Simu imewakutanisha....hatimae wameoana!

Maalim Jumar

JF-Expert Member
Dec 28, 2010
1,259
117
Jambo JF!
Kwa wakati wa mwanzo ilionekana simu hasa hizi mob.... kua zinachangia kwenye uhalifu mwingi kwa watu wasio waaminifu.
Sasa jamaa yangu ananieleza kua hiyo siku alipokea sim ya dada asiemfaham...alipomuuliza huyo dada ataje jina lake...hakujibu.
Lakini jamaa nae akawa akimtafuta...hatimae wakawa wakipigiana sim ...wakijuliana hali na kubadilishana mawazo...
Hatimae jamaa amemuoa.
1-Je hili walionaje?
2-Watafika mbali hawa?
Nawakilisha.
 
Wasifike mbali kisa?Hiyo ni kama kukutana na mtu tu kawaida...labda kama hawajatumia muda kufahamiana ndo tatizo!
 
Wanandoa / Wapenzi wote lazima kuwe kuna kitu ki1 kimewakutanisha. Mimi sina wasiwasi na hiyo ndoa itadumu sana ilimradi VIGEZO NA MASHARTI vizingatiwe.
 
mapenzi au ndoa haviathiriwi sana na namna wapendanao walivyokutana, bali namna wanavyoendelea kuwa pamoja.
 
kila mwanandoa ana namna yake alivyokutana na mwenzake na hiyo ni mojawapo. kikubwa ni namna ya kulitunza hilo pendo mpaka mwisho
 
Watu wanakutana mazingira tofauti.
Wanaweza wakadumu/wasidumu.
Hilo swala halijaliishi walikutana vipi.
 
Wanandoa / Wapenzi wote lazima kuwe kuna kitu ki1 kimewakutanisha. Mimi sina wasiwasi na hiyo ndoa itadumu sana ilimradi VIGEZO NA MASHARTI vizingatiwe.
Hiyo hali ni wajibu iwepo!
Lakin ndugu yangu mazingira ndio kitu cha kutazama kwa umakini.
Huwezi kumpata mpz wako mazingira hayana adabu utegemee nae ataadabika!
Hilo walionaje?
 
mapenzi au ndoa haviathiriwi sana na namna wapendanao walivyokutana, bali namna wanavyoendelea kuwa pamoja.

Lakini kuna kitu kinaangaliwa...unapoanza kwa njia hiyo unategemea itakuaje?
Usiangalie kufanikisha lengo lako...maana huo ni mwanzo na haitokua ndio mwisho.
Huoni utaumia baadae?
 
Hiyo hali ni wajibu iwepo!
Lakin ndugu yangu mazingira ndio kitu cha kutazama kwa umakini.
Huwezi kumpata mpz wako mazingira hayana adabu utegemee nae ataadabika!
Hilo walionaje?

Ni mazingira yapi hayana Adabu?
Unataka watu wakutane kwenye futari?
Unataka hadi wakutane kwenye Send off au Harusi?
Sikubalianai na wewe hata nukta, watu wanaweza kukutana Popote na from there nuru ya Upendo ikawa kati yao na wakawa wanandoa mahiri wa kuigwa kwa wanavyopendana na kuheshimiana!
 
Watu wanakutana mazingira tofauti.
Wanaweza wakadumu/wasidumu.
Hilo swala halijaliishi walikutana vipi.
Husninyo!
Hapo ndio tatizo mnaliendeleza...maana wapo wanawake wengi hua hawangalii baadae itakuaje?...
Wao wanataka kuolewa tu. Au wanataka kua na mahusiano tu.
Hilo ni tatizo kubwa kwenye mahusiano.
Kama ndio ww utapenda kwa muda mchache utelekezwe/uachwe?
 
ukichukua karatasi nyeupe..then ukachukua pen halafu ukaweka dot(.) kwenye ile karatasi..baada ya hapo itundike karatas upande wa pili wa ukuta (kuanzia mita 6 na kuendelea) na wewe simama upande wa pili wa ukuta kisha kitazame kile ki-dot ulichokiweka kwenye karatas.....hakika hutakiona vizuri.....jaribu kuwa unaisogolea karatasi taratibu.....hakika kadri unavyoikarinia ile karatas ndivyo unavyoweza kuionaile dot vizuri....ndugu zangu ndoa iko hivyo...mwenzio akiwa mbali na mkawa mnawasilia kwa hizi simu wao wanaita (cyber marriage/relatiship) huwez kujua tabia yake...lakini kama ikitokea mkakaa pamoja kwa mda flani lazima utagundua vitu amabavy tofauti na vile ulivyofikirri wakati yuko mbali.....
kwa hawa kwa kuwa wameona time will tell.....pengine chemistry zao ziko sawa.
lakini kumbuka kitanzi cha ndoa huja taratibu sana mwisho unajikuta umekivaa...wengi wapo wanalia sana na wengine siku hizi wanasingizia kuwa hakuwa/hukuwa chagu langu.....
 
Jambo JF!
Kwa wakati wa mwanzo ilionekana simu hasa hizi mob.... kua zinachangia kwenye uhalifu mwingi kwa watu wasio waaminifu.
Sasa jamaa yangu ananieleza kua hiyo siku alipokea sim ya dada asiemfaham...alipomuuliza huyo dada ataje jina lake...hakujibu.
Lakini jamaa nae akawa akimtafuta...hatimae wakawa wakipigiana sim ...wakijuliana hali na kubadilishana mawazo...
Hatimae jamaa amemuoa.
1-Je hili walionaje?
2-Watafika mbali hawa?
Nawakilisha.

Mapenzi yanaweza kustawi bila kujali namna ya wahusika walivyokutana ali mradi tu kuna mapenzi ya kweli kati ya wahusika hao. Wanaweza kabisa kufika mbali wakiweka bidii kubwa katika penzi/ndoa lao/yao ili kuhakikisha linadumu/inadumu kwa muda mrefu. Nawatakia kila la heri kwenye ndoa yao.
 
Husninyo!
Hapo ndio tatizo mnaliendeleza...maana wapo wanawake wengi hua hawangalii baadae itakuaje?...
Wao wanataka kuolewa tu. Au wanataka kua na mahusiano tu.
Hilo ni tatizo kubwa kwenye mahusiano.
Kama ndio ww utapenda kwa muda mchache utelekezwe/uachwe?
wewe umeongelea kukutana kwao kama kutafanya uhusiano udumu.
Kama kwenye ndoa watapendana na kuheshimiana lazima watadumu bila kujali walikutana kwenye simu, baa, kanisani au vichochoroni.
 
Ni mazingira yapi hayana Adabu?
Unataka watu wakutane kwenye futari?
Unataka hadi wakutane kwenye Send off au Harusi?
Sikubalianai na wewe hata nukta, watu wanaweza kukutana Popote na from there nuru ya Upendo ikawa kati yao na wakawa wanandoa mahiri wa kuigwa kwa wanavyopendana na kuheshimiana!
Nmefundishwa adabu!
Adabu ni kufanya kitu mahala pake.
Hata mtu akiwa mlevi akampata mchumba wake mazingira hayo hapo amefanya adabu...
Ni ajabu sheikh akamtafute mchumba sehemu za mcharuko atarajie atamuenzi hiyo itakua si adabu kwa shaykh huyo.
Futari ...au kula sijajua umekusudia nini?
Labda uende kwa akina mama lishe ndio utafute mchumba...pia itategemea mama lishe yupi umtakae?
Suala nalo hoji hapo...vip hayo mazingira yao yatakuaje?
Kwa wenye tabia za kukusanya ilimrad amepata mwanamke/mwanaume hapo ni sawa.
 
Wasifike mbali kwanini? wapi pameandikwa kuwa kuna sehem maalum ya kukutana na MUPENZI? popote mwaweza kukutana na maisha yakaendelea kama kawa!!!
 
ukichukua karatasi nyeupe..then ukachukua pen halafu ukaweka dot(.) kwenye ile karatasi..baada ya hapo itundike karatas upande wa pili wa ukuta (kuanzia mita 6 na kuendelea) na wewe simama upande wa pili wa ukuta kisha kitazame kile ki-dot ulichokiweka kwenye karatas.....hakika hutakiona vizuri.....jaribu kuwa unaisogolea karatasi taratibu.....hakika kadri unavyoikarinia ile karatas ndivyo unavyoweza kuionaile dot vizuri....ndugu zangu ndoa iko hivyo...mwenzio akiwa mbali na mkawa mnawasilia kwa hizi simu wao wanaita (cyber marriage/relatiship) huwez kujua tabia yake...lakini kama ikitokea mkakaa pamoja kwa mda flani lazima utagundua vitu amabavy tofauti na vile ulivyofikirri wakati yuko mbali.....
kwa hawa kwa kuwa wameona time will tell.....pengine chemistry zao ziko sawa.
lakini kumbuka kitanzi cha ndoa huja taratibu sana mwisho unajikuta umekivaa...wengi wapo wanalia sana na wengine siku hizi wanasingizia kuwa hakuwa/**hukuwa chaguo langu.....**
Nami hukutana nayo majuto hayo hapo kwenye nyota. Sijui chaguo hutokea baada ya kuishi nae au baada ya kuishi nae ?
 
wewe umeongelea kukutana kwao kama kutafanya uhusiano udumu.
Kama kwenye ndoa watapendana na kuheshimiana lazima watadumu bila kujali walikutana kwenye simu, baa, kanisani au vichochoroni.
Mapenzi huanzia wapi?
Maana wengine wanasema siku hizi sikupendi....love parometre ikoje?
 
Wasifike mbali kwanini? wapi pameandikwa kuwa kuna sehem maalum ya kukutana na MUPENZI? popote mwaweza kukutana na maisha yakaendelea kama kawa!!!
Umenichekesha kweli kweli...
Hakuna mwanadam mwenye umakin ataeweza kuamua katenda kitu chake bila kufikiri...inaweza ikawa amepatia...au hakupatia.
Inategemea kanuni gani alioitumia!! Hapo ndipo huanzia maswali....kwanin ilifanyika vile/hivi?
 
Mapenzi yanaweza kustawi bila kujali namna ya wahusika walivyokutana ali mradi tu kuna mapenzi ya kweli kati ya wahusika hao. Wanaweza kabisa kufika mbali wakiweka bidii kubwa katika penzi/ndoa lao/yao ili kuhakikisha linadumu/inadumu kwa muda mrefu. Nawatakia kila la heri kwenye ndoa yao.
Sasa! BAK kuna tatizo limejitokeza kati yao....bibie anazo mali nyingi kuliko jamaa...pia anao watoto wawili....jamaa nae ana mtoto mmoja. Tatizo huja bibie akifanya shopping...wanae wanapata vzur kuliko mtoto wa jamaa. Sasa jamaa inamuuma ila hana maamuzi!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom