Kudo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2017
- 1,809
- 6,081
KABURINI AMA GEREZANI!
NA; BAHATI MWAMBA
SIMU; 0658564341/0758573660.
1: KIKAO…
Ilikuwa ni ndani ya baa moja maarufu sana ndani ya jiji la Dar es laam, baa ambayo milango yake haikuwahi kufungwa, iwe ahsubuhi, mchana ama usiku, burudani ziliendelea kama kawaida. Kilichokuwa kikibadilika kwenye baa ile ni wahudumu ambao walipeana nafasi ya kuhudumu kila baada ya saa nane. Wahudumu hao walikuwa kwenye jinsia zote, yaani walikuwepo wahudumu wa kike na wa kiume na walikuwa katika mgawanyo wa majukumu, wapo ambao kazi yao ilikuwa ni kuhudumia chakula, wengine vinywaji vikali na laini, wengine walihusika na kuchoma nyama tu huku wengine kazi yao ilikuwa ni kuhakikisha meza zote zipo safi muda wote. Kama zilivyo baa zingine kuwa na meneja, meneja wa baa ile alikuwa ni mtu mzima karibu miaka hamsini na tano hadi sitini, lakini alikuwa ni aina ya wazee ambao hawajawahi kukubali umri unanafasi kwenye maisha, wao waliibua msemo wao kwamba umri ni namba na walihalalisha huo msemo ili wapate nafasi ya kuyarudi ya ujanani na vijana wadogo ama mabinti wadogo.
Meneja huyo ambae wafanyakazi wake waliamua kumpachika jina la Baba usinipite, alijikuta akilowea kwenye maisha ya anasa na kuiweka kazi kama pitio la kuharakisha anasa zake, kwa tabia yake hiyo alijikuta akilazimika kuwa nje ya kazi kwa saa nyingi zaidi, hapo ndipo alipopata wazo la kumwamini mmoja wa wafanyakazi wake, na turufu hiyo ikamuangukia kijana mtiifu ambae wenzake walimfahamu kwa jina la Gunga. Gunga halikuwa jina lake halisi na hakuna aliyewahi kulijua jina lake kwenye hayo mazingira yake ya kazi. Umri wake ulikuwa kwenye makadirio ya miaka ishirini na nane hadi thelathini.
Elimu yake ilikuwa ni elimu ya chuo kikuu na aliwahi kufanya kazi kwenye kampuni fulani wakati akingojea ajira, ajira hazikutoka na bahati mbaya kampuni aliyokuwa akiifanyia kazi ikatetereka kiuchumi na wafanyakazi wakapunguzwa na yeye akiwa mmoja wao. Kazi aliyoifanya kwa miaka mitatu ikaota mbawa na bahati mbaya zaidi wakati huo alikuwa ameshaoa, alimuoa mwanamke wake wa tangu balehe. Tangu asimamishwe kazi ilikuwa imekatika miaka miwili na miezi sita, ukiunganisha na ile miaka mitatu ya kazi na na ndoa, jumla ilikuwa miaka mitano na miezi sita.
Gunga kwenye ile baa alikuwa na zaidi ya miezi tisa, kazi yake ilikuwa ni kuhakikisha meza zote zinakuwa safi wakati wote na jioni alikuwa anapewa ujira wa shilingi elfu tatu hadi elfu tano kama posho ya kazi aliyoifanya. Kitendo cha meneja wake kumuamini na kumuongezea jukumu la kusimamia ile baa wakati akiwa hayupo, kwake ilikuwa ni furaha kubwa. Posho yake iliongezeka na kuwa elfu saba hadi elfu kumi na wakati mwingine hadi elfu kumi na tano. Saa za kazi nazo zikaongezeka na wakati mwingine alikesha na wakati mwingine alilazimika kutoka usiku mnene.
Licha ya kuwa msaidizi wa kuaminika wa meneja, lakini Gunga hakuwahi kuzidisha posho yake wala hakuwahi kutamani kujiongeza kwa kupiga pesa kwa namna yoyote, alikuwa mwaminifu haswaa kiasi hata chenji ya shilingi hamsini alihakikisha haibaki mfukoni mwake. Wafanyakazi walimpenda na wateja walimpenda, alipendwa na kila mtu hapo kazini kwake. Licha ya kuwa na nyota ya kupendwa lakini hakuna aliyewahi kujua anaishi wapi wala hakuna aliyewahi kujua anamke nyumbani, tena mke wa ndoa, yote tisa, kumi ni kwamba hakuwa akiifurahia ndoa yake, aliishi kwa karaha kubwa lakini licha ya karaha hizo, hakuwahi kuinua mdomo wake na kumtusi mke wake wala kumpiga, ijapokuwa, mke wake alikuwa akimtusi na kumkejeli sana. Kwa nini? Kwa sababu mke wake ndiye alikuwa kichwa cha familia ya watu wawili tu, hawakuwahi kupata mtoto na sababu siyo kama walikuwa wagonjwa, la hasha, sababu ni mwanamke hakuwa tayari kuzaa kwa sababu aliamini mume wake hawezi kumtunza mtoto.
Siku hiyo akiwa amekaa kwenye kaunta ya meneja huku macho yake yakitalii huku na huko kuhakikisha wahudumu wapo kwenye maeneo yao, kumbukumbu za maisha yake na mke wake zikamzonga, akatikisa kichwa kupambana nazo lakini hakufua dafu, zikambeba.
“Siwezi kuzaa na mwanaume ambae najua hawezi kununua nepi ya elfu moja.” Ilikuwa ni kauli chungu kutoka kwenye kinywa cha mke wa Gunga, tena haikuishia kuwa kauli tu bali na msonyo ulifuatia huku macho ya mke wake yakicheza kinyalinyali, kama haikutosha, mwanamke akajigeuza na kumsukuma mwanaume kwa guu lake la kulia, Gunda akaenda chini kitako kutoka sofani alipokuwa amekaa na mke wake.
“Lakini wewe ni mke wangu halali kabisa, kwa nini unanifanyia hivi? Kwa nini hutaki kuzaa na mimi ambae nimefunga ndoa na wewe?” Gunga alimuuliza mkewe huku akiinuka kutoka chini. Mwanamke akasimama na kushika kiuno, mishipa ya uso ikiwa imemsimama kama kiazi kitamu kilichopigwa na jua la saa saba mchana.
“Eti mke wako, ni lini umenipeleka saluni? Lini umekuja na nguo ya dukani, lini umewahi kununua hata mafuta ya kulembesha midomo yangu? Umewahi kununua vocha angalau nitume ujumbe mfupi?” Mwanamke alimkoromea huku akitikisa kalio moja kwa namna ya kusuta.
“Lakini vyote ulivipata wakati nina kazi, hata sasa sina kazi lakini nguo za Mwenge najitahidi kupitia ila huwa unazikataa, unataka niibe?” Gunga aliongea kinyonge.
“Ukiiba nitakuwa wa kwanza kukukamata na kukutia ndani, mwanaume pambana…. Au una hawara mahali fulani ambae unamjali? Ratiba zako zimebadilika siku hizi na sijui huwa usiku unatoka wapi na unakaidi amri yangu ya kukutaka urudi nyumbani kabla sijafika kutoka kazini.”
Gunga alitabasamu kidogo kisha akamtazama mke wake kwa sekunde kadhaa na kusema,..
“Unataka nichakarike na bado unataka niwahi kurudi nyumbani kama kondoo. Usijisahau ukahisi umeota ndevu na unaweza kunifanya lolote.” Alipiga hatua na kuelekea chumbani akiwa anasindikizwa na maneno ya kejeli na dhihaka kutoka kwa mke wake, hakujali, aliingia chumbani na kujitupa kitandani, mawazo yakambeba.
