Ni kweli yaani Mