Simulizi: Kazi ya mzungu

Simulizi: Kazi ya mzungu

KAZI YA MZUNGU 20


Alipoingia tu kwenye apartment ya Issa, Molio alimkumbatia kwa furaha kubwa. Akambusu shavuni, shingoni, puani, machoni, kwenye paji la uso, kote kote akiacha mdomo pekee kwenye so wa Issa. Halafu bila kusema neno, Molio Huku akijipigisha mluzi wa furaha, akaingia jioni kuandaa chakula cha jioni. Issa alibaki anamtazama tu, huku akifurahi. Alijua chanzo cha furaha ya mpenziwe, na kulijua hilo kulimpa faraja moyoni mwake. Issa akaonelea vema kujitazamia zake runinga ajue kinachoendelea duniani.


Katika taarifa ya habari iliyorushwa na kituo kutoka Tanzania, kulikuwa na taarifa za kukamatwa kwa mtu aliyejulikana kwa jina la Sheikh Abuubakr Ramadhan huko kisiwani Zanzibar. Taarifa zilisema Sheikh Abuubakr alikamatwa kwa kile kilichoitwa kushirikiana na wahuni na kusababisha Askari wa jeshi la polisi kudhurika walipokuwa wanapambana na wahuni hao. Sheikh huyo hakuwataja wahuni hao Ni Nani kwa madai hakuwafahamu. Jeshi la polisi kupitia msemaji wake liliapa kuwasaka wahuni hao, huku likitangaza donge nono kwa mtu ambaye angejitokeza kutoa taarifa za mwonekano wao.


Habari hiyo ikavuta makini ya Issa Musa. Jina la Sheikh Abuubakr halikuwa geni kwenye maskio yake. Wapi alipata kulisikia? Ilipompambazukia, akajua jina Hilo Ni jina la baba mzazi wa Mwamvita. Yule binti aliyesafiri naye. Akapiga hatua na kuingia jikoni, alikokuwa Molio, akiandaa chakula kwa ajili yao.

'Dear, umeisikia habari toka Zanzibar? Inasemekana Sheikh Abuubakr Yuko mikononi mwa polisi. Baba yake Mwamvita.'

'Wee. Kulikoni?'

'Inasemekana ameshirikiana na wahuni kuwashushia kipigo polisi, haha!'

'Sheikh kawapiga polisi? Haiwezekani. Ila nahisi kitu kimoja tu, Sheikh Abuubakr alikuwa anashirikiana na polisi dhidi ya wahuni, wahuni wamewashinda nguvu, Sasa wanamgeuka mtu wao.'

'Mh, hao wahuni lengo lao Nini, na Kama wahuni TU wanaweza kuwatandika polisi, Ni dhahiri polisi ya bongo Sasa inazingua.'

'Hahaha, Kuna wahuni watata wewe!'

'Hatari'


Ukweli Ni kwamba, polisi walimweka ndani Sheikh Abuubakr kufuatia kipigo walichopewa, kwa sababu ya kizushi. Hilo likitokana na kukiri kwake kuwa alijua bintiye Yuko wapi na Yuko na Nani na bado akataka kuwabambikiza makosa vijana wale waliowashushia kipigo. Hata majirani wale waliokuwepo kwenye tukio waliposikia dau likitangazwa, walipoenda kituoni kuwaelezea Masu na Yusuf ili wajipatie Hilo dau, waliishia kupigwa biti na polisi wakae kimya. Hakukuwa na pesa ya kugawa.


Chakula kilipoiva, Molio alipakua na kuweka mezani. Wakala wakatosheka. Hapo Sasa, ule mshawasha wa Molio ukaanza upya.

'Enhee babe, yamenifika hapa,niambie habari njema tafadhali.' Molio akatamka akionesha shingoni yalikomfika hayo aliyosema.

'Yaraslav Yuko Zanzibar, Safari hotel. Yupo huko kwa likizo. Nimemgusia suala lako kwa kifupi na nikapendekeza aje kumalizia likizo yake hapa Oman. Amesema hakuna shida. Kwa hiyo mahabuba, kaa ukijua tutamudu kulipatia jibu suala lako mapema sana.'

'Waoo mpenzi. Nakupenda sana Issa wangu. You're the best. Mmmmwaah!' Molio akaonesha furaha yake, halafu akaongezea.

'Leo nimekutana na Mwamvita. Nimesungumza naye. Amenipatia namba za bwanake. Utazihitaji?'

'Ndiyo mpenzi, namuonea Sana huruma huyo binti hasa kwa vile Ni mdogo halafu Tena mjamzito, kwa Kweli ni ukatili wa kijinsia. Sijapenda kabisa utaratibu huo wa entry. Kwa nini wanateka watoto wadogo, mabinti wadogo hivyo?'

'Mh, entry biashara zao Ni zile haramu. Watoto unaosema wewe,kwa entry Ni watu wazima. Tena shukuru Mwamvita kaangukia mikononi mwa Halfani Nassor. Kwa maana kwamba anakuwa mke wake, Tena kwa kuridhia kwa wazazi wake vinginevyo angepelekwa kwenye makasino.'

'Dah, hatari Sana. Hivo wataka kunambia wazazi wake wanalifahamu hili?'

'Ndiyo, Sema hawajui Kama huyo bwana mwenyewe Ni mtu hatari. Wenyewe wanajua Ni mtu mwenyewe pesa na hivyo Kwao wanaona mtoto wao atakuwa na maisha mazuri. Mzazi gani hapendi mwanae awe na maisha Bora? Na, iko hivi, huyo boyfriend wake,Hana maisha ya kumpa binti yao, ndio maana wamefanya Kama kumtorosha, inaelekea binti hakutaka kusikia la adhana Wala mnadi swala, alikuwa miguu juu, kichwa chini jinsi alivyoangukia kwenye penzi la huyo mwanaume wake'

'Mh, napata picha sasa. Sasa, huyo bwana yake tukimjulisha atafanya Nini Kama Hali yake pangu pakavu Tia mchuzi?'

'Kusema Kweli hakuna Cha maana atakachofanya, ila siye tutakuwa tumetimiza ahadi yetu kwa Mwamvita. Lakini, nahisi tutakuwa tumemsaidia huyo Jamaa kukabili maumivu yake kiume, kwa Sasa bila shaka Yuko kwenye sintofahamu.' 'Hebu nipatie hizo namba za Masu.' Molio akamtajia, Issa akazihifadhi kwenye rununu yake.

'Kwa hiyo dear, Yaraslav Huku anaingia lini?' 'Keshokutwa!'

'Anhaa, oh Asante Sana mpenzi. Hatimaye, hatimaye nakuwa huru.'

'Kabisa mpenzi, hebu ngoja nimpigie Masu.' Issa akamweleza Molio. Akaweka code ya simu ya Tanzania, akapiga namba ya Masu aliyopewa.

Simu ikaita Kidogo ikapokelewa kwa sauti thabiti.

'Masuke Masuke, Nani mwenzangu?'

'Naitwa Issa Musa, mwenyeji wa huko Zanzibar, kwa Sasa Niko Dubai. Nilikutana na binti mjamzito akanipa namba yako nikupigie. Alisema nikikupa taarifa hii utaelewa maanake Nini, anaitwa Mwamvita. Nafahamu alipofikia, ingawa nahisi alipo SI mahali pazuri kwake. Anatia huruma Sana.'

'What?' Masu akahamaki. Lakini akajiambia, hakuna haja ya kupaniki, akatulizana halafu akatamka.

'Ok braza,Asante kwa taarifa ndugu Issa. Kesho naingia huko Oman. Vipi tunaweza kuonana nikifika huko? Kwa bahati mbaya Sana sio mwenyeji kabisa huko. Itakuwa safari yangu ya kwanza. Itanifaa Sana nikipata mwenyeji.' Masu akaongea kwa ushawishi. Issa Musa akashituka. 'Au tumekosea namba?' akajiuliza, lugha na jibu la Masu, halikuyumkinika vipi awe huyo maskini aloelezewa habari zake. Huyo alisikika Kama mtu tajiri, mwenye kila dalili ya uweredi wa Mambo tofauti na alivyodhania hapo awali alipokuwa akielezewa na Molio.

'Usijali juu ya kuonana. Kusema Kweli, kwa lolote utalohitaji, Wala usisite kunijulisha, ukitaka pia kampani yangu kwenye hiyo misheni, count me in (Hesabu kuwa nipo ndani)'

'Nashukuru Sana Kaka. Basi Kumbe nitahitaji mengi na Nina bahati kukupata wewe.'

'Pamoja sana.'

Aliposhusha simu yake chini, Issa Musa akamgeukia Molio na kumtazama kwa jicho la kutafuta majawabu!

'Nini?' Molio akamuuliza baada ya kuuona ule mtazamo.

'Una hakika Jamaa Ni hohe hahe?'

'Yeah, I mean, ndivyo nilivyoambiwa! Kwa Nini wauliza hivyo?'

'Ah, jinsi alivyozungumza, haelekei kuwa mtu duni kwa jinsi nilivyochukulia Maelezo yako, ukiongezea na kwamba Jamaa Kesho anaingia Salalah! Kama angekuwa msukuma mikokoteni tu, bila shaka Hilo lisingewezekana.'

'Mh, unanifanya na Mimi kufikiri aisee. The guy could be one of those government agents or worse one of the terrorists gang members.'( Jamaa asijekuwa Ni shushushu wa serikali au mbaya zaidi akawa miongoni mwa magenge ya kigaidi)

'Hahaha, I can't wait to meet the guy. Naanza kuona picha la hatari na msukuma kokoteni akiwa staring!'

'Unajua hiyo ina maana gani mpenzi?' Molio akauliza kwa unyonge.

'Ina maanisha Nini?' Issa akauliza Kama mbulula.

'Ina maana Kwamba naweza kuingia kwenye mpambano na huyo Jamaa. Nisingependa kuwa kwenye Vita hiyo. Maana kutoka moyoni mwangu, natamani huyo Masu ashinde, na hiyo ina maana nishindwe Mimi. Shida ya Vita, Ni kwamba, utaua au utauwa.!'

'Lakini mpenzi, wewe na Mimi tutakuwa zetu mbali. Usinambie unafikiria kuingia kwenye huo mpambano?'

'Unajua Sina namna Kama wataniamrisha kufanya hivyo. Yaani natamani Kweli huyo Yaraslav angekuwa keshaingia Huku tayari na kuniweka huru.!'

'Ok, nimekusoma. Cha kufanya, kwanza tumcheleweshe huyo Masu ili mishe zake zianze baada ya Yara kufanya muujiza wako. Hilo Nina hakika tunaliweza.'


***

Nzinyangwa akiwa ameambatana na bodyguard wake mpya. Huyu alikuwa raia wa Marekani, mwamerika mweusi, mwenye mafunzo ya juu ya kikomandoo. Kumuajiri mtu huyo kukitokana na lile tukio la kupoteza milioni mia moja hamsini kwa sababu aliyoiita 'ya kizembe'. Alikuwa amejifunza kigumu.


Hapa walikuwa kituo Cha polisi kufuatia ile taarifa ya polisi kuwa wahuni wawili walimudu kuwachakaza polisi wenye mafunzo. Taarifa ile, kwa Nzinyangwa haikuwa ya kupuuzwa hata Kidogo, la hasha, alikuwa na biashara kubwa ya kulinda. Biashara kubwa ya kutanua. Alikuwa na ndoto ya kuwa tajiri nambari moja Africa mashariki. Hao wahuni aliwahitaji kwenye genge lake.


'Ndio bwana Nzinyangwa, karibu sana.' Askari wa Zamu alimkaribisha. Hawa kina Nzinyangwa walikuwa Ni watu maarufu hapo kituoni. Walikuwa miongoni mwa VIP hasa kwa wale Askari potofu kwa maadili ya kazi yao. Nzinyangwa na matajiri wengine wengi walijua jinsi ya kudili na wanausalama ili kujihakikishia maslahi yao hayaguswi aslani. SI ajabu kuwa walikuwa na fungu maalum kwa ajili ya kulipa Askari hao.


'Asante Sana kamanda Shamte. Nimesikia Kuna wahuni walifanya kulitia doa jeshi la polisi. Ningependa kupata taarifa kamili kuhusu watu hao. Nataka nitumie watu wangu kuwapiga tafu Kidogo haha!' Nzinyangwa alizungumza na kumaliza kwa kicheko Cha kebehi. Angekuwa Ni Askari mwadilifu, bila shaka angeshitukia kicheko hicho, lakini pia, taarifa za kipolisi, huwa na mtiririko wake, huyu raia, Nzinyangwa, hakupaswa kuelezwa chochote kinachoendelea kwenye idara hiyo muhimu seuze kupendekeza kulisaidia jeshi Hilo? Mtu mmoja awezaje kulisaidia jeshi kazi yake? Mtu mwenyewe akiwa raia mhalifu ambaye genge lake lilihusishwa na vifo vya watu, kufilisi biashara halali, na kuwafanya wengine kupata stroke kutokana na madhila waliyowasababishia.

Lakini, Shamte na Askari wengi kituoni hapo walipokea masurufu kemkem kutoka kwa bwana huyo, Sasa akawa Kama mwajiri wao pia. Aliwatumia atakavyo. Angeweza kuwachukua wakamkamata mtu aliyedaiwa na Nzinyangwa, wakamsulubu, na hata kumnyang'anya Mali yake kwa maelekezo ya bwana huyo. Walichojali zaidi Ni ile habari ya masurufu na bakshishi zake za Mara kwa mara.

Shamte akajichekesha Kama punga,

'Hehehe sawa bosi. Ungependa nikupatie taarifa zao. Hehehe!'

'Ee, hili hapa faili lao, hehehe Nzinyangwa buana!'

Msaidizi wake akalichukua faili na kupitia Maelezo yaliyokuwamo.

Huyo Sheikh Abuubakr naweza kuonana naye?'

Ah hehe, kwa vile Ni wewe hehe, hatakiwi aonane na mtu.'

Nzinyangwa na bodyguard wake wakaingia lockup kuonana na Sheikh Abuubakr. Alipotaka kufuatana nao, Shamte akazuiwa.

'We endelea na majukumu hapo, Usijali!' Nzinyangwa akamuamrisha Shamte.

'Hehe sawa tu!'


Hawakuwa na muda wa kupoteza, walikuwa na maswali muhimu ya kujibiwa waende zao.

'Mzee Abuubakr, nimeelezwa kuwa Kuna wahuni ulishirikiana nao kuwapa kisago Hawa polisi. Nataka majina na anuani zao, hicho tu, Basi!' Nzinyangwa alimkoromea Sheikh.

'Mimi nishawaeleza polisi siwajui hao naoambiwa nimeshirikiana nao. Waulize watakuambia.'

'Najua hujawaambia pia. Lakini Mimi Ni Nzinyangwa, Mie sio polisi. Kama hutaki wawajue, Mie Sina shida na huo msimamo wako. Nachotaka Mimi, uniambie Mimi TU, Wala sitawaeleza hao, itakuwa Siri yetu Mimi na wewe.!'

Sikiliza bwana Nzinyangwa, Mimi hao watu siwafahamu. Hivi aliyepigwa ashindwe kuwatambua Mimi nayezushiwa Ndiyo niwatambue? Miujiza Basi!'

Nzinyangwa akamkonyeza bodyguard wake. Mzee Abuubakr hakutarajia hili. Alijikuta amepokea kibao kikali kwenye shavu la kushoto akaangukia upande wa kulia.

'Utatueleza ama utaanza ngonjera za karudi baba mmoja?' Nzinyangwa akamnong'oneza, Huku akilivuta sikio la kulia la Sheikh Abuubakr na kumsababishia maumivu makali.

Sheikh Abuubakr akajaribiwa awataje,lakini akalikumbuka jicho la onyo alilomzodoa nalo Masu. Ha! Hakutaka kurudia kosa Tena. Kama polisi waliwafahamu na kuamua iwe Siri, yeye Nani hata atoe Siri hiyo?. Sheikh Abuubakr akaamua liwalo na liwe, hatoi jina. Na hapo akapata Wazo la kuondokana na shuruba ya Nzinyangwa. Mzee huyo akapiga yowe kwa sauti Kali ya kuugulia maumivu.

'NAKUFAA!'

Nani alitaka uchunguzi wa kifo Cha mahabusu?, Shamte akatoka mbio kwenda kwenye chumba Cha lockup, mlangoni akapishana na Nzinyangwa na bodyguard wake. Ni Kama hawakumuona. Wakalifuata gari lao, gari la kifahari aina ya Range, wakaondoka hapo kituoni.

'Twende nyumbani kwa huyo Sheikh. Kwenye Maelezo pale wameandika anaishi Mwembe makumbi.' Nzinyangwa akamweleza bodyguard.

David Ngocho Samson


FB_IMG_1583317191932.jpg
 
KAZI YA MZUNGU 21


Mama Mwamvita alikuwa anajiandaa kupeleka chakula kwa mumewe sheikh Abuubakr wakati alipopata ugeni. Gari la Nzinyangwa lilipaki nje ya geti lao, wanaume wawili waliovalia kiukwasi wakawa wanasubiri kukaribishwa ndani. Nzinyangwa alikuwa kavalia nguo fulani za mishono ya kinaijeria. Kichwani mwake alikuwa kaweka kibandiko sawa na zile wavaazo mayahudi kwenye ibada. Bodyguard wake alikuwa ndani ya suti nyeusi.

'Karibuni' mama Mwamvita aliwakaribisha wageni hao ambao hata hivyo alibaini hawakuwa wageni wema asilani. La sivyo, Basi walikuwa wanaonesha kuwa wao Ni daraja lingine kuling'anisha na la huyo mama. Hivyo, ndivyo mama Mwamvita alivyowasoma wageni wake hao.

'Mh' Nzinyangwa aliguna.

'Nimepata habari Kuna wahuni walishambulia polisi hapa nyumbani kwako,la Kweli Hilo?'

'Baba, labda ningewafahamu Kwanza ingekuwa Vema zaidi ili tuongee Kama waungwana. Kwenu nyiye salamu inagomba?' Mama Mwamvita alizungumza kuwazodoa hao wageni wasokuwa na heshima. Hakuwahi kuona vijana wenye kiburi na majivuno Kama Hawa. Kama ukwasi ndio kitu kilichowafanya wawe hivyo, Basi Hawa walikuwa malimbukeni kutoka bara bila Shaka. Mama Mwamvita alishagaona matajiri wakubwa wenye kumiliki viwanda na utajiri wao kutoa ajira na bado walikuwa watu wenye heshima wasojikweza. Akilini mwake mama Mwamvita akahitimisha kuwa Hawa walikuwa malimbukeni majinuni toka bara.

Nzinyangwa akatafakari, Kama ataendelea kuonesha ubabe wake hatofanikiwa lengo lake. Akazuga utakatifu.

'Samahani Sana mama, ah haya maisha yanatusumbua akili zetu kwelikweli. Nisamehe kabisa mama. Shikamoo!'

'Marahabaa' mama Mwamvita akaitika moyo wake ukiwa umetakata.

'Ndiyo baba, nawasikiliza.!' akaongezea mama Mwamvita.

'Mama, Mimi naitwa Joseph Mafuru, Ni afisa upelelezi kutoka makao makuu ya polisi. Tupo hapa kutaka kujua hasa Nini kilitokea hata polisi kujeruhiwa vibaya hapa nyumbani kwako. Ni Hilo tu mamaangu.'

Mama Mwamvita akatafakari Kidogo. Swali likamjia kichwani mwake. Anawataja vipi wakwe zake? Masu alionesha Nia njema, wao wakamfanyia ubaya, akichotenda kwa polisi, Ilikuwa Ni kujitetea dhidi ya uvamizi wa ghafla. Hakuwa na kosa. Mama huyu akawaangalia watu hao mbele yake kwa Mara nyingine. Akakosa Imani. Hawa hawakuwa watu wema. Asingefanya makosa aliofanya mumewe. Akatunga kisa kichwani mwake.

Tulikuwa tunakula chakula cha mchana, wakagonga hodi vijana wawili, tukawafungulia. Tuliwakaribisha chakula, badala yake wakatuonesha bastola. 'Tunataka fedha' mmoja wao akatamka.

Mume wangu alikuwa ndani wakati huo na ukiangalia pale dirishani, kila kitu huonekana ukiwa mle chumbani. Alipoona tumetolewa bastola, akapiga simu polisi. Polisi hawakukawia. Walifika wakati mwafaka. Wakati huo, wale vijana walikwishaingia ndani ili kuchukua hizo fedha. Wakashitukizwa na ujio wa polisi. Polisi waliwaweka Kati, wakaamrisha waweke silaha zao chini, vijana wale wakazitupa chini na kuzisogeza kwa miguu kwenda kwa polisi. Wakati polisi wanapoziokota, ndipo wale vijana wakawashambulia na wao kutoroka.'

'Unaweza kuwaelezea jinsi walivyo muonekano wao?'

'Ni wahuni tu, manywele timutimu, suruali za jinzi zenye kuning'inia makalioni, masikio wameweka hereni. Misokoto ya bangi mdomoni na lugha chafu mdomoni. Kusema Kweli, sijui vipi walimudu kuwashambulia polisi namna ile. Ni Kama wagonjwa kwa jinsi walivyokonda' mama Mwamvita akauza simulizi yake. Nzinyangwa akaonekana kupotezwa kabisa. Watu aliowadhania hawangekuwa Hawa alioelezea huyu mama. Akaona Ni muda wamepoteza. Hawakuhitaji mateja. Walihitaji timamu. Hakujua, mama Mwamvita alikuwa anawaelezea vijana waigizaji anaowatazama kila jumamosi kwenye igizo lao kwenye runinga. Simulizi ile ikanunuliwa na Nzinyangwa.

Asante mama, tunakushukuru kwa ushirikiano wako uliotuonesha.'

'Karibuni Sana'

Nzinyangwa akaondoka akiwa amepoteza kabisa hamu ya kuwatafuta hao vijana.


***

Alipokuwa anampa chakula mumewe kule lockup, mama Mwamvita alimsimulia kisa Cha watu waliojiita wapelelezi. Akamweleza jinsi walivyokuwa wamevalia. Sheikh Abuubakr akajua Ni Nzinyangwa na bodyguard wake.


'Umefanya Vema kuwatungia hiyo simulizi ya mateja. Yule Ni tapeli mkubwa hapa Unguja. Kazi yake kutapeli Mali za watu hasa wastaafu. Yeye amekuwa anakula pensheni za wazee na kuwasababishia vifo na stroke. SI mtu mzuri kabisa. Mbaya zaidi alishawaweka polisi kwenye kiganja chake. Anafanya atakalo bila kuogopa mkono wa sheria.' sheikh Abuubakr akamweleza mkewe.

'Hivo Eeh, ah mume wangu nakueleza, nilipomuangalia Mara ya pili baada ya kujifanya msafi, moyo wangu ulidundia kulia. Ha! Nikaona maajabu, moyo wangu utoke kushoto uende kulia? Nikajua hii Ni taarifa kwamba Hawa sio wanavyosema ndiwo, nikapata Hilo Wazo la kuwatungia simulizi.'

'Hahaha, shukuru kwamba hawaangalii hicho kipindi kwenye runinga. Wangekufahamu. Mie mwenzio, wamenipiga vibao hapa, mashavu SI yangu Haya. Nisingepiga uyowe, wangeniumiza Sana wale washenzi. Nashukuru Mungu nilipopiga yowe TU Inshallah, nikawaona hao wanajiondokea zao.'

Mama Mwamvita akawa anayashika mashavu ya mumewe yaliojaa sharubu na kumpa pole.

'Bwanawee, Hivo humu ndani watakuweka Hadi lini? Ona unavyozeeka bwana wewe? Kwani wao wananataka Nini?'

'Bibie, watataka Nini Kama sio fedha? Hapa zatakwa fedha tu! Kunitungia uongo ule lengo wapate fedha kufidia maumivu waliyopata. Sikujua yule kijana ni mtu hodari vile!'

'Ulimtenda ubaya kijana wa watu. Mbona ukafanya vile, hujui tamaduni zetu Sheikh wangu? Huleti Vita nyumbani, Vita hufanywa huko mbali na nyumbani. Wewe ukaamua kuleta Vita yako nyumbani hukufikiria matokeo yake?'

'Yeishe bibie, najua nilifanya makosa. Sasa, nataka nione kwa siku mbili tatu hivi Kama bado wataendelea kunishikilia. Kama ikitokea hivyo, Kuna ile mahari aliyotoa bwana Kisiki, itabidi tuchote Kiasi watakachowapa unitoe humu. Naona nimeanza kupata wageni wengi Sana hapa wakiwamo waumini wenzangu. Hii hainijengei heshima.'

'Wewe waongea waumini na heshima ilihali habari yako imekuwa gumzo mitandaoni na taarifa yako imeripotiwa Hadi BBC?'

'Ati wasema?'

'Kesi yako yaweza kuwa Ni kubwa kuliko udhaniavyo, Kuna watu wanakuhusisha na makundi ya kigaidi huko kwenye vyombo vya habari. Kama lipo la kufanya Heri lifanyike mapema mume wangu!' mama Mwamvita akamrai mumewe.

'Sijui vipi nimeingia kwenye upuuzi huu. Sasa yaananipata makubwa. Na nikishatumia fedha ya mahari ya bwana Kisiki, Masu akafanikiwa kumpora mke, atayataka mahari yake. Nitafanyaje sasa.?'

'Ujifunze kwa hili baba Mwamvita,enzi zile za kutafutiwa mke au mume na wazazi, vijana wa Leo hawazijui. Sasa unaona? Walosema majuto mjukuu, Sasa wayaona mwenyewe. Tuwaache vijana waoane.'

'Dah, mahari yenyewe Haina faida kwangu, zaidi zaidi itaniweka kwenye Vita na mzee Kisiki. Ama kwa hakika, mtaka nyingi nasaba ataka mwingi msiba!' Sheikh Abuubakr Sasa alikuwa kwenye majuto. Kipi alichopata? Hakukuwa, zaidi ya kupigwa na kuumizwa na polisi wenye hasira, lakini pia kupigwa na tapeli bila sababu, kupoteza Mali kwa kesi isiyo na kichwa Wala miguu. Utumbo mtupu!.


'Nimekumbuka kitu mke wangu, mahari ya bwana Kisiki usiyaguse. Kuna wale 'wapenda haki', unawakumbuka? Enhee, ile fedha waliyotupatia, niliihifadhi pale pale pa siku zote, Kesho unapokuja, zibebe zote, nadhani zilibaki laki sita Kati ya milioni. Tutauliza zatakiwa ngapi kuniachilia.'

'Sawa mume wangu. Nitafanya hivyo!'

'Lo, yamenikuta Mie, Kama hawajanifilisi Hawa!...' sheikh Abuubakr akaendelea kuomboleza.

David Ngocho Samson
FB_IMG_1583317191932.jpg
 
KAZI YA MZUNGU 21


Mama Mwamvita alikuwa anajiandaa kupeleka chakula kwa mumewe sheikh Abuubakr wakati alipopata ugeni. Gari la Nzinyangwa lilipaki nje ya geti lao, wanaume wawili waliovalia kiukwasi wakawa wanasubiri kukaribishwa ndani. Nzinyangwa alikuwa kavalia nguo fulani za mishono ya kinaijeria. Kichwani mwake alikuwa kaweka kibandiko sawa na zile wavaazo mayahudi kwenye ibada. Bodyguard wake alikuwa ndani ya suti nyeusi.

'Karibuni' mama Mwamvita aliwakaribisha wageni hao ambao hata hivyo alibaini hawakuwa wageni wema asilani. La sivyo, Basi walikuwa wanaonesha kuwa wao Ni daraja lingine kuling'anisha na la huyo mama. Hivyo, ndivyo mama Mwamvita alivyowasoma wageni wake hao.

'Mh' Nzinyangwa aliguna.

'Nimepata habari Kuna wahuni walishambulia polisi hapa nyumbani kwako,la Kweli Hilo?'

'Baba, labda ningewafahamu Kwanza ingekuwa Vema zaidi ili tuongee Kama waungwana. Kwenu nyiye salamu inagomba?' Mama Mwamvita alizungumza kuwazodoa hao wageni wasokuwa na heshima. Hakuwahi kuona vijana wenye kiburi na majivuno Kama Hawa. Kama ukwasi ndio kitu kilichowafanya wawe hivyo, Basi Hawa walikuwa malimbukeni kutoka bara bila Shaka. Mama Mwamvita alishagaona matajiri wakubwa wenye kumiliki viwanda na utajiri wao kutoa ajira na bado walikuwa watu wenye heshima wasojikweza. Akilini mwake mama Mwamvita akahitimisha kuwa Hawa walikuwa malimbukeni majinuni toka bara.

Nzinyangwa akatafakari, Kama ataendelea kuonesha ubabe wake hatofanikiwa lengo lake. Akazuga utakatifu.

'Samahani Sana mama, ah haya maisha yanatusumbua akili zetu kwelikweli. Nisamehe kabisa mama. Shikamoo!'

'Marahabaa' mama Mwamvita akaitika moyo wake ukiwa umetakata.

'Ndiyo baba, nawasikiliza.!' akaongezea mama Mwamvita.

'Mama, Mimi naitwa Joseph Mafuru, Ni afisa upelelezi kutoka makao makuu ya polisi. Tupo hapa kutaka kujua hasa Nini kilitokea hata polisi kujeruhiwa vibaya hapa nyumbani kwako. Ni Hilo tu mamaangu.'

Mama Mwamvita akatafakari Kidogo. Swali likamjia kichwani mwake. Anawataja vipi wakwe zake? Masu alionesha Nia njema, wao wakamfanyia ubaya, akichotenda kwa polisi, Ilikuwa Ni kujitetea dhidi ya uvamizi wa ghafla. Hakuwa na kosa. Mama huyu akawaangalia watu hao mbele yake kwa Mara nyingine. Akakosa Imani. Hawa hawakuwa watu wema. Asingefanya makosa aliofanya mumewe. Akatunga kisa kichwani mwake.

Tulikuwa tunakula chakula cha mchana, wakagonga hodi vijana wawili, tukawafungulia. Tuliwakaribisha chakula, badala yake wakatuonesha bastola. 'Tunataka fedha' mmoja wao akatamka.

Mume wangu alikuwa ndani wakati huo na ukiangalia pale dirishani, kila kitu huonekana ukiwa mle chumbani. Alipoona tumetolewa bastola, akapiga simu polisi. Polisi hawakukawia. Walifika wakati mwafaka. Wakati huo, wale vijana walikwishaingia ndani ili kuchukua hizo fedha. Wakashitukizwa na ujio wa polisi. Polisi waliwaweka Kati, wakaamrisha waweke silaha zao chini, vijana wale wakazitupa chini na kuzisogeza kwa miguu kwenda kwa polisi. Wakati polisi wanapoziokota, ndipo wale vijana wakawashambulia na wao kutoroka.'

'Unaweza kuwaelezea jinsi walivyo muonekano wao?'

'Ni wahuni tu, manywele timutimu, suruali za jinzi zenye kuning'inia makalioni, masikio wameweka hereni. Misokoto ya bangi mdomoni na lugha chafu mdomoni. Kusema Kweli, sijui vipi walimudu kuwashambulia polisi namna ile. Ni Kama wagonjwa kwa jinsi walivyokonda' mama Mwamvita akauza simulizi yake. Nzinyangwa akaonekana kupotezwa kabisa. Watu aliowadhania hawangekuwa Hawa alioelezea huyu mama. Akaona Ni muda wamepoteza. Hawakuhitaji mateja. Walihitaji timamu. Hakujua, mama Mwamvita alikuwa anawaelezea vijana waigizaji anaowatazama kila jumamosi kwenye igizo lao kwenye runinga. Simulizi ile ikanunuliwa na Nzinyangwa.

Asante mama, tunakushukuru kwa ushirikiano wako uliotuonesha.'

'Karibuni Sana'

Nzinyangwa akaondoka akiwa amepoteza kabisa hamu ya kuwatafuta hao vijana.


***

Alipokuwa anampa chakula mumewe kule lockup, mama Mwamvita alimsimulia kisa Cha watu waliojiita wapelelezi. Akamweleza jinsi walivyokuwa wamevalia. Sheikh Abuubakr akajua Ni Nzinyangwa na bodyguard wake.


'Umefanya Vema kuwatungia hiyo simulizi ya mateja. Yule Ni tapeli mkubwa hapa Unguja. Kazi yake kutapeli Mali za watu hasa wastaafu. Yeye amekuwa anakula pensheni za wazee na kuwasababishia vifo na stroke. SI mtu mzuri kabisa. Mbaya zaidi alishawaweka polisi kwenye kiganja chake. Anafanya atakalo bila kuogopa mkono wa sheria.' sheikh Abuubakr akamweleza mkewe.

'Hivo Eeh, ah mume wangu nakueleza, nilipomuangalia Mara ya pili baada ya kujifanya msafi, moyo wangu ulidundia kulia. Ha! Nikaona maajabu, moyo wangu utoke kushoto uende kulia? Nikajua hii Ni taarifa kwamba Hawa sio wanavyosema ndiwo, nikapata Hilo Wazo la kuwatungia simulizi.'

'Hahaha, shukuru kwamba hawaangalii hicho kipindi kwenye runinga. Wangekufahamu. Mie mwenzio, wamenipiga vibao hapa, mashavu SI yangu Haya. Nisingepiga uyowe, wangeniumiza Sana wale washenzi. Nashukuru Mungu nilipopiga yowe TU Inshallah, nikawaona hao wanajiondokea zao.'

Mama Mwamvita akawa anayashika mashavu ya mumewe yaliojaa sharubu na kumpa pole.

'Bwanawee, Hivo humu ndani watakuweka Hadi lini? Ona unavyozeeka bwana wewe? Kwani wao wananataka Nini?'

'Bibie, watataka Nini Kama sio fedha? Hapa zatakwa fedha tu! Kunitungia uongo ule lengo wapate fedha kufidia maumivu waliyopata. Sikujua yule kijana ni mtu hodari vile!'

'Ulimtenda ubaya kijana wa watu. Mbona ukafanya vile, hujui tamaduni zetu Sheikh wangu? Huleti Vita nyumbani, Vita hufanywa huko mbali na nyumbani. Wewe ukaamua kuleta Vita yako nyumbani hukufikiria matokeo yake?'

'Yeishe bibie, najua nilifanya makosa. Sasa, nataka nione kwa siku mbili tatu hivi Kama bado wataendelea kunishikilia. Kama ikitokea hivyo, Kuna ile mahari aliyotoa bwana Kisiki, itabidi tuchote Kiasi watakachowapa unitoe humu. Naona nimeanza kupata wageni wengi Sana hapa wakiwamo waumini wenzangu. Hii hainijengei heshima.'

'Wewe waongea waumini na heshima ilihali habari yako imekuwa gumzo mitandaoni na taarifa yako imeripotiwa Hadi BBC?'

'Ati wasema?'

'Kesi yako yaweza kuwa Ni kubwa kuliko udhaniavyo, Kuna watu wanakuhusisha na makundi ya kigaidi huko kwenye vyombo vya habari. Kama lipo la kufanya Heri lifanyike mapema mume wangu!' mama Mwamvita akamrai mumewe.

'Sijui vipi nimeingia kwenye upuuzi huu. Sasa yaananipata makubwa. Na nikishatumia fedha ya mahari ya bwana Kisiki, Masu akafanikiwa kumpora mke, atayataka mahari yake. Nitafanyaje sasa.?'

'Ujifunze kwa hili baba Mwamvita,enzi zile za kutafutiwa mke au mume na wazazi, vijana wa Leo hawazijui. Sasa unaona? Walosema majuto mjukuu, Sasa wayaona mwenyewe. Tuwaache vijana waoane.'

'Dah, mahari yenyewe Haina faida kwangu, zaidi zaidi itaniweka kwenye Vita na mzee Kisiki. Ama kwa hakika, mtaka nyingi nasaba ataka mwingi msiba!' Sheikh Abuubakr Sasa alikuwa kwenye majuto. Kipi alichopata? Hakukuwa, zaidi ya kupigwa na kuumizwa na polisi wenye hasira, lakini pia kupigwa na tapeli bila sababu, kupoteza Mali kwa kesi isiyo na kichwa Wala miguu. Utumbo mtupu!.


'Nimekumbuka kitu mke wangu, mahari ya bwana Kisiki usiyaguse. Kuna wale 'wapenda haki', unawakumbuka? Enhee, ile fedha waliyotupatia, niliihifadhi pale pale pa siku zote, Kesho unapokuja, zibebe zote, nadhani zilibaki laki sita Kati ya milioni. Tutauliza zatakiwa ngapi kuniachilia.'

'Sawa mume wangu. Nitafanya hivyo!'

'Lo, yamenikuta Mie, Kama hawajanifilisi Hawa!...' sheikh Abuubakr akaendelea kuomboleza.

David Ngocho Samson
View attachment 1488226
Shukran mkuu.
Tunaomba uongeze ongeze sehemu nyingine zaidi mkuu.
 
KAZI YA MZUNGU 22.


Masu alizama kwenye ndege ya Ethiopian Airways, akaketi kwenye kiti chake na kutulia. Muda SI mrefu, akaingia Jamaa mwingine Mzungu akiwa kavalia miwani ya macho. Haikuwa miwani ya Kawaida. Kwenye mafunzo yake kule hotelini, alijifunza kwamba Kuna miwani ambayo hutumiwa na majasusi, miwani ambayo huwa na memory card ndogo Sana lakini yenye uwezo wa Hadi gb kadhaa. Miwani ile huchukua video na kuhifadhi video Hizo kwenye hiyo memory card. Walijifunza sifa za miwani hiyo. Mara moja Masu akabaini yule Mzungu SI raia wa kawaida. Akatulia. Hakuwa na shida na jasusi.


Mzungu huyu alipofika kwake, alisimama, Mara akaketi. Ndiyo, alikuwa siti ya jirani yake.

'Hello!' Mzungu akamsabahi.

'Hi'. Masu akajibu salamu.

'First trip on board Ethiopian Airways. Gotta have to learn new experience!( Mara yangu ya kwanza kupanda ndege ya shirika hili. Natarajia kupata uzoefu mpya) Mzungu akamweleza Masu.

'First trip to Oman. Very excited!' (Mara yangu ya kwanza kwenda Oman) Masu akamjibu Mzungu.

'Oh yeah, that's great. It's my first time too. By the way I am Yaraslav, my friends calls me Yara.' (Ahaa, sawa, Mimi pia Ni Mara ya kwanza kwenda Oman. Naitwa Yaraslav,lakini marafiki huniita Yara)

'Oh, nice to meet you Mr Yaraslav, my name is Masuke, my friends calls me M'bara!' (Sawa sawa, Mimi naitwa Masuke ingawa marafiki huniita M'bara)

'Mubara, I'd rather call you Masu.' (Mubaraa, ah, naona Bora nikuite Masu)

'That's also acceptable.'(Hilo pia linakubalika)


Walizungumza na kufahamiana. Safari yake haikuboa. Yara alikuwa mtu wa simulizi nyingi, mcheshi na mpenda utani. Masu naye hakuwa nyuma upande huo.

Tayari Masu alijua kuwa Yara alikuwa anaenda kwa rafikiye waliyesoma wote huko UK. Na kwa upande wake alijitahidi kutolizungumzia suala lake lililompeleka huko Oman. Ilipaswa kuwa Siri.


Walipotua uwanja wa ndege wa Salalah, Issa Musa alikuwa pale kumpokea Yaraslav, Masu hakumjua Issa, hivyo aliagana na Yara na kumtafuta Issa kwenye simu. Simu ya Issa ikaita, na yeye akajiweka pembeni baada ya kuona jina la Masu kwenye skirini ya simu yake.


'Naam ndugu Masu, habari?'

'Njema Kaka. Nilitaka kukujulisha kwamba nimekwisha kuingia Oman, nipo hapa Salalah airport, nimeingia na ndege ya shirika la Ethiopia Airways.'

'Ah haha Safi Sana Kaka. Habari njema Ni kwamba Mimi pia nipo hapa uwanjani. Kuna mgeni wangu nimekuja kumpokea na yeye ameingia kwa ndege hiyo hiyo uliyokuja nayo. Ningependa kujua unaonekanaje kwa leo.'

'Oh, imekuwa Heri Sana. Kwa utambulisho zaidi nimeninginiza skafu ya bendera ya taifa shingoni. Nimevaa suti ya blue..'

Issa Musa akageuka, Kuna mtu alimuona akiwa kavaa namna hiyo. Alikuwa anaagana na Yara. Akamuona Jamaa akiwa anazungumza kwenye simu.

'Nishakuona Kaka, nipo nyuma yako.' Issa Musa akamweleza Masu. Masu akageuka. Mwenyeji wa Yara alikuwa awe mwenyeji wake pia. Bahati ilioje!

Wakasalimiana kwa kukumbatiana Kama vile walifahamiana siku nyingi. Uzuri wa wabongo, wakiwa nje ya mipaka ya nchi yao, hasa ughaibuni, haijalishi Ni kabila gani, au Kanda gani anatokea. Wanakuwa Ni Kama ndugu wa damu kabisa. Hivyo haikushangaza Masu na Issa kuwa Kama ndugu Huku ugenini.

'Pole kwa safari! Na karibu Salalah!' Issa Musa alitamka. Halafu akamgeukia Yara.

'Mr Yara, meet my brother Masu, you just exited the same plane!'

Jamaa hao Masu na Yara badala ya kusalimiana, Wakaangua kicheko kikubwa, halafu wakakumbatiana kwa furaha.

'You know what, Issa, we were chatting all the way from Zanzibar and we had a lot of time getting to know each other. It surely has been a beautiful journey.' Yara akamweleza Issa Musa.

'Hey bro, you didn't mention it was Issa you were coming to meet. Haha!' Masu akamtania Yara.

'I told you I was meeting an old friend, only I didn't mention his name.'

Wakafurahi Sana. Kwa muda wote huo, Molio alikuwa ametulia anawatazama wanaume hao. Ajabu watu wasiofahamiana kufurahiana namna hiyo, Kama vile Ni marafiki wa tangu zama hizo. Wanaume, ah kwake ikawa kitendawili. Akajaribu kuwaza ingekuwa Ni Wanawake. Bila shaka wangeleteana mashauzi Kwanza, Hadi kuzoeana, ingewachukua muda mrefu.

'Guys, meet my beautiful and wonderful girlfriend Molio. Molio, these are the guys I told you about. Masu and Yara.'

'Wow, she is emaculate! Hi, my name is…'

'Yara, I know it already.' Molio akatamka Huku akiachia tabasamu lake akimkatisha Yara aliyekuwa anajitambulisha kwa mbwembwe kibao.

'Nice to meet you, Molio!' Yara akatamka.

'Nice to meet you Yara. I'm glad you could come.'

'Of course, I had to, we are, you know, family haha!'

'Thank you' Molio akashukuru.

'Hi shemeji. Mambo?' Molio akahisi sauti ya Masu, Ni sauti ya kipekee. Sauti nzito yenye mvuto.

'Poa Masu. Pole kwa safari na karibu Oman. Pole kwa yote pia.' Molio akamkaribisha Masu.


Mshangao ulikuwa bayana. Masu aliyeambiwa habari zake na kumtengenezea taswira kichwani mwake, hakuwa huyu. Huyu alionekana mtu tofauti na fikra zake. Huyu anazungumza kizungu kwa ufasaha, Ni mtanashati kwelikweli, mtu ambaye hafananii usukuma mkokoteni. Molio akakiri nafsini mwake, huyu Kama Kweli alikuwa anasukuma mkokoteni, Basi Ilikuwa katika kazi maalumu. Huyu alikuwa na kila sifa ya jasusi. Masu alipomshika mkono, Molio alihisi kitu mwilini mwake. Na alipotazamana naye usoni. Alijikuta anashikwa na aibu za kike. Akafanya hima kuuchomoa mkono wake. Mfadhaiko wa huba. Ndani yake Kuna kitu kilikuwa kinaumbika. Hakujua Ni Nini. Vyovyote vile, alipaswa kuwa mbali na Masu. Molio alijiambia nafsi yake.


'Welcome to Oman guys, feel at home!' Molio akapaza sauti yake kwa utani Huku akirusha mikono yake. Wakatoka Huku walizungumza wawili wawili. Issa Musa na Yaraslav Huku Masu na shemejie Molio. Wakawa wanatembea mdogo mdogo kuelekea kule walikopaki gari.

'Molio, napenda niwashukuruni Sana kwa kunipa taarifa za Mwamvita, kusema Kweli sijui mzee wake Ana shida gani hata.'

'Mie pia nashangazwa. Nilipoambiwa huyo mwanaume anayemng'ang'ania binti yao Ni msukuma mkokoteni, nikajua wazazi wa Mwamvita wanajaribu kumtafutia binti yao maisha Bora. Maana Kisiki Ni Kisiki Kweli, ana fedha Sana. Sema, ana maisha ya hovyo Sana pia. Lakini, heri nusu Shari kuliko shari kamili. Huyo msukuma mkokoteni kusema Kweli angempa tu shida.'

'Haha kwa hiyo wewe huamini kwamba Mimi msukuma mkokoteni siyo?'

'Kwani wewe unaamini habari hiyo?'

'Enewei, tuachane na hayo shemeji. Nimekuja kumfuata mama watoto, mchumba, mtoto wa babamkwe wangu bandidu!'

'Hahaha, umempata. Uzuri Ni kwamba Inajulikana wapi kafichwa, kumpata umempata. Hofu yangu Ni je utafanikiwa kuondoka naye?'

'Hah kwa Nini wadhani hivyo shemeji?

'Mh, nimejiuliza TU. Maana hapo alipo mzee wake keshakula mahari, najiuliza ni mwanaume gani atakubali mkewe achukuliwe hivi hivi!'

Masu akakumbuka taarifa alizopata kwa Yusuf kabla hajaingia kwenye ndege pale Kisauni.

'Huyo mzee Ni Mafia mbaya, anamiliki genge la uhalifu, Ni brigedia mstaafu. Amewekeza Sana Asia. Anamiliki kampuni la usafirishaji mizigo la transport Asia world-wide, Ana hisa nyingi kwenye mahoteli ya kitalii, mahoteli ya kisasa, makasino nk. Ushawahi kusikia genge la uhalifu linalojihusisha na usafirishaji wa binadamu, la entry? Basi Jamaa anahusishwa nalo pia.' Yusuf alikuwa kampa habari hizo.


Alipozidi kulichakata suala Hilo akilini mwake, alibaini kuwa hapa alikuwa kaingia kwenye mtego hatari. Kina wakati aliwaza endapo kulikuwa na haja kubwa kujiingiza hatarini, akajiuliza kulikuwa na baraka gani kung'ang'ania penzi ikiwa binti keshaozwa. Wazazi wamechukua mahari kwingineko, na binti yao Huenda karidhia. Kwa Nini Mwamvita alimdanganya anaenda Mafia, baadaye apate habari Yuko Oman? Je, Hilo halikumaanisha kuwa mwanamke huyo alikuwa amekusudia kumpoteza maboya Huku akiridhia kuwa mke wa mtu mwingine? Wazo Hilo likamfanya Masu ajione zoba, zumbukuku la mapenzi. Akajiona swakala kabisa. Alijiua sheikh Abuubakr, mwenye kingi kisununu, alikuwa kajaa TU unoko, lakini Sasa alianza kuhisi labda mzee huyo alikuwa sahihi muda wote. Labda alidhamiria kumwepusha na mtu mbaya Kisiki. Labda Kweli alikusudia kumpa maisha Bora binti yake. Masu akajikuta anajiuliza, Nini Cha mno angempa Mwamvita? Ukiacha vijisenti alivyopora kwa Nzinyangwa, alikuwa msukuma mikokoteni tu. Akajaribu kuvaa viatu vya baba mkwe, mwenye maisha ya wastani. Hakutoka jasho Sana ndio apate mkate wa siku. Lakini hakuna siku familia ilishinda njaa, wala kukosa mahitaji muhimu. Binti aliyezoea maisha Hayo, binti yake ampendaye, akaolewe na mbeba mizigo? Hata kidogo, asingekuli kamwe. Akadhamiria moyoni kumuacha Mwamvita, Kama itaonekana ameridhia kuwa na mzee Kisiki.


'Shem, mawazo mengi eeh?' Molio akamzindua kwenye lindi la mawazo.

'Acha tu shemeji, vipi umepata kuonana na Mwamvita siku za karibuni?'

'Ndiyo Shem, juzi tu nimeonana naye. Ndiyo alitupatia namba yako.'

'Vipi afya yake?'

'Yuko mzima wa afya kabisa, alishakubaliana na Hali ya hewa ya Huku, Yupo vizuri kiafya.'

'Je anaonekana kufurahia maisha anayoishi hapa?'

'Ah, Hilo kwa Kweli Sina hakika nalo Sana. Unafahamu, Inawezekana mtu kalia wee halafu kilio kikaisha akakubaliana na matokeo. Nachojua, umejaa tele moyoni mwake. Haachi kukuongelea, akitamani kukuona, na Mimi naweza kuona kwa Nini, alibahatika Sana kukupata Shem, we Ni mwanaume na nusu' Molio alizungumza Huku akimwangalia Masu kwa namna ambayo, ilimsisimua kijana huyo lakini akabaini huyu hakuwa binti TU, alikuwa mchumba wa mtu, ambaye ugenini Huku alikuwa tayari kumpa mkono. Akalifuta Wazo Hilo haraka.

'Unadhani nachofanya Ni sahihi shemeji? Nimejikuta nafunguka akili yangu baada ya kukanyaga ardhi ya Oman. Kama unavyosema kuwa wazazi wa Mwamvita wamekula mahari, hiyo Ina maana Ni mke wa mtu tayari. Je Ni sahihi Mimi kumfuatilia Tena? Nahisi spidi niliyotoka nayo huko imekuja kuishia hapa uwanjani. Ningelijua hili, Wala nisingehangaika. Kinachoniumiza Ni mtoto. Nilitamani Sana Kama ningemlea Mwanangu Mimi mwenyewe!' Masu akajikuta anafunguka mengi.

'Ahm, Shem kwa Kweli hapo Sina nachoweza kusema, Sina kabisa mamlaka ya kukushauri lolote, Cha kufanya, fuata matakwa ya moyo wako. Wala usitake kusikiliza sauti nyinginezo.' Molio akatamka. Tayari walikuwa wamelifikia gari la Molio. Wakaingia ndani, wakaliwasha na kuelekea kwenye apartment ya Issa Musa.

David Ngocho Samson
FB_IMG_1582711137383.jpg
 
KAZI YA MZUNGU 23


Jioni saa mbili hivi, Issa Musa na wageni wake, walikuwa wamekaa kuzunguka meza katika moja ya mgahawa maarufu jijini Salalah. Walikuwa na mengi ya kuzungumza. Moja ikiwa Ni juu ya suala la Molio. Namna gani alitaka mpenziwe awe huru dhidi ya Entry.

'Kwa uzoefu wangu, ili kuitoa hiyo chip, itahitaji operesheni kubwa Sana. Nasema hivyo kwa sababu chip za Entry hawaziweki kwenye ngozi, washenzi wale huwamezesha hizo chip, wakishameza, huzivuta kwa sumaku ili zijibane kwenye utumbo badala ya kwenda kwenye mfumo wa mmeng'enyo wa chakula. Hivyo, haziwezi kutoka kwa njia ya haja kubwa. Chip zao Ni za kisasa zaidi, wanaziendesha kwa kutumia satellite. Hivi Ni kusema kwamba,kokote alipo, wakimhitaji, wanatumia satellite kumuona halafu, wanazi-activate kwa mionzi, na hapo ndio mtu anapata maumivu makali sana, kuishiwa nguvu na kupoteza fahamu. Shida nyingine ya hizo chip Ni kwamba ukitaka kuzitoa, unahitaji kuwa eneo ambalo, hiyo mionzi haiwezi kuwa active.' Yaraslav aliwaeleza.

'Kunao uwezekano wa kuitoa lakini?' Molio aliuliza kwa wahka.

'Upo, lakini Ni operesheni kubwa Sana na hatari. Chip kwa mfano ikia-activate, Kuna hatari ya kupoteza maisha, na operesheni yenyewe inahitaji angalau madaktari watatu,na inachukua hadi masaa matatu. Hapo tena utahitaji kupumzishwa kwa muda mrefu uli kupona vizuri.!'


Maelezo ya Yara yakamvunja nguvu molio na kumkondesha ghafla Issa Musa. Molio alihitajika kuwepo kazini kila siku, alihitaji kuwepo kwenye vikao vyao vya Mara kwa Mara. Asingepata muda wa kufanyiwa operesheni kabla hawajamshitukia. Mkwamo ukasomeka barabara kabisa usoni mwake. Huzuni ikatamalaki ukumbini hapo. Kimya kikatamalaki, huenda shetani alikuwa anapita, haha! Kimya hicho kikavamiwa kwa kushitukizwa na kicheko kikubwa cha Yaraslav.

'Hahahaha, guys I got you, haha I totally got you' Yaraslav akaangua kicheko cha nguvu kushinda cha awali. Jamaa wakabaki wanashangaa. Kulikoni! Isijekuwa wamemleta chizi.

'..The heck is funny, Yara? The news you just gave are devastating and yet you can laugh your ass out?' Masu akamuuliza Yara, Nini maana ya kicheko chake ikiwa Ilikuwa habari mbaya Kwao.

'Ok guys, calm down. Ok, just calm down.. I have another solution to the problem. I didn't come all the way down here to give you the worst news of the millennium apocalypse, haha!

'You mean there is another way around the problem?

'Yes, the simplest one. All you'll need is about fifteen minutes top. The good news is that, we can deactivate the chip and render it impotent forever. How would you like that, Molio?'

'Are you my long awaited for Messiah?' Molio akasimama na kumrukia Yara, akamkumbatia. Uchozi ukamtiririka shavuni.

Habari hiyo ikawa habari njema Sana kwa wapenzi wawili, Molio na Issa.


***

Awali, Issa na Molio walikuwa wamemshawishi Masu kusubiri kwanza mpango wake, ili Kama Jambo lile likifanikiwa basi yeye Molio, angemtoa huko Matekani mpenziwe Masu, Mwamvita. Lakini Sasa, ilionekana Jambo la Masu lingewezekana kufanyika kwanza.


Molio aliwaaga marafiki wale watatu, akaondoka na kuelekea kwa mzee Kisiki, Halfani Nassor residence. Huko, alijua mzee Kisiki kwa ratiba yake, angekuwa bado Dubai kwa mradi wa watoto na angetoka hapo angeenda kwa wakeze wa Zanzibar kabla ya kurejea tena Oman.

'Oy Moudy! Ni aje?' Molio alimsabahi mlinzi getini kwa Kisiki.

'Ah mtoto Molio. Kwa mudi hiyo leo, naamini Mahmoud Mimi nitapata jibu la uhakika. Nambie mtu wangu!' Mahmoud akachomekea huku akitabasamu kama kawaida yake amuonapo Molio.

'Poa Sana Moudy, dah na kusema Kweli Leo mudi yangu iko freshi Sana. Utanitoa out leo?' Molio alichombeza kwa sauti ya makusudi, sauti iliyokusudia kumtikisa Moudy na moyo wake.

'Ah kudadeki, unantania au unasema Kweli Molio?'

'Eh, naapia wallah!' Molio akapitisha kidole shingoni.

'Ah Moudy Mimi Nina mkosi gani mie.' Moudy akalalamika

'Inamaanisha Nini kusema hivyo? Siku zote Molio Molio, Leo nakukubalia unadai Una mkosi,mbona nyie wanaume hamsomeki? Ushaniboa tayari.' Molio akaendelea kumzuga mlinzi.

'Dah, Basi Nina ugomvi na wewe mtoto mzuri kuitikia mwito wangu? Wala, sema da, Kweli ng'ombe wa maskini hazai, Nina maana Leo Sina wa kunibadilisha hapa getini. Hemed anaumwa!'

'Loh, Basi Tena Moudy, mzuka nao umekata kabisa kunambia hivyo.'

'Tufanye Kesho Basi mpenzi ee, Kesho nikupeleke ghettoni kwa mchizi Moudy ukalitie barka!'

