The Donchop
JF-Expert Member
- Jan 10, 2014
- 294
- 381
Habarini wadau wa humu?
Nina kama wiki tatu toka tumeachana na boyfriend wangu. Tuliachana kwa mesej zenye maneno makali sana. Yeye akinitolea laana nami nikimkashifu.
Tumekuwa watu wa kugombana kila mara hata baada ya kuachana.
Mwenzangu siku zote alikuwa akipata shida yoyote ndogo basi alikuja kwangu kuniambia na hapo moyo wake uliridhia. Hata kama siwezi kusaidia lolote ye akiniambia tu anaridhika.
Baada ya maugomvi yale muda mrefu sana hatukukaa kuongea lolote. Ilikuwa ni msg ya kejeli inarudi msg ya dharau.
Shemela wenu kunirusha roho akaniambia ye amepata mtu na ana ujauzito wake hivyo nimsahau kabisa katika maisha yangu. Akaapa kwa miungu yote haitotokea akarudi kwangu hata iweje. Wala hana future nami.
Kilichonishangaza baada ya ukimya wa siku kadhaa, jana amenitafuta kwa adabu zote. Ana shida ambayo ni mimi tu ninayeweza kumsaidia.
Nina uhakika hana mpenzi lakini nimemjibu hiyo shida hata mkewe anaweza kumsaidia.
Sijui kama nipo sahihi ndugu zangu. Ni mtu ambaye nilimsaidia kwa mengi sana kipindi ambacho hakuwa na msaada lakini baada ya kupata kazi tu akautumia msaada niliompa kama fimbo ya kunisengenya na kunichapa mwenyewe.
Nimejuta kumsaidia na ingawa namuonea imani bado nina mashaka kuwa baadae atarudi kunitukana kwa msaada nitakaompatia muda huu.
Siku zote mthamini mtu kwa kile kidogo alichokusaidia hata kama leo una kikubwa zaidi ya kile ndugu zangu.
Nina kama wiki tatu toka tumeachana na boyfriend wangu. Tuliachana kwa mesej zenye maneno makali sana. Yeye akinitolea laana nami nikimkashifu.
Tumekuwa watu wa kugombana kila mara hata baada ya kuachana.
Mwenzangu siku zote alikuwa akipata shida yoyote ndogo basi alikuja kwangu kuniambia na hapo moyo wake uliridhia. Hata kama siwezi kusaidia lolote ye akiniambia tu anaridhika.
Baada ya maugomvi yale muda mrefu sana hatukukaa kuongea lolote. Ilikuwa ni msg ya kejeli inarudi msg ya dharau.
Shemela wenu kunirusha roho akaniambia ye amepata mtu na ana ujauzito wake hivyo nimsahau kabisa katika maisha yangu. Akaapa kwa miungu yote haitotokea akarudi kwangu hata iweje. Wala hana future nami.
Kilichonishangaza baada ya ukimya wa siku kadhaa, jana amenitafuta kwa adabu zote. Ana shida ambayo ni mimi tu ninayeweza kumsaidia.
Nina uhakika hana mpenzi lakini nimemjibu hiyo shida hata mkewe anaweza kumsaidia.
Sijui kama nipo sahihi ndugu zangu. Ni mtu ambaye nilimsaidia kwa mengi sana kipindi ambacho hakuwa na msaada lakini baada ya kupata kazi tu akautumia msaada niliompa kama fimbo ya kunisengenya na kunichapa mwenyewe.
Nimejuta kumsaidia na ingawa namuonea imani bado nina mashaka kuwa baadae atarudi kunitukana kwa msaada nitakaompatia muda huu.
Siku zote mthamini mtu kwa kile kidogo alichokusaidia hata kama leo una kikubwa zaidi ya kile ndugu zangu.