Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

SEHEMU YA 80

Kimsingi ulikuwa ni utaratibu wenye kuudhi sana na kwa kweli Nasra alikuwa akiumizwa mno na utaratibu huo wa maisha, kuna wakati nilipokuwa nikimwangalia usoni niliona haiba ya majonzi na fadhaa kubwa.

Nilimwona mwanamke mwenye majuto maishani, uso wenye kunyanyasika kwa kukosa haki, nilimwona kiumbe mwenye machungu na maumivu makali.

Bahati mbaya au nzuri hakuwa na la kunifanya, wala pa-kunipeleka, alitambua kwamba, kama angaliamua kwenda mahakamani au kwenye taasisi mbalimbali za kirai, ili kudai haki ya kuwa huru na mtoto wake, kama mzazi. Kivyovyote Lazima ningemshinda tu. Pesa zangu zilifanya kazi ya kubatilisha sheria katika jambo hilo.

Nasra aliendelea kuishi katika madhila ya nafsi kwa muda mrefu tu. Wakati mke wangu wa zamani, Nasra Mfaume, akiwa kwenye hangaiko la kukosa haki zake za msingi, kama mama wa mwanangu. Uhusiano wangu na Debora uliendelea kuwa moto.

Nilinenepa nikaongezeka uzito. Msongo wa wa mawazo nilio kuwa nao mwanzo, ulitorokea Dirishani na kuishia zake. Debora naye alikuwa mwenye tabasamu wakati wote. Katikati ya furaha hiyo, likaongezeka jambo jingine lililotuongezea siku za kuishi, vicheko na tabasamu.

Mpenzi wangu Debora, alipandishwa cheo kazini, katika teuzi za rais, naye aliteuliwa kuwa mkurugenzi wa Wilaya ya Misungwi, huko mkoani Mwanza.

Fursa ile ilitufurahisha. Halikuwa jambo dogo kuaminiwa na rais na kupewa mamlaka yale si jambo la kubeza. Nakumbuka baada ya uteuzi, mke wangu alitakiwa kusafiri hadi jijini Mwanza. Huko aliapaishwa. Siku iliyofuatia akaanza kazi.

Nikiwa nimeambatana naye kama ishara ya kumpa sapoti, baada ya kiapo, nilikaa naye Mwanza kwa kwa siku mbili tatu, kisha nikarejea Dar kuendelea na shughuli zangu.

Huo ukawa mwanzo wa kuwa mbali na Debora. Ile furaha ya kupanda cheo, ghafla ikawa mateso. Hii ni kutokana na umbali uliokuwepo baina yetu.

Maisha yetu yaliendelea. Umbali kati yangu na Debora ukawa ni mtihani mkubwa. Kwa siku za awali nilivumilia, lakini siku zilivyozidi kwenda mbele, nikawa nashidwa kustahimili kumkosa kiumbe yule mrembo.
 
SEHEMU YA 81

Nilikuwa nikifunga safari za mara kwa mara kwenda Mwanza, huko sikuwa nakaa sana.

Kuna wakati nilifikiria kuhamia Mwanza, wazo hilo likawa gumu kiutekelezaji kutokana na miradi yangu mingi kuwa Dar es salam. Debora alikuwa akinishirikisha kwenye baadhi ya kazi zake, na mimi nilikuwa nikimpa msaada kadiri ya uwezo wangu.

Siku moja nilifunga safari hadi Mwanza, nilifika mapema tu, majira kama ya saa nne asubuhi. Nakumbuka Ilikuwa siku ya Ijumaa.

Baada ya kufika kwenye nyumba aliyokuwa akishia, bahati nzuri au mbaya sikumkuta.

Lakini kwa vile nilikuiwa mwenyeji, nikapitiliza hadi chumbani.

Nilipofika ndani baada ya kuoga na kupumzika, nikiampigia simu kumwambia nimekwisha fika. “Kwa nini uje mapema ?” Debora aliuliza kwa sauti ya ukali hadi nikaogopa. “Sioni ubaya.

Maadhali hapa ni nyumbani, hata ningekuja saa nane usiku, ni sawa tu.” “Sipendi tabia za Kiswahili mimi.” Debora akapayuka. “Ni jambo dogo hilo mpenz…” “Nimekwambia sipendiii!”akapayuka kwa ukali zaidi.

Ikabidi nikate simu, nikafikiria sababu inayomfanya Debora akasirike kiasi kile, bado nikaona jambo lililomudhi ni la kipuuzi tu. “Wanawake bwana, sasa hilo ndio la kumkasirisha!”

Nikiwa katika tafakuri macho yangu yakatua juu ya droo ya kitanda, nikaona kuna pakiti za dawa, nikavutika kutaka kujua dawa zile ni za nini, maana sikuwahi kupata taarifa zozote kama Debora ni mgonjwa.

Nikasogea Nilipoiangalia pakiti ile. Sikuamini nilichokiona!. Kwanza pakiti ile ilionesha kuna tembe kama tano ambazo zimekwisha tumika, ila kubwa lililonishangaza ni kukuta vidonge vile vilikuwa ni vya kuzuia mimba. “Inamaana Debora hataki kuzaa na mimi!” nilijiuliza kimoyomoyo.

“Kwa nini? Anamipango gani? Kwa nini hanishirikishi.?” Maswali yote hayo yalipita akilini mwangu kwa wakati mmoja, kengele ya hatari ikalia kichwani kwangu, nikaanza kuwa na wasiwasi huenda Debora naye ananicheza mchezo mchafu kama alivyofanya mke wangu wa zamani, Nasra.

Nikiwa kwenye mkanganyiko ule, sijui niliwaza nini bwana, nikaanza kukagua kona moja hadi nyingine ndani ya chumba kile.

Nilivuta droo ya kabati la nguo ambapo huwa tunaweka makablasha mbalimbali. Ile navuta tu. Lahaula!!!!...
 
SEHEMU YA 81

Nilikuwa nikifunga safari za mara kwa mara kwenda Mwanza, huko sikuwa nakaa sana.

Kuna wakati nilifikiria kuhamia Mwanza, wazo hilo likawa gumu kiutekelezaji kutokana na miradi yangu mingi kuwa Dar es salam. Debora alikuwa akinishirikisha kwenye baadhi ya kazi zake, na mimi nilikuwa nikimpa msaada kadiri ya uwezo wangu.

Siku moja nilifunga safari hadi Mwanza, nilifika mapema tu, majira kama ya saa nne asubuhi. Nakumbuka Ilikuwa siku ya Ijumaa.

Baada ya kufika kwenye nyumba aliyokuwa akishia, bahati nzuri au mbaya sikumkuta.

Lakini kwa vile nilikuiwa mwenyeji, nikapitiliza hadi chumbani.

Nilipofika ndani baada ya kuoga na kupumzika, nikiampigia simu kumwambia nimekwisha fika. “Kwa nini uje mapema ?” Debora aliuliza kwa sauti ya ukali hadi nikaogopa. “Sioni ubaya.

Maadhali hapa ni nyumbani, hata ningekuja saa nane usiku, ni sawa tu.” “Sipendi tabia za Kiswahili mimi.” Debora akapayuka. “Ni jambo dogo hilo mpenz…” “Nimekwambia sipendiii!”akapayuka kwa ukali zaidi.

Ikabidi nikate simu, nikafikiria sababu inayomfanya Debora akasirike kiasi kile, bado nikaona jambo lililomudhi ni la kipuuzi tu. “Wanawake bwana, sasa hilo ndio la kumkasirisha!”

Nikiwa katika tafakuri macho yangu yakatua juu ya droo ya kitanda, nikaona kuna pakiti za dawa, nikavutika kutaka kujua dawa zile ni za nini, maana sikuwahi kupata taarifa zozote kama Debora ni mgonjwa.

Nikasogea Nilipoiangalia pakiti ile. Sikuamini nilichokiona!. Kwanza pakiti ile ilionesha kuna tembe kama tano ambazo zimekwisha tumika, ila kubwa lililonishangaza ni kukuta vidonge vile vilikuwa ni vya kuzuia mimba. “Inamaana Debora hataki kuzaa na mimi!” nilijiuliza kimoyomoyo.

“Kwa nini? Anamipango gani? Kwa nini hanishirikishi.?” Maswali yote hayo yalipita akilini mwangu kwa wakati mmoja, kengele ya hatari ikalia kichwani kwangu, nikaanza kuwa na wasiwasi huenda Debora naye ananicheza mchezo mchafu kama alivyofanya mke wangu wa zamani, Nasra.

Nikiwa kwenye mkanganyiko ule, sijui niliwaza nini bwana, nikaanza kukagua kona moja hadi nyingine ndani ya chumba kile.

Nilivuta droo ya kabati la nguo ambapo huwa tunaweka makablasha mbalimbali. Ile navuta tu. Lahaula!!!!...
Maninaa na bado punguwani wewe,na ukimwi juu
 
sio wazenj wote jamani. Hata usenge siku hizi hakuna ukabila vijana wengi wanajiingiza
Ambaruty..na kina kaoge wametokea zenj!

Huko tanga wasenge kibao na Dar ndio kabisa wanawake Sodom ndio fashen.. .ila hawasemi!
Huko zenj wanaojiuza wengi ni kutoka huko huko na hakuna uchafu wasiofanya!
Sodom ndio biashara nje nje ...
Tatizo unafiki tu....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom