Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 153,149
- 454,448
- Thread starter
- #541
SEHEMU YA 101
“Haya nashukuru, waweza kundoka.” Nilimwambia. Tatu alipondoka, nikarudi macho kwenye kile kipande cha karatasi na kusoma maandishi yaliyoandikiwa na Nasra Mfaume.
Mke wangu wa zamani. Ujumbe ule ulikuwa ulisomeka hivi: Mpenzi Faraji. Awali ya yote nakupa pole kwa shughuli za mchana kutwa. Dhumuni la ujumbe huu ni kukueleza machache juu ya hatima yangu nawe, mpenzi.
Tangu nimefahamiana ni nyakati chache sana ilipatikana furaha baina yetu, muda mwingi tumepitia katika machozi na maumivu makali. Utukufu wa ndoa yangu niliukanyagia viatu vya maliwato, nimesalimu amri kushindwa kwa kushindwa kuuteka moyo wako .
Nitajiulumu mwenyewe kwa mpumbavu huo milele. Utoto na ushamba wa mji ulinifanya nilivamie jiji ambalo lilinipokea kwa uso wa tabasamu, jiji likanitafuna kisha likanitema kama ganda la muwa.
Kila mmoja anahadithi yake yenye maumivu maishani na moyo unatudhihirishia ni kiungo pekee chenye kujali na kuhifadhi hisia.
Matatizo ni kioo, hata wazuri na wabaya hujitazama kwa jicho tofauti, lakini hakuna anayejisifu mbele ya kioo hicho. tunaishi kwakuwa tulikosea, maisha ni makosa na msamaha ni furaha.
Faraji mpenzi, nisikuchoshe kwa semi za Kiswahili na tungo zenye kufikirisha akili, jambo kubwa napenda utambue ni hili: Kuanzia sasa nitakuwa mbali na wewe milele.
Nimepata mwanaume mwingine mswalihina, mwenyeji wa huko Chakechake Zanzibar Kisiwani Pemba, nimekiri makosa yangu yote kwakwe, yuko amekuwa radhi na mimi na natarajia kufunga naye ndoa. Faraji baba, naomba umtunze vema mtoto wetu, Mwanda, hata wewe pia ujitunze.
Nimeshindwa kumlea mwanangu. Tunu pekee niliyopewa na Mungu. Acha basi niawachie wenzangu wafanye kazi hiyo, mchunge na mlinde na hila za mama wa kambo.
Mwisho napenda nikuombe radhi kwa makosa mengi niliyokutendea maishani mwako, lakini pia nakusihi uache pombe, na utafute mwanamke mwingine mwema uoe.
Ni mimi mkeo wa zamani.
NASRA MFAUME.
Nilirudia tena kusoma ule ujumbe, kadiri nilivyokuwa nikiyapitia maandishi yale ilikuwa ni kama vile naisikia sauti ya Nasra ikinieleza waziwazi maneno yale.
“Haya nashukuru, waweza kundoka.” Nilimwambia. Tatu alipondoka, nikarudi macho kwenye kile kipande cha karatasi na kusoma maandishi yaliyoandikiwa na Nasra Mfaume.
Mke wangu wa zamani. Ujumbe ule ulikuwa ulisomeka hivi: Mpenzi Faraji. Awali ya yote nakupa pole kwa shughuli za mchana kutwa. Dhumuni la ujumbe huu ni kukueleza machache juu ya hatima yangu nawe, mpenzi.
Tangu nimefahamiana ni nyakati chache sana ilipatikana furaha baina yetu, muda mwingi tumepitia katika machozi na maumivu makali. Utukufu wa ndoa yangu niliukanyagia viatu vya maliwato, nimesalimu amri kushindwa kwa kushindwa kuuteka moyo wako .
Nitajiulumu mwenyewe kwa mpumbavu huo milele. Utoto na ushamba wa mji ulinifanya nilivamie jiji ambalo lilinipokea kwa uso wa tabasamu, jiji likanitafuna kisha likanitema kama ganda la muwa.
Kila mmoja anahadithi yake yenye maumivu maishani na moyo unatudhihirishia ni kiungo pekee chenye kujali na kuhifadhi hisia.
Matatizo ni kioo, hata wazuri na wabaya hujitazama kwa jicho tofauti, lakini hakuna anayejisifu mbele ya kioo hicho. tunaishi kwakuwa tulikosea, maisha ni makosa na msamaha ni furaha.
Faraji mpenzi, nisikuchoshe kwa semi za Kiswahili na tungo zenye kufikirisha akili, jambo kubwa napenda utambue ni hili: Kuanzia sasa nitakuwa mbali na wewe milele.
Nimepata mwanaume mwingine mswalihina, mwenyeji wa huko Chakechake Zanzibar Kisiwani Pemba, nimekiri makosa yangu yote kwakwe, yuko amekuwa radhi na mimi na natarajia kufunga naye ndoa. Faraji baba, naomba umtunze vema mtoto wetu, Mwanda, hata wewe pia ujitunze.
Nimeshindwa kumlea mwanangu. Tunu pekee niliyopewa na Mungu. Acha basi niawachie wenzangu wafanye kazi hiyo, mchunge na mlinde na hila za mama wa kambo.
Mwisho napenda nikuombe radhi kwa makosa mengi niliyokutendea maishani mwako, lakini pia nakusihi uache pombe, na utafute mwanamke mwingine mwema uoe.
Ni mimi mkeo wa zamani.
NASRA MFAUME.
Nilirudia tena kusoma ule ujumbe, kadiri nilivyokuwa nikiyapitia maandishi yale ilikuwa ni kama vile naisikia sauti ya Nasra ikinieleza waziwazi maneno yale.