Mtoboasiri
JF-Expert Member
- Aug 6, 2009
- 5,101
- 1,948
Mtu mmoja alikuwa anasafiri peke yake kwa miguu na njia pekee ya kumfikisha aendako ilihusisha kupitia kwenye pori. Akiwa katikati ya pori alikutana na simba, akapanda juu ya mti pekee uliokuwa karibu japo ulikuwa si mrefu sana. Jamaa akamuomba Mungu ili amfanye yule simba awe mkristo. Mara jamaa akamsikia simba akisali: Nibarikie Mungu wangu mimi na chakula changu ulichonipa nipate nguvu za kukutumikia vema, amen".