwa lakini hakuwa na mke ila alikuwa na msichana wa kazi na watoto wake watatu ambao walikuwa wakubwa mmoja alikuwa ameolewa na wadogo walikuwa chuo.

Siku ya pili mzee Kubo aliondoka asubuhi kwenda kazini na kuniacha na msichana wa kazi na kurudi usiku majira ya saa tatu usiku.Baada ya chakula tulikaa nje ya nyumba peke yetu, yule mzee alikuwa mvutaji mzuri wa bangi alivuta kwanza kama misokoto miwili kisha tulipata muda wa kuzungumza.

Alianza kuonesha furaha usoni mwake kitu kilichongeza matumaini moyoni mwangu, kisha aliniita jina langu.

“Tito.”
“Naam.”
“Mambo yamekwenda vizuri kazi utaanza kesho.”
“Asante mzee wangu Mungu atakulipia kwa kila akifanyacho,” nilitamani kumlamba miguu.

“Najua kazi yenyewe itakushtua, nataka uyaweke moyoni haya nitakayo kwambia, chochote anachokiweza kukifanya mwanadamu mwenzako wewe kisikushinde hasa ukiwa mtoto wa kiume.

Ni kosa kubwa kuchagua kazi kwa kuyaogopa macho ya watu au kuamini ya watu fulani.”
Nilijiuliza ni kazi gani hiyo ambayo ilinitisha ambayo ilianza kutangulizwa taadhali.

“Ndiyo nimekuelewa, ni kazi gani hiyo?”
“Ni kazi ninayoifanya mimi na ndiyo iliyonipa maisha haya.”

“Sawa mzee, ni kazi gani mbona unanitisha?” Nilijikuta nikiingia wasiwasi huenda ni kazi ya ujambazi ambayo sikuwa radhi kuifanya japo wenzangu wanaiweza.

“Mimi ni mhudumu wa mochwari.” Timo alishtuka.
“Eti umesemaa!” nilimsikia lakini sikumwelewa.
“Mimi ndiye mhudumu mkuu wa chumba cha maiti.”
“Sasa mimi nimekuja kufanya kazi gani?”

“Kazi ninayoifanya mimi ndiyo utakayoifanya wewe.”
“Mzee, yaani mimi niwe mhudumu wa maiti?”
“Ndiyo.”
“Mzee kwa nini hukuniambia toka nyumbani nisingekuja huku.”

“Nilijua ningekueleza mapema usingekuja, lakini haya ndiyo maisha unatakiwa kujitoa na kupambana. Kilicho mbele yako ni wasiwasi wa moyo, lakini ile ni kazi kama kazi nyingine nakuhakikishia ukiizoea hutaiacha.”
“Nisiiache kwa sababu gani?” Timo alimshangaa mzee Kubo.

“Mshahara wake kwanza ni mkubwa, pia una malupulupu kutoka kwa watu wanaofuata marehemu wao. Wengine wapo wanaotaka maiti wao kuoshwa lazima watakupa pesa, kijiwe kikichanganya kuna siku unatoka na la laki mbili mpaka tatu.

Kila siku pesa ya chini kutoka nayo tofauti na mshahara elfu ishirini umekosa nini?”
“Mzee, ile kazi ni ngumu yataka moyo wa chuma mtu kukaa na kiume kisicho na uhai yataka moyo.”

“Najua ni wasiwasi umekutawala lakini nakuhakikishia kabla ya kukukabidhi kazi peke yako tutakuwa pamoja nitakufundisha taratibu utaielewa na kuiona ya kawaida tu.”

“Mmh! Sijui kama nitaiweza,” nilijikuta kwenye mtihani mzito maisha mwangu.
“Narudia kazi anayoiweza mwenzako wewe isikushinde.”
“Ni kweli lazini kazi ya mochwari mmh! Hapana.”

“Mawazo, hata mimi siku ya kwanza nilikuwa kama wewe, haya maneno aliyo yasema Timo ndiyo niliyo mwambia mwanzo aliponiomba niifanye kazi ile na kuachana na kazi yangu ya ulinzi.Niliona kama ni maneno tu ya kwenye kanga lakini baada kukomaa nilithibirisha kauli yangu,” Somati alisema na kuendelea kunipa mkasa wa rafiki yake Timo.

Basi rafiki yangu Somati aliendelea kunieleza jinsi rafiki yake Timo alivyoweza kuingia kwenye kazi ya uhudumu wa chumba cha maiti:
“Basi rafiki yangu Timo aliendelea kunielezea mkasa wake na kusema: Mzee Kubo aliweza kunishawishi na siku ya pili nilikwenda kazini huku nikiwa mtu niliyejaa aibu na woga.

Aibu ilikuwa kwa watu kuniona nafanya kazi ya mochwari, woga wa kukaa na maiti. Siku ile nilifanya kazi kama msaidizi, kazi kubwa aliifanya mzee Kubo kama kuweka maiti kwenye droo na kumsaidia kuzipanga.
 
Sehemu ya 05

Siku ya pili kama kawaida nilikutana na rafiki yangu Somati kwenye bar ya jirani na kuzungumza mawili matatu kisha yeye alienda kazini. Baada ya kukutana aligundua siku ile sipo kwenye hali nzuri aliponidodosa nilimweleza ukweli.

“Rafiki yangu kazi naitaka lakini siyo ile ya kutunza maiti, ndoto imenionesha kuna jambo mbaya mbele yangu.”
“Mawazo acha kujitoa akili, tokea lini ndoto ikawa na ukweli?”

“Hii inaweza kuwa na ukweli.”
“Mawazo, ndoto wakati mwingine huwa si ukweli, wengi huota wameokota fuko la pesa lakini asubuhi wakiamka ujikuta na umaskini wao. Acha kuishi kwa kuangalia ndoto,kama ungeota umekufa usingenyanyuka kitandani?”
“Nitanyanyuka.”

“Basi achana na ndoto pambana mwanaume, kazi ninayotaka kukuachiaunaweza ona ya mchezo lakini pale ni sawa na mtu kukuachia shimo la madini ukichimba lazima upate utajiri.”
Somati aliendelea na ushawishi wake na kuufanya moyo wangu kujaa ujasiri na kujikuta nikijisema: Sitatishika na kitu nami nitapambana mpaka pumzi zangu za mwisho ili kujitoa kwenye umaskini ili niache kuwa tegemezi.
***
Siku iliyofuta nilianza kazi nikiwa chini ta rafiki yangu, siku ya kwanza tulipokea maiti moja ya mtoto mdogo. Sikupata shida kuiweka kwenye droo za kuhifadhia maiti zenye ubaridi ili kuifanya maiti isiharibike. Saa tisa za usiku nikiwa nimejilaza rafiki yangu Somati alinifuata na kutaka tutoke nje.

Nilifanya vile kwa kuongozana naye hadi nje ya ofisi yetu, alisogea pembeni hadi tukawa tumekiacha chumba cha maiti kwa miguu ishirini hivi. Tulifika nyuma ya wodi ambako tulimkuta mtu mmoja.
“Za saizi kaka?” yule mtu alinisalimia.
“Zuri tu kaka.”
“Mawazo, huyu ni ndugu yetu anaitwa kindevu.”

“Nimefurahi kumfahamu.”
“Kidevu, huyu ni ndugu yetu anaitwa Mawazo, ni zaidi ya ndugu. Ndiye mtakayefanya naye kazi kipindi mimi sipo ,nina imani mtakwenda vizuri kwa sababu yeye ndiye mimi.”

“Nashukuru kumfahamu, akiwa kama wewe nina imani hakitaharibika kitu.”
Tulipeana mikono huku nikiwa bado sielewi kitu gani kinachoendelea, sikutaka kuuliza kwa vile nilijua mengi ningeelezwa na Somati.

“Mawazo, hawa ndiyo watu wa kufanya kazi nao, ukienda vizuri muda si mrefu maisha yako yatabadirika.”
“Sawa hakuna tatizo,” nilijibu bila kujua kilichokuwepo.

“Basi bwana kindevu ule mzigo tuangalie kesho, wiki hii si nzuri.”
“Hakuna tatizo ukipatikana nijulishe, yaani ukipata tunapiga hela nzuri.”
“Nina imani wiki hii mambo yatakuwa mazuri.”

“Sasa mimi niwaache mfanye kazi tutaonana,” Kindevu alisema huku akiingiza mkono mfukoni na kutoa pesa ambazo alihesabu na kunipatia.
“Kaka tatufanya kazi.”
“Asante,” nilipokea na kuziweka mfukoni bila kuhesabu.

Baada ya kuondoka tulirudi kazini na Somati huku akili zangu zikinituma yule ni mfanyakazi mwenzetu. Baada ya kukaa Somati alinieleza:

“Rafiki yangu huyu ni mmoja ya watu utakaofanya nao kazi, hawa ndiyo wanaotuweka mjini. Jeuri yote unayoiona ni kwa ajili yao, hivyo ukienda nao vizuri maisha utayaona tambarale.”
“Kwani wao wapo upande gani hapa hospitali?”
“Hawa hawafanya kazi hapa bali ni watu wanaokuja kuchukua bidhaa kwenye kazi yetu.”

“Bidhaa gani?”
“Unajua kuna watu huwa wanahitaji viungo vya binadamuwaliokufa, vipo vinauzwa elfu hamsini laki mpaka milioni. Kuna vitu vingine vya pesa ndogondogo kama maji ya maiti, uchafu wa michwari kuna watu huja kununua kwa bei ya elfu kumi mpaka ishirini.”

“Mmh!” niliguna baada ya kujua biashara yenyewe.
“Usigune umeisha ingia kwenye kazi changamkia tenda maisha yakiwa mazuri achana nayo kula raha.”

“Kwa hiyo wakifika nawakatika kiungo anachotaka?”
“Hapana wanakata wao.”
“Sasa ukimkata maiti kiungo ndugu zao wakija wakati wa kuosha si watagundua mapungufu kwenye mwili wa marehemu?”

“Kuna aina mbili za utoaji wa viungo, maiti zisizo na ndugu zinazozikwa na jiji, hizo unakata kama kawaida. Lakini zenye ndugu hukata mwenyewe kimazingara na mwili wa marehemu kuonekana upo kawaida.”

“Mmh! Kazi ipo.”
“Si kazi, ikiizoea utaona ya kawaida tu.”
“Lakini Somati uharamu wa kazi unaanzia hapa, huoni kama ni kuitafuta laani kukata viungo vya maiti?”
“Kazi hiyo hufanyi wanafanya wao, hata ukikataa kuiifanya wewe wataifanya wao wenyena kukuacha ukifa maskini.”
“Wataifanya vipi wakati sijawaruhusu.”
“Kichawi.”

“Mbona unanipa mtihani mzito.”
“Kwani jamaa kakupa kiasi gani?”
Bila kujibu niliiingiza mkono mfukoni na kutoa pesa nilizipewa na kindevu, nilizihesabu na kukuta laki moja.
“Laki moja.”

“Unaona hujafanya kazi umepwa laki moja, nilivyokueleza huu ni utajiri nilikuwa na maana yangu nawe umefika tu umepata lakini bila kazi yoyote.”
“Mmh! Unajua umeniingiza kwenye mtihani mzito.”

“Wasiwasi wako, asilimia kubwa ya matajiri unaowaona hawana utajiri wa halali na maisha yao yanaendelea.”
“Lakini kufanya hivyo ni kumkosea mwenyezi Mungu.”
“Mawazo, nataka kuuliza kitu, hivi unakumbuka ulifukuzwa kazi kwa sababu ya gani?”

“Ya fitina za watu.”
“Nataka useme ukweli, kwa sababu gani?”
“Nilikuwa nauza maziwa.”
“Lilikuwa kosa au siyo kosa?”
“Ni kosa kwa vile niliuza bila idhini ya mwenye mali.”

“Kuiba ni dhambi siyo dhambi?’
“Ni dhambi.”
“Sasa nataka kukueleza hakuna dhambi ndogo wala kubwa lolote ukilifanya kinyume na maamlisho ya Mungu ni dhambi.”

“Lakini hii ya kuuza viungo ni kubwa zaidi.”
“Walaa, sikiliza hebu acha mawazo ya woga, mimi nimefika hapo kutokana na ujasiri, mwanzo kazi ilinishinda lakini niliyekuwa naye alinitia moyo na sasa nakula maisha.”

“Kwa vile nakuheshimu nitafanya, lakini ikinishinda nitanyanyua mikono.”
“Baada ya wiki tu itazoea nami nitakuwa nawe kwa mwezi.”

Siku ziliendelea huku nikianza kuzoea kidogokidogo, kuna siku walikuja watu ambao Somati alifahamiana nao. Baada ya kusalimiana kama kawaida aliwatambulisha kwangu kuwa watafanya kazi na mimi baada ya yeye kusafiri. Tulitambuana na kupeananamba za simu.
“Vipi?” mmoja ya watu waliokuja aliuliza.
“Mambo yapo kama tulivyo panga,” Somati alijibu.

“Kila kitu kipo tayari?”
“Nilifikilia hamji kwa vile hakukuwa na mawasiliano toka jioni.”
“Kaka mkubwa, si nilikueleza umuhimu wa kitu hicho.”
“Poa basi tupe dakika tano kila kitu kitakuwa tayari.”

“Poa.”
“Mawazo tuingie ndani kidogo.”
Tuliingia ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti, rafiki yangu aliniuliza:
“Eti zile maiti zinazotakiwa kuzikwa kesho zisizo na ndugu tuliziweka wapi?”
“Upande huu.”
“Ile niliyokueleza uiwekee alama unakumbuka droo yake?”
“Hii hapa.”

Nilimuonesha droo yenye mwili wa maiti iliyoiwekea alama ilikuwa maiti ya mwanaume mwenye mshipa (busha) ambaye alikaa hospitali kwa miezi sita bila kuwa na ndugu na alipofariki alitakiwa azikwe na jiji. Tulivaa gloves na kuifungua droo na kuitoa maiti ile iliyokuwa kwenye shuka.

Tuliilaza sehemu ya kuoshea maiti kisha Somati alikwenda ofisini na kurudi na kisu kikubwa kiasi, wakati huo nilikuwa tayari nimemuondoa nguo zote na kumlaza chali. Alipofika aliniambia nishike lile busha nami nilifanya kama nilivyoelekezwa. Baada ya kulishika alikata na kuliondoa na sehemu zake za siri.

Wakati akizikata nilifumba macho kwa woga mpaka alipomaliza kuzikata alinieleza nizitie kwenye mfuko. Niliziweka kwenye mfuko kisha alinawa na kuvua floves na kutoka na mzigo ule ambao tuliwapelekea wale watu. Baada ya kuwapa walitupa bahasha kisha waliondoka.

Baada ya kuondoka tulirudi ofisini kwetu na kutoa kilichokuwemo kwenye mfuko, zilikuwa noti za elfu kumikumi.

“Zihesabu,” Somati aliniambia.
Nilizihesabu na kukuta zipo milioni moja, nilinyanyua macho kumtazama Somati na kuamini lazima atanipa kifuta jasho japokuwa kazi kubwa aliifanya mwenywe.Nilijua sikosi laki moja au mbili, lakini baada ya kuzihesabu aliniuliza:

“Zipo shilingi ngapi?”
“Milioni moja.”
“Si unajua mimi ndoyo naacha kazi na wewe ndiye utakaye bakia?”
“Ndiyo,” nilijibu huku moyo wangu ukijua kabisa Somati anataka kuchukua zote kwa vile anataka kuacha kazi.

“Na sasa hivi mwenye kazi hii ni wewe hivyo hela yote iliyoingia leo ni yako.”
“Eti?” nilimsikia lakini sikumuelewa.
“Nasema hiyo milioni yote ni yako mimi sitaki hata senti tano.”

“Kwa nini na kazi umefanya wewe?”
“Mawazo, pesa mimi ninayo na kuna pesa itaingia kesho ambayo nilifanya biashara na mtu ambaye alisafiri kaniambia amerudi kesho nitakuwa na zaidi ya milioni kumi.”

“Ha! Sasa kwa nini unataka kuacha kazi yenye pesa hivi?”
“Mawazo, pesa haiishi utamu, nilichochuma kinatosha sasa ni zamu yako nawe kuyabadili maisha yako na familia yako.”

“Basi nashukuru sana ndugu yangu.”
“Na hiyo milioni kumi nikizipata nitakupa tatu ukatafute kiwanja na uanze ujenzi mara moja.
“Hakuna tatizo ndugu yangu.”
****
Sikuzilikatika nikizidi kuizoea kazi huku tamaa ya fedha ikinitawala na kujikuta nami nikiwaza mambo makubwa kama ya rafiki yangu ambaye wakati huo alikuwa na nyumba zaidi ya nne na gari tano. Ilikuwa haipiti siku mbili bila kuingiza fedha ambayo iliongeza ujasiri moyoni mwangu.

Nakumbuka siku moja Somati alikuwa akiumwa, siku hiyo nilikwenda kazini peke yangu, japo nilikuwa na woga wa kuifanya kazi ile peke yangu, lakini pia niliomba Mungu watu naokuja kununua viungo vya maiti wasitokee siku ile kwani niliamini nisingeweza kumkata kiungo maiti.

Nashukuru siku ile hakukuwa na mtu yeyote aliyekufa wala kutokea wale watu wenye kuhitaji kitu chochote kutoka kwenye chumba cha maiti. Siku iliyofuata pia Somati hakutokea nilikwenda kazini peke yangu. Siku ile kulikuwa na maiti nne za wanawake wawili, mtoto mmoja na mwanaume mmoja.

Kwa vile walikuwa freshi nilizipokea na kuwaweka kwenye friji na kuendelea na kazi mpaka asubuhi. Kwa siku mbili nilizofanya kazi peke yangu nilijikuta nikijenga kujiamini. Siku ya tatu Somati alikuja kazini tulifanya kazi kwa muda mfupi ilipofika saa sita aliniaga kuwa anarudi kupumzika.
“Mawazo, mi naondoka ila naomba unijulishe maiti zitakazo ingia usiku wa leo.”

“Hakuna tatizo.”
“Halafu aliyekuachia zamu alisemaje kuhusiana na maiti ya yule mjamzito ambaye kachelewa kupata ndugu?”
“Amesema ni mmoja wa watu watakaozikwa kesho na jiji.”
“Duh! Pesa hiyo.”

“Inasikitisha kweli, nasikia kumbe alikuwa na mimba ya mapacha.”
“Mawazo, hela hiyo tena kuna watu nawapigia simu sasa hivi tunafanya biashara.”

“Ukiwakosa je?”
“Hakikisha unampoza jamaa elfu ishirini ili asiitoe kwenye maiti zinazotakiwa kwenda kuzikwa.”
“Yule mtu wangu, jamaa ni mwelewa sana.”

Ilikuwa maiti na mwanamke mjamzito aliyefariki kwa kugongwa na gari majira ya usiku na maiti yake kuokotwa barabarani siku ya pili asubuhi. Taarifa za kuokotwa mauti ya mwanamke mjamzito ilitangazwa zaidi ya siku nne bila kuonekana ndugu yake.

Hivyo hospitali waliamua ikazikwe na jiji, baada ya kuamliwa kuzikwa na jiji, Somati aliwasiliana na watu waliotoa oda kutaka baadhi ya viungo vya mwanamke mjamzito ikiwa pamoja kiumbe kilichokuwemo tumboni kila kimoja kilikuwa na bei yake.
 
Sehemu ya 06

Ilikuwa maiti na mwanamke mjamzito aliyefariki kwa kugongwa na gari majira ya usiku na maiti yake kuokotwa barabarani siku ya pili asubuhi. Taarifa za kuokotwa mauti ya mwanamke mjamzito ilitangazwa zaidi ya siku nne bila kuonekana ndugu yake.

Hivyo hospitali waliamua ikazikwe na jiji, baada ya kuamliwa kuzikwa na jiji, Somati aliwasiliana na watu waliotoa oda kutaka baadhi ya viungo vya mwanamke mjamzito ikiwa pamoja kiumbe kilichokuwemo tumboni kila kimoja kilikuwa na bei yake.
Somati alitoka nje kuzumgumza na simu kisha alirudi na kusema:

“Jamaa nimewapata, kama nilivyokueleza bei ya kila kiungo utawasikiliza wanataka viungo gani.”
“Sawa, lakini naona kama siwezi kuvikata.”

“Wataka wenyewe.”
Kabla ya kuondoka tuliiweka vizuri maiti na mwanamke ambayo ilikuwa ikitakiwa baadhi ya viungo.Kisha aliondoka na kuniacha nikiendelea na kazi, huku hali ya kujiamini ikiongezeka. Majira ya saa tisa za usiku nilishtuliwa na simu yangu, niliamka na kuipokea.

Aliyepiga aliniuliza kama Mawazo ni mimi, nilimjibu ndiyo mimi, niliuiliza kama nilikuwa na ujumbe wowote kutoka kwa Somati.

“Ujumbe gani?” niliwauliza sikutaka ujiingiza kingi.
“Kuhusu kufanya biashara na wewe.”
“Ooh! Sawa.”
“Tupo nje ya uzio wa hospitali.”
“Mwambie mlinzi mnakuja kwangu.”
“Sawa tunakuja.”

Baada ya muda walikuja watu wanne ambao niliwapokea, katika makubaliano ya biashara wao walisema wanamtaka mtu mzima bila kukatwa kiungo chochote. Hapo kidogo sikuelewa niwauzie kiasi gani. Kwa vile bei ilinichanganya nilimpigia simu Somati aliyenieleza bei yake ambayo ilinitisha na kuona kama hawataweza kuitoa.

Baada ya kuelezwa niwauzie kiasi gani, niliwaeleza kiasi kinachotakiwa kwa maiti nzima.
“Ha! Mbona nyingi sana.”
“Ndiyo bei yake,” nilijibu kwa mkato.
“Tutakupa nusu yake.”

“Sikilizeni kuna watu wamepiga simu wanataka mali hii kwa mara moja na nusu yenu, lakini tumewakatalia kwa vuke tayari tuliisha kubaliana na ninyi. Kama kiasi hicho hamna sio lazima siku nyingine akipatikana na ninyi mkiwa na hiyo pesa tutafanya biashara.”

Baada ya kuwaeleza vile walisogea pembeni na kuzungumza kwa muda kisha walirudi na kusema watatoa. Nilimuingiza mmoja ndani kuangalia biashara yetu na kukubaliana nayo. Walinipa kiasi tulichokubaliana na wao walisogeza gari na kuchukua mwili wao.

Nilimpigia simu Somati kuwa nimefanya biashara kwa fedha tuliyokubaliana.
“Fedha hiyo unayo?”
“Ndiyo.”
“Nina imani umeuona utajiri, kuna baadhi ya maiti ukiwa nayo ni biashara nzuri.”
“Kwa hiyo nikitoka kazini nitakuja kwako ili ufanye mgao.”

“Wa nini?”
“Wa kazi iliyofanyika.”
“Mawazo, hiyo ni kazi yako wewe, sasa hivi ndiyo upo kazini rasmi, jumatatu nakupeleka kwenye uongozi ili uajiliwe kabisa na utambulike kama mfanyakazi.”
“He! Ina maana ndiyo umeacha kazi?”
“Ndiyo maana yake, ningekueleza naacha kazi najua ungeingia wasiwasi.”

“Basi nikupehata kidogo.”
“Somati mimi pesa ninayo wewe ndo’ unaanza maisha hivyo hakikisha kiasi kidogo unapeleka nyumbani na kinachobakia unafanya mambo ya maendeleo.”

“Nashukuru ndugu yangu.”
“Kingine kila unachokifanya iwe siri yako pia hutakiwi kuishi maisha ya kujionesha kwa watu. Fanya haraka maliza nyumba yako ili uondoke kwenye macho ya watu waliokuzoea.”
“Sawa kaka nitafanya hivyo.”
****

Siku ya jumatatu Somati alinipeleka kwenye uongozi wa hospitali, nilipokelewa na kuajiliwa kama mhudumu wa mochwari nikiwa na mkataba wa mfanyakazi wa hospitali hiyo niliyetambulika mpaka serikalini. Mshahara nilitajiwa japo haukuwa mbaya sana, lakini niliamini kwa biashara ninayoifanya sitaugusa zaidi ya posho ya kazi yangu ambayo nilijikuta nikiipenda.

Nilijenga nyumba kwa muda mfupi kisha nilihama ushwahili na kuhamia kwangu rasmi.Mke wangu alishangazwa na mabadiliko yangu ya ghafla kama moto kwenye majani makavu. Siku moja tuliwa tumekaa aliniuliza swali juu ya utajiri wangu.
“Mume wangu samahani kwa nitakalo kuuliza.”

“Bila samahani,” nilijibu bila kujua mke wangu anataka kuniuliza nini.
“Mume wangu kwanza nashukuru kwa kuyabadili maisha yetu ambayo nilikuwa nikiyaota kwenye ndoto.”
“Ni kawaida tu.”
“Lakini mume wangu kuna kitu nataka kujua.”

“Kitu gani?”
“Mume wangu, siamini kazi ya ulinzi ndiyo iliyokupa maisha haya, nina imani kuna kitu cha ziada hebu niweke wazi nijue mume wangu una kitu gani kinginetofauti na kazi ya ulinzi?”
“Mke wangu shida yako ni maisha mazuri au kujua nafanya kazi gani?”
“Pamoja na maisha mazuri, lakini lazima niijue kazi ya mume wangu.”

“Nauza madawa ya kulevya.”
“Ha! Mume wangu kazi gani huyo ukishinwa si utafia gerezani?”
“Mwenye pesa hata siku moja hafungwi.”
“Mume wangu kwa nini umeingia kwenye biashara haramu?”

“Mke wangu naomba kuanzia leo sitaki swali lolote la kijinga, nimekupa maisha mazuri tulia ule maisha kama yamekuchosha unaweza kuondoka. Kuna watu wanateseka kuyatafuta maisha mazuri wewe unayapata unataka kujifanya unajua kuyachunguza. Nikisia swali lolote kama la leo ujue talaka yako inafuata.”

“Basi mume wangu nisamehe nimekoma.”
“Na ibakie siri yako nikiisikia nje nitajua ni wewe.”
“Mume wangu nakuahidi itabakia siri yangu.”
Japo nilijisikia vibaya kumkalipia mke wangu lakini niliamini ile ilikuwa njia sahihi ya

kumnyamazisha.
****
Niliendelea na kazi yangu ya kuhudumia maiti huku nikiyabadili maisha ya familia yangu kijijini kwa haraka sana. Kijijini kwetu mimi na Somati ndiyo familia zatu zilikuwa na maisha mazuri. Niliendelea kumshukuru rafiki yangu kwa kuweza kuyabadili maisha yangu.

Kazi nayo iliendelea kama kawaida huku nikizidi kuizoea hata kuwajua wateja wenye fedha nyingi na wenzangu na mimi ambao walikuwa wakitoa pesa za kwenyea bia kama elfu kumi mpaka hamsini. Wengi walikuwa wakinisaidia kufanya usafi kwa kufuata uchafuwa mochwari hata sanda zenye damu ambazo siku za nyuma nilikuwa nikizichoma moto.
Lakini zilikuwa na wateja wake ambao walipenda sanda zenye damu ambazo niliuza mpaka laki moja.

Wapo waliofuata uchafu wa kabati la kuhifadhi maiti, sikujuawalichukuauchafu ule kwa ajili gani. Wengine walichukua maji ya kuoshea maiti, mwanzo nilikuwa namwaga baada ya kuosha maiti lakini toka nilipojua dili nikawa naweka kwenye dumu la lita tano tano na kuuza.

Niliuza maji kwa lita kila kipimo kilikuwa na bei yake, haikuishia hapo wapo waliokuwa wakija na kulala ndani ya chumba cha maiti mpaka asubuhi kwa ajili ya masharti ya mganga. Walikuwa hawalali bure, aliyekuja kwa kazi hiyo mganga aliyemleta ambaye huwa mteja wangu anayenunua bidhaa toka kwenye idara yangu hulipa kiasi cha fedha.

Baada ya siku kukatika kijiwe kikaanza kuwa kibaya pamoja na kuwepo maiti wengi lakini wateja walipotea. Nilijikuta nikikata miezi miwili nikipata elfu kumi ikizidi elfu hamsini wakati nilizoea kwa wiki lazima nishike laki tano mpaka milioni. Pamoja kuwa nilikuwa na pesa ndani lakini nilianza kuingiwa wasiwasi wa kazi kuwa mbaya.

Mwezi wa tatu ulikatika hali ikiwa ileile huku kazi niiona ngumu hasa baada ya kufuruliza kwa ajalimbaya zenye maiti za kutishakutokana na mwisho wa mwaka ulikuwa na ajali nyingi. Hata ile biashara ya sanda zenye damu nayo ilidoda nilikaa nazo mpakanikazichoma moto.

Hali ile ilinitisha sana na kuamua kumfuata Somati. Nilimkuta akiwa mtu wingine baada ya kufungua bar kubwa ambayo ilikuwa ikijaza watu wengi na baadhi ya dawa za kujaza watu alichukua kazini kwangu.

Baada ya mazungumzo mafupi nilimgusia kilichonitokea kwa miezi mitatu. Baada ya kunisikiliza alitulia ameshika kichwa na kusema:
“Kuna mteja yoyote umegombana naye?”

“Mmh!” nilijifikiria kwa muda kuwaza nani nimekwazana naye kazini kwangu lakini sikukumbuka.
“Hapana,” nilikataa.
“Kumbuka, lazima kuna mtu ulikwaruzana naye kumbuka.”

“Mmh!” nilirudisha kumbukumbu nyuma na kukumbuka kuna mzee alifuata maji ya maiti na kunipa pesa kidogo na kumnyang’anya. Pamoja na kusema kuwa nitaona bado sikuamini kama angenifanyia kituchochote kibaya kwa vile ni yeye aliyekuja na pesa kidogo.

Nilimweleza Somati nilivyo kwaruzana na mzee mmoja baada ya kuja na pesa kidogo kutaka maji ya maiti kwa kutoa elfu moja kitu nilichokichukulia kama dharau kwangu. Lakini nilikumbuka pamoja na kusema yale sikumjibu kitu chochote. Baada ya kumwambia vile alisema:

“Hiyo ndiyo sababu, wazee wale hutafuta chokochoro ili kumkomoa mtu, lakini tutawakomesha.”
“Tutafanya nini?”
“Nitakuelekeza kwa mzee mmoja ukifika mwambie wewe ni ndugu yangu nina imani atakusaidia.”

“Sawa.”
Somati baada ya kunipa moyo niliondoka na siku iliyofuata nilikwenda kwa huyo mtaalamu aliyekuwa akikaa nje ya mji. Nilipofika na kumweleza kuwa mimi ndugu yake Somatialifurahi sana na kuniuliza:
“Aloo! Huyo bwana hajambo?”

“Hajambo.”
“Mmh! Karibu sana.”
“Asante.”
‘Mmh! Unatatizo gani?”
Nilimweleza tatizo langu lililonipeleka pale, baada ya kumweleza matatizo yangu aliangalia katika ramli na kusema kama Somati nimechezewa na wachawi baada ya kuonekana mwepesi hivyo walitumia mwanya huo kuingia mochwari na kufanya wanavyotaka.

“Kama vipi?”
“Sasa hivi wanaingia ndani na kujichukulia wanachotaka bila kizuizi na wewe kubakiaukilinda maiti bila faida yoyote.”

“Sasa utanisaidiaje?”
“Ni kuwadhibiti.”
“Kivipi?”
“Wakifika wasiweze kuingia hivyo lazima wakuone wewe, pia hata kukuondolea kiza walichotupa kwenye kazi yako ndiyo maana hupati pesa kwa sasa.”
“Nitashukuru sana.”

Aliniambia gharama yake ambayo ilinitisha sana na kuomba kupunguziwa.
“Kijana hii kazi ninayoifanya nawachokoza watu, naingia kwenye vita na wachawi na kuuza uhai wangu lazima watanitikisa lakininitapambana nao. Kama unaona gharama wakati unaingiza mamilioni unaweza kuacha.”

Kutokana na hali niliyokuwa nayo nilikubaliana nagharama zake japo zilikuwa za juu. Aliingia kwenye kazi ya kunisafisha nyota usiku alikuwa kutegua mabomu ya wachawi na kuondoa kiza kwenye kazi yangu na kunieleza nitaona mabadiliko baada ya siku mbili.
***
 
Sehemu ya 07

Baada ya kufanya dawa za kuzuia wachawi ambao walikuwa wameanza kunifanya niyaone maisha magumu ya kukosa wateja huku wao wakichukua viungo vya maiti au maiti wa nyama kwa njia ya kichawi bila mimi kujua. Siku ya kwanza baada ya zoezi lile nikiwa kazini kama kawaida nilishtuka kusikia sauti za watu wakitembea mbele ya ofisi lakini ajabu sikuwaona.

Baada ya muda nilisikia mlango wa kuingilia chumba cha maiti ukifunguliwa, lakini ajabu nyingine pamoja na kusikia ukifunguliwa bado kwa macho yangu mawili niliuona upo vilevile nilivyoufunga tena kwa funguo. Hali ile ilinitia woga kwani toka nianze kazi sikuwahi kusikia kitu kama kile.

Kama mganga angenieleza kuwa siku ile ndiyo wachawi wanakuja kuchukua maiti au viungo vyake ningekubali lakini ilikuwa tofauti kwani siku alizosema kuwa walikuja kuchukua maiti au viungo vyake hakukuwa na kelele zozote ajabu ni siku ile ambayo niliamini kweli wachawi walikuja kuchukua maiti.

Lakini kilichoni shangaza wakati hajafanya dawa hakukuwa na kitu cha kutisha lakini siku aliyoweka dawa palitokea mambo ya ajabu. Nilijiuliza hiyo kinga aliyosema mbona haifanyi kazi matokeo yake wachawi ndiyo wamekuwa wakinitisha na kuamini kama hali ile itaendelea kazi nitaiona chungu kwani vitisho vile ilitakiwa uwe na moyo wa chuma.

Nilitaka kuingia chumba cha maiti ili nione kuna nini kinaendelea baada ya kusikia mlango ukifunguliwa. Lakini wasiwasi wangu ulikuwa kama watu wamepita sikuwaona nikiwafuata ndani wanaweza kunifanyia kitu kibaya.

Niliamua kubaki palepale huku nikimuomba Mungu kukuche haraka ili nitoke kazini na kwenda kwa mganga kumweleza kilichotokea nikiamini dawa zake zimeshindwa kuzuia wachawi zaidi ya kunitisha.

Baada ya muda nilisikia droo ikivutwa ndani, nilijua ndiyo wanachukua maiti. Wasiwasi wangu ulikuwa kama watachukua maiti ya mtu na kuondoka nayo nini nitawaeleza nini wenye maiti yao ambao wanajua ipo kule baada ya kukabidhiwa na muuguzi aliyethibitisha kifo chake na maiti kuletwa kwangu.
Kingine kilichonitisha kama hao wachawi watachukua viungo toka moja ya maiti nitaeleza nini baada ya kugundulika ina viungo pungufu. Kwa kweli nilikuwa kwenye wakati mgumu, nikiwa katikati ya dimbwi la mawazo nilisikia madroo yakifungwa. Nilijua tayari wamechukua walivyofuata na kuniachia msala mzito.

Nilisikia mlango wa mochwari ukifungwa na sauti za miguu zikisogea upande wangu, lakini nilitulia ili nisijulikane nimesikia kwa vile mchezo ule waliufanya muda mrefu hivyo wangepita bila kunifanya kitu. Niliwasikia wakizungumza wenyewe tena mbele yangu wakiwa wananiangalia.

Nami nilitulia tu kwa kuhofia huonesha kushtuka wangenifanya kitu kibaya lakini mapigo ya moyoyalikuwa juu. Hawakuwa na nguo mwilini walikuwa wanawake sita na wanaume wanne. Mmoja alisema:
“Mmh! Ina maana wameisha ichukua ile maiti yao?”

“Waichukue waipeleke wapi ikiwa nasikia mazishi ni leo,” mwingine aliochangia.
“Sasa atakuwa amemweka wapi?”
“Hapo ndipo panapo nichanganya.”
“Halafu kuna kitu mmegundua?”
“Kitu gani?”

“Chumba kizima hakina maiti hata mmoja.”
“Kweli jamani hata mimi nimeshtuka, tena nimekasilika au wamefanya usafi?”
“Tokea lini chumba cha maiti kikifanyiwa usafi maiti wote wanatolewa, na kama wametolewa wamewekwa wapi?”

“Yaani si unajua mama Kinena alikuwa anataka uume wa mtoto mdogo kwa ajili ya kumfunga mumewe, nimekosa hela hivihivi,” mmoja alisema kwa sauti ya kusikitika.
“Si wewe mbona ile maiti ya mtoto tungeigawana mimi nilikuwa nimefuata kiganja cha mtoto.”

“Mmh! Leo imekula kwetu.”
“Jamani twende mbele na nyuma ile si hali ya kawaida lazima kuna kitu.”
“Ina maana ameshtuka?”
“Ndiyo maana yake, niliwaeleza tusimfungie kazi yake bali tuendelee na kazi yetu ya kuchukua maiti na viungo bila mwenyewe kujua. Kama ameshtuka itakuwa imekula kwetu.

Lazima naye alihangaika na kutukuta ni sisi tumemfanyia mchezo ule.”
“Mmh! Na kweli, lakini mbona haoneshi dalili zozote za kushtuka tulivyompita ndivyo tulivyomkuta.”
“Jamani tukafanye uchunguzi kilioni tutajua yote na wengine alfajiri muwe hapa kuja kipi kinaendelea kama kuna watuwamefuata maiti zao.”

“Sawa.”
Waliondoka na kuniacha nikiwa na wasiwasi mwingi, kilichonishtua sana ilikuwa kauli yao kuwa ndani hakukuwa na maiti yoyote wakati droo zilijaa mpaka wengine wanne niliwalaza chini. Sikwenda haraka ndani ya chumba cha maiti nilisibiri nusu saa kwa kuhofia kuna mtu ananiwinda kuona nitafanya nini.

Baada ya nusu saa ya ukimya nilinyanyuka nikiwa sijiamini na kwenda kuuvuta mlango la mochwari ambao niliuona mgumu. Niliuvuta kwa nguvu lakini ilionesha umefungwa. Nilitoa funguo na kufungua, nilipoingia ndani nilikuta maiti wapo kama kawaida .


Sikuridhika nilikwenda kufungua kwenye droo nako kulikuwa na maiti kama nilivyo ziweka. Nilijiuliza wao walikuwa wakitaka maiti gani ambayo hakuonekana mule ndani. Lakini kauli zao zilioonesha hawakuiona kitu chochote na kufikiri labda kumefanyika usafi na kuzihamisha maiti zote.

Nilirudi kwenye kiti changu kuendelea na kazi, nilipata wazo la kumpigia simu Somati kumwelezea kilichotokea. Lakini ajabu simu yake ilikuwa haipatikani kitu ambacho hakikuwahi kutokea kwa Somati. Namba zake zote zilikuwa hazipo hewani, lakini nilipanga nikitoka kazini nianzie kwa mganga kisha kwake.

Asubuhi baadaya kukabidhi kazi nilitoka kazini na kuelekea kwa mganga kumweleza kituko cha usiku ili nimsikie ataniambia nini japo majibu nilitakiwa kupeleka baada ya siku mbili kuwa nimeona au kusikia nini. Nilipofika hakushtuka kuniona alinikaribisha, niliingia ndani na kwenda moja kwa moja kilingeni.

Kilichonishangaza siku ile hakukuwa na wagonjwa kabisa tofauti na siku zote, muda ule huwa kuna wagonjwa wengi lakini sikutaka kuuliza.
“Karibu.”
“Asante.”
“Mbona leo badala ya kesho?”
Nilimweleza kilichonitokea usiku, baada ya kunisikia alicheka kidogo na kusema:
“Nilifanya vile ili uone kazi niliyofanya, bila hivyo ungejua kazi yetu ni uongo.

Waganga wengi tunadharaulika hivyo basi nina imani jibu umelipata baada ya kuwaona wachawi waliokuwa wakikufanyia mchezo ule.”
“Nimewaona, mbona wameweza kuingia mpaka ndani?”
“Nilifanya vile makusudi kwa vile nilijua hawafanyi kitu.”

“Kwa hiyo?”
“Usiku wa leo utapata majibu mengine, japo wameshindwa lakini hawakubali lazima watarudi wakijiuliza wameshindwa wapi.”
“Utakuja?”
“Walaa, nitakupa dawa ya kumwaga ndani ya chumba na nyingine kuzunguka chumba cha maiti.”

“Sawa.”
Baada ya mazungumzo mganga alinipa dawa ya kutega ofisini kwangu, niliaga na kuondoka. Nilirudi nyumbani mapumziko ya kukesha kazini, nilioga na kujitupa kitandani. Niliamka jioni na kujiandaa kwenda kazini, kabla ya kwenda kazini nilipitia sehemu kushtua akili.

Muda ulipofika nilikwenda kazini kama kawaida, majira ya saa nne usiku niliweka dawa niliyopewa na mganga. Niliweka dawa kama nilivyoelekezwa, baada ya zoezi lile niliendelea ma kazi kama kawaida kwa kujipumzisha ofisini kwangu. Kwa vile mchana sikulala vizuri sikuchelewa usingizi ulinichukua.
 
Sehemu ya 08

Baada ya mazungumzo mganga alinipa dawa ya kutega ofisini kwangu, niliaga na kuondoka. Nilirudi nyumbani mapumziko ya kukesha kazini, nilioga na kujitupa kitandani. Niliamka jioni na kujiandaa kwenda kazini, kabla ya kwenda kazini nilipitia sehemu kushtua akili.

Muda ulipofika nilikwenda kazini kama kawaida, majira ya saa nne usiku niliweka dawa niliyopewa na mganga. Niliweka dawa kama nilivyoelekezwa, baada ya zoezi lile niliendelea ma kazi kama kawaida kwa kujipumzisha ofisini kwangu.

Kwa vile mchana sikulala vizuri sikuchelewa usingizi ulinichukua.
Kishindo cha watu kuanguka na vilio vya maumivu kilinishtua toka kwenye usingizi mzito, baada ya kuamka nilitulia na kusikia sauti za watu wakisema:
“Mmh! Hii ngoma ngumu.”
“Sasa tutafanyaje?”
“Kama nilivyowaeleza yote tumeyataka wenyewe.”
“Mnafikiri kama amegundua tulimfanyia kitu itakuwaje?

“Itabidi tutumie njia nyingine.”
Kwa vile walikuwa wakiondoka eneo la chumba cha maiti yaliyoendelea sikuyasikia. Nilibakia na maswali juu kile kilichotokea cha muanguko na vilio vya watu pia kauli zao juu ya kushindwa kuingia chumba cha maiti.

Niliamini kweli dawa za mganga zimefanya kazi nilijiuliza kauli yao ya kusema wamekwenda kujipanga watarudi vipi.
Nikiwa nipo katikati ya mawazo simu yangu ya mkononi iliingia, ilikuwa namba ngeni. Nilipokea na kuzungumza:

“Haloo.”
“Haloo, nina imani mazungumza na Mawazo?”
“We nani?” sikutaka kujibu mara moja.
“Najua hunijui, namba yako ya simu nimepata toka kwa ndugu yako Somati.”
“Ooh! Unasemaje?”

“Nina shida nawe, kesho ukitoka kazini tuonane.”
“Wapi?”
“Kuna mtu atakufuata hapo kazini.”
“Sawa.”
Nilikata simu na kujiuliza jamaa ana shida gani kama bidhaa za kazini kwangu angekuja kazini kwangu. Lakini sikutaka kuumiza kichwa kwa vile kesho haikuwa mbali pia sikuwa na wasiwasi baada ya kupewa namba na rafiki yangu Somati.

Baada ya muda Somati alipiga simu kuniuliza kama nimepigiwa simu, nilimkubalia na kuniambia kikifanikisha dili lile nitapata fedha nzuri. Baada ya kazi sikutoka haraka nilisubiri mtu kunifuata kutokana na makubaliano na mteja wangu. Robo saa toka muda wangu wa kazi kuisha nilipigiwa simu ambayo nilipokea.

“Haloo.”
“Haloo, samahani wewe ndiye Mawazo?”
“Ndiyo, nani mwenzangu?”
“Nimetumwa nikufuate kama mlivyo kubaliana jana.”
“Ooh! Upo wapi?”
“Njoo mpaka nje ya hospitali nipo kwenye maegesho ya magari utaona Prado nyeupe njoo moja kwa moja na kuingia mlango wa mbele.”

“Sawa nakuja.”
Baada ya kukata simu nilitoka hadi nje ya hospitali, nilielekea kwenye maegesho wa magari yanayoingia hospitali. Sehemu ile kulikuwa na magari machache, nililiona Prado ambalo lilikuwa lipo peke yake sehemu ile.

Nilikwenda na kuingia katika mlango wa mbele na kufunga mlango.
Utashangaa sikuwa na wasiwasi wowote ilitokana na mteja yule kuletwa na rafiki yangu Somati lakini angekuwa simjui nisingekubali. Pamoja na kuifanya kazi ile hatukumjua mzuri na mbaya unayeweza kuingia kichwakichwa kumbe ishu ya biashara ya viungo imevuja unaangukia mikononi mwa wazee.

Baada ya kukaa dereva wa gari aliyeonekana kijana mdogo alinisalimia:
“Habari za asubuhi Brother?”
“Nzuri sijui zako.”
“Zangu nzuri.”

Baada ya salamu hakuzungumza lolote aliondoa gari, nami sikusema lolote kwa vile nilijua yule kazi yake ilikuwa kunifuata tu, hivyo sikutakiwa kuzungumza chochote baada ya salamu. Gari lilitembea kwa dakika ishirini baada ya kutoka mjini na kuelekea sehemu zenye nyumba za kifahari za watu wanene.
Nikiwa ndani ya gari nilikuwa na mawazo mengi juu ya wito ule na kujiuliza kuna biashara gani inataka kufanyika tena nje ya eneo la kazi.

Baada ya muda gari lilisimama mbele ya geti la jumba moja la kifahari. Mlango ulifunguliwa na gari kuingia ndani. Gari kutembea kidogo mpaka kufia jumba la kifahari kutokana na geti kuwa mbali kidogo na nyumba. Baada ya gari kusimama dereva aliteremka na kuzunguka kunifungulia kama mgeni rasmi na kunikaribisha.

“Karibu.”
“Asante.”
Niliongozana naye hadi ndani ya jumba la kifahari ambako alinikaribisha kwenye sebule ya kifahari na kuniomba nimsubiri mzee. Nilitulia kwenye sofa kumsubiri mwenyeji wangu. Nikiwa bado nimebung’aa nikitembeza macho kila kona ya sebule ile.
Alitokea mhudumu wa kike akiwa na beseni la chupa ya maziwa na kahawa na kuniwekea mbele yangu na kunikaribisha kwa heshima zote.

“Karibu kaka.”
“Asante.”
Baada ya kuondoka nilijimiminia kahawa kwenye kikombe na kutulia kumsubiri mwenyeji wangu. Baada ya nusu saa alitokea yule kijana aliyenifuata na kunieleza naitwa ndani. Nilinyanyuka na kumfuata mpaka kwenye sebule nyingine na kumkuta mzee wa makamo akiwa amekaa kwenye kochi.

“Karibu sana.”
“Asante.”
Nilijibu huku nikikaa na yule kijana aliyenipeleka pale akiondoka, baada ya kukaa nilimsalimia kwa vile alikuwa akinizidi umri.

”Shikamoo mzee.”
“Marahaba, karibu sana.”
“Asante.”
“Sasa kijana bila kupoteza muda kuna kitu nimekuitia hapa ili tuzungmze kwa siri sikutaka sehemu yoyote kwa kuhofia macho ya watu kwa hiyo nahitaji msaada wako.”

“Msaada upo mzee?”
“Nina imani wewe na Somati ni ndugu?”
“Ndiyo.”
“Kama kweli nina imani hutaniangusha kwa kazi nitakayokupa.”

“Sawa kabisa.”
“Unajua kijana sisi matajiri tuna mambo mengi ambayo yanatofanya tuwe na fedha, kuna baadhi ya vitu lazima tuvifanye ili kuilinda fedha tunatokuwa nayo. Hivyo basi kuna jambo nataka unisaidie kwa usiku wa leo.”
“Japo gani?”

“Nahitahi maiti ya mjamzito leo.”
“He! Unataka uipeleke wapi?” nilishtuka japo haikuwepo.
“Tena ya mapacha wawili.”
“Sawa, unataka kuipeleke wapi?”
“Hapana kuna kitu nataka kufanya kwa muda mfupi kisha naondoka.”
“Mmh! Sijawahi kupokea maiti yenye kiumbe tumboni, mara nyingi mwanamke akifariki anafanyiwa upasuaji na kuletwa akiwa ametenganishwa na watoto au mtoto wake.”

“Leo kuna maiti ya mjamzito italetwa kinakosa, kabla hawajashtuka na kuifuata ninatakiwa nije nifanye mambo yangu na kuondoka.”

“We umejuaje?” nilishtuka kusikia vile.
“Bwana Mawazo mengine tutazungumza siku inayofuata naomba itekeleze hili kwanza.”
“Kama atakuwepo mimi sina tatizo.”
Mzee alinyanyuka na kuingia ndani baada ya muda alitoka na mfuko wa kaki na kunikabidhi.

“Nina imani kiasi hiki kitatosha kwa kazi ya leo.”
Nilipokea bahasha ile ambayo ilikuwa nzito bila kujua kuna kiasi gani.
“Basi kijana kapumzike tutaonana usiku.”

“Sawa mzee.”
Nilinyanyuka ili nitoke wakati huo kijana aliyenileta alikuwa amefika na kuniongoza kutoka nje ili nirudi nyumbani kupumzika ili mujiandaa na kazi ya usiku. Nilitoka hadi kwenye gari na yule kijana alinipeleka mpaka sehemu ambayo nilijua nitamkuta dereva wangu.

Baada ya kuniacha nilimpigia simu dereva wangu ambaye hakuwa mbali, alifika na kunichukua mpaka nyumbani. Alipofika nilifikia chumbani nikiwa na shauku wa kujua kwenye bahasha kuna kiasi gani. Nilipozihesabu sikuamini kupewa pesa kiasi kile, nilijiuliza mbona kanipa pesa kiasi kile kwa kazi asiyo na uhakika nayo.

Sikutaka kuzitumia niliamua kuziweka kwanza ili kazi ikishindikana ni mrudishie, niliziweka kabatini na kuzifungia na ufunguo nilificha mke wangu asiuone. Baada ya kuhakikisha pesa zipo kwenye usalama nilikwenda kuoga kisha nilipata supu na kupanda kitandani kulala.
 
Sehemu ya 09

Kama kawaida muda ulipofika niiingia kwenye gari langu mpaka kwenye bar ya Somati ambayo ndiyo niliyoichagua kupata kinywaji kabla ya kutimua zangu ofisini. Uvaaji wangu ulikuwa na tofauti na wenzangu wenye kufanya kazi kama yangu, nilikuwa navaa kama nakwenda ofisi ya kawaida hivyo nilijipenda.

Nguo za nyumbani nilikuwa navua na kuziweka sehemu nzuri na nilipomaliza kazi nilioga na kubadili nguo huku nikijipulizia utuli.

