Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

Simulizi: Baradhuli mwenye mikono ya chuma

***SURA YA KUMI***


(MSIMU WA 02)







Akiwa amejitanda khanga, mama Miraji alikuwa ameketi kwa utulivu juu ya kitanda pamoja na mwanae mkubwa wa kiume asiye na fahamu.



Umbali wa hatua chache tu alikuwa amejilaza Jombi. Hakuonekana tofauti na Miraji kwa kutulia kama maji ya mtungini. Kitu pekee kilichokuwa kinaonyesha kwamba wapo hai ilikuwa ni pumzi tu waliyokuwa wanatoa ikiashiriwa kwa kutanuka na kusinyaa kwa vifua vyao.



Kila baada ya muda kidogo, Mama Miraji alihamia kitanda kingine na kutazama mgonjwa. Alifanya hivyo kwa mara tatu, akanyanyua simu yake na kupiga.



“Haloo inspekta … Eeh baba, mbona kimya sana siku hizi sikuoni, kuna tatizo? … He! We! We! We! … Mbona hukunambia baba? … Mungu wangu! … sasa hivi upo wapi? … eeh we nielekeze tu … Haya, naja baba … muda si mrefu.”



Mama Miraji alisimama akiwa na uso wa papara. Alivaa viatu vyake vilivyokuwa vimeacha miguu kipindi amekaa kitandani akatoka nje ya wodi. Akiwa anatembea haraka, alikatiza mtaa mpaka kituoni alipopanda daladala na kuelekea kwa inspekta. Inspekta akiwa amejilaza kochini na sura iliyojaa uchovu, sauti ya mama Miraji iliita mlangoni.



“Hodiii!”



Inspekta alinyanyuka akaenda kumfungulia mlango. Waliketi sebuleni wakaanza kuteta juu ya vifo vya familia ya inspekta, habari hizo zikionekana kumshangaza na kumstaajabisha mama Miraji. Katika wasaa huo, Kaguta alitia miguu nyumbani hapo naye akaungana na maongezi. Baada ya muda usiozidi lisaa, mama Mriraji aliaga akaondoka, wanaume wakabaki wenyewe.



“Vipi, mbona hukunipa taarifa?” Inspekta aliuliza. Kaguta alitabasamu akasugua viganja vyake.
“Mwanangu, acha tu. Nimefika pale nikakuta wadada watatu visu.”
“Eeeh … mi ndo’ mana nilikuwa sitaki uende!”
“Aaah baba … Hakuna kilichoharibika mbona. Sema nimetumia teknik moja matata sana, itanufaisha pande zote mbili.”



Inspekta hakutia neno, aliacha macho yake ya mshangao pamoja na kebehi yamtizame Kaguta.



“Sasa nikawaza nitumie njia gani ya kumwingilia. Maana huwezi tu ukaanza eti wewe unamjua mwanaume mmoja alikuja hapa kununua barua sorry bahasha. So nikaanza kutumia njia laini, mtoto akatabasamu…”
“Sasa ni hivi, kesho naenda mwenyewe.” Inspekta alimkatisha Kaguta.
“Wapi?”
“Hapo stationary, naona unazingua tu, Kaguta.”
“We vipi Vitalis? … Nimekuambia hiyo kazi nitaifanya mie. Tatizo lako unataka kila mtu atumie njia zako. We acha nikuonyeshe sio tu njia yako ndio ielekeayo mbinguni.”



Inspekta alitikisa kichwa chake akanyanyuka na kuliendea jokofu akatoa chupa ya maji ya baridi na kuiweka mezani akiambatanisha na kikombe. Alipiga mafundo kadhaa akajilaza kochini. Kaguta alimtizama mwenzake akapiga mguno wa kicheko.



“Hivi umekula hata? … Alafu nikuambie kitu, ungemuambbia yule mama akupikie. We umemuacha kaenda hivi hivi.”



Inspekta kimya.



“Ila usikonde mwanangu mimi si nipo. Nitakupikia.”



Inspekta akashtuka. “Hapana! Leo napika mimi. Ule ugali wa jana hapana. Ugali una sura ya dodoki, uji mixer mabuje, mweh mtori si mtori. Ah ... ah!” Inspekta alinyanyuka akaelekea jikoni. Kaguta alibaki sebuleni akicheka mbavu hana.



Usiku wa siku hiyo uliishia nyumbani kwa inspekta. Asubuhi ya saa kumi na mbili ilipojiri, Kaguta alikuwa yupo kwenye gari lake tayari amevaa na kujiweka sawa. Aliondoa chombo mpaka maeneo ya mwenge akapaki sehemu ya wazi na kurusha macho yake chini ya mwamvuli wa kituo cha daladala. Kulikuwepo na watu kadhaa ambao Kaguta aliwatizama na kuachana nao.



Alikuwa kama kuna mtu anamtafuta ama kumngojea. Ilipofika mida ya saa moja Kaguta akiwa anapiga piga mihayo, alimshuhudia Sandra akiwa ndani ya sare anajongea kwenye kituo cha daladala akaketi pembezoni ya mwamvuli. Kaguta alitabasamu kisha taratibu akalisogeza gari lake eneo alilopo mwanamke Sandra. Alishusha kioo akamtizama Sandra na macho yaelezeayo utulivu na dhaka ya uanaume wa kistaarabu.



“Twende basi nikupeleke mama.”



Sandra alitabasamu akatikisa kichwa. Alinyanyua miguu yake minene na kufuata gari akienendea mlango wa nyuma. Kaguta alimshtua na kumtaka akae naye mbele. Sandra hakuleta ubishi, alihamia mbele akaketi na Kaguta.



“Umependeza.”
“Mmmh jamani, kweli?”
“Kweli.”
“Mbona nilikuwa hivi hivi hata jana?”
“Kila siku ni tofauti, unajua?”
“Ahsante sana.”
“You are welcome.”



Walinyamaza kwa muda. Baadae kidogo Kaguta alivunja ukimya.



“Hivi mfano nikitaka kuandika barua, mnaweza mkanisaidia pale ofisini kwenu?”
“Barua ya aina gani?”
“Ya kiofisi labda … ”
“Naweza nikakusaidia.”
“Wenzako je?”
“Hapana, haiwezekani. Labda kama ni ushauri ila si kumuandikia mtu barua. Kwanini umeniuliza?”
“Basi tu. Nilikuwa nina shida ya kuandikiwa barua.”
“Lini?”
“Hata leo.”
“Twende ofisini naweza nikakusaidia.”



Waliposhuka mbele ya ofisi, waliongozana mpaka ndani. Wahudumu wengine wawili walikuwa tayari wameshafika, walisalimiana, Kaguta akakabidhiwa kiti kilichokaa mbadala na meza iliyobebelea tanakilishi.



“Fungua Microsoft Word uendelee, nakuja. Au hujui?” Sandra alimuongelesha Kaguta.
“Najua. Ila usichelewe basi.”
“Usihofu, napanga panga hapa nakuja.” Sandra alisema kisha akafuata shelvu na kupukutisha faili kadhaa akaanza kuzipekua. Kaguta alivuta kipanya akabofya program ya Microsoft word. Ilipofunguka alifungua karatasi mpya na kuanza kuandika mithili ya barua hapo.



Huku macho yake yakiwa na tahadhari, muda mwingine Kaguta aliacha kuandika barua na kuanza kupekua nyaraka zingine zilizoandikwa karibuni. Alizifungua na kuzipekuwa kwa siri moja baada ya nyingine. Alizimaliza zote lakini haikuonekana hata moja iliyokamata hisia zake. Alinyanyua shingo akatizama tanakilishi za wahudumu wengine. Kwa siri alipenyeza mkono wake kwenye C.P.U akanyofoa nyaya fulani, tarakilishi ikazima.



“Sandra, imezima.”
“Hilo computer nalo!” Alilaumu Sandra huku akisogea karibu ya Kaguta. Aliitizama tanakilishi huku akijaribu kuiwasha bila ya mafanikio.
“Winner!” Sandra aliita.
“Abee!” Mwenzake aliitikia.
“Naomba huyu kaka aje hapo kwenye PC yako mara moja anahitaji kuandika barua, yangu imezima.”
“Mwambia aje tu. Ila kaka fanya haraka kuna kazi zinanisubiria.”
“Hana utaalamu sana na hayo mambo.” Sandra alimtetea Kaguta.
“Usiofu nitajitahidi tu. Si unajua tena ukiwa shidani.” Kaguta alijikomboleza huku akielekea kwenye tanakilishi elekezi. Alikaa na kufungua karatasi mpya akawa anaandika mithili ya barua. Ila kwa wakati huo huo akaanza kuufanya mchezo aliokuwa anaufanya hapo awali; wa kufungua na kusoma nyaraka zilizopata kuandikwa hapo mapema.



Wakati anafungua fungua, alikutana na nyaraka iliyobeba jina la Robson. Ndani ya hiyo nyaraka kulikuwa na nyaraka ndogo ndogo nane. Moja baada ya moja, Kaguta alianza kuzifungua kwa kuibia.



Nyaraka ya kwanza ilikuwa barua;



Kwako mshenzi mpuuzi.



Barua hii haina kichwa cha habari ila punde itadai kichwa chako na cha mshenzi mwenzako.



Hili ni onyo. Acha kutufuatilia. Endapo ukikaidi, utajuta wewe na kizazi chako.



By Mchinjaji Batili.




Kabla hajaendelea kusoma nyaraka nyingine, Kaguta aliingiza mkono mfukoni mwake akatoka na flash. Alikata sauti ya tanakilishi kwa kuhofia inaweza toa mlio wa tahadhari atakapoiunganisha na flash. Kwa haraka alinyonya nyaraka zile kisha akaendelea na igizo lake la kuandika barua.



Baada ya dakika chache Sandra alimjia Kaguta wakasaidiana kumaliza barua. Kaguta alitoa pesa barua ikaprintiwa akakabidhiwa kisha aliaga akaondoka zake.



“Mmmh Sandra, umemtoa wapi huyo kibopa?” Winner aliuliza kwa kipashkuna. Sandra alitoa cheko nene akalegeza na kurembua macho yake.
“Watu na bahati zao bibi eeh …”



Wote wakaangua kicheko na kugongeshana mikono. Hawakujua, Kaguta aliyekuwepo kwenye gari akielekea nyumbani kwa inspekta alikuwa amebebelea nyaraka muhimu, na si tu muhimu bali za siri.



Ndani ya dakika zisizozidi kumi na tano, Kaguta akawa tayari yupo nje ya nyumba ya inspekta. Upesi alishuka garini na kuingia ndani. Alimuita inspekta sebuleni akimuagiza aje na tanakilishi mpakato (laptop). Inspekta alikuja sebuleni akapokelewa na taarifa za Kaguta huko atokako. Waliketi na kuanza kuperuzi nyaraka zilizokombwa toka Rosemath Stationary.



“He! Kaguta. Hii ndio barua niliyotumiwa!” Inspekta alitahamaki kuona nyaraka yenye maandishi sawa sawa na yale aliyopata kuyasoma pindi mtoto na mke wake walipouwawa.
“Ina maana na hiz barua zingine ni mauaji tayari yameshafanyika?” Kaguta aliuliza.
“Bila shaka.” Inspekta alijibu. Waliendelea kufungua na kuzisoma barua. Walipofika kwenye nyaraka moja kabla ya kuifungua, walishangaza na maelezo ya juu yake.



Ilikuwa imebebelea tarehe ya kesho kutwa. Walipoifungua na kuisoma, walikuta maudhui yale yale ya mauaji. Mwisho wa barua anwani ya eneo inapotakiwa kutumwa ikiwa imewekwa. Inspekta na Kaguta walitizamana kwa mshangao. Hata pale waliposoma barua mbili zilizosalia, mtindo ulikuwa ni ule ule wa tarehe ya siku za mbele ikiwa imebeba miadi ya kuchinja na mchinjaji batili.



“Kwahiyo ina mana kuna mtu anapewa kuzipeleka hizi barua, ama? Anwani za nini?” Kaguta aliuliza.



“Ngoja kwanza. Tusachi hizi tarehe za barua zilizopita tuone kama kweli zote zina mauaji.” Inspekta alitoa wazo. Walifungua mtandao na kuweka tarehe zile husika, majibu yakaja yakionyesha mauaji sehemu mbali mbali jijini Dar es Salaam. Wahusika wakiwa wamechinjwa.



“Kazi ipo, Vitalis.” Kaguta alinena.
“Inabidi tuzuie mauaji haya ya mbele. Lazima tumtie huyu mshenzi nguvuni. Ila kuna haja ya kurudi Rosemath Stationary.”
“Kufanya nini?”
“Inaelekea kuna mambo mengi ya kuyafahamu huko.” Inspekta alisema, Kaguta akatabasamu.
“Si nilikuambia. Niamini. Ila mwanangu kuna mtoto kisu!”
Inspekta alitabasamu akamshika rafikiye bega; “Fanya kazi kaka.”
“Sijakataa. Ila siwezi nikamuacha.”
“Haya. Kumbuka upo kwenye mdomo wa simba.”
“Wala! Wao ndio wapo kwenye mdomo wa mamba.”



Inspekta alitabasamu baada ya kusikia hiyo kauli. Alinyanyuka akaelekea jikoni na kurudi na sahani iliyo na maandazi manne na mayai mawili ya kuchemsha pamoja na kikombe cha chai, akaweka mezani kisha akaleta na maji ya kunawa.



“Karibu.”
“Ahsante. Ulijuaje kama nina njaa?”
“Si ulitoka bila ya kunywa chai.”
“Nashukuru sana.”
Kaguta alinawa mikono akamega andazi.
“Mmmh … umenunua wapi haya?” Alitahamaki.
“Kwani vipi?”
“Matamu!”
“Nimepika mwenyewe.”
“Wapi wewe. Au yule madha kaja kukupikia?”
“Nimepika mwenyewe. Unadhani mimi kama wewe?”
“Aisee kama unajua kupika hivi, ulioa ya nini?”
“Umeanza mambo yako sasa.” Inspekta alisema kisha akanyanyuka. “Naelekea chumbani, ukimaliza utanikuta huko.” Aliongezea na kuanza kuondoka.
“Poa. Ila zingatia ushauri wangu.”
“Upi?” Inspekta alisimama akamtizama Kaguta aliyekuwa anakunywa chai.
“Yule mama yule.”
“Mama yupi?”
“Mama Miraji.”



Inspekta alisonya akitikisa kichwa chake na kujiondokea.




Masaa yalichukua nafasi na kuuleta usiku kwa kasi. Inspekta pamoja Kaguta hawakwenda popote katika wasaa huo, waliketi sebuleni na kuchosha macho yao kwa kuangalia movie za kizungu. Usingizi ulipowaahidi makao, walizima kila kitu wakaenda kulala. Ndani ya asubuhi ya mapema, Kaguta alidamka na kumwacha inspekta kitandani.




Alichukua shati la inspekta kabatini akalinyoosha na kuliweka mwilini. Alipanda gari akaelekea moja kwa moja kule alipokwenda jana yake; maeneo ya Mwenge.




Alikaa hapo kusubiria, ndani ya muda mfupi mno akatokea mwanadada Sandra. Ila hakuwa mwenyewe, alikuwa anaongozana na mwanaume mmoja mrefu wa wastani akiwa amevalia suti ya kijani. Walikuwa wanateta. Kabla ya Kaguta kusogeza gari lake aliwatizama kwa dakika zisizozidi mbili akapiga ngumi usukani.




***

☆Steve
 
***SURA YA KUMI NA MOJA***



(MSIMU WA 02)





“Mbona haondoki?” Aling’aka. Aliwasha gari akalisogeza mpaka mbele ya Sandra, akapiga honi na kushusha kioo.
“Mambo?” Kaguta alirusha salamu.
“Poa, vipi?” Sandra alijibu na kurudishia.
“Shwari tu.” Kaguta alijibu kisha akamtazama yule mwanaume aliyekuwa Sandra.
“Oya vipi?” Kaguta alisalimia. Mwanaume yule hakusema kitu. Alimtizama Kaguta kwa macho makali. Sandra alijitabasamisha akaaga;
“Mi naondoka Roby. Baadae.” Alimwambia mwanaume aliyekuja naye kisha akafuata gari la Kaguta na kuondoka.
“Jamaa yako nini yule?”
“Hamna ni mfanyakazi mwenzangu.”
“Mbona jina lake la kike, Roby?”
“Ha ha ha hapana. anaitwa Robson. Sema huwa nafupisha tu.”
“Anaitwa Robson?”
“Ndio.”



Uso wa Kaguta ukaonekana kumezwa na mawazo. Ni kama vile alisikia kitu cha kushangaza. Japokuwa macho yake yalikuwa yanatizama mbele, lakini alionekana hayupo pale kifikra. Nyuma yao, Robson bado hakuwa ameondoka pale kituoni. Alikuwa analitizama gari la Kaguta likiishia. Lilipopotea kabisa, alitoa simu yake mfukoni akapiga.



“Yeah … nimemuona yule jamaa wake inspekta … yupo na Sandra … Muda si mrefu … Fanya uje unichukue hapa kituoni …”




Alikata simu. Baada ya muda kidogo, pikipiki ilkuja kumchukua. Ilikuwa ni pikipiki ile ile iliyomfuatilia inspekta na Kaguta siku zile.



“Twende huku! Fasta!” Robson alimuelekeza mwenzake akinyooshea kidole kule gari la Kaguta lilipoelekea. Pikipiki ilendeshwa kwa kasi. Baada tu ya muda kidogo, waliliona gari la Kaguta.




“Walee! Wafuatilie taratibu tu tuone wapi wanaelekea.” Robson aliwika. Dereva wa pikipiki aliweka sawia pikipiki yake kwenye mstari lililopo gari la Kaguta kisha akapunguza mwendo.
“Inabidi huyu mpumbavu afe. Si chini ya leo na kesho. Huwezi jua amepata nini toka kwa Sandra.” Robson alimwaga maneno.
“Kweli. Ila inabidi tuwe makini, mkuu. Hawa jamaa wapo vizuri.”
“Hamna lolote!” Robson alipuuza, “wapo vizuri kwa watu wengine, si kwangu.”



Dereva hakutia tena neno. Wote walinyamaza wakawa wanatizama mbele waendako. Baada ya muda mfupi, polisi wa barabarani aliwapungia mkono na kuwataka wapaki chombo pembeni.




“Shit! Nini tena hiki?” Robson alilalama.
“Tusimame, mkuu? … au nipitilize?” Dereva aliuliza.
“Simama tuepushe matatizo mengine.” Robson alitoa maelezo. Pikipiki ilisimama ikapaki pembezoni mwa barabara, polisi akasonga.
“Habari zenu?”
“Safi tu afande, za kazi?”
“Njema. Kwenu helmet ni nini?”
“Helmet?”
“Ndio, hujanisikia? … kwenu nyie helmet ni nini?”
Dereva aligeuza shingo akamtizama Robson.
“Samahani Afande, tumesahau.” Robson alijitetea.
“Sawa mie naweza nikakusamehe lakini ajali je? Umeipa taarifa?” Afande aliongea kwa sura isiyo na utani. Robson alitazama barabara akaona gari la Kaguta linaishia. Haraka alishuka akangiza mkono wake mfukoni na kutoa shilingi elfu hamsini.
“Poza basi na hii, Afande. Tuache twende.”
“Kwahiyo unanihonga, sio?” Afande aliuliza kwa kebehi. Ghafla, bunduki ndogo ikadondokea kiatu cha Robson. Alikuwa kaiweka nyumaya suruali kiunoni. Afande alipoona bunduki, alitoa macho kwa kustaajabu. Upesi alinyofoa bunduki yake iliyokuwa imekaa kwenye kamfuko kadogo hips ya kulia akawanyooshea watuhumiwa.
“Mikono juu! … Sogeza hiyo bunduki huku!” Afande aliamuru. Robson alipiga teke bunduki kumfuata Afande.
“Shuka! … Upesi! … Nimesema mikono juu!” Afande alimwamuru dereva. Dereva alishuka akaungana na mwenzake aliyesimama mikono ikiwa hewani.




Afande alitoa radio call yake iliyokuwa imeshikishwa na kamba kifuani akaweka kinywani na kupasha taarifa wenzake. Ndani ya muda mfupi, defender ilikuja ikiwa na maaskari watatu, Robson na mwenzake wakaswekwa ndani ya gari pamoja na pikipiki yao.Upande wa pili wa shilingi, gari la Kaguta lilikuwa tayari lishatua mbele ya ofisi ya Rosemath Stationary.



Kaguta alishuka akamfungulia mlango bibie Sandra mithili ya malkia. Sandra alishuka kwa mbwembwe na madaha, wakaongozana na Kaguta kwenda ndani.




“Karibuni!” Winner aliwakaribisha kwa tabasamu pana.
“Ahsante, Winner. Tumekaribia.” Sandra aliitikia.
“Habari za asubuhi?” Kaguta aliwasalimu wadada wawili aliowakuta; Winner na Rahma.
“Njema tu. Za kwako?”
“Safi. Mmependeza mno kama vile mwaenda maonyesho.”



Winner na Rahma walicheka kusikia hilo.




“Ahsante. Hata wewe pia umependeza.”
“Mmmh … kweli?”
“Kweli.”
“Basi kheri. Mungu ashukuriwe.”
“Sio mke?” Winner aliuliza kichokozi. Sandra na Rahma wote wakamtizama Kaguta.
“Hapana jamani. Sijaoa mie, nipo nipo tu. Single but lazy to mingle.”



Wanawaka wakadondosha cheko tena.




“Vipi lakini, mlifanikiwa kutengeneza ile computer yenu?” Kaguta aliuliza kwa kumtazama Sandra.
“Hapana! … Yani hapa mpaka fundi aje.”
“Ohoo! … Huyo fundi anakuja lini sasa?”
“Anaweza akaja siku yoyote, tumeshawasiliana na bosi.” Rahma alieleza.
“Mpaka aje huyo fundi si mmepata tabu sana. Naweza nikajaribu kuitengeneza?” Kaguta alijinasibu.
“Unaweza tu. Huogopi kupigwa shoti?” Sandra aliuliza.
“Hapana. Kwani hutaki nife?”
“Ndio sitaki!”
“Kwanini? … unaogopa mzoga ofisini mwako?”
“Hapana. Sitaki tu ufe.”
“Ahsante. Nimefurahi kusikia hilo.” Alisema Kaguta na kusogelea tanakilishi ya Sandra. Huku kichwa chake kikienda huku na huko, alipepesa macho yake kuitizama tanakilishi kama mtu atafutaye kitu kibovu.




Baada ya kuzunguka zunguka na kutizama tizama aliketi kwenye kiti na kufungua CPU. Wakati huo Sandra na wenzake walikuwa wakiendelea na shughuli zao zingine.



Kaguta alishika waya aliouchomoa siku ya jana yake, akauchomeka na kuwasha tanakilishi, ikawaka. Kabla ya kuwaambia wakina Sandra alichomeka flash yake na kuanza kunyonya mafaili kadha wa kadha. Alipomaliza, alishusha pumzi ndefu akatabasamu.




“Tayari! … Njoeni muone.” Alitangaza ushindi. Haraka, Sandra, Winner na Rahma wakajongea kuja kuona ya Musa.
“Wow! … Kumbe we ni fundi?” Sandra alitahamaki.
“Tutakuwa tunakuita wewe uje kututengenezea.” Winner aliongezea.
“Nashukuruni sana. Sema nimegundua kuna kitu kina mushkeli kidogo kwenye PC zenu. Kama mnaweza kuniruhusu, ningependa kurekebisha kwenye mashine ya kila mtu ili isije kuwasumbua tena.”
“Anza na ya kwangu!” Winner aliwahi kunyoosha mkono.
“Mie wala sishindani. Ukimaliza tu baba hamia kwangu.” Rahma alisema kwa mng’ao wa tabasamu.
“Basi sawa.” Alisema Kaguta kisha akanyanyuka kuifuata tanakilishi ya Winner na kuanza kuipekua pekua kama vile anatafuta ufunguo uliopotea mchangani.




Alipopata wasaa aliketi na kunyonya mafaili ambayo hayakubeba jana. Kila kitu kilichokuwa kwenye faili alikibeba na kukitupia kwenye flash. Mchezo ukawa huo huo na kwenye tanakilishi ya Rahma. Alipomaliza aliweka flash yake mfukoni akasimama na kujinyoosha.




“Tayari jamani. Mie naomba niende tu.”
“Umemaliza?” Rahma aliuliza.
“Ndio. Nimekamilisha kila kitu.” Kaguta alisema kwa majivuno.
“Ahsante sana. Tukulipe sh’ngapi?” Winner aliuliza.
“Aaah jamani, mnilipe tena? …Wala! Mie nimewafanyia tu.”
“Ahsante sana. Alafu wenzako hatujui hata jina lako, yani tunashindwa hata tukuiteje.” Rahma alitanabahi.
“Naitwa Alkareem.”
“Unafanya kazi wapi?” Rahma aliongezea swali.
“Mmm … Nanyiee! Mbona maswali mengi!” Sandra aliingilia kati. Kaguta akamtuliza;
“Acha tu waulize.” Kisha akamgeukia Rahma,“Mimi ni mjasiriamali. Nachukua mizigo toka China kuileta hapa.” Kaguta alijibu kimujarab. Wanawake wakatabasamu na kushukuru wakaendelea na kazi zao. Kaguta alimsogelea Sandra akamnong’oneza.
“Please naomba nikutoa dinner leo?”




Sandra alitabasamu akamtizama Kaguta kwa macho fulani hivi yasemayo ahsante.




“Sawa. Haina shida., utancheki basi kwa namba yangu.” Mwanamke alisema kwa sauti yake nyororo. Kaguta alimtizama akalamba lips zake. Aliaga wakina Winner na kufuata gari lake akahepa.
“Mmmh … Sandra umeshanshinda tabia, mama.” Winner alisema huku akishikilia kiuno chake. “Naona unawaokoteza tu, utuachiage na sie mweh!”
Rahma na Sandra wakaangua kicheko.
“Nakuambia mahandsome wote yeye. Kuanzia Roby mpaka Alkareem.” Rahma alijazia maelezo.Sandra aliangua tu kicheko, alipomaliza akashika kiuno.
“Jamani sijawaambia kilichonitokea leo. Si nilikuwa na Roby wakati nakuja kupitiwa na gari!”
“Enhe?” Rahma alidakia. “Ikawaje na ninavyomjua Roby kwa wivu.”
“We acha tu. Niliaga nikaondoka ila ile hali niliyomuacha nayo. Sijui!” Sandra aliongea na kubinua mdomo wake.
“Kuwa mwangalifu, mama. Si unajua Roby si mtu mzuri?” Winner alishauri. Waliacha kupiga stori wakaendelea na kazi.




Upande wa kwanza shilingi, nje ya kituo kikubwa cha police Oysterbay, Robson alionekana akiwa na dereva pamoja na mwanaume mwingine mzee aliyevalia shati la kitenge na suruali nyeusi ya kitambaa. Walikuwa wanatembea wakitoka eneo la polisi, dereva akiwa anakokota pikipiki. Walipolifikia gari jeusi aina ya Suzuki Escudo, walisimama hapo.




“Kuweni makini bwana. Mim sitokuja kuwatoa tena kwa makosa ya kizembe kama haya. Umesikia Roby?”
“Ndio.”
“Umesikia Yobo?”
“Ndio.”




Mwanaume yule aliyevalia shati la kitenge alishika mlango wa gari, Roby akamuita.



“Ila bosi. Kuna jambo nataka nikueleze.”
“Nini tena, Roby?”
“Kuna mtu anatusumbua, tunataka tummalize.”
“Sasa? … Unataka nini? … Si ummalize?”
“Nahitaji pesa bosi.”
“Unataka kiasi gani Roby? … na huyo mtu ni nani kwani?”
“Ni jamaa fulani hivi, mjinga mjinga hivi, mmojawapo wa wale waliowauwa wenzetu.”



Mzee kusikia hivyo, alitahamaki.




“Ina mana mpaka leo hii wapo hai? … Roby unafanya kazi gani sasa?”
“Hapana bosi … tayari tumeua familia ya mmoja wao.”
“*** you! … Familia yao ndio umepunguza idadi yetu? …kwahiyo ina mana bado wote wawili wapo hai? … What the *** are you doing? Umeshindwa kazi?”
“Hapana bosi!”
“Hapana nini? … Baadae uje kuchukua pesa, na nakupa wiki moja tu sitaki kusikia ushuzi wa hao watu.” Mzee alifungua mlango wa gari akaingia na kuubamiza kwanguvu. Aliwasha gari akapotea.



“Tuondoke, Yobo.” Robson alimwamba dereva wakapanda pikipiki nao wakaondoka.




****
☆Steve
 
***SURA YA KUMI NA MBILI***




(MSIMU WA 02)






****
Pipiiii!



Kaguta alipiga honi nje ya nyumba ya inspekta. Alishuka akiwa na furaha mkononi kabebelea flash yake. Huku akipiga mluzi alitembea kwa kudunda mpaka mlangoni. alifungua mlango akamkuta inspekta pamoja na mama Miraji. Tabasamu la uongo likajaa usoni mwake.




“Habari zenu jamani?”
“Njema tu. Karibu.” Mama Miraji alisema kwa tabasamu wakati inspekta akiwa kimya anamtizama tu Kaguta.
“Ahsante … Ahsante sana, mama.” Alisema Kaguta bila hata ya kuingia ndani. Alimrushia inspekta flash kisha akamkonyeza.
“Mie wala siingii. Nilikuja tu kuleta mzigo huo, baadae!” Alisema Kaguta, kabla hata hajajibiwa alishafunga mlango na kushika njia.
“Mbona hujamkaribisha mwenzio?” Mama Miraji alimuuliza inspekta. Inspekta alitikisa kichwa akaguna.
“Ana yake huyo. Si mgeni wa kukaribishwa.”



Mama Miraji alitabasamu na kucheka kidogo; “Haya bana, waarabu wa pemba mwajuana kwa viremba.”




Walicheka kwa pamoja kisha wakatizamana kama watu wasio na maneno mapya ya kuongea.



“Sasa … acha basi nikuandalie chakula mgeni wangu upate kula.” Inspekta alinyanyuka.
“Hapana bana. Usijichoshe bure.”
“Bure? … si bure kukupikia. Nisingependa mgeni utoke hapa bila ya kutia chochote mdomoni maana hata kinywaji umekataa.”
“Hamna shida bwana, inspekta. Mie nipo sawa tu.”
“Tia hata sunna basi.”
“Mila zetu haziruhusu mwanamke kukaa alafu mwanaume aingie jikoni. Naomba basi nikusaidie kupika.”
“Jamani, mgeni tena?”
“Kwani kuna shida?”
“Hapana. Haya twende nikuelekeze. “



Mama Miraji alisimama na kuongozana na inspekta mpaka jikoni. Wakati akiwa anapika, inspekta alileta tanakilishi mpakato yake sebuleni akachomeka flash na kuanza kuperuzi kilichowekwa humo na Kaguta.
Baada ya muda si mrefu, chakula kilikuwa tayari juu ya meza.




Inspekta akishirikiana na mama Miraji waliweka sahani mezani, maji ya kunywa na kunawa pamoja na matunda kadhaa. Chakula kilikuwa wali njegere ukiwa na nyama ndani yake.




Inspekta alimnawisha mikono mama Miraji, mama Miraji naye akafanya vivo hivyo. Wakaanza kula.




“Kwahiyo kwa sasa unajishughulisha nini, mama?”
“Nabangaiza na vibiashara vyangu. Nauza vitenge na madela kwa kupitisha pitisha majumbani.”
“Hongera sana.”
“Kwa lipi?”
“Kutafuta pesa. Familia inakula hapo.”
“Nashukuru Mungu, anajaalia.”
“Mtoto wako anaendeleaje?”
“Marietta anaendelea vizuri. Muda si mrefu sana atarudi toka shule. Alafu nimekumbuka, nimepitia hospitali wakati nakuja huku. Jombi ameanza kuongea japokuwa kwa shida.”
“Kweli?”
“Ndio. Daktari amesema muda si mrefu atarudi katika hali yake ya kawaida. Ila kuna kitu nimegundua, hii hospitali waliyopo sasa wanahudumiwa vizuri kuliko kule.”
“Yap. Ile hospitali ni ghali kuliko ile ya mwanzo.”




Walimaliza kula wakakaa kwa muda kidogo Mama Miraji akaaga anaenda nyumbani kumuwahi mwana. Inspekta alimsindikiza mpaka barabarani akamkodishia mwanamama pikipiki. Walihaidiana kuonana tena kesho hospitalini.




Baada ya masaa kadhaa jua likiwa tayari limeshazama, Kaguta alirudi nyumbani kwa inspekta. Akiwa na tabasamu pana, alimkumbatia mwenzake kwanguvu;
“We jembe! … Jembe haswaa? … Vipi anasemaje?”
“Nani?”
“Aaah … Hujui namuongelea nani banaa? … Si mama Miraji!”
“Tumepiga naye tu story, ameshaondoka. Picha ya mke wangu bado imeng’ang’ania ubongo wangu, Kila nikikaa na mama Miraji namkumbuka mke wangu.” Inspekta alisema kwa sauti ya upole. Kaguta akamshika bega.
“Najua jinsi unavyojisikia. Lakini huwezi ukaishi hivi milele, Vitalis? Inabidi ufungue moyo wako upate angalau faraja.”
“Sijui. Labda huko mbele. Embu kaa kwanza tufanye kazi kuna vtu nimeviona kwenye ile flash.”
“Wee nani akae sasa hivi? … Tutafanya baadae bwana saa hizi nina miadi na mtoto mzuri tunaenda kupata dinner.”
“Duh! … nani tena?”
“Sandra. Anafanya kazi kule Rosemath stationary.”
“Haya dinner njema.”
“Baade kaka.”
“Poa, take care.”




Kaguta alitoka nje akakwea garini na kupotea eneo lile. Ni baada ya dakika kama thelathini tu alikuwa tayari ameshafika eneo la miadi. Haikuchukua muda, mrembo Sandra naye akatokea.




Alikuwa amenoga mno kwa gauni lake refu jeusi la kumeta-meta. Gauni lilimbana vizuri na kumchora umbo lake kuntu namba nane. Lips zake zilitiwa nakshi ya lipstick kwa mbali na sura yenye make-up kwa wastani.



Kaguta alinyanyuka akampa mwanamke kumbato. Alisogeza kiti akamkaribisha malkia. Mhudumu alisogea na menyu, wahusika wakaagiza chakula na vinywaji wavitakavyo.




Wakiwa wanapata chakula, kwa nje ya hoteli. Pikipiki ilijisogeza eneo la kupaki ikiwa na mtu mmoja tu aliyevua kofia yake ngumu nyeusi akaiweka juu ya usukani. Loh! Alikuwa ni Robson. Alinyofoa ufunguo wa pikipiki na kuingia ndani ya hoteli. Moja kwa moja alienda kukaa sehemu aliyokuwa anawachora Kaguta na Sandra kwa mbali.




“You really look very beautiful. Sitosheki kukutazama.” Kaguta alinong’oneza huku akitizama macho ya Sandra.
“Ahsante. Usin’sifie sana n’tashindwa kula mwenzio.” Sandra alisema kwa tabasamu jembamba macho yakielekea chini.
“Kizuri kipe sifa yake, mama. Mimi si wale wasemayo ya moyoni mtu angali maiti.”
“Nashukuru, Al Kareem. Kama jina lako lilivyo, wewe ni mkarimu sana.”
“Kweli?”
“Haswaa!”
“Nafurahi kusikia hayo toka katika kinywa chako kitamu. Natumai yametoka katika moyo wako uliolemewa na upendo.”



Sandra alitabasamu akachoma kipande cha chips na uma akapeleka mdomoni.




“Una maneno wewe, Kareem. Kama vile unanishushia mashairi.”
“Hamna bana, mie na ughani wa mashairi wapi na wapi. Sema tu nasema kile kilichopo moyoni. Heri kufa macho, Sandra, kuliko moyo.”
“Ni kweli.”




Kaguta alikunya fundo moja la mvinyo, akakata kipande cha kuku na kukiweka mdomoni. Alipotafuna na kukimeza, alilonga;
“Una muda gani pale kazini kwako?”
“Miaka miwili na nusu sasa.” Sandra alijibu.
“Upo tayari kuacha kazi yako?”
“Mmmh … Hapana. Hata kama nitakuwa tayari sitaweza.”
“Kwanini? … Wanakulazimisha?”
“Hapana. Ni mkataba wangu tu ndivyo usemavyo.”
“Kwamba hakuna kuacha kazi?”




Sandra alipeleka kwanza glasi yake ya mvinyo mdomoni akanywa mafundo mawili;
“Huwezi kuelewa, Kareem. Tuachane tu na hayo maongezi.”




Kaguta hakuongeza tena neno. Alimaliza mvivyo wake kwenye glasi akawa anamtazama tu Sandra.




“Umekasirika?”
“Hapana. Sidhani kama naweza kupata sababu ya kumkasirikia mrembo kama wewe.” Alisema Kaguta huku akilazimisha tabasamu. Sandra alitabasamu na kutikisa kichwa bila kusema kitu, aliacha mikono na mdomo wake vifanye kazi ya kujaza tumbo kwa chakula na kinywaji. Alipomaliza, alijifuta mdomo wake na tishu akamtazama Kaguta na jicho lililosikia mvinyo.




“Ahsante sana. Umefanya siku yangu ya leo iwe very special.”
“Usihofu, malkia. Wastahili haya.” Alisema Kaguta kwa pambe. Alinyanyua tishu yake akaondoa kajipande ka chakula kalichobakia shavuni mwa Sandra.
“Ahsante.”
“Karibu sana.”




Kaguta alimuita muhudumu akalipia chakula kisha wakanyanyuka yeye na Sandra wakiwa wameshikana mikono wakalifuata gari. Kaguta alimfungulia mwanamke mlango, ndipo na yeye akaingia na kuwasha chombo.




Tofauti kabisa na siku zingine, Kaguta aliendesha kwa mwendo wa kawaida usio na papara. Aliwasha radio yake ya gari na kuchomeka flash iliyokuwa imeketi juu ya dashboard, muziki ukaanza kufanya kazi yake ya kuwakonga nyoyo huku wakipashana habari za hapa na pale. Ni baada ya muda kidogo, Kaguta aligundua kuna pikipiki inawafuatilia nyuma. Aliongeza kidogo mwendokasi akamwambia Sandra;
“Itabidi ukalale kwangu leo.”
“Kwanini?”
“Kwa usalama wako.”
“Usalama wangu? … Kivipi?”
“Tizama hapo kwenye kioo.” Kaguta alionyeshea kioo cha gari kilichojishikiza darini. “Umeona hiyo pikipiki, inatufuatilia.”




Sandra alitzama kwa umakini kiooni. Uso wake ulianza kujenga hofu akawa anatizama tizama nyuma kila muda.




“Usihofu, funga mkanda.”
Upesi, Sandra alifunga mkanda akamtizama Kaguta; “Tayari!”
“Mbona una woga hivyo, unamjua huyo anayetufuata?”
“Ndio. Ni Roby … Robinson!”
“Unamuogopa enh?”
“Si mtu mzuri, Kareem. Kaa naye mbali sana.”
“Kwanini?”
“Huwa hajiulizi mara mbili kumuua mtu. Ni muuaji!”
“Kwanini atufuatilie? … Anataka nini kwetu?”
“Sijui!”
“Hapana, Sandra. Kuna kitu unanificha. Hawezi akatufuatilia hivi hivi. Au unataka kuniua, Sandra?”
“Hapana!”
“Bali?”
“Kusema ukweli nilikuongopea. Mimi na Robinson tuna mahusiano, ni mchumba wangu. Atakuwa amenifuatilia toka nyumbani. Ni mtu mwenye wivu sana, mkali na asiyeelewa.”
“Unakaa naye?”
“Hapana. Ila huwa anakuja kunitembelea mara kwa mara. Si mtu wa kukaa sana, huwa anabanwa sana na kazi.”
“Ulinambia ni mfanyakazi mwenzako, uongo kweli?”
“Kweli. Ni mfanyakazi mwenzangu.”
“Anafanya kazi wapi? … Stationary?”
“Hapana. Tuko kampuni moja tu, ila vitengo tofauti. Yeye husimamia usalama pamoja na usiri wa kampuni.”
“Kampuni yenu inaitwaje?”
“Mikmath Company Limited.”
“Makao yake makuu yapo wapi?”
“Barmuda. Ila kwa hapa Tanzania yapo Posta mpya.”
Kaguta hakuuliza tena swali jingine. Aliacha barabara kuu ya lami akashika ya vumbi.
“Acha nikuonyesha shoo.” Kaguta alimwambia Sandra kwa sura ya tabasamu. Alizima taa za gari na kuburuta matairi kwenye vumbi kwanguvu huku gari likiwa haendi popote. Vumbi lilitapakaa kama wingu kisionekane cha mbele. Robinson alipunguza mwendo akapita kwa uangalifu ndani ya vumbi lile nene.




Alipochomoza upande wa pili, hakuona kitu. Hakukuwa na ishara yoyote ya gari mbele yake wala mbali yake. Alisimama kwa muda kutazama apate jua cha kufanya. Ghafla … Taa za gari zilimmulika usoni! Gari lilichomoza toka kwenye eneo lenye mifungamano ya miti na kuifuata pikipiki kwa haraka na kuigonga tairi la mbele kabla Robinson hajachukua hatua yoyote.





Pikipiki ilirukia kando ya barabara dereva wake akirushwa mbali. Tairi lake la mbele lilipinda na kutengeneza umbo la zigzag. Kaguta alirudisha gari lake nyuma na kuliondoa kwa kasi kufuata barabara ya lami. Ndani ya muda mfupi akawa tayari ameshafika nyumbani kwake. Alishuka akamfungulia Sandra mlango na kuingia ndani.




“Umeinjoy show yangu?” Kaguta alimuuliza Sandra kwa sauti ya kebehi. Sandra alifungua mikono yake akamkumbatia Kaguta na kumbusu.
“Leo umekuwa shujaa wangu.”




Kaguta alipeleka mdomo wake kwenye mdomo wa Sandra wakaanza kunyonyana ndimi. Hawakukomea hapo, mikono yao ilifanya kazi ya kupapasana huku na kule kwa papara. Ni Sandra ndiye aliyekatisha hilo zoezi kwa kusema;
“Twende tukaoge kwanza.”




Hao walielekea chumbani. Kaguta alivua nguo zake kisha akahamia kwa mwanadada, Sandra. Kwa taratibu na kwa madaha, Kaguta alifungua zipu ya gauni la Sandra na kuishusha chini, Sandra akabakia na sidiria na tight nyeupe.





Kaguta aliondoa sidiria akahamia kwenye tight nayo akaishusha chini. Mwanamke akabakia na bikini nyeupe, sasa hapo Kaguta akapata kuona tattoo kubwa pajani mwa Sandra. Tattoo ya mtu kivuli. Tattoo ya mtu mteketezaji. Kaguta alipigwa na butwaa kutazama mchoro huo. Sandra akiwa na macho ya kilevi, aliuliza;
“Vipi, kuna lolote baya?”
“Hapana!” Kaguta aliwahi kusema. “Nilikuwa nashangaa tu hii tattoo.”
“Umeipenda?”
“Inatisha. Sema tu ipo kwenye paja lako, ingekuwa kwenye paja la mwingine ningezirai.” Alitania Kaguta huku akishusha nguo ya mwanadada iliyobakia. Walienda kukoga, walipojilaza kitandani waliacha tamaa za miili yao ziongee, wakatimiziana haja.




****
☆Steve
 
SteveMollel imekuaje tena mzee? Mwaga mzigo.
Nimekuja mzee. Karibu
Katekwa na ispecta vital kwa kurusha siri zake jf
Hahahhaha hatimaye ameniachia!
Siamini kama tumeula wa chuya.
Usijali mkuu. Ratiba tu zabanana.
steve vp.mbona leo umeshusha kiduuchu
Mkuu, nisije shtakiwa nawapatia madawa!
Ahsante sana ndugu steve

Sent from my HTC Desire 820G PLUS dual sim using JamiiForums mobile app
Karibu sana mkuu.
SteveMollel lete vitu nimekomaa mpaka nimefika hapa
Haha hongera sana mkuu kwa kukaza.
Steve mbona unatufanyia hivi
Unavyolalamika we mwanamke...
Dah miaka mingi sijapata soma sinulizi kama hii
Bas ndio hii hapa. Enjoy!
Shati la njanoooo

Naomba muite kwa ile sauti yako ile!

steve bado hujatoka central?
Nimeshapewa dhamana mkuu!
Ongeza mbili mkuu
Ntashtakiwa kukupa madawa
mkuu shusha zingine basi

mpk huruma vip unaendelea steve
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom