SURA YA KWANZA (MSIMU WA 02)
MAUAJI TENA!
Kichwa kimojawapo cha gazeti kilisomeka hivyo. Chini yake kulikuwa na picha tatu ambazo kama hutozitizama vema basi utaishia kusema ni maghofu ya miji ya kale. La hasha! Kumbe ni mabaki ya nyumba ya Mtemvu, ama tumuite marehemu Mtemvu kwa sasa – aliyekuwa afisa polisi kanda maalum Dar es Salaam.
Yeye pamoja na mkewe wote waliaga dunia ndani ya mlipuko mkubwa wa mabomu. Hakuna masalia yoyote ya miili yao
Mtemvu pamoja na mkewe walifariki ndani ya nyumba, pia nyumba yao kuteketea kwasababu ya kukawia kwa zimamoto. Zaidi ya hapo, watuhumiwa wa tukio walikuwa chini ya ulinzi hospitali wakipata matibabu.
Kwa upande wa Miraji hali yake haikuwa tenge kabisa, ni kama vile alikuwa wa kwenda ndani ya muda mchache ujao; risasi ya mgongo iliyotuama kwenye uti wake wa mgongo ilimweka katika hatari ya kupooza mwili. Kichwa kingine cha habari ilikuwa ni juu ya kuachiwa huru kwa bibie Bernadetha Kombo, yeye pamoja na binti yake, Marietta, ambaye alikuwa chini ya uangalizi maalum wa watoto.
Hakukuwa na gazeti, chaneli wala stesheni iliyokwepa habari hizo. Lakini swali kubwa lililotawala ni kwanini Miraji auwa washirika wa karibu wa babaye? Kutafuta majibu ya swali hilo, waandishi wa habari wakawa wanazonga hospitalikwa ajili ya Miraji na nyumbani kwa marehemu mzee Malale wakiwahitaji wahusika wawapatie majibu. Bahati mbaya Mama Miraji, Bernadetha, hakuwa tayari kuongea na waandishi wa habari kuhusu chochote na kwa Miraji bado hakuwa na afya ya kutosha kumfanya afungue kinywa.
Siku moja inspekta Vitalis akiwa ameketi pembeni ya kitanda alicholazwa Jombi, alianza kudadisi kutaka kufahamu nini kinachoendelea nyuma ya pazia la mashambulizi. Aliamuru polisi na manesi wampe faragha, wakafanya hivyo na kumpa mwanya wa kuongea. Baada ya kujiridhisha yupo mwenyewe na mhusika wake, alianzisha soga;
“Uliniahidi kuniambia nini kipo nyuma ya yote haya. Sasa waweza kuniambia?” Alisema inspekta Vitalis katika sauti ya kuuliza. Jombi alishusha pumzi ndefu kisha akang’ata lips zake. Alinyanyua mkono wake usio na pingu akajikunia kichwa na kusema;
“Ndio, naweza.” Alijibu na kuongezea. “Mimi ni mtu tu niliyejitolea kumsaidia Miraji kutimiza adhma yake ya kulipiza kisasi, na si zaidi ya hapo hivyo sikuona kama nastahili adhabu ile ya kifo.”
“Kisasi?” Inspekta Vitalis alijita. “Kisasi kwa kina nani na kwanini?”
“Kisasi kwa wale wote ambao walishiriki kumuua baba yake.” Alijibu Jombi.
“Una uhakika kwamba baba yake aliuwawa?”
“Ndio. Miraji aliambiwa kila kitu na mama yake juu ya kifo cha baba yake.”
“Kwamba?”
“Baba yake aliuwawa na washirika wenzake baada ya dili ya magendo waliyoifanya kubumburuka. Hivyo wakamtoa sadaka kuficha identity na reputation zao mbele ya jamii.”
“Miraji alikuambia kuhusu hilo dili?”
“Kidogo. Aliniambia lilikuwa linahusu kusafirisha pembe za tembo kuelekea Italy, Rome. Na watu walioshiriki ni wale wote ambao tumewaua.”
“Una uhakika na unachokiongea?”
“Absolubtely. Nimekuambia kile chote nikijuacho.”
Inspekta alitulia kwanza kwa muda kama mtu anayefikiria jambo. Kisha akaendelea kuuliza;
“Wewe na Miraji mna mahusiano gani?”
“Ni rafiki yangu tokea zamani sana, tangu tupo kindergarten.” Jombi alijibu kwa kujiamini.
“Na kwa sasa wewe unafanya kazi gani?”
“Nafanya biashara tu.”
“Ipi?”
“Ya kuuza nguo. Nina duka langu la nguo maeneo ya Tandika.”
“Na kuhusu silaha na vifaa, mlikuwa mnavitolea wapi?”
Jombi alinyamaza kwa muda kidogo baada ya hilo swali. Ni kama vile alikuwa anafikiria cha kujibu. alimtazama kwa kumkazia macho, akatazama chini.
“Tulikuwa tunanunua.”
“Pesa mlikuwa mnapata wapi?”
“Tulikuwa tunakwapua pesa toka nyumbani kwa wakina Miraji.”
“Yote hiyo ya kununulia vifaa kama vile?”
Baada ya hilo swali, ghafla Jombi alishika kichwa na kulalama kinamuuma. Hakuweza kuongea tena zaidi alikuwa akilalamika na kugugumia kwa maumivu ya kichwa. Inspekta akampa muda wa kupumzika, ila wakati inspekta ananyanyuka apate kwenda, Jombi alijikakamua kuongea akamuomba simu inspekta kwa madai ya kuwasiliana na kuwajuza nduguze, bila hiyana, inspekta akampatia kisha akasonga pembeni. Jombi aliweka namba akapiga. Sauti yake aliishusha ikawa ya kunong’ona.
“Haloo boss…Jombi hapa…ndio, Jombi kijana wako…nipo Regency hospital kwa sasa, ila nipo chini ya ulinzi…naomba uniokoe boss wangu…kazi nimeshamaliza…Miraji bado, ila atakufa muda si mrefu sana hivyo sio wa kumuhofia kabisa…sawa sawa…ni ghorofa namba mbili, wodi ya tatu…sawa boss wangu…”
Alikata simu haraka baada ya kuona inspekta anakuja akiongozana na polisi. Inspekta aliposogea alitwaa simu yake na kuaga akiahidi kurudi baadae. Huku nyuma, Jombi alibakia akitabasamu na uso wake ulionyesha matumaini.
Usiku ulipoingia, macho ya Jombi yalikuwa yakipepesa pepesa huku na kule huku akipumua kwanguvu. Ni kama vile mtu aliyekuwa anategemea kitu muda si mwingi. Kushoto kwake alikuwa ameketi polisi aliyevalia bunduki, kulia kwake kulikuwa na vitanda vingine kadhaa vikiwa vimebebelea wagonjwa, na kitanda cha tatu toka cha kwake alikuwa amelala Miraji akiwa hana fahamu.
…moja…mbili…tatu…nne…tano…
Miraji alikuwa anahesabu kwa kunong’ona huku akipangua vidole vyake. Ilipofika kumi, mwanaume mrefu mweusi aliyekuwa kavalia nguo za daktari aliingia wodini. Macho yake yalitizama huku na kule kama mtu atafutaye ufunguo kwenye mchanga. Pap! Alikutana macho kwa macho na Jombi. Taratibu akaanza kusogea akimfuata Jombi. Tap! Tap! Tap! Viatu vyake viligonga sakafuni. Alipofika aliwasha tabasamu lake akamsalimia polisi kisha akamsalimia na Jombi.
“Unaendeleaje?” Alimtanabahi mgonjwa.
“Naendelea vizuri tu, dokta.”
“Sawa sawa. Sasa…” Dokta alisema kisha akakatisha ghafla na kumtizama polisi.
“Naomba utupishe kidogo, tuna maongezi ya siri na mgonjwa wangu.”
Polisi bila ya kuuliza akasonga nje ya wodi akasubiria mlangoni. Mwanaume yule aliyevalia kama daktari akamuuliza Jombi,
“Umemwambia yeyote kuhusu boss?”
“Hapana. Hakuna anayejua.” Jombi alijibu.
Mwanaume yule aliyevalia koti la daktari, aliingiza mkono wake kwenye mfuko akatoa sindano iliyobebelea kimiminika cha rangi ya njano. Ghafla, akamziba Jombi mdomo na kumshindilia sindano kwenye mguu wa kulia. Jombii alitapatapa kwa muda kidogo tu kisha akalegea kama mtu asiye na nguvu.
Haraka mwanaume yule akatoka wodini isijulikane wapi alielekea. Polisi aliporudi alimkuta Jombi anamimina povu,macho yamepanda juu huku akitikisa miguu kwa mbali kama mtu akataye roho.
Haraka polisi alitoka mbio akarudi na daktari.
***
Muendelezo soma hapa