Ball possesion haiwezi kuwa hiyo mkuu waambie hao Kiss FM wataje ya ukweli, hao marefa utawasingizia tu kwamba waliibeba Simba, sehemu moja tu ambayo refa alitubeba nayo ni kutompa red Haruna hata jukwaani tulipokuwa tumekaa tuliona hilo na tukasema hapo refa katubeba, lakini ile njano aliyopewa Edward, Cannavaro alisukuma na ingekuwa penati, Cannavaro kamchezea rafu nyingi sana Sunzu mara zote wakati wanawania mpira alikuwa anamsukuma na mwisho refa alikosa uvumilivu akampa red, Mwasika naye alimuchezea rafu Kazimoto lakini mbali na kutopewa kadi hata faulo tu haikupigwa, siwezi kumlaumu refa labda alikuwa mbali na matukio au makosa ya kibinadamu tu lakini huwezi kusema kwamba aliibeba Simba. Wale wasaidizi kama ulikuwa makini kuangalia utaona Bahanuzi alikuwa anabaki peke yake akisubiri kupitishiwa kwa nini asiwe offside na ulitaka mwamuzi msaidizi amwache.
kuhusu kutawala kama dakika 10 za mwisho ilichangiwa na kutoka kwa Mkude na kuingia na kuingia Haruna Moshi, kiungo kilipoteana na baada ya rafu mbaya ambayo Haruna aliifanya nayo mchezoni, kama binadamu isingekuwa rahisi afanye ile faulo halafu aendelee kucheza vizuri hata ukiangalia picha vizuri amekita ule mkuu lakini usoni anaonekana kuumia kama vile yeye ndo alikanyagwa kwa hiyo hata yeye hakuifurahia hiyo faulo ilimtoa mchezoni kiukweli.
Mi naona wewe ndio unaongea kishabiki zaidi........Kimahaba zaidi......
Ball possession ni Yanga 52% na Simba 48% yet unasema Yanga walikuwa wanacheza physical zaidi.....Mabeki wa Simba walikuwa wanacheza offside trick ndio maana washambuliaji wa Yanga wameotea zaidi ya mara 10......Ona sasa unaaza na hadithi za 'angekuwepo Okwi angeisumbua beki ya Yanga'......Football ni nothing but a game of chance, ndio maana unaona hata baada ya Simon Msuva kutolewa kwa kadi nyekundu Yanga waliendelea kuwashambulia Simba, hii ni kwa sababu walikuwa wakitengeneza chance nyingi hasa eneo la kiungo ambalo liliimarika baada ya Frank Domayo kuingia....Simbaa mpira wamecheza dakika 30 za mwanzo baada ya hapo game ilibalance na dakika 10 za mwisho wa kipindi cha kwanza Yanga waliutawala mchezo.....Hata baada ya Kavumbangu kuingia Yanga waliendelea kuutawala mchezo kwa kutengeneza nafasi za kushambulia ambazo zilikuwa zikiishia kuwa offside kutokana na mbinu iliyotumiwa na beki ya Simba.....
All in all mchezo wa leo ulikuwa mzuri, timu zote mbili zimecheza vizuri na Yanga nawasifu zaidi kwani hata baada ya Simon Msuva kutolewa kwa kadi nyekundu hawakutetereka kwa kulinda goli/kufunga tela badala yake waliendelea kushambulia..............
Nini Tanzania, Buhanuzi ni the best striker in East Afrika.....The Top scorer in 2012 CECAFA Kagame Cup