Simuelewi mke wangu

Kama vile nakujua jirani pole uwe unaendaga na kusali basi sio muda wote wewe na kazi kazi na wewe
 
Utapata muhuni labda uache pombe umrudie muumba wako
Alikwambia nani Mungu hutafuta kondoo waliozizini mkuu...
Hebu niache huko niendelee kujiwasha matungi aisee..
 
Sawa wewe ambae huna utoto mkuu..ukilinganisha miandiko ya huko Jf na akili za watu utakwenda na maji joo..🤪🤪🤪

Hebu niache nijiinjoy na utoto wangu chief
Tulia Chakorii😀😀😀😀. No hard feelingss...Nilikuwa nakupa tu kauzoefu kutoka kwa legendariiii, kwamba unavyodhani ndivyo sivyo. Siwezi nikakuacha ndugu yangu uamini kwamba suluhisho ni kumuoa rafiki yako halafu ukakuta mambo tofauti, ukapata dissapointment (hapa ndo ndoa zinapata ufa maana tunashindwa kuhimili tukikuta matarajio hayaendani na hali halisi), utabaki unatulaumu wakulungwa kwa kutokukuambia ukweli mapema..😀😀. Ndoa ni compromise ya watu wawili wamekubaliana kuyafumbia macho mapungufu yao madogo madogo. Hakuna mkamilifu dunia hii zaidi ya Mungu pekee. Malezi uliyopata kwenu na malezi aliyopata kwao hata siku moja hayawezi kulingana. Unakuta huyu amezoea tabia ya kutafuna chakula huku mdomo upo wazi, wewe unakuta umefunzwa kwenu kutokufanya hivyo. Lazima utumie busara kumuambia mpenzi wako na usimzodoe, kitu kama hicho kinaonekana ni kidogo lakini ndo kinaweza kuleta mgogoro kwa maana mwenzio anaona wewe kazi yako ni kutafuta tu makosa yake kama wewe upo mkamilifu. Huu ni mfano tu. Mawasiliano yanaanza kuvunjika kwa vitu vidogo vidogo tu, usaliti huwa ni matokeo ya kupishana vitu vidogo vidogo kwa muda mrefu na kutopata wasaa wa kujaribu kuelewana.
 
Fanya uchunguzi mzee lazima unagongewa. Wanawake wakipata mtu anayemfeel anapoteza mapenzi kwa mme wake na uwa ni automatic wenyewe hata hawastuki inatokea naturally. Chunguza simu yake utagundua mengi sana

Pole sana
Sio kweli, suala hapa ni hela

Hii ndo imeleta yote haya
 
Mkuu, lakini mwanamke "anayejitambua" Hadi kufikia hivi ujue Kuna shida ya muda mrefu mumewe aliipuuzia

Wanawake huchukua muda mrefu Hadi kuanza kufanya ujinga huu wa kujipoza kwa kuchepuka
Tatizo wanaume akiambiwa kitu wala hakichukulii kwa umuhimu, unajua kupuuzwa huumiza sana, wanaume hawajuagi tu
 
Muulize kwa utaratibu atasema tu. Labda umepunguza kuleta vijizawadi au kumtoa out.
 
Jaribu kubadili mazingira mtoe hata out safari ya mbali huko msiende hata na mtoto. Mtoto mpeleke kwa bibi. Mchimbe taratibu.

🤔Tunaoshauri maswala ya ndoa hatuko ndoani😀
 
Khaaa nimecheka duh.
 
MPANDISHE CHEO MFANYE MKE MKUBWA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…