Mogambi
JF-Expert Member
- May 25, 2012
- 213
- 357
- Thread starter
- #21
KAZI YA MZUNGU 13
DAVID NGOCHO SAMSON
#TULIPOISHIA
'Hilo la kheri sheikh wangu, SI vema kuendelea kumweka hapa shughuli zake zikiendelea kulala. Ila hapo utachangia shilingi elfu hamsini TU, kufidia usumbufu uliojitokeza kwa jeshi la polisi'
'Hamna tabu, wacha tulimalize hili.' sheikh Abuubakr akatamka akijua wazi ile Ilikuwa hongo. Lakini yeye hakuona Hilo, alijua baadhi ya watumishi wa jeshi la polisi kwa hongo Ni chuma kwa sumaku, na hapa alikuwa anakimbizana na muda! Wapenda haki walimpa muda mahsusi kutekeleza Rai yao.
KAZI YA MZUNGU 13
Million 75 kwa kila mmoja wao, Ilikuwa Ni hela kubwa. Nzinyangwa alijua ingekuwa rahisi kuwakamata wezi wake. Alikadiria kwamba, wezi wake wangeonesha umwamba, kutumia isivyo Kawaida. Anasa kwa wingi. Akawapanga vijana wake kuzungukia maeneo ya starehe kuangalia watu ambao wangekuwa na matumizi yasiyo ya Kawaida. Hiyo ingekuwa Kweli kama Masu na Yusuf wangekuwa waswahili, kwani waswahili huamini maskini akipata sijui nini hulia mbwata. Alipoteza muda.
Masu na Yusuf walikuwa na Wazo tofauti. Walikubaliana kuhifadhi zile fedha na kutulizana kwanza. Waliwaza kuwa kutumia pesa isivyo Kawaida yao, ingevutia nzi Kama inavyokuwa kwa mizoga. Kila mmoja akaichimbia alikoona Salama. Hawakuzihifadhi benki. Kama kazi ya Mzungu ingeonekana namna gani, walikusudia kuondoka Zanzibar na kuanzisha biashara au kuwekeza fedha zao kwenye makampuni makubwa kwa mtindo wa kununua hisa au hatifungani. Nzinyangwa asingewapata.
Mara baada ya kuachiliwa huru, Bakari aliona Zanzibar kunamwekea usiku. Rafikize walipompatia Kiasi kile Cha fedha, aliondoka Zanzibar na kurejea kwao Iringa. Fedha ile akaitumia kununua mashamba yenye miti izalishayo mbao, Cyprus na pines. Kiasi Kidogo akaanzisha biashara ya duka la jumla. Mungu akaibariki kazi yake mpya. Akafanikiwa sana. Miaka mitano mbeleni, Bakari, ambaye Sasa alijulikana kwa jina lake halisi Paulo, alikadiria kwamba angepata mamilioni ya fedha kwa kuchana na kuuza mbao kwa ile miti yake.
***
Siku moja baada ya kuachiwa kwa Bakari, Masu na Yusuf waliomba kikao na sheikh Abuubakr. Sheikh Abuubakr akawakaribisha nyumbani, wakawa wameketi wanakunywa ghahawa. Masu alikusudia kumweleza sheikh Abuubakr, kuwa kusudio la safari yao hapo Nyumbani, Ilikuwa kuutaka mkono wa bintiye Mwamvita kwenye ndoa tukufu.
'Sheikh, sisi Ni vijana wako, tupo hapa kwa sababu tunahitaji kuzungumza nawe.. Mimi naitwa Yusuf, na huyu mwenzangu anaitwa….'
'Naitwa Masuke Masuke mzee wangu!' Masu alidakia kabla Yusuf hajamalizia kumtambulisha. Lafudhi yake ya bara ikimtambulisha vilivyo kuwa yeye Ni mtu kutoka bara. Akaunyoosha mkono wake amsalimie sheikh Abuubakr. Ah wapi!? Sheikh Abuubakr aliposikia jina Hilo, kumbu kumbu yake ikamtendea haki. Ikamweleza kuwa mkewe mama Mwamvita akikwishamwelezea hofu yake kuwa Masu alihusika na mimba ya binti yao. Haikuwa kitambo, Ilikuwa usiku wa Jana baada ya kumweleza habari za Bakari. Aliyakumbuka vema Maelezo ya mkewe.
'Mume wangu, Kama ulosema Ni sahihi, Basi mie namhisi kijana mmoja, rafikiye huyo Bakari, kuwa ndiye mhusika wa hiyo mimba. Aitwa Masu. Nasema hivyo kwa sababu, huyo kijana alikuwa na mazoea ya kuniita mamkwe, na si mara moja alipomwita Mwamvita Malkia nikaliona huba machoni mwa binti yetu kwa kijana huyo. Sikutilia maanani kwa sababu kijana mwenyewe alikuwa mwadilifu sana, ila alipotoweka ghafla, Hakuna alojua kendaapi, zikavuma habari alitekwa na wasiojulikana! Hivi unapoongea habari za Bakari, ndio umenifanya niliwaze hili.'
Hasira zikamvaa sheikh Abuubakr, akaona kijana huyo alikuwa analeta dhihaka. Akanyanyua bakora yake amtandike nayo kijana huyo. Mara akaisikia sauti ya mkewe.
'Sheikh Abuubakr mume wangu.' sheikh Abuubakr akaishusha chini bakora yake.
Busara yake ikamshawishi kutuliza hasira na kuwasikiliza hao wageni wake.
'Enhee, mwasemaje vijana?' akauliza, macho kayatua barabara usoni mwake Masu.
Huenda akawa SI huyu, maana Masuke aliyenieleza mke wangu alikuwa mlalahoi, mla kwa jasho litokanalo na kusukuma guta na mikokoteni, akajiwazia Sheikh Abuubakr. Alimtazama kijana huyo, akajaribu kutafuta hiyo hadhi ya msukuma mikokoteni asiione. Huyu.., ah! huyu alionekana kuwa mtumishi wa serikali, kitengo nyeti chenye kucheua marupurupu na mshahara mnono bila shaka. Masuke alikuwa katinga suti Safi ya hudhurungi. Nywele zake nyeusi zilichanwa Vema na kungara kwa mafuta ghali ya nywele. Mguuni alitinga moka safi, Loh, hakuvaa soksi. 'Vijana wa siku hizi!' akawaza Sheikh Abuubakr. 'Hawafanyi kitu kikamilike wasikitie doa, kapendeza lakini kaharibia hapo tu, mbona asivae soksi?' akaendelea kujiuliza.
'Eeh, mzee tumekuja na kijizawadi Kidogo. Tunaomba ukipokee kabla hatujaeleza dhumuni la ujio wetu.' Yusuf akazungumza, Huku Masu akitoa bahasha na kumkabidhi mzee huyo. Sheikh akaipokea zawadi. Akachungulia ndani na kuona burungutu la fedha.
'Nyie vijana Ni Nani? Mnataka Nini? Hii maana yake Nini?' Sheikh akalipuka kwa hasira.
'Tumekuja kuomba radhi kwa usumbufu tulokusababishia. Tunajua Kuna namna tumekufanya uwe na hasira na hata kufikiria vibaya. Kama nilivyojitambulisha awali, Mimi naitwa Masuke. Mimi ndio mhusika wa mimba ya Mwamvita.' Masuke akajieleza. Safari hii akachezea bakora.
'Wapuuzi Sana nyie watoto, kwa hiyo mmeona mlete dhihaka hapa, sivyo?' Sheikh alikuwa kasimama Sasa. Amefura kwa hasira!
'Hapana mzee, Tumekuja kwa Nia njema TU. Tunatakutaka radhi na pia tunaomba ruhusa ya kumuoa binti yako Mwamvita.' Yusuf akaingilia Kati.
'Mmeona haitoshi kumtia mimba Mwanafunzi Sasa Unataka kunihonga Mimi nishiriki makosa yako? Jela ndiko kunakokufaa. Mjinga mmoja wewe?' sheikh Abuubakr alikuwa mbogo.
Mwamvita alikuwa chumbani kwake. Uzuri wa chumba chake, dirisha lake lilitazama hapo walipokaa Masu, Yusuf na wazazi wake, Chini ya mnazi. Alishuhudia harakati zile zilizokuwa zinaendelea. Masu alivyokula bakora, Mwamvita uvumilivu ukamshinda, Heri hizo bakora azipate yeye pia. Akatoka ndani akilia.
