Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Wanawake wa kipemba na asili Ya kiarabu wengi wana silidi kwenye mwandu tu Ila back stage ni mseleleleka wa mlima kitonga
SEHEMU YA 11

Nilistushwa na mionzi hafifu ya jua la asubuhi ambalo huwa mara nyingi linapenya chumbani kwangu kupitia dirishani.

Pembeni , mke wangu alikuwa bado akikoroma, saa ilionyesha ilikuwa saa mbili asubuhi, nilipiga miayo ya kivivu, nikajiondoa kitandani.

Nilikuwa mtupu, taswira ya penzi la mwanamwali lilikuwa likijitengeneza upya akilini mwangu. Nilitabasamu na kujiona kidume mwenye bahati kubwa maishani.

Kuwa na mke ambaye hajawahi kuguswa na mwanaume ni ushindi mkubwa kwenye dunia ya leo, nilijiambia kimoyomoyo.

Nilisogea kwenye kioo na kusimama wima, nikaona ukoko wa damu ya Mwanamwali iliyogandana kwenye nyeti zangu, nikatabasamu tena huku moyo wangu ukiwa wenye faraja.

Nilipoyarudisha macho kitandani, Mwanamwali alikuwa bado akiuchapa usingizi.
Niliyatembeza macho pale kitandani, sikuwa nimeona kitu kingine nilichotarajia kukiona, nikasogea karibu zaidi.

Naam! hapo nikaona.

Damu ilikuwa imetapakaa kwenye mashuka meupe, nikajipongeza kimoyomoyo kwa kazi nzuri niliyoifanya usiku wa kuamkia siku hiyo.

Kazi ya kufungua bikira ya mwanamwali. ***** Maisha yangu na mke wangu, yalikuwa ni ya furaha, tulipendana na nilimwamini mno. Kama walivyo wanawake wengine wa Kipemba, Nasra alikuwa ni mwanamke mpole, msikivu na mchamungu.

Angalau hata ile aibu iliilipungua. Kwakweli alikuwa na kila kitu ambacho mwanaume yeyote angetaka mkewe awenacho. Wazungu wanasema ‘Wife material’

Ni miezi sita ilikuwa imepita, mjomba Majeed alikwisha rejea kijijini, katika mji wangu tulikuwa tumebakia watatu, yanii mimi, mke wangu, pamoja shemeji yangu Aisha. Huyu ni yule ndugu wa mke wangu.

Nakumbuka siku moja, baada ya kurudi kutoka kazini, kama kawaida yangu huwa napenda kujituliza nyumbani majira ya saa mbili kwa ajili ya kufuatilia taarifa ya habari katika vituo mbalimbali vya runinga.

Wakati huo mke wangu na nduguye walikuwa wakiendelea na matayarisho ya chakula cha usiku.

Nikiwa pale sebuleni, na rimoti mkononi, nikiwa nahamisha stesheni moja hadi nyingine, mara simu ya mke wangu ilianza kuita. Iliita muda mrefu hadi ikakatika.
 
SEHEMU YA 23

Mama alinisihi nimkanye mke wangu kwa tabia ya kupenda kuwa bize katika mitandao ya kijamii kiasi cha kusahau majukumu yake muhimu.

Kama niliyosema awali, sikuchukulia kwa uzito mkubwa jambo hilo, nadhani ni kwakuwa muda mwingi nilikuwa nikishinda ofisini, hivyo sikuona athari za jambo alilonieleza mama yangu.

Mke wangu naye hakuisha kunishitakia mapungufu ya mama, alimtuhumu kwa tabia ya kumchunga kama mtoto mdogo, akamtuhumuwa kuwa alikuwa na hasira za karibu.

Mambo yaliendelea kuwa hivyo bila mimi kuchukua maamuzi yoyote. Jioni moja mama aliniomba nimpe nauli ili siku inayofuatia arejee Kigoma.