'Hah, sijui, labda tuangalie itakavyokuja hiyo Kesho. Naomba nikamuone Malkia Mwamvita!'

'Malkia Yupo ndani bwana , we pita TU, ila Leo haki ya Nani, Leo nailaani Sana mizimu yangu!'

Hahaha!' Molio akacheka Huku akiingia kwenye kasri la Halfani Nassor. Alikuwa anafahamu ishu ya Hemed kuumwa na ndio maana alichomekea ishu ya outing akijua Moudy asingeweza kuacha lindo.


***

Sebuleni aliwakuta Mwamvita na Aneth wakiwa wanasukana nywele. Aneth ndio alikuwa anamsuka Mwamvita.

'Habari za hapa mabosi wangu!' Molio akawasabahi kwa bashasha.

'Haha da Mariamu bwana, Nani bosi hapa, labda Aneth!' Mwamvita akatabasamu alipotamka Hayo.

'Leo umevalia miwani mwenyewe. Enhe nambie da Mariamu, ulifikisha ujumbe wangu?' akaongezea huku akimtazama Molio barabara machoni.

'Naam,niliufikisha haswaaa. Nilimpatia Issa akampigia.'

'Enhe akasemaje!' Mwamvita akauliza kwa mchecheto.

'Aseme Nini maskini wa watu, alichanganyikiwa Sana. Pesa za kukufuata Huku Ndiyo imekuwa muhali kidogo. Nadhani atakuwa anahangaika kutafuta namna ya kuja huku.'

'Lo Jamani Masu. Heri tu asije. Maana mmh, namtesa bure Masu wangu jamani.'

'Kwa Nini?'

'Najua kutakuwa na ugumu wa kupata fedha,na .. hata akaipata hiyo fedha, wazazi Kumbe washakula mahari ya mzee Kisiki da Mariamu, hiyo Ina maana kuwa Mimi Ni mke wa mtu sasa.'

'Ndiyo kusema umeridhia Iwe hivyo?'

'Da Mariamu, kungekuwa na namna, nakuapia ningefanya chochote nipewe talaka. Lakini hapa, ah hapa Ni Kama tu Niko utumwani. Fikiria tangu niingie humu, nikitoka Basi inakuwa Ni kuzunguka TU ndani ya fensi hii. Siwezi kutoka nje ya geti nikaujua walau mji!'

'Mh na Hayo Kweli si maisha. Vipi waonaje nikikutoa out leo?' Molio akamuuliza Mwamvita.

Mwamvita akamtazama Aneth Kama anayetafuta majibu machoni kwake. Aneth akabetua mabega kumaanisha Hana majibu. Mwamvita akamuomba waende wote. Aneth akakubali Kama Molio hakuwa na kipingamizi. Hakukuwa na kipingamizi chochote. Molio akaambatana na wasichana hao wawili wakatoka ndani ya mjengo wa Kisiki. Zoezi la kusukana likaahirishwa Tena huku vichwa vyao vikisitiriwa na mitandio maridadi.

'Moudy, nawarudisha baada ya masaa mawili au matatu, ngoja niwaoneshe mji kidogo.' Molio akamweleza mlinzi. Moudy hakutakiwa kuwaachia hao watoke, alipaswa kuwazuia. Lakini Leo hii Ndiyo kwanza alikuwa kakubaliwa na Molio. Angewezaje kumpa jibu ambalo lisingemfurahisha? Akajing'ata ng'ata midomo, wakati anapofungua mdomo aseme kitu, Molio na wakeze Kisiki walikuwa wameshatoka. Akaishia kujisemea.

'Basi msichelewe Sana kurudi' dah, akageuka na kupiga teke ukuta. Haikutosha akautandika ngumi ukuta. Alikuwa anaweka kibarua chake matatani.


***

Yale yote walivyokuwa wanazungumza Molio na Mwamvita, yalimfikia mbashara kabisa Masu akiwa na Jamaa zake. Ile miwani aliyovaa Mwamvita, Ilikuwa inachukua sauti na video na kuzituma moja kwa moja kwenye simu ya Yaraslav. Ilikuwa Kama live broadcast. Masu alijikuta anaumia kwa maneno Yale aliyozungumza Mwamvita. Kwamba alikuwa mke wa mtu tayari. Vipi hakuona kwamba yeye pia alikuwa anamhitaji awe mkewe?. Kwa Nini akubaliane na suala Hilo kirahisi hivyo? Na Kuna sehemu aligusia kwamba Heri asingekuja Oman? Machozi yakatengeneza dimbwi machoni. Akayafuta kwa kificho wenzake wasimshitukie.

'Akisema hanitaki nitafanya Nini?' alikuwa awaze Kumbe akawaza kwa sauti.

Yara na Issa wakamgeukia kumwangalia.

'Pole Sana. Nakushauri usiliwaze Hilo kwa sasa.' Yara akamweleza.

'Mimi nadhani, ukubaliane na kile atakachokuambia. Kama Ni mke wa mtu tayari, umma wakijua kwamba wataka kumchukua, adhabu yake bila shaka ni mawe. Heri kumwepuka tu ndugu yangu. Maisha ni bora zaidi. Wanawake wapo wengi na ungekuwa muislamu kama mimi, kwa waislamu sisi hata wanne ruksa, ya Nini uumie sababu hiyo? Chukulia poa na Anza upya maisha.' Issa Musa akamwaga nasaha zake. Masu alikuwa njia panda.


Dakika kadhaa mbele, gari la Molio likafika hapo kwa apartment ya Issa Musa. Wakashuka na yeye Molio akawaongoza wasichana wale kuingia ndani.

Ile kufika mlangoni kuingia sebuleni, Mwamvita akamshuhudia Masu. Nguvu zikamwishia, akaketi chini. Masu akamkimbilia na kumnyanyua taratibu. Akamkokota Hadi kwenye sofa pale sebuleni.

'Umekuja Masu?' akajitahidi na kutoa sauti kwa bidii.

'Nisamehe tafadhali, Nisamehe Sana.!' Mwamvita akanong'ona.

'Usijali, Niko hapa. Nimekuja nikuchukue wewe na mwanetu mpendwa. Usihofu Tena. Kila kitu kitakuwa sawa mpenzi. I missed you!' Masu akazungumza. Sauti ya chini. Mwamvita akawa anatikisa kichwa kulia kushoto kushoto kulia. Masu akawa haelewi.

'Nisamehe tafadhali Masu.' Mwamvita akatamka Tena. Hali hiyo ikamchanganya zaidi Masu.

'Usijali mpenzi, najua SI makosa yako. Nafahamu kila kitu. Niko hapa kwa ajili yako.' Mwamvita roho ikamuuma, maumivu makali yakalikata tumbo lake kikatili. Akayakumbuka maneno ya Aneth aliposimulia kisa cha mpenziwe Halima, mke mwingine wa Kisiki. Mwamvita akajuta kwa kumwingiza Masu kwenye kumi na nane za mzee Kisiki. Akagutuka, na Ni Kama vile alizinduka kwenye coma. Akaongea kwa sauti iliyosikika Vema.

'Nakuomba urudi nyumbani Masu. Pliiz. Huku tayari nilishaolewa.' machozi yakateremka shavuni kwa Mwamvita.

'Najua mpenzi, lakini SI kwa kupenda kwako siyo?' sauti ya ubembelezi ya Masu ikasikika, lakini Mwamvita hakuisikia, alichosikia ni;

'Walimdhalilisha Sana' sauti yenye mwangwi ya Aneth, ikajirudia Tena na Tena kichwani mwa Mwamvita.

'Da Mariamu, naomba nirudishe kwa mume wangu tafadhali. Nakuomba' Mwamvita akamsihi Molio.

Kauli hiyo ikamfadhaisha Sana Masu. Hakuamini. Safari yake Oman, Ina maana Ilikuwa kuja kutembea tu?. Haikuwa misheni kama alivyokusudia? Mwanaume akanyanyuka na kujifuta machozi.

'Nimekuelewa mpenzi. Usijali. Najua Cha kufanya.' maneno Hayo yakamtoa mbio Mwamvita. Akatoka ndani huku akiomboleza.


Molio akawarejesha wakeze Kisiki kwenye kasri lao.

David Ngocho Samson
FB_IMG_1582711137383.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom