Simiyu: Makatibu Kata Mkoa wa Simiyu Wakabidhiwa Vitabu vya Kanuni za CCM

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,897
942
Simiyu: Makatibu Kata Mkoa wa Simiyu Wakabidhiwa Vitabu vya Kanuni za CCM

MJUMBE wa Mkutano Mkuu Taifa (MNEC), kutoka Mkoa wa Simiyu, Gungu Silanga amekabidhi vitabu vya kanuni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa Makatibu Kata wa mkoa huo ili waendelee kusimamia Utekelezaji wa Ilani ya chama hicho na kusimamia maadili ya Chama.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu Shemsa Mohamed alisema Chama Cha Mapinduzi kimefanya mambo makubwa katika nchi hii ikiwemo kuimarisha upatikanaji wa huduma kijamii.

Aliwataka wanaCCM kuendelea kuunga mkono juhudi za Dk. Samia Suluhu Hassan huku akiwata Mabalozi kuhakikisha wanapita nyumba kwa nyumba ili CCM ishinde katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025.

Kwenye Maadhimisho hayo CCM ilipokea wanachama wapya 50 waliopatiwa kadi za CCM pamoja na vijana wengine 50 waliopatiwa kadi za Umoja wa Vijana (UVCCM).

Aidha, Katika Maadhimisho hayo, Mwenyekiti Shemsa alichangia mifuko 50 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya CCM kata ya Nyaruhande, pia aliendesha harambee ambayo alifanikiwa kupata jumla ya mifuko 75 ya saruji na fedha kiasi cha shilingi 850,00/=.

MWISHO

DSC_4281.JPG
DSC_4349.JPG
DSC_4344.JPG
DSC_4315.JPG
DSC_4313.JPG
DSC_4247.JPG
DSC_4292mnjhu.JPG
DSC_4304kiop.JPG
DSC_4240xzsaq.JPG
 
Back
Top Bottom