“Kuna nini. Mbona ghafla?” “Nilikuja kwa ajili ya kumsaidia mkeo.Nimemaliza” “Sasa kwa nini uondoke kama unakimbizwa, si ukae tuiandae safari vizuri.”

“Nimekwisha kaa sana hapa, kesho lazma niondoke.” Uso wake ulionesha kama alikuwa na jambo zito lililomkwaza moyoni, nilihisi huenda kulitokea sintafahamu kubwa kati yake na mke wangu siku hiyo.

“Kwani mama una tatizo gani?” “Kivipi?” “Unaonekana hauko sawa.” “Siku zote sipo sawa, we’ wagundua leo?” “Ni nini hasa?”

“Hujui?” “Ni yaleyale ya siku zote?” “Ndio hayo hayo.” “Mama unajua sivutiwi na namna mnavyoshindwa kuishi vizuri na mke wangu.” “Ndio maana nataka kesho nijiondokee ili uwe na amani moyoni.”

“Kwani ni kipi hasa alichokufanyia mke wangu?” “Sijafanyiwa mimi ila unafanyiwa wewe,” alisema. “Nafanyiwa nini?” Hakunijibu. Alisisitiza nimpe nauli ili siku inayofuatia arejee Kigoma.

“Kwa kuwa mama aling’ang’ania sana kuondoka, nilichofanya ni kuindaa safari jioni hiyo hiyo.

Nilimpigia simu jamaa yangu mmoja aitwaye Frank Mjige, ambaye alikuwa akifanya kazi katika shirikika la ndege la FastJet nikamwomba aniafanyie mpango wa tiketi asubuhi ya kesho.
 
SEHEMU YA 24

Kupata tiketi chini ya Frank Majige ilikuwa ni kazi rahisi. Sikutaka mama asafiri kwa basi au treni kutokana na kadhia ya usafiri huo. Siku iliyofuatia, nilimsindikiza mama uwanja wa ndege wa mwalimu Julius Nyerere, akapanda ndege ya saa mbili kamili na kurudi Kigoma.

Baada ya kuhakikisha mama ameondoka, nilirudi kwenye gari ili kuendelea na latiba zangu nyingine. Nikiwa njiani narudi nyumbani, sikuwa na raha kabisa, uondokaji wa mama sikuupenda, zadii ya dada wa kazi , aitwaye Doreen, si shemeji yangu Aisha wala mke wangu Nasra aliyemwambia mama neno kwaheri.

Niliazimia nitakaporejea nyumbani, lazima nimweke kitako mke wangu na nimkanye juu ya tabia hiyo.

Sikupenda Nasra aendelee kuwa na uhasama na mama. Nilipowasili nyumbani, mke wangu alikuwa sebuleni, alikuwa bize na simu yake. Nilimtaka aje chubani.

Mimi nikatangulia ndani, nilipoingia tu, nikamkuta mtoto analia huku akiwa ametota kwa mkojo.

Mara mke wangu naye akaingia, alipoona mtoto analia huku akiwa amejikojolea ndio akajitia kushituka na kwenda kumnyanyua.

“Wewe kwa nini unamwacha mtoto kwenye hali hii?” nilimuuliza kwa ukali. “Sikujua kama angeamka sasa hivi.” “Nilipoambiwa kwamba mitandao ya kijamii imekuteka akili, nilibisha, lakini leo nimejionea.”

“Sasa hayo yametokaea wapi mume wangu?” “Unawezaje kuwa facebook kiasi cha kumsahau mwanao?”

“Nikwambie mara ngapi sikujua kama angeamka sasa hivi.” “Hebu nenda kamsafishe kisha urudi hapa tuzungumze,” nilimwambia.

Aliondoka muda mfupi badaye akarejea. “Ulishindwa hata kumwambia mama kwaheri.” Nilianza kumpasha. “Mbona yeye hakuniaga?”

“Kwa hiyo unashindana na mzazi?” “Wala.” “Kumbe?” “Mama yako anamatatizo mengi.” “Sawa, ila wahenga wanasema, mzazi hakosei.”

“Mama yako anakosea, na amezidi.” “Sasa nisikilize…” nilimwambia. “Unatakiwa kumwomba msamaha mama.” “Kwa kosa gani?”

“Siyo kwa kosa gani Nasra mke wangu, unachokifanya ni kutengeneza mahusiano mazuri na wazee.”

“Nitakuwa mnafiki kama nitafanya hilo unalolitaka, sintaweza,” mwanamke yule alinikatalia kwa ujasiri mkubwa.

Nikabaki kinywa wazi. Nilimsihi sana na kumweleza faida ya kufanya jambo hilo, lakini mke wangu alinikatalia katakata
 
SEHEMU YA 25

Maisha yaliendelea, jambo lile nikalipuuza na kulitupilia mbali!. Na kadiri siku zilivyozidi kwenda ndivyo hata songombingo la tuhuma za mke wangu kuwahi kuwa na tabia za mkushiriki mapenzi kinyume na maumbile nalo nikaliona la kawaida tu.

Nikijibidiisha sana katika kazi zangu, miladi yangu ilizidi kukua siku hadi siku, miezi michache badaye niliamua kuacha kazi serikalini na kuweka nguvu katika biashara zangu.

Muda wangu wa kutulia na familia yangu ukawa mdogo, nilikuwa nikitoka nyumbani asubuhi, kurudi kwangu ilikuwa ni saa nne usiku hadi saa sita.

Katika nyakati zilezile nilipata pigo baya maishani, nakumbuka ilikuwa ni asubuhi moja nilipata simu mbaya kutoka nyumbani, baba yangu mzee Hussein Mpangalala alinguka bafuni kutokana na presha iliyopanda, na alifariki njiani alipokuwa akiwahishwa hospitalini.

Ulikuwa ni msiba mzito maishani, mimi na mke wangu, tulisafiri hadi Kigoma kwenye mazishi ya baba.

Baada ya mazishi, watu walikaa matanga siku kadhaa huku tukisubiri 40 kwa ajili ya kisomo. Tukiwa tunagoja 40, Mke wangu nilimtaka arudi Dar ili akasimamie maduka ambayo kwa wakati huo yalikuwa chini ya wafanyakazi.

Kwa kuwa mimi ndio nilibaki kuwa kiongozi wa familia, nikabakia na mama pale nyumbani kama sehemu ya kumtia nguvu na faraja katika kipindi kile kigumu. 40 ilipopita, nilirudi Dar es salama kuendelea na maisha. Nilipofika nyumbani nilikuatana hali iliyonishangaza.

Mtoto wangu Mwanda, ambaye kwa nyakati zile alikuwa na kama mwaka mmoja na nusu, alikuwa amekondeana sana, nywele zake zilikuwa zimenyonyoka, mwili wake akionekana kudhoofu.

“Anaumwa?” nilimuuliza mke wangu “Aka.” “Sasa kwa nini yupo hivi?” “Mwenyewe nashangaa.” “Ushawahi kumpeleka hospitali?”

“Bado.” “Kwa nini?” “Sijaona athari za moja kwa moja.” Majibu ya mke wangu yalinifanya nitamani kumzaba kibao, lakini nilijiuzua.

Nilichofanya ni kumchukua mwanangu mimi mwenyewe na kumpeleka hospitali ya Regecy.
Nilikutana na dokta Chale.

Baada ya dokta kumfanyia vipimo aliniita ofisini mwake ili anipe majibu. “Faraji majibu nitakayokupa lazima ustahimili.”
maneno ya dokta Chale yalinitisha
 
Bosi wangu alifiwa na baba pamoja na mama ndani ya mwaka mmoja....alilia sana kwa sauti alijikaz ila alipowaona mama zake wadogo na wakubwa wakilia alishindwa kujizuia .....je, uyu nae atakuwa anavimelea vya kike aruhusiw kuvaa kaptura kama usemavyo?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom