Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Umerudia
Sehemu ya 76

Dakika chache zilizofuata, tuliwasili nyumbani kwangu, Kinondoni studio, kama tulivyotegemea, Nasra alikuwa ameketi kitako, amegea ukuta wa nyumba yangu.

Alipoliona gari, akasimama na kusogea, tembea yake ilionekana ni mwenye maumivu ya tumbo, nadhani ni athari za lile teke. Nilisogeza gari hadi getini, naye akasogea upande wangu.

Nilipandisha vioo, yeye hakuniona ila mimi niliomwona. Vioo vilikuwa ‘tinted’ akiwa dirishani akawa analia mikono yake akionesha ishara ya kuniomba kwa kunibembeleza.

Wakati uwazi wa geti unazidi kufunguka ndivyo Nasra alivyokazana kunisihi nimlete mtoto amwone, katika muda wa sekunde za kuhesabu, geti lakawa wazi.

Kwa kutumia kioo cha mbele, nikampa ishara mlinzi amzuia kiumbe yule asithubutu kuingia ndani wakati naliingiza gari.

Nasra akaendelea kulia machozi aliniomba nimkutanishe na mwanaye, labda kwa mtu mwingine aliyekuwa akishuhudia jambo lile angeweza kushikwa na huruma, lakini moyo wangu haukuwa na huruma hata chembe na mwanamke yule.

Nikawa nalingiza gari, huku naye akilifuata, alikaribia getini, mlinzi akamzuia. Akalia kama mtoto, masikini Nasra alitia huruma mno. Nilimteremsha mke wangu mtarajiwa Debora, nikamwingiza sebuleni.

Baadaye nika nikarudi nje kumweleza ukweli mwanamke yule kwamba mtoto alikuwa kwa bibi yake.

Nilipotokeza tu, kama kawaida Nasra alinifuata na kunipigia magoti. “Niko chini ya miguu yako, naomba nimwone mtoto japo kwa dakika moja tu.”

“Nisikilize Nasra…” nilisema, nikaendelea. “Mtoto hayupo hapa, anaishi kwa bibi yake huko Nguruka Kigoma,”nilimwambia, alibakia kimya, ni kama vile alikuwa akisubiri aambiwe jambo hilo ili atulie, alikuwa mtulivu ni kwikwi za kilio tu ndio zilimtoka.

Baada ya kumweleza hayo, nilirudi ndani. sikujua baada ya pale Nasra alielekea wapi, sikutaka kujua maisha yake wala lolote kumuhusu.

Ninachokumbuka baada ya kama siku tatu nikapoke simu kutoka kwa mama. “Mwanao amepotea,” lilikuwa ni neno la kwanza kuzungumzwa na mama baada tu ya kupokea simu yake. “Nini!!!” nilishituka. Nikamkumbua Nasra.

ITAENDELEA…..
 
Sehemu ya 76

Dakika chache zilizofuata, tuliwasili nyumbani kwangu, Kinondoni studio, kama tulivyotegemea, Nasra alikuwa ameketi kitako, amegea ukuta wa nyumba yangu.

Alipoliona gari, akasimama na kusogea, tembea yake ilionekana ni mwenye maumivu ya tumbo, nadhani ni athari za lile teke. Nilisogeza gari hadi getini, naye akasogea upande wangu.

Nilipandisha vioo, yeye hakuniona ila mimi niliomwona. Vioo vilikuwa ‘tinted’ akiwa dirishani akawa analia mikono yake akionesha ishara ya kuniomba kwa kunibembeleza.

Wakati uwazi wa geti unazidi kufunguka ndivyo Nasra alivyokazana kunisihi nimlete mtoto amwone, katika muda wa sekunde za kuhesabu, geti lakawa wazi.

Kwa kutumia kioo cha mbele, nikampa ishara mlinzi amzuia kiumbe yule asithubutu kuingia ndani wakati naliingiza gari.

Nasra akaendelea kulia machozi aliniomba nimkutanishe na mwanaye, labda kwa mtu mwingine aliyekuwa akishuhudia jambo lile angeweza kushikwa na huruma, lakini moyo wangu haukuwa na huruma hata chembe na mwanamke yule.

Nikawa nalingiza gari, huku naye akilifuata, alikaribia getini, mlinzi akamzuia. Akalia kama mtoto, masikini Nasra alitia huruma mno. Nilimteremsha mke wangu mtarajiwa Debora, nikamwingiza sebuleni.

Baadaye nika nikarudi nje kumweleza ukweli mwanamke yule kwamba mtoto alikuwa kwa bibi yake.

Nilipotokeza tu, kama kawaida Nasra alinifuata na kunipigia magoti. “Niko chini ya miguu yako, naomba nimwone mtoto japo kwa dakika moja tu.”

“Nisikilize Nasra…” nilisema, nikaendelea. “Mtoto hayupo hapa, anaishi kwa bibi yake huko Nguruka Kigoma,”nilimwambia, alibakia kimya, ni kama vile alikuwa akisubiri aambiwe jambo hilo ili atulie, alikuwa mtulivu ni kwikwi za kilio tu ndio zilimtoka.

Baada ya kumweleza hayo, nilirudi ndani. sikujua baada ya pale Nasra alielekea wapi, sikutaka kujua maisha yake wala lolote kumuhusu.

Ninachokumbuka baada ya kama siku tatu nikapoke simu kutoka kwa mama. “Mwanao amepotea,” lilikuwa ni neno la kwanza kuzungumzwa na mama baada tu ya kupokea simu yake. “Nini!!!” nilishituka. Nikamkumbua Nasra.

ITAENDELEA…..
Weka nyingine bana hii marudio
 
SEHEMU YA 77

Ndugu wa Nasra wanasema hawaoni kama mtoto wao yupo katika hatia ya wizi wa mtoto, maana yule ni mwanaye aliyemzaa, hivyo anayo haki ya kuwa naye wakati wowote.”

Nilishusha pumzi ndefu, hasira zikiwa zimenijaa kifuani, niliagana na mama nikamwambia nitamwambia hatua nitakayoichukua.

Nilichofanya ni kumipigia simu mchumba wangu Debora, na kumpa taarifa juu ya mke wangu wa zamani, Nasra, kumwiba mtoto wangu Mwanda. “Si nilikwambia kwamba jambo hilo linaweza kutokea. Unakumbuka?” “Nakumbuka mpenzi.Uliniambia.” “Ameibwa lini?”

“Tangu asubuhi ya leo.” “Na umesema amesafiri leo kuja Dar?” “Ndio.” “Kwa usafiri gani?” “Treni” “Huyo tunamkamatia hapahapa Dar, wala usijali mpenzi wangu…sawa?” “Tutafanyaje?”

“Mahakama ilikwishapitisha hukumu wewe ndiye unatakiwa kuishi na mtoto wenu, hadi atakapofikisha miaka saba, kitendo cha Nasra kumchukua kinyamela ni kosa kisheria.”

“Kwa hiyo?” “Kachukue RB No kituo cha polisi, mimi nitawasiliana na kamanda wa polisi kitengo cha reli, Gideon Nkeremi, huyu ni class mate wangu. Atatusaidia kumtia mbaroni.”

Hiki ndicho kitu ninachompendea Debora, ni mwanamke mwenye akili za haraka haraka, ambaye anajiongeza kila wakati, amekuwa msaada mkubwa kwenye matatizo yanayonipa wakati mgumu.

Nilitabasamu, uso wangu ukarudi kwenye haiba yake ya kawaida, nilikwenda kituo cha polisi na kufungua ‘RB NO’ ya kesi ya kuibiwa mtoto.

Debora naye akaniambia kila kitu kimeikwisha kamilika, amekwisha mweleza kamanda wa kikosi cha reli na muda si mrefu msako polisi wataanza kazi ya kumsaka Nasra ndani ya treni zote zilizokuwa safarini.

Hata hazikupita dakika 20 Debora akanipigia simu, akaniambia tayari Nasra amekamtwa akiwa Igalula mkoani Tabora, na anasafirishwa kwa treni kuja jijini Dar chini ya ulinzi wa polisi.

“Na mtoto anaye?” nikahoji. “Ndio, amekamatwa akiwa na mtoto wake.” Asubuhi ya siku iliyofutia, Nasra alifikishwa Dar na kukabidhiwa kwenye kituo cha mjini kati, Posta. Niliongozana na mke wangu mtarajiwa, Debora, na kwenda kituoni.

Nasra na mwanaye walikuwa wamewekwa kwenye moja ya ofisi ndani ya kituo. Mtoto wangu aliponiona alinikimbilia na kunikumbatia.

ITAENDELEA KESHO..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom