Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

SEHEMU YA 26

Nikajiweka vizuri kitini kumsikiliza. “Nieleze tu dokta haina shida” “Iko hivi…”akaanza kunieleza.

“Mwanao amebemedwa.” “Kubemendwa ndio nini?” nikauliza nikiwa makini sana.

“Kubemendwa ni hali ya mtoto kunyonya maziwa ya mama yake yaliyochanganyikna na mbegu za kiume, yanii manii.”

“Duu! Mbona hilo jambo geni inakuwaje mtoto anyonye maziwa yenye mbegu za kiume?” nikahoji.

“Ngoja nikufundishe kitu…” dokta Chale alisema, akajikohoza kidogo kisha akaanza kunieleza.

“Kitaalamu ndani ya manii au mbegu za kiume kuna vitu vikuu vine. Protein, acid, chromosome na virus, nitakueleza kuhusu Acid kwa kuwa ndio kitu kilicholeta madhala kwa mwanao.

“Acid ni mfano wa tindikali, yaani kitu chenye ladha ya ukali mfano ndimu. Na kitu chenye tindikali kina kawaida ya kuunguza na pia kulegeza, ndiyo sababu kitaalam ukimlinganisha mwanamke aliyeolewa na asiyeolewa kisha akawa hafanyi zinaa maumbile yao yanatofautiana.”

Alisema kisha akaendelea. “Yule aliyeolewa mwili wake unakuwa laini zaidi sababu ya acid inayopatikana ndani ya manii.

Nitakupa mifano mingi iliyo hai ili akili yako ikubali kwamba mwanao amenyonya maziwa ya mama yake yaliyochanganyikana na manii ya mwanaume asiye baba yake.

“Ukitaka kuthibitisha zaidi acid katika manii kuwa inaunguza nakulegeza, ukiwa na kidonda kibichi jaribu kutia manii, kidonda kitauma mara mbili zaidi sababu ya acid.

“Mfano mwingine tazama kwa wale watoto wa kiumeambao wanaingiliwa kinyume na maumbile (mashoga) hata kama zamani alikuwa strong kiasi gani akiingiliwa tu, basi analegea kuanzia kutembea, kuzungumza na kila kitu,sababu ni Acid inayopatikana ndani ya manii.

Ndio maana tunashauri kutomuingilia mwanamke anayenyonyesha sababu ukimuingilia ukamuingizia manii
ambayo yana acid, acid ile itapanda katika matiti na kuyaharibu maziwa na hapo mtoto akinyonya atanyonyamaziwa yenye acid.

Halia hiyo, itasababisha mtoto kuwa katika hali kama aliyonayo sasa.

“Lakini kama atakula acid ya baba yake hatadhurika sana,sababu atakula acid ambayo kwa asili ndiyo iliyomtengeneza.
 
SEHEMU YA 27

“Ila mwanamke akiziniwa na mtu mwingine mtotoataathirika sana kama huyu wako na pengine itakuwa ni sababu ya kifo chake, kwa kuwa amekula acid ambayo si ya asili kutoka kwa wazazi wake.

“Mungu wangu!....” nilihamaki. “Kwa hiyo unataka kuniambia mke wangu anatoka na mwanaume mwingine?” niliuliza swali la kibwege. “Sijasema hivyo.” “Sasa?” “Inawezekana wewe ndio ukawa tatizo.”

“Kivipi?” “Labda mtoto huyu si wako ndio maana mbegu zako za kiume zinamuharibu.” kauli ile ya dokta ilizidi kunikata maini.

Sasa nikawa kwenye mkandamizo wa mambo mawili, aidha mke wangu anaye mwanaume mwingine ambaye anazini naye kiasi cha kumuharibu mtoto, au mimi nikawa si baba wa mtoto yule na ndiye ninaye muharibu.

Nilijikuta katika hali mbaya sana kifikra. “Najua hali unayopitia Faraji,” dokta akanishitua baada ya ukimya mfupi kupita kati yetu.

“Nitachukua sample ya damu yako na ya mwanao ili niwapime DNA tuone kama damu zenu zina-match ili tuone kama wewe ni chanzo cha mtoto kuwa hivi ama laa!.” aliniambia.

Sikuwa na sababu ya kukataa ushauri ule, Dk Chale alichukua damu zetu. Kisha akaenda kuzifanyia vipimo, masaa machache badaye akanipa majibu.

Majibu yalionyesha DNA yangu na ya mtoto ziliendana, kwa hiyo jawabu lilikuwa ni moja. Mke wangu alikuwa akitoka kimapenzi na mwanaume mwingine kiasi cha kumuharibu mwanangu.

Jambo lile liliniumiza sana, kila nilivyokuwa nikimfikiria mke wangu, sikuamini kama kiumbe yule aliyekuwa mpole na msikivu kama njiwa angeweza kufanya ushenzi wa namna ile, kitendo cha kunisaliti na kumbemenda mtoto wangu kiliniuma sana.

Niliporejea nyumbani, nilimkuta akiwa sebuleni, muda wote alikuwa bize Facebook, Whatsapp, na Instagram. Aliponiona alikuja kunipokea mtoto. “Vipi mmepata matibabu?” aliniuliza huku akimchukua mtoto.
 
SEHEMU YA 28

“Njoo chumbani,” nilimwambia bila kujibu swali lake.

Tuliongozana hadi chumbani mtoto tukimwacha mikononi kwa dada wa kazi. Doreen. “Mke wangu,” nilimwita tukiwa chumbani.

“Bee.” “Ungependa kuona maisha ya mwanao yakishia kulelewa na baba au mama wa kambo?” “Kivipi mume wangu?” “Sikutoshelezi kimapenzi?”

“Mbona sikualewi? “Tupo wanaume wangapi tunaokuvua nguo yako ya ndani?” “Heeee!!!” alihamaki baada ya swali hilo.

“Nakuuliza tena, tupo wanaume wangapi tunaokuvua nguo yako ya ndani?” “Faraji naomba unitake radhi,” akaniambia kwa ukali.

Nilinyamaza nikavuta pumzi, donge zito lilinikaba kooni, nilimsimulia mambo yote niliyoelezwa na daktari.

Habari ile ilimshitua sana mke wangu, lakini bado uso wake uliendelea kuonesha ni kuumbe asiyekuwa na hatia yoyote maishani.

“Faraji kama umenichoka niambie, lakini siyo kwa kunitafutia sababu namna hii” hatimaye akaniambia. “Kukutafutia sababu!!!.”

“Ndio, unanitafutia sababu” “Kwa taarifa yako, hili siyo jambo la kwanza kuelezwa juu ya uhuni ufanyao…” nikasema nikiwa nimemkazia macho.

“Wakati unajifungua ulijisaidia sana haja kubwa kitandani, na madaktari husema hali hiyo huwatokea wanawake wanaojihusisha na ngono kinyume na maumbile.”

Nilimpasualia. “Faraji shika adabu yako” aliniambia kwa ukali. “Sasa niambie ni lini nilikuingia kinyume na maumbile” “Unikome!!” alisema

Nikamchapa kibao. Akabweka kama jibwa koko. Bila kutegemea Akanivaa akiwa amechanua vidole vyake na kuniparua usoni kwa makucha.

Hasira zilinipanda nikamtandika kofi jingine usoni. Kilichofuata baada ya hapo ulikuwa ni ugomvi mkubwa sana.

Songombingo lile likawakusanya majirani ambao walikuja hadi chumbani kutuamulia, mke wangu alikuwa na hasira za mbogo akaanza kupasua vitu vya ndani hovyo.

Wakati huo mwanangu asiyejua lolote alikuwa akilia muda wote. Ghafla ndoa ikawa chungu kama shubiri.

JE NINI KILITOKEA?
 
Nilipoigia tu chumbani, macho yangu yalitua kwa kiumbe aliyekuwa amejilaza kitandani huku akiwa amevalia ‘night dress’ nyepesi iliyoacha maungo yake yaharibu kabisa mfumo thabiti wa upumuaji wangu.....


Alikuwa amejilaza kifudifudi kanga nyepesi aliyokuwa ameivaa lubega ilikuwa ikitoa picha ya makalio yake yaliyokuwa yameumuka kama kichunguu.

HII SEHEMU YA 9.
Naomba Faraji atuambie, mkewe hasa alivaa kitu gani!?
Khanga au Night dress?
 
mjinga sana " hakuna hata sehemu moja ambayo inaonyesha kuwa Aliamua kufanya kikao cha watu wawili baina yake na mama yake " walau kutaka kujua indeep kuhusu lawama anazozitoa mama yake dhidi ya mkewe
Ukitekwa na mapenz kw mwanamke unashindwa ata kuuliza kitu hata km unajua ukwel
 
SEHEMU YA 29

MTOTO alikuwa akilia bila kujua chochote, mke wangu naye akaendelea kupiga kelele za kilio huku akipasua vioo vya magari. Vituko vile vilizidi kunitia ghadhabu, watu wakaendelea kunisihi niwe mtulivu.

Wanaume watatu akiwemo mwenyekiti wa mtaa, wakamkamata mke wangu na kumdhibiti. Wakati huo watu walikuwa wamefurika nyumbani kwangu wakijionea video ya bure. Kwakweli mambo yale yalinifedhehesha mno.

Baada ya mke wangu kutulizwa na kutulia, na kutokana na utitiri wa watu kufurika nyumbani kwangu, kilichofanyika ni kuwaondoa ili taratibu zingine ziendelee.

Kwa msaada wa mwenyekiti wa mtaa, watu waliondolewa wakabakia wachache, mtoto naye aliyekuwa mikononi mwa dada wa kazi alikwisha nyamaza kulia. “Ni nini hasa tatizo?” mwenyekiti wa mtaa aliuliuliza baada ya utulivu.

Nilimweleza kwa kifupi kiongozi yule wa mtaa chanzo cha songombingo lile, alinisikiliza kwa makini maelezo yangu kisha akamgukia mke wangu ili naye atoe maelezo yake.

“Sina chochote cha kuzungumza zaidi ya kutaka talaka yangu,” alisema “Eeh!.” mwenyekiti akahamaki. “Ndio nataka talaka yangu, sijaolewa ili nipigwe,” akasisitiza. “Unadhani hiyo ndiyo suluhu ya changamoto za ndoa?” “Nimesema nataka talaka yangu, sitaki siasa.” Mke wangu akasisitiza kwa jeuri.

Ndani ya muda huohuo mara mageti ya nyumba yakagongwa kwa nguvu. Watu wote tukabaki tukishangaa.

Mwenyekiti akasimama kwenda kufuangua, mara askari polisi wakaingia wakiwa wameongozana na shemeji yangu Aisha. “Tumeambiwa kuna vita hapa?” afande mmoja akauliza.

“Hakuna vita afande, ilitokea sintafahamu kidogo lakini tumeimaliza” mwenyekiti wa mtaa alijibu. “Amenipiga, ameniumiza na damu zimevilia kwa ndani” mke wangu alidakia, halafu palepale akaangusha kilio.

Watu wote wakapigwa na butwaa, wale polisi wakamgeukia mwenyekiti: “We unasema hukuna vita wakati watu wanatoana ngeu?” “Aagh…unajua mambo ya familia…”
 
SEHEMU YA 30

“Faraji ni nani?” askari akauliza kwa ukali, hakuta kumsikiliza yule mwenyekiti. “Huyu hapa” mke wangu akawaonyesha wale polisi kwa kunisonta. “Mkamateni,” amri ikatoka. Nikakamatwa na polisi.

Nilipotaka kujieleza kwa wale mabwana, sikupewa nafasi hiyo, waliniburuza kwa nguvu hadi nje. Mtoto wangu mdogo akaanza kulia tena kwa uchungu.

Niliingizwa kwenye gari la polisi kama gaidi, kisha safari ya kituo cha polisi cha Oystabay ikaanza, nilijisikia uchungu sana kwa kile kilichokuwa kikinitokea. Nilijikuta namchukia sana mke wangu. Hasira dhidi yake ikawa kubwa.

Baada ya kufikishwa kituoni, sikuchukuliwa maelezo yoyote zaidi ya kutakiwa kuvua mkanda na viatu, pamoja na kukabidhi vitu vyangu, kisha nikaingizwa selo.

Tangu nizaliwe sikuwahi kuingia ‘lockup’ na sikudhani kama siku moja ningeingia sehemu mbaya kama ile. Mule ndani kulikuwa kunanuka mkojo na hewa ilikuwa nzito sana. Chawa na kunguni lile lilikuwa ni zizi lao.

Nikiwa mule ndani, nikaamini muda si mrefu marafiki na jamaa wangekuja kuniwekea dhamana endapo wangepata taarifa juu ya maswahibu yale.

Nusu saa ilipita bila kuona dalili zozote za kuchomoka, nilimwita askari aliyekuwa kaunta nikamwomba anisaidie kufanya mawasiliano na moja ya marafiki zangu ili wajue nipo kwenye madhila.

“Hata kama akipatikana mtu wa kukuwekea dhaman, kwa muda huu siyo rahisi kutoka,” yule askari aliniambia. “Kwa nini?”

“Ni utaratibu tu, usiku huwa hatutoi dhamana.” “Kwa hiyo nitalala humu hadi asubuhi?” “Ndio maana yake.” “Mungu wangu,” nilimaka.

Hata hivyo kabla sijawasiliana na jamaa yangu kwa ajili ya kumpa taarifa za kukamatwa kwangu, mwenyekiti wa mtaa alifika.

Aliomba kuzungumza na mimi, kisha akasogea katika geti. “Kesho utaachiwa…” aliniambia. “Kweli leo haiwezikani?”

“Ndio, dhamana mara nyingi zinatolewa mchana sio usiku, vinginevyo labda tutumie njia za panya” alisema, nikamwelewa hapo lazima rushwa utumike. “Haina shida we waulize wanataka kiasi gani.” “Basi subiri kidogo,” aliniambia.

Akatoka na kwenda kuzungumza na polisi, sikujua alimkabili nani ila muda mfupi badaye akarudi. “Jamaa wanasema wanataka laki moja.” “Haina neno, pesa siyo tatizo, ninachotaka ni kutoka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom