Uwanja wa Taifa: Simba SC 4-0 Gendarmarie Nationale FC, Kombe la Shirikisho Barani Afrika

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
486c651c125b4e2ea68f3c43812dcfb4.jpg
Klabu ya Simba Sports Club leo Jumapili inajitupa katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, kuanza harakati za kupambana kimataifa kwa kucheza na klabu ya Gendarmarie Nationale FC, ya nchini Djibout kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya awali ya michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika.

Simba SC, Mnyama wanarejea michuano ya kimataifa huku wakiwa na matokeo mazuri kwenye Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara VPL, hali inayoaminiwa na mashabiki na wanachama wao kuwa huenda furaha ikawa chachu ya wachezaji wao kuendeleza furaha.

Utashuhudia pambano hili Live kupitia Azam Sports 2 kuanzia saa 10: jioni. Kaa nasi kukuletea yatakayojiri, usikose ukaambiwa

Vikosi vya timu zote vitakavyotoshana nguvu kwa upande wa Simba SC;

Aishi Manula, Shomari Kapombe, Asante Kwasi, James Kotei, Yusuf Mlipili, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Shiza Kichuya, Said Ndemla, John Bocco, Emmanuel Okwi.

Sub; Emmanuel Mseja, Mzamir Yassin, Mwinyi Kazimoto, Moses Kitundu, Paul Bukaba, Ally Shomari, Juuko Murshid.

Coaches; Pierre Lechantre - Head Coach
Masoud Djuma - Assistant Coach Mohamed Aymen - Fitness Coach Muharam Mohamed - Gk Coach

Timu tayari ipo uwanjani kwa mtanange huu. Na Rais Mstaafu Ndugu Ali Hassan Mwinyi ambaye ni mgeni rasmi kwenye mchezo huu tayari anakagua timu zote mbili.
623d2f792360ba5b461c9ec04ec1bf20.jpg


Wakati wowote mpira utaanza hapa uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Naam mpira umekwisha ananza uwanja wa Taifa


00' Simba SC 0-0 Gendarmarie Nationale FC.

02 ' Goooooooooaal Said Ndemla amepiga faulo na kutinga wavuni moja kwa moja

Simba SC 1-0 Gendarmarie FC


15' uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam

Simba SC 1-0 Gendarmarie Nationale FC

30' uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam

Simba SC 1-0 Gendarmarie FC

32 ' Goooooooooaal John Bocco anaandika bao la pili kwa kichwa kazi mzuri kutoka upande wa kushoto.

Simba SC 2-0 Gendarmarie Nationale FC

45' Goooooooooaal goooooooooaal goooooooooaal John Bocco anaandika bao la tatu upande wa Simba SC

97775bc5bdcc640c3a88eef4ee1cc6d0.jpg
45' Naam mpira ni mapumziko hapa uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Simba SC wanakwenda wakiwa mbele ya magoli tatu bila majibu dhidi ya Gendarmarie Nationale FC
5695a04c83757e113ce41a90f93db36b.jpg


Naam mpira umeanza kipindi cha pili uwanja wa Taifa.

50' Gendarmarie FC wanapata penati. Inapigwa Penaltiiiiiiiii lakini golikipa Aishi Manula anapangua mkwaju huo na kuwa konaa.

Konaaaaa inapigwaaaa la la la nje!

65' Simba SC 3-0 Gendarmarie Nationale FC

70' Jezi namba 5 wa Gendarmarie FC anapewa kadi ya njano kwa kuchezea vibaya Kichuyaa

72 ' Kichuyaa anakwenda kwenye benchi na nafasi yake anachukua Mzamir Yassin

75' Said Ndemla anakwenda benchi na nafasi yake anachukua Mwinyi Kazimoto

85' Simba SC 3-0 Gendarmarie Nationale FC

90+3 ' Okwiiiii Okwiiiii Goooooooooaal. Emmanuel Okwi anaandika bao la nne kwa shuti kali la adhabu.
0a4548354eb9f8467e27ab41b99c6541.jpg


Simba SC 4-0 Gendarmarie Nationale FC

Wakati wowote mpira utakuwa umekwisha hapa uwanja wa Taifa.

Naam mpira umekwisha ambapo Simba SC imeibuka na ushindi wa magoli manne bila majibu dhidi ya Gendarmarie Nationale FC
8d9f7058bf2bbe9763e7c1a6859381b0.jpg
 
Hivi hizi jezi za blue zinauzwa wapi maana haina jinsi lazima tukamchinje mmnyama
 
Yah hapo unapiga kauzi ka chelsea na vinywele unaweka wave unatafuta na vikuber kidogo unakuwa waria kabisa au hawajamaa hawafanani na msomali
 
486c651c125b4e2ea68f3c43812dcfb4.jpg
Klabu ya Simba Sports Club leo Jumapili inajitupa katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, kuanza harakati za kupambana kimataifa kwa kucheza na klabu ya Gendarmarie Nationale FC, ya nchini Djibout kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya awali ya michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika.

Simba SC, Mnyama wanarejea michuano ya kimataifa huku wakiwa na matokeo mazuri kwenye Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara VPL, hali inayoaminiwa na mashabiki na wanachama wao kuwa huenda furaha ikawa chachu ya wachezaji wao kuendeleza furaha.

Utashuhudia pambano hili Live kupitia Azam Sports 2 kuanzia saa 10: jioni. Kaa nasi kukuletea yatakayojiri, usikose ukaambiwa

Vikosi vya timu zote zimetoshana nguvu kwa upande wa Simba SC;

Aishi Manula, Shomari Kapombe, Asante Kwasi, James Kotei, Yusuf Mlipili, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Shiza Kichuya, Said Ndemla, John Bocco, Emmanuel Okwi.

Sub; Emmanuel Mseja, Mzamir Yassin, Mwinyi Kazimoto, Moses Kitundu, Paul Bukaba, Ally Shomari, Juuko Murshid.

Coaches; Pierre Lechantre - Head Coach
Masoud Djuma - Assistant Coach Mohamed Aymen - Fitness Coach Muharam Mohamed - Gk Coach
Pamoja mkuu, Leo ni leo' asiye na mwana akabebe jiwe.
 
Nakubali sana kazi zako mkuu, nafatilia nyuzi hii mpaka asubuhi.
Simba 5 - Gendarmerie 0
Tukutake saa 10:00 jioni
Asante mkuu.. Tupo pamoja katika kujuzana yale tunayoyaweza.. This is Simba
 
Rais Mstaafu Awamu ya ya Pili Ndugu Ali Hassan Mwinyi ambaye ni mgeni rasmi kwenye mchezo huu tayari anakagua timu zote mbili
 
Back
Top Bottom