Mogambi
JF-Expert Member
- May 25, 2012
- 213
- 357
- Thread starter
- #81
KAZI YA MZUNGU 26
MTUNZI: DAVID NGOCHO SAMSON
Masu alikata tiketi ya ndege siku hiyo. Alijipa moyo kwa ule msemo wa kizungu, usichokiona kwa macho, hakikai akilini. Alijua atamsahau Molio. Asingependa aendelee na kile walichokuwa wamefanya. Hatia ya usaliti ilimgongelea nyundo moyoni.
Jioni, Issa Musa na Yara walirejea. Vifaa walivyodhania kwa zoezi lile walivipata lakini kwa njia za panya. Kifaa muhimu kikiwa kile ambacho kinaweza kusoma ni wapi ilipowekwa chip mwilini na cha pili kikiwa cha kuitia virus ile chip ili isiweze kuitikia maagizo ya kompyuta za ENTRY. Kifaa cha mwisho alitakiwa mtaalamu wa upasuaji. Huyo pia waliambatana naye.
Molio akitaka kumuoneshea Masu kuwa alimaanisha alichosema hapo awali, hakuonesha tabia tofauti na kawaida alipokuwa kaiona toka awasili Oman, alikuwa kando ya Issa Musa akimuonesha mahaba kama ilivyokuwa awali. Na zaidi hakuonesha dalili hata moja ambayo ingeonesha walakini kwa Issa Musa kuwa kuna kitu kikifanyika kisogoni mwake.
Hali hiyo ndio iliyomchanganya zaidi Masu. Mwanamke huyu hakuwa wa kawaida. Hakuonekana hata kidogo kuwa anajutia usaliti uliofanyika. Mbaya zaidi, kwa jinsi alivyokuwa anaonekana, ni kama kweli hakikutokea kitu baina yao. Masu akajiuliza kama Yara naye hangeingizwa kwenye mtego na binti huyo mrembo na mtata. 'Kama Molio ni jasusi, angekuwa jasusi hatari.' Masu alijiwazia mwenyewe. Maana si kwa tabia hiyo aliyoishuhudia. Masu akashukuru vile kesho angeondoka kwenda Zanzibar. Kuendelea kukaa Oman, angejikuta anakosana na Issa Musa. Maana moyoni mwake, Masu alikiri, Molio alikuwa ni mwanamke hatari.
Jioni ya saa mbili, daktari mwenye asili ya kikorea Myung Sun Han, aliwasili Jawhareit apartments. Akapokelewa kwenye apartment ya Issa Musa. Zoezi likaanza.
***
Akiwa maabara ambamo komputa zilizokuwa zinasoma eneo walipo wafanyakazi wa ENTRY popote pale walipo, Philip Mwangaza aligundua kitu kisicho cha kawaida. Alikuwa hasa amezingatia kuangalia mwenendo wa Molio. Alikuwa kwa siku nyingi anamuwazia binti huyo mapenzi. Ilikuwa inamuuma kwamba Molio kwa siku za hivi karibuni, alikuwa halali kabisa kwenye apartment yake iliyopo mtaa wa Al Gawarif bali alionekana kuwa alilala kwenye apartment mbili tofauti pale Jawhareit apartments. Wivu huo na mapenzi kwa mwanamke huyo, yakamfanya Philip kuwa mfuatiliaji sana (stalker) kwa mwanamke huyo.
Mara, akahisi kama kuna kitu ambacho si cha kawaida kimetokea. Akacheki komputa yake vizuri kwa jicho la mshituko lakini likidadisi kwa undani. Je alichokiona kilikuwa sahihi? Au kuna namna usingizi ulimkamata na kumfanya aote kuwa anashuhudia badiliko la ghafla la mahali alikokuwa mrembo huyo.
Philip alivua miwani yake ya macho, akaifuta kwa kitambaa laini. Akaitazama komputa kwa mshituko bayana. Molio alisemekana yuko New York huko Marekani. Dakika kumi kabla hajagundua badiliko hilo, komputa hiyo ilimuonesha kuwa Molio alikuwa Jawhareit apartments, sasa vipi ndani ya dakika kumi tu awe ameondoka Salalah na awe yupo huko Marekani? Philip Mwangaza akalisogelea karo na kuruhusu maji yatiririke kwenye bomba. Akayakinga kwenye viganja vyake hayo maji, akajirushia usoni kama kusudio la kufukuzia usingizi mbali na macho yake. Moyoni mwake akaomba akirejea kwenye komputa, awe sahihi kuwa ilikuwa mawenge yake tu. Na kweli, Philip alipoyarejesha macho yake kwenye skirini, akamuoma Molio akiwa kwenye moja ya apartment za Jawhareit. Akavuta pumzi ndefu ya kutuliza moyo. Molio alikuwa bado ndani ya uangalizi wa ENTRY. Pumzi hiyo aliyovuta ikamkumbusha vile uhai ni muhimu. Maana kupotea kwa mtu wa ENTRY kwa umbali wa New York kutokea Salalah, ingemaanisha kwamba, hawangeweza kumpata kwa urahisi. Ingeingiza ENTRY kwenye gharama za kuwatuma watu wao huko na kama wangelazimika kum-gandisha mtu wao Molio, kumgandisha ilikuwa na maana kwamba walikuwa na uwezo wa kumtia radi kwenye ubongo akawa kama mtu aliyeumwa ghafla, maumivu makali ambayo yasingemruhusu kuendelea na shughuli yoyote popote ambapo angekuwa. Kwa umbali huo, wangekuwa na uwezekano wa kumpoteza jumla. Hakuwa tayari kulishuhudia hilo.
Kitu kimoja hakujua, ile tahadhari ya mwanzo ilikuwa ya muhimu kufanyiwa kazi. Alipoipuuza kama ni wenge lake binafsi alikuwa kafanya kosa kubwa sana.
Asubuhi mapema, Philip Mwangaza alipokeza kijiti usimamizi wa mitambo kwa kijana mwingine asili ya kiarabu, akaondoka zake kupumzika nyumbani.
***
Baada ya kuiona ile chip mwilini mwa Molio, Yara akitumia program zake za ki-Russia, alimudu kuichanganyia habari, akaipa eneo jipya, New York City, ikakubali, sasa ilikuwa inapokea maelekezo toka kwa komputa ya Yaraslav na si kwa komputa za ENTRY. Akaiamrisha isome tena Oman, hapo walipokuwa wao, Jawhareit apartments. Sasa, Daktari Myung Sun Han akamweka Molio kitandani. Operesheni ndogo ya kuichomoa chip ikafanyika. Dakika arobaini na tano zoezi likiwa limekamilika, daktari akafunga mizigo yake na kuondoka zake.
"Free at last." (Huru hatimaye) Molio alitamka kwa furaha. Ingemchukua takribani wiki mbili kuwa sawa kabisa. Teknolojia ya mionzi aliyotumia Daktari Myung Sun Han, haikuacha alama kuonyesha kuna operesheni imefanyika. Ilikuwa teknolojia ya kisasa zaidi. Hangegundulika kabisa kwa muda mrefu, kuwa alikuwa kafanyiwa operesheni. Hakukuwa na dalili ya kovu kwamba mtu huyo kafanyiwa operesheni.
Ile chip sasa ilihifadhiwa kwenye kifaa maalum, ikaprogramiwa upya ili iwe na safari za jijini Salalah, safari zilizotengenezwa kufuatia maelezo ya ratiba za Molio za kila siku. Muda wa kuwepo kazini, kwenda airport kuchukua mizigo (watu). Kwenda sokoni, club, mazoezini, na maeneo mbalimbali aliyokuwa na kawaida ya kwenda mara kwa mara. Zoezi hilo lingeendelea hadi pale ambapo Molio angekuwa keshaondoka Oman na kuishilia zake mbali na mkono wa ENTRY.
Masu jioni hiyo akaaga kwa marafiki zake Issa Musa na Yara, alikuwa aondoke kurejea Zanzibar kesho yake. Wakati akiwaaga wenzake, Molio pia alikuwepo hapo. Akaona ili abaki kwa muda na mwanaume huyo alitakiwa kufanya jambo ambalo lingemlazimu Masu kubakia. Akamweleza Masu hatima ya mwanae kama angesalia mkononi mwa mzee Kisiki.
'Pale alipo mzee Kisiki, ana wake watano. Wote walikuja wakiwa ni wajawazito. Ana kawaida ya kuoa wajawazito. Anafanya hivyo kwa sababu, lengo ni watoto wanaozaliwa na mabinti hao kuwa faida kwa ENTRY. Wakishazaliwa watoto hao, hunyonya kwa mama zao kwa miezi sita, halafu huhamishwa kutoka Oman kwenda Dubai. Huko kuna Lab (maabara) kubwa ambapo watoto hao huwa chini ya uangalizi wa wanasayansi wa ENTRY wakifanyiwa majaribio mbalimbali. Kuna dhana ambayo sijathibitisha kwamba watoto hao hufunzwa kufanya mambo ya kikatili bila hisia, na kwa hatua ya juu zaidi, hutumika kutengenezewa watu wengine. Wanaita clones. Yaani watu ambao hutengenezwa maabara wakiwa wanafanana kwa kila kitu na original wao. ENTRY in mpango mbaya sana na dunia hii Masu. Kwa sababu ENTRY ni sehemu tu ya genge kubwa kabisa duniani ambalo linakusudia kupunguza idadi ya watu duniani kwa njia za kikatili.' Molio alimweleza vizuri kabisa habari hizo Masu mbele ya Issa Musa na Yara. Wote walikuwa kimya wakiwa wamevutika na simulizi hiyo. Molio akaendelea kusimulia.
'Lengo la ENTRY sio zuri kwa sababu, hebu fikiria, wanachukua watoto wadogo miezi sita wanawafanyia majaribio ya kisayansi ili wawe kama silaha. Watoto hao baadaye wanatumika kama vile maroboti kukusanya data kutoka mataifa mbalimbali ambayo ENTRY ina maslahi nazo aidha kwa faida au hasara. Ona kwa mfano, yule binti niliyemchukua leo asubuhi, Anastela Kilapi, wasichana warembo kama yule, huchukuliwa, wakapendezeshwa kwa madawa ya maabara na upasuaji wa kuboresha viungo vya mwili (Plastic surgeries), halafu huchomwa sindano za viruses mbalimbali ili kueneza magonjwa hatari kwa walimwengu. Maana baada ya hapo, warembo hao husambazwa kwenye maeneo mbalimbali ya starehe, vilabu vya usiku, madanguro na kadhalika. Hao wasichana naopokea mimi wanaotoka Afrika Mashariki, yupo mtu mwingine ambaye anapokea wanaotoka Thailand, Singapore, na mataifa ya Asia. Kila eneo, duniani, ENTRY hutafuta vijana na kuwafunza lugha muhimu wanazoona vema ili kuzitumia kuwasiliana kwa ajili ya kazi za ama kusafirisha binadamu au dawa za kulevya. Hayo na mambo mengine kibao, ikiwamo kuwatumia wanasiasa wa mataifa mbalimbali duniani kuruhusu mambo ya hovyo kama biashara ya umalaya, ushoga na hata sera za kuzuia uzazi.
'Unaambiwa wana lengo la kupunguza watu duniani kwa sababu wanaamini kuwa, dunia inapoelekea itaangamizwa na idadi kubwa ya watu wanaozidi kuongezeka kila leo. Wanaamini, ni wajibu wao kuhakikisha dunia inaendelea kuwepo kwa miaka milioni na milioni kwa siku za usoni. Kwa idadi ya watu waliopo duniani, ENTRY wanaamini kuwa huenda miaka mia ijayo ikashuhudia anguko la dunia nzima, watu wakiuana kwa sababu ya njaa, jua kali likangamiza watu baada ya miti kupotea vile matumizi ya mimea yamezidi kuwa makubwa na hovyo. Oxygen itauzwa kwa vile itabaki ya kuzalishwa maabara, baada ya kuteketea miti na oxygen asilia. Kutakuwa hakuna maji fresh maana vyanzo vya maji vitakuwa vimeangamizwa na idadi kubwa ya watu wanaosaka maisha kwa kutegemea kilimo, ujenzi, madini, kazi zote hizo zikihitaji matumizi makubwa ya maliasili na mimea.
Wanaamini idadi kubwa ya watu itahitaji kulishwa, na hivyo wanyama watatumika zaidi kama vitoweo, wakiisha wa kufugwa, wataingia kutafuta wa mwituni, wakimaliza hao, wataanza kukulana wao kwa wao. Wanakadiria kwamba hadi kufikia hapo, binadamu wote watapotea duniani kama walivyopotea dinosaurs wa kipindi cha mamilion ya miaka iliyokwishapita.
'ENTRY, wanaamini namna pekee ya kuhifadhi kizazi cha binadamu, ni kuwa na kiwango fulani cha idadi ya watu duniani, idadi ambayo inaweza kuishi vema bila ya kuhofia raslimali na mahitaji yao kupotea. Idadi hiyo, imekwisha kupita na sasa dunia ina mara sita ya watu wanaostahili kuwepo duniani. ENTRY wanaamini wapo ili binadamu adumu kuwepo. Watu bilioni sita ni ziada ya watu wanaopaswa kuwepo duniani. Hakuna namna zaidi ya kukomesha ukomo wa binadamu isipokuwa kupunguza idadi hiyo kubwa angalau, dunia ibakiwe na watu bilioni moja na nusu hivi. Majaribio yanayofanyika maabara, yanalenga kupunguza uzazi kwa binadamu, kuondoa wasiohitajika kwa maaana jamii ambazo zinachukuliwa kuwa ni less intelligent, (jamii duni kiintelijensia) na jamii hizo ni kama vile waafrika, waaboriginal, watu wa America ya Kusini, baadhi ya jamii za Asia, waarabu na jamii zote zinazoonekana duni. Kigezo wanachotumia kuzitambua jamii hizo ni maendeleo yao na tamaduni zao duni na dhaifu. ENTRY wanaamini kuwa jamii zote zinazoonekana kuwa na imani zaidi kuhusu Mungu au miungu, yaani ambazo culture zao zinaishi kwa kutegemea miungu au Mungu, basi ni jamii duni ambazo zinastahili kuondoka.
'Lakini ajabu ni kuwa lengo sio kuziondoa jamii hizo zote kwa ujumla wao, hapana, kwa sababu ENTRY huamini kuwa, hakuna jamii duniani isiyoamini kwa Mungu au miungu. Hivyo, ENTRY wanachofanya ni kuhakikisha wanatengenza utamaduni mpya unaofanana, ambao hauamini kwenye Imani hizo asilia, isipokuwa kwenye sayansi na uwezo mkubwa wa binadamu. Wao wanaamini kwamba, kuamini kwenye kitu zaidi ya binadamu mwenyewe kujiaminia, ndio kumepelekea dunia kuwa hovyo kwa kutowajibika na kutegemea nguvu ya ziada. Watu wamekaa wakingojea Mungu au miungu iwatendee, na kwa kufanya hivyo wameiacha dunia izidi kuharibika kwa kutowajibika kwao….' Molio aliendelea kusimulia, lakini maelezo hayo yote yalipita sikio la kushoto yakatokea sikio la kulia la Masu, kitu pekee kilichokuwa akilini mwake, ni hiyo habari ya mtoto wake na Mwamvita. Alikuwa anapanga namna ya kumtorosha mwanamke huyo, usiku huo huo, ili aondoke naye kesho yake.
ITAENDELEA.....
MTUNZI: DAVID NGOCHO SAMSON
Masu alikata tiketi ya ndege siku hiyo. Alijipa moyo kwa ule msemo wa kizungu, usichokiona kwa macho, hakikai akilini. Alijua atamsahau Molio. Asingependa aendelee na kile walichokuwa wamefanya. Hatia ya usaliti ilimgongelea nyundo moyoni.
Jioni, Issa Musa na Yara walirejea. Vifaa walivyodhania kwa zoezi lile walivipata lakini kwa njia za panya. Kifaa muhimu kikiwa kile ambacho kinaweza kusoma ni wapi ilipowekwa chip mwilini na cha pili kikiwa cha kuitia virus ile chip ili isiweze kuitikia maagizo ya kompyuta za ENTRY. Kifaa cha mwisho alitakiwa mtaalamu wa upasuaji. Huyo pia waliambatana naye.
Molio akitaka kumuoneshea Masu kuwa alimaanisha alichosema hapo awali, hakuonesha tabia tofauti na kawaida alipokuwa kaiona toka awasili Oman, alikuwa kando ya Issa Musa akimuonesha mahaba kama ilivyokuwa awali. Na zaidi hakuonesha dalili hata moja ambayo ingeonesha walakini kwa Issa Musa kuwa kuna kitu kikifanyika kisogoni mwake.
Hali hiyo ndio iliyomchanganya zaidi Masu. Mwanamke huyu hakuwa wa kawaida. Hakuonekana hata kidogo kuwa anajutia usaliti uliofanyika. Mbaya zaidi, kwa jinsi alivyokuwa anaonekana, ni kama kweli hakikutokea kitu baina yao. Masu akajiuliza kama Yara naye hangeingizwa kwenye mtego na binti huyo mrembo na mtata. 'Kama Molio ni jasusi, angekuwa jasusi hatari.' Masu alijiwazia mwenyewe. Maana si kwa tabia hiyo aliyoishuhudia. Masu akashukuru vile kesho angeondoka kwenda Zanzibar. Kuendelea kukaa Oman, angejikuta anakosana na Issa Musa. Maana moyoni mwake, Masu alikiri, Molio alikuwa ni mwanamke hatari.
Jioni ya saa mbili, daktari mwenye asili ya kikorea Myung Sun Han, aliwasili Jawhareit apartments. Akapokelewa kwenye apartment ya Issa Musa. Zoezi likaanza.
***
Akiwa maabara ambamo komputa zilizokuwa zinasoma eneo walipo wafanyakazi wa ENTRY popote pale walipo, Philip Mwangaza aligundua kitu kisicho cha kawaida. Alikuwa hasa amezingatia kuangalia mwenendo wa Molio. Alikuwa kwa siku nyingi anamuwazia binti huyo mapenzi. Ilikuwa inamuuma kwamba Molio kwa siku za hivi karibuni, alikuwa halali kabisa kwenye apartment yake iliyopo mtaa wa Al Gawarif bali alionekana kuwa alilala kwenye apartment mbili tofauti pale Jawhareit apartments. Wivu huo na mapenzi kwa mwanamke huyo, yakamfanya Philip kuwa mfuatiliaji sana (stalker) kwa mwanamke huyo.
Mara, akahisi kama kuna kitu ambacho si cha kawaida kimetokea. Akacheki komputa yake vizuri kwa jicho la mshituko lakini likidadisi kwa undani. Je alichokiona kilikuwa sahihi? Au kuna namna usingizi ulimkamata na kumfanya aote kuwa anashuhudia badiliko la ghafla la mahali alikokuwa mrembo huyo.
Philip alivua miwani yake ya macho, akaifuta kwa kitambaa laini. Akaitazama komputa kwa mshituko bayana. Molio alisemekana yuko New York huko Marekani. Dakika kumi kabla hajagundua badiliko hilo, komputa hiyo ilimuonesha kuwa Molio alikuwa Jawhareit apartments, sasa vipi ndani ya dakika kumi tu awe ameondoka Salalah na awe yupo huko Marekani? Philip Mwangaza akalisogelea karo na kuruhusu maji yatiririke kwenye bomba. Akayakinga kwenye viganja vyake hayo maji, akajirushia usoni kama kusudio la kufukuzia usingizi mbali na macho yake. Moyoni mwake akaomba akirejea kwenye komputa, awe sahihi kuwa ilikuwa mawenge yake tu. Na kweli, Philip alipoyarejesha macho yake kwenye skirini, akamuoma Molio akiwa kwenye moja ya apartment za Jawhareit. Akavuta pumzi ndefu ya kutuliza moyo. Molio alikuwa bado ndani ya uangalizi wa ENTRY. Pumzi hiyo aliyovuta ikamkumbusha vile uhai ni muhimu. Maana kupotea kwa mtu wa ENTRY kwa umbali wa New York kutokea Salalah, ingemaanisha kwamba, hawangeweza kumpata kwa urahisi. Ingeingiza ENTRY kwenye gharama za kuwatuma watu wao huko na kama wangelazimika kum-gandisha mtu wao Molio, kumgandisha ilikuwa na maana kwamba walikuwa na uwezo wa kumtia radi kwenye ubongo akawa kama mtu aliyeumwa ghafla, maumivu makali ambayo yasingemruhusu kuendelea na shughuli yoyote popote ambapo angekuwa. Kwa umbali huo, wangekuwa na uwezekano wa kumpoteza jumla. Hakuwa tayari kulishuhudia hilo.
Kitu kimoja hakujua, ile tahadhari ya mwanzo ilikuwa ya muhimu kufanyiwa kazi. Alipoipuuza kama ni wenge lake binafsi alikuwa kafanya kosa kubwa sana.
Asubuhi mapema, Philip Mwangaza alipokeza kijiti usimamizi wa mitambo kwa kijana mwingine asili ya kiarabu, akaondoka zake kupumzika nyumbani.
***
Baada ya kuiona ile chip mwilini mwa Molio, Yara akitumia program zake za ki-Russia, alimudu kuichanganyia habari, akaipa eneo jipya, New York City, ikakubali, sasa ilikuwa inapokea maelekezo toka kwa komputa ya Yaraslav na si kwa komputa za ENTRY. Akaiamrisha isome tena Oman, hapo walipokuwa wao, Jawhareit apartments. Sasa, Daktari Myung Sun Han akamweka Molio kitandani. Operesheni ndogo ya kuichomoa chip ikafanyika. Dakika arobaini na tano zoezi likiwa limekamilika, daktari akafunga mizigo yake na kuondoka zake.
"Free at last." (Huru hatimaye) Molio alitamka kwa furaha. Ingemchukua takribani wiki mbili kuwa sawa kabisa. Teknolojia ya mionzi aliyotumia Daktari Myung Sun Han, haikuacha alama kuonyesha kuna operesheni imefanyika. Ilikuwa teknolojia ya kisasa zaidi. Hangegundulika kabisa kwa muda mrefu, kuwa alikuwa kafanyiwa operesheni. Hakukuwa na dalili ya kovu kwamba mtu huyo kafanyiwa operesheni.
Ile chip sasa ilihifadhiwa kwenye kifaa maalum, ikaprogramiwa upya ili iwe na safari za jijini Salalah, safari zilizotengenezwa kufuatia maelezo ya ratiba za Molio za kila siku. Muda wa kuwepo kazini, kwenda airport kuchukua mizigo (watu). Kwenda sokoni, club, mazoezini, na maeneo mbalimbali aliyokuwa na kawaida ya kwenda mara kwa mara. Zoezi hilo lingeendelea hadi pale ambapo Molio angekuwa keshaondoka Oman na kuishilia zake mbali na mkono wa ENTRY.
Masu jioni hiyo akaaga kwa marafiki zake Issa Musa na Yara, alikuwa aondoke kurejea Zanzibar kesho yake. Wakati akiwaaga wenzake, Molio pia alikuwepo hapo. Akaona ili abaki kwa muda na mwanaume huyo alitakiwa kufanya jambo ambalo lingemlazimu Masu kubakia. Akamweleza Masu hatima ya mwanae kama angesalia mkononi mwa mzee Kisiki.
'Pale alipo mzee Kisiki, ana wake watano. Wote walikuja wakiwa ni wajawazito. Ana kawaida ya kuoa wajawazito. Anafanya hivyo kwa sababu, lengo ni watoto wanaozaliwa na mabinti hao kuwa faida kwa ENTRY. Wakishazaliwa watoto hao, hunyonya kwa mama zao kwa miezi sita, halafu huhamishwa kutoka Oman kwenda Dubai. Huko kuna Lab (maabara) kubwa ambapo watoto hao huwa chini ya uangalizi wa wanasayansi wa ENTRY wakifanyiwa majaribio mbalimbali. Kuna dhana ambayo sijathibitisha kwamba watoto hao hufunzwa kufanya mambo ya kikatili bila hisia, na kwa hatua ya juu zaidi, hutumika kutengenezewa watu wengine. Wanaita clones. Yaani watu ambao hutengenezwa maabara wakiwa wanafanana kwa kila kitu na original wao. ENTRY in mpango mbaya sana na dunia hii Masu. Kwa sababu ENTRY ni sehemu tu ya genge kubwa kabisa duniani ambalo linakusudia kupunguza idadi ya watu duniani kwa njia za kikatili.' Molio alimweleza vizuri kabisa habari hizo Masu mbele ya Issa Musa na Yara. Wote walikuwa kimya wakiwa wamevutika na simulizi hiyo. Molio akaendelea kusimulia.
'Lengo la ENTRY sio zuri kwa sababu, hebu fikiria, wanachukua watoto wadogo miezi sita wanawafanyia majaribio ya kisayansi ili wawe kama silaha. Watoto hao baadaye wanatumika kama vile maroboti kukusanya data kutoka mataifa mbalimbali ambayo ENTRY ina maslahi nazo aidha kwa faida au hasara. Ona kwa mfano, yule binti niliyemchukua leo asubuhi, Anastela Kilapi, wasichana warembo kama yule, huchukuliwa, wakapendezeshwa kwa madawa ya maabara na upasuaji wa kuboresha viungo vya mwili (Plastic surgeries), halafu huchomwa sindano za viruses mbalimbali ili kueneza magonjwa hatari kwa walimwengu. Maana baada ya hapo, warembo hao husambazwa kwenye maeneo mbalimbali ya starehe, vilabu vya usiku, madanguro na kadhalika. Hao wasichana naopokea mimi wanaotoka Afrika Mashariki, yupo mtu mwingine ambaye anapokea wanaotoka Thailand, Singapore, na mataifa ya Asia. Kila eneo, duniani, ENTRY hutafuta vijana na kuwafunza lugha muhimu wanazoona vema ili kuzitumia kuwasiliana kwa ajili ya kazi za ama kusafirisha binadamu au dawa za kulevya. Hayo na mambo mengine kibao, ikiwamo kuwatumia wanasiasa wa mataifa mbalimbali duniani kuruhusu mambo ya hovyo kama biashara ya umalaya, ushoga na hata sera za kuzuia uzazi.
'Unaambiwa wana lengo la kupunguza watu duniani kwa sababu wanaamini kuwa, dunia inapoelekea itaangamizwa na idadi kubwa ya watu wanaozidi kuongezeka kila leo. Wanaamini, ni wajibu wao kuhakikisha dunia inaendelea kuwepo kwa miaka milioni na milioni kwa siku za usoni. Kwa idadi ya watu waliopo duniani, ENTRY wanaamini kuwa huenda miaka mia ijayo ikashuhudia anguko la dunia nzima, watu wakiuana kwa sababu ya njaa, jua kali likangamiza watu baada ya miti kupotea vile matumizi ya mimea yamezidi kuwa makubwa na hovyo. Oxygen itauzwa kwa vile itabaki ya kuzalishwa maabara, baada ya kuteketea miti na oxygen asilia. Kutakuwa hakuna maji fresh maana vyanzo vya maji vitakuwa vimeangamizwa na idadi kubwa ya watu wanaosaka maisha kwa kutegemea kilimo, ujenzi, madini, kazi zote hizo zikihitaji matumizi makubwa ya maliasili na mimea.
Wanaamini idadi kubwa ya watu itahitaji kulishwa, na hivyo wanyama watatumika zaidi kama vitoweo, wakiisha wa kufugwa, wataingia kutafuta wa mwituni, wakimaliza hao, wataanza kukulana wao kwa wao. Wanakadiria kwamba hadi kufikia hapo, binadamu wote watapotea duniani kama walivyopotea dinosaurs wa kipindi cha mamilion ya miaka iliyokwishapita.
'ENTRY, wanaamini namna pekee ya kuhifadhi kizazi cha binadamu, ni kuwa na kiwango fulani cha idadi ya watu duniani, idadi ambayo inaweza kuishi vema bila ya kuhofia raslimali na mahitaji yao kupotea. Idadi hiyo, imekwisha kupita na sasa dunia ina mara sita ya watu wanaostahili kuwepo duniani. ENTRY wanaamini wapo ili binadamu adumu kuwepo. Watu bilioni sita ni ziada ya watu wanaopaswa kuwepo duniani. Hakuna namna zaidi ya kukomesha ukomo wa binadamu isipokuwa kupunguza idadi hiyo kubwa angalau, dunia ibakiwe na watu bilioni moja na nusu hivi. Majaribio yanayofanyika maabara, yanalenga kupunguza uzazi kwa binadamu, kuondoa wasiohitajika kwa maaana jamii ambazo zinachukuliwa kuwa ni less intelligent, (jamii duni kiintelijensia) na jamii hizo ni kama vile waafrika, waaboriginal, watu wa America ya Kusini, baadhi ya jamii za Asia, waarabu na jamii zote zinazoonekana duni. Kigezo wanachotumia kuzitambua jamii hizo ni maendeleo yao na tamaduni zao duni na dhaifu. ENTRY wanaamini kuwa jamii zote zinazoonekana kuwa na imani zaidi kuhusu Mungu au miungu, yaani ambazo culture zao zinaishi kwa kutegemea miungu au Mungu, basi ni jamii duni ambazo zinastahili kuondoka.
'Lakini ajabu ni kuwa lengo sio kuziondoa jamii hizo zote kwa ujumla wao, hapana, kwa sababu ENTRY huamini kuwa, hakuna jamii duniani isiyoamini kwa Mungu au miungu. Hivyo, ENTRY wanachofanya ni kuhakikisha wanatengenza utamaduni mpya unaofanana, ambao hauamini kwenye Imani hizo asilia, isipokuwa kwenye sayansi na uwezo mkubwa wa binadamu. Wao wanaamini kwamba, kuamini kwenye kitu zaidi ya binadamu mwenyewe kujiaminia, ndio kumepelekea dunia kuwa hovyo kwa kutowajibika na kutegemea nguvu ya ziada. Watu wamekaa wakingojea Mungu au miungu iwatendee, na kwa kufanya hivyo wameiacha dunia izidi kuharibika kwa kutowajibika kwao….' Molio aliendelea kusimulia, lakini maelezo hayo yote yalipita sikio la kushoto yakatokea sikio la kulia la Masu, kitu pekee kilichokuwa akilini mwake, ni hiyo habari ya mtoto wake na Mwamvita. Alikuwa anapanga namna ya kumtorosha mwanamke huyo, usiku huo huo, ili aondoke naye kesho yake.
ITAENDELEA.....