“Mh!” Gunga alijikuta akiguna peke yake huku akirejesha mawazo ndani ya eneo lake la kazi, akazungusha macho yake huku na huko na mwisho akaishia kuinua mkono wake wa kushoto na kutazama majira ya saa yake, ilikuwa inakaribia kutimia saa tano na dakika arobaini na tano usiku. Akashuka kwenye kiti na kuutazama mlango wa VIP, akafikiria kidogo kisha akainua mguu wake na kusogea karibu na mlango ule ambao kwa siku hiyo ulipambwa na kibao kilichokuwa kimeandikwa.. ‘CLOSED' ilimaanisha hakukutakiwa mtu kuingia huko na kwa siku hiyo wale wanaopenda kujikweza maeneo ya starehe, hawakuruhusiwa kabisa kwa madai kwamba, kulikuwa na matengenezo kidogo ndani ya ukumbi huo mdogo ndani ya baa hiyo maarufu jijini Dar es laam.
Gunga alifika hadi mlangoni na kisha akatoa ufunguo na kuingiza kwenye kitasa cha mlango, akazungusha na kabali za kitasa zikaachia kisha akausukuma mlango na kuingia ndani. Dakika tano zilikatika akiwa huko VIP, dakika ya sita akatokea mlangoni na kuuacha bila kuufunga, aliugesha.
Alirejea kwenye kiti cha meneja huku macho yake yakiwa kwenye mlango wa kuingilia ndani ya baa. Akili yake akaiweka hapo licha ya sekunde chache kulazimika kuzungusha kichwa huku na huko ili kuhakikisha kazi zinaendelea. Licha ya watu kuwa wengi na wengine kuinuka na kucheza, lakini jicho lake lilikuwa makini sana na mlango wa kuingilia na alikuwa akimuona kila aliyekuwa akiingia na kutoka. Gunga kuna jambo alikuwa analisubiri na alilitarajia kuanzia saa sita za usiku, muda ambao tarehe hubadilika.
NA; BAHATI MWAMBA
SIMU; 0658564341/0758573660.
1: KIKAO…
Ilikuwa ni ndani ya baa moja maarufu sana ndani ya jiji la Dar es laam, baa ambayo milango yake haikuwahi kufungwa, iwe ahsubuhi, mchana ama usiku, burudani ziliendelea kama kawaida. Kilichokuwa kikibadilika kwenye baa ile ni wahudumu ambao walipeana nafasi ya kuhudumu kila baada ya saa nane. Wahudumu hao walikuwa kwenye jinsia zote, yaani walikuwepo wahudumu wa kike na wa kiume na walikuwa katika mgawanyo wa majukumu, wapo ambao kazi yao ilikuwa ni kuhudumia chakula, wengine vinywaji vikali na laini, wengine walihusika na kuchoma nyama tu huku wengine kazi yao ilikuwa ni kuhakikisha meza zote zipo safi muda wote. Kama zilivyo baa zingine kuwa na meneja, meneja wa baa ile alikuwa ni mtu mzima karibu miaka hamsini na tano hadi sitini, lakini alikuwa ni aina ya wazee ambao hawajawahi kukubali umri unanafasi kwenye maisha, wao waliibua msemo wao kwamba umri ni namba na walihalalisha huo msemo ili wapate nafasi ya kuyarudi ya ujanani na vijana wadogo ama mabinti wadogo.
Meneja huyo ambae wafanyakazi wake waliamua kumpachika jina la Baba usinipite, alijikuta akilowea kwenye maisha ya anasa na kuiweka kazi kama pitio la kuharakisha anasa zake, kwa tabia yake hiyo alijikuta akilazimika kuwa nje ya kazi kwa saa nyingi zaidi, hapo ndipo alipopata wazo la kumwamini mmoja wa wafanyakazi wake, na turufu hiyo ikamuangukia kijana mtiifu ambae wenzake walimfahamu kwa jina la Gunga. Gunga halikuwa jina lake halisi na hakuna aliyewahi kulijua jina lake kwenye hayo mazingira yake ya kazi. Umri wake ulikuwa kwenye makadirio ya miaka ishirini na nane hadi thelathini.