Ilikuwa vigumu mtu kujua nafanya kazi za kuhudumia maiti. Bahati nilikutana na rafiki yangu Somati ambaye tulipotezana kwa muda wa wiki mbili baada ya kwenda nyumbani kuwasalimia wazazi.
“Vipi za siku mbili tatu?”
“Mmh! Nzuri, vipi wazazi nyumbani?”
“Hawajambo, nilifika hadi kwenu wote hawajambo.”

“Nashukuru kaka mi nipo nakomaa na maisha.”
“Ndicho kilichotuleta mjini, komaa ndugu yangu najua kazi ngumu ila kwa muda mfupi unaweza kubadili maisha yako na kuachana nayo.”

“Ni kweli kazi ile ngumu kuna kipindi huwaza mengi, hivi mfano maiti waaamke unafikiri mimi nitafanya nini?”
“Hao mawazo ya uoga tu aliyekufa amekufa atakayeamka ujue hajafa huyo.”
“Nasikia kuna maiti huamka toka chumba cha maiti?”

“Mi ilinishatokewa mara mbili, japokuwa madaktari alihakikisha kuwa amekufa lakini ajabu sehemu niliyomlaza nilishtuka kuona viungo vikimcheza. Japo nilipata mshtuko mkubwa lakini nilipiga moyo konde na kumsogelea. Baada ya kumuangalia vizuri niligundua yupo hai ndipo nilipotoa taarifa.

“Walikuja kumchukua na kumrudisha wodini na baada ya matibabu alitoka katika afya njema. Lakini nilipata taarifa mtu yule alitoweka baada ya wiki katika mazingira ya kutatanisha, mpaka leo sijapata habari zake kama alionekana au alitoweka moja kwa moja.”

“Mmh! Una moyo, mimi ningetimua mbio.”
“Ukimbie nini wakati ile ndiyo kazi tuliyoichagua, kingine kama nilivyokueleza hakuna kiumbe kinachofufuka, ukiona kaamka basi jua huyo hajafa unatakiwa kumsaidia haraka kwa kupeleka ripoti ili apatiwe huduma ya haraka.”

“Mmh! Kazi ya kuhudumia maiti yataka moyo, pamoja na kuanza kuizoe kuna kipindi huingia woga baada yasikia upepo ukipita kisha panapita ukimya wa ajabu mpaka nywele huwa zinanisimama na kuingia na woga wa ajabu.”
“Hali hiyo huendelea kwa muda gani?”
“Kama dakika tano kisha hurudi katika hali yake ya kawaida, lakini dakika tano kama miaka mia tano.”

“Hiyo hali ya kawaida, sehemu ile ina mambo mengi hasa kutokana na kuwa na maiti, vitu vingine vikitokea unaachana navyo. Ukitaka kujua yote kila unaloliona au kusikia kazi ile huifanyi. Tena shukuru mzee yule kukupatia dawa bila hivyo usingekaa sehemu maiti zinapokaa kuna mauzauza ya ajabu.

Unaweza kusikia watu wanaingia mara droo zinafunguliwa watu huwaoni, wachawi wakorofi sana tena wasumbufu sana wanapenda kuwatisha watu ili wapate njia ya kufanya mambo yao.”
“Pesa tunapata, lakini chumba cha maiti kigumu sana hasa nyakati za usiku, kuna suku taa zilizimika ghafla nusra haja ndogo initoke hali ilikuwa inatisha. Baada ya hapo droo za maiti zikawa zinafunguliwa ovyo kisha palitulia na taa kuwaka. ”

“Kweli nimekumbuka, jana usiku mzee Ufunguo alikupigia simu?”
“Ndiyo na asubuhi nilipitia kwake.”
“Basi mzee yule mzungu hulipa kabla ya kazi, akienda naye vizuri atafurahi.”
“Lakini Somati anataka maiti ya mjamzito nitaipateje?”

“Itapatikana tu.”
“Hata ikipatikana si itakuwa tayari imefanyiwa upasuaji?”
“Mawazo, yule mzee akichokisema ana sababu zake maiti itapatikana na atafanya anachotaka kufanya.”
“Sasa anataka kufanya nini na maiti ya mjamzito, nahofia anaweza kuinyofoa kiungo akanitia matatani.”

Somati alicheka kusikia nilichokizungumza kisha alisema:
“Unajua ndugu yangu uoga umekutawala sana, yule mzee huwa ana utajiri wa ndagu(dawa). Ukiona anatafuta maiti ya mapacha basi ujue mali zake zimeanza kupungua kuna kosa amefanya.

Ili kuirudisha lazima alale na maiti ya mapacha ambayo ni sawa ya yeye mali yake kuongezeka mara dufu. Baada ya mali yake kuongezeka lazima apate maiti ya bubu ambayo huikata ulimi ili kufanya mali isitoke.”

“Sasa ya bubu tutaipata wapi na nitaijuaje?”
“Kila kitu muachie huyo mzee Ufunguo, mganga wake ana darubini yake akiona anakupigia simu ujue siku hiyo utapata maiti anayoitaka.”

“Somati hayo yote umeyajulia wapi?” nilishangaa Somati kuyajua yote.
“Nilimuuliza mganga aliyekusaidia yule mzee anajua vitu vingi sana hasa vya wachawi. Alinieleza vitu vingi kuhusiana na viungo vya binadamu vinavyochukuliwa na watu au wachawi vinafanya kazi gani.”

“Mmh! Kazi ipo, sasa kama haitapatikana?”
“Mawazo, yule mzee ana mganga wake ambaye hujua nini kitatokea mbele, hiyo maiti itapatikana leo.”

“Mmh! Sawa.”
Kwa vile muda ulikuwa umekwenda sana kutoka na mazungumzo ya muda mrefu ambayo yalinifanya hata nisinywe sana kwani nilikuwa makini na mazungumzo mazito kama yale ambayo sikutakiwa kupepesa macho. Ilibidi nichukue mzinga wa pombe kali ambayo ningekuwa kazini baada ya kazi kupungua.

Niliagana na Somati ili niwahi kazini kwani muda ulikuwa umekimbia sana, dereva wangu alinichukua kuniwahisha kazini na kuniacha karibu na hospitali. Sikutaka ajue nafanya kazi gani siku zote alizonibeba aliniacha barabrani na siku iliyofuata alinifuata palepale na kurudi naye nyumbani.

Kama kawaida nilipofika ofisini nilibadili nguo na kuvaa sare ya kazi, kabla ya kupokea shifti nilipitia ripoti ya mchana na kukuta kuna maiti saba zimetoka na sita kuingia. Ripoti ilielezea kulikuwa na maiti tatu wanawake wawili na mwanaume mmoja zilizokuwa zikisubiri kutambuliwa na ndugu zake na kukosa na siku ile ilikuwa ya mwisho hivyo zilitakiwa zizikwe na manispaa siku ya pili.

Maiti zile ndizo zilizokuwa biashara nzuri kwa washirikina kwani unakuwa na uhuru wa kuuza kiungo chochote bila kuulizwa na mtu. Mwanzo nilikuwa nikifanya biashara huku hofu ya Mungu ikiwa mbele, lakini baada ya kupata fedha woga ulinitoka na kutamani kuuza maiti wote ili nipate pesa.

Asikuambie mtu moyo wa tamaa huna hauna hofu ya Mungu, nilijikuta tamaa ya fedha ikinitawala na kutamani kujenga nyumba kama ya Somati ya ghorofa mbili. Somati aliniambia ghorofa alilipata kwa biashara ya watu wawili tajiri wa kiarabu na mswahili ambao wote walikuwa wakisifika kwa utajiri.

Mmoja alitaka sehemu za siri za binti bikira na jamaa mwingine aliyetaka nyeti ya mwanaume asiye riziki. Aliniambia ilikuwa kazi kuvipata kwani alichukua miezi mitano kupata vitu vile ambavyo aliahidiwa pesa nyingi na alipovipata alipewa kiasi kile kilichomfanya ajenge nyumba ya ghorofa mbili.

Nami nilijikuta nikiingia tamaa ya kupata mteja mwenye kutaka kiungo kwa fedha nyingi. Ilifika kipindi nikakosa roho ya huruma na kuwaona wanadamu wenzangu kama bidhaa iliyokuwa sokoni.
Kila maiti zilizokosa ndugu nilipata pesa nzuri kitu kilichofanya kuondokwa na moyo wa kiutu.

Baada ya kusoma ripoti, nilikagua kuangalia kama kweli maiti walioandikwa kwenye kitabu kama zipo sawa. Baada ya kujiridhisha kila kitu kipo sawa niliagana na mwenzangu na kuanza kazi rasmi kwa kuingia ofisini kujipanga kwa kazi ya usiku.
 
Sehemu ya10

Baada ya kusoma ripoti, nilikagua kuangalia kama kweli maiti walioandikwa kwenye kitabu kama zipo sawa. Baada ya kujiridhisha kila kitu kipo sawa niliagana na mwenzangu na kuanza kazi rasmi kwa kuingia ofisini kujipanga kwa kazi ya usiku.

Mwenzangu aliyetoka aliniachia maiti mbili zilizokuwa zinatakiwa kuwekwa kwenye friji, kwa vile zilifika akiwa ameisha jiandaa kuondoka, aliniachia mimi ili nikiingia niziweke vizuri. Niliziweka kwenye friji na kurudi ofisini kwangu kuendelea na kazi huku nikijiuliza kama nilicho agizwa kitawezekana.

Nilijikuta nikianza kusinzia, majira ya saa sita za usiku zilishtushwa na mlango wa chumba cha mochwari kufunguliwa. Nilifumbua macho na kutulia kama naota au kweli. Lakini sauti ya kitanda cha magurudumu ziliendelea kusikika kuonesha kumekucha Mwenyezi Mungu kesho chukua roho ya mja wake.

Nilinyanyuka na kuelekea eneo la kazi, nilikutana na wauguzi wawili wa kike wakikisukuma kitanda kilichokuwa na mwili wa mtu. Nilishtuka kuona juu ya kitanda mwili ulioletwa wa mwanamke mwenye mimba. Kwangu ulikuwa muujiuza mkubwa, ningeweza kukataa kuupokea kwa vile ulitakiwa kufanyiwa upasuaji ndipo uletwe chumba cha kuhifadhi maiti.

Lakini kwa vile nilikuwa najua nini kinaendelea sikusema kitu nilipokea mwili ule ambao niliuweka sakafuni kabla ya kuuingiza kwenye friji. Baada ya kuufikisha waliondoka kurudi wodini. Nilibakia nimesimama kama sanamu ajabu mapigo ya moyo yalinianza kwenda mbio.

Nilijiuliza wasiwasi ule nimeutoa wapi, nilishika mkono kifuani kupunguza hofu iliyonipata ghafla, nikiwa bado nimesimama huku miguu ikinitetemeka. Mlio wa simu ulinishtua toka katika dimbi la mawazo ya hofu yaliyosababisha kutokwa jasho jembamba.

Nilitoa simu mfukoni na kuangalia nani anapiga, ilikuwa namba ngeni, nilipokea:
“Haloo.”
“Eeh, Mawazo.”
“Naam, nani mwenzangu?”
“Ni mimi, vipi ile maiti imepatikana?”
“Mmh! Wewe nani?” sauti ilinichanganya japo akili iliniambia huenda ni mzee Ufunguo aliyenipa kazi ile.

“Aah Kijana, kwani nilikupa kazi gani?”
“Ooh, Mzee! Upo wapi?”
“Bado hujajibu swali langu.”
“Swali gani?”
“Kuhusu kupatika hiyo maiti ya mjamzito.”

“Dah! Mzee kama mchawi kuna mwili wa mjamzito umeingia sasa hivi, upo wapi fanya haraka maana nina wasiwasi wamejichanganya wanaweza kushtuka kabla hujatimiza unachokitaka,” nilimuhimiza huku nikiwa na wasiwasi tofauti na siku nyingine.
“Sipo mbali na chumba chako cha maiti nina saa mbili toka nifike.”

“Basi njoo haraka.”
“Nakuja sasa hivi.”
Baada ya dakika tano mzee Ufunguo alifika, nilimuingiza chumba cha kuhifadhia maiti, alipoiona maiti ya mjamzito imelala chini aliniambia:
“Kijana kazi nzuri ukiendelea kunielewa utafurahi mwenyewe.”

“Hakuna tatizo mzee,” nilijibu huku wasiwasi wangu ukiwa kwa wauguzi kukumbuka kama wameuleta mwili wa mjamzito kimakosa bila kufanyiwa upasuaji.
“Sasa kijana naomba ivue maiti nguo zote na ulilaze chali.”

“Sawa.”
Nilifanya ile kazi kwa haraka huku moyo ukinienda mbio kwa kuamini tukikutwa kazi sina na kifungo juu. Baada ya kumaliza kufanya kama alivyotaka aliniomba nitoke nje, wazo lake la kutoka nje niliona kama halifai kwa vile wauguzi wakirudi nitashindwa kuwazuia kuingia ndani na wakiingia wakimkuta anaichafua maiti na kufanya nieleweke vibaya.

Nilimwambia nibaki na kufunga mlango kwa ndani hata wakija wagonge, nami nitawachelewesha kwa muda ili amalize zoezi lake kisha yeye alale chini kama maiti ili wakiingia nisingizie nilikuwa napanga maiti wakitoka na mzee Ufunguo naye atoke. Wazo langu aliliona halina umuhimu kwa kunihakikishia hatatokea mtu yoyote mpaka amalize haja zake.

Nilitoka nje huku nikioomba Mungu asiletwe mtu muda ile aliyefariki ili mzee amalize haja zake na kuondoka. Nilikaa kwa muda wa dakika ishirini ndipo mzee alipomaliza na kuniita ili nikamvushe nguo ile maiti ya mjamzito.
Niliingia ndani na kuukuta mwili umechafuliwa, tena ilionesha hakutumia hata kinga.

Niliusafisha mwili na kuufunga vizuri nguo na kuwa kama ulivyoletwa, niliuacha palepale chini nikisubiri mzee Ufunguo aondoke ili nipige simu wodini kuulizia kuletwa mwili wa mjamzito bila kufanyiwa upasuaji na kutolewa kiumbe kilichokuwemo tumboni.
Nilitoka nje na kumkuta mzee Ufunguo akinisubiri nje aliponiona aliniuliza:

“Vipi tayari?’
“Ndiyo.”
“Naomba unichukulie maji ya maiti.”
“Sawa nakuletea.”
Nilirudi ndani na kwenda sehemu ninayo yahifadhi na kumletea lita tano ya maji ya maiti.
“Naomba unipelekee kwenye gari langu.”
“Hakuna tatizo.”

Nilimbebea hadi kwenye gari lake na kurudi sehemu yangu ya kazi, nilipofika nilishtuka kuwakuta wauguzi wakiwa wamesimama mlango wa chumba cha maiti huku mlango wake ukiwa wazi. Nilificha mshtuko wangu na kuwasogelea, nilijifanya kushtuka:

“Vipi mmeleta mtu?”
“Hapana kuna kosa limefanyika.”
“Kosa gani?” nilijifanya kushtuka.
“Tumeleta mwili wa mjamzito kwa bahati mbaya.”
“Ina maana mlikuwa hamjui?” nilijifanya kuwauliza.

“Tunajua, hata hatujui ilikuwaje kuuleta mwili huku bila kufanyiwa upasuaji.”
“Kwa hiyo mnasemaje?”
“Tumeufuata ili tumrudishe wodini.”
“Ningekuwa nimeuweka kwenye friji?”
“Tunashukuru umechelewa kuuingiza kwenye friji.”

Waliuchukua ule mwili wa mjamzito na kuurudisha wodini kwa ajili ya kufanyiwa kwanza upasuaji ili kutoa kiumbe kilichomi tumboni. Baada ya kuondoka nilifunga mlango na kurudi ofisini kwangu na kutulia kwenye meza huku kichwa kikiwa na mawazo mengi sana.

Kwangu kila kilichotokea muda ule kilikuwa kitu kilichoniacha mdomo wazi, kwanza ilikuwa kuletwa mwili wa mjamzito chumba cha kuhifadhia maiti kitu ambacho kilikuwa hakiwezi kufanyika. Pili mzee Ufunguo kufanya mapenzi na maiti ya mjamzito na tatu waunguzi kugundua kosa baada ya mzee kuondoka.
 
Sehemu ya 11

Waliuchukua ule mwili wa mjamzito na kuurudisha wodini kwa ajili ya kufanyiwa kwanza upasuaji ili kutoa kiumbe kilichomi tumboni. Baada ya kuondoka nilifunga mlango na kurudi ofisini kwangu na kutulia kwenye meza huku kichwa kikiwa na mawazo mengi sana.

Kwangu kila kilichotokea muda ule kilikuwa kitu kilichoniacha mdomo wazi, kwanza ilikuwa kuletwa mwili wa mjamzito chumba cha kuhifadhia maiti kitu ambacho kilikuwa hakiwezi kufanyika. Pili mzee Ufunguo kufanya mapenzi na maiti ya mjamzito na tatu waunguzi kugundua kosa baada ya mzee kuondoka.

Niliamini kweli uchawi upo, nilijikuta nikiwaza mengine kuhusu kifo cha mjamzito yule kinaweza kusababishwa na mzee Ufunguo ili afanye uchafu wake. Nilikubaliana na kauli ya Somati kuwa mganga wa mzee Ufunguo kiboko anayefahamu kila kinachokuja mbele japo niliamini hajui siku yake ya kufa.

