Dan Zwangendaba
JF-Expert Member
- Apr 25, 2014
- 5,507
- 7,511
Bila shaka, kijana mdogo Mohamed Mussa ni hazina. Mchezaji huyo aliyesajiliwa na Simba katika dirisha dogo kutoka Malindi ya Zanzibar alikuwa kwenye kiwango bora sana katika Ligi ya Zanzibar na mashindano ya Mapinduzi. Binafsi huwezi kunishawishi kuwa Kibu Dennis ni bora kuliko Mohammed Mussa.
Kitendo cha Simba kutompa nafasi takribani mechi zote za Ligi hadi sasa ni kuandaa mipango ya kuua kipaji cha kijana huyu. Nashauri mtumieni kijana huyu atakuja kuwa msaada mkubwa tofauti na mnavyomfanyia Sasa.
Jifunzeni kwa Yanga ambapo wachezaji karibu wote hupewa fursa ya kuonesha kipaji chao.
Kitendo cha Simba kutompa nafasi takribani mechi zote za Ligi hadi sasa ni kuandaa mipango ya kuua kipaji cha kijana huyu. Nashauri mtumieni kijana huyu atakuja kuwa msaada mkubwa tofauti na mnavyomfanyia Sasa.
Jifunzeni kwa Yanga ambapo wachezaji karibu wote hupewa fursa ya kuonesha kipaji chao.