Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,845
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 49
" Fantastic!!!, Big up Mwanasheria mlevi kwa ugunduzi lazima tuingie humu"
"Hallo, Inspekta Jasmin bado upo hewani, njooni haraka sana Sabasaba" Daniel alisema.
Jasmin hakuwa na haja ya kuuliza kulikuwa na nini? Alikuwa amesikia kila kitu katika simu yake.
"Dokta Yusha twende Sabasaba fasta" Jasmin alisema.
"Kuna nini?" Dokta Yusha aliuliza.
"Nitakusimulia njiani"
Dakika kumi tu zilitosha kuwafikisha wakina Jasmin Sabasaba. Waliungana na wakina Daniel kuanza kuichunguza chemba ile ambayo Mwanasheria mlevi aligundua kwamba ilikuwa ni njia ya kuelekea chini ambapo bila shaka kulikuwa na handaki.
"Sasa yatupasa tuingie hapa. Maana tumejaribu kuchunguza maeneo ya jirani labda njia hii itakuwa imetokea mahali lakini hatujaona. Inaonesha ni njia ya chini iliyoenda mbali kidogo. Lazima tuingie tukawakamate hawa wanaharam" Daniel alisema.
"Tuingie wote?" Mwanasheria mlevi aliuliza. " Vipi kuhusu msako wa kumsaka Elizabeth Neville huku juu? Kwanini wasiingie wachache na wengine waendelee kumsaka Elizabeth? "
"Come on Mwanasheria! Bila ya shaka hawa watu ndio watakuwa wamemteka Elizabeth Neville pale hospitali. Tukienda na kuwaangamiza hawa tutakuwa tumemwokoa na Elizabeth. Tuingie tu humu tukaumalize mchezo" Jasmin alisema.
"Mpo kamili?" Daniel aliuliza. " Hatujui tunaenda wapi? Tunaenda kupambana na watu wa aina gani? Na wapo wangapi? Tunaenda kuweka rehani roho zetu kwa ajili ya Taifa letu. Wahitajika umakini mkubwa sana, kosa lolote lile haliruhusiwi, marufuku kufanya hata kosa dogo sana" Daniel alimalizia kwa kuonya.
Wote waliitikia kwa kichwa na kuanza kuingia kwenye lile shimo ambalo lilielekea kusikojulikana.
Mwanaume, Daniel Mwaseba ndiye alitangulia kuingia mle shimoni. Baada ya kuufunua mfuniko wa pale juu walikuta ngazi ambazo zilithibitisha hisia za Mwanasheria. Lile halikuwa shimo la kawaida. Daniel alishuka zile ngazi taratibu huku akiwa ameishika imara bastola yake kwa mkono wa kulia. Alikanyaga ngazi ya kwanza, kisha ya pili na Dokta Yusha nae akiwa na begi lake mgingoni akifuata nyuma yake. Na bastola yake iliyojaa risasi ikiwa kaishikililia kwa mkono wa kulia. Wakati Daniel anaikanyaga ardhi ya kule chini huku juu Mwanasheria mlevi ndiye aliyekuwa anaingia akiwa ametanguliwa na askari makini wa kike, Inspekta Jasmin. Mwanasheria mlevi kwa mkono wake wa kushoto alikuwa ameishikia bastola yake tayari kwa lolote lile. Dakika nne baadae wote waliikanyaga ardhi wakiwa shimoni. Kote kulikuwa na giza totoro.
Daniel aliitoa kalamu ndogo katika mfuko wake wa shati. Aliibonyaza. Mwanga mkali ulimulika kule chini. Ile kalamu ilikuwa ni kalamu ya ajabu sana. Kalamu iliyokuwa imetengenezwa kwa teknolojia ya hali ya juu huko nchini Urusi.
" Fantastic!!!, Big up Mwanasheria mlevi kwa ugunduzi lazima tuingie humu"
"Hallo, Inspekta Jasmin bado upo hewani, njooni haraka sana Sabasaba" Daniel alisema.
Jasmin hakuwa na haja ya kuuliza kulikuwa na nini? Alikuwa amesikia kila kitu katika simu yake.
"Dokta Yusha twende Sabasaba fasta" Jasmin alisema.
"Kuna nini?" Dokta Yusha aliuliza.
"Nitakusimulia njiani"
Dakika kumi tu zilitosha kuwafikisha wakina Jasmin Sabasaba. Waliungana na wakina Daniel kuanza kuichunguza chemba ile ambayo Mwanasheria mlevi aligundua kwamba ilikuwa ni njia ya kuelekea chini ambapo bila shaka kulikuwa na handaki.
"Sasa yatupasa tuingie hapa. Maana tumejaribu kuchunguza maeneo ya jirani labda njia hii itakuwa imetokea mahali lakini hatujaona. Inaonesha ni njia ya chini iliyoenda mbali kidogo. Lazima tuingie tukawakamate hawa wanaharam" Daniel alisema.
"Tuingie wote?" Mwanasheria mlevi aliuliza. " Vipi kuhusu msako wa kumsaka Elizabeth Neville huku juu? Kwanini wasiingie wachache na wengine waendelee kumsaka Elizabeth? "
"Come on Mwanasheria! Bila ya shaka hawa watu ndio watakuwa wamemteka Elizabeth Neville pale hospitali. Tukienda na kuwaangamiza hawa tutakuwa tumemwokoa na Elizabeth. Tuingie tu humu tukaumalize mchezo" Jasmin alisema.
"Mpo kamili?" Daniel aliuliza. " Hatujui tunaenda wapi? Tunaenda kupambana na watu wa aina gani? Na wapo wangapi? Tunaenda kuweka rehani roho zetu kwa ajili ya Taifa letu. Wahitajika umakini mkubwa sana, kosa lolote lile haliruhusiwi, marufuku kufanya hata kosa dogo sana" Daniel alimalizia kwa kuonya.
Wote waliitikia kwa kichwa na kuanza kuingia kwenye lile shimo ambalo lilielekea kusikojulikana.
Mwanaume, Daniel Mwaseba ndiye alitangulia kuingia mle shimoni. Baada ya kuufunua mfuniko wa pale juu walikuta ngazi ambazo zilithibitisha hisia za Mwanasheria. Lile halikuwa shimo la kawaida. Daniel alishuka zile ngazi taratibu huku akiwa ameishika imara bastola yake kwa mkono wa kulia. Alikanyaga ngazi ya kwanza, kisha ya pili na Dokta Yusha nae akiwa na begi lake mgingoni akifuata nyuma yake. Na bastola yake iliyojaa risasi ikiwa kaishikililia kwa mkono wa kulia. Wakati Daniel anaikanyaga ardhi ya kule chini huku juu Mwanasheria mlevi ndiye aliyekuwa anaingia akiwa ametanguliwa na askari makini wa kike, Inspekta Jasmin. Mwanasheria mlevi kwa mkono wake wa kushoto alikuwa ameishikia bastola yake tayari kwa lolote lile. Dakika nne baadae wote waliikanyaga ardhi wakiwa shimoni. Kote kulikuwa na giza totoro.
Daniel aliitoa kalamu ndogo katika mfuko wake wa shati. Aliibonyaza. Mwanga mkali ulimulika kule chini. Ile kalamu ilikuwa ni kalamu ya ajabu sana. Kalamu iliyokuwa imetengenezwa kwa teknolojia ya hali ya juu huko nchini Urusi.