Nilishukuru Mungu siku ilivuka salama bila tatizo lolote, asubuhi kabla ya kuondoka nilipigiwa simu na mzee Ufunguo kuwa kuna mzigo wangu kampa kijana wake aniletee. Baada ya muda kijana aliyetumwa alinipigia simu nimkute sehemu nilitoka hadi katika maegesho ya magari ambapo niliona gari la mzee Ufunguo.

Niliingia na yeye kuondoa gari mpaka sehemu niliyomwelekeza anishushe na kunipa bahasha iliyokuwa na pesa. Niliagana naye na mimi kumpigia simu dereva wangu aliyenifuata kunipeleka nyumbani.
***
Usiku kama kawaida nilikwenda zangu kazini, moyo wangu ulijaa furaha baada ya milango ya fedha kufunguka niliamini kabisa dawa za mganga wa Somati zinafanya kazi kwani ugumu wa kupata pesa unaondoka.

Usiku kama kawaida nilisikia vishindo vya watu kuanguka ilionesha wachawi wamegonga ukuta tena kuingia kwenye chumba cha maiti kuchukua viungo vya maiti bila idhini yangu.
Siku iliyofuata nikiwa nakaribia mlango mkuu wa kuingilia hospitali nilisimamishwa na wazee watatu wawili wa kiume na mmoja wa kike.

Hawakupenda niingie ndani walitaka tuzungumzie ndani. Tulisogea pembeni na kuwasikiliza wananiitia nini, niliwaona kama wakisakiziana nani azungumze. Niliona kama wanataka kunichelewesha niliwauliza:
“Wazee wangu mnasemaje?”
“Kijana tulikuwa na shida na ofisini kwako.”

“Shida gani?”
“Nina imani hutufahamu?”
“Ndiyo,” nilijibu huku nikiwangalia vizuri lakini sura zao zilijirudia akilini na kumkumbuka mmoja alikuwa kwenye kundi la wachawi. Haraka akili yangu ilijua ile dawa imefanya kazi. Kama mganga alivyonieleza watakuja tu kwani hawakuwa na ujanja.

“Tulikuwa na shida ofisini kwako.”
“Shida gani?”
“Nina imani siku za nyuma kuna wenzetu walikuwa wakifanya biashara na wewe, lakini kutokana na matatizo hatukuweza kuendelea na biashara ile lakini kwa sasa tumerudi hivyo tunaomba kuendelea na biashara kama zamani.”

“Kweli mnataka kufanya kazi na mimi?”
“Ndiyo.”
“Basi naomba muwe wakweli muda ambao hakuja kwangu mlikuwa mkifanya nini?”
“Tulikuwa na matatizo.”
“Nataka kuwaeleza ukweli kuwa mlinizunguka kwa hiyo ili tufanye kazi naomba mnilipe pesa zangu za muda wote mlio nizunguka. Kama hamtanilipa sitafanya kazi na ninyi.”

“Mmh!” waliguna na kutazamana kisha aliomba wazungumze pembeni.
Niliwaruhusu wazungumze kwa kujua nimewashika vibaya pia walishtuka kuona nimewaumbua. Baada ya mazungumzo ya pembeni walinifuata na kusema:
“Sasa kijana tunaomba basi tuondoke tutarudi baadaye.”
“Mkirudi mje na pesa yangu ya kipindi chote mliokuwa kijichukulia vitu kama vyenu.”

“Mmh! Sawa.”
Waliondoka lakini kabla sijafika ofisi kwangu, mzee mmoja alinifuata na kunieleza:
“Samahani kijana tulikuwa tunaomba msaada mmoja.”
“Msaada gani?”
“Kuna msichana mmoja aliyefariki ghafla leo usiku tulikuwa tunaomba msaada wako.”
“Msaada gani?”

“Tunataka kucha na nywele zake, tutakupa kiasi chochote ukitakacho.”
Kazi haikuwa kubwa ya kuwapa nywele na kucha hata bure ningewapa kwa vile maiti isingeonekana na kasoro yoyote. Lakini kitendo walichonifanyia kiliniuma sana lakini Mungu aliwaleta nami nilipanga kumaliza hasira zangu kwao.
“Jamani kama nilivyosema sitabadilika mpaka mlipe kwa vile ulikula bila kutoka jasho.

“Kijana ni kweli tulikukosea, kwani ulikuwa unataka kiasi gani?”
“Mnajua wenyewe, mnajua tulikuwa tukiuziana kiungo cha binadamu kwa shilingi ngapi, kwa hiyo pigeni hesabu mlete hela zangu.”
“Kijana hiyo hela tutakupa, ila tunaomba msaada huo mdogo.”
“Kwani mwanzoni mlikuwa mkimuomba nani?”

“Kijana tunajua tumefanya kosa tunaomba tusahau yaliyopita ili tutanye kazi kama zamani.”
“Basi kafanyeni kama nilivyowaeleza.”
“Sawa tumekubali, lakini tulikuwa tunaomba msaada huu.”
“Mzee wangu kuwa mwelewa basi.”
“Sawa kijana,” mzee alikubali shingo upande na kuondoka zake.

Niliachana na yule mzee na kuingia ofisini, nilmkuta mwenzangu ameishajiandaa kuondoka. Nilimpokea na kukabidhiana ripoti ya mchana baada ya kukagua na kukuta kila kitu kipo sawa. Baada ya kuondoka mwenzangu nilibadili nguo na kuanza kazi huku mawazo yangu yakiwa kwa wale wazee wachawi waliokuwa wakiniibia viungo vya maiti na kukwama.

Niliamini kupitia shida yao ambayo iliwafika shingoni na kuamua kunifuata ili niwasaidie, hivyo ile ndiyo mami ilikuwa nafasi yangu ya kumaliza machungu yangu. Niliachana na mawazo yao kwa kuamini lazima watarudi tu. Nikiwa naendelea na kazi nilipigiwa simu toka wodini kuwa kuna maiti mbili hivyo nilitakiwa kuzifuata.

Nilifanya hivyo mara moja kwa kufuata maiti hizo na kuzipanga kwenye droo kisha nilirudi kupumzika. Nikiwa ndiyo naanza kusinzia wazee wale walirudi tena, nilitoka nje ya ofisi ili niwasikilize.
“Ndiyo wazee wangu.”
“Sasa kijana tuna kiasi kidogo tumekusanya ili kupunguza deni unalotudai.”

“Mmeleta kiasi gani?”
Walinipa kiasi cha fedha ambacho nilikihesabu na kukiona si kibaya kwa vile kilizidi mara tatu kiasi nilichompa mganga kunifanyia kazi yangu, kisha niliwauliza:
“Hii sasa nusu au robo?”
“Robo mzee,” alijibu kwa unyenyekevu.
“Haya na ya kazi mpya?”

“Unataka kiasi gani?”
“Tutakupa (wanataja kiasi)”
“Hicho kidogo sana.”
“Kijana mbona vitu vyake ni vya kawaida wala si vya kivile.”
“Mzee wangu ukisema hivyo unaonesha dharau, basi mngeachana navyo.”
“Samahani kijana, basi nitaongeza kiasi (anataja kiasi).”

“Hapana bado mpo chini sana.”
Tulivutana mpaka tukafikia kiasi ninachokitaka, waliponipa niliwaelekeza ilipo maiti waliyotaka na kuchukua vitu walivyovitaka bila kuongeza kitu. Baada ya kuchukua wanavyotaka waliondoka huku wakiwa wametia akili.
 
Sehemu ya 12

Siku zilizidi kukatika huku biashara haramu ikienda vizuri, wakati huo nilikuwa nimenunu eneo lingine ambalo nilipanga kujenga nyumba ya ghorofa moja kwani kuna kazi nilipewa ya pesa nyingi japokuwa ilikuwa kazi kupata vitu wanavyotaka lakini niliamini ipo siku nitavipata.

Maisha yaliendelea huku wachawi wote wakawa wakitaka kitu lazima wanione kwa vile hawakuwa na njia yoyote ya kuchukua kitu bila idhini yangu. Ile ilinifanya niingize pesa kila siku hata pale walipotaka maji ya maiti ya mtu walioshiriki kumuua huchukua vile ili kutengeneza mazingira ya kumpata baada ya kumzikwa.

Siku zote kila kitu kina uzuri na ubaya, nakumbuka siku moja nilipata oda ya viganja cha mtoto. Kwa vile wiki ile kulikuwa na maiti tatu hazina ndugu mmoja katika zile maiti kulikuwepo ya mtoto. Kama kawaida kabla ya kwenda kuzizika maiti zisizo na ndugu nilikata viungo vilivyotakiwa kisha nilizifunga vizuri kusubiri kwenda kuzikwa.

Siku ya pili tulizika zile maiti na jioni yake wateja walikuja kuchukua viungo vyao, baada ya kuuza nilitulia kwenye ofisi yangu. Nikiwa nasinzia nilishtuliwa na mlinzi wa getini akiwa amemshika mtu ambaye nilikuwa namjua.
“Vipi?” nilimuuliza.
“Huyu mtu unamjua?” aliniuliza, mtu nilimjua alikuwa mteja alitefuata viungo vya mtoto muda mfupi.

“Simjui,” nilimkana.
“Huyu mtu hivi kavipata wapi?”
“Vitu gani?”
Alichukua mfuko ambao nilijua una viganja vya mtoto na kuuweka mezani.
“Hivi kavipata wapi?”
“Muulize mwenyewe.”
“Eti umetoa wapi?”
“Afande tuzungumze tuyamalize ni jambo la kuelewana kwa nini tulifanye liwe kubwa wakati linazungumzika,” mteja wangu alijitetea.

“Sikiliza huu mtego tumeutega muda mrefu na leo umenasa hivyo mimi sina maamuzi bali kwa wakuu wangu.”
“Sasa mimi nikifukuzwa kazi na kufungwa utafaidi nini, nitakupa laki tano umuachie huyu mtu.”

“Kaka hata milioni sichukui, nakueleza huu ni mpango maalumu kwa hiyo na wewe upo chini ya ulinzi.”
“Nipo chini ya ulinzi kwa kosa gani?”
“Hujui, basi ukifika mahakamani ndipo utajua kosa lako,” baada ya kusema vile redio call yake iliuliza:

“Afande Chuku amefikia wapi? Ova.”
“Mkuu mpaka sasa nipo na watuhumiwa, nasubiri nguvu zetu tuwakamate, Ova.”
“Tumekaribia, tunafika sasa hivi, ova.”
Kauli ile ilinifanya nisikie mwili wote ukiingia baridi na kujisemea moyoni “Nimekwisha.” Lakini nilipata moyo na kuona njia sahihi ya kuokoka ni kumkana yule jamaa kuwa simjui na aeleze amepata wapi vile viganja wa mtoto. Baada ya sekunde chache nilisikia mlio wa gari.

Waliingia kikosi cha ulinzi ambao walimkuta yule jamaa aliye muuzia viungo yupo na mfuko wake mweusi.
“Afande hawa ndiyo watuhumiwa.”
“Samahani ndugu mimi unaniita mtuhumiwa kwa sababu gani?” nilihoji.
“Nimemkamata huyu jamaa akitoka kwako kununua viungo, nilipo mbana alisema wewe ndiye uliyemuuzia na hii biashara si ya mara moja.”

“Afande huu ni udhalilishaji, hivi viungo nimuuzie kutoka wapi wakati humu ndani kila maiti ina ndugu yake.”
“Afande lazima kutakuwa na vingo vingine pia maiti zilizo na viungo nusu,” alisema mmoja wa askari.

“Basi tufanye msako.”
“Msako mtafanya lakini lazima uongozi wa hospitali wajue,” nilisema vile japokuwa nilijua najipalia mkaa.
“Viongozi wako wanajua kila kitu na huu mpango wanaujua.”

Kauli ile ilinishtua na kuona nimekwisha, nilipanga kumruka futi mia aliyekamatwa na viungo. Wakati huo baadhi ya viongozi wa hospitali walifika na kuona viungo vilivyokamatwa. Mara moja niliwekwa chini ya ulinzi, msako ulianza mara moja kuangalia kama kuna maiti iliyokatwa kiungo.
 
Sehemu ya 13

“Msako mtafanya lakini lazima uongozi wa hospitali wajue,” nilisema vile japokuwa nilijua najipalia mkaa.
“Viongozi wako wanajua kila kitu na huu mpango wanaujua.”

Kauli ile ilinishtua na kuona nimekwisha, nilipanga kumruka futi mia aliyekamatwa na viungo. Wakati huo baadhi ya viongozi wa hospitali walifika na kuona viungo vilivyokamatwa. Mara moja niliwekwa chini ya ulinzi, msako ulianza mara moja kuangalia kama kuna maiti iliyokatwa kiungo.

Baada ya msako mkubwa hakukuta kitu chote, lakini bado nilichukuliwa kwenda kutoa maelezo polisi pamoja mtu aliyekamatwa kung’ang’ania mimi ndiye niliyemuuzia. Nilishukuru siku ile nilitoa viungo tu pesa walikwisha nilipa muda kama ningeuza siku ile ningekuwa na kizibiti.

Nilipomaliza kutoa maelezo niliingizwa mahabusu kusubiri kupelekewa mahakamani baada ya ushahidi kukamilika. Nikiwa mahabusu niliwaza mengi wasiwasi wangu nilijua lazima watataka kwenda nyumbani kupekua lazima maisha yangu ya juu na mali nilizokuwa nazo mimi mhudumu wa chumba cha maiti lazima wangehoji kazi na vitu nilivyokuwa navyo kuna tofauti kama mbingu na ardhi.

Moja kwa moja wangeamini nafanya biashara haramu hivyo wangekuwa na kila sababu ya kunifungulia mashtaka na kunifunga. Kingine ambacho kilinisaidia ilikuwa simu niliyokuwa naitumia. Somati alinikataza nisitumie simu yangu ya kawaida kufanyia mambo yangu hivyo nilikuwa na simu nyingine ya kawaida niliyokuwa nikiwasiliana na watu kuhusu biashara.

Wengi walipewa namba na Somati ya kazi, hata nilipokamatwa walichukua simu yangu kubwa lakini ndogo niliwahi kuificha. Kabla kuingizwa mahabusu nilivua mkanda viatu pesa kidogo nilizokuwa nazo. Siku zote niliondoka na elfu ishirini ya kula na kunywa hivyo mpaka nakamatwa nilikuwa na elfu nane tu.

Simu yangu waliichukua muda walipo nikamata, niliamini waliamini ule ulikuwa ushahidi wa kwanza. Lakini kwa vile simu ile haikuwa sehemu ya kufanyia biashara zangu niliamini wangechemsha wasiwasi wangu ulikuwa kwa aliyekamatwa kama angetoa siri japokuwa siku ile ndiyo ilikuwa ya kwanza kufanya naye biashara.

Baada ya askari walionipeleka polisi kuondoka nilimuomba askari aliyekuwa zamu simu yake niweze kuzungumza na ndugu yangu. Askari alikuwa muungwana alinipa simu, Baada ya kunipa simu aliondoka na kusema nikimaliza kuzungumza nimwite.

Kwa vile namba za Somati zilikuwa nayo kichwani nilimpigia kumjulisha nimekamatwa. Alishtuka sana baada ya kumweleza sababu ya mimi kukamatwa na muda ule nilikuwa ndani.

“Dah! Kuna ushahidi wowote wamekushika nao?”
“Hakuna, ni yule jamaa aliyekamatwa tu.”
“Askari aliyekupa simu yupo karibu?”
“Hapana hupo mbali.”
“Kwa hiyo jamaa aliyekamatwa anasemaje?

“Anasema mimi ndiye niliyemuuzia na ile ni biashara yangu ya siku zote.”
“Mmh! Isiwe katumwa na watu?”
“Inawezekana kwani hata aliyemkamata anasema walikuwa wakinitega bila mafanikio lakini leo nilikuwa nimeingia kwenye mtego wao.”

“Mmh! Kazi ipo,” kuguna kwa Somati kulinimaliza nguvu kwani niliamini yeye ni mzoefu basi angenisaidia lakini niliona kama amekata tamaa.

“Sasa ndugu yangu badala ya kunisaidia unaguna, nina imani naweza kufungwa.”
“Siyo kuguna kwangu nimekuacha la hasha, lazima kichwa kichemke kwa vile kazi iliyopo mbele yetu ni kubwa sana tukifanya mchezo unaweza kuozea gerezani.”

“Sasa ndugu yangu utanisaidiaje? Maana hapa nilipo nimechanganyikiwa.”
“Nyumbani una kiasi gani?”
“Mmh! Sidhani hata milioni mbili zinafika.”

“Wewee! Pesa zote umezipeleka wapi?”
“Nilinunua nyumba katikati ya mji nataka kujenga hoteli kubwa, kuna kazi niliyokuwa nikiitegemea kuipiga ningepata pesa nzuri ya kuanzia ujenzi. Pia kulikuwa na kazi zingine mbili nyumba ingeisha. Lakini naona sasa imekula kwangu kweli ng’ombe hazai.”
“Sasa tutafanyaje maana lazima tutoe kiasi kikubwa cha pesa ili utoke nje kwanza kabla ya kurudi polisi tuwe tumesafiri kwenda kuizika kesi la sivyo utafungwa.”

“Kwani kinatakiwa kiasi gani?”
“Milioni tatu za kumziba mdomo mkuu wa polisi ili wadogo wasipate upenyo wa kusema chochote. Tungeweza kuizima kesi kwa pesa kama tutakuwa na milioni tano mkononi. Lakini tatizo lipo ofisini kwako lazima hawatakubali kurudi hivyo utaadhilika kwa vile bado hujajipanga. Sasa lazima tufike kwa babu ili kuwazika wote na kukusahau ili urudi kazini.”
“Sasa tutafanyaje?”
“Itabidi nitoe zangu ukitoka unirudishie.”
“Hakuna tatizo, nitauza hata gari langu.”
“Bado tu?” sauti ya juu ya askari iliuliza.

“Namalizia mkuu,”nilijibu kwa sauti na kuona kweli nizungumza kwa muda mrefu alikuwa na haki ya kuuliza.
“Basi malizia utanunua vocha?”
“Wala usihofu utapata nikitoka.”
“Haya malizia.”
“Sawa.”
Nilirudisha simu sikioni kuendelea kuzungumza na Somati.

“Haloo.”
“Eeh, vipi kwani?”
“Afande aliyenipa simu aliulizia kama bado nazungumza.”
“Basi ndugu yangu, leo lala huko kwa vile muda umekwenda, ila kesho nakuhakikishia kutoka.”
“Nitashukuru ndugu yangu maana bila wewe sijui ingekuwaje.”

“Lazima ujue jinsi ya kukabiliana na matatizo, pia kwa kazi zetu lazima tuwe na akiba ndani. Leo bahati nzuri nina pesa, kuna kipindi huwa natoa pesa zote kwenye biashara zangu hivyo ingekuwa tatizo japo nina uhakika ningekutoa tu na mambo mengine yangeendelea.”
“Nitashukuru rafiki yangu nikuache ulale najua imekushtua usingizini.”
“Walaa usijali ni wajibu wangu kama ndugu yako.”

Baada ya mazungumzo nilimwita askari wa zamu anichukulie simu yake, alikuja kuchukua simu yake. Nilimshukuru na kumuahidi nikitoka nitampatia asante yake, naye aliahidi kunipa ushirikiano wa kutosha nitakapokwama.
***
Siku ya pili saa nne asubuhi nilitolewa mahabusu kwa dhamana aliyoniwekea Somati. Ambaye wakati huo alikuwa mtu mzito mjini hakuna ambaye hakumjua mjini kwa wakati ule. Wakubwa wengi alikuwa nao karibu hivyo hakupata kazi kubwa kuniwekea dhamana japo zilimtoka milioni nne kwani walitaka kukataa kunitoa mpaka ushahidi ukamilike.

Simu sikuichukua kwa vile walisema bado wana kazi nayo japokuwa mkuu wa kituo alisema wameiacha ili walalamikaji hospitali wasione kama kuna mazingira ya rushwa ila alinieleza kuwa hakuna tatizo lolote simu haikuwa na ushahidi wowote bali wanamtegemea aliyekamatwa na viungo vya binadamu kutoa ushahidi utakaoniingiza hatiani.

Nilirudi nyumbani kuoga kisha Somati alinichukua siku ileile kwa gari lake kwenda nje ya mji kwa mtaalamu wake mwingine. Nilimuulizia mganga wa awali aliyenipeleka mwanzo

“Mawazo, hili lazima tukaloge, ni kesi imekaa vibaya sana baada ya kuzungumza na mkuu wa kituo. Aliniambia nifanye kazi ya ziada bila hivyo naweza kukupoteza,” Kauli ili iliufanya moyo wangu utetemeke.

“Mmh!”
“Sasa huko tunakwenda kufanya kufuru tukirudi kila kitu kimepinduka anajiita mzee wa kubadili matokeo.”
“Nitashukuru maana hapa nilipo kila nikikumbuka naona utumbo unanicheza.”
“Yataisha tu.”

Tulitembea kwa muda wa saa zaidi ya tano na kuingia kijijini kwa vile barabara haikuwa na lami. Tulifika safari yetu saa kumi na mbili jioni, ilikuwa sehemu iliyojitenga pembezoni mwa mji mpakani na nchi ya jirani. Kwa muda tuliofika niliamini kabisa siku ile hatuwezi kurudi siku ileile.

Baada ya kupokewa tulikaa chini ya mti kwenye magogo kusuburi kuonana na mganga aliyekuwa akiwahudumia wagonjwa wengine. Baada ya muda tuliitwa ndani kuonana na mganga. Ilionesha Somati alikuwa mzoefu anga zile, mzee alipomuona alimchangamkia.
“Ooh! Kijana za siku?”

“Nzuri tu babu.”
“Hata mimi naona, naona umekija na mgeni?”
“Ndiyo babu ni ndugu yangu ana matatizo yamemsibu si unajua kazi zetu matatizo kila kukicha.”
“Kwa nini hukumleta mapema ili kuondoa matatizo kama haya.”

“Babu wee acha tu, mambo ya mjini yanachanganya sana.”
“Mmh! Ana tatizo gani?”
Nilimwelezea tatizo langu bila kuficha kitu kutokana na Somati alinieleza nisifiche kitu ili niweze kupewa msaada wa kweli. Baada ya kumweleza mzee yule alichukua kibuyu kidogo na kutoa simbi nne na kuzichekecha kisha alizitupa mbele na kuziangalia huku akiigusa moja kwa kujiti kirefu.

Alikuwa akigusa simbi moja na kuangalia kama ameona kitu kisha aligusa nyingine mpaka akamaliza zote nne. Alinyanyua uso wake na kunitazama kisha alisema:
“Mmh! Hii kesi ni nzito sana tukifanya mzaha inaweza kumfanya mtu afie gerezani,” kauli ile ilinishtua na kufanya mapigo ya moyo yaende mbio.
 
Sehemu ya 14

Nilimwelezea tatizo langu bila kuficha kitu kutokana na Somati alinieleza nisifiche kitu ili niweze kupewa msaada wa kweli. Baada ya kumweleza mzee yule alichukua kibuyu kidogo na kutoa simbi nne na kuzichekecha kisha alizitupa mbele na kuziangalia huku akiigusa moja kwa kujiti kirefu.

Alikuwa akigusa simbi moja na kuangalia kama ameona kitu kisha aligusa nyingine mpaka akamaliza zote nne. Alinyanyua uso wake na kunitazama kisha alisema:

“Mmh! Hii kesi ni nzito sana tukifanya mzaha inaweza kumfanya mtu afie gerezani,” kauli ile ilinishtua na kufanya mapigo ya moyo yaende mbio.
“Na kesi hii inaonekana itakugusa hata wewe mzee,” alisema huku akimunesha Somati na kijiti cha kupigia lamri.
“He! Na mimi niwemo kivipi?” Somati alishtuka.

“Mwenzako atafungwa lazima watachunguza mali zake kapata vipi, kwa vile kamba yenu ni moja lazima watafika kwako. Hivyo lazima utachunguzwa na mwisho ni kifungo.”

“Duh!” Somati alibakia kinywa wazi.
“Lakini msiwe na wasiwasi kwa vile mmewahi kuja kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa. Hapa panaonesha atarudishwa kazini, lakini hutakaa muda mrefu kesi yako utaendelea baada ya kusimamishwa na hapo waajili wako watapeleka ushahidi utaokufunga.”

“Sasa tutafantaje?” niliuliza.
“Kwa vile mmefika hapa kazi hii niachieni mimi, ila kwa sasa sitafanya kitu chochote mpaka zoezi hili la kurudishwa kazini lifanyike.”
“Lakini bado sijafukuzwa kazi,” niliuliza kwa vile nilitoka mahabusu na kwenda kwake.

“Ukienda kazini utakutana na barua yako ya kusimamishwa kazi na baada ya uchunguzi kukamilika utafukuzwa kazi kabisa wakati huo utakuwa unaendelea na kesi ambayo ingekufunga.”
“Sasa kwa nini hufanyi kitu babu?” Somati aliuliza.

“Siwezi kufanya kitu kwa vile akienda kazini atakutana na barua ya kumsimamisha kazi huku wakianza mchakato wa kutafuta mtu mwingine. Lakini ndani ya siku nne watakufuata uendelee na kazi ili wajipange kukufunga. Hapo ndipo ninapopataka kwa vile kurudi kwako kazini tutaozika kesi na mawazo yao.”

“Sawa mzee sisi tunakusilikiza wewe,” Somati alisema kwa upole kwani naye hofu iliisha muingia moyoni kutokana na kuonekana tatizo langu na yeye litamgusa.

“Kuna dawa nitakupa kama ukirudi kazini utaiweza sehemu za nyuma za maiti kwa kuziingiza ndani huku ukinuiza kuwa kama maiti inaamka basi na wewe mambo yako yaendelee lakini kama maiti ikizikwa haifufuki basi na wewe unazima kila baya kila tatizo kila kitu kibaya kilicholengwa kwako.

“Baada ya kuzuia utaiingiza dawa sehemu hizo hakikisha maiti inayozikwa siku ya pili ikiwezekana na wewe uwepo kwenye mazishi hayo baada ya kuondoka chukua mchanga wa kaburini na kuja kuumwaga ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti na usiku uoge maji ya maiti.

Hapo kazi itakuwa imekwisha, hata wakukamate na nini hawatakuwa na nguvu ya kukufanya lolote.”
“Tutashukuru,” alisema Somati.
Baada ya maelezo yale alitoka nje na kurudi na majani aliyoyachanganya na dawa zaidi sita kisha alizifunga kwenye sanda ambayo aliitengeneza kama hirizi na kunikabizi mkononi.

“Hii kijana itamaliza kila kitu.”
Nilipokea na kushukuru, Somati alimhesabia yule mzee shilingi milioni moja taslimu na kumkabidhi. Babu alipokea na kushukuru huku akituhakikishia yeye ndiye mzee wa kubadili matokeo. Kwa vile kazi ilifanyika kwa muda mfupi tuliamua kurudi siku ileile.

Tulimuaga babu na kurudi mjini, nilifika nyumbani saa kumi na moja alfajiri, kwa vile nilikuwa tumechoka sana kila mmoja alikwenda kwake kulala, Nilipamga siku ya pili niende kazini ili nipewe hiyo barua yangu ya kusimamishwa kazi.
****
Siku ile nililala muda mwingi kitandani kujipumzisha ajili ya safari ya jana pia sikupata muda wa kutulia kutokana kulala mahabusu hivyo nililala sana.

Nilipozinduka usingizini nilijikuta jikiwa na mawazo mengi juu ya tukio lililonitokea, sikuamini kama yule aliyekamatwa ilikuwa bahati mbaya bali alitumwa na wale wazee ambao niliwabana hivyo waliamua kunifukuzisha kazi ili waendelee kujichukulia kama shamba la bibi.

Pamoja na kuona uwezo wa dawa za asili kugeuza mambo lakini suala la kusimamishwa kazi na kurudishwa nililiona gumu, kwanza nilijiuliza ninawezaje kurudishwa kazini wakati kuna ushahidi wa kunifunga. Lakini sikutaka kuumiza kichwa kwa vile siku iliyokuwa ikifuata ilikuwa jumatatu.

Nilipanga kwenda kazini japo moyo haukukubali kwa vile nilijiona kama nimechafua kambi, nilijiuliza madaktari na wauguzi watanitazamaje. Nilijikuta nikiwa katika wakati mgumu wa maamuzi kwa vile nilijiona kama mtu niliyevuliwa nguo kila mmoja pale hospitali angeniona kituko.

Lakini niliamini kwa vile nilikuwa naingia usiku nilijua hakuna wa kuniona zaidi ya watu wachache hata kama ningefukuzwa tofauti kama ingekuwa mchana. Kwa vile nilikuwa nyumbani na hali ya ofisini sikuijua siku hiyo sikuonja kinywaji kikali chochote nilikwenda macho makavu.

Nilinunua konyagi kubwa na kuiweka kwenye mfuko na kwenda kazini. Kama kawaida nilikuwa naingia saa mbili za usiku nikichelewa ilikuwa haifiki saa tatu usiku. Nilipofika nilimkuta mwenzangu akiwa bado yupo bize na kazi, nilimweleza apumzike kwa vile nimefika.
“Mawazo nilielezwa usianze kazi mpaka uonane na uongozi wa hospitali.”
“Mmh! Kwa nini wamekuambia hivyo?”
“Kwani kuna nini kimetokea?”
“Nikuulize wewe.”

“Mawazo, mwenye tatizo wewe uniulize mimi?”
“Kuna tatizo kidogo.”
“Basi ndilo hilohilo.”
“Kwa hiyo usiku anaingia nani?”
“Sasa hivi naingia asubuhi mpaka saa saa sita usiku nachukuliwa na gari mpaka nyumbani na kufuatwa alfajili kwa siku ambazo wewe hukuwepo.”

“Kwa hiyo baada ya kuondoka wewe nani anaingia kukupokea?”
“Huwa nafunga mpaka atakapopatikana mfanyakazi mwingine.”
“He! Ina maana kazi nimefukuzwa?” nilishtuka.

“Sijui, ila nilisikia kesi yako ni nzito kwa vile imechafua sifa ya hospitali na kuonekana maiti za watu huondoka na viungo nusu. Mi mwenyewe niliitwa polisi na kuhojiwa kwa siku nzima. Pamoja na vitisho nilikataa sijui kitu chochote japo wewe unajua umekuwa ukinipa pesa kiduchu kwa kazi kubwa.”

“Kwa hiyo wameamua kunifukuza kazi?”
“Sijajua ila nimesikia wanatafuta mtu mwingine ili nisaidizane naye, hata mimi wameisha nituma nitafute mtu nitakayefanya naye kazi.”
“Umeisha mleta?”
“Nimpate wapi kila mtu nikimgusia kazi ana kuwa na shauku lakini nikimweleza kazi yenyewe anaruka kama kaona nyoka mbele yake.”

“Poa, nikuache uendelee na kazi.”
“Hakuna tatizo, ila kesho kawasikilize huenda mkalimaliza.”
“Poa.”
Niliagana na Joseph na kurudi zangu nyumbani, nilimpigia simu dereva wangu ananifuate. Baada ya kunifuata sikwenda nyumbani moja kwa moja nilikwenda kwenye bar ya Somati. Aliponiona usiku ule aliniuliza:
“Vipi leo hukwenda kazini?”
“Nimekwenda.”

“Sasa mbona upo hapa?”
“Mmh! Mambo yameiva.”
“Kwani wamesemaje?”
“Nimeambiwa nisiingie kazini mpaka nionane na uongozi.”

“We nenda nina imani mambo yatakwenda kama ulivyoelezwa na mzee.”
“Mmh! Sawa, japo imenitisha kidogo.”
“We, kesho nenda kawasikilize watakachokisema wala usipingane nao.”
“Poa.”
Siku ile nilikunywa sana na kurudi nyumbani saa nane za usiku, nilipofika nilala mpaka saa tatu.

Niliamka na kupata kifungua kinywa kisha nilipelekwa na gari langu mpaka karibu na hospitali. Nilimweleza dereva wangu anisubiri kwenye maegesho mpaka nitakapotoka.
Nilikwenda hadi ofisini ya mganga mkuu, alipofika nilikaa kwenye viti kumsubiri kwa vile ilionesha hayupo ofisini. Baada ya nusu saa alionekana akiingia ofisini huku akiwa mwenye haraka. Mara alitoka ofisini bila hata kunisemesha alinipita kama hanioni.

Sikutaka kumshtua alionekana anakwenda wodini, niliendelea kumsubiri kwa zaidi ya saa mbili. Baada ya muda huo alirudi ofisini kwake wakati nataka kwenda nilimuona anatoka akiwa amevua nguo za kazi ikionesha anatoka. Pamoja na kuniona alionesha kutonijali. Kabla hajanipita nilimfuata na kumsemesha:
“Bosi vipi ina maana unanipita hunioni?”
“Una shida gani?” aliniuliza kama hanijui.

“Niliambiwa nisifanye kazi mpaka nikuone.”
“Nenda kwa sekretari kuna barua yako,” kauli ile ilinifanya nikumbuke maneno ya mganga ya kusimamishwa kazi ili kesi ikiisha wanifukuze rasmi.

“Sawa.”
Hakuongeza neno aliondoka zake kama amekutana na mzoga wa mbwa ilionesha wazi hakupenda kuniona kutokana na kashfa nzito iliyokuwa mbele yangu. Niligeuka kuelekea kwa sekretari kuchukua barua yangu ambayo sikujua imeandikwa nini japo niliamini kabisa ilikuwa ya kusimamishwa kazi.
Nilipofika kwa sekretari aliponiona alinishangaa kama ndiyo siku ya kwanza kuniona na kuniuliza.

“E’he nikusaidie nini?” aliniuliza kwa dharau kwa hali ile nilijiona tayari nimenuka.
“Nimefuata barua yangu.”
“Ooh! Ndiyo wewe unayegeuza bucha la viungo vya binadamu?

Siku mjibu alimwangalia tu kwa vile niliamini nina makosa hivyo sikutakiwa kujibu chochote zaidi ya kuchukua barua yangu na kuondoka. Aliinama kutafuta barua yangu kisha alinyanyua uso wake uliojaa dharau na kuniuliza:
“Unaitwa nani kweli?”
“Mawazo.”
“Oke, hii barua yako,” alisema huku akinikabidhi.

Niliipokea bila kusema kitu na kugeuka kuondoka, nilitembea huku moyo wangu ukiwa umetawaliwa na aibu. Niliajiona kama sina nguo japo nimejaa kwa kujua kila mtu pale hospitali anajua mchezo wangu mchafu wa kuuza viungo vya binadamu.
 
Sehemu ya 15

“Nimefuata barua yangu.”
“Ooh! Ndiyo wewe unayegeuza bucha la viungo vya binadamu?”
Siku mjibu alimwangalia tu kwa vile niliamini nina makosa hivyo sikutakiwa kujibu chochote zaidi ya kuchukua barua yangu na kuondoka. Aliinama kutafuta barua yangu kisha alinyanyua uso wake uliojaa dharau na kuniuliza:

“Unaitwa nani kweli?”
“Mawazo.”
“Oke, hii barua yako,” alisema huku akinikabidhi.
Niliipokea bila kusema kitu na kugeuka kuondoka, nilitembea huku moyo wangu ukiwa umetawaliwa na aibu. Niliajiona kama sina nguo japo nimejaa kwa kujua kila mtu pale hospitali anajua mchezo wangu mchafu wa kuuza viungo vya binadamu.

Pamoja na kuhakikishiwa na mganga kuwa kila kitu kitakwisha na mimi kurudi kazini, kwa hali niliyokutana nayo niliona kurudi kwangu kazini kutakuwa sawa na ngamia kupita kwenye tundu la sindano. Kufukuzwa kazi haikuwa tatizo kwa vile nilikuwa nimejipanga kimaisha tatizo kubwa lilikuwa kuondoka kwa kashfa.

Nilitembea nikiwa sijiamii kabisa kwani nilitamani niruke niwe ndani ya gari au kutokee giza linifiche na kutembea bila kuonekana. Lakini haikuwa hivyo nilijikausha na kwenda kwa mwendo wa haraka huku moyo ukinipasuka kila watu waliponiangalia au kusikia kicheko chochote niliamini watu hao wananiongelea.

Lakini nilifika mpaka kwenye gari langu bila kusemeshwa na mtu, baada ya kukaa kwenye kiti na kufunga mlango wa gari nilishusha pumzi ndefu na kutulia kwa muda huku kijasho kikinitoka. Muonekano wangu ulimtisha dereva wangu aliyetaka kujua kulikoni.

“Vipi bosi?”
“Mmh! Acha tu.”
“Hapana bosi inaonekana haipo sawa kabisa.”
“Nipo sawa, nipeleke nyumbani.”
“Sawa.”

“Dereva aliwasha gari kuondoka eneo la hospitali, nilipanga kuisoma barua baada ya kufika nyumbani lakini ghafla nilipata wazo la kwenda kwa Somati ili tujue tutafanya nini. Nilimpigia simu rafiki yangu aliyenieleza yupo kwake, nilimwambia asitoke nakwenda kwake.
“Kuna usalama lakini?”
“Kiasi.”
“Umepewa barua yako?”
“Ndiyo natoka kuichukua sasa hivi.”
“Inasemaje?”

“Sijaisoma, ila leo nimenyanyapaliwa vibaya.”
“Dah! Ilikuwaje?”
Nilimweleza kilichotokea pale hospitali baada ya kuonekana kama mimi ni kiumbe wa ajabu.
“Duh! Pole sana ndugu yangu ila nataka kukueleza kwa mzee kila kitu kitakwenda kama tulivyoambiwa. Sasa barua utaisoma muda gani?”
“Nakuja nayo kwako ili tujue wameandika nini.”

“Hakuna tatizo.”
Nilimwambia dereva anipeleke kwa Somati badala ya nyumbani, alinipeleka mpaka kwa rafiki yangu na kumweleza nikimuhitaji nitampigia. Niliamini pale nisingeondoka mapema. Niliagana na dereva wangu na kuingia ndani kwa Somati nilipokelewa kama kawaida kwa heshima zote.

Baada ya kukaa mke wa Somati alikuja kunisamilia:
“Jamani mpenzi karibu.”
“Asante.”
“Mke mwenzangu hajambo?”
“Hajambo.”
“Watoto wetu?”
“Wote hawajambo, sijui ninyi?”
“Mmh! Hatujambo, haya mume nikuletee supu au maji makali?”
“Maji makali, supu nimeisha kunywa kwa mwenzako.”

Siku zote mke wa rafiki yangu hakutaka msichana wa kazi anihudumie kwani alipenda kunihudumia kama mumewe hasa kutokana na kuujua urafiki wetu. Baada ya kuniletea chupa kubwa ya whisky na glasi mbili. Mara alitokea rafiki yangu Somati nilinyanyuka na kukumbatiana.

“Karibu best.”
“Asante.”
Baada ya kukaa na kuanza kunywa whisky taratibu, niliitoa barua na kuisoma peke yangu iliyoonesha nimesimamishwa kazi kwa tuhuma za kuhusika na uuzaji wa viungo vya maiti mpaka uchunguzi utakapomalizika. Baada ya kusoma nilimpa Somati naye alisoma na kuniambia:

“Ni yaleyale tuliyoelezwa, nina imani mambo yanakwenda kama yalivyopangwa.”
“Lakini mbona kuna kitu kinanitisha?”
“Kitu gani hicho?”
“Hali niliyoikuta inaonesha nimenuka hispotalini.”

“Hiyo yote inajulikana ndiyo maana ukaelezwa ukirudi kazini na kuiweka ile dawa kutokana na maelezo ya mganga kila kitu kitakuwa sawa hata asiyekupenda atabadirika na kukupenda. Ondoa wasiwasi kazini utarudi na ukirudi usifanye makosa tena.”
“Nimekuelewa rafiki yangu.”
Siku ile nilikaa kwa Somati mpaka usiku na kurudi kwangu nikiwa nimependeza kichwani baada ya kunywa pombe za kutosha.
***
Nilikaa nyumbani kwa wiki moja huku nikisubiri kupelekwa mahakamani baada ya upelelezi. Nilijikuta mtu mwenye mawazo mengi juu ya kusubiri upelelezi kukamilika kwa kuamini lazima nitakutwa na hatia kutokana na mtuhumiwa namba moja kukutwa kweli na viungo vya binadamu.

Niliendelea kukaa nyumbani huku hali yangu ya kifedha ikiwa si nzuri hasa kutokana na kuweka pesa nyingi katika miradi yangu hasa katika ujenzi wa nyumba yangu ya ghorofa moja. Nilijiuliza kama sitarudishwa kazini nitafanya nini, lakini siku zote Somati alinipa moyo kwa kunieleza jambo lile ni dogo lazima litaisha tu.

Katikati ya wiki ya pili nikiwa nyumbani nilipata simu kutoka hospitali, nilijiuliza ya nini. Baada ya kupokea nilielezwa natakiwa hospitali mara moja. Niliwaeleza kama suala lipo polisi wasubiri kwa vile hata wakiniita siwezi kuwasaidia chochote. Walinieleza wanachoniitia ni kitu kingine kabisa.

“Samahani Mawazo si suala la polisi bali tuna shida na wewe.”
“Shida gani?”
“Ya kurudishwa kazini.”
“Nitarudi vipi ikiwa kesi haijaisha?”
“Sawa nitakuja.”

Baada ya kukata simu nilimpigia simu Somati kumweleza habari zile:
“Mawazo kila alichokisema mzee kinaonekana, umepewa barua ya kusimamishwa kazi na leo umeitwa kazini. Nina imani kazi yako itakuwa ndogo.”
“Na kweli rafiki yangu, unajua wiki mbili tu akili imekaa sawa sijui ingekuwa miezi ingekuwaje?”

“Polw, nenda kawasikilize.”
“Poa.”
Baada ya kuzungumza na Somati nilijiandaa na kutoka kwenda kazini kusikiliza wanasemaje. Nilipofika nilikwenda moja kwa moja ofisi ya mganga mkuu kama nilivyopewa maelezo. Ilikuwa tofauti na siku niliyokwenda kuchukua barua ya kusimamishwa kazi.

Nilimkuta secretari akisoma kitu kwenye kompyuta nilimsamilia, aliponyanyua macho na kunitazama aliponiona ni mimi alisema:
“Ooh! Mawazo umefika?”
“Ndiyo.”
“Subiri kwenye kochi.”
“Sawa.”

Nilirudi kukaa kwenye kochi kusubiri kupewa ruhusa ya kuonana na mganga mkuu. Nikiwa nimekaa nilijiuliza maswali mengi juu ya wito ule na uchangamfu wa secretari ambaye siku ya kwanza alininyanyapaa kwa kunitazama kama kinyesi lakini ajabu siku ile tabasamu lilimtawala usoni.

Nilijiuliza wamegundua kitu gani mpaka kuamua kunirudisha, lakini nilikumbuka maneno ya mganga watanirudisha kwa muda ili kuvuta siku waweze kunifunga. Kutokana na maelezo ya mganga kuwa kurudishwa kwangu ni kumaliza tatizo zito lililokuwa mbele yangu kwa kukiweka dawa sehemu za nyuma za maiti.
Nikiwa katikati ya mawazo secretari wa mganga mkuu aliniita:
“Kaka Mawazo.”
“Naam.”
“Unaambiwa uingie.”
 
Sehemu ya 16

Nilijiuliza wamegundua kitu gani mpaka kuamua kunirudisha, lakini nilikumbuka maneno ya mganga watanirudisha kwa muda ili kuvuta siku waweze kunifunga. Kutokana na maelezo ya mganga kuwa kurudishwa kwangu ni kumaliza tatizo zito lililokuwa mbele yangu kwa kukiweka dawa sehemu za nyuma za maiti.
Nikiwa katikati ya mawazo secretari wa mganga mkuu aliniita

“Kaka Mawazo.”
“Naam.”
“Unaambiwa uingie.”
Niliingia ofisini kwa mganga mkuu, aliponiona alisimama kwa heshima.
“Ooh! Bwana Mawazo.”
“Naam mkuu.”
“Karibu sana.”
“Asante.”

Alinionesha kiti nikae nami nilikaa na kusubiri kusikiliza wameniitia nini, baada ya ukimya mfupi alisema:
“Ndiyo bwana Mawazo, kutokana na uchunguzi wetu tumeona kama tuhuma zilizopo mbele yako hazina ukweli wowote. Hivyo basi uongozi wa hospitali wameamua kukurudisha kazini.”
“Asante bosi wangu.”

“Sasa kuanzia leo utaanza kazi mara moja, kwa vile sasa hivi mwenzako ana matatizo utakuwa unaingia saa kumi na mbili alfajiri na kutoka saa sita usiku mpaka hapo mwenzako atakaporudi hivyo mtaendelea na zamu zenu za kawaida. Saa zote za ziada zitalipwa kama over time.”

“Hakuna tatizo.”
“Vipi unaweza kuanza leo?”
“Hakuna tatizo.”
Baada ya mazungumzo nilipewa funguo na kwenda sehemu yangu ya kazi, nilimkuta mhudumu akiingiza maiti kwenye chumba cha kuhifadhia maiti. Nilipoingia nilikwenda ofisini kwangu na kuchukua nguo zangu za kazi na kuanza kazi mara moja. Ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti, maiti zilikuwa zimekaa hovyohovyo.

Niliingia kwenye kazi ya kuzipanga vizuri na zingine kuziweka kwenye majokofu. Kazi ile niliifanya kwa zaidi ya saa mbili bila kupumzika. Baada ya muda chumba kilikuwa katika muonekano nzuri.

Kama kawaida mnilifanya kazi mpaka saa sita usiku, kwa vile sikujiandaa hata dawa yangu sikuichukua. Muda ulipotimu nilipofuatwa na gari kunipeleka nyumbani, lakini niliwaambia wanishushie njiani ili nipande gari langu na kurudi nyumbani.

Baada ya kunifikisha sehemu niliyo waelekeza niliteremka na kusubiri gari langu lililonichukua mpaka nyumbani. Kabla ya kulala nilimpigia simu Somati kumweleza kilichojili naye alinieleza:
“Kazi kwako kila kitu kinakwenda kama alivyosema mzee sasa ushindwe mwenyewe.”
“Kazi yenyewe naifanya kesho chelewachelewa wanaweza kubadili mawazo.”

“Wakati ni huu rafiki yangu.”
“Nimekuelewa.”
Siku ya pili niliamka saa kumi na moja na kupanda gari mpaka sehemu ambayo gari la kazini lingenipitia. Baada ya muda gari lilinipitia hadi kazini na kuingia kazini siku ile nilikuwa na kazi ya kujua kuna maiti ngapi zilizoingia na zinazotakiwa kutoka zisizo na ndugu ambazo zilitakiwa kuzikwa na jiji.

Siku ile nilikuwa na kazi nzito ya kupitia kila kitu, ilikuwa kazi nzito sana, lakini niliifanya vizuri na kuweka mambo sawa. Katika mauti zilizotakiwa kutoka siku inayofuata nilichagua moja ambayo ilikuwa na jina la kikiristo ambayo niliamini nikiiwekea dawa haitaguswa baada ya kuoshwa palepale hospitali na kuvishwa nguo baada ya hapo ni kuwekwa kwenye jeneza kusubiri kwenda kuzikwa.
Niliitafuta moja na kuiweka sehemu ya karibu ili nisipate shida kufanya mambo yangu.

Majira ya saa tatu usiku nilijifungua ndani na kuitoa maiti ya msichana aliyekufa kwa kunywa sumu na kuilaza sehemu ya kuoshea. Niliichukua dawa na kunuiza kama nilivyoelekezwa kisha niliingiza sehemu ya nyuma za yule mwanamke.

Niliingiza yote kisha nilimrudisha katika hali ya kawaida na kumrudisha kwenye jokofu. Baada ya zoezi kwenda vizuri niliendelea na kazi zangu kama kawaida mpaka muda wa kutoka. Siku ya pili nilidamka alfajiri na kuwahi kazini kama kawaida kuendelea na majukumu yangu ya kila siku.

Wakati huo muda wangu wa kurudi mahakani ulikuwa ukikaribia.
Siku ile zilikuwa zikitoka maiti kama nne na niliyoiwekea dawa ilikuwa moja wapo, kutokana na masharti ya mganga nilitakiwa kujua maiti inakwenda wapi na mimi kuhudhulia mazishi yake. Nilikumbuka ndugu wa marehemuwalipoileta mwili kuuhifadhi walisema angezikwa siku ile palepale mjini.

Lakini ratiba iligeuka baada ya bibi kizaa baba amesema hawezi kuja kuzika hivyo mjukuu wake amfuate hukohuko kijijini ili amzike. Hivyo niliona mipango yangu yote ilivurugika. Mwili ungechukuliwa na kupelekwa kijijini kwa mazishi na si mjini tena, baada ya kuoshwa na kuvishwa nguo na kina mama ungesafilishwa.

Hapo nilichanganyikiwa na kuona kama mambo yanataka kwenda ndivyo sivyo, nilijiuliza nitafanyaje ikiwa maiti ile itasafilishwa na kwenda kuzikwa sehemu nyingine. Heri taarifa nimezipata mapema ningefanya mchakato kuitoa dawa niliyoiweka japo niliamini huenda ingenipa kazi kuitoa kwa vile niliingiza ndani sana.

Ajabu nyingine ndugu wa marehemu waliwahi asubuhi sana kwa ajili ya maandalizi ya kumpamba marehemu ili waondoke mapema kuwahi kufika na kumzika siku ileile.

Nilijiuliza kama akizikwa mimi bila kuona madhara yake nini, kingine kibaya nilijilaumu nilipokuwa kwa mganga sikuuliza kama maiti ikizikwa mbali inakuwaje. Yote ilitokana na kujiamini maiti ambayo ningeiwekea dawa itazikwa palepale mjini.
Ningeweza kuweka katika maiti zangu zisizo na ndugu, lakini sharti kubwa lazima maiti azikwe na umani wa watu na si wachache. Niliamua kumpigia simu Somati kumuuliza itakuwaje.

“Kwani tatizo nini?”
“Si unakumbuka mzee alisema ikiwezekana nihudhulie mazishi ili nione anavyozikwa.”
“Hakusema lazima bali kama ingekuwa na nafasi ya kuhudhulia ingekuwa vizuri zaidi.”

“Nina wasiwasi na maiti inayosafilishwa wanaweza kwenda kinyume.”
“Kinyume vipi?”
“Wanaweza wasimzike.”
“Acha mawazo ya kitoto, umesema wamesema wanakwenda kumzikia kwao si kwenda kumtupa wewe wasiwasi wako nini?”

“Nilifikiria labda kuna tatizo.”
“Hakuna tatizo lazima atazikwa tu.”
“Ooh! Afadhali maana nilichanganyikiwa.”
Baada ya kukata simu nilipumua pumzi ndefu kushusha hofu iliyokuwa imetanda moyoni mwangu. Wakati huo niliendelea na zoezi la kutoa miili ya marehemu waliofuatwa na ndugu zao.

Maiti iliyoiwekea dawa niliitoa na kuiweka juu ya karo la kuoshea na kuwachia kina mama wamuandae na kumvisha nguo kabla ya kumlaza kwenye jeneza.
Ili kutaka kujua kila kitu cha yule marehemu nilijifanya kuonesha masikitiko kwa ndugu wa marehemu. Nilimfuata mmoja na kumdodosa bila kujua.

