Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

SEHEMU YA 104

Mpenzi msomaji,mikasa yote hiyo ilinitokea kwa muda mchache mno, kama utakuwa ulinifatilia kwa makini, utabaini kwamba, kupolomoka kwangu kiuchumi kulitokea ndani ya masaa 72 tu.

Na sasa niliona natakiwa kuuza nyumba niliyokuwa nikiishi ili mtoto wangu apone.

Naam! ilikuwa ni lazima akafanyiwe upasuaji wa moyo nchini India. Zaidi ya milioni 22 za matibabu ilitakiwa ili mwanangu aendelee kuishi. Nifanye nini mimi!.

Nilijiuliza kimoyomoyo, mwanangu nilimwitaji sana maishani, lakini hata nyumba yangu pia sikupenda kuipoteza kabisa.

Nilikwenda kwenye ATM ya pale pale Muhimbili nikangalia kiasi cha fedha kilichosalia kwenye akaunti yangu.

Nikakuta nina milioni nane peke yake. Kwa hesabu za harakaharaka, nilikuwa bado nahitaji angalau milioni 15 ili kuyanusuru maisha ya Mwanda.

Niliwafikiria ndugu na marafiki zangu, nikaona naweza kujaribu kuomba msaada hata kwa kukopeshwa ili niweze kupata kiasi kile cha fedha.

Nilichofanya ni kuwasilina na watu wangu wa karibu. Waswahili wanao msemo usemao, siku ya kufa nyani, miti yote hueteleza.

Kila rafiki na ndugu niliyekuwa nikimgusa, naye alinibwagia matatizo yake lukuki.

Hadi jioni inatimu sikuwa nimepata mtu yeyote wa kunisaidia. Nilirudi wodini alipokuwa amelazwa mwanangu, nikaketi kando ya kitanda chake.

Mtoto wangu mzuri, alikuwa katika usingizi wa nusu kaputi. Alikuwa akipumua kwa kutumia Mashine maalumu za Oxjen, hata kula alitumia mipira.

Nikiwa pale, niliwasiliana na mama yangu, nikampa taarifa juu ya hali ya mtoto wangu na maamuzi ya mke wangu wa zamani Nasra.

Kunitelekezea mtoto na kwenda kuolewa na mwanaume mwingine huko visiwani pemba. “Mwanamke punguani kweli huyo, kaamua tena kumkimbia mwanaye!”

“Ndiye mke mliyekuwa mmenichagulia mama.” Kauli yangu ilimuumiza mno mama. Kupitia simu nikamsikia akinung’unika kwa makosa waliyoyafanya yeye na marehemu baba kunitafutia mke mpumbavu.
 
Sehemu ya 105

Nikajikuta namwonea huruma tena mama, nafsi yangu ikajilaumu kwa kumsimanga mzazi wangu.

Sikutakiwa kufanya hivyo. Hapakuwa na tija ya kuendeleza lawama kwa mama hasa ukizingatia mimi mwenyewe nilibariki mchakato wa kutafutiwa mke kutoka kijijini kwetu.

Kama ni makosa tuliyafanya sote. Kimsingi mimi na wazazi wangu, kwa pamoja tulipuyanga katika fikra za kutafutiana mke wa kuoa.

Kwa dunia ya leo jambo la kuoa ama kuolewa hubakia kwa mtu binafsi, vinginevyo ni kuingizana lawamani. “Basi mama usijilaumu, hayo yamekwishapita.”

“Hili kosa litaendelea kunitafuna siku zote maishani, kwa kweli tulikosea sana kukuchagulia mwanamke mjinga wa kiwango hicho.”mama alilalama.

“Kuna jambo nataka nikuombe mama,”nilimwambia, nikamwondoa kwenye mada zile za mke wangu. “Jambo gani?”

“Nahitaji uje Dar es salam, ubakie na mji wangu maana kwa hali ya uchumi inayonikabili itabidi tatu arudi kwao.” “Hilo liko ndani ya uwezo wangu, unajingine?” “Ni hilo tu, hakuna jingine.” Tulizungumza mambo mengi kisha tukaagana.

Nilichofanya baada ya kuagana na mama ni kurejea nyumbani kwa ajili ya kuoga na kubadili nguo kabla ya kurudi tena hospitali kumuguuza mtoto.

Nilipofika nyumbani, nilimkuta dada wa kazi, Tatu, akiendelea na majukumu yake ya kawaida ya nyumbani. Nilimwita na kuongea naye: “Kwanza Tatu nakushukuru kwa wema wote ambao unaotenda hapa nyumbani...”nilisema nikaendelea.

“Pili nasikitika kukwambia, itabidi tuvunje mkataba wa kazi kuanzia muda huu.” “Kwa nini baba, nitakwenda wapi mimi?” Tatu alihamaki.

“Usijali Tatum, nitakulipa stahiki zako zote.” “Kuna jambo nimekosea?” “Hakuna, Ila nina matatizo mengi sana Tatu, ukiendelea kufanya kazi hapa, itafikia hatua nitashindwa kukulipa mshahara wako.”

“Kivipi baba?” Nilimuhadithia kwa kifupi. Tatu akaridhika kwa shingo upande. Nikamlipa stahiki zake zote, kisha akakusanya kila kilicho chake na kuondoka. Wakati Tatu anaondoka, kwa kweli nuilijisikia vibaya, Tatu
 
Sehemu ya 106

Alininusuru na kifo pale nilipojaribu kujiua, ni Tatu aliyemsaidia mwanangu kwa kipindi kirefu sana hata nilipokuwa mbali naye. Leo alikuwa akiondoka. Sikuwa na namna.

***** Majibu ya daktari wa kitengo cha Moyo, Hopsitali ya Muhimbili alithibitisha na kuungana na yale majibu ya Hospitali ya Regency, mwanangu alikuwa na tatizo la moyo, kulikuwa na valve zilizokuwa zimezorota, hivyo alitakiwa kufanyiwa upasuaji ili kupandikiza mishipa mingine.

Wakati napewa majibu hayo, tayari nilikuwa nimekwisha pitisha uamuzi mgumu. Sikuwa tayari kabisa kuuza nyumba yangu ya Kinondoni. Nyumba ya ndoto zangu.

Kitu pekee nilichokuwa nimewaza ni kuweka rehani nyumba hiyo ya mamilioni ya fedha. Kuliko kuuza heri niweke rehani. Nilikuwa nikijiambia kimoyomoyo.

Na Hadi wakati huo nilikuwa nimekiwsha pata mahali pakwenda kupewa milioni 16 ambayo ningeongezea na ile milioni nane niliyokuwa nayo benki.

Nilichofanya baada ya kupewa majibu ya mwanangu, nilikwenda kwenye tasisi ya mikopo iitwayo Wezesha mzawa, ipo Sinza.

Nikajaza fomu na kuandika barua ya kuomba mkopo, siku tatu badaye nikabidhi hati ya nyumba, kisha nikapewa kiasi kile cha fedha.

Upesi sana nilianza kufanya mchakato wa wa safari ya India, na kwa kuwa nilikuwa na pesa mkononi, hakuna kilichonikwamisha.

Baada ya kukamilisha masuala yote ya viza na passport, nikalipia kabisa matibabu ya mwanangu kupitia benki za kimataifa. Siku chache zilizofuata nilikuwa ndani ya ndege ya shirika la Fly Emerates Airlines
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom