Simbachawene: Mpango wa gesi utatekelezwa

Simbachawene: Mpango wa gesi utatekelezwa

only83

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2010
Posts
5,342
Reaction score
2,528
Katika hali ya kusikitisha naibu waziri George Simbachawene anaendelea na porojo zile zile za waziri wake na serikali yake kuhusu gesi ya Mtwara.

Leo kaibuka anasema kuwa wananchi wa Mtwara watapata majibu ya hoja zao kama wataruhusu bomba ya gesi lijengwe. Anasema kuwa wanaowavuruga wana Mtwara wengi ni watu wasio na mahusiano yoyote na mkoa wa Mtwara kwa maana ya kuwa si wakazi wa Mtwara.

Nadhani hizi ni dharau kwa wana Mtwara na watanzania, maafa yale yote yaliyotokea bado hii serikali dhaifu haioni aja ya kuwasikiliza wana Mtwara.

UPDATE:
Naibu wa Wizara ya Nishati na Madini, George Simbachawene, amesema serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) itakuwa tayari kuhukumiwa na wananchi wa Mtwara katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kama mikakati iliyopangwa na serikali katika kutekeleza mradi wa gesi itakuwa ni ya kuwadanganya.

Alisema hayo juzi wakati akizungumza katika mahojiano kwenye kipindi cha dakika 45 kinachorushwa na kituo cha televisheni cha ITV kila Jumatatu.

Simbachawene aliseama serikali ya CCM ni makini na inatambua kuwa msingi wa utawala ni watu, hivyo haiwezi kudhalau watu wa Mtwara na Lindi hata kama ni wachache kiasi gani, kinachotakiwa wawe tayari kuelewa, lakini wakiwa hawapo tayari kuelewa wanaipa tabu sana serikali katika utekelezaji wa mradi huu.

Alisema Serikali ya CCM ilishinda uchaguzi kihalaki, haikushinda kidikiteta, kwa hiyo iachwe ifanye kazi na ihukumiwe inaposhindwa kufanya mambo iliyoahidi, wananchi wa Mtwara kama wanasema haya tunayoyaeleza tunawadanganya watusubiri 2015 watuhukumu lakini sisi tunarudia kusema watuelewe waache tutekeleze mradi huu.

"Sisi kama serikali tunao askari, tunalo Jeshi tunaweza kutekeleza kwa nguvu, lakini hatutaki kufika huko, tunaamini tutaelewana, tunaamini katika suluhu,tunaamini huu upotoshaji uliopelekwa kwa wananchi wa Mtwara utakwisha," alisema Simbachawene.


CHANZO: NIPASHE
 
Hivi mnataka gesi isafirishwe kwa malori?
Hakuna kitu kama hicho duniani, gesi inasafirishwa kwa bomba, sasa wasiotataka gesi ije dar wanataka ipelekwe wapi? Waziri anasema viwanda vyote vya kutengeneza gas vitakuwa mtwara sasa mnatakaje?
 
Uhuru ulipatikana Daslam au Tanganyika?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
huyu waziri bado anaendelea kutufanya wajinga wana mtwara.
enyi ndugu zangu wana mtwara na watetea haki wote tuwe imara katika hili tusisikilize uchafu huu anaoongea simba chawene
 
Watu wakiwaita dhaifu wanamind...je amesema kuna ulazima gani wa gas kwenda huko dar labda!!??
 
Machungu na unyanyasaji ndiyo unafanya wana MT kuwa na hasira na serikali ya JK. Huwezi nyanyasa mnyonge kila siku kwani iko siku atakutoa ngebe tu.
 
huyu waziri bado anaendelea kutufanya wajinga wana mtwara.
enyi ndugu zangu wana mtwara na watetea haki wote tuwe imara katika hili tusisikilize uchafu huu anaoongea simba chawene

uchafuuu????ni bora mkausikiliza huo uchafu sasa msije mkachelewa mkaja kuutafuta mkaukosa kabisa.hii tz mkuu muda si mrefu mtaanza kugawanyika hasa baada ya wengine kugundua kuwa ngd zao wanapoteza maisha au wako ndani na hakuna support yoyote wanayopata kutoka kwa hao surppoters wenu!!!
 
wanamtwara hawajakataa gesi kwenda mtwara wanachotaka ni kujua watanufaikavipi.
kwa hili waziri aache porojo,wana mtwara wanaakili wanajua usanii wa serikali,haya yanafanyika kigamboni yamefanyika kwenye reli kupitia rites ya india yamefanyika kwenye madini.

kauli za rais,muhongo,simbakalia na sasa simbachjawene hazileti matumaini kwa wana mtwara.
 
Watu wakiwaita dhaifu wanamind...je amesema kuna ulazima gani wa gas kwenda huko dar labda!!??

kwa sababu kuna soko kubwa la gesi na haiji kugawiwa bure!!!so tuambieni mnataka malori yatumike kuileta dar badala ya bomba?
 
Kwani hiyo gesi ikija huku Dar mtaacha itumia nyie wana Mtwara?
Naamini hiyo gesi itafika Dar na wasumbufu watafungwa
 
kwa sababu kuna soko kubwa la gesi na haiji kugawiwa bure!!!so tuambieni mnataka malori yatumike kuileta dar badala ya bomba?

hiyo gesi ije dar kufanya nini we mburula? hicho inachokwenda kufanya dsm kifanyike lindi au mtwara kwanza, dms kitu gani we bata.
 
kwa sababu kuna soko kubwa la gesi na haiji kugawiwa bure!!!so tuambieni mnataka malori yatumike kuileta dar badala ya bomba?
Acha akili za zidumu fikra za mwenyekiti,zishapitwa na wakati na wanamtwara wameshaamka,gesi iende bagamoyo ili iweje?
 
Amemchana prof lipumba eti anadanganya watu wa mtwara kwamba wanatakiwa kupewa hela kwa kutumia namba zao za cm
 
kwa sababu kuna soko kubwa la gesi na haiji kugawiwa bure!!!so tuambieni mnataka malori yatumike kuileta dar badala ya bomba?

Hayo masoko mbaki nayo huko dar,viwanda vyote vijengwe mtwara na lindi then tutwaletea gas iliyo tayari kwa consuption mtumie huko dar kwenu mbumbumbu wew..kwani watanzania wengine hawatumii gas ni dar tu...
 
hiyo gesi ije dar kufanya nini we mburula? hicho inachokwenda kufanya dsm kifanyike lindi au mtwara kwanza, dms kitu gani we bata.

akili zako ndo zimeishia hapo!???poleeee mwanego!!!!hujui kuwa hiyo ni product ambayo inatakiwa wawekezaji wauze???tatizo lenu wengi hamjitambui na hata mnachokitaka hamkijui ndo maana wengine wanashindwa kuwasapoti!!!haya ibaki mtwara alafu iweje???
 
Hayo masoko mbaki nayo huko dar,viwanda vyote vijengwe mtwara na lindi then tutwaletea gas iliyo tayari kwa consuption mtumie huko dar kwenu mbumbumbu wew..kwani watanzania wengine hawatumii gas ni dar tu...

si ajabu coz hujitambui.tusubiri na wanasumbawanga nao waje na madai hatutaki mtoe mahindi yetu mtwara njooni mjenge viwanda vya kusaga unga huku huku ndo muuze unga!!!hebu kama wewe zimo kweli nitajie matumizi matano ya hiyo gesi unayoipigania
 
Acha akili za zidumu fikra za mwenyekiti,zishapitwa na wakati na wanamtwara wameshaamka,gesi iende bagamoyo ili iweje?

hata ikienda bagamoyo unadhani itaenda kugawiwa bure???swali la msingi,mtafaidikaje????huo upuuzi haitoki haitoki wanasema mapoyoyo kama wewe.
 
Katika hali ya kusikitisha naibu waziri George Simbachawene anaendelea na porojo zile zile za waziri wake na serikali yake kuhusu gesi ya Mtwara. Leo kaibuka anasema kuwa wananchi wa Mtwara watapata majibu ya hoja zao kama wataruhusu bomba ya gesi lijengwe. Anasema kuwa wanaowavuruga wana Mtwara wengi ni watu wasio na mahusiano yoyote na mkoa wa Mtwara kwa maana ya kuwa si wakazi wa Mtwara. Nadhani hizi ni dharau kwa wana Mtwara na watanzania, maafa yale yote yaliyotokea bado hii serikali dhaifu haioni aja ya kuwasikiliza wana Mtwara.

Semunye na Simbachawene wote ni wapuuzi....kamanda only83 ulipotelea wapi?
 
Ooh huyu waziri hajui watanzania wa leo,kwanza kwa nini anaongelea kwenye luninga?si aende akaongelee Mtwara!!!Badala ya kutoa mchanganuo analeta porojo na dharau kwa wana mtwara kupata kazi za vibarua na mama ntilie.Oooh!shame on U Simba fisadi.Hebu tuambie mgao wako ni ngapi au unaimba mziki usioujua???
 
Hivi mnataka gesi isafirishwe kwa malori?
Hakuna kitu kama hicho duniani, gesi inasafirishwa kwa bomba, sasa wasiotataka gesi ije dar wanataka ipelekwe wapi? Waziri anasema viwanda vyote vya kutengeneza gas vitakuwa mtwara sasa mnatakaje?

Wajenge kwanza hivyo viwanda ndipo wamalizie na bomba,
ajue yeye pamoja na baraza la mawaziri hawana veto kwa maliasili yetu ambayo ibara ya 9 ya katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania imetupa haki na wajibu wa kuilinda.
WAACHE UJINGA KUNGALI UJANJA UNAPATIKANA, WASISUBIRI MTUNGI WA MAJI UVUNJIKE NA MAJI KUREJEA KISIMANI (mwenye masikio na asikie)
 
Back
Top Bottom