Simulizi: Kisanga

Simulizi: Kisanga

KISANGA!!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao

MSIMU 1

Sehemu 2 C

Tuendelee Sasa

....sio kawaida” aliongea Nkole mkono wake ukiwa umeshikwa na Mbonde “Mambo sio shwari kiongozi tupo hapa kuokoa maisha yako” “Maisha yangu?...” Nkole alishtuka jicho likamtoka akamtazama mwanawe ambaye alikuwa bize kanyanyua shingo akifatilia watu wanaoshuka kwenye basi, Nkole alionekana kuwaza kidogo akashika kiuno na kubana meno yake, kisha akamtazama Mbonde

“Gari ipo tayari kukuchukua wewe na mwanao, nitawapeleka mimi mwenyewe hatuna muda nifate” wakaongozana moja kwa moja hadi kwenye gari ndogo ya binafsi “Tafadhari naomba uingie” aliongea tena Mbonde, wakati wote huo Nkole alikuwa kwenye sintofahamu macho yake yakidhihirisha kitu Fulani kinachoendelea akilini mwake Mbonde alibaki kumuangalia kwa kuibia ibia mara kabla ya kuingiza mwili mzima garini Nkole akashtuka “Kwenye Siti number 28 kwa juu kuna begi mbili moja jeusi na lingine la njano ni ya kwangu” aliongea Nkole akimtazama Mbonde, Mbonde alionekana kuelewa haraka akaelekea kwenye basi. “Nini kinaendelea hapa” aliongea Burushuti akimtazama Mti Mkavu “Tusubiri tuone” aliongea Mti Mkavu akimkodolea macho Nkole mwenye mawazo kichwa kakiegemeza kwenye Kioo.

“Sasa tunaweza kwenda kila kitu kipo tayari” aliongea Mbonde akiingia garini akivuta mkanda wa usalama na kuufunga, akaliwasha gari. “Kwa kweli ulifanya maamuzi sahihi sana yaani naona wazi unamaadui wengi sana nyuma yako tena wenye mtandao mkubwa na hapa nahisi tutakuwa tunafatiliwa”

aliongea Mbonde akitupia macho kwenye saitimila, muda wote Nkole alibaki kumkazia macho kwa ishara Fulani, Gotwa nyuma yao nae njia panda akionekana kusumbua bongo lake masikio yamemsimama kuhofiwa kupitwa na habari akisikiliza bila kufahamu kushotoni na kuliani kwake yupo na vizuka asio waona, hakuna aliye waona wakiwa pamoja nao ila walikuwa nao safarini “Nafikiri sio pahala pake kuyaongelea hayo tupo na mtoto hapa” Nkole aliongea kwa sauti kavu, afande akageuza shingo macho yakautana na ya Gotwa asijue kuwa wapo na vizuka na sio Gotwa pekee akatingisha kichwa kuelewa jambo.

Vizuka kuliani na kushotoni mwa Gotwa wakabaki kutazamana tu.

Baaada ya lisaa kupita.
“Enhe hebu nieleze vizuri anaonekana amelala…ilikuwaje mbona inashangaza” Nkole aliongea sasa akimtazama Mbonde, Vizuka wakiwa tuli wakitazama tu zamu zamu

“Sina hakika…lakini inavyoonekana wapinzani wako wameshajua utawaangusha kama ulivyofanya mwezi uliopita na kuzua tafrani balaa zito kisha kupotea kama mzuka…wamenuia kukupoteza kabisa, yaani ni vile unajificha nyuma ya kalamu si rahisi watu kukujua kwa macho, wanaweza shtukia tu umepigwa kisu au risasi wasijue kwanini” aliongea mbonde na kumuacha Nkole katumbua macho ya umejuaje? Kabla hajauliza Mbonde akaongea tena

“..nimeunganisha matukio, kwanza gari yako kukutwa imetobolewa tank la mafuta kwa makusudi na kulegezwa breki na leo kusemekana kuna watu wasio julikana kupanga kukuteka ndani ya basi” Nkole akashtuka na macho kayatoa akibwenza bweza. Wale vizuka wakatazamana kwa mshangao “…haupo salama, tusingelazimisha safari siku ya leo ungekuwa kwenye matatizo zaidi” aliongea Mbonde akisikitika kwa kichwa huku akifungua karatasi akatoa bablish na kuibugia “Nyinyi mlijuaje mkaja mbiombio? Na kwanini nikuamini wewe” Nkole alihoji akimtazama kwa makini

“...ni mambo ya kipolisi cha msingi amini upo sehemu salama” aliongea akiwa bize na usukani akiendelea kutafuna “Sehemu salama unachekesha Mbonde” Nkole aliongea akimaanisha kwa uso wa mashaka “…Nkole ni hivi kuna abiria waliokuwa wakitiliwa shaka kwa kuwa walikuwa wakikufatilia mala zote lakini watu hao wameonekana mara kazaa kwenye maeneo unayoishi na mmoja kati yao ulipanda nae gari leo na muda huu ninao kwambia yupo kizuizini na ushahidi upo” Mbonde aliachia mkono mmoja na kutoa bahasha moja na kuzimwaga picha pembeni yake huku akiendesha kwa mkono ulio baki.

Nkole alizitazama picha zile kwa awamu na alipofika kwenye picha tatu za mwisho alionekana kushtuka na akakaza macho kama mtu aliyekumbuka kitu Fulani macho yakaingiwa wasiwasi akamtazama Mbonde aliyekuwa bize akiiendesha akauma meno akiwaza na mara akaangua kicheko cha dharau na kuongea huku akimnyooshea kidole “Mnatania mnanitengenezea skendo sio, mmetumwa?!” Mbonde akageuza shingo kumtazama Nkole kwa mshangao “Skendo…sijakuelewa unamaanisha nini, unaongea ujinga gani?!” aliongea Mbonde uso ukiwa umejaa hamaki ya tani akimaanisha kwa macho ya viulizo “Mnanitengenezea mtego ili mzijue siri zangu vizuri, aisee umekosea mimi siamini watu kirahisi hivyo,

mnajifanya mnanijaali ili mniingize kwenye mtego eti mnanilinda serikali hii au nyingine nishamjua mtu aliye kutuma, alafu wanakutumia wewe unazani nitakuamini hata kama nakujua?” aliongea Nkole kwa hasira na mara akapiga yowe “Simamisha gari Mbonde nasema simamisha gari” aliongea Nkole macho kayatoa kifua juu kakinyanyua akimtazama Mbonde. Gotwa akiwa kajilaza akapenyua macho fififi kushuhudia. “Sawa…sawa sawa nimekuelewa” Mbonde alisalimu amri akatia brek gari na kuegesha kandoni mwa barabara kwenye


Itaendeleaa...
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact 0658328596

Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 1

Sehemu 2 D

Tuendelee...

....mtu aliye kutuma, alafu wanakutumia wewe unazani nitakuamini hata kama nakujua?” aliongea Nkole kwa hasira na mara akapiga yowe “Simamisha gari Mbonde nasema simamisha gari” aliongea Nkole macho kayatoa kifua juu kakinyanyua akimtazama Mbonde. Gotwa akiwa kajilaza akapenyua macho fififi kushuhudia.

“Sawa…sawa sawa nimekuelewa” Mbonde alisalimu amri akatia brek gari na kuegesha kandoni mwa barabara kwenye eneo la msitu wa Pondemo. “Nipatie funguo za buti” aliongea tena Nkole kibabe akimshambulia kwa macho ya kutisha, Mbonde akatoa funguo na kumpatia, aligeuza shingo yake akimtazama Nkole kwa jicho chunguzi. Nkole akatoka garini kavimba moja kwa moja hadi kwenye buti ya gari, akafungua.

Alichokutana nacho kilimfanya akodoe macho kwa mshangao mabegi mawili meusi yaliyofanana yalikuwa mbele yake pamoja na begi la njano. Mdomo wake ulibaki wazi kwa sekunde kazaa. Nkole akimtazama kwa makini tu kupitia kioo cha ndani ya gari juu yake ya kichwa karibu kabisna kioo cha mbele cha gari hiyo.
“Haya mabegi vipi…hapa la kwangu ni lipi?…begi langu ni lipi Mbonde?” Badaa ya kujishauri alipaza sauti tena Mbonde akimfatilia tu kwa karibu zaidi.

Mkono wa Nkole mmoja kiunoni akiyatazama kwa kuchunguza zamu zamu huku akipepesa macho kwa taharuki ya kutoamini akitazamacho. Mara Mbonde akatoka garini kafula bastola ndogo mkononi na kumnyooshea Nkole,

Nkole mshtuko huu wapa asiamini anachokiona akaanza kurudi nyuma akiikodolea bastola mbele yake ‘Haya maigizo au?!” alihoji Nkole akimtumbulia macho Mbondealiyeonesha kutotania, Kulikoni!? “Umebeba vitu gani?” aliongea Mbonde akimaanisha kwa kumsukuma, swali lilionekana wazi kumpagawisha Nkole akabaki akichezesha mdomo asijue la kusema mwili ukimtetemeka ujanja mfukoni.

Bado macho ya mbonde yenye chunguzi hayakukauka usoni mwa Nkole “Weka chini bastola tuongeee ndugu yangu, mbona sikuelewi Mbonde” Nkole hali tete akimtazama Mbonde yupo makini akimaanisha kwa sura iliyokunjamana. “Hujajibu swali langu mikono juu na ujieleze haeraka” Mbonde alifoka tena kwa sauti “Unamaanisha nini mbona sikuelewi Mbonde rafiki yangu” alisema Nkole kwaa mashaka makuu

“Nilikuwa nakuamnini sana lakini naona unauvunja uwaminifu yani wewe unashirikiana na waarifu na heshima yote ya kutukuka!?” Mbonde akatoa pingu mfukoni “Afande Mbonde, nimekuuliza kwa wema tu maana haya mabegi mawili yanafanana sijui langu ni lipi na lipi sio la kwangu, lakini naona mwenzangu unanigeuzia kibao sikuelewi” aliongea kwa kumaanisha huku akiwa amenyanyua mikono juu macho ya huruma akimtazama Mbonde.

Mbonde akamtazama kwa muda akiyapima maneno ya Nkole kisha akaongea huku akimtazama machoni “Unaweza nitajia kila kilichomo ndani ya begi lako kwa usahihi” “Bila shaka…” Nkole alijibu kwa haraka na kendelea “…kuna nyaraka muhimu sana pamoja na nguo zangu… suruari za kitambaa mbili, jinsi moja, mashati matatu na fulana mbili” akamaliza “…haya anza kufungua moja kabla ya lingine makinika na usifanye ujanja wowote” Nkole huku akiwa na wasiwasi akionekana akishughulishwa na mawazo ayajuaye yeye mwenyewe huku akichukua moja ya begi mara alipatwa na mshtuko mkubwa macho akayatoa mwili ukianza kutetemeka.

Huenda ndicho alichotegemea au kutotegemea “Hee! Madawa!?” Nkole akajikuta akilowa tweee nguvu zikamuisha akapatwa na bumbuazi domo wazi macho kayatoa, Mbonde kwa tahadhari akasogea huku akinyanyua shingo yake kuchungulia vishangazo “Hapana hili begi sio la kwangu, huwezi kunifanyia hivi…mbonde siwezi kukudanganya niokoe kwenye hili” aliongea Nkole kwa kuhamaki sasa akiwa mpole kweli kweli.

Redio call iliyoninginizwa pembeni ya bega la Mbonde ikaanza kunguruma ikifoka akaitoa katika bega iliposhikizwa na kusogea kando kidogo huku akimuelekezea Nkole bastola. “…mi tatu kumi na moja over…ndio nipo nae hapa Over…” masikio ya Nkole hayakuhitaji kuhadithiwa yalisikia kila kitu na kumfanya Nkole anyong’onyee uso ukipoteza tumaini majuto yakionekana usoni mwake macho yakiwa mekundu tayari kwa kulia.

“Mbonde naomba unifunge pingu kama huniamini, na pia na mimi nitakuamini nikushirikishe kitu” Nkole aliongea akitilia huruma. Mbonde akamtazama


Itaendeleaa...
 
Una uandishi wa tofauti na waandishi wengi wa hiki kizazi cha sasa, kazi yako ni nzuri. Mi naona ungefanya mchakato hiki kitabu chako kipitiwe na kusomwa huko mashuleni, kwakupitia kusomwa kwa hiki kitabu wengi watapata hamasa ya kuandika simulizi kwa lugha inayofuata misingi yake
Kwa kweli nimefurahi, na Nina ndoto ya kuwa juu zaidi tena katika uandishi wa tija. Asante nitaongeza juhudi zaidi na kufikia tamaa yako siku hiyo isiyo na jina
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact: 0658328596
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 1

Sehemu 2 E

Ilipoishia

“Mbonde naomba unifunge pingu kama huniamini, na pia na mimi nitakuamini nikushirikishe kitu” Nkole aliongea akitilia huruma. Mbonde akamtazama na kuongea “Hebu fungua na hilo begi lingine” Nkole kama zoba hakufikiri mara mbili akatii “Tazama mkuu kama nilivyokueleza Afande kila kitu hapa ni cha kwangu” aliongea akitoa moja kabla ya nyingine.

Mbonde akasogea kupata ushuhuda “Uhhhh! sasa bwaana…umeupoteza uwaminifu funga buti” akazirusha pingu juu ya buti, Nkole akazivaa “Ingia garini” Nkole akafata maelekezo baada ya kufunguliwa mlango akiwa mtuhumiwa.

Mlango ukafungwa.
Hawakuamini walichokiona, Gotwa alikuwa amekaza macho akiwatazama kwa uwoga

“Nimesikia kila kitu…baba hausiki kwa lolote” aliongea bila kumeza mate akimtazama Mbonde amabaye aliyarudisha macho kwa Nkole kisha akaongea “Nini unachokijua wewe…” sasa akimtazama Gotwa, Nkole wasiwasi umemtawala huku akimeza mate kwa tabu shingo kaipindia mbele kama mtu mwenye kutubia “Namna gani tena!” kwa sauti ya chini alijisemea “Nilimuona mtu akiwa na begi kama la baba, alinioneshea kidole ninyamaze huku akinitazama kunitisha” aliongea Gotwa na yeye macho akiwa kayatoa.

Mbonde akabaki kumtazama Gotwa kwa muda kama mtu anae kagua kitu “Mhh! Sioni dalili za uongo kwa huyu mtoto…Nkole unanini…nini unachonificha kwanini usiniambie” Mbonde aliongea na mara simu yake ikatoa mlio Fulani, macho akayageuza na kuichukua surualini “Mhh! Naona kuna kitu kisicho eleweka hapa” aliongea huku akiutazama ujumbe wa maneno simuni.

“Skia Nkole uso wako unaonekana una siri nzito ni kama mtu aliye ficha moto ilahali wamuunguza ndani kwa ndani angalia utachelewa naz utakuwa umeshakusamabaratisha niambie nijue namna ya kukusaidia, lasivyo utaingiza familia yako matatizoni” aliongea Mbonde sasa akigeuza mwili kumtazama kwa uzuri. Nkole kalowa kola kwa jasho joto joto limemtawala kwa hofu wazi akijishauri moyo ukimuenda kasi, Mbonde aliona akawasha kipupwe kilichobadili hali kwa kuleta ubaridi, kwa dakika kazaa ikawa ahuheni .

Nkole akamtazama Mbonde mdomo ukicheza cheza kama mtu mwenye shinikizo la ndani likimsumbua mwisho akishinda hali inayomzuia “Mbonde naomba tutoke nje nikakusimulie vizuri” aliongea huku macho akiyasokomezea chini kwa aibu, Gotwa akaonekana kushtuka na kumeza mate akiutazama usogo wa babaye. Vizuka vikimtazama tu.

Afande mbonde akatabasamu “Sikia rafiki, sioni haja ya kuongelea nje, humu ni salama hakuna mpelelezi hapa” aliongea “…au unampango mwengine, unikimbie?” aliongea Mbonde akimkazia macho Nkole, Nkole kwa mashaka akamtazama Afande Mbonde na kumpa Ishara Fulani ya macho kiasi cha kumfanya Afande Mbonde kuangua kicheko cha chini chini “Usinitanie hebu acha maigizo Nkole, huyu mtoto atabaki hapa na sisi hatutatoka,

hivi unajua huyu mtoto ni wa ajabu sana hujui? Hebu ona anavyo jiamini, jasiri nani hataki kuwa na kijana kama huyu ehh? Nambie… kama ninge kupiga risasi ya kichwa naamini huyu mtoto angefanya kitu kikubwa sana juu yangu kwa ajili ya haki yako hebu ona namna alivyotayari kukutetea alafu unataka asijue siri yako? Mwache aijue kama ni makosa yako ayajue ili ajue namna ya kukutetea na kama umeonewa ajue namna ya kuitafuta haki yako siku moja” aliongea Mbonde akimaanisha kwa kulishika bega la Nkole. Gotwa akionekana kutabasamu akivutiwa na Afande Mbonde.

Nkole shingo akaiangusha pumzi nzito akazitoa akizitazama pingu mkononi mwake. “Sawa lakini sipendi mwanangu ajihusishe na hatari ninayo pitia ndio maana nikaomba tukaongelee nje kwa kuwa mpini unao wewe mshika panga sina budi kutoboa siri.

Kumbukumbu ikamjia mawazoni.

Itaendeleaa....
 
Hapa nitatia kambi nisome vizuri, ila kwa leo nakupa kongole bw. mwandishi.
 
Hapa nitatia kambi nisome vizuri, ila kwa leo nakupa kongole bw. mwandishi.
Nitashukuru, shida yangu watu wajue yaliyo ndani yangu, watu tujifunze na tuyajue maisha ya kweli
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

MSIMU 1

Sehemu 2 F

Ilipoishia...

Nkole shingo akaiangusha pumzi nzito akazitoa akizitazama pingu mkononi mwake. “Sawa lakini sipendi mwanangu ajihusishe na hatari ninayo pitia ndio maana nikaomba tukaongelee nje kwa kuwa mpini unao wewe mshika panga sina budi kutoboa siri.

Kumbukumbu ikamjia mawazoni.

Kilitolewa kitambaa usoni mwake na akajikuta katikati ya wanaume nane walioshika mapanga na mmoja wao akiwa na bunduki kubwa ya kuulia tembo, akajaribu kuangaza macho akifikilisha bongo lake kung’amua yuko wapi macho yakisindikizwa kule na kule, miti mikubwa mingi kwa idadi iliyoshonana na kuleta kiza hafifu huku sauti za ndege mbalimbali ikisikika huku na kule huku nyumba moja tu iliyotengenezwa kwa mbao ikiawa mbele yake “Huwezi kupajua hapa hata nikikuacha mwenzi mzima kuzurura kwa masafa ya mashariki kwa magharib wala kusini na kaskazini”

alishtushwa na sauti hiyo iliyomtoa mawazoni akageuka kumtazama aliye msemesha “Karibu sana Nkole, punguza hofu, weka maswali kando sikiliza maagizo yangu” aliongea bwana huyo kwa majivuno na kuangua kicheko cha kujibana akicheka chini chini huku akimzunguka Nkole aliyesimama kama mstimu mkono wake ukiwa begani mwa Nkole akimbinya binya

“Mwenye kutaka nae hutakwa hakuna kazi ya bure bure, tazama pale ule ni mzigo wangu naomba usafiri nao mpaka Nyatumbu baaasss, wewe utakuwa umepata na mimi nitapata” aliongea tena huku akifinya finya macho yake na kutabasamu huku akimuoneshea mkono wa ishara kusogelea meza kubwa ya mbao isiyohamishika kwa kusimikwa ardhini hatua chache mbele yake juu ikiwa na sanduku dogo la mbao

“Unaweza chungulia kilichomo bwana Nkole Mshona maneno” Nkole akasogelea na kufungua huku akimeza mate huku akimtazama kwa kuibia ibia.

“Nini hiki…” alijikuta akiuliza kwa mashangao macho akiwa kayatoa akimtazama bwana yule “Hee! Mbona hamaki kubwaa hivyo Bwana Nkole, majibu mbona unayo mwenyewe” wale watu nane wakaanza kuangua kicheko kumcheka “Mh. Maduku unataka nifanye nini…haya si ni madawa ya kulevya haya ehh” Nkole aliongea akimtazama Maduku kwa hasira za wazi

“Unampango gani Mheshimiwa” “Hhahhaha Nkole unataka msaada wangu au hutaki...” aliongea Maduku sasa akimsogolea Nkole. “Hata kama, mimi ni adui wa hivi vitu nachukia, kwanini unafanya hivi” aliongea Nkole hasira na huzuni vikichanganyikana

“Sikiliza wewe mwanasiasa mdogo tambua kuwa mimi ni kama baba yako na ni mtu hatari pia utake usitake utasafiri na mzigo wangu mpaka Nyatumbu na usitake kujua naupeleka wapi we fata maelekezo tu mpeni makarakatasi yake tuone atafikia wapi!” aliongea Maduku, bwana mmoja akasogea na bahasha kuubwa ya kaki na kuiweka mezani “Vitu vinavyokusumbua hivyo hapo taarifa nyingi nzuri kuhusu nchi hii ya gizani zimo humo” aliongea Maduku na kuangua kicheko

“Hunifanyi lolote na huwezi kunikwepa, mimi sasa ni kivuli chako, mzee wako Chogo najua anapoishi nikipiga simu tu saizi utakuta maiti” aliongea kwa madoido huku akimtazama Nkole kwa dharau “Kijana we bado mdogo sana watu tulikuwa na moyo huo huo lakini ona tulipo, sasa pesa ndio kila kitu tafuta pesa achana na kupigania watu walio lala” aliongea maduku huku akimtazama Nkole aliyekuwa kajiinamia tu

“Acha kufata upepo utakuja kufa masikini kama baba yako muondoeni hapa haraka ananitia kichefu chefu” aliongea Maduku.

Na Nkole akavishwa tena kitambaa kuficha macho.
“Hicho ndicho ninachokikumbuka bwana Mbonde, sipajui pale ni wapi nilikuja shtukia tu nikiwa mlangoni nyumbani tena mlangoni nilijishangaa nilitazama kila kona lakini siku muona mtu wa kumshuku usiku ule na hata nilipojikagua kama nina jeraha lolote siku liona kwa kifupi nilikuwa timamu na salama mkononi nikiwa na ile bahasha kubwa, lakini…” Nkole akaibana midomo yake

“Nilipopata wazo la kujisachi nilitoa kikaratasi kilichoandikwa ujumbe ukinitaka nisafiri leo hii asubuhi na wala siku panga iwe hivyo na baadae ujumbe wako wa simu” aliongea Nkole “Duhh! Pole sana, sasa inaonekana Mh. Maduku ni mtu mwenye akili nyingi sana…skia ilinibidi nije na mabegi yote kwa sababu yanafanana dhumuni langu lilikuwa ni kurejesha moja kituoni kwaz madai ya kuchukuliwa na abiria kwa bahati mbaya, ilinibdi nifanye hivyo kwa kuwa nilipata hbari za begi jeusi la madawa ya kulevya hivyo kweli ungeingia hatiani leo” afande Mbonde akakusanya viganja vyake na kufunika paji lake la uso kwa muda. Nkole akabaki kumtazama Mbonde, haelewi!

Itaendeleaa...

 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact: 0658328596
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 1

Sehemu 2 G

Ilipoishia...

...Nilipopata wazo la kujisachi nilitoa kikaratasi kilichoandikwa ujumbe ukinitaka nisafiri leo hii asubuhi na wala siku panga iwe hivyo na baadae ujumbe wako wa simu” aliongea Nkole “Duhh! Pole sana, sasa inaonekana Mh. Maduku ni mtu mwenye akili nyingi sana…skia ilinibidi nije na mabegi yote kwa sababu yanafanana dhumuni langu lilikuwa ni kurejesha moja kituoni kwaz madai ya kuchukuliwa na abiria kwa bahati mbaya,

ilinibdi nifanye hivyo kwa kuwa nilipata hbari za begi jeusi la madawa ya kulevya hivyo kweli ungeingia hatiani leo” afande Mbonde akakusanya viganja vyake na kufunika paji lake la uso kwa muda.

Nkole akabaki kumtazama Mbonde haelewi!

Tuendelee....

....Mbonde akaendelea “…kazi ipo, mimi pia nilipokea ujumbe wa maneno ukisema…” Mbonde akaichukua simu yake “…Muokoe Nkole kuna mtu amepanga kumuua yupo na siri nzito ya taifa” akamtazama Nkole baada ya kusoma ujumbe huo,

“Umeona Nkole!? na muda huo mimi na timu yangu tulikuwa tukikufatilia muda mrefu tukihakikisha usalama wako hata kusikia kuwa ulikutana na Mh. Maduku pahali japo haikuwa na uwakika tunazo, sasa ukichanganya tukio la gari yako kutobolewa tenk na kulegezwa brekii ukiunganisha huwezi acha kuiamini hii meseji…shenzi Mh. Maduku ametuweza kweli kweli” aliongea Afande Mbonde “Hebu nikufungue pingu” aliongea akimtazama Nkole mkononi Funguo “Asante sana Mbonde…sasa nifanyaje? mimi sielewi cha kufanya nimeshaingia kwenye mtego mzito sana” aliongea Nkole akijishika kichwa kwa masikitiko Gotwa akiwatazama tu kwa nyuma.

Vizuka nao hawavumi lakini wamo wakatazamana tena. Yule bwana mfupi alikuwa na gazabu kubwa zaidi uso wake ukiwa na maswali akimtazama mti Mkavu kwa jicho la Hebu niambie! Hakuna aliccho pata “Aisee mbona sasa wote wanadanganya, wanasema uongo kiasi hiki?!” alisema Burushuti akimtazama Mti Mkavu aliyeonekana kukosa la kusema pasina kuonekana.

“Nkole si wa kuaminika wacha ni mguse nisome kumbukumbu zake” akijiandaa kushika shingo ya Nkole hakupata bahati hiyo Mti Mkavu aliurusha mkono wake kuupangua Hoi! Tafran Gari ilikuwa kama imesukumwa hivi mara moja iliyumba kiasi cha kumshangaza Mbonde aliyeuwahi usukani uliopoteza muelekeo kwa myumbo huo na breki zikafungwa mara moja macho yakamtoka yakakutana na ya Nkole aliyekuwa tayari kajishikilia vizuri kwa kujiandaa na Ajali. “Kitu gani Mbonde?!” Nkole alisema akihema kwa hofu macho kayatoa “Sijui imekuwa ghafla tu…” Mbonde akageuza shingo kutazama nyuma ya gari lakini hapakuwa na gari wala ishara ya tofauti.

“Acha mawazo tupo barabarani ujue” alisema Nkole akimtazama Mbonde “Mh! Hapana nakataa sio mawazo kuna upepo mbaya utakuwa umetupitia tushukuru mungu bahati nzuri ipo kwetu.” Akaitoa gari na kuanza kuendesha “Mambo ya nguvu za giza hayo ulimwengu una siri nyingi sana” alijisemea Nkole akimtazama Mbonde.
Upande wa Gotwa alibaki katumbua macho akitazama kuliani na kushotoni mwake akionekana kuwa na hisia kali sana.

Macho yake yakionesha hali Fulani ya uoga kiasi cha kuwashtua Vizuka waliokuwa karibu yake nao wakabaki kumtazama na kutazamana kwa zamu. “Ingelitokea ajari na mtu kuumia nakwambia nisinge jari wewe ni nani tungechimbana hapa” aliongea Burushuti akimtazama Mti Mkavu aliyekuwa katulia tuli kama sio yeye.

“…Au na wewe unayajua nisiyoyajua upo kwa ajili ya kumlinda sio? Nakuona, nayaona mabadiliko yako ndugu hilo si jambo la busara kuchagua njia yape yako” aliongea Burushuti, Gotwa akiwa karibu yake zaidi kiasi cha kupeleka mkono wake na kujaribu kushika kisicho shikika, hakushika kitu zaidi ya hamna.
“Siulisema una muda mrefu hujaingia mtandaoni?” Mbonde aliuvunja Ukimya “Ndio, ndio nina muda hata simu huwa naiwasha kwa machale tu” aliongea Nkole akipepesa macho yake kwa haya.

Mbonde akamtazama kwa muda “Duhh! Basi vizuri acha iwe hivyo kipindi nafikiri cha kukushauri..Hebu wacha tuondoke eneo hili kwanza tutajua cha kufanya mbele kwa mbele” Afande Mbonde akatia ufungu gari na kuingiza tena barabarani. Kilipita kimya kila mtu akiwa na la kwake kichwani Gotwa akiwatazama tu na yeye akionekana kuwa na ya kwake. “Unajua nini Nkole muda ule nimekushikia bastola nilipokea taarifa mbili moja kumhuhusu Maduku, alivamiwa nyumbani kwake na hakukukutwa na chochote cha kumtilia shaka.

Na wakati huo huo walifanikiwa kufika katika sehemu iliyosemekana ndio kiwandani katikati ya shamba lake la nyuki na miti lakini hawakukuta kitu cha kutilia mashaka zaidi ya kuwakuta wafanyakazi wake wakiendelea na majukumu yao ya kila siku” aliongea Mbonde huku akitingisha kichwa Mbonde akatabasamu, akamuangalia Mbonde kwa jicho mshangazo akionekana kujishauri kuamini au kuto kuamini, akasema

“Mimi pia alinitumia ujumbe wa kutaka kumsafisha kuhusiana na Kashfa inayomkabili kwa hiyo hata mimi naona yeye ndiye aliyeusuka mpango huu sasa yeye ni nani zaidi ya tunavyojua?..kweli nimejiingiza kwenye mtego” aliongea Nkole akijisikitikia Afande Mbonde akimtazama “Mhh Mti Mkavu Nkole mbona anazidisha chumvi, hapa hakuna wa kumuamini hata mmoja” aliongea Burushuti akimkazia macho Mti Mkavu aliye tuli kama hajasikia vile. “Aisee pole sana upo katika wakati mgumu, Maduku ametuchezea mchezo sisi sote nakwambia lakini tutamjua tu” Mbonde aliongea baada ya kumtazama. Nkole akabetua macho yake huku akiwa kainamisha kichwa na kutabasamu kwa dharau pasina kuonekana akimtazama Mbonde kwa jicho la chini chini. Burushuti aliona akauma meno akimtazama Mti Mkavu aliye jikausha.

Itaendeleaa...
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact : 0658328596
Email akidasiri@gmail.com


Ilipoishia...

...aliongea Burushuti akimkazia macho Mti Mkavu aliye tuli kama hajasikia vile. “Aisee pole sana upo katika wakati mgumu, Maduku ametuchezea mchezo sisi sote nakwambia lakini tutamjua tu” Mbonde aliongea baada ya kumtazama.

Nkole akabetua macho yake huku akiwa kainamisha kichwa na kutabasamu kwa dharau pasina kuonekana akimtazama Mbonde kwa jicho la chini chini. Burushuti aliona akauma meno akimtazama Mti Mkavu aliye jikausha.

Tuendelee....

Sehemu 3A

JIJINI NYATUMBU

Hakuna refu bila ncha, Dhuhur ikawakutia Jijini Nyatumbu, Muwadhini akinadi swalaa wao wakikata mitaa macho yamekodolea nje ya gari kutazama Mji huo uliosheheni majengo marefu ya kisasa, barabara za hadhi.

Kadamnasi kubwa ya watu wakienda na kurudi magari mengi ya kila sampuli yakipishana, piki piki, wengine wakienda na kurudi kwa miguu maduka makubwa makubwa yakisheheni vitu vingi vya kisasa pamoja na vyombo vya usafiri, mavazi, mapambo ya nyumba kadha wa kadha, Watanashati kwa warembo mavazi yenye thamani milini kwa mitindo mbali mbali si wazee si vijana si watoto.

Mafukara ombaomba machokoraa nao kandoni mwa bararabara wakihaha na jua kali pekua miguuni wengine ndala za mashimo kisiginoni nguo zilizokosa rangi maalumu nywele timu timu.

Wala haikuwa simulizi wote waliyaona vizuri kupitia vioo vya gari hiyo ni baada ya gari kusimama kwenye mataa ya nenda kwa usalama.

“Ebwana ni kama jana vile lakini sivyo mji umekuwa sasa na maendeleo ya kadri” alisema Burushuti kwa sauti ndogo akimtazama Mti Mkavu aliyekimya muda wote, akamtazama lakini aliambulia ukimya tu akauchuna zake.


“Ukitazama mazingira na watu wake kama hakuna kufa vile, Watu hatuwezi kuwa sawa hata siku moja…Dunia haina usawa” aliongea Nkole akavuta hewa na kuzitoa kwa mdomo kama azimae moto huku akimtazama mama mmoja aliye kuwa akihimiza akigonga kioo cha gari mkononi ameshika bakuli la bati bila shaka akihitaji kitu chenye thamani toka kwao, ni omba omba! Nkole akashusha kioo pesa ya noti akaiwekea bakulini. Loo! Furaha ya wazi ilionekana usoni mwake “Asante sana baba…mungu akubariki baba akubari dua zako baba, utimize ndoto zako baba” aliongea mama yule na kuwacha madimpozi yake na mapengo takriban matatu au manne yakionekana Mhh! Sijui alikumbwa na nini!? wala haikufanya kuutoa uzuri wake wa asili usoni mwake.

Nkole Akafunga kioo na kulazimisha tabasamu. “Hapo utakuta alizalishwa akatelekezwa, au baba wa mtoto hamjui kabisa au pia inawezekana yupo ila ni wale wanaoabudu pombe tu” aliongea Mbonde. “Ndio maana nilisema watu hatuwezi kuwa sawa, wewe ukiwaza hili na mimi naliwaza lile” aliongea Nkole. “….ni mwanamke mzuri kwa hakika …masikini amekosa mtu wakumjali” Nkole alisema.

Wote waliyasikia maneno ya Nkole yaliyoonekana kutoka katika uvungu wa moyo kabisa yenye hisia kiasi cha kumfanya yeye mwenyewe kulengwa lengwa na machozi. Vizuka wakatazamana na kustaajabu ya Nkole.
Huzuni iliendelea kubaki kwa Nkole huku kajiegemeza ubavuni mwa mlango akimtazama mwanamke yule mwenye mtoto akienda zake kwa furaha.

Tabasamu lake likamjia usoni mwa Nkole tabasamu la kweli! Tabasamu hilo likampa safari ya bure mpaka miaka ya nyuma akimuona mwanamke aliyempenda kwa mapenzi mazito sana mwanamke aliyempa kila alicho nacho kwa kadri na kadri. Mapenzi ya juu, juu zaidi kama sehemu ya kuonesha namna alivyo thamini na kumthamini mwanamke huyo mmoja tu wa malengo yake wa maisha yake wa moyo wake.

Mawazoni alimuona mwanamke huyo akicheka kwa kicheko chake cha pamoja kicheko, Kicheko cha jumla jumla kilichomg’arisha macho na kumpendezesha sana machoni mwake hasa yale meno yake meupe pee macho yake ya wastani yaliyoregea wala si kwa kungu za mashariki ya mbali bali asili yake.

Wenyewe wakienda mikono imeshikana mapenzi ya kumbi kumbi! wakila na kulishana masorotojo, mashanta shanta kababu kalimati kama njiwa wakishirikiana. Wakishirikiana kwenye mambo kadha wa kadha kama siafu.

Penzi lilikuwa motomoto mbali na watoto, mwenyewe akimbidiisha katika masomo kwa namna na kadri alivyoweza zaidi kufikia hatua nzuri ya ufaulu wenye kuridhisha katika mchepuo wake lakini siku ile! ile siku moja! Moja tu katika maisha iliyoingiwa na

Jinamizi la sikitiko zaidi ya yule Winfrida wa kitabu cha Ukweli Uliofichika toka kwa Mtunzi Akida Siri Rambao toka nchi ya Mashariki hukooo, alichopenda kukisoma mara zote akiwa na huzuni Loo! Huzuni ile ilimrudi ilimrudi kwa namna ya tofauti hatoisahau maisha mpaka kufa kwake.

Mwanamke yule wa maisha yake alikuja mbele yake kachukia kweli kweli hashikiki hakamatiki mkali huyo mbogo kasingiziwa! akimrushia makaratasi huku macho kayatoa.

Nkole akiwa kitandani alishtuka na kupatwa na bumbuazi mdomo wazi “Kulikoni Habib!” alihoji mbele yake huku akichukua makaratasi yaliyo sambaa kitandani nakupitisha macho kujionea “Mjamzito!!?” ndio neno lililotoka kinywani mwake tabasamu likiranda randa usoni mwake.

Mambo hayakuwa baridi kwa tabasamu lake bali dharau usoni mwa Mwanamke yule alishtukia kitu kikimpiga kichwani mwake kabla haja tia neno msururu wa maneno ya kashfa machafu chafu yasiyosemeka wala kuandikika magumu masikioni mwake akishuhudia kwa macho yake mawili namna mwanamke yule alivyokusudia au kujipanga kwa shambulizi hilo la kushtukiza bila kutoa nafasi ya Utetezi akitamba jukwaani “…kumbe uliyapanga haya? ulipanga unifanyie hivi sio? Ulipanga kuniharibia malengo yangu si ndio?” aliongezea

Itaendeleaa...
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

MSIMU 1

Sehemu 3 B

Ilipoishia...

kichwani mwake kabla haja tia neno msururu wa maneno ya kashfa machafu chafu yasiyosemeka wala kuandikika magumu masikioni mwake akishuhudia kwa macho yake mawili namna mwanamke yule alivyokusudia au kujipanga kwa shambulizi hilo la kushtukiza bila kutoa nafasi ya Utetezi akitamba jukwaani

“…kumbe uliyapanga haya? ulipanga unifanyie hivi sio? Ulipanga kuniharibia malengo yangu si ndio?” aliongezea huku akimshambulia na kila alichokiona mbele yake kuthibitisha hasira zake hadi kalamu alitupiwa siku hiyo akawa kama jalala!

Tuendelee...
“…siwezi kuzaa na wewe nakwambia siwezi amini hilo hii mimba nitaitoa na ulichokitaka hakita timia shika maneno yangu mpuuzi baladhuri wee” aliongea mwanamke yule kwa sauti yake kali machozi yakimtoka kama mvua kisha huuyooo alitoka chumbani mule na kuubamiza mlango kwa nguvu Mbaaa! Nkole alibaki asijue ni maagizo au ni kweli kweli alibaki kaganda Ngaa! “Hivi leo nisiku ya wajinga au?!”

alijisemea na kujiridhisha kwa kupeleka dole la shahada ukutani juu ya kalenda ya mwaka kutazama wala haikuwa uwenda alitamani iwe haikuwa bali tarehe ishirini na nane mwezi Januari wapi na wapi na mwezi Aprili moja?! Macho aliyatoa asiamini akitazamacho akitamani miujiza na uchawi lakini wapiii!! Akayafinya finya macho yake akizani yu ndotoni lakini wapiiii! Akajitupa kitandani alale walau vijidakika kutoa wenge la mawazo akiomba muujiza lakini wapiii! Lakini alibakiwa na sauti ya mwanamke yule ikijirudia masikioni mwake tena na tena.

Siku ile ngumu isiyosahaulika maishani mwake ndio siku iliyoweka kidonda cha moyo kisichopona na sio kovu. Ndio siku aliyogundua asiyoyajua kuhusu mwanamke yule aliye mpa moyo wake wote na kuingiza mwili wake wote kwenye biashara ya penzi la milele kwa mara ya kwanza tangu baleghe yake.


Ni siku iliyofichua yaliyozikwa ni siku aliyogundua kuwa mwanamke yule si lolote si chochote mwanamke wa yeyote yule. Hii ni baaada ya kulifikirisha bongo lake kwa makini na kutathmini kwa kina maana hayakuwa maigizo alidhamiria kweli. Siku ile alipokutana nae katika joto la huba walikuwa tilalila chakari kwa pombe walizobeba toka kwenye sherehe ya kumuaga moja ya rafiki wa chuo aendae Ughaibuni kimasomo. Lilimkaa mawazoni lakini hakulipatia uzito japo lilikuwa zito kuvumilia.

Jogoo lake kupitiliza mtungini bila kizuizi halikuwa jambo la kuvumilia sio jambo la mchezo mchezo! Wee hatarii mwanaume! akili yake ikawa sawa macho! Wenge la pombe likamuisha Mvurugo si mchezo! Alikesha akimtazama asimmalize anajiuliza mweneyewe na kujibu mwenyewe Usingizi ukamchukua. Palipo pambazuko mwanamke yule hakuonekana machoni mwake. Palibaki manukato yake tu na chupa za bia zikiwa zimesambaa. Chumba kikiwa vururu. Huenda alijihami alijua kilichotokea? nani anajua! Mwezi ulikatilia mbali bila ukaribu ule wa kale uliotukuka. Akimuona akipitia mbali akikwepwa, simu zikikatiliwa mbali.

Penzi lilifubaa sababu ya kiapo “Nkole Umevunja kiapo chetu uliniingilia kinguvu, ulinibaka” aliongea hivyo bila mwanya wa kusikiliza utetezi wa Nkole kweli alimuonea akasahau chake cha usichana haikutosha hadi bwawa la maji pwapwa tapwa tapwaa!! Na ulevi waliokuwa nao usiku ule kiasi cha mtu yeyote angeweza kuteleza akaangukia uzinini. Pombe sio chai! Pombe ilimuumbua usiku ule alisahau jina la Manyasi alilokuwa akilitaja kila akipanda mlima na kuteremka mpaka kumzibua masikio Nkole asione ni mchezo akayajua asiyoyajua usiku huo. “ Huna jipya Nkole unajitetea tu!”. Kila lifanywalo gizani huishia mwangani, siku za mwizi arobaini sio ishirini wala thelathini macho kwa macho alimbamba.

Alimkuta msichana wake huyo akilibembeleza penzi lililovuja kwa kupitia simu alibembeleza kwa kulitaja jina la Manyasi mara kazaa na kuahidi kwenda kulala kwake siku hiyo. Kijana aliyekuwa Raisi wa wanafunzi chuoni pale, akimuomba msamaha wa kweli huku akilia, Nkole siku ile alinyong’onyea nyong’onyo alitepweta tepwe! Loo! Kumbe ndiye aliyekuwa waubani wake siku nyingi ndipo akakumbuka matukio kadha wa kadha. Kutotaka simu yake itumiwe na Nkole, kuwa bize usiku akiongea na simu huku akijetetea kuwa ni marafiki ndio walikuwa wakiitumia, shemeji zake nao walikwa wakijua kilichokuwa kikiendela ilimuuma sana, walimuunga mkono kuficha madhambi yake. Kumbe kipindi akijitutumua akipita kwa kujidai kujipatia mwanamke mzuri anayetikisa wavulana wengi, bila kuligusa tunda kwa ahadi ya Ndoa, watu kama Manyasi walikuwa wakijimegea bila gharama yoyote huku yeye akijihimu kujitoa kimasomaso kuhakikisha ufaulu kwa binti yule. Watu walikuwa wakimdhihaki kwa kutokujua ya nyuma ya pazia, kumbe mwanamke genda heka asiye jua tofauti ya sakafu na mkeka.

Alisononeka na kujisikia vibaya sana Mwanamke yule alipogeuka alimkuta Nkole akiwa kalowa kwa machozi ya maumivu ya ndani wala hakujigusa aliishia kukimbia eneo hilo kwa aibu aliyoipata. Nkole wa watu akapiga moyo konde, maisha yaliendelea.

Mwanamke yule mwishowe alikuja simamisha masomo baada ya ujauzito kukataa kutoka, akajifungua bila ya kutaka msaada wa Nkole na kuamua kumtelekeza mtoto wake wa kiume mlangoni mwa chumba cha Nkole pamoja na ujumbe mzito wa maneno karatasini, hii ni baada ya miezi sita tu tangu kujifungua kwake. Na yeye kuishia kwenda kuzamia penzini mwa Manyasi mwanaume aliyeonekana kuwa ndiye chaguo lake sahihi.

Itaendeleaa...

 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact: 0658328596
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 1

Sehemu 3 C

Ilipoishia

....Mwanamke yule mwishowe alikuja simamisha masomo baada ya ujauzito kukataa kutoka,

akajifungua bila ya kutaka msaada wa Nkole na kuamua kumtelekeza mtoto wake wa kiume mlangoni mwa chumba cha Nkole pamoja na ujumbe mzito wa maneno karatasini, hii ni baada ya miezi sita tu tangu kujifungua kwake. Na yeye kuishia kwenda kuzamia penzini mwa Manyasi mwanaume aliyeonekana kuwa ndiye chaguo lake sahihi.

Tuendelee...

...Masikini machozi yakaanza kumtililika kumbukumbu imeisha hakuweza jizuia akachukua leso yake mifukni mwa suruali akaiweka usawa wa macho na kujikuta akilia kimya kimya. Gotwa na Mbonde walikuwa mashahidi lakini walibaki kutazama tu wasitamani kujua zaidi.

Maana mwenye kulia ndiye mwenye kujua kimlizacho. Mizuka wakaangaliana tena, Burushuti akitamani kutia neno akajimezea mate tu.
Mataa yalibadilika kuruhusu safari, hao wakatoka kuifata njia inayowahusu. “Una kalamu…” Nkole alimsemesha Mbonde, Mbonde hakujibu alipeleka mkono akabetua sehemu na kuchomoa kalamu na kumpatia.

Namba zikacharwazwa karatasini na neno likafata. “Namba za simu…FIYONA” alitamka Mbonde baada ya kupokea toka kwa Nkole aliyejipinda kurudisha kijitabu cha kumbu kumbu mfukoni.

“FIYONA” alisema tena Mbonde akihitaji kusikia jambo toka kwa Nkole kashikilia tu kikaratasi mkono mmoja usukunanini uso kaukunja “Ndio, kama itatokea tatizo la kimatibabu tafadhari naomba mpigie huyo” Nkole alijibu.