“Kwani mnakwenda kuzikia wapi?”
“Kijijini.”
“Dah, binti kaniuma sana alikuwa mdogo sana.”
“Bwana wangu wee mapenzi ya kitoto yamepelekea yote haya, alikatazwa kuolewa kwa vile alitakiwa aendelee kusoma yeye akaamua kujiua.”
“Poleni sana, sasa ndugu yangu kwa kweli msiba huu umenigusa kuliko misiba mingi iliyowahi kuiona.”

“Ni kweli alikuwa bado binti mdogo hata wazazi wake walimtegemea, kama angezikwa hapa msiba wake ungekuwa na watu wengi sana hata hivyo watu tunaokwenda kijijini ni wengi sana kuna mabasi sita, coaster tano gari ndogo zipo kumi na tano nafikiri umeona wingi wa watu.”

“Mmh! Kweli, sasa hebu nipe namba yako ya simu ili nijue kama mmezika salama.”
Jamaa alinipa namba bila kujua dhamira yangu ilikuwa tofauti na mawazo yake.
“Mnategemea kuzika lini?”

“Leoleo ndiyo maana tunatoka asubuhi sana ili mpaka saa saba tuwe tumefika na kufanya maandalizi yote ikiwemo ibada na kuaga. Nafikiri mpaka saa kumi tutaweza kuuhifadhi mwili wa mwanetu.”
“Mwenyezi Mungu atampumzisha kwa amani.”

“Amen.”
Kwa vile nilikuwa bado na majukumu mengi niliachana na yule mtu na kuendelea na majukumu mengine. Baada ya matayarishi yote mwili iliingizwa kwenye jeneza na kupelekwa kwenye gari maalumu. Watu walipanda kwenye magari na kuondoka wakiniacha nikiendelea na kazi yangu.

Majira ya saa kumi na mbili jioni nilimpigia simu yule jamaa niliyezungumza asubuhi na kunipa namba ya simu:
“Haloo ndugu yangu.”
“Ndiyo, nazungumza na nani?” aliniuliza.
“Yule jamaa wa chumba cha kuhifadhia maiti.”

“Ooh! Kaka za muda?”
“Nzuri, mmefika salama?”
“Tunashukuru Mungu, tumefika salama yaani ndiyo tumetoka kuzika hivyo kuna watu watarudi leo na wachache tutabakia.”
“Ooh! Mungu ampe mapumziko mema marehemu wetu,” nilimuombea marehemu kinafiki.

“Amen.”
“Basi nikuache upumzike kwanza.”
“Hakuna tatizo ndugu yangu jioni njema.”
“Asante.”
Nilikata simu na kushusha pumzi ndefu na kunyanyua mikono juu kushukuru mambo kwenda kama yalivyopangwa. Moyo wangu ulijaa furaha na kuifanya kazi kwa amani huku nikisubiri majibu ya kitu nilichokifanya. Nilimpigia simu Somati kumjulisha kilichojili.

“Sasa umeona, ulikuwa na wasiwasi bure nani aliisha uchukua mwili wa ndugu yake na kwenda kuutupa au kuula nyama?”
“Hakuna, lakini hali ilikuwa inatisha, si unajua narudi mahakamani wiki ijayo.”
“We nenda tu hakuna kitu, kila kitu umekizika, kama maiti anafufuka basi na tatizo lako litaendelea.”
“Duh, baada ya tatizo hili natakiwa niwe makini sana.”

“Walaa, hakuna tena tatizo fanya kazi zako kama kawaida, sikukuambia tu hata mimi iliisha wahi kunikuta kama yako nami nilifanya kama ulivyofanya mambo yote yalijizika.”

“Kama ni hivyo nitafurahi sana.”
“Yule mzee mwisho wa maneno.”
Baada ya kukata simu niliendelea na kazi zangu huku furaha ikizidi japokuwa bado sikuwa na uhakika asilimia mia moja kuwa kila kitu kimejizika.
 
Sehemu ya 17

Yalikuwa maajabu ya karne kesi iliitwa mara mbili na kutolewa hukumu na mahakama kutuachia huru kutokana na kukosekana ushahidi wa kweli. Kizibiti kilichokuwa kama ushahidi wa viungo vya binadamu kilionekani si viungo bali vipande vya mti. Askari na baadhi ya madaktari pamija na wauguzi wa hospitali niliyokuwa nafanya kazi waliokuwepo mahakamani alishtuka sana lakini ukweli ukabakia palepale kuwa hatuna hatia.

Baada ya mahakama kunisafisha niliendelea na kazi huku nikiombwa radhi na kulipwa fedha za usumbufu. Niliamini watu wanajua kufuru ya kushindana na Mungu kwa kuibadilisha kweli kuwa uongo. Walishindwa kitu kimoja kuurudisha uhai wa mtu tu lakini vingi walijifanya kumchokoza Mungu.

Baada ya kesi yangu niliendelea na kazi yangu huku woga ukiwa mkubwa japokuwa Somati alinitoa hofu na kunieleza niendelee na biashara yangu kama kawaida. Pamoja na unitoa hofu nilikaa kwa muda wa miezi mitatu huku nikipokea oda na kuwaeleza watulie kwa muda ili waajili wangu hata kama wana wasiwasi na mimi hofu yao iondoke.

Nilipoona mambo yametulia nilianza rasmi biashara yangu safari ile nilikuwa na oda nyingi sana za pesa nyingi. Nilipanga nikimaliza oda ile niache na kazi ili nifanye mambo mengine kama Somati ikiwezekana nimrudie Mungu kwani niliamini niliyoyafanya yote yalikuwa chukuzo la Mungu pamoja sikutoa uhai wa mtu lakini kufanya viungo vyao biashara lazima nilimuuzi muumba.

Wiki ya kwanza kuanza tena biashara yangu nilitengeneza pesa kama sina akili nzuri, biashara ya watu watatu ilinipatia pesa nyingi. Miezi sita niliamini inanitosha kufanya kazi ile na kuachana nayo. Biashara iliendelea vizuri huku kipato kikiongezeka mara mbili ya mwanzo.

Miezi mitatu baadaye nakumbuka siku moja ambayo haitatoka akilini mwangu mpaka nakufa. Nilipata tenda ya pesa nzuri sana ambayo nilipewa na mtu mmoja mwenye uwezo wake mkubwa sana. Alikuwa akitaka maiti ya mtoto mwenye jinsia mbili na kuzikata zote na kumpelekea.

Kazi ile niliamini ni vigumu kuipata kwa vile asilimia kubwa ya maiti za watoto huzikwa na familia yake labda zile ambazo hazijatimiza muda tulizizika wenyewe kwa malipo.

Kazi ya kuzika nilimpa aliyekuwa akiingia asubuhi kwa vile pesa yake ilikuwa ya sabuni tu. Kwa vile mchana sikuwepo nilimpa wanawake wawili wa upande wa leba tenda ya kutafuta maiti ya mtoto mwenye jinsia mbili japo nilijua kuipata ilikuwa nguvu.

Nilitoa ofa ya shilingi milioni moja, niliyemwambia aliona utani, nilimweleza kama akipata asinipe mzigo mpaka nimpe kiasi chake. Ili kuwavuta kila nilpokutana nao niliwapa pesa ya chai mpaka ikafikia hatua ya kuniona nipo serious.

Nao waliniahidi kunipa ushirikiano mkubwa.
Haikupita hawa wiki mbili nikiwa nyumbani baada ya kutoka kazini nilipigiwa simu na mmoja ya watu niliowapa kazi ya kutafuta mwili wa mtoto mwenye jinsia mbili akiniambia mzigo umepatikana kwanza sikuamini nilimuuuliza mara mbilimbili.

“Unachosema ni kweli au unatania?”
“Kweli kabisa.”
“Umemuangalia ana jinsia mbili?”
“Ndiyo.”
“Ulimpataje?”
“Kaka wewe hebu nielekeze upo wapi ili nikuletee mzigo tumalizane.”
“He! Umetoka nao?” nilishtuka.
“Bwana wee mbona sikuelewi biashara inafanyika au haifanyiki?”

“Inafanyika.”
“Basi nielekeze upo wapi nikuletee mzigo.”
“Upo wapi?”
“Nipo sehemu baada ya kutoroka kazini na kuacha msala.”
“Kwa hiyo kuwa watu wamekuona?”
“Kaka hii ni biashara ya hatari nimejitolea maisha yangu si ya kuzungumza kwenye simu.”

“Nielekeze upo wapi nije nikufuate.”
Alinielekeza alipo nilimtuma gari mbili moja kuchukua mzigo na kuupeleka katika jumba ninalojenga ambako ndipo nilipopaona panafaa kuifanya kazi ya kumkata viungo na kuviuza. Kwa vile kazi ya kuuza viungo ilikuwa ya siri nilimweleza kijana wangu asifungue mzigo atakaopewa na kwenda kuuweka kwenye moja ya chumba kilichokuwa na mlango.
 
Sehemu ya 18

Alinielekeza alipo nilimtuma gari mbili moja kuchukua mzigo na kuupeleka katika jumba ninalojenga ambako ndipo nilipopaona panafaa kuifanya kazi ya kumkata viungo na kuviuza. Kwa vile kazi ya kuuza viungo ilikuwa ya siri nilimweleza kijana wangu asifungue mzigo atakaopewa na kwenda kuuweka kwenye moja ya chumba kilichokuwa na mlango.

Baada ya muda nilielezwa kila kitu kimekwenda vizuri, nilimweleza dereva aliyembeba yule muuguzi ampeleke sehemu. Nilichukua fedha ya malipo ya kazi na gari jingine na kwenda kumalizana. Nilikwenda sehemu tuliyomuelekeza kijana wangu.
Nilikutana na muuguzi yule aliyekuwa mama mtu mzima, aliponiona aliniambia kitu:
“Mwanangu imebidi nipate dhambi kwa ajili yako.”

“Kwa nini?”
“Wakati tunamzalisha mzazi alipoteza fahamu dakika za mwisho lakini mtoto alikuwa ametoka salama, mimi ndiye niliyempokea baada ya kumuona ana jinsi mbili nilishtuka sana. Niliwangalia wenzangu waliokuwa katikati pilikapilika za kumhudumia mzazi nikaona ile ndiyo nafasi yangu. Kwa vile ilikuwa lazima nimpate ilibidi nimkabe kumuua huoni hapo baba nimepata dhambi ya kuua?”
“Mama dhambi kaumbiwa mwanadamu, kwa vile umefanya kazi ya ziada nitakupa milioni mbili.”

“Ha! Kweli?” alishtuka.
“Umefanya kazi kubwa sana,” nilimpa milioni mbili na kumwambia dereva wangu ampeleke kwake.

Baada ya kuachana na yule muuguzi nilijikuta nikiwa na shauku ya kuuona mzigo, niligeuza gari langu na kwenda kwenye jumba langu lililokuwa katika hatua nzuri hasa baada ya kurudi kwa kasi katika kuendelea na ujenzi baada ya kukwama kutokana na matatizo ya mmoja ya wateja wangu kukamatwa na viungo vya binadamu.

Nilikwenda hadi kwenye saiti ya ujenzi wa jumba langu, niliingia kwenye chumba cha nilichoelekeza mzogo uwekwe. Nilifungua na kuukagua na kukuta kweli ni maiti ya mtoto yenye jinsia mbili. Moyo wangu ulilipuka kwa furaha kwa kuamini nilikuwa natengeneza pesa nyingi sana kwa biashara ile.
Nilimpigia simu mteja wa mzigo ule ambaye hakuamini kusikia nimepata mzigo aliokuwa anataka kwa udi na uvumba.

“Siamini kweli unachokisema?”
“Kazi yangu si unaijua kama huamini njoo uone mwenyewe kabla sijamkata viungo.”
“Basi nitamtuma mtu usiku afuate mzigo wewe njoo tumalizane kabisa uchukue chako.”

“Mzigo siyo upo hospitali ninao mwenyewe.”
“Usiniambie!” jamaa alishtuka.
“Kaka ninapopewa kazi na watu wazito kama ninyi huwa sifanyi mchezo nimehakikisha unapatikana kwa hali na mali.”
“Kaka sikuwezi, kwa hiyo unaniletea sasa hivi.”
“Ndiyo maana yake, kama unaweza njoo umuone kabisa kabla sijamkata.”
“Hapana nakuamini, njoo na mzigo nikupe chako.”

“Sawa, nitafika muda si mrefu.”
Kwa vile sikuwa na vitu vya kukatia nilimtuma dereva wangu akaninunulie kisu kikali na gloves na kalatasi la sandarusi kwa ajili ya kutandika kwenye meza wakati wa kuvikata viungo maiti ya kichanga kile. Kwa vile maduka hayakuwa mbali sana baada ya muda mfupi nililetewa vifaa nilivyoagiza.

Nilijifungua ndani na kutandika kalatasi pana la sandarusi na kuilaza maiti ya kichanga. Nilivaa gloves na kushika kisu ili nianze kuikata viungo huku mapigo ya moyo yakienda mbio kwani muda si mrefu nilijua nitashika pesa nyingi sana ambazo zingeniweka katika hatua nyingine kabisa katika maisha yangu.

Nilianza kukata kiungo cha kwanza, ajabu baada ya kisu kuanza kukata ilitoka damu nyingi tofauti na mwili unavyokuwa ukipoa. Sikuacha niliendelea kukata lakini ghafla kile kichanga nilichokuwa nakikata kilianza kulia kwa maumivu. Nilishtuka na kujiuliza kile kiumbe kililetwa kipo hai au kimekufa.
Sauti ile iliendelea na kunifanya nichanganyikiwe kwani kwa uzoefu wangu wa kukutana na miili kama ile niliamini kile kichanga hakikuwa na uhai.

Sauti yake ilikuwa kali iliyooneka kama inasikika nje. Wakati huo nje nilisikia sauti za watu wakizungumza kama wamesikia sauti ya yule mtoto akilia.
Niliweka kisu kando na kuvua gloves kisha nilifunika na nilikwenda kufungua mlango ili niwaone hao watu waliokuwa wakipiga kelele huku nijiuliza waliwezaje kuingia ndani bila kuzuiwa na mlinzi. Wakati huo sauti ya kilio cha mtoto ambaye hakuonesha uhai lakini aliendelea kulia ilizidi nayo kunichanganya.
Nilitoka hadi kwenye kurido ambako kulikuwa juu ghorofa ya kwanza na kuangalia chini.

Nilishtuka baada ya kuona chini kumejaa watu ambao walinitisha sana walikuwa ni maiti walionekana wamefufuka wapo waliokuwa na sanda mpya wengine zilizokwisha na miili yao kuonekana imeharibika.

Kwanza niliona kama njozi lakini kilichokuwa mbele yangu haikuwa njozi bali kitu cha kweli. Getini mlinzi alikuwa amekaa akionesha hajui kitu kilichokuwa kikiendelea wakati ule. Nilitahidi kufikicha macho kupata ukweli lakini haikuwa njozi bali kitu cha kweli.

Nilijiuliza mbona mlinzi haoneshi kushtushwa na viumbe wale, kilichonishtusha sana katika kundi la wale maiti ambao baadhi walikuwa na viungo nusu hazikuwa ngeni machoni mwangu nilizikumbuka niliwahi kuziona hata zingine kushiriki kukata viungo vyake.

Nilijiuliza walipitaje toka makaburini mpaka kwangu bila kuonekana. Kati ya zile maiti kuna moja ilizikwa mbali sana mfano ya binti aliyejiua alizikwa kwao mbali lakini na yeye alikuwemo hata mama mjamzito aliyesafilishwa nje ya nchi kutokana na uraia naye alikuwepo. Wote walikuwa wamesimama mbele ya nyumba yangu wakinishutumu kwa unyama niliowafanyia.

Hali ya hewa ilianza kubadilika na kuwa nzito kutokana na harufu kali kutawala eneo lote iliyotokana na baadhi ya maiti zingine zilizooza kutoa harufu kali. Wakati nikuwa bado sijakubaliana na kilichokuwa mbele yangu ambacho nikiamini ni ndoto tu wala si kitu cha kweli.

Wale maiti waliokuwa kama katika muziki wa Michael Jackson ‘Thiriler’ walianza kunifuata kupitia njia ya ngazi kunipandia juu. Ilionesha kila mtu alikuwa akilalamika lake kutokana na kitendo changu cha kikatili cha kuthamini pesa kuliko utu wa mtu. Wapo waliposema nami watanikata viungo mwingine alisema ile ndiyo ilikuwa siku yangu ya mwisho.

Zogo lilikuwa kubwa sana mpaka ngoma za sikio niliziona kama zinataka kupasuka. Sauti zilizodi kunisogelea zikionesha zina hasira sana na mimi, nilijiuliza wale watu wakinishika watanifanya nini. Nilijikuta nikipata wazo la kijinga kuruka toka juu ili kuwakimbilia.

Nilishtuka kuwaona wakitokea kwenye mlango wa kuelekea nilipokuwa nimesimama huku nimechanganyikiwa. Sikukubali wanikamate kwani maneno yao yalionesha wana hasira na mimi. Niliwapowaona wakinisogelea bila kuangalia nitaangukia wapi nilijiachia nilipokuwa nimesimama na kujitupa chini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom