Simulizi: Kisanga

Simulizi: Kisanga

KISANGA (Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao

Sehemu 4F

Ilipoishia....
.... wa Nkole yupi, Nkole kwani anamtoto?!” Fiyona alisema sasa akisimama katoa macho huku akizivuta kumbukumbu taratibu, Mbonde akimshanga tu “…ina...Ohh! yule ni mtoto wa Nkole!?” “Unashangaza sana wewe, naz utashangaa mengi mwaka huu, ni mtu usiyejali kabisa hisia za mtu mwengine umejawa na ubinafsi tu” Mbonde alisema nakutoka nje mkuku mkuku akimuacha Fiyona njia panda.

Tuendelee...
MUDA HUO HUO
MTAA WA KIPASO-JIJINI NYATUMBU
Gotwa hofu ilikuwa machoni akihema akichungulia, mbele yake wanaume wasioleweka lakini shari ikiwa wazi wakisemeshana kwa ishara nyuso zikiwa na vinyago, bastola mikononi wakitawanyika kila kona ya nyumba “Hakikisheni tuna upata mzigo haraka iwezekanavyo. Bila kuacha ushahidi na kumuacha Nkole salama” mmoja aliongea kwa sauti kavu na nzito yenye amri. Mti Mkavu alishtuka kusikia sauti hiyo akapatwa na shangazo “Mbona hii sauti sio ngeni” alijismea kwa kunon’gona kiasi cha kumshangaza Mti Mkavu na kisha akatingisha kichwa kukubali “Inamaana wamekuja tena au..” alisema tena Gotwa na kuikumbatia vzuri tarakilishi mpakato.

Mti Mkavu pembeni yake akionekana kuweka ulinzi dhidi yake aliduwaa akimtazama Gotwa “Mzigo huu hapa nimeupata” mmoja alisikika akiongea “Shabbash imekaaa vizuri sasa yuko wapi Nkole muda huu?!” aliongea bwana yule wa mwanzo akitaraji jibu kwa watu walio mzunguka kwa kuwatazama kwa zamu “Twendeni hili ni muhimu zaidi” huyo mbele yao nyuma akifatwa na vibaraka wake. “Mti Mkavu nafikiri umeshahakikisha vya kutosha inatosha tuanze kazi yetu” sauti ya Burushuti ilimpitia Mti Mti Mkavu “…naona akili yake inavyofanya kazi haraka, ameigundua karata inayotumika mara mbili” alisema Mti Mkavu aliyekusanya mikono yake kifuani akimtazama tu Gotwa kwa makini sana akimchimba.

Si muda, Mbonde akapaki gari yake kando ya barabara umbali wa mita khamsini hivi na kuzima taa za gari mikono ikiwa usukanini akijiwazia. Macho mbele, uso wake ukabadilika “Kina nani tena?!” akajituliza akiangalia vizuri watu kama sio saba basi nane wakiingia kwenye gari mbili nyeusi wakitokea kwenye nyumba ya Nkole na kutimka zao “Mhhh!” akatoka garini na kuelekea kwenye nyumba ya Nkole. Mngurumo toka surualini ndio ulio mshtua kiasi cha kushika kifua chake huku macho kayafumba asiamini, aliitoa na kupokea “…aisee jamaa tulia waambie amenitoroka tulipokuwa tukipata staftahi pale Yombo…ndio waeleweshe hivyo hivyo mtu wangu…nakuaminia” akakata na kuirejesha simu mfukoni akatafakari kidogo akafonyaa huku akichalanga mbariga.

Alikomea nyuma ya nyumba akaingia kwa mtindo aliuzoea huku akitazama madirishani. Burushuti akiwaz karibu yake akimfatilia tu. Mbonde akaupiga mluzi na kutulia ukasikika mluzi upande wa ndani akatabasamu, huyo akaufata mlango na kuingia. Macho kwa macho alikutana na Gotwa amesimama “Vipi mjomba baba yupo wapi?” lilikuwa ni swali la Gotwa uso mashakani “Yupo sehemu salama…” aliongea huku akishangazwa na mazingira yalivyo kila kitu kimechanguka, akaikunja midomo yake kisha kamtazama Gotwa akiyaona majibu usoni mwake akauma meno “…lakini sio salama sana, Gotwa hivi kuna kitu unachokijua kuhusu baba yako na unaweza niambia walau kiduchu” “Ndio mjomba nifate kuna kitu mimekigundua kipindi tu ulipo toka wewe” Gotwa akatangulia huku Mbonde akimfata nyuma. “Ndugu yangu kuna mambo mengi yanaendelea kumuhusu huyu Mbonde kama tulivyo wasiliana ni wazi ana msaada lakini si wa kuaminika naomba tumpe nafasi kidogo ya leo tupate majibu kamili kabla ya kumkausha” aliongea Burushuti wakipiga hatua kuwafata “Sawa naona unakaribia kushinda” alisema Mti Mkavu na kutabasamu. Safari yao iliishia kwenye moja ya chumba.

Chumba kilichoonesha wazi ndio hasa chumba cha mwandishi Nkole kutokana na nguo zake pamoja na picha za ukuta zikining’inia hakukuwa na haja ya kuuliza. “…mjomba baba sio mtu wa kawaida ukimuona kama mjinga mjinga lakini ni mtu mwenye kufanya mambo makubwa hebu ona” Mbonde alitamani kucheka lakini akajizuia akifata maelekezo ya Gotwa asiye na shaka akijua akifanyacho, Ajabu! Gotwa akasogea hadi kwenye kabati lililojengewa ukutani akazitoa nguo kulikuwa na kitu kama mfuniko mweupe akauzungusha na kamlango kadogo ka mbao kakafunguka Mbonde mdomo ukamshuka macho katumbua “…nifate mjomba” Gotwa aliongea na kumtoa Mbonde kwenye Mgando, wakaingia kwa kuinama.

Kachumba kadogo kalikuwa mbele yao chenye upana wa mita tatu kwa mbili.
Mbonde macho kayatumbua akitazama tarakirishi mbili moja ikiwa imewaka ikionesha matukio yanayoendelea nyumba nzima kwa kamera zilizo tegeshwa akatabasamu aliona bunduki ndogo mbili mezani kando ya komputa , vifaa vya kisasa vya uchunguzi, picha za viongozi kazaa ukutani magazeti kazaa ya kitaifa na kimataifa “Nkole wewe ni nani hasa!!!?” alijikuta akiongea Mbonde kwa mshangao asiamini anachokiona “Baba ni Mpelelezi kama wewe” aliongea Gotwa pasina wasiwasi bila uwoga, Mbonde akashtuka akimtazama vizuri kwa jicho la Umejuaje? Akimtafakari kwa udogo wake na namna mazneno mazito ayatoayo pasina shaka “Ndio mjomba nimejua ulivyoondoka tu nilichunguza kila kitu nilimchunguza namna alivyokuwa msiri kuyafanya mambo yake”

Mbonde mdomo ukabaki wazi Mwaa! “We mtoto mbona unahatari…baba yako anajua kuwa unajua siri zake?” “Angeshaniua” aliongea Gotwa kwa kujiamini akimtazama Mbonde “Mjomba hii yapa tarakirishi yake” Gotwa akaifungua tarakirishi na kuweka password kwa neno JASUSI kwa herufi kubwa Mbonde yupo tu kama mtu aotae macho wazi “Umeona mjomba…subiri hapo hapo…” kwa wepesi na hali ya uzoefu Gotwa akaanza kuperuzi mafaili kiasi cha kumfanya Mbonde kushika kiuno akimshangaa Gotwa namna alivyokuwa akiitumia tarakilishi hiyo kama mali yake “Tazama mjomba” Gotwa alimsogezea Mbonde Tarakilishi “Mhhhhh we mtoto unajua ni kiasi gani ni hatari lakini” Mbonde aliongea huku akitazama na kuendelea kutazama mambo mazito ayaonayo

“Najua ndio maaana nikakuonesha wewe mjomba nimekuona muda mrefu ni mtu mzuri na hilo halikwepeki na pia niliona hakuna mtu wa kukuthibitishia kuwa baba ni mtu mzuri nikaamua kuwa mimi wewe pia unampeleleza baba nje ya upolisi wako si ni kweli? Nime kuona na kukusikia ukitoa tarifa za uongo kuhusu baba” Mbonde alishtuka macho yasifiche hisia zake akayasogeza pembeni mwili ukimkataa kuzificha hisia zake aibu hii yapa Gotwa akimkazia macho tu. ‘Huyu mtoto atakuja kuniumbua huyu’ alijisemea nafsini “…tuachane nayo sio muhimu sana naomba tafadhari msaaidie baba tafadhari yeye sio mtu mbaya na wewe ni askari mzuri si ndio? Ni ahidi utamsaidia baba” Mbonde alichoka hoi, akasogeza kiti cha matairi na kukaa “Gotwa nani kakufundisha mambo yote haya”

Mbonde uvumilivu ulimshinda baada ya sekunde kazaa aliongea “Shuleni, kuna mwalimu alikuwa ananifundisha tarakirishi na mimi pia napenda sana kujifunza kwa ajili ya kusaidia watu kama baba” aliongea haraka haraka kwa kujiamini “Sawa sasa Gotwa..Mhh sijui nisemaje sawa wale watu walio ondoka walikuwa wanasemaje?” aliongea Mbonde huku akikusanya mikono yake kifuani akimtazama Gotwa aliyemuacha hoi “Mjomba wale walikuja kufata mzigo wao na mimi nilijua tu kuwa watakuja tena hivyo nilikuja kuukuta huku nikautegesha sehemu ambayo haitakuwa na maswali sana kule sebureni ili tu waondoke zao wasikijue hiki chumba cha siri’’ aliongea Gotwa na kumuacha Mbonde akitabasamu aone kama sinema za kizungu “ Wewe mtoto ni shida si wakawaida una akili sana umenivutia sana, unakipaji na akili yako inafanya kazi kwa haraka sana utakuja kuwa mtu mkubwa sana wewe” aliongea Mbonde huku akimshika kichwa “…Nitakusaidia na nitamlinda baba yako kuanzia sasa na sema kuanzia sasa” aliongea Mbonde na kumfanya Gotwa amtazame kwa muda ni kama hakuelewa au kushangazwa na maneno hayo naye akavunga kwa tabasamu “Asante mjomba” akasogea na kumkumbatia, nyuma akionekana kuuvimbisha mdomo wake.

Itaendeleaa...
image1648835658587.jpg
 
KISANGA!!! ( Hisia za Mrithi)
Mtunzi Akida Siri Rambao
0658328596

MSIMU 1

Sehemu 4 G

Ilipoishia...
.....da ni kama hakuelewa au kushangazwa na maneno hayo naye akavunga kwa tabasamu “Asante mjomba” akasogea na kumkumbatia, nyuma akionekana kuuvimbisha mdomo wake.

Tuendelee...
Mbonde akaanza kucheza na tarakirishi iliyopo mezani akisaidiana na Gotwa wakaanza kuona video zilizo rekodiwa kwa kamera tegeshwo “Mjomba hivi yule mwanamke ni nani mbona alikuwa akilia sana na wala hakusalimiana na mimi alipofika. Mbonde aliacha kucharaza tarakilishi akageuka macho yakakutana Gotwa akionesha kuwa na mguso uliodhirishwa machoni mwake alitazama pembeni na kusema “Kwakweli sijui chochote baba yako alinipa tu namba za simu endapo tu kama itatokea shida ya kimatibabu basi” aliongea Mbonde na kuendelea kuchunguza picha za video zilizo naswa na kamera za siri. Gotwa akatazama pembeni, hakuridhika na jibu jepesi, Anadanganywa au ?! “…alafu tena mjomba ilikuwaje ukajua kuwa baba yangu yupo kwenye matatizo na ukaja kumsaidia katika muda sahihi?” aliongea tena Gotwa akimtazama Mbonde kiasi kilicho mfanya Mbonde kumeza mate, alisikia maana moyo ulishtuka na kuongeza mapigo yake ubaridi ukamvaa kakodolea kioo chaz tarakilishi afanyaje sasa?!

Swali limemkalia pabaya akafumba macho na kuacha anachokifanya. Akatabasamu akamtazama Gotwa, “Skia Gotwa ilikuwa kama bahati tu nilikuwa nimechukua likizo ya mwaka baada ya siku mbili nilifika ofisini kwa dharura ndipo kuna askari aliyekuwa amepangwa kukamilisha misheni moja ya Mh. Maduku alipatwa na msiba wa mama yake kwa bahati mimi nilikuwa naranda randa ofisini Mkuuu aliniita nakunipa habari nzima na kunitaka nisimamie baada ya chunguzi zangu za awali ndipo nikagundua kuwa ndani yake kuna mtu mwengine aliyeingia kimakosa” aliongea Nkole akichezesha chezeha macho akijiuma uma uma Gotwa bila kupepesa macho aliendelea kumtazama usoni tu. “…ambaye ambaye ni baba yako nikapanga kuyanusuru maisha yake…japo upande mwengine ilionekana kuwa baba yako huwenda alikuwa ni mshirika wa Mh Maduku… kutokana kwa kufatiliwa mawasiliano yake ya simu,

kwa kuwa namjua japo sio sana ilinibidi ni mtonye juu ya mambo kadhaa yanayomzunguka ikiwemo watu Fulani kupanga kumuua japo sijajua ni kina nani lakini waliweza kulegeza breki za gari yake niliongea naye hivyo siku moja kabla ya safari”
Aliongea Mbonde na kukusanya mikono yake “…nafikiria namna yakutoka hapa salama bila kuvuruga hali ya hewa na ni baki kuwa polisi ili niyajue mengi…nahitajika kupata ushahidi utakao nisaidia na kumlinda baba yako…sijui nifanyaje” aliongea Mbonde na kuendelea kuwaza.

Safari hii hisia zake zilisadifu sana muonekano wake “…Nawaza kama kuna mtu ananifatilia alafu anaushahidi wa picha nitakuwa na kipi cha kujibu” aliongea akimtazama Gotwa kana kwamba anongea na mtu mzima mwenzake. “Mjomba chukua baadhi ya video ziweke kwenye simu zitakulinda kwa mkuu wako wa kazi kama atakushuku” aliongea Gotwa. Mbonde bongo likafunguka akatabasamu huku akitingisha kichwa kukubali wazo la Gotwa . Baada ya dakika ya robo saa. “Ngoja nikusaidie kunakitu muhimu cha kufanya kwenye video hizi sitakuwa na muda wa kuzipamba kuna mengine hayapaswi kuwepo lazima tutengeneze kitu kipya hapa cha kuonesha kuwa Baba yako atatekwa” aliongea Mbonde huku Gotwa akifatilia kila kitu “Shule zinafunguliwa lini Gotwa?” “Mhh mbona bado” “Sawa sasa wewe itakubidi nikupeleke mahali ukakae kwa muda mpaka nitakapo kufata kukupeleka shule” “Sawa huko nitakutana na baba?” alihoji Gotwa “Nafikiria iwe hivyo ngoja tutajua kwanza tutokea hapa nifanye kitu Fulani” aliongea Mbonde na kumshika mkono Gotwa na kutoka nae.

Mbonde alitafuta jina la mtu katika wasapu yake na kuzituma video zote, na kuandika ujumbe chini yake “Ushahidi huo, fanya mpango wa kunitoa kwenye shida nasubiria”. “Sasa wewe Gotwa nifate nikupeleke mahali” aliongea Mbonde akiongoza njia. “Vipi umeona kitu” Mti Mkavu aliongea akimtazama Gotwa “Ndio nimeona yaani Mhh! hapa ni kumlinda zaidi Gotwa kwa Nkole kumesha chuja habari zake kwisha asubiri rehma za mola wake mambo ni binua binua tu akili ya Mbonde ipo kaskazini na magharibi, haijatulia” alisema Burushuti simanzi ikiwa usoni “Ndugu yangu tuta yakosa maji na moto kwa subra, tuanze kazi” alisema tena Burushuti akimtazama Mti Mkavu.

MTAA WA MAOKA- KANDO YA MJI -NYATUMBU
Mvizio wake huo aliendelea kuufanya akizani haonwi! akinyata kwa minyato ya paka shume mwituni. Baridi likimkusudia na kumtandika kweli kweli akipasha mikono kwa kusugua na kuacha na kurudia tena. Mwishowe akawa dirishani mbele ya balaza matumbo ya viganja vya mikono yake akaviegesha kwenye nyavu ya dirisha karibu na paji la uso akichungulia yaliyomo yamo?! Hamadi bila taarifa, alishtushwa na Gongo la mgongo kidogo limvunje mbavu change “Uwiii mama weeee!” alipiga ukelele haja kaa vizuri lingine likikusudia usawa wa kiuno akahepa huku akishika sehemu ya jeraha akiugulia maumivu. Sasa alimuona aliyemjeruhi akabaki kumtazama tu kwa uchungu. “Nitakuuwa nilikwambia sitaki kuona pua yako hapa” mwanamke mtu mzima alipayuka macho kayatoa akimnyooshea Gongo Mbonde aliye mbali mita kadhaa akiugua. “… mtoto mshenzi wewe ningesema nibane pumzi zangu ungekuwa mtu wewe? Ondoka haraka nisije kukutapika hapa” aliongea pasina nukta akimwacha amsemeshae kando huko kajiinamia, mtuhumiwa!

Mwanamke wa makamo alifika tokea ndani mbio mbio “Kaka Mbonde” aliita, kisha “Mama…!” akamshika vizuri mama yao huyo huku akimrudisha kwa nyuma akimuacha mama huyo akilia kwa sauti uchungu wa ndani kwa ndani akikipiga kifua chake gongo lenye fagio la mti akiliachilia mbali likiangukia sakafuni na kuongeza nguvu ya kupiga kifua chake kwa mikono yake yote kutaka kutoa kitu kinacho mkwaruza au kumkereketa ndani kwa ndani. “Namtaka mjukuu wanguuu…namtaka mjukuuu wangu” alilalama sasa akirusha miguu yake akimzidi nguvu amshikae.

Hali ya huzuni isiolelezeka ilidhihirika, mbonde alishindwa jizuia machozi haya kasimama tu akisindikiza vilio vya mama vilivyomuumiza moyo wake asijue afanye nini. Alishtuka baada ya kushikwa mkono “Kaka tuongee kwanza” aliongea dada huyo akimvutia upande wa baraza. “Ni makosa yangu kaka nisamee” aliongea dada mtu machozi yakimlenga lenga akitazama miyale ya jua changa lichomozalo “Najua, pole ni mapito tu” alijibu Mbonde huku akifinya finya macho yake kiume.

Dada yake alishtuka na kumtazama kwa kushangazwa na jibu lake macho yake yakidhihirisha maswali ya wazi wazi hisiani. “Mara zote nakuja nyumbani kwetu kama mwizi nikivizia na kuweka kichwa cha mama yangu mapajani akiwa usingizini, nikivuta vuta nywele zake au kumtazama kwa mbali tu” Mbonde alishindwa na uchungu uliomjaa akajikuta akijifuta machozi zaidi. “Sijui kilichofichika lakini lawama za mama zanirudi kwangu nampatia wapi mimi binti yule” alisema tena Mbonde kwa machungu “Samahani kwa yote kaka, nisamee mimi sikuweka uangalizi mzuri kwake” alisema dada ake na kuendelea. “ Nimekuomba tuonane kwa sababu hali yake inazidi kuwa mbaya licha ya kilio cha Mjukuu wake kilicho na sura kubwa ya maisha yake lakini uvimbe wake uumechukua sura mpya na pesa hizi za madafu…ahh! Umasikini mbaya!?” nae akaangua kilio cha kwikwi Mbonde alimtazama kisha akamkusanya ubavuni dada yake huyo huku akimpiga piga kwa mapenzi. “Usijali hivi leo nitapata pesa na zitakuja umpeleke hospitali” aliongea Mbonde akitoa tabasamu fififiii! “Nimakosa yangu kaka sikumpa mapenzi yule binti akapotea toka mikononi mwangu, mimi ndiye niliyemwambia mama kuwa umemchukua mjukuu wake kipenzi” alisema dada wa Mbonde akidhihirisha akitoka kwenye kumbatio akishuka taratibu na kuyakita magoti ardhini mikono akificha uso wake kwa aibu. Ilikuwa ajabu kweli kweli machoni na masikioni mwa Mbonde akionekana si mwenye kuyajua wala kudhani kujua uso ulijawa na babaisho kama si bumbuwazi.

Akabaki kumtumbulia macho tu “Kitu gani dada Jojo… ulifanya nini dada Jojo!” alisimama akimtazama kwa mshangao majibu akiwa nayo mana kasha ya sikia, anahakiki!? “Namna gani! napitia mapito ya kuchuja kwa mahaba ya mama yangu mzazi aliye hai sasa ni miaka kumi na ushee vipi sasa maisha aya ishiyo binti yangu!?… si watakuwa wameshamzalisha jamani” aliongea sikitiko limemtawala mwili umenyong’onya nguvu hakuna akajikalisha kama mzigo balazani “… kukosa kwako mtoto kulikupasa umpende zaidi yule binti kwa mapenzi ya juu maana ni mtoto wa kaka ako inatosha wewe kuwa baba yake, mjomba ni mama shangazi ni baba! Makubwa ya ulimwengu haya damu yangu wewe… si wa ziwa moja?! Wewe si ulinilea mimi” aligeuza uso kumtazama dadaye mbele yake akilia kimya kimya “Ndomana nikashangaa wewe wa kukataa kuolewa na kubaki umtazame tu mama miaka yote hii kumbe ulikuwa ukijaribu kupunguza zambi zako ulizozitenda huku ukizidisha ukarimu kumbe una sababu zako zinazo kuchimba” aliongea Mbonde kwa hasira akimkazia macho dada yake.
Kikapita kimya kila mmoja akitazama upande wake, wamewekeana mgongo. “Haya sawa tuone bahati iliyobakia kama ni yetu” alisema Mbonde na kunyanyuka zake akiondoka akimuacha dada Jojo kashika tama kama yupo msibani.

Itaendeleaa....

image1648835658587.jpg
 
KISANGA (Hisia za Mrithi)
Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com

Ilipoishia....
kapita kimya kila mmoja akitazama upande wake, wamewekeana mgongo. “Haya sawa tuone bahati iliyobakia kama ni yetu” alisema Mbonde na kunyanyuka zake akiondoka akimuacha dada Jojo kashika tama kama yupo msibani.

Sehemu ya 5 A:

Tuendelee....
HOSPITALI YA BOJOBOJO, JIJINI NYATUMBU
Watu kwengi walikuwa nje ya wodi maalumu aliyo lazwa Nkole wengi wao walikuwa ni waandishi wa habari wakiwa kwenye vikundi wakipiga domo nyuso ni kama za kuomboleza. Wakijitahidi kumuhoji kila kiongozi waliomtambua akifika au kutoka eneo hilo lakini walitoka kapa “Yaaani huu ni ubaya uliokithiri eeeh! watu kumvamia mwandishi mkubwa kama Nkole na kumpiga na gongo zito kama lile sio jambo la kupendeza, vibaya ni kusema kweli na kuwavumbua watu wabaya hilo ndio kosa?! hapana hatutaondoka mpaka kieleweke na katoroshwaje hospitalini kizembe hivi” mwanamama mmoja alibwatuka akihimiza hisia za wenzake walioonekana kushika vinasa sauti na kamera “Ndio nchi nzima sasa ishajua kuwa walikuwa wakimtafuta ubaya tu Mh Maduku walipo ona Nkole atawafichua wakamfanya vibaya…Maduku hana hatia serikali inampakazia Nkole amethibitisha kwenye ukurasa wake jana japo aliwazia iwafikie wananchi leo lakini watu tuliupata ujumbe wake alio uchapisha dakika kumi tu kabla ya kuvamiwa mnaona?”

“Ndio huo ni ukweli ukweli kabisa” mwengine alidakia na mwengine tena akadakia akipaiza sauti na si tena kwa sauti ya kawaida “Lazima mtueleze inakuwaje mtu shujaa kama Nkole kushindwa kupatiwa watu wa kumlinda katika harakati zake wakati ni mpigania haki” kisha akaendelea huku macho kayatoa kwelikweli “Tunataka kuona kwenye wodi kuna nini wasitufanye watoto tudhihirishe kama kweli hayupo” mwengine akapokea sasa wakisogea kule kwenye mlango wa wodi wengine hamaso likawaingia wakaungana na kundi hilo kutengeneza idadi kubwa ya watu mchanganyiko .

Pukurushani ikashika nafasi vuta nikuvute “Tupisheee tupite…tuachieni tukaone…Rudini tutawapiga virungu ondokeni” mapolisi walizuia watu hao kuingia wakivutana. Kama ilivyo kidole kimoja hakivunji chawa tahamaki wapo wodini kwa umoja, chezea Raia wewe! hao hima hima huku kamera zikiwa hewani kurusha habari laivu, loo! Nguvu ziliwaishia walibaki wameduwa hawaamini mboni zao pakawa ziii! kimya kizito kila mmoja akitazama. Chumba kilivyo kuwa.

Chumba kimejaa madamu kitanda ndio usiseme. Polisi nao wakabaki wakishangaa “...hizi si ni damu??!!” mwanahabari mmoja alihoji kwa kuoneshea kidole. “Nkole amekufa au…” mwengine alidakia. “Kumbe serikali ilitaka kufanya siri kuhusu kufa kwa Nkole mkatutangazia kuwa eti alitekwaa kumbe amevamiwa tena hapa hospital na kuuwawa kinyama hivi” mwana mama mmoja aliongea kwa uchungu sasa akilia na mara akamvamia polisi mmoja ambaye naye aliungana kushangaa asiyoyajua, kikamshukia kipondo cha helaiki ya wanahabari hao. Vurumai ikashika hatamu yake vita ya wanahabari walioungana na raia dhidi ya polisi wachache walio kuwa wakiweka ulinzi eneo hilo, walikuwa wakilinda chumba pasina mtu, imekuwaje?! Ikawa piga ni kupige vuta nikuvute.

Polisi wa kutuliza ghasia wakamwagwa kama mchele wakitembeza mkong’oto wa haja na majeruhi kupatikana nao wakipigwa na mawe.
“Kumuhusu Mwandishi Nkole a.k.a mshona maneno. Kila mmoja alisema lake lakini la wengi likabaki kuwa Marehemu Nkole alikuwa mwanaharakati wa siri mwandishi hodari na msema kweli kila mwanahabari mwenye ndoto alitamani kuwa kama Nkole kwanini wasema kweli hufa mapema jamani?” aliongea moja ya waandishi wa habari aliyekuwa akihojiwa katika chaneli Fulani na kushindwa kuvumilia na kuangua kilio cha msiba. Mwanahabari aliyekuwa akimuhoji mwandishi akarudisha kipaza sauti kwake naz kuanza kuongea “Kama mjuavyo na nyinyi ni mashahidi kwenye hili kuvamiwa kwenye nyumba yake na kuokolewa na polisi na hatimaye kuvamiwa tena katika chumba cha ICU alipokuwa akipata matibabu, kama mlivyoona kipande cha video kikionesha chumba alichokuwemo akipata matibabu kutapakaa damu na kuleta hisia za kuwa huenda alivamiwa na kujeruhuliwa tena maana watu hao walitaka roho yake,

lakini pia mapaka sasa hakuna anae jua mwili wa Nkole upo wapi muda huu kila mtu anasubiria. Pia Afande aliyekuwa ameokoa maisha yake kwa mara ya kwanza yupo mikoni mwa polisi kiuchunguzi zaidi nani anajua hakuna ane jua nini kitajiri baada ya hapo tafadhari tukutane tena kipindi kijacho cha habari maridhawa, ni mimi mtangazaji wako Namala Manuvi wa SYT” sauti hiyo ilisikika toka kwenye luninga za kumbi za starehe, majumbani, mahospitalini, na kwenye mikusanyiko ya watu na kuzua mizozo namna kwa namna.

MADONA BWALO-WILAYA YA CHOZI
Macho yalikuwa yamekaza katika kichwa cha habari kilichoonekana kushika chati kwa namna kilivyokolezwa kwa wino mweusi na kuenea karibia ukurasa wote wa mbele huku picha ya Nkole ikiwa chini yake. Alibadili mkao huku akitoa muhemo wa kuchoka, akauvuta mdomo wake kwa mbele, yu mawazoni! Haikutosha, akanyanyuka huku akilipiga piga gazeti hilo mezani. Akageuka na kuitazama picha kubwa. “Sizani kama atakuja wa mfano wako wewe tumekiuka maneno yako na usia ulio tuachia siku nyingi, imebaki simulizi zako na mikanda ya sauti yako ikituzodoa, itabidi nibadilike sasa nirudi nilipotoka” alionekana kujisikia vibaya kiasi cha kutoa kitambaa na kukausha machozi nyemelezi yaliyo tayari machoni naz kuweka ganja la mkono karinu kapbisa na pigo la moyo. Kisha akavuta simu ya mezani akabonyeza namba na kupiga.

“Fanyeni kuja haraka sana ofisini kwangu” akarudisha pahala pake, hata hakukaa kitini teyari mlango ulikuwa wazi wanaume sita mbele yake, Kwa mstari msawazo wakasimama, macho wakiyachimbia sakafuni. “Mnajua mlicho mfanyia Nkole sina maongezi bali ukweli tupu” Maduku aliongea na kuwaacha wakitazama kwa zamu. Maduku akavuta droo mbele ya meza yake ya ofisi na kutoa mguu wa kuku bunduki ndogo ya risasi tano. Akaweka sawa tayari kufyatua akimuelekezea mmoja kati yao. “Mkuu haikuwa sisi” Mmoja aliongea akiwa kainamisha macho kwa hofu akiyapeleka huku na kule chini chini akijihami! Mara sauti ya maumivu ilisikika kati yao na mmoja wao akaanguka kama mzigo akigugumia,

haamini kilichomkuta mikono ikijaribu kuzuia damu kifuani katika sehemu ya mapigo ya moyo macho yamemtoka huku akimtazama mmoja ya wao aliyekuwa akikwepesha macho yake lakini umauti ulikuwa mbele yake akijitahidi kushindana nao na hali akihaha kusema kitu sauti ikimsaliti hakuipata bahati hiyo roho ikaacha mwili pale pale.

Itaendeleaa....
image1648835658587.jpg
 
KISANGA!!! ( Hisia za Mrithi)
Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact 0658328596

MSIMU 1

Ilipoishia...
ya mapigo ya moyo macho yamemtoka huku akimtazama mmoja ya wao aliyekuwa akikwepesha macho yake lakini umauti ulikuwa mbele yake akijitahidi kushindana nao na hali akihaha kusema kitu sauti ikimsaliti hakuipata bahati hiyo roho ikaacha mwili pale pale.

Tuendelee...

Sehemu 5B
..."Poo na Jeba hebu nipisheni muende kule kwenye chumba cha Mateso. Vijana wawili walio tuna tuna walitoka katikachumba hicho na kumuacha Maduku na wanaume wanatu “Mwengine anayetaka kusema kitu cha uwongo nina mikono kila mahali mlizani sitajua uchafu wenu? video ni nazo za upuuzi wenu mlioufanya!” aliongea Maduku akiwatazama vijana wake.

Wote walionekana kuwa na mashaka makubwa wawili wao wakionekana kukonyezana ni hali wakipanga mipango yao ya chini kwa chini.
Maduku akaanza kutembea kwa maringo akipita nyuma yao, mara wanaume wale wawili waligeuka na kumvaa Maduku lakini waliambulia koti la suti kabla hawaja fikiria jambo la kufanya teyari walijikuta wakipiga kelele za maumivu mikono ikiwa imegeuzwa upande Maduku akiwa juu yao, wamelazwa sakafuni! majuto yakiwa usoni wakitamani msamaha ile kufumba na kufumbua wakawa kimya wakiteteleka sakafuni kama kuku teyari walishalambwa shaba za sogo zao na kubakisha madamu tu yakimwagika.

Aliyebaki alijikuta akilowa jasho kwa hofu macho kayatoa, zamu yake imefika! Hajui afanye nini alijikuta akiangua kilio vha mtu mzima cha sauti kweli yame mkuta! “Hii ndio dawa ya wasaliti Paso una mke na watoto wawili, mabinti unao wapenda sana” Paso akapigiza magoti sakafuni akiendeleza kulia “Mkuu samahani haikuwa mpango nilishinikizwa tafadhari niamini siwezi kukudanganya” aliongea Paso kwa unyenyekevu wa hali ya juu sana. Maduku akamtazama kwa dharau akiyapima maneno yake, aamue nini akaisogeza bunduki na kuinusa huku akikaa juu ya meza

“Paso ulijua kila kitu lakini hukusema kitu wazi inaonekana mmefanya mambo mengi nyuma yangu basi jaribu kunitajia nani anaye walipa” aliongea Maduku akisogea karibu yake na kumshika begani “Naelewa sasa kuwa unaelewa mengi tu hebu jaribu kuniambia…ohh! Usilie kama zuzu hebu nitazame” alisema Maduku akimtazama usoni Paso makamasi yakimchuruzika “…Ohh unahitaji muda kidogo sawa nitakupa muda lakini tambua usifanye kosa lolote ita watu na waje kusafisha uchafu huu” aliongea Maduku na Paso akanyanyuaka asiamini bahati hiyo akimuangalia mara mbili mbili

“…usije fanya ujanja” alisema tena Maduku Paso akachapuka kutoka haraka haraka. Akachukua simu yake ya kiganjani na kupiga “Hebu mpeni adhabu ya kutosha aseme kitu nitakuja hapo sasa hivi” akakata simu.

'Naona Nkole umenisaidia vya kutosha, naona juhudi zako zilivyo na matumaini lakini sasa upo wapi muda huu!? Hivi ni kweli umekufa kirahisi hivi' aliongea nafsin Maduku akijisonya kila wakati huku akiipiga piga mikono yake mezani na kuendelea ‘Nimeshakuamini Nkole uko wapi sasa umeshanitoa nilipokuwa sasa uko wapi?’ “Lazima Mbonde anajua… lazima nimtafute” safari hi alisema kwa sauti Huzuni ya wazi ilikuwa machoni mwake akifinya finya macho yake

‘Hakika wewe unastahiki sifa na ulinzi wewe ni Jasusi Nkole nimeamini hilo, lakini mpango wetu umefeli kwa kiwango kikubwa nimeshindwa kukusaidia kwa wakati’ akachukua simu yake na kutafuta jina Mbonde! Palisomeka akapiga na kuweka sikioni akisikiliza alifanya hivyo mara tatu mfululizo kimya! “Amezima simu huyu” alijisemea na kujikalisha kwenye kiti alijiwazia nafsini. Mara akanyanyuka toka katika chumba hicho akiwa na jazba.

*****
Mlango ulifunguliwa, Maduku akaingia na kuongozwa njia hadi katika moja ya chumba cha mita saba kwa saba hivi “Vipi amesemaje baada ya kumuhoji” aliongea Maduku akikaa katika kiti cha bati. “Mkuu amekuwa mgumu kuongea kitu licha ya adhabu kazaa alizopatiwa” aliongea bwana mmoja aliyetuna kwa misuri iliyokakamaa na kuonesha ugumu wake na uhodari wake katika mazoezi magumu. “Basi atasema kitu nisogezeee huo mkebe” Vijana wale wakatizamana na mmoja akasogeza Mkebe wa bati mkubwa na kufunguliwa

“Safi ni namna gani… namna gani unavyotunza kiapo kwa mabosi wako haya ngoja tuone namna gani ulivyo mtiiifu” Maduku akachukua mkasi, prais na …. Kumsogelea bwana mmoja aliyekuwa ameshikizwa na kamba mikononi na kukaa mkao wa msalaba mwili ukiwa umelowa jasho kama si maji kajiinamia tu alama za majeraha zikizunguka eneo kubwa la mwili wake. Baada ya kumtazama akatabasamu akashikiza… kwenye kucha ya dole la shahada vizuri tu akimtazama pasina uwoga akavuta kwa nguvu na kuitoa kucha bila huruma, Ukatili!

“Mamaaweeeeee!” alipiga ukelelee wa haja ponyo na msaada akidhihirisha maumivu na uchungu mwingi akitazama madamu yakivuja kidoleni “Unanifanya nikumbuke kazi niliyoiacha siku nyingi” Maduku akasogea na kumshika kichwa akimpalaza nywele “Kijana wewe ni bado mtoto mdogo na isitoshe upande uliochagua sio upande sahihi hebu jisalimishe kwangu mapema unachelewa” aliongea Maduku na kuweka prais katika jino moja la mbele la Paso “Nitasema nasema Mkuu nitasema yote” aliongea Paso na Maduku akatabasamu “Vizuri sana” Haya vijana hebu mtupishe mara moja. Aliongea Maduku, na ikawa hivyo.

KITONGOJI CHA NYAKWA-WILAYA YA CHOZI
“Yuko huko kwenye chumba chenu, kajaa tele” alisema Bibi Gotwa kwa sauti ya kukauka yenye kutetemeka mkono wenye kipande cha kanga ukiziba sehemu za uso macho mekundu kweli kweli. Hiyo ni baada ya maswali mawili matatu aliyoulizwa na wageni hao wazee akiwa kajifunga kanga gubi kubi akivuta kamasi akihema kwa tabu, Kulikoni!

“Haya twende zetu” Mmoja alisema akiongoza njia huku wakimuacha Bibi Gotwa akienda kulia wao wakienda kushoto sura zikiwa simanzini akiutupa mkongojo wenye kusaidia mwendo wake wa kudema dema akiupeleka na kuupeleka tena mbele kila afikishapo hatua Mzee mwenzake akija tu nyuma nyuma mikono nyuma ya kiuno.

Wakasogea na kusogea hadi kwenye kajumba kalicho tengwa.
“Wazee wenzangu nafikiri habari zimetapwikwa kila mahala na mnazijua” aliongea Mzee Chogo kwa mtizamo wa hatarishi, wazee wale wawili wakatizamana. “Tunazo, tuambie nini kilimkuta kabla kijana wetu wa bahati” aliongea Mzee yule mwenye Mkongojo akiweka kiwiko cha mkono juu ya kishiko akaegemeza kidevu chake macho kayabetua. “Mzee Kiko mnisamee sana, kijana wetu bwana amekuwa msiri sana siku hizi za karibuni, simuelewi kwa tukio kubwa kama hili nahisi ni kile chamaa” aliongea Mzee Chogo akalivimbisha domo lake na kuikusanya mikono yake akipeleka macho..

Itaendeleaa...
image1648835658587.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom