Tisha-TOTO
JF-Expert Member
- Feb 10, 2010
- 1,175
- 604
Simba wameanza kuchoka yanga wameanza kuonana.
Nadhani matokeo ya mwisho yatakuwa kama "Dk" Uwesu alivyotabiri...embu checki hapa chini...
Dakika chache zilizopita nilikuwa nasikiliza Capital Radio walikuwa na Simba v Yanga match preview programme. Mmoja wa wachangiaji waalikwa alikuwepo "Dk" Uwesu ("mtaalamu" wa tiba asilia na mtabiri wa nyota).
Nanukuu hapa chini alichokisema "Dk" Uwesu...
"Utabiri wa mechi ya Simba na Yanga ni mgumu sana. Lakini hadi dakika hii inaonyesha Simba 2 na Yanga 1. Hata hivyo, kwa kawaida Jumatano huwa ni siku ambayo hutawaliwa na rangi ya njano. Hii maana yake nini? Tafsiri yake ni kwamba Simba watatawala sana mwanzoni mwa mchezo lakini Yanga nao watatawala sana mwishoni mwa mchezo na hivyo kinyota matokeo ya mchezo yatageuka kuwa Simba 1 Yanga 2"