Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

SEHEMU YA 85

Siyo makazini kwao hata majumbani mwao, ni viumbe wasiogopa lolote, sio watu wa kujishusha hata kama wao ndio wakosaji, wakati wote hujiona wako sahihi. Wanawake viongozi huathiriwa sana na mazingira.

Pamoja na kwamba ni watu wanaojua kupenda wakiwa wamezama penzini, lakini ni viumbe hatari na wajanja sana pale wanaokuwa wamekinaiwa na wapenzi wao. “Sikiliza wewe mwanamke…”nilisema.

Nikaendelea. Usiniletee siasa ndani mwangu, kimsingi kama hutaki kunipa maelezo ya kina juu ya mipira ya kiume iliyotumika humu ndani mimi na wewe basi.” “Kila la kheri Faraji.” Debora alikazia “Eeh!!” “Ndio ondoka.”

“Unanifukuza!!” “Kwani hapa ni kwa nani?” Debora alisema akiwa amenikazia macho. Nilishikwa na kizunguzungu, nikawaza sijui nimtandike vibao ila nikaona kwa wadhifa wake, nitaishia Jela. “Kumbe nawe ni mshenzi tu kama viruka njia wengine,”

Nikaunguruma. “Ni maoni yako juu yangu, nimeyapokea.” Alinijibu kwa pozi. Halafu akaniuliza tena. “Huondoki?” Ebwana wee! Nilipagawa. Uhusiano wangu na Debora ulikuwa unavunjika kama mzaha.

“Hustahili kuwa kiongozi, mnafiki na mkatili mkubwa, hustahili kuwa kioo cha jamii wewe.” “Hata hilo pia nalipokea. Haya ondoka kabla sijapiga simu moja tu, ukaishia lockup siku ya leo.” “Usinitishe wewe!”

“Sikutishi!” Debora alindelea kuongea kwa pozi tena kwa sauti ya kawaida ila iliyobeba ujeuri wa kiwango kikubwa. Akaendelea kunieleza. “Leo ni ijumaa, nikikutupa selo hutotoka hadi jumatatu, hilo usilisahau Faraji….Ishia zako.”

Ilikuwa halmanusura nicheke, mambo yalikuwa yamebadirika kama utani tena kwa kasi sana, mwanamke niliyemwamini na kumpa mapenzi yote leo alikuwa akinitishia ‘kuniswenteka’ ndani, kwa sababu tu alikuwa amepewa mamlaka. Ama kweli dunia uwanja wa fujo.

Sikuwa na namna Niliondoka. Nilikwenda kituo cha tax nikajitoma kwenye moja katika nyingi zilizokuwepo. “Twende.” Nikwambia dereva kwa amri “Wapi bosi?” “Buhongwa…kwenye Lodge yoyote nzuri.”

Tukaanza safari. Nusu saa badaye, tukafika Buhongwa kwenye lodge moja inaitwa Maganga. Baada ya kumlipa dereva, pia nikafanya malipo ya chumba, nikaingia ndani, huko nikalia kama mtoto.
 
SEHEMU YA 86

Ujasiri niliofundwa na marehemu baba yangu, kuwa mwanaume jasiri, nifichaye machozi yangu, nilishindwa. Mapenzi yalikuwa yananizidi nguvu ujasiri wangu.

Siku hiyo nililia hadi macho yakavimba, Debora naye alikuwa amenipiga pigo takatifu. Siku hiyo nililala pale. Asubuhi na mapema siku iliyofutia nikaondokea Nyegezi, nikapanda basi la Abood, nikarudi Dar es alama kuanza maisha mapya.

**** Baada ya kuwasili Dar es Salam, siyo kwamba maumivu ya kusalitiwa na kuachana na Debora yalikwisha. Laa! Niliendelea kuteseka mchana na jioni, kila wakati nilikuwa nammiss mwanamke yule. Nilivumilia kwa wiki mbili, tatu.

Lakini kadiri nilivyoendelea kuwa naye mbali ndivyo nilivyosahau vituko alivyonifanyia. Huku Msukumo wa kutaka nirudiane naye ukiwa mkubwa. Wakati mwingine nikawa naongea peke yangu, nikawa najiambia, lazima nivumilie. Lazima nimsahau Debora.

Lakini wapi bado moyo wangu ulimuhitaji mwanamke yule. Katika hali hiyo, nikawa naonekana kama nimerukwa na akili. Maneno maneno yakawa mengi mtaani. Wengine wakasema nimerogwa!!!. KATIKATI ya hali hiyo ndipo wakajitokeza marafiki na jamaa ambao sikusita kuwashirikisha katika mambo yanayonisibu.

Nilipewa ushauri mwingi tofauti, kuna walioniambia niachane na Debora, kama nilivyofanya dhidi ya mke wangu wa kwanza, Nasra. Ushauri huu sikuupenda kwa kuwa bado moyo wangu ulikuwa unamwitaji Debora.

Wapo walionishauri nimrudie, ikiwezekana nimwombe radhi tuanze maisha mapya. Hapa ngoja niseme kitu kimoja. Maishani mwangu nilikuwa na tabia moja. (nitaileza) tabia ambayo kimsingi siyo nzuri na ningependa mtu mwingine ajifunze kupitia mimi.

Kila nilipokuwa nikipitia wakati mgumu, nilikuwa napenda kusikiliza na kufuata ushauri ambao ulikuwa unanifurahisha nafsi, hata kama ushauri huo siyo mzuri, kwa kuwa tu umenipendeza ungekuwa swahiba wangu mkubwa kwa kunipa ushauri huo na mwisho wa maongezi ungeondoka na zawaidi kibao kutoka kwangu. Hivyo basi, watu wote walinishauri nirudi kwa Debora nilijikuta napenda nikae nao muda wote kisha tuzungumzie namna nitakavyorudi kwenye mikono ya Debora.

Na kwa kweli watu wangu walipoijua tabia hii walinipa ushauri vile nilivyopendelea mimi. Wachache sana waliokuwa wakiniambia ukweli
 
SEHEMU YA 87

Maishani mwangu nilikuwa na tabia moja. (nitaileza) tabia ambayo kimsingi siyo nzuri na ningependa mtu mwingine ajifunze kupitia mimi.

Kila nilipokuwa nikipitia wakati mgumu, nilikuwa napenda kusikiliza na kufuata ushauri ambao ulikuwa unanifurahisha nafsi, hata kama ushauri huo siyo mzuri, kwa kuwa tu umenipendeza ungekuwa swahiba wangu mkubwa kwa kunipa ushauri huo na mwisho wa maongezi ungeondoka na zawaidi kibao kutoka kwangu.

Hivyo basi, watu wote walinishauri nirudi kwa Debora nilijikuta napenda nikae nao muda wote kisha tuzungumzie namna nitakavyorudi kwenye mikono ya Debora. Na kwa kweli watu wangu walipoijua tabia hii walinipa ushauri vile nilivyopendelea mimi.

Wachache sana waliokuwa wakiniambia ukweli wa mambo ulivyo. Ndipo katika kuishi kwa mateso makubwa kwa masiku kadhaa, mwishowe nikafuata ushauri wa marafiki. Usiku mmoja wa saa nne nikampigia simu Debora.

Wakati simu ipo sikioni mapigo ya moyo yalikuwa yakinidunda kama vile simu ile ilikuwa imetegeshwa bomu kwamba itakapo pokelewa tu ingelipuka.
Simu iliita kwa muda mrefu, bila kupokelewa. Nikapiga tana. Safari hii iliita kidogo tu ikapokewa na sauti ya mwanaume.

“Hellow” sauti ya kiume ilisikika.
Nikajikutana nashindwa kuongea, fikra lukuki zikapita kichwani mwangu juu ya mtu aliyepokelea simu ya Debora. Mtu huyu ni nani? Hawara wake? Yupo na Debora kitandani usiku huu? Nilijiuliza kimoyomoyo
“Hellooow” suati ile ilinisemesha tena kwa nguvu.
“Mwenye simu yuko wapi?” hatimaye nikaunguruma.

“We ni nani?” jamaa naye akaniuliza kwa pozi. Nilihisi tumbo likifukuta joto. Nikaamini kivyovyote vile jamaa ni bwana wa Debora. “Wewe ni nani unayeniuliza mimi hivyo?” nikaunguruma tena kwa sauti yenye mamlaka.

Simu ikakatwa. Nikabaki nimeduwaa simu ikiwa bado imenata sikioni. Roho iliniuma vibaya sana, wivu wa mapenzi ukanichemka mwilini na nafsini.

Debora yupo na mwanaume mwingine wasaa huu. Kitandani! Wanafanya mapenzi au wamelala. Fikra hizi zilipita akilini mwangu, nikajikuta napatwa na donge rohoni.

Sikukoma. nikapiga tena. Safari hii nikajisemea kimoyomoyo kama akipokea tena yule jamaa mpuuzi, matusi yote ya duniani yangekuwa halali yake.
 
SEHEMU YA 88

Simu iliita kisha ikapokelewa. Naam! wakati huu aliyepokea alikuwa ni Debora.
“We nani?” Debora aliongea kwa ukali mara baada tu ya kupokea. Sauti yake ilionesha kama aliyetoka usingizini. Nilihisi akili ikinizunguka. Vipi leo naulizwa mie nani na Debora.

Mwanamke huyo aliyenipenda kwa hisia kali hadi kulia machozi, ambaye alifanya kila awezalo kunitoa katika machungu na simanzi ya usaliti wa mke wangu wa mwanzo, Nasra Mfaume. Akaahidi kunipenda maisha yake yote, leo ananiuliza mimi nani?

inamaana namba yangu alikwisha ifuta kwenye simu yake? Namba hiyo aliyokuwa ameishika kichwani mwake kama kiitikio cha wimbo wa taifa. Hata ungeamshwa usiku wa manane angetaja namba yangu kwa usahihi, amekwisha isahau na kuifuta kwenye simu yake?

Mambo yote hayo niyafikiria kwa harakaharaka sana simu ikiwa sikioni huku nikitakiwa kujibu swali nililoulizwa. Mimi ni nani?

“Hunijui Debora?” na mimi nikamuliza kwa upole. “Sauti yako sio ngeni.”
“Ebwana wee!” nilimaka.
“Niambie wewe nani?” akaongea kwa amri.
“Hebu amka usingizi. Unashindwaje kunijua leo.”

“Kama hutaki kusema wewe ni nani nakata simu.” Debora akang’aka.
“Faraji.” Hatimaye nikasalimu amri, nikajibu kwa mkato huku nikihisi hasira kali rohoni.
“Unasemaje?” akaniuliza kwa kiburi.
“Ushanijua ama bado hujanikumbuka?”
“Sema shida yako.”

“Ulimpa nani simu yako Debora?”
“Hiyo ndio shida uliyonayo?”
“Tuanzie hapo kwanza kisha nitakueleza sababu ya kukupigia.”
“Wewe kama nani unaniuliza swali hilo?”
“Hujui mimi ni nani kwako?” “Hebu zungumza mambo sensitive we’ mtu, maswali gani hayo unauliza?”

“Ni wiki mbili tu zimepita tangu tutarafiane, leo mwenzangu ushapata mwanaume mwingine.”
“Kwani kuna kanuni ama utaratibu wowote katika hilo?”
“Nisikilize Debora…” nilisema. Nikaendelea.

“Usiwe kama Nasra, wewe ni mwanamke wa kipekee sana, nakutegemea kwenye maisha yangu. Tafadhali.”
“Sikia wewe!!” Debora aliongea, ni kama vile alichukulia nilikuwa mpuuzi mmoja nisiye jielewa.

“Usiwe mwanaume mpumbavu…”aliniambia. Akaendelea.
“Mrudie mkeo mlee mtoto wenu. Mimi tayari nina maisha yangu mapya, ni mwanamke wa kigogo mkubwa tu hapa nchini, kama hutaki kupata matatizo kwenye biashara zako kaa mbali na mimi.
 
SEHEMU YA 89

Maneno yake yalichoma ndani kabisa kwenye nyama ya moyo wangu, nikahisi maumivu ambayo sikuwahi kuyasikia kabla, mate mepesi nayo yalinijaa kinywani.

Maumivu ya kuachwa yalikuwa makali zaidi ya jeraha la kisu.
Sikujua simu ilikatika muda gani, ninachokumbuka nilijikuta nashindwa kuona vizuri kutokana na machozi yaliyokuwa yamejikusanya kwenye mboni za macho yangu.

Kwa mara nyingine katika maisha yangu, nikajikuta nalia kama mtoto mdogo kwa sababu ya mapenzi.

“Wanawake wote, kasoro mama yangu mzazi na mlaniwe.” nilinong’ona kibwege machozi yakitengeneza mifereji mashavuni pangu.
“Nakosea wapi mimi!” niliendelea kuogea mwenyewe.

Usiku ule ulikuwa mrefu mno chumbani mwangu, kila wakati sauti ya Debora ikinisihi nikae naye mbali ilijirudia akilini mwangu. Niliamini sikuachwa na wanawake wale wawili, kwa sababu sina pesa. Laa!. Bali sikuwa nimeweka mizizi ya kudumu katika nyoyo za watu wale wawili.

Hakika Mungu hakupi vyote, nimepewa mali na fedha, nimenyimwa penzi la kweli. Mkosi huu.

Nikiwa katika tafakuri taswira fulani mawazoni ikanizoa, ikanipeleka hadi Mwanza, nikajiona nipo chumbani kwa Debora. Nimesimama mbele ya chumba ninachokitambua.

Mbele yangu namwona Debora akiwa amejilaza, akiwa mtupu. Amelala kihasara hasara, mwanaume wa miraba minne yupo kando ya kitanda, mikono yake ikifanya ziara kwenye kiwiliwili cha Debora.
Nikaendelea kumwona Debora akijinyonga nyonga huku akitoa sauti ya mahaba, kama vile alivyokuwa akinifanyia mimi, sasa anamfanyia mwanaume mwingine.

Ndani ya chumba nilichokizoea tena kwenye kitandani ninacho kifahamu.
Debora hanijui tena. Amenisahau kabisa kama aliwahi kinipenda. Penzi langu anagawiwa mtu mwingine.

Kadiri taswira hiyo ilivyozidi kupita kwenye akili yangu ndivyo wivu wa mapenzi ulivyozidi kunifukuta kifuani. Maumivu yakawa makali hatimaye. Nikakata shauri ya kuishi. Nikaona heri nife.

Fikra za kujinyonga kwa kamba zikaanza kutekenya ubonga wangu, nikamini njia pekee ya kuondokana na maumivu ya mapenzi ni kujiua. Nikaitafuta kamba ili nijiue.

ITAENDELEA JUMATATU...
 
Hapo sasa Faraji ameanza kuwaza kama mwanaume. Alaaaaaah hehehe
Sawasawa
Ajiue bwana. Mambo gani ya kipumbav kuteswateswa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom