Mtanzanias
JF-Expert Member
- Jul 30, 2021
- 1,747
- 3,719
Nilikuwa nasubilia kwa hamu Sana nione timu inayosemwa iko vizuri msimu huu maana yanga ilipofungwa na zanaco kuna wajinga fulani fulani humu waliibuka na kuanza kutoa kila aina ya kejeli na maneno ya udaku, sasa tumewaona live hakika mtamkumbuka chama na mikson, mapengo yao yameonekana dhahiri shairi.
Mnabaki kumtegemea Morrison akibanwa ndo ivyo kwaheri mwalimu, tunaangalia vitu kiufundi zaidi Kama tp mazembe wangekuwa makini leo kwenye safu ya ushambuliaji wangeondoka na goli 4, shukrani kwa manura, amekuwa bora Leo vinginevyo mngepata aibu ya mwaka.
Hatutaki porojo za kusema eti kocha alikuwa anaangalia kikosi kwakuwa hoja hiyo ilikataliwa kwa yanga ivyo basi mnayo kazi ya ziada na nyie kuitengeneza timu la sivyo mkishupaza shingo na kujiona bado mnao ubora ule ule mtakipata cha moto.
Kwanza nendeni kwenye takwimu za mechi za kirafiki karibu zote safu yenu ya ulinzi imeruusu magoli ata mlizoshinda pia magoli mliruusu sasa iyo ni alarm inatakiwa mshtuke vinginevyo tutakuja na utetezi mwingine apa siku sio nyingi.
Mnawacheka yanga lakini na nyie ugonjwa ni ule ule
Mnabaki kumtegemea Morrison akibanwa ndo ivyo kwaheri mwalimu, tunaangalia vitu kiufundi zaidi Kama tp mazembe wangekuwa makini leo kwenye safu ya ushambuliaji wangeondoka na goli 4, shukrani kwa manura, amekuwa bora Leo vinginevyo mngepata aibu ya mwaka.
Hatutaki porojo za kusema eti kocha alikuwa anaangalia kikosi kwakuwa hoja hiyo ilikataliwa kwa yanga ivyo basi mnayo kazi ya ziada na nyie kuitengeneza timu la sivyo mkishupaza shingo na kujiona bado mnao ubora ule ule mtakipata cha moto.
Kwanza nendeni kwenye takwimu za mechi za kirafiki karibu zote safu yenu ya ulinzi imeruusu magoli ata mlizoshinda pia magoli mliruusu sasa iyo ni alarm inatakiwa mshtuke vinginevyo tutakuja na utetezi mwingine apa siku sio nyingi.
Mnawacheka yanga lakini na nyie ugonjwa ni ule ule