Mbonde alitulia na kutafakari akizitazama kwa nyakati tofauti namba zile uso wa kujadili. Anazifahamu?!! Pumzi akazishusha macho mbele. “Huo mzigo vipi!?” alidokeza Mbonde baada ya kimya kupita na kushika barabara yakuelekea nje ya Jiji makini na usukani akikwepa mashimo barabarani.

Nkole akamrushia jicho lenye chuki, hakupendezwa! Aliugezia uso wake mbele, uso ulioonesha kuchoshwa na swali lenye utata, mawazoni ajibu nini?! Wacha achambue. Bongo kazini kichwa kikamzidi uzito na maumivu yakimnyemelea yupo matatani.

Mwishowe “Kaka Nina ombi moja wacha waauchukue huu mzigo wao lakini nahitaji msaada mkubwa sana wa uaminifu toka kwako sifurahii kutumika kiasi hiki, hii dhambi itanigharimu” “Sawa lakini kumbuka hata mimi utaniweka katika wakati mgumu ni vipi kama siri itatoboka, mimi nitakuwa mgeni wa nani? askari makini na ninaye aminika kama mimi niachie kapu la dhambi lipite tu Mhh! Utaniingiza kwenye matatizo yako, sitaki!” aliongea Mbonde akimaanisha kwa kuikunja sura yake akimkazia macho Nkole, Nkole akajikuta akiishiwa nguvu macho kayatumbua, haamini masikio yake.

“Mbonde nisipofanya hivi familia yangu itakuwa matatizoni, nilikuwa nafikiria namna ya kumkwepa na nilishajua nimemkwepa lakini nisikufiche shida zangu ndizo zimeniingiza kwenye mtego wake na hata hivyo hatukupata kubaliano zuri sikujipanga kwa hili” aliongea Nkole nakumfanya Mbonde amtazame kwa mshangao akaongea

“…nakuona unajieleza sasa toboka na utapike vizuri naona jambo lingine tofauti na nakala, mbona unakuwa mbinafsi sana wewe kumbuka hapa nimevunja maadili ya kazi kutoka kumuokoa Raia dhidi ya mikono ya wadharimu hadi…” alijikuta akishindwa kumalizia akapigiza mkono wake katika usukani

“Jinga ujinga kabisaz huu” alilaani vilivyo misonyo ikifatana. Nkole uso ukambadilika akionekana kuchukizwa uvumilivu ukamshinda, akajigeuza kumuangalia vizuri dereva wake huyo

“wanionaje kwani wewe?! Ehh! Ndio, shida yangu kubwa ni ulinzi unajua sasa nipo katika hali ya uwoga sana kuwachezea watu weupe sio jambo dogo”

aliongea akimtazama Mbonde aliyekuwa bize kuendesha gari yeye akiendeleza kurap akirusha rusha mikono kwa mifano ya haja

“…nilitegemea serikali ingefanya jambo kunihusu mimi kwa yale niliyoyafichua kuhusu ule mgodi wa Igombe yule bedui mshenzi alikuwa akiinyonya nchi hii kupitia madini, nikijiingiza katika hatari mbalimbali, lakini ona sasa kama sio wewe mimi ningekuwa wapi saizi ehh? unalaani eti umevunja maadili ya kazi wakati umemuokoa mtu mzalendo unajua mangapi nimeyafanya mwaandishi mimi kupitia kalamu eeeh! Nijibu sasa hivi?” aliongea kwa hasira akimuangalia Mbonde. Vizuka wakatazamana “Nini kinaendelea Mti Mkavu bwana huyu anaongea kwa hisia mpaka ananichoma moyo loo!” Burushuti alitingisha kichwa, sikitiko la moyo.

“Nimejitoa maisha yangu kwenye hatari mbalimbali kwa kificho nikiigiza maisha ya watu nikikusanya taarifa hatarishi za watu wabaya dhidi ya hii nchi maisha ya vitisho kujificha ficha mtoto wangu anaishi kivyake na mimi kivyake kwa sababu ya haki za watu wa nchi hii, alafu leo unasema eti umevunja maadili ya kazi sawa nipeleke polisi sasa hivi fanya kunipeleka polisi nasemaa” povu la mate lilimtoka Nkole akimaanisha kwa kuyatoa macho yake makubwa akimtazama Mbonde ambaye alionekana kuwa mpole. Gotwa konani akionekana kuguswa ndani kabisa kiasi cha kumfanya machozi yamlenge lenge alishuhudia ukweli uliodhihirishwa na sauti na macho ya baba yake. ‘Baba analia’ alijisemea nafsini alijikuta ni kama mtu aliyepatwa na bumbuwazi Fulani akishuhudia hali ngumu ya maisha yaliyo nyuma ya baba yake yenye hatari kubwa na usalama kiduchu.

Alijikuta akitingisha kichwa kuelewa jambo analo lijua yeye mwenyewe. Kimya kilipita midomo ikiwa imeshonwa wakitupiana macho yenye kusema ya moyoni, kuonewa! Vizuka wakibaki kutazamana tu mwishowe Burushuti ikambidi aangue kicheko kiasi cha kushika kitambi chake, Mti Mkavu akiwa mkavu kama jina lake akimtazama tu bila neno.

Itaendeleaa...
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact 0658328596
Email akidasiri@gmail.com

Tuendelee...

...akionekana kuguswa ndani kabisa kiasi cha kumfanya machozi yamlenge lenge alishuhudia ukweli uliodhihirishwa na sauti na macho ya baba yake.

‘Baba analia’ alijisemea nafsini alijikuta ni kama mtu aliyepatwa na bumbuwazi Fulani akishuhudia hali ngumu ya maisha yaliyo nyuma ya baba yake yenye hatari kubwa na usalama kiduchu. Alijikuta akitingisha kichwa kuelewa jambo analo lijua yeye mwenyewe.

Kimya kilipita midomo ikiwa imeshonwa wakitupiana macho yenye kusema ya moyoni, kuonewa! Vizuka wakibaki kutazamana tu mwishowe Burushuti ikambidi aangue kicheko kiasi cha kushika kitambi chake, Mti Mkavu akiwa mkavu kama jina lake akimtazama tu bila neno.

Sehemu 4 A

MTAA WA KIPASO-JIJINI NYATUMBU
Mtikisiko wa gari ndio uliomtoa Nkole mawazoni kiasi cha kumfanya ashtuke na kuangaza macho huku na kule, huyo akafungua mlango na kutoka bila kusema kitu moja kwa moja hadi kwenye Buti akalifungua na kutoa mabegi matatu akimuacha Gotwa akifatia kutoka pamoja na Vizuka.

Muda wote huo Mbonde alikuwa ameshika tama akishuhudia kwenye kioo cha saitimila yu njia panda. Hao baba na mwana hadi getini. Mlnago ukafunguliwa Gotwa akatangulia na Nkole akafata mara Mkono ukazuia mlango wa geti uliokuwa ukisukumwa kufungwa, alikuwa Mbonde mbele ya macho ya Nkole

“Nikusaidie nini…?” Mbonde akatulia kwa sekunde kazaa huku akisikitika kwa kichwa “Samahani Nkole, unajua haya mambo yanahitaji akili nyingi sana kuyafikiri nina wazo nimepata naweza kukushirikisha.” Aliongea Mbonde sasa akiyabana meno “Mbonde fanya kitu kimoja wewe nenda kesho tutaonana hapa,

nahitaji kupumzika” Nkole alimkatisha Mbonde akimtazama kwa macho makavu na yakutishia “…Mdaku hawezi kunifanya kitu chochote kibaya itakuwa vizuri kama utaondoka ili usijiingize zaidi kwenye matatizo,

maana kama utaonekana umefika mpaka hapa wanaweza jua kuna mpango kinyume nimeupanga dhidi yake” aliongea Nkole na Mbonde akatingisha kichwa kukubali “Ni sawa, basi sawa nimelewa” akautoa mkono wake genitini na kushika njia yake huku Nkole akiufuga mlango. “Ahh namna gani tena” Mbonde alilaani na kukunja ngumi uso kaukunja kweli kweli kashika kiuno midmo akiipinda panda kwa jazba. Akachukua simu yake na kuitazama. “Nini cha kufanya sasa, nimwambie nimuache?!” Huyo akaingi agarini akaiwasha na kuitoa eneo hilo.

Majira ya saa tatu na nusu usiku Nkole akiwa sebureni na tarakilishi mpakato mapajani, Gotwa kwa hatua za kunyata alikuwa akitoka chumbani kwake akielekea upande aliopo baba yake kwa tahadhari kuu.

Nkole bado bize akiandika anachokijua baaada ya kumaliza akaelekeza kasa hadi katika kitufe cha save akakibofya, akaikuna pua yake na kuanza kuusoma ujumbe huo kwa sauti neno kwa neno.
“Mh. Mdaku na shutma za kichovu, Serikali Itafakari tena.”

Na Mwandishi Nkole S. Kileo
Imekuwa desturi ya kupaka sifa zilizokosa shuhuda kwa viongozi waliojihimu kiuchumi tokana na vyanzo mablimbali vya kiuchumi vilivyo wekezwa kwa jasho lao kama ndugu Mh.Mdaku na wengineo.

Hali hii hatarishi si sawa kwani inaleta vuguvugu la mawazo hasi kwa vijana wanao chepuka kwa kasi hivi sasa na viongozi wenginneo wanaohitaji kuipeleka nchi kwenye uchumi wa kati kama serikali inavyotamani, kiasi cha kuwafanya wazawa kumiliki viwanda na kuzalisha bidhaa sisi wenyewe na sio kuzikabidhi kwa wale wageni walio na tama ya kujenga kwao, maana mtu kwao.

Tafakur inahitajika sana na chunguzi zenye tija dhidi yake na si mkurupuko kama uliofanyika jana nyumbani kwake na katika shamba lake kuubwa la nyuki na miti wilayani Chozi kwa kumshinikiza atoe na kueleza ghala la madawa ya kulevya analo limiliki,

swali kwanini asibanwe aliyetoa shutma hiyo kabla ya hatua kuchukuliwa? Je! tunafikilia kuhusu athari itakayo mkuta Mh. Huyu katika jimbo lake na nchi nzima? Wangapi watakuwa wamepoteza imani dhidi yake.

Naiomba serikali iwaangalie tena askali iliyo nao katika jeshi la Polisi maana kuna mandumilakuwili wengi,

siku tutapoteza watu muhimu kwa kutengeneza kesi zenye ushahidi wa uonevu kwa sababu zimwi likujualo halikuli likakwisha”

Alimaliza kusoma, Nkole akatabasamu “Nimepiga jiwe moja nimepata ndege wawili mimi ndio mshona maneno rafiki wa kalamu, kalamu kamwe haiwezi kuniangusha Maduku lazima utayaamini maneno yangu” akatabasamu

Itaendeleaa...
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

MSIMU 1

Sehemu 4B

Ilipoishia...

“Nimepiga jiwe moja nimepata ndege wawili mimi ndio mshona maneno rafiki wa kalamu, kalamu kamwe haiwezi kuniangusha Maduku lazima utayaamini maneno yangu” akatabasamu kisha akaenda hadi katika sehemu iliyoandikwa send na kubofya kupitia kasa.

Tuendelee...

...Haikuchukua muda ujumbe ukaingia akatabasamu pumzi zikasushwa sasa kajiegemeza sofani akitazama saa ya ukutani. Akachukua simu yake ya kisasa akaiwasha, baada ya kuwaka akaanza kutafuta kitu akagota “Mh. Maduku” alitaja jina hilo tayari akiibonyeza, Gotwa aliona upenyuni mwa pembe akichungulia masikio yake makubwa kayasimamisha akipumua kwa utulivu akatabasamu,

Mara Hodi! Wote wakapeleka macho mlangoni mlango ukagongwa tena. Nkole akachukua bastola yake ndogo nyuma ya kiuno akaiweka tayari kushambulia macho kayatuliza akanyanyuka sofani. Macho mlangoni akiufata hhuku mkono mmoja ukizima simu na kuisusia mfukoni mwa suruali yake. Gotwa akimtazama tu.

Kabla ya kuufungua mlango akalipenyua pazia la dirisha kuchungulia kwa tahadhari kubwa, lakini uso wake ulirudi ukiwa umepwaya macho kayatoa. Kama aliyeona kitu cha mshngazo au kuogofya akameza funda la mate kwa shida “Kina nani?!” alihoji sasa kakishika kitasa na mkono mmoja bunduki yake. Lilikuwa kosa kubwa alishtukia yupo chini mlango ukiwa wazi wanaume sita wakiwa mbele yake wakimtazama kama windo, nyuso zao zikimkebehi.

Nkole aliwatazama kwa muda kisha akasema “Niwasaidie nini?” aliongea akiitazama bunduki yake mita moja pembeni yake hamu ya kuikwapua ajitete! Haikuwa, alishuhudia ikipigwa teke na kusukumiziwa mbali huko ni kama zilisomwa hisia zake. Yu matatani! “Unajifanya Makini na mjuaji sana, huna kazi za kufanya?” Nkole aliwatazama kwa makini nyuso zao zikidhihirisha shari. “Tupatie mzigo wetu tuondoke” aliongea tena bwana yule akipiga hatua kwa dharau kumsogolea “Mzigo gani?” aliongea Nkole huku akisimama.

“Huyu anaongea nini anatuuliza jibu akiwa nalo tumjibu nini” alisema bwana yule akiwageukiaz wenzake na kuangua kicheko cha dharau kilicho muudhi Nkole kiasi cha kutupa woga “Sikiliza Jamaa Biashara haikuwa hivyo mpigie simu nihakikishe?”

aliongea Nkole akimkazia macho huku akimsogolea kibabe meno kayauma “Inamaana hauamini au jeuri?” aliongea bwana yule aliyeonekana kuwa ni kiongozi kwa kupaza sauti “Aisee nimemaliza kama hamuwezi mnaweza kwenda tu kama baya liwe baya” aliongea Nkole akionesha mkono kwa ishara.

Wale wanaume sita wakatizamana kama watu wanao subiria dhamila yao ifike, kiongozi wao akasonya na kuitoa simu yake mfukoni na kuweka sikioni “Ndio Mkuu…hapana anaonekana kusumbua…shika simu” aliitoa masikioni na kumuwekea Nkole mezani, Nkole akaichukua na kuiweka masikioni “Hallow Mh…” kabla hajatia neno lingine fumba na kufumbua alishtukia kitu kizito kikigongwa usogoni mwake na kuangukia meza Mguno tu wa uchungu ndio uliosikika huku akipeleka mkono kushika majeraha yake.

Gotwa aliona alishtuka na kujiziba mdomo mwili ukimtetemeka. Si yeye tu vizuka nao walikuwepo wakitoa macho Burushuti akimtazama Mti Mkavu “Aisee si unaona nilikwambia Nkole haaminiki umesahau? Tufanye kumuokoa haraka watamuua bure” alisema tena Burushuti.

Nkole akiwa anasikikilizia maumivu ya kichwa asijue la kufanya akigaa gaa kwa maumivu akapatwa na mshtuko mwengine baada ya kitu kizito kugongwa kwenye utosi wa kichwa chake Loo! Mwili ukamuisha nguvu akajikuta macho yakipoteza nuru na mwisho akayafumba kabisa. “Shenzi! jamaa umeingia cha kike leo kazi kwisha” aliongea mmoja wao. “Sasa fanyeni kuutafuta ule mzigo haraka iwezekanavyo pia msisahau kuchunguza kama kuna kamera za siri, hatuna muda” yule kiongozi aliongea na wote wakatawanyika.

Gotwa alishuhudia akajikuta akirudi kinyume nyume taratibu hadi mlango wa uwani akaufungua na kutoka macho yakiwa yamemtoka akionekana kutafuta kitu. “Mti Mkavu tunafanyaje mbona usemi kiti jamaa yangu” alisonona Burushuti na Mti Mkavu akimuangalia tu kwa muda akidhihirisha huzuni yake machoni.

“Tumefanya makosa makubwa sana amekufa huyu sioni akihema” mmoja wao alionekana akikitoa kidole kwenye tundu za pua ya Nkole, “Tunge hakikisha anatupa kwanza mzigo wetu ndio tumuue, tumekosa bara naz Pwani”

Nyakati hizo hizo Mbonde alikuwa maeneo ya nje ya nyumba ya Nkole akitazama kwa makini, mara akasikia simu ikiita “Mh Maduku...” alitaja jina hilo baada ya kutazama kwenye kioo cha simu yake

“Hallow…ndio nasubiria mzigo wangu…Mhh! mbona majukumu unayaongeza nina shida na hiyo hela Mzee, Ahhh!” alipwaya msimamo huu miguu ikagoma macho kayatumbulia ardhini “…nilichokiona kuna njemba zimefika naamini ni watu wako… umewatuma…nini?!”

alitahamaki akageuza shingo kutazama alikotoka domo limemuanguka uso umemshuka huku mapigo ya moyo yakimuenda matitit kweli kweli, hakutegemea taarifa hiyo! “Mhh…sasa itakuwaje Mzee mbona unanididimiza shimoni nitatokaje, siku zania haya ulinihakikishia…nakwambia hakuna aliyenusa nyayo zangu naijua kazi yangu vyema…nina shida na hiyo aisee”

Tititiii tititiii “Amekata?!” akaitazama simu yake kama akisubiri imjibu, hola! Kabaki kaishika tu huku akinesehaa kichwa chake “…nini la kuchagua sasa lipii?” akatazama huku na kule kupata wakumjibu, nani wakumjibu?!
Sasa alibaki akikuna kichwa
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 1

Sehemu 4C

Ilipoishia...

... Ahhh!” alipwaya msimamo huu miguu ikagoma macho kayatumbulia ardhini “…nilichokiona kuna njemba zimefika naamini ni watu wako… umewatuma…nini?!”

Tuendelee...

alitahamaki akageuza shingo kutazama alikotoka domo limemuanguka uso umemshuka huku mapigo ya moyo yakimuenda matitit kweli kweli, hakutegemea taarifa hiyo! “Mhh…sasa itakuwaje Mzee mbona unanididimiza shimoni nitatokaje, siku zania haya ulinihakikishia…nakwambia hakuna aliyenusa nyayo zangu naijua kazi yangu vyema…nina shida na hiyo aisee”

Tititiii tititiii “Amekata?!” akaitazama simu yake kama akisubiri imjibu, hola! Kabaki kaishika tu huku akinesehaa kichwa chake “…nini la kuchagua sasa lipii?” akatazama huku na kule kupata wakumjibu, nani wakumjibu?!
Sasa alibaki akikuna kichwa kujua cha kufanya

“…lazima nifanye kitu kuokoa maisha ya Nkole haraka iwezekanavyo…ahh sasa kwa namna gani?!” akijisemea peke yake akajikuta akikuna kichwa.

Akienda akirudi kapagawa!? Akawa ngaa! macho mbele “Nikisema niende mzima mzima wakitoka wakiniona ni mshirika nikisema nipige simu bado maswali yatakuwa mengi” Mbonde akajiinamia akifikiri, mara akatoka mawazoni baada ya kuona gari iliyopaki umbali wa mita ishirini toka usawa wa nyumba ya Nkole kuwashwa ikageuza na kuondoka, “Afadhari” alijiongelea na kutoka mafichoni akasogea kwa kukimbia mkimbio wa kuinama bila kutoa sauti ya vishindo vya mguu hadi kwenye ukuta akainama nakujirusha mzimamzima mikono ikashika upande wa juu wa kuta akajivuta na kujirusha.

“Unajua nini Burushuti” Mti Mkavu aliuvunja Ukimya akamtazama Burushuti wakiwa wamesimama mbele ya mwili wa Nkole. Kabla hajatia neno la dhamira. Kilisikika kishindo, “..nani?” alisema Burushuti akimtazama Mti Mkavu “Pana mgeni wa mashaka teyari twende” alisema Mti Mkavu akawa wa kwanza kuyeyuka yayuu! Akifatiwa na Burushuti.

Mbonde akiwa kachuchuma goti moja limeinama, Kulia kushoto macho yalitazama kisha akatoka hadi upande wa nyuma ya nyumba kwa mvizio mkuu. Akasogea hadi kwenye madirisha akichungulia kwa tahadhari lakini aliambulia alichokiwaza “Hakuna mtu wa ziada!” alijisemea sasa huyo kwa mwendo ule ule aliouchagua hadi upande wa nyuma ya nyumba “Gotwa…Gotwa..” aliita kwa sauti fifiiii ya kunong’ona masikio juu juu akiyatega kama antenna kunasa majibu, akarudia kuita tena “Naam niko huku” Gotwa aliitika toka katika msongamano wa makorokoro pembeni ya gofu la banda.

Gotwa alitoka mafichoni “Nifate huku mjomba” Gotwa aliongea na kuongoza njia, nae bila maelekezo akinyata kiasi cha kumfanya Mbonde atabasamu nyuma yake. “Huyu mtoto anaisuuza roho yangu, mjanja mjanja na akili mingi” alisema Burushutu na kutoa ulimi wake mrefu akijilamba midomo hadi sehemu ya juu ya mustachi wake kwa jicho la uchu mashavu yakipanda kwa juu, Mti mkavu akamkata jicho pembe kijicho pancha kisha huyo akatangulia ndani Burushuti akimng’ong’a kwa nyuma.
“Mbonde akiwa na Gotwa waliingia hima hima.

“Aisee hali yake ni mbaya sana…hapa cha kufanya ni kuokoa maisha yake lakini huu pia ni mtego” Mbonde akanyanyuka na kumtazama Gotwa aliyekuwa akimtazama “Baba yako hajakufa lakini inaweza kuwa kama atakosa huduma mapema na kwa haraka zaidi, ubaridi umemuanza” Mbonde akatoa simu yake na kakikaratasi toka mfukoni mwa suruali yake akaanza kuziandika. Mshangazo zilionekana katika simu yake “Nilijua tu…” aliongea pekee na kutingisha kichwa cha masikitiko

“Hallow…tafadhari Nkole yupo mahututi nyumbani kwake…acha basi nasema kweli sitanii …hupajui! Inawezekanaje?!!” aliongea kwa tahamaki na kugeuka akimtazama Nkole aliyekuwa hajijui hajitambui “…sawa nitakuelekeza” akaanza maelekezo akimaanisha kwa kunyanyua mikono hivi na vile.

“Sawa sawa nitakusubiri nje” aliongea Mbonde kisha akashusha pumzi nzito na kumtazama Gotwa “Usijali baba yako atapona tusubiri msaada, lakini kipindi tunafanya hivyo usiguse chochote na pia kuna mwanamke atakuja mruhusu aingie funguo hizo” aliongea Mbonde kisha akatoka. Jamaa wacha nikamtazame huyu bwana maana namuona ni wamashaka kweli sina imani nae” aliongea Burushuti na kuyeyuka Yayuu! Akimuacha Mti Mkavu akimtazama tu Nkole pale sakafuni Gotwa akiwa pemebni yake.

Mbonde Aliacha uelekeo wa geti hadi kwenye ukuta akakusanya mwili kama paka kwenye mawindo na kuruka mikono ikashika sehemu ya juu ya ukuta akajivuta na kurukia upande wa pili, tayari nje ya uzio. Macho kulia macho kushoto kwa tahadhari akiwa kachutama macho makini

“Amani” alijisemea kwa sauti ya chini na kukaa nyuma ya ua lilliloshonana na kuweka kificho kwa chaka lake kushikana. “Nafanyaje sasa, kweli shida mwanaharamu watu kweli hawaaminiki loo!, nishaingia ngomani sasa hiki ni Kisanga tena Kisanga kweli kweli hiki ni Kisanga” akajikuta akianza kujicheka mwenyewe na kisha kununa.

Akaitoa simu akiitazama akijishauri cha kufanya. “Anataka kuniingiza matatizoni huyu nishajipaka kinyesi teyari nzi wataniumbua si muda mrefu lazima niwe na machaguo ya wastani haraka iwezekanavyo” alijisemea akitingisha kichwa kukubali maneno yake. Burushuti pembeni yake alitingisha kichwa kukubali kitu akiwa pembeni ya Mbonde na Mbonde asifahamu jirani yake huyo.

Itaendeleaa
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact 0658328596
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 1

Sehemu 4 D

Ilipoishia...

haraka iwezekanavyo” alijisemea akitingisha kichwa kukubali maneno yake. Burushuti pembeni yake alitingisha kichwa kukubali kitu akiwa pembeni ya Mbonde na Mbonde asifahamu jirani yake huyo.

Tuendelee...

MTAA WA BONYO -JIJINI NYATUMBU

“Nkole amepatwa na nini jamani…” aliongea mwanamke huyo akiwa kitandani mwake ameshikilia simu akiitazama kwa muda kama akihitaji imjibu nayo ikamkodolea tu ikimshangaa kwa swali la kizushi kaweka kishoka godoroni mlalo upande simu kashikilia. Umbo la ajabu kweli kweli si kwa mkunjo ule wa nane kubwa! “…Wacha nije mpenzi, wacha nije niokoe maisha yako haraka…”

akakurupuka kitandani simu akiacha kando, asiwe na habari nguo kaicha nyuma kwa kujivuta kwake. Sehemu zake za thamani huko bavuni zikaonekana! kwani nani kaona?!! Si yupo peke yake?! Nani kasema? Haikuwa hivyo! Bwana mmoja alikuwa dirishani akitazama picha ya bure bure akiumia rohoni anaweweseka akiguna miguno ya ajabu kwa maumivu ya huba! moyo ukimuenda matiti akitamani apitie dirishani akamvae lakini ikawa ya “Nakula kwa macho nakula kwa macho” ataipaatia wapi bahati hiyo? Teyari alisimama “…hii ni nafasi yangu ya pekee lazima nije, nakuja” alisema sasa kalivamia kabati akiwa na nguo moja tu ya kulalia.

Nguo nyeupe ya mterezo iliyoshika maungo hasa kwa upana ule lakini haikufua dafu kwa umbo lake la ajabu ya maajabu ya muumba! Ashukuriwe sana! Si kwa umbo hilo la uchochozi wa mtima. Mwili ulio tuna tuna si wa madawa tembe wala sindano choma.

Weusi ang’avu, kiuno kilicho shikwa na mgongo kikabanwa na kutoa mkunjo wa cha! huyo kama nyigu fungasho la haja nyuma yake hachoshi machoni mwa rijali lazima udenda utamtoka kwa uchu na pupa ya penzi kula vyote vya ndani kulamba sahani kwa kutoisha hamu ya tamuni. Penzi kweli Mafua ukiwa nayo Ni homw. Fiyona akaacha chuchumio asijue kuna mtu anakaribia kukata roho kwa kiu ya huba akisonona kwa dua za kila lugha maombi yasiyo na kipimo jasho la sikio likitoka ubaridi ukimshika asijue maumivu ya mbu wanaonyonya damu yake,

Hanahabari nao yupo kwenye bahari ya huba yenye ubaguzi akijutia kuingia akimtazama tu mwanamke huyo aliyetayari kidhi hitaji lake mkono ukatoka na vazi alilokusudia akaachia vifungo chini kidogo ya kifua chake mfanowe vifuu viwili vya nazi. Nguo yake ya usingizi ikajimwaga sakafuni mwaa! Bwana yule alijikuta ameganda ngaa! na mdomo ukaanguka asijue anavuta hewa au anatoa mshtuko wa ghafla! Nini kaona?! Akajikuta akinyong’onya mwili ukamuisha nguvu akaambaa na ukuta taratibu na kulalaa usingizi kabisa.

Amekoma! Mbona yalimkuta bwana yule wa chabo Sizani kama atapona!! . Muhusika wenyewe hana habari, cha kwanza vazi lake refu la heshima akatupia maungoni kishapo kuvaa na kuva vya kumfaaa. “Sasa nakuja” akashika simu yake kipochi kwapani na kutoka chumbani.
Wee Ntobo aliita na kuita tena na tena akienda varandani, mlango wa chumba na kisha nje kabisa.

Bwana yule alikurupuka, Kapona!! “Naitwa…” alijiseme kwa mashaka wasiwasi huu hapa akatulia kidogo akipeleka macho kule na huku “Ndio” alijijibu mwenyewe sasa akatoka eneo hilo akienda upande mwengine tofauti na sauti itokako huku akijikung’uta vumbi “Naam” alisema nyuma ya mwanamke yule “Hee! Muda wote naita! wewe…haya nifate” Aakatangulia mbele asijue anammaliza kihisia bwana huyo aliyejaa tele akiteseka kwa huba la sirini.

Akimeza mate na kuumia ndani kwa ndani asitamani kukumbuka aliyoyaona akikwepesha macho asitazame ya mbele yake asije pata maradhi ya kuanguka bure maana alienda akitetema kama yumo shotini ya umeme mbaya namna aliyoyaona muda hule akihisi akimuona akiwa wote wote. “Hapana hapana” alijikuta akisema pasina kutarajia “Nimesikia kitu” aliohoji mwanamke yule “…hapana hakuna kitu” alizuga Ntobo akifinya finya macho yake akilazimisha tabasamu “Ohh sawa…nafikiri ujumbe wangu wa simu uliipata bila shaka” alisema tena na kumfanya Ntobo ajichekeshe akaitoa simu mfukoni

“..ndio ndio” akijichekesha chekesha huku akitazama ujumbe simuni akimuacha mwanamke yule akijiegemeza kwenye kioo mawazoni. “Twende chapuchapu nataka kuokoa maisha yake haraka sana” alisema tena akiwa kakaa vile vile uso wa wingi mashaka na hamu zaidi ya kukamilisha ya moyoni. Gari iliwashwa Geti likafunguliwa na bwana aliyeonekana kuwa ndiye hasa mlinzi wa eneo hilo.

Gari hiyo ikafata njia iliyoelekea kusini Magharibi huku ikiacha majengo ya thamani yaliyo randana mshonano mataa yaki mulika kila mahala huku sauti ya majibwa yakifoka kwa kupokezana. ‘Jamani naomba usife wangu usife sitaki ufe wangu’ aliongea nafsini macho teyari machozi hakuwa na kazi nayo akayaacha yamwagike kichwa kakilaza.

Ntobo alibaki kumtazama tu na kutingisha kichwa akisikitika, nikama anajua yamlizayo au asitamani kuyajua hakutia neno zaidi ya kumuangalia kwa kuibia mdomo ukimcheza nafsi ikimsukuma aseme ya moyoni huku akili ikimzuia na hata kuhisi nafsi yake mwenyewe ikimcheka, hakutamani hakutamani chochote. Aliishia kutingisha kichwa kuvuruga mawazo yaliyomtawala.

Itaendelea

 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact 0658328596
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 1

Sehemu 4 D

Ilipoishia...

haraka iwezekanavyo” alijisemea akitingisha kichwa kukubali maneno yake. Burushuti pembeni yake alitingisha kichwa kukubali kitu akiwa pembeni ya Mbonde na Mbonde asifahamu jirani yake huyo.

Tuendelee...

MTAA WA BONYO -JIJINI NYATUMBU

“Nkole amepatwa na nini jamani…” aliongea mwanamke huyo akiwa kitandani mwake ameshikilia simu akiitazama kwa muda kama akihitaji imjibu nayo ikamkodolea tu ikimshangaa kwa swali la kizushi kaweka kishoka godoroni mlalo upande simu kashikilia. Umbo la ajabu kweli kweli si kwa mkunjo ule wa nane kubwa! “…Wacha nije mpenzi, wacha nije niokoe maisha yako haraka…”

akakurupuka kitandani simu akiacha kando, asiwe na habari nguo kaicha nyuma kwa kujivuta kwake. Sehemu zake za thamani huko bavuni zikaonekana! kwani nani kaona?!! Si yupo peke yake?! Nani kasema? Haikuwa hivyo! Bwana mmoja alikuwa dirishani akitazama picha ya bure bure akiumia rohoni anaweweseka akiguna miguno ya ajabu kwa maumivu ya huba! moyo ukimuenda matiti akitamani apitie dirishani akamvae lakini ikawa ya “Nakula kwa macho nakula kwa macho” ataipaatia wapi bahati hiyo? Teyari alisimama “…hii ni nafasi yangu ya pekee lazima nije, nakuja” alisema sasa kalivamia kabati akiwa na nguo moja tu ya kulalia.

Nguo nyeupe ya mterezo iliyoshika maungo hasa kwa upana ule lakini haikufua dafu kwa umbo lake la ajabu ya maajabu ya muumba! Ashukuriwe sana! Si kwa umbo hilo la uchochozi wa mtima. Mwili ulio tuna tuna si wa madawa tembe wala sindano choma.

Weusi ang’avu, kiuno kilicho shikwa na mgongo kikabanwa na kutoa mkunjo wa cha! huyo kama nyigu fungasho la haja nyuma yake hachoshi machoni mwa rijali lazima udenda utamtoka kwa uchu na pupa ya penzi kula vyote vya ndani kulamba sahani kwa kutoisha hamu ya tamuni. Penzi kweli Mafua ukiwa nayo Ni homw. Fiyona akaacha chuchumio asijue kuna mtu anakaribia kukata roho kwa kiu ya huba akisonona kwa dua za kila lugha maombi yasiyo na kipimo jasho la sikio likitoka ubaridi ukimshika asijue maumivu ya mbu wanaonyonya damu yake,

Hanahabari nao yupo kwenye bahari ya huba yenye ubaguzi akijutia kuingia akimtazama tu mwanamke huyo aliyetayari kidhi hitaji lake mkono ukatoka na vazi alilokusudia akaachia vifungo chini kidogo ya kifua chake mfanowe vifuu viwili vya nazi. Nguo yake ya usingizi ikajimwaga sakafuni mwaa! Bwana yule alijikuta ameganda ngaa! na mdomo ukaanguka asijue anavuta hewa au anatoa mshtuko wa ghafla! Nini kaona?! Akajikuta akinyong’onya mwili ukamuisha nguvu akaambaa na ukuta taratibu na kulalaa usingizi kabisa.

Amekoma! Mbona yalimkuta bwana yule wa chabo Sizani kama atapona!! . Muhusika wenyewe hana habari, cha kwanza vazi lake refu la heshima akatupia maungoni kishapo kuvaa na kuva vya kumfaaa. “Sasa nakuja” akashika simu yake kipochi kwapani na kutoka chumbani.
Wee Ntobo aliita na kuita tena na tena akienda varandani, mlango wa chumba na kisha nje kabisa.

Bwana yule alikurupuka, Kapona!! “Naitwa…” alijiseme kwa mashaka wasiwasi huu hapa akatulia kidogo akipeleka macho kule na huku “Ndio” alijijibu mwenyewe sasa akatoka eneo hilo akienda upande mwengine tofauti na sauti itokako huku akijikung’uta vumbi “Naam” alisema nyuma ya mwanamke yule “Hee! Muda wote naita! wewe…haya nifate” Aakatangulia mbele asijue anammaliza kihisia bwana huyo aliyejaa tele akiteseka kwa huba la sirini.

Akimeza mate na kuumia ndani kwa ndani asitamani kukumbuka aliyoyaona akikwepesha macho asitazame ya mbele yake asije pata maradhi ya kuanguka bure maana alienda akitetema kama yumo shotini ya umeme mbaya namna aliyoyaona muda hule akihisi akimuona akiwa wote wote. “Hapana hapana” alijikuta akisema pasina kutarajia “Nimesikia kitu” aliohoji mwanamke yule “…hapana hakuna kitu” alizuga Ntobo akifinya finya macho yake akilazimisha tabasamu “Ohh sawa…nafikiri ujumbe wangu wa simu uliipata bila shaka” alisema tena na kumfanya Ntobo ajichekeshe akaitoa simu mfukoni

“..ndio ndio” akijichekesha chekesha huku akitazama ujumbe simuni akimuacha mwanamke yule akijiegemeza kwenye kioo mawazoni. “Twende chapuchapu nataka kuokoa maisha yake haraka sana” alisema tena akiwa kakaa vile vile uso wa wingi mashaka na hamu zaidi ya kukamilisha ya moyoni. Gari iliwashwa Geti likafunguliwa na bwana aliyeonekana kuwa ndiye hasa mlinzi wa eneo hilo.

Gari hiyo ikafata njia iliyoelekea kusini Magharibi huku ikiacha majengo ya thamani yaliyo randana mshonano mataa yaki mulika kila mahala huku sauti ya majibwa yakifoka kwa kupokezana. ‘Jamani naomba usife wangu usife sitaki ufe wangu’ aliongea nafsini macho teyari machozi hakuwa na kazi nayo akayaacha yamwagike kichwa kakilaza.

Ntobo alibaki kumtazama tu na kutingisha kichwa akisikitika, nikama anajua yamlizayo au asitamani kuyajua hakutia neno zaidi ya kumuangalia kwa kuibia mdomo ukimcheza nafsi ikimsukuma aseme ya moyoni huku akili ikimzuia na hata kuhisi nafsi yake mwenyewe ikimcheka, hakutamani hakutamani chochote. Aliishia kutingisha kichwa kuvuruga mawazo yaliyomtawala.

Itaendelea

Mpo????!!!!
 
KISANGA (Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Email akidasiri@gmail.com
Contact 0658328596

MSIMU 1
Sehemu 4 E

Ilipoishia...

.... alibaki kumtazama tu na kutingisha kichwa akisikitika, nikama anajua yamlizayo au asitamani kuyajua hakutia neno zaidi ya kumuangalia kwa kuibia mdomo ukimcheza nafsi ikimsukuma aseme ya moyoni huku akili ikimzuia na hata kuhisi nafsi yake mwenyewe ikimcheka, hakutamani hakutamani chochote. Aliishia kutingisha kichwa kuvuruga mawazo yaliyomtawala.

Tuendelee...

HOSPITALI YA BOJOBOJO-JIJINI NYATUMBU
Gari tu ilipo simama wasichana watatu waliivaa na kumtoa Nkole akiwa hajijui hajitambui mzobe mzobe wakamtia macherani mkuku mkuku hima hima wakiikimbiza machela wakikata kona na kuingia kona nyingine hadi mbele ya mlango mmoja wenye kibao cha DHARURA. Wakazama. Punde mwanamke yule akatokea akichepuka kwa kukazana akiwa na vazi jeupe maalumu nae akaingia. Kama si dakika kumi basi ishirini mlango ukafunguliwa na Nkole akatolewa akiwa na mavazi ya kijani akikokotwa na wadada watatu dripu ikiwa imekitwa mkononi puani akiwa na kifaa cha usaidizi wa kupumua.

Mwanamke yule akiwa mbele mbele yao akiongoza njia huku akipishana na baadhi ya wauguzi wagonjwa na wasaididizi wao hao hadi wodi namba 28 katika kibao ikisomeka. “Skia Ntobo fanya uwende nyumbani niko salama hapa nenda na ufanye niliyo kwambia” aliongea akimtazama Ntobo aliyekaa kimya akilazimisha tabasamu lilikatalika moyoni. Anaficha hisisa zake! “Sawa ubaki salama Fiyona na usizime simu tafadhari” alishika mkono wa Fiyona kwa mikono miwili mshiko uliomshtua sana Fiyona kiasi cha kuitazama ikifikisha ujumbe wa hisia alizokataa kuziamini akapandisha macho kumtazama Ntobo aliyeishia kutabasamu tu macho yakisema kitu, Mapenzi! Kisha huyo akashika njia.

Fiyona alimeza mate akimsindikiza Ntobo lakini akaachana nae na kukatisha mawazo yake na e akafata njia yake. Waaguzi waliyafanya ya kwao Walifanya majukumu yao kishapo wakatoka Fiyona akibaki pekee. Fiyona alibaki kumuangalia Nkole asimmalize, akionekana wazi ni mtu anaye pitia magumu mtu mwenye majuto mengi. Mkono wake ukiwa kiganjani mwa Nkole aliye tuli kama maji mtungini, asiyejulikana yupo anga za dunia au akhera. Akabaki kumeza mate yaliyopita kwa tabu kooni akifinya finya macho yake Loo! Machozi hayo mashavuni yakimtiririka na mwisho sauti ya uchungu toka ndani kabisa ya moyo wake ikatoka na kushindwa kuvumilia kilio kikachukua nafasi yake.

Mlango ulipo gongwa akageuka na kukutana na Mbonde akiwa teyari mbele yake amefura kwa hasira za wazi lakini akionekana ni mtu anaye jizuia. “ Hebu nieleze nini kinaendelea hapa kitu gani nisichokijua kukuhusu” aliongea Mbonde akimkazia macho Fiyona, macho yenye kuonesha Wivu wa wazi wazi. Burushuti aliduwaa akimtazama Mbonde machoni kabisa karibu zaidi na kumtazama Fiyona. “Nikuuulize wewe nini kimemtokea Nkole mpaka amekuwa hivi?” maneno ya uchungu yalimtoka Fiyona, lakini yalikuwa kama yasiyoleweka mbele ya Mbonde uso wa viulizo katoa macho kama saa iliyoisha betri, akagutuka “Unasemaje Fiyona” “Umesikia sana ila kusudi tu” alipewa jibu la mkato “Yani sielewi mna mipango gani najikuta nimeingia kwenye vita isiyonihusu tena…ni nani yako huyu” alijikuta anaingia kwenye maana yake Fiyonaz akageza uso kumtazama Mbonde kwa macho ya shangazo wakatazamana,

Fiyona hakuwa na cha ksema akageuza uso na kuushika mkono wa Nkole na kuuweka karibu na kifua chake huku akigugumia kwa maaumivu kiasi cha kuzidisha shangazo la Mbonde. "Hapa teyari nimesha haribu kazi yangu nimevunja uwaminifu wangu kwa ajili yake…hebu niambie Fiyona huyu ninani yako usinifiche na hapa sielewi naona mapenzi yakidhihirishwa mbele yangu tafadhari usije sema eti unampenda!” aliongea Mbonde macho kayatoa akimnyoosheakidole chaz ole wako!

Fiyona akageuza tena uso kumtazama Mbonde “Huyu ndiye mwanaume ninaye muhusudu kupita kitu chochote duniani nakwambia” Mbonde akapatwa na uduwanzi “Sijasikia vizuri ama!” “Umesikia sana sema unataka nirudie ni hivi nampenda sana Nkole” aliongea Fiyona na sasa akimpa uchogo Mbonde aliye simama nyuma yake Mbonde akajikuta akiishiwa nguvu akajishika kiuno asijue la kufanya kusuka au kunyoa!?

“…najua upo na hasira sana na nilijua tu utachukia, huyu ndiye yule mwanaume niliyempoteza na niligharamika kurudisha imani yake kwangu sikufanikiwa ila leo wewe umeyafanya haya, naomba tu unisamee Mbonde hili ndio chaguo langu nina weza kuligharamia amuzi langu kwa gharama yoyote ni baki na Nkole tu” aliongea huku akimtizama Mbonde aliye simama tu.

Burushuti akatingisha kichwa cha sikitiko akisikiliza tu majibizano “Vipi kuhusu mimi sasa, kazi yangu Penzi langu muda wangu ehhh! mbona sijakuelewa Fiyona mambo gani haya unanipiga dana dana kila siku husomeki waniacha feli nikishangaa meli bila kunipa jibu langu ukikazana kuwa wanichunguza ukinipa moyo wa hivi na vile eeh!?” alilalama Mbonde akimshika mkono Fiyona kumbembeleza kwa jicho la huba linalo sema Tafadhari huku akiyakita magoti sakafuni.

“Hebu ona tangu umeachika na mumeo nimekuwa karibu yako nikikuliwaza nyakati za chache tu tukila pamoja leo wanilipa haya kwa mtu huyu” alianza kulengwa na machozi “Masikini mie mbona nilichelewa kuyajua haya teyari nimeshaoza mwili wote” alinung’una Mbonde kwa sauti ya sikitiko yenye mikwaruzo “Hapana siwezi kuhudumia mabwana wawili kwa wakati mmoja kama ni kuhusu Pesa hiyo hapo” alichukua begi lake na kutoa mfuko uliokuwa na mabunda ya noti hizo ni pesa nyingi sana zitakusaidia” “Pumbavu huu ni ujinga” aakaupigaza mkono mfuko ukaanguka sakafuni na kutoka zake kwa hasira.

Mwili ulimuelemea akabaki kupiga hatua za kujilazimisha wazi haamini kilichotokea machoni mwake minyoso tu ikipokezana mdomoni mwake kichwa kikimuuma kwelikweli “Nini maana ya haya yote!” alijisemea kwa sauti kisha akajikalisha kwenye kiti cha mapumziko na kujiinamia mikono kichwani “Nitafanya nini…Hebu ngoja niondoke hapa...sasa naenda wapi muda huu usiku huu mzito?!” alijisemea kwa huzuni Burushuti akimsoma tu kwa makini na mara akajigeuza na kutoa simu yake aliufungua ujumbe wa maandishi aliokutana nao kisha kashusha pumzi nzito na kujiegemeza “Haa! Gotwaa! Gotwa yupo wapi saii” Alitaharuki, akanyanyuka na kurudi upande aliutoka dakika kazaa nyuma.

Burushuti akimfata tu kwa nyuma “Fiyona Gotwa yupo wapi umemuacha wapi “ alivamia mkono ukiwa umeshikilia kitasa baaada ya kuingia Fiyona akageuza shingo yake “Gotwa! Ndio nani?” alihoji Fiyona “Mtoto wa Nkole umemuacha wapi?!... Nakuuliza Fiyona!” alihoji tena Mbonde akimtazama Fiyona aliyebung’aa tu “Mtoto wa Nkole yupi,

Nkole kwani anamtoto?!” Fiyona alisema sasa akisimama katoa macho huku akizivuta kumbukumbu taratibu, Mbonde akimshanga tu “…ina...Ohh! yule ni mtoto wa Nkole!?” “Unashangaza sana wewe, naz utashangaa mengi mwaka huu, ni mtu usiyejali kabisa hisia za mtu mwengine umejawa na ubinafsi tu” Mbonde alisema nakutoka nje mkuku mkuku akimuacha Fiyona njia panda.

Itaendeleaa...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom