Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

ndo wanisema hivi babe?? hebu relax

Mine eyes umeridhika sasa??
SEHEMU YA 77

Ndugu wa Nasra wanasema hawaoni kama mtoto wao yupo katika hatia ya wizi wa mtoto, maana yule ni mwanaye aliyemzaa, hivyo anayo haki ya kuwa naye wakati wowote.”

Nilishusha pumzi ndefu, hasira zikiwa zimenijaa kifuani, niliagana na mama nikamwambia nitamwambia hatua nitakayoichukua.

Nilichofanya ni kumipigia simu mchumba wangu Debora, na kumpa taarifa juu ya mke wangu wa zamani, Nasra, kumwiba mtoto wangu Mwanda. “Si nilikwambia kwamba jambo hilo linaweza kutokea. Unakumbuka?” “Nakumbuka mpenzi.Uliniambia.” “Ameibwa lini?”

“Tangu asubuhi ya leo.” “Na umesema amesafiri leo kuja Dar?” “Ndio.” “Kwa usafiri gani?” “Treni” “Huyo tunamkamatia hapahapa Dar, wala usijali mpenzi wangu…sawa?” “Tutafanyaje?”

“Mahakama ilikwishapitisha hukumu wewe ndiye unatakiwa kuishi na mtoto wenu, hadi atakapofikisha miaka saba, kitendo cha Nasra kumchukua kinyamela ni kosa kisheria.”

“Kwa hiyo?” “Kachukue RB No kituo cha polisi, mimi nitawasiliana na kamanda wa polisi kitengo cha reli, Gideon Nkeremi, huyu ni class mate wangu. Atatusaidia kumtia mbaroni.”

Hiki ndicho kitu ninachompendea Debora, ni mwanamke mwenye akili za haraka haraka, ambaye anajiongeza kila wakati, amekuwa msaada mkubwa kwenye matatizo yanayonipa wakati mgumu.

Nilitabasamu, uso wangu ukarudi kwenye haiba yake ya kawaida, nilikwenda kituo cha polisi na kufungua ‘RB NO’ ya kesi ya kuibiwa mtoto.

Debora naye akaniambia kila kitu kimeikwisha kamilika, amekwisha mweleza kamanda wa kikosi cha reli na muda si mrefu msako polisi wataanza kazi ya kumsaka Nasra ndani ya treni zote zilizokuwa safarini.

Hata hazikupita dakika 20 Debora akanipigia simu, akaniambia tayari Nasra amekamtwa akiwa Igalula mkoani Tabora, na anasafirishwa kwa treni kuja jijini Dar chini ya ulinzi wa polisi.

“Na mtoto anaye?” nikahoji. “Ndio, amekamatwa akiwa na mtoto wake.” Asubuhi ya siku iliyofutia, Nasra alifikishwa Dar na kukabidhiwa kwenye kituo cha mjini kati, Posta. Niliongozana na mke wangu mtarajiwa, Debora, na kwenda kituoni.

Nasra na mwanaye walikuwa wamewekwa kwenye moja ya ofisi ndani ya kituo. Mtoto wangu aliponiona alinikimbilia na kunikumbatia.

ITAENDELEA KESHO..
Jamani hakuna Deborah kama wa faraji humu, maana moyo umeanza kuloana....tafadhari jamani, kama yupo anyooshe mkono juu tu.....

#Deborah akili mingi mingi...
 
SEHEMU YA 28

“Njoo chumbani,” nilimwambia bila kujibu swali lake.

Tuliongozana hadi chumbani mtoto tukimwacha mikononi kwa dada wa kazi. Doreen. “Mke wangu,” nilimwita tukiwa chumbani.

“Bee.” “Ungependa kuona maisha ya mwanao yakishia kulelewa na baba au mama wa kambo?” “Kivipi mume wangu?” “Sikutoshelezi kimapenzi?”

“Mbona sikualewi? “Tupo wanaume wangapi tunaokuvua nguo yako ya ndani?” “Heeee!!!” alihamaki baada ya swali hilo.

“Nakuuliza tena, tupo wanaume wangapi tunaokuvua nguo yako ya ndani?” “Faraji naomba unitake radhi,” akaniambia kwa ukali.

Nilinyamaza nikavuta pumzi, donge zito lilinikaba kooni, nilimsimulia mambo yote niliyoelezwa na daktari.

Habari ile ilimshitua sana mke wangu, lakini bado uso wake uliendelea kuonesha ni kuumbe asiyekuwa na hatia yoyote maishani.

“Faraji kama umenichoka niambie, lakini siyo kwa kunitafutia sababu namna hii” hatimaye akaniambia. “Kukutafutia sababu!!!.”

“Ndio, unanitafutia sababu” “Kwa taarifa yako, hili siyo jambo la kwanza kuelezwa juu ya uhuni ufanyao…” nikasema nikiwa nimemkazia macho.

“Wakati unajifungua ulijisaidia sana haja kubwa kitandani, na madaktari husema hali hiyo huwatokea wanawake wanaojihusisha na ngono *******************.”

Nilimpasualia. “Faraji shika adabu yako” aliniambia kwa ukali. “Sasa niambie ni lini nilikuingia *******************” “Unikome!!” alisema

Nikamchapa kibao. Akabweka kama jibwa koko. Bila kutegemea Akanivaa akiwa amechanua vidole vyake na kuniparua usoni kwa makucha.

Hasira zilinipanda nikamtandika kofi jingine usoni. Kilichofuata baada ya hapo ulikuwa ni ugomvi mkubwa sana.

Songombingo lile likawakusanya majirani ambao walikuja hadi chumbani kutuamulia, mke wangu alikuwa na hasira za mbogo akaanza kupasua vitu vya ndani hovyo.

Wakati huo mwanangu asiyejua lolote alikuwa akilia muda wote. Ghafla ndoa ikawa chungu kama shubiri.

JE NINI KILITOKEA?
Tuliongozana hadi chumbani mtoto tukimwacha mikononi kwa dada wa kazi. Doreen. “Mke wangu,” nilimwita tukiwa chumbani.

Nasra au Doreen mkuu? Hapa umeniacha
 
SEHEMU YA 78

Alionekana kuchoka kwa urefu wa safari. Nasra alibaki ameketi kitako, macho yake yalikuwa mekundu na yaliyovimba kwa kilio. “Namtaka mwanangu! Kama kufa na nife mwanangu simwachi!” alipayuka na kuangua kilio ndani ya kito cha polisi.

Askari wakabaki wakishangaa,Nasra akazidi kuchanganyikiwa kwa kelele za kilio. “Kama ni makosa niliyafanya mimi!. Kama niadhabu nastahili nipewe mimi! Lawama na mateso yote nastahili! Lakini sio kumyima mwanangu haki yake! Haki ya kulelewa na mama yake mzazi anastahili....“

“Kelele ebo!! Kama hayo yote unayajua kwa nini ulivunja ndoa yako?” nikabwatukia kwa ukali. Ikabidi polisi wafanye kazi ya kumtuliza. Na kilichofanyika ni kumuingiza mahabusu, mimi na Debora tukakabidhiwa mtoto, lakini tukatakiwa kufika siku inayofuatia wakati polisi wanakamilisha uchunguzi.

Tukaondoka kurudi nyumbani, Nasra tukamwacha selo. nikawajulisha ndugu zangu juu ya mafanikio niliyapata katika songombingo lile.

Siku iliyofuatia tulirudi kituo cha polisi, kwa ajili ya mahojiano, nilionana na mkuu wa kituo ambaye aliniuliza maswali mawili matatu juu ya wizi ule na mimi nikamweleza ukweli.

“Kama ni hivyo mimi nadhani jambo hili mlimalize kwa hekima tu.”mkuu wa kituo alishauri “Kivipi?”

“Nadhani muweke makubaliano ya amani, juu ya mwanenu, unajua mtoto ni wenu wote, siyo vizuri mkiendelea kugombana kwa jambo hili.”

Tuliupokea ushauri wa yule kamanda, Nasra akachiwa huru. Baada ya kuwa huru, kwa pamoja tukazungumza naye, na tukakubaliana awe anakuja nyumbani kwangu kumsalimia mtoto muda wowote anaojisikia bila kuathiri hukumu ya mahakama.

Kuanzia wakati huo Nasra akawa anakuja nyumbani kwangu mara kwa mara kumjulia hali mtoto wangu.

Katika nyakati hizo, nikaja kugundua mwanamke yule aliachana na hawara siku chache baada ya ndoa yao, kuvunjika kwa ndoa yao ni baada ya kubainika kwamba alifunga ndoa ilihali akiwa bado ni mke wa mtu.

Nikaendelea kubaini kwamba, kumbe baada ya ndoa ile kuvunjika, bwana yule hakutamani tena kumwoa Nasra, akawa na wanawake wengine katika maeneo mbalimbali, huku nasra akibakia ndani akililia ndoa.

Penzi langu na Debora lilizidi kunoga, kama nilivyosema awali wote tulikuwa kwenye hamu kubwa.
 
Sehemu ya 79 .

Hata hivyo, kama wasemavyo Waswahili:

Kisicho riziki, hakiliki. Pamoja na penzi moto moto lililokuwepo kati yetu, huku suala la ndoa likizidi kugonga vichwa vyetu, nikaja kubaini kwamba, suala kufunga pingu za mausha na mwanamke yule lingekuwa gumu kutokana na jambo moja tu. Tofauti ya dini zetu.
Kwa kweli jambo hilo lilitukosesha raha, na hii ilichangizwa na sote kutokuwa tayari kuziacha dini zetu na kumfuata mwenziye.
Kikwazo cha dini kikayeyusha ndoto zetu, tukaendelea kuishi pamoja bila kufunga ndoa.

Maisha yangu na Debora yalikuwa mazuri sana, pesa na mafanikio niliyokuwa nayo ikanifanya nifurahie maisha wakati wote. Mtoto wangu Mwanda, naye akazidi kukua kwa kimo na hekima.

Mke wangu wa zamani,Nasra. Alikuwa akija kumwona mwanaye kila mwisho wa wiki, yanii jumamosi na jumapili. Na mara nyingi kila alipokuwa akifika, nilihakikisha haendi popote na mwanangu, walikaa kwenye bustani asubuhi hadi jioni. Alipondoka mtoto alibaki kwangu.

Kitendo cha kutokuwa huru na mwanaye kilikuwa kikimuudhi mno Nasra, lakini mimi sikujali, nilichokuwa nakitaka kwa wakati huo ni kubaki na mwanangu, japokuwa nilitambua nilikuwa nikikosea lakini sikuomwonea huruma hata kidogo mwanamke yule. Nilimwona ni binadamu asiyestahili kuonewa huruma.

Kila alipokuwa akifika kumwona mtoto, nilikuwa nikihisi hasira kali dhidi yake, mambo aliyonifanyia kipindi cha nyuma yalikuwa yakijitengeneza akilini mwangu mara kwa mara.

Kuna kitu nilisahau kukisimulia. Wakati mtoto wangu namrejesha mikononi mwangu, baada ya kuwa ameibwa na Nasra, kule Nguruka. Nilitafuta dada wa kazi. Msichana mdogo tu wa miaka kumi na tano au kumi na saba, binti huyo aliitwa Tatu.

Wakati mimi na Debora tukiwa bize na kazi, Tatu ndiye mara nyiingi alikuwa akibaki na Mwanda, alimwangalia asubuhi hadi jioni, alimwogesha, akampa chakula na kila kitu anachostahili mtoto.

Nilimpa tatu maelekezo juu ya utaratibu wa Nasra kumwona mwanaye.
Nilimwambia kila Nasra alipokuwa akifika nyumbani kwangu kumwona mwanaye, kama sipo nyumbani, ilikuwa ni lazima Nasra amwombe Tatu ndipo amwone mtoto, kisha Tatu naye sharti awasiliane aidha na mimi au mpenzi wangu Debora
 
Naomba unijulishe kila ukiweka muendelezo wa hizi story mbili,, yaan na ile ya ulinisaliti juliet
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom