Simkubali kabisa Magufuli, lakini apewe heshima yake wakati maono yake yakitekelezwa

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,129
35,152
Kwanza kabisa napenda kuweka kumbukumbu sawa, mimi ni miongoni mwa member wa JF ambaye sikuwahi kumkubali Magufuli na mara zote (mpaka sasa hivi) nimepingana na siasa chafu na siasa za kikatili zilizokuwa zikifanywa na Magufuli na utawala wake, yaani mimi ni against Magufuli. Kwangu mimi rais Samia ni bora zaidi kuliko Magufuli, japokuwa wote wawili hawastahili kutuongoza sisi watanzania.

Kuna mambo kadhaa Magufuli (maono yake au maono ya waliomtangulia lakini yalikuwa yamekufa akayafufua) aliamua kuyaibua, kuyasimamia kwa nguvu kubwa, mengine ya kipuuzi kabisa lakini kwa bahati mbaya akafa kabla ya kukamilika, na aliyemfuata (Rais Samia) amepambana kuyatekeleza na mengine bado anapambana kuyatekeleza huku utawala huu wa Samia ukikwepa sana (kimakusudi) kumtaja au kumwagia sifa Magufuli katikati ya mambo hayo. Hii sio sawa, sio haki na wala sio heshima. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, Magufuli apewe heshima yake katika mema yake. Hapa chini nitataja baadhi ya maono ya Magufuli.
1. Kuhamia Dodoma.
2. Ujenzi wa Ikulu ya Chamwino
3. Ujenzi wa bwawa la umeme la Nyerere
4. Kukuza lugha ya Kiswahili
5. Ujenzi wa reli ya SGR
6. Ujenzi wa daraja/kivuko cha Kigogo Busisi

Nimesukumwa kuandika hapa leo baada ya kusikia kuwa kuna ujenzi utaendelea ndani ya Ikulu mpya ya Chamwino, Dodoma ambapo utahusisha jengo jipya na kubwa la kisasa ambalo litaitwa Samia Complex, binafsi sijafurahishwa na hilo neno. Kwa heshima kubwa ingepaswa hilo jengo liitwe Magufuli Complex kwa sababu kuu mbili kuu.

1. Kulinda heshima ya Magufuli aliyewekeza nguvu na akili zake ili kujengwa hiyo Ikulu, na akajilazimisha kuhamia moja kwa moja hata kabla ya Ikulu kukamilika.

2. Kwa sasa Magufuli ni marehemu, na ndio kipindi bora zaidi cha kutumia jina lake kwa yale yanayomstahili kumpa heshima yake kuliko wakati mhusika akiwa hai kwa kuwa huenda mhusika angebadilika na kuja na sifa nyingine mbaya ambayo ingeharibu taswira nzima ya vitu vilivyoitwa kwa jina lake.

Kama Rais Samia naye anataka au tunataka vitu fulani vya kudumu viitwe kwa jina lake ili kumkumbuka na kumpa heshima yake basi asubiri kwanza siku akitoka madarakani au akitangulia mbele za haki tutampa. Sio haki na busara kujipendelea wakati ukiwa madarakani, hata Magufuli alikosea sana kujipa majina ya vitu vya kudumu wakati akiwa bado madarakani, mfano wa stendi ya mabasi ya mikoani ya Dar pale Mbezi. Pia Magufuli alikosea sana kubeza, kufifisha, kufunika na kushindwa kutambua maono ya mtangulizi wake (Kikwete).

Kile kilikuwa ni kitendo kibaya sana na huenda hichi kinachoendelea sasa ni kisasi dhidi ya Magufuli kwa uovu ule alioufanya dhidi ya Kikwete.

Binafsi ninaona Kikwete alijitahidi zaidi kuutambua mchango wa mtangulizi wake (Mkapa) na pia alijenga msingi mzuri wa mipango endelevu kwa aliyemfuata (Magufuli).
 
Majizi yanaonea gere kazi za Magufuli.

Walitumia muda wao wote wa urais kuzurura angani, kukwapua tembo na kubembea ulaya.

Tunapomzungumzia Magufuli tunazungumzia KAZI, na sio ubabaishaji wa MACHEKIBOBU YA MSOGA yanayojiita majasusi huku yanazurura angani kama MATIARA.

Haya MACHEKIBOBU YA MSOGA yanatamani kufanya yaliyofanywa na Magufuli lakini muda umeshawatupa, wamebaki kujitutumua tutumua na kujikosha kosha kwa vijipropaganda vya kuokoteza na kudonoa donoa.

Wampe sifa anazostahili, ni kazi ya mikono yake!!! Acheni wivu! FANYENI KAZI.
 
Majizi yanaonea gere kazi za Magufuli.

Walitumia muda wao wote wa urais kuzurura angani, kukwapua tembo na kubembea ulaya.

Tunapomzungumzia Magufuli tunazungumiza kazi, na sio ubabaishaji wa MACHEKIBOBU YA MSOGA yanayojiita majasusi huku yanazurura angani.

Haya MACHEKIBOBU YA MSOGA yanatamani kufanya yaliyofanywa na Magufuli lakini muda umeshawatupa. Wampe sifa anazostahili, ni kazi ya mikono yake.

Wivu huo veepeee!!! Fanyeni kazi.
 
Majizi yanaonea gere kazi za Magufuli.

Walitumia muda wao wote wa urais kuzurura angani, kukwapua tembo na kubembea ulaya.

Tunapomzungumzia Magufuli tunazungumzia kazi, na sio ubabaishaji wa MACHEKIBOBU YA MSOGA yanayojiita majasusi huku yanazurura angani.

Haya MACHEKIBOBU YA MSOGA yanatamani kufanya yaliyofanywa na Magufuli lakini muda umeshawatupa. Wampe sifa anazostahili, ni kazi ya mikono yake.

Wivu huo veepeee!!! Fanyeni kazi.
Usitukumbushe habari za mporipori wa Chato, mpoteza watu
 
mpoteza watu
Na hata wewe ungepotezwa ingependeza sana. Nchi lazima iende mbele, ukijitia kigingi utasogezwa.

Ndio maana unamuona yule Kilema anazurura anapiga poyoyo na kutetea mabeberu.

Kwa sasa, Magufuli sio mtu ni FALSAFA. Na nyie majizi machache hamuwezi kushinda, mtasogezwa mmoja baada ya mwingine kiulaini. Na hapo ndipo utakapojua kwamba hii nchi sio kitalu cha MAJIZI na MATAPELI.
 
Kwanza kabisa napenda kuweka kumbukumbu sawa, mimi ni miongoni mwa member wa JF ambaye sikuwahi kumkubali Magufuli na mara zote (mpaka sasa hivi) nimepingana na siasa chafu na siasa za kikatili zilizokuwa zikifanywa na Magufuli na utawala wake, yaani mimi ni against Magufuli. Kwangu mimi rais Samia ni bora zaidi kuliko Magufuli, japokuwa wote wawili hawastahili kutuongoza sisi watanzania.

Kuna mambo kadhaa Magufuli (maono yake au maono ya waliomtangulia lakini yalikuwa yamekufa akayafufua) aliamua kuyaibua, kuyasimamia kwa nguvu kubwa, mengine ya kipuuzi kabisa lakini kwa bahati mbaya akafa kabla ya kukamilika, na aliyemfuata (Rais Samia) amepambana kuyatekeleza na mengine bado anapambana kuyatekeleza huku utawala huu wa Samia ukikwepa sana (kimakusudi) kumtaja au kumwagia sifa Magufuli katikati ya mambo hayo. Hii sio sawa, sio haki na wala sio heshima. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, Magufuli apewe heshima yake katika mema yake. Hapa chini nitataja baadhi ya maono ya Magufuli.
1. Kuhamia Dodoma.
2. Ujenzi wa Ikulu ya Chamwino
3. Ujenzi wa bwawa la umeme la Nyerere
4. Kukuza lugha ya Kiswahili
5. Ujenzi wa reli ya SGR
6. Ujenzi wa daraja/kivuko cha Kigogo Busisi

Nimesukumwa kuandika hapa leo baada ya kusikia kuwa kuna ujenzi utaendelea ndani ya Ikulu mpya ya Chamwino, Dodoma ambapo utahusisha jengo jipya na kubwa la kisasa ambalo litaitwa Samia Complex, binafsi sijafurahishwa na hilo neno. Kwa heshima kubwa ingepaswa hilo jengo liitwe Magufuli Complex kwa sababu kuu mbili kuu.

1. Kulinda heshima ya Magufuli aliyewekeza nguvu na akili zake ili kujengwa hiyo Ikulu, na akajilazimisha kuhamia moja kwa moja hata kabla ya Ikulu kukamilika.

2. Kwa sasa Magufuli ni marehemu, na ndio kipindi bora zaidi cha kutumia jina lake kwa yale yanayomstahili kumpa heshima yake kuliko wakati mhusika akiwa hai kwa kuwa huenda mhusika angebadilika na kuja na sifa nyingine mbaya ambayo ingeharibu taswira nzima ya vitu vilivyoitwa kwa jina lake.

Kama Rais Samia naye anataka au tunataka vitu fulani vya kudumu viitwe kwa jina lake ili kumkumbuka na kumpa heshima yake basi asubiri kwanza siku akitoka madarakani au akitangulia mbele za haki tutampa. Sio haki na busara kujipendelea wakati ukiwa madarakani, hata Magufuli alikosea sana kujipa majina ya vitu vya kudumu wakati akiwa bado madarakani, mfano wa stendi ya mabasi ya mikoani ya Dar pale Mbezi. Pia Magufuli alikosea sana kubeza, kufifisha, kufunika na kushindwa kutambua maono ya mtangulizi wake (Kikwete).

Kile kilikuwa ni kitendo kibaya sana na huenda hichi kinachoendelea sasa ni kisasi dhidi ya Magufuli kwa uovu ule alioufanya dhidi ya Kikwete.

Binafsi ninaona Kikwete alijitahidi zaidi kuutambua mchango wa mtangulizi wake (Mkapa) na pia alijenga msingi mzuri wa mipango endelevu kwa aliyemfuata (Magufuli).
Umeongea vizuri mkuu.
Ninachoona ni mwendrlezo wa alichojianzisha yeye mwenyewe. Alijimilikisha kila ujenzi hata ulioanza wakati wa jk. Ila kweli hilo jengo longeitwa magufuli. Sema haya mambo ya kuita kila.mradi majina ya viongozi nao ni wa kiporipori.
Ila hii nchi ina mpasuko mkubwa na watu wataendelea kufanyiana visasi kwa muda mrefu mpaka ije kurudi kwenye line si leo. Na huenda samia mwenyewe hakusema jengo liitwe samja ila ndio hao watendaji kwa kujipendekeza wakaja na wazo hilo.
All in all yote kheri ila wakumbuke km kadhaa kutoka ikulu hiyo kubwa kweli kweli ilipo kuna watu wanaishi kwenye vijumba vya udongo vifupi kama mashimo ya sungura. Hiini reflection ya maisha ya mtanzania yalivyo magumu
 
Ninapenda ulivyonyoosha maelezo.
Sina ugomvi na Samia lkn nilishtuko alivyotamka Samia complex, haijakaa sawa.
Hata Magufuli stand pia alivyojitamkia Magufuli nayo ilinishtua vile vile.

Majina ya mahali hitolewa kwa heshima kuwa enzi watangulizi, Samia ameanza kujienzi hii sio sawa
 
Binafsi sioni shida kwa raisi Samia kutaka kujimilikisha kazi na jasho la raisi Magufuli kwanza ni Mwanamke na hiyo kwa wanawake siyo ajabu pili walifanya kazi pamoja shida ni Wanaume ambao wanataka kupora kazi alizopiga na jasho alilotoka Mwanaume mwingine na kusema ni zao mfano Bwawa la Nyerere Waziri mwanaume mzima na mwenye familia ya kuongoza anataka kuipora na kusema ni wazo lake na raisi Kikwete sijui ndiye aliyeanza kujenga, I mean Mwanaume mzima hata haya hauna ? Wakati kila mtu anajua wakati Magufuli anaanza kujenga Bwawa la Nyerere mlipinga na kusema linaharibu mazingira leo hii limesimama mnasema ni kazi yenu, kama siyo unusu uanaume ni nini?

Hayo mambo wawaachie Wanawake lkn sijui janaume zima linasimama bila ya haya na kujimilikisha kazi na jasho ya Mwanaume mwingine wakati Dunia nzima inajua kwamba hakuna kitu lilifanya, siyo kabisa yani, …
 
Majizi yanaonea gere kazi za Magufuli.

Walitumia muda wao wote wa urais kuzurura angani, kukwapua tembo na kubembea ulaya.

Tunapomzungumzia Magufuli tunazungumzia KAZI, na sio ubabaishaji wa MACHEKIBOBU YA MSOGA yanayojiita majasusi huku yanazurura angani kama MATIARA.

Haya MACHEKIBOBU YA MSOGA yanatamani kufanya yaliyofanywa na Magufuli lakini muda umeshawatupa, wamebaki kujitutumua tutumua na kujikosha kosha kwa vijipropaganda vya kuokoteza na kudonoa donoa.

Wampe sifa anazostahili, ni kazi ya mikono yake!!! Acheni wivu! FANYENI KAZI.
Mpk leo Machekibobu hao wanaendelea kula bata angani sijui ulaya nk wakati lile shetani lenu la Chato likiendelea kula kibano huko kuzimu
 
Na hata wewe ungepotezwa ingependeza sana. Nchi lazima iende mbele, ukijitia kigingi utasogezwa.

Ndio maana unamuona yule Kilema anazurura anapiga poyoyo na kutetea mabeberu.

Kwa sasa, Magufuli sio mtu ni FALSAFA. Na nyie majizi machache hamuwezi kushinda, mtasogezwa mmoja baada ya mwingine kiulaini. Na hapo ndipo utakapojua kwamba hii nchi sio kitalu cha MAJIZI na MATAPELI.
Asingethubutu, angethubutu kwake kusingebaki hata panya. Siyo kila kichuguu kinafyekwa, vingine mtego!
 
Umeongea vizuri mkuu.
Ninachoona ni mwendrlezo wa alichojianzisha yeye mwenyewe. Alijimilikisha kila ujenzi hata ulioanza wakati wa jk. Ila kweli hilo jengo longeitwa magufuli. Sema haya mambo ya kuita kila.mradi majina ya viongozi nao ni wa kiporipori.
Ila hii nchi ina mpasuko mkubwa na watu wataendelea kufanyiana visasi kwa muda mrefu mpaka ije kurudi kwenye line si leo. Na huenda samia mwenyewe hakusema jengo liitwe samja ila ndio hao watendaji kwa kujipendekeza wakaja na wazo hilo.
All in all yote kheri ila wakumbuke km kadhaa kutoka ikulu hiyo kubwa kweli kweli ilipo kuna watu wanaishi kwenye vijumba vya udongo vifupi kama mashimo ya sungura. Hiini reflection ya maisha ya mtanzania yalivyo magumu

Ujenzi upi wa Kikwete ambao unaitwa Magufuli? Isitoshe mradi pekee ambao una jina la Magufuli ni stendi ya mabasi nijuavyo kama kuna mwingine embu utaje.

Magufuli kwanza ndiye alieanzisha utaratibu wa kuwaenzi Mainjinia na watu wa kawaida waliofanikisha kazi ili iwe kama motisha kwa wengine mfano kwa kuita Daraja la Kijazi au Mfugale flyover, …
 
Ujenzi upi wa Kikwete ambao unaitwa Magufuli?
Soma uelewe hakuna sehemu nimesema ujenzi wa kikwete uliitwa magufuli, bali nimesema kuna projects za kikwete zilikuwa planned au kuanza kwa kikwete ila credits akachukua magufuli. Au umesahau hata barabara zote zilikuwa zinasemwa kajenga magufuli?
 
Back
Top Bottom