Elimu yake ilikuwa ni elimu ya chuo kikuu na aliwahi kufanya kazi kwenye kampuni fulani wakati akingojea ajira, ajira hazikutoka na bahati mbaya kampuni aliyokuwa akiifanyia kazi ikatetereka kiuchumi na wafanyakazi wakapunguzwa na yeye akiwa mmoja wao. Kazi aliyoifanya kwa miaka mitatu ikaota mbawa na bahati mbaya zaidi wakati huo alikuwa ameshaoa, alimuoa mwanamke wake wa tangu balehe. Tangu asimamishwe kazi ilikuwa imekatika miaka miwili na miezi sita, ukiunganisha na ile miaka mitatu ya kazi na na ndoa, jumla ilikuwa miaka mitano na miezi sita.
Gunga kwenye ile baa alikuwa na zaidi ya miezi tisa, kazi yake ilikuwa ni kuhakikisha meza zote zinakuwa safi wakati wote na jioni alikuwa anapewa ujira wa shilingi elfu tatu hadi elfu tano kama posho ya kazi aliyoifanya. Kitendo cha meneja wake kumuamini na kumuongezea jukumu la kusimamia ile baa wakati akiwa hayupo, kwake ilikuwa ni furaha kubwa. Posho yake iliongezeka na kuwa elfu saba hadi elfu kumi na wakati mwingine hadi elfu kumi na tano. Saa za kazi nazo zikaongezeka na wakati mwingine alikesha na wakati mwingine alilazimika kutoka usiku mnene.
Licha ya kuwa msaidizi wa kuaminika wa meneja, lakini Gunga hakuwahi kuzidisha posho yake wala hakuwahi kutamani kujiongeza kwa kupiga pesa kwa namna yoyote, alikuwa mwaminifu haswaa kiasi hata chenji ya shilingi hamsini alihakikisha haibaki mfukoni mwake. Wafanyakazi walimpenda na wateja walimpenda, alipendwa na kila mtu hapo kazini kwake. Licha ya kuwa na nyota ya kupendwa lakini hakuna aliyewahi kujua anaishi wapi wala hakuna aliyewahi kujua anamke nyumbani, tena mke wa ndoa, yote tisa, kumi ni kwamba hakuwa akiifurahia ndoa yake, aliishi kwa karaha kubwa lakini licha ya karaha hizo, hakuwahi kuinua mdomo wake na kumtusi mke wake wala kumpiga, ijapokuwa, mke wake alikuwa akimtusi na kumkejeli sana. Kwa nini? Kwa sababu mke wake ndiye alikuwa kichwa cha familia ya watu wawili tu, hawakuwahi kupata mtoto na sababu siyo kama walikuwa wagonjwa, la hasha, sababu ni mwanamke hakuwa tayari kuzaa kwa sababu aliamini mume wake hawezi kumtunza mtoto.
Siku hiyo akiwa amekaa kwenye kaunta ya meneja huku macho yake yakitalii huku na huko kuhakikisha wahudumu wapo kwenye maeneo yao, kumbukumbu za maisha yake na mke wake zikamzonga, akatikisa kichwa kupambana nazo lakini hakufua dafu, zikambeba.
“Siwezi kuzaa na mwanaume ambae najua hawezi kununua nepi ya elfu moja.” Ilikuwa ni kauli chungu kutoka kwenye kinywa cha mke wa Gunga, tena haikuishia kuwa kauli tu bali na msonyo ulifuatia huku macho ya mke wake yakicheza kinyalinyali, kama haikutosha, mwanamke akajigeuza na kumsukuma mwanaume kwa guu lake la kulia, Gunda akaenda chini kitako kutoka sofani alipokuwa amekaa na mke wake.
“Lakini wewe ni mke wangu halali kabisa, kwa nini unanifanyia hivi? Kwa nini hutaki kuzaa na mimi ambae nimefunga ndoa na wewe?” Gunga alimuuliza mkewe huku akiinuka kutoka chini. Mwanamke akasimama na kushika kiuno, mishipa ya uso ikiwa imemsimama kama kiazi kitamu kilichopigwa na jua la saa saba mchana.
“Eti mke wako, ni lini umenipeleka saluni? Lini umekuja na nguo ya dukani, lini umewahi kununua hata mafuta ya kulembesha midomo yangu? Umewahi kununua vocha angalau nitume ujumbe mfupi?” Mwanamke alimkoromea huku akitikisa kalio moja kwa namna ya kusuta.
“Lakini vyote ulivipata wakati nina kazi, hata sasa sina kazi lakini nguo za Mwenge najitahidi kupitia ila huwa unazikataa, unataka niibe?” Gunga aliongea kinyonge.
“Ukiiba nitakuwa wa kwanza kukukamata na kukutia ndani, mwanaume pambana…. Au una hawara mahali fulani ambae unamjali? Ratiba zako zimebadilika siku hizi na sijui huwa usiku unatoka wapi na unakaidi amri yangu ya kukutaka urudi nyumbani kabla sijafika kutoka kazini.”
Gunga alitabasamu kidogo kisha akamtazama mke wake kwa sekunde kadhaa na kusema,..
“Unataka nichakarike na bado unataka niwahi kurudi nyumbani kama kondoo. Usijisahau ukahisi umeota ndevu na unaweza kunifanya lolote.” Alipiga hatua na kuelekea chumbani akiwa anasindikizwa na maneno ya kejeli na dhihaka kutoka kwa mke wake, hakujali, aliingia chumbani na kujitupa kitandani, mawazo yakambeba.
“Mh!” Gunga alijikuta akiguna peke yake huku akirejesha mawazo ndani ya eneo lake la kazi, akazungusha macho yake huku na huko na mwisho akaishia kuinua mkono wake wa kushoto na kutazama majira ya saa yake, ilikuwa inakaribia kutimia saa tano na dakika arobaini na tano usiku. Akashuka kwenye kiti na kuutazama mlango wa VIP, akafikiria kidogo kisha akainua mguu wake na kusogea karibu na mlango ule ambao kwa siku hiyo ulipambwa na kibao kilichokuwa kimeandikwa.. ‘CLOSED' ilimaanisha hakukutakiwa mtu kuingia huko na kwa siku hiyo wale wanaopenda kujikweza maeneo ya starehe, hawakuruhusiwa kabisa kwa madai kwamba, kulikuwa na matengenezo kidogo ndani ya ukumbi huo mdogo ndani ya baa hiyo maarufu jijini Dar es laam.
Gunga alifika hadi mlangoni na kisha akatoa ufunguo na kuingiza kwenye kitasa cha mlango, akazungusha na kabali za kitasa zikaachia kisha akausukuma mlango na kuingia ndani. Dakika tano zilikatika akiwa huko VIP, dakika ya sita akatokea mlangoni na kuuacha bila kuufunga, aliugesha.
Alirejea kwenye kiti cha meneja huku macho yake yakiwa kwenye mlango wa kuingilia ndani ya baa. Akili yake akaiweka hapo licha ya sekunde chache kulazimika kuzungusha kichwa huku na huko ili kuhakikisha kazi zinaendelea. Licha ya watu kuwa wengi na wengine kuinuka na kucheza, lakini jicho lake lilikuwa makini sana na mlango wa kuingilia na alikuwa akimuona kila aliyekuwa akiingia na kutoka. Gunga kuna jambo alikuwa analisubiri na alilitarajia kuanzia saa sita za usiku, muda ambao tarehe hubadilika.