Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

SEHEMU YA 98

Kila wakati Nasra alisema neno nisamehe, ikafikia hatua nikahisi huenda Nasra anakazana kuniomba msamaha katika kipindi kile kigumu kwangu akiamini inaweza kuwa faida kwakwe kwa kuwa nilikuwa napitia nyakati ninazo hitaji faraja. Maisha yaliendelea.

Siku moja nikapata taarifa kuwa lile duka langu la posta la vipodozi, lilikuwa likitaifishwa na maofisa wa TRA. Aliyenipa taarifa alikuwa ni muuzaji wangu. Upesi nikaendesha gari kueleekea posta.

Duka lile ndio kitega uchumi pekee nilichokuwa nimebakiza na ninachotegemea kuendesha maisha yangu. Nilipofika, nilikuta maofisa wa TRA wakifungasha bidhaa na kupakia kwenye gari lao.

Ofisa mmoja akanipa dokomenti inayoonesha nimekuwa nikikwepa kulipa kodi ya serikali kwa zaidi ya miaka mitatu.

“Mungu wangu!” nilimaka. Nilijaribu kuwasihi wale maofisa wanipe siku kadhaa niweze kulipa kodi yao, lakini wa wapi. Jamaa waligoma kabisa.

Duka la posta nalo likataifishwa na serikali. Kwa kweli ulikuwa ni mwaka mbaya sana. Nilikuwa napitia nyakati zenye mitihani mizito mno kwenye maisha yangu ya ujana.

Nilirudi nyumbani nikiwa nimechanganyikiwa sana. Siku hiyo nilikwenda baa, nikanywa pombe nyingi ili kupoteza mawazo, nilirudi nyumbani usiku mkubwa nikiwa nimelewa chakari.

Dalili za kuanguka na kuishi maisha ya kifukara ikawa inanukia, kwa kweli sikuwa tayari kuona hali hiyo inatokea. Siku ya pili asubuhi, tayari nilikuwa nimepata wazo moja. Kuuza gari langu.

Nikawa endapo nitauza lile gari naweza kupata sio chini ya milioni 12 nikaona nikiongezea pesa iliyo katika akaunti yangu ya benki naweza kuwa na kiasi cha kutosha cha kuanzisha mradi utakao nikwamua.

Nilimpigia simu rafiki yangu mmoja anaitwa George, huyo huwa ni dalali wa kuuza magari, nilipanga nimpe kazi ya kunitafutia mteja wa gari langu.

Bahati mbaya Simu yake ilikuwa ikiita muda mwingi bila kupokelewa, kwa vile nilikuwa nikitambua wapi pakumpatia niliamua kumfuata. La charse pub, Sinza.

Ilikuwa ni majira kama ya saa moja jioni, siku, nakumbuka ilikuwa ni jumamosi, nilipofika pale, nikakuta maegesho ya magari yamejaa, nilichofanya ni kutafuta sehemu nyingine karibu na pale na kupaki gari langu.
 
SEHEMU YA 99

Nilipoingia ndani ya baa ile wala haikupita muda mrefu, nikampta George.

Baada ya salamu na stori za hapa na pale nikamweleza shida yangu. “Kwa hiyo gari lenyewe liko wapi?” akaniuliza. “Lipo nyuma hapo nimekuja nalo.” “Twende tukalione.” Tukaongozana hadi nje.

Lahaula!! pale nilipokuwa nimepaki, gari halikuwepo! “Liko wapi gari!” nilimaka. George akabaki akinishangaa. NILIHISI akili inanizunguka kwa kasi sana, kwa muda mfupi, nikatambua gari langu lilikuwa limeibwa.

Bila kutaraji nilijikuta naketi chini kitako, nikanyoosha miguu kisha nikaangua kilio kama mtoto mdogo. Ndani ya nusu dakika watu walifurika kama siafu, wakanizunguka.

Goerge akawa na kazi moja tu. Kuwaelezea kisanga kilichonikuta. “Amekutwa na nini?” watu waliuliza. “Ameibiwa gari lake.” “Wapi?” “Hapahapa.” “Aina gani?”

“Ni Land Rover Discovery 3 la rangi nyeusi” “Hilo gari niliona wakati limepaki hapa, lakini muda mfupi badaye nikaona linatoka, sikuona aliyekuwa anaendesha, na pia sikujua kama ndio linaibwa.”

Mtu mmoja alisema. “Itabidi tukatoe taarifa polisi.”George alinishauri. Nilisimama wima, nilikuwa nimetapakaa vumbi, na kwa kweli nilikuwa nimeghafirika vibaya sana.

Tukaelekea kituo cha polisi cha mabatini na kufungua RB. Kama mjuavyo taratibu za kipolisi wa nchi yetu, baada ya kufungua jarida la kesi, nikaambiwa nirudi siku inayofuatia ili nikutane na mpepelezi ambaye atakabidhiwa shauri langu.

Tukio lile lilichukuliwa kawaida tu askari polisi, hakuna aliyeonesha kustushwa, ilikuwa ni kama kuibiwa kuku tu mtaani. Nilirejea nyumbani nikiwa nimezodoka, mwili na nafsi.

Nilikuwa napitia mkandamizo mkubqwa sana maishani. Niliwasili nyumbani kwangu na kuingia ndani, nyumba niliiona ilikuwa kubwa mno, halafu ilikuwa impooza. Tofauti na siku nyingine, siku hiyo niliona upweke umezidi zaidi.

Zadi ya mtoto wangu Mwanda na dada wa kazi, hapakuwa na mtu mwingine aliyekuwa akiishi nyumbani kwangu. Kiu ya faraja ikanizidi, kwa masaa mchache nilikuwa nimepitia majaribu makubwa. Maisha yangu yalikuwa yamevurugika kwa kasi sana.
 
SEHEMU YA 100

Niliketi sofani, Tatu akaniletea kinywaji cha baridi, baada ya kupiga fundo refu, binti yule alibakia amesimama kando akiniangalia ninavyo kunywa maji, halafu akaniambia:

“Baba tangu ulivyoondoka mtoto amekuwa akilalamika kifua kinamuuma.” Alisema.

Nilitamani nimtandike vibao yule binti kwa kuniletea taarifa mpya zilizozidi kukoroga mtima wangu. “Anaendeleaje?”

nikaunguruma. “Kwa sasa amelala, lakini hali yake sio nzuri.” “Umempa dawa za maumivu?” “Nimempa lakini aliendelea kulalamikia.” “Kesho nitampeleka hospitali.” nilisema.

Japo binti alikuwa akinipa taarifa muhimu, ila niliona kama mwenye kuniongezea gozigozi kwa makusudi kabisa. “Huondoki?” Niliongea kwa ukali baada ya kuona ameendelea kunisimamia kama mlingoti.

“Baba,” aliniita katika namna ya mashaka na wasiwasi. Nikageuka. Nikamwangalia kwa jicho lililosema, nini shida. “Mama alikuja leo.” “Nani?” “Nasra, mama Mwanda.”

“Anasemaje?” niliunguruma sikupenda kabisa kusikia habari za mke wangu yule wa zamani. Na sikupenda kuendelea kuzungumza na binti yule wa kazi wasaa ule.

“Alikusubiri sana, lakini baada ya kuona unakawia aliamua kukuachia ujumbe huu hapa.” Alinipa kipande cha karatasi.

Ujumbe kutoka kwa Nasra. lakini vipi aniachie ujumbe kwa njia ya karatasi ambayo ipo uchi. Bila bahasha. Ingawa sikujua kilichokuwa kimeandikwa ni maneno yahusuyo jambo gani, lakini sikuvutiwa na njia aliyotumia kunifikisha ujumbe ule.

Karatasi isiyo na bahasha.Ilikuwa ni njia ambayo siyo faragha. “Umeandika nini?” nilimuliza swali la kijinga. “Hata sijasoma.” “Kwa nini hakunipigia simu?”

“Alikupigia lakini simu yako ilikuwa haipatikani.” Kauli ile ikanikumbusha kuwa simu, nayo ilikuwa kwenye gari ambalo liliibwa. Awali nilikuwa nimesahau kabisa kama simu nayo nilikuwa nimepoteza.

Tulipoizungumzia simu ndipo nikakumbua simu yangu ilikwenda na gari. Roho ilizidi kuniuma sana. Nikamlaani mwizi wa gari langu. “Haya nashukuru, waweza kundoka.”

Nilimwambia. Tatu alipondoka, nikarudi macho kwenye kile kipande cha karatasi na kusoma maandishi yaliyoandikiwa na Nasra Mfaume. Mke wangu wa zamani. Ujumbe ule ulikuwa ulisomeka hivi: Njoo kesho tusome barua....
 
Yaani wewe mama Shunie kila panapokucha na ndio makande yanazidi kuwa matamu....ila na wewe ndio kwanza unatupunguzia kipimo. Plz tuonee huruma bhana...tupe hayo mavitu mazima mazima, ongeza angalau kidogo madam.
 
Huyu bwana faraji wenda anahujumiwa ili apate kurudi kwa Nancy but all in all Ata fanya kosa kubwa kurudi kwa awa Wana wake
Iwe Nancy or Deborah
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom