Amani iwe nanyi wapendwa katika bwana
Ilikuwa ni siku ya Jumapili asubuhi saa nne kama na nusu vile. Bibi yangu aliniita Kafuku njoo hapa upesi nilienda upesi kumusikiliza bibi anataka nini.
Baada ya kufika alinikalisha kitandani na kuanza kunambia anataka anitume mbali sana lakini niwahi kurudi kufikia saa moja jioni niwe nisharudi.
Nilimuuliza ni wapi huko bibi si unajua mimi huwa naendesha baisikeli kama kichaa. Akanambia hapana ni mbali sana kwa baskeli huwezi fika, nikamuuliza ni wapi sasa akanambia ni Tanga. Nikashituka kidogo nikamwambia sasa mbali kote huko nitawezaje kurudi leo leo, akasema nitakupa usafiri wa ajabu ambao ni wa haraka kufika.
Nikamuuliza usafiri gani huo akasema nakupa fisi mjukuu wangu lakini iwe siri yako usimwambie mtu. Nilikubali maana sikupenda kumubishia bibi yangu.
Alinielekeza sehemu ya kuongeza speed na kupunguza speed. Sikio la kushoto ni la kuongeza speed halafu la kulia ni la kupunguza speed.
Muda ulifika saa tano na nusu nikaanza safari kutoka Simiyu kwenda Tanga. Nilimpanda yule fisi na bibi alinipaka dawa watu wasinijue wala kuniona.
Safari ikaanza nilikuwa namkimbiza yule fisi kama sina akili aisee niliwahi sana kufika Tanga yaani saa saba nilikuwa nishafika zamani sana na kupewa ule mzigo niliokuwa nimeagizwa nikageuka, aisee ule muda wa kurudi kidogo tu nipate ajali maeneo ya Kondoa nikiwa narudi.
Lakini ile ajali niliweza kusevu na kusepa zangu nilifika Simiyu saa kumi na moja. Nilikabidhi mzigo wa bibi kama kawaida.
ZAMANI PALIKUWA PANAITWA SHINYANGA KWA SASA SIMIYU
This is true story
LONDON BQBY