Simu ya Rais haina tija

Umenena Bramo: Kwa nini hawamuulizi masuala ya tija ya kitaifa -- kama vile kwa nini Kagoda haipelekwi mahakamani iwapo ushahidi upo kibao kwamba nani alikupua ile mihela? CRDB walitakiwa kueleza walimpa nani hiyo mihela --SIMPO!!

Au kwa nini Chenge hasimamishwi mahakamani kwa tuhuma za kuchukuwa mlungula wa radar na huku wapelelezi wa UK -- SFO wamesha nena, na BAE wenyewe kukubali kosa?

Halafu mwasema eti simu yake ina tija yoyote. MIAFRIKA BWANA!!!!!!

Si kila kitu ni tija kwa kila mtu! pia hizo habari za chenge na wengine ni ngumu kuzijibu kwenye sms! how?
 
[QUOTE=jaxonwaziri;925680]Watu wengine bwana, pengine huwa wanauliza ',....eeeh, mu-hesimiwa laisi, kale ka-thuti ulikokavaa wakati bushi alipokuja ulikanunua bei gani wapi...?' Ama '....eti mu-ishimiwa laisi, mbona katika kale ka mkutano ka Weldi ikonomiki foramu kalikofanyika pale jiji la mlimani ulioneka upo-tense na uncomfortable sana kama vile upo kwenye intavyuuu ya kutafuta ka-ajira ....'
Mimi nadhani simu ni kitu kizuri na itumike vizuri, ila kama hadharani, mfano pale Diamond jubilee alijibu malalamiko ya wafanyakazi kwa kutumia takwimu zisizo sahihi (ikumbukwe hotuba ya rais anayoitoa hadharani itakuwa imefanyiwa kazi kweli kweli kuhakikisha haina mushkeli) na madudu mengine kibao, je hayo majibu ya srini kwa mtu mmoja mmoja kwa kupitia sms yatakuwa na ukweli kweli? Ama ndo ile ya danganya toto kuwa watoto wanauzwa hospitalini katika maboksi??....Mie simo, ni mtazamo tu![/QUOTE]

Hayo ni mawazo yako juu ya sms zetu kwa rais wetu!!!! katu hatujipendekezi kwa mtu ambaye wala hatujui !!!! mimi nawashauri nyie ambao hajawahi kuandikiana mgs nae hebu pata hoja mwandikie halafu utajua nini huwa kinaandikwa kwenye sms kwa rais.
Rais si mjinga angeshasema jamani mkome kuniandikia mambo ya kipuuzi ya kunialika kwenye kipaimara huko majimatitu nataka msg za namna hii tu! katu hajawaji kuzikejeli hadharani msg zetu badala yake amekuwa akisema zinanisaidia endeleeni kuandika nami naamini matatizo ni mengi hawezi kuyatatua yote kwa juma au siku moja

(kwenye pink) yanakuwa na ukweli ndio maana hatuchoki kuandika
Si kila jambo lazima lifanyike kwenye mkutano wa hadhara....huwezi kumwambia rais hadharani kuwa hebu nchunguze msaidizi wako fulani katika hili tunaona anaharibu .....

'Za kuambiwa changanya na za kwako'
 
Si kila kitu ni tija kwa kila mtu! pia hizo habari za chenge na wengine ni ngumu kuzijibu kwenye sms! how?

C'mon Kapwani. nimesema tija kwa taifa. siyo kwa kila mtu! Na kama hawezi kujibu kwa sms, kwa nini katoa namba na kukaribisha watu katika mawasiliano?
 
Mmmmh! Mimi simo huko. Mwambie aingie na Fesibuku ili achati globale teh!teh!teh!. Uhuni mtupu, anakimbia kuongea na waandishi wa habari anakimbilia kujibu sms, Shame on him. Gud for nothing Prezidaa!!!!! I am not supporting the style!!
Hao waandishi wa habari wanashindwa nini kumpigia au kumwandikia sms Mheshimiwa Rais, wakati namba yake wanayo na simu anapokea!?
 
C'mon Kapwani. nimesema tija kwa taifa. siyo kwa kila mtu! Na kama hawezi kujibu kwa sms, kwa nini katoa namba na kukaribisha watu katika mawasiliano?

mambo yote hayawezi kuwa tija kwa taifa kuna yenye tija kwa kijiji changu,kata yangu na tarafa kwa level ya taifa hayajafikia....
nadhani unaelewe fika kwamba lazima uchague topic ambayo inaandikika na kujibika katika ujumbe mfupi....ishu za kina chenge nadhani (mimi) na sio mawazo ya rais ni kama tamthiliya ndefu sana kuanza kutaka majibu yake kwenye sms
Mimi ninakushauri jambo moja namba yake ndiyo hiyo please mwandikie hizo habari ...naamini atakujibu tu
'changanya na za kwako'
 
Rais mwenye majukumu ya kutosha na hasa katika kanchi masikini kama haka ketu kuongea na mtu mmoja mmoja ni kupoteza muda wake na wa hawa wanaowasiliana naye. Hii pia haionyeshi uwajibikaji kwa watu ambao wanapaswa kumsaidia kazi rais. Sikubaliani wala sioni sababu ya yeye kufanya hivyo.
 
Haya - wadau mliojaribu kuwasiliana na Muungwana kupitia simu hiyo twawaomba mtupatie yaliyowafika.
Simu haipo hewani na meseji zote fail.
Nadhani ameona imekuwa kasheshe baada ya sms nyingi kumwomba michango ya harusi na kuzindua viduku kaamua kuifunga kabisa
 
Simu haipo hewani na meseji zote fail.
Nadhani ameona imekuwa kasheshe baada ya sms nyingi kumwomba michango ya harusi na kuzindua viduku kaamua kuifunga kabisa

Tatizo lako mkuu umebip hahahahahahahh
 
hehehe MASA nilituma sms kama tano kumweleza jambo muhimu la kitaifa lakini zote zikaishia kwenye reject box za server. sasa nikaamua kubip nione kama yupo hewani, nikakuta simu haipo kabisa.
Sasa hiyo namba imekuwa kama ile website yake aliyoianzisha kwa mbwembwe kumbe kuuza sura tu
 
hehehe MASA nilituma sms kama tano kumweleza jambo muhimu la kitaifa lakini zote zikaishia kwenye reject box za server. sasa nikaamua kubip nione kama yupo hewani, nikakuta simu haipo kabisa.
Sasa hiyo namba imekuwa kama ile website yake aliyoianzisha kwa mbwembwe kumbe kuuza sura tu

HAhahahahah nimecheka sana mkuu! Umenikumbusha nilienda club, demu mmoja nilimzimia sana! Nikamkaribisha akapata Savanna za kutosha na maraha yote, nikajua siku ya pili msela nitauwa...akanipa contacts....zile simu zake zote huwa hazipatikani hadi leo! na sijawahi mtia machoni tena....! Nikaambiwa demu wa mujini malizana naye siku hiyo hiyo yabaki mahesabu tu!
 
HAhahahahah nimecheka sana mkuu! Umenikumbusha nilienda club, demu mmoja nilimzimia sana! Nikamkaribisha akapata Savanna za kutosha na maraha yote, nikajua siku ya pili msela nitauwa...akanipa contacts....zile simu zake zote huwa hazipatikani hadi leo! na sijawahi mtia machoni tena....! Nikaambiwa demu wa mujini malizana naye siku hiyo hiyo yabaki mahesabu tu!
hehehehe pole ndo maisha.
wanasema ukipata nafasi ya kupiga penati hakikisha unalenga goli na si kona ya goli
 
Mmmmh! Mimi simo huko. Mwambie aingie na Fesibuku ili achati globale teh!teh!teh!. Uhuni mtupu, anakimbia kuongea na waandishi wa habari anakimbilia kujibu sms, Shame on him. Gud for nothing Prezidaa!!!!! I am not supporting the style!!
yupo facebook tena watu wanatuma kero zao
 
Mimi nilizungumza naye wakati wa sakata la vijana waliokwama Ukraine mara kadhaa.. jibu lake lilikuwa "kama Wizara wameshindwa kushughulikia wangeniambia, sikiri kama wameshindwa"..
 
Back
Top Bottom