'Mimi ndiyo nastahili hizo bakora baba, Mimi ndio nikiyekufedhehesha. Sikumpa nafasi Masu kufanya maamuzi Sawa, Mimi ndio niliyemfuata kwake na kusababisha hii Hali. Kama Ni adhabu nastahili Mimi. La sivyo, nakuomba baba, tafadhali tusamehe. Yalikwisha tokea ya kutokea, tusamehe baba, tunahitaji baraka zako tuanze familia.'
'Sheikh Abuubakr mume wangu. Hebu punguza jaziba baba watoto. Wasikilize watoto. Wameonesha kujutia makosa yao, wape nafasi ya kujisahihisha tafadhali!' mama Mwamvita akaongea kwa hekima kubwa. Sheikh Abuubakr yakamwingia Hayo maneno. Mara nyingi, sauti ya mkewe Ilikuwa na athari kwenye moyo wake. Tangu alipomuoa, sauti yake Ilikuwa sauti iliyompa tumaini na kumpitisha kwenye changamoto. Aliiheshimu sauti hiyo. Akatuliza munkari. Akapumua Vema. Akapata kufikiri Vema bila ushawishi wa hasira.
'Hamna wazazi nyie?' lilikuwa swali la msingi.
Swali ambalo huenda vijana hao hawakulitarajia.
Wakabaki wanatazamana.
'Kama lengo Ni kuleta barua ya posa, nyie hamjui taratibu?' akaongezea Tena Sheikh Abuubakr.
'Ah, mzee wangu Hilo litafuata hivi punde. Sisi tulitaka tu tuweke Mambo sawa kabla ya kuanza hatua rasmi za taratibu za kuoa. Tumekuja kwa lengo la kukutaka radhi.'
Sheikh Abuubakr akarudisha moyo wa imani.
'Mama Mwamvita mke wangu, hebu kawaandalie chakula wageni wetu.'
'Rabeka mume wangu, naenda Sasa hivi. Haya, amka twende mama!' mama Mwamvita akazungumza huku akimwashiria Mwamvita kuongozana naye. Nyuso zao ziling'ara kwa tabasamu. Mwamvita alifurahi mno!
'Enhee, Sasa naweza kuwasikiliza. Jitambulisheni Tena tufahamiane vizuri. Hivoo, umesema wewe wafanya kazi gani?' Sheikh akauliza. Alikuwa akitafakari habari kwamba, kijana huyo alotaka kumuoa bintiye Ni mbeba mizigo. Akatafakari pia juu ya yule mzee aliyeonesha Nia ya kutaka kumuoa binti yake, aluwatani Kisiki.
Mzee Kisiki alijulikana Sana hapo mtaani. Mwanajeshi mstaafu aliyetukuka kwa sifa kibao, ikiwamo ile ya kuongoza kikosi kilichofanikisha kurejesha amani visiwani Comoro. Mzee huyu, alikuwa na jumla ya wake nane, hivyo Ni kusema Mwamvita angefikisha namba Tisa. Kilichomfanya mzee Kisiki amudu kuwa na wake wengi hivyo Ni uchumi wake mzuri. Alikuwa Ni miongoni mwa watu wenye hisa nyingi kwenye makampuni makubwa anuai hapo Zanzibar na kule bara. Mahotel ya nyota tatu Hadi tano, mzee alikuwa na mkono wake ndani. Alitumia Vema nafasi yake ya ukubwa jeshini wakati wake, kuwekeza.
Sheikh Abuubakr alitafakari Sana. Moyo wa bintiye ulikuwa umemwangukia mhuni, msukuma guta.. angeishi maisha hovyo Sana ya kimaskini kwa kuambatana na kijana huyo. Wakeze Kisiki walikula maisha, wengi aliwaoa TU ili kuwanusuru. Alifanya Kama kuoa Ni sadaka kuwasaidia wanawake waliokimbiwa na kuachiwa mimba, ama kutelekezwa na watoto wao. Hao ndio wakeze Kisiki. Aliwachukua hao, akawapatia maisha, kila mmoja akawa na uhakika wa kuingiza kipato. Akawafungulia miradi wasimamie. Hata ikawa kila mkewe, aliweza kula na kulala pazuri, kusomesha watoto kwenye skuli za kufunza kwa kiingereza, na wote waliendesha magari kwa ufahari. Huyo ndiyo mtu alotaka achukue dhamana ya bintiye. SI mhuni mmoja kutoka bara!
Sasa akabaki yuajiuliza, namna gani bintiye alichagua mtu lofa, avujaye jasho kupata' mkate usotosha hata kusaza? Sheikh Abuubakr akajikuta kwenye mtihani mgumu. Akatega sikio amsikilize kijana huyo, huenda akabaini hicho kilichomfanya bintiye azuzuke. SI Ni Kweli kwamba wapo maskini wa Mali lakini wakawa matajiri wa busara? Alitafakari..
Masuke moyo ukamlipuka kwa furaha, akaweka tabasamu usoni kwake na kuanza kujieleza, tayari alikwisha hisi ushindi Unamnyemelea! Akajikohoza Kidogo na kulegeza Kidogo tai yake, akaweka pozi la ushindi.
'Ah, mzee wangu Mimi naitwa Masuke Masuke, Ni mzaliwa wa kijijini Malonje mkoani Morogoro. Kwa Zanzibar, huu Ni mwaka wa pili Sasa tangu nilipokuja Huku, SI haba, mwenyezi Mungu aliniangazia Nuru zake tangu nakanyaga hapa, akanibariki kupata' kipato changu Kidogo lakini halali, kwa kujituma kutumia mikono na nguvu zangu. Nimekuwa nafanya kazi ya kubeba mizigo lakini kwa Sasa natarajia kuanza kazi yangu mpya mwezi ujao, kwenye Hotel moja ya Mzungu hapa hapa kisiwani. Itakuwa kazi yenye maslahi mazuri na nakuahidi binti yako atakuwa kwenye mikono Salama, inshallah, kwa uwezo wa Mungu. Huyu mwenzangu Ni rafiki yangu ambaye tumekuwa tukifanya naye kazi pamoja'. Masuke alijieleza kwa ufahari.
Mzee Abuubakr alimtazama kijana huyo akakosa tumaini. Suti hii ya gharama, Kumbe kapewa na Mzungu kwa ajili ya kazi ya uhudumu hotelini. Eti maslahi mazuri, kwa kazi gani? Kwa mtu alozoea kupewa Mia tano miambili akfu moja, kazi nzuri itakuwa ya shilingi ngapi? Laki moja kwa mwezi? Sheikh Abuubakr akamdharau Sana kijana. Hata hivyo hakutaka kuonesha Hali hiyo. Wakaendelea kupiga soga, chakula kikaletwa wakala na hatimaye wakaagana.
'Kumbuka kunisalimia wazazi wenzangu huko. Bila shaka tunawatarajia kwa ajili ya kukamilisha Taratibu hizi. Muhimu wakinipa taarifa mapema juu ya ujio wao.' Sheikh Abuubakr akachombeza.
Masu na Yusuf wakaondoka wakiwa na nyuso za furaha. Mwamvita furaha yake ndio kabisa, Ilikuwa haisimuliki.
***
'Naam Sheikh, …… nakupata vizuri Sheikh……. Hewalaa sheikh wangu. Sasa, Mimi Nina mpango maalumu wa kutatua Hilo tatizo, Wala lisikusumbue Hilo, sisi watu wazima bwana, watoto hawawezi kutuzingua kabisa. Unaonaje tuonane baada ya swala ya jioni nikushirikishe mpango huo?' Ilikuwa sauti ya mzee Kisiki!
'Naam, nitafanya hivyo!'
Jioni ya siku hiyo iliwakutanisha mzee Kisiki na sheikh Abuubakr. Wakazungumza mengi. Alipotoka hapo, Sheikh Abuubakr alikuwa na jibu dhidi ya suala la bintiye. Katu hangeridhia fukara msukuma mikokoteni ayaharibu maisha ya bintiye
2020
David Samson Ngocho
Sent using Jamii Forums mobile app
DAVID NGOCHO SAMSON
#TULIPOISHIA
'Hilo la kheri sheikh wangu, SI vema kuendelea kumweka hapa shughuli zake zikiendelea kulala. Ila hapo utachangia shilingi elfu hamsini TU, kufidia usumbufu uliojitokeza kwa jeshi la polisi'
'Hamna tabu, wacha tulimalize hili.' sheikh Abuubakr akatamka akijua wazi ile Ilikuwa hongo. Lakini yeye hakuona Hilo, alijua baadhi ya watumishi wa jeshi la polisi kwa hongo Ni chuma kwa sumaku, na hapa alikuwa anakimbizana na muda! Wapenda haki walimpa muda mahsusi kutekeleza Rai yao.
KAZI YA MZUNGU 13
Million 75 kwa kila mmoja wao, Ilikuwa Ni hela kubwa. Nzinyangwa alijua ingekuwa rahisi kuwakamata wezi wake. Alikadiria kwamba, wezi wake wangeonesha umwamba, kutumia isivyo Kawaida. Anasa kwa wingi. Akawapanga vijana wake kuzungukia maeneo ya starehe kuangalia watu ambao wangekuwa na matumizi yasiyo ya Kawaida. Hiyo ingekuwa Kweli kama Masu na Yusuf wangekuwa waswahili, kwani waswahili huamini maskini akipata sijui nini hulia mbwata. Alipoteza muda.
Masu na Yusuf walikuwa na Wazo tofauti. Walikubaliana kuhifadhi zile fedha na kutulizana kwanza. Waliwaza kuwa kutumia pesa isivyo Kawaida yao, ingevutia nzi Kama inavyokuwa kwa mizoga. Kila mmoja akaichimbia alikoona Salama. Hawakuzihifadhi benki. Kama kazi ya Mzungu ingeonekana namna gani, walikusudia kuondoka Zanzibar na kuanzisha biashara au kuwekeza fedha zao kwenye makampuni makubwa kwa mtindo wa kununua hisa au hatifungani. Nzinyangwa asingewapata.
Mara baada ya kuachiliwa huru, Bakari aliona Zanzibar kunamwekea usiku. Rafikize walipompatia Kiasi kile Cha fedha, aliondoka Zanzibar na kurejea kwao Iringa. Fedha ile akaitumia kununua mashamba yenye miti izalishayo mbao, Cyprus na pines. Kiasi Kidogo akaanzisha biashara ya duka la jumla. Mungu akaibariki kazi yake mpya. Akafanikiwa sana. Miaka mitano mbeleni, Bakari, ambaye Sasa alijulikana kwa jina lake halisi Paulo, alikadiria kwamba angepata mamilioni ya fedha kwa kuchana na kuuza mbao kwa ile miti yake.
***
Siku moja baada ya kuachiwa kwa Bakari, Masu na Yusuf waliomba kikao na sheikh Abuubakr. Sheikh Abuubakr akawakaribisha nyumbani, wakawa wameketi wanakunywa ghahawa. Masu alikusudia kumweleza sheikh Abuubakr, kuwa kusudio la safari yao hapo Nyumbani, Ilikuwa kuutaka mkono wa bintiye Mwamvita kwenye ndoa tukufu.
'Sheikh, sisi Ni vijana wako, tupo hapa kwa sababu tunahitaji kuzungumza nawe.. Mimi naitwa Yusuf, na huyu mwenzangu anaitwa….'
'Naitwa Masuke Masuke mzee wangu!' Masu alidakia kabla Yusuf hajamalizia kumtambulisha. Lafudhi yake ya bara ikimtambulisha vilivyo kuwa yeye Ni mtu kutoka bara. Akaunyoosha mkono wake amsalimie sheikh Abuubakr. Ah wapi!? Sheikh Abuubakr aliposikia jina Hilo, kumbu kumbu yake ikamtendea haki. Ikamweleza kuwa mkewe mama Mwamvita akikwishamwelezea hofu yake kuwa Masu alihusika na mimba ya binti yao. Haikuwa kitambo, Ilikuwa usiku wa Jana baada ya kumweleza habari za Bakari. Aliyakumbuka vema Maelezo ya mkewe.
'Mume wangu, Kama ulosema Ni sahihi, Basi mie namhisi kijana mmoja, rafikiye huyo Bakari, kuwa ndiye mhusika wa hiyo mimba. Aitwa Masu. Nasema hivyo kwa sababu, huyo kijana alikuwa na mazoea ya kuniita mamkwe, na si mara moja alipomwita Mwamvita Malkia nikaliona huba machoni mwa binti yetu kwa kijana huyo. Sikutilia maanani kwa sababu kijana mwenyewe alikuwa mwadilifu sana, ila alipotoweka ghafla, Hakuna alojua kendaapi, zikavuma habari alitekwa na wasiojulikana! Hivi unapoongea habari za Bakari, ndio umenifanya niliwaze hili.'
Hasira zikamvaa sheikh Abuubakr, akaona kijana huyo alikuwa analeta dhihaka. Akanyanyua bakora yake amtandike nayo kijana huyo. Mara akaisikia sauti ya mkewe.
'Sheikh Abuubakr mume wangu.' sheikh Abuubakr akaishusha chini bakora yake.
Busara yake ikamshawishi kutuliza hasira na kuwasikiliza hao wageni wake.
'Enhee, mwasemaje vijana?' akauliza, macho kayatua barabara usoni mwake Masu.
Huenda akawa SI huyu, maana Masuke aliyenieleza mke wangu alikuwa mlalahoi, mla kwa jasho litokanalo na kusukuma guta na mikokoteni, akajiwazia Sheikh Abuubakr. Alimtazama kijana huyo, akajaribu kutafuta hiyo hadhi ya msukuma mikokoteni asiione. Huyu.., ah! huyu alionekana kuwa mtumishi wa serikali, kitengo nyeti chenye kucheua marupurupu na mshahara mnono bila shaka. Masuke alikuwa katinga suti Safi ya hudhurungi. Nywele zake nyeusi zilichanwa Vema na kungara kwa mafuta ghali ya nywele. Mguuni alitinga moka safi, Loh, hakuvaa soksi. 'Vijana wa siku hizi!' akawaza Sheikh Abuubakr. 'Hawafanyi kitu kikamilike wasikitie doa, kapendeza lakini kaharibia hapo tu, mbona asivae soksi?' akaendelea kujiuliza.
'Eeh, mzee tumekuja na kijizawadi Kidogo. Tunaomba ukipokee kabla hatujaeleza dhumuni la ujio wetu.' Yusuf akazungumza, Huku Masu akitoa bahasha na kumkabidhi mzee huyo. Sheikh akaipokea zawadi. Akachungulia ndani na kuona burungutu la fedha.
'Nyie vijana Ni Nani? Mnataka Nini? Hii maana yake Nini?' Sheikh akalipuka kwa hasira.
'Tumekuja kuomba radhi kwa usumbufu tulokusababishia. Tunajua Kuna namna tumekufanya uwe na hasira na hata kufikiria vibaya. Kama nilivyojitambulisha awali, Mimi naitwa Masuke. Mimi ndio mhusika wa mimba ya Mwamvita.' Masuke akajieleza. Safari hii akachezea bakora.
'Wapuuzi Sana nyie watoto, kwa hiyo mmeona mlete dhihaka hapa, sivyo?' Sheikh alikuwa kasimama Sasa. Amefura kwa hasira!
'Hapana mzee, Tumekuja kwa Nia njema TU. Tunatakutaka radhi na pia tunaomba ruhusa ya kumuoa binti yako Mwamvita.' Yusuf akaingilia Kati.
'Mmeona haitoshi kumtia mimba Mwanafunzi Sasa Unataka kunihonga Mimi nishiriki makosa yako? Jela ndiko kunakokufaa. Mjinga mmoja wewe?' sheikh Abuubakr alikuwa mbogo.
Mwamvita alikuwa chumbani kwake. Uzuri wa chumba chake, dirisha lake lilitazama hapo walipokaa Masu, Yusuf na wazazi wake, Chini ya mnazi. Alishuhudia harakati zile zilizokuwa zinaendelea. Masu alivyokula bakora, Mwamvita uvumilivu ukamshinda, Heri hizo bakora azipate yeye pia. Akatoka ndani akilia.
'Mimi ndiyo nastahili hizo bakora baba, Mimi ndio nikiyekufedhehesha. Sikumpa nafasi Masu kufanya maamuzi Sawa, Mimi ndio niliyemfuata kwake na kusababisha hii Hali. Kama Ni adhabu nastahili Mimi. La sivyo, nakuomba baba, tafadhali tusamehe. Yalikwisha tokea ya kutokea, tusamehe baba, tunahitaji baraka zako tuanze familia.'
'Sheikh Abuubakr mume wangu. Hebu punguza jaziba baba watoto. Wasikilize watoto. Wameonesha kujutia makosa yao, wape nafasi ya kujisahihisha tafadhali!' mama Mwamvita akaongea kwa hekima kubwa. Sheikh Abuubakr yakamwingia Hayo maneno. Mara nyingi, sauti ya mkewe Ilikuwa na athari kwenye moyo wake. Tangu alipomuoa, sauti yake Ilikuwa sauti iliyompa tumaini na kumpitisha kwenye changamoto. Aliiheshimu sauti hiyo. Akatuliza munkari. Akapumua Vema. Akapata kufikiri Vema bila ushawishi wa hasira.
'Hamna wazazi nyie?' lilikuwa swali la msingi.
Swali ambalo huenda vijana hao hawakulitarajia.
Wakabaki wanatazamana.
'Kama lengo Ni kuleta barua ya posa, nyie hamjui taratibu?' akaongezea Tena Sheikh Abuubakr.
'Ah, mzee wangu Hilo litafuata hivi punde. Sisi tulitaka tu tuweke Mambo sawa kabla ya kuanza hatua rasmi za taratibu za kuoa. Tumekuja kwa lengo la kukutaka radhi.'
Sheikh Abuubakr akarudisha moyo wa imani.
'Mama Mwamvita mke wangu, hebu kawaandalie chakula wageni wetu.'
'Rabeka mume wangu, naenda Sasa hivi. Haya, amka twende mama!' mama Mwamvita akazungumza huku akimwashiria Mwamvita kuongozana naye. Nyuso zao ziling'ara kwa tabasamu. Mwamvita alifurahi mno!
'Enhee, Sasa naweza kuwasikiliza. Jitambulisheni Tena tufahamiane vizuri. Hivoo, umesema wewe wafanya kazi gani?' Sheikh akauliza. Alikuwa akitafakari habari kwamba, kijana huyo alotaka kumuoa bintiye Ni mbeba mizigo. Akatafakari pia juu ya yule mzee aliyeonesha Nia ya kutaka kumuoa binti yake, aluwatani Kisiki.
Mzee Kisiki alijulikana Sana hapo mtaani. Mwanajeshi mstaafu aliyetukuka kwa sifa kibao, ikiwamo ile ya kuongoza kikosi kilichofanikisha kurejesha amani visiwani Comoro. Mzee huyu, alikuwa na jumla ya wake nane, hivyo Ni kusema Mwamvita angefikisha namba Tisa. Kilichomfanya mzee Kisiki amudu kuwa na wake wengi hivyo Ni uchumi wake mzuri. Alikuwa Ni miongoni mwa watu wenye hisa nyingi kwenye makampuni makubwa anuai hapo Zanzibar na kule bara. Mahotel ya nyota tatu Hadi tano, mzee alikuwa na mkono wake ndani. Alitumia Vema nafasi yake ya ukubwa jeshini wakati wake, kuwekeza.
Sheikh Abuubakr alitafakari Sana. Moyo wa bintiye ulikuwa umemwangukia mhuni, msukuma guta.. angeishi maisha hovyo Sana ya kimaskini kwa kuambatana na kijana huyo. Wakeze Kisiki walikula maisha, wengi aliwaoa TU ili kuwanusuru. Alifanya Kama kuoa Ni sadaka kuwasaidia wanawake waliokimbiwa na kuachiwa mimba, ama kutelekezwa na watoto wao. Hao ndio wakeze Kisiki. Aliwachukua hao, akawapatia maisha, kila mmoja akawa na uhakika wa kuingiza kipato. Akawafungulia miradi wasimamie. Hata ikawa kila mkewe, aliweza kula na kulala pazuri, kusomesha watoto kwenye skuli za kufunza kwa kiingereza, na wote waliendesha magari kwa ufahari. Huyo ndiyo mtu alotaka achukue dhamana ya bintiye. SI mhuni mmoja kutoka bara!
Sasa akabaki yuajiuliza, namna gani bintiye alichagua mtu lofa, avujaye jasho kupata' mkate usotosha hata kusaza? Sheikh Abuubakr akajikuta kwenye mtihani mgumu. Akatega sikio amsikilize kijana huyo, huenda akabaini hicho kilichomfanya bintiye azuzuke. SI Ni Kweli kwamba wapo maskini wa Mali lakini wakawa matajiri wa busara? Alitafakari..
Masuke moyo ukamlipuka kwa furaha, akaweka tabasamu usoni kwake na kuanza kujieleza, tayari alikwisha hisi ushindi Unamnyemelea! Akajikohoza Kidogo na kulegeza Kidogo tai yake, akaweka pozi la ushindi.
'Ah, mzee wangu Mimi naitwa Masuke Masuke, Ni mzaliwa wa kijijini Malonje mkoani Morogoro. Kwa Zanzibar, huu Ni mwaka wa pili Sasa tangu nilipokuja Huku, SI haba, mwenyezi Mungu aliniangazia Nuru zake tangu nakanyaga hapa, akanibariki kupata' kipato changu Kidogo lakini halali, kwa kujituma kutumia mikono na nguvu zangu. Nimekuwa nafanya kazi ya kubeba mizigo lakini kwa Sasa natarajia kuanza kazi yangu mpya mwezi ujao, kwenye Hotel moja ya Mzungu hapa hapa kisiwani. Itakuwa kazi yenye maslahi mazuri na nakuahidi binti yako atakuwa kwenye mikono Salama, inshallah, kwa uwezo wa Mungu. Huyu mwenzangu Ni rafiki yangu ambaye tumekuwa tukifanya naye kazi pamoja'. Masuke alijieleza kwa ufahari.
Mzee Abuubakr alimtazama kijana huyo akakosa tumaini. Suti hii ya gharama, Kumbe kapewa na Mzungu kwa ajili ya kazi ya uhudumu hotelini. Eti maslahi mazuri, kwa kazi gani? Kwa mtu alozoea kupewa Mia tano miambili akfu moja, kazi nzuri itakuwa ya shilingi ngapi? Laki moja kwa mwezi? Sheikh Abuubakr akamdharau Sana kijana. Hata hivyo hakutaka kuonesha Hali hiyo. Wakaendelea kupiga soga, chakula kikaletwa wakala na hatimaye wakaagana.
'Kumbuka kunisalimia wazazi wenzangu huko. Bila shaka tunawatarajia kwa ajili ya kukamilisha Taratibu hizi. Muhimu wakinipa taarifa mapema juu ya ujio wao.' Sheikh Abuubakr akachombeza.
Masu na Yusuf wakaondoka wakiwa na nyuso za furaha. Mwamvita furaha yake ndio kabisa, Ilikuwa haisimuliki.
***
'Naam Sheikh, …… nakupata vizuri Sheikh……. Hewalaa sheikh wangu. Sasa, Mimi Nina mpango maalumu wa kutatua Hilo tatizo, Wala lisikusumbue Hilo, sisi watu wazima bwana, watoto hawawezi kutuzingua kabisa. Unaonaje tuonane baada ya swala ya jioni nikushirikishe mpango huo?' Ilikuwa sauti ya mzee Kisiki!
'Naam, nitafanya hivyo!'
Jioni ya siku hiyo iliwakutanisha mzee Kisiki na sheikh Abuubakr. Wakazungumza mengi. Alipotoka hapo, Sheikh Abuubakr alikuwa na jibu dhidi ya suala la bintiye. Katu hangeridhia fukara msukuma mikokoteni ayaharibu maisha ya bintiye
2020David Samson Ngocho
Sent using Jamii Forums mobile app


Namshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema na Pendo. Kwa neema zake, hatimaye nimekamilisha ahadi niliyowaahidi ya kuwaleteeni kitabu cha MATEKA WA HUBA ifikapo June. Nilitarajia kingetoka mwanzoni mwa Mwezi huu lakini si vibaya, bado lengo la kukitoa Mwezi huu limekamilika. 
Kona ya riwaya Kinondoni B - 0655428085/0784122598
Joint aka Kiroboto 0717301966 atakuletea ulipo kwa makubaliano maalum juu ya nauli.
Kariakoo 065227777/0653799999

BEI NI TSH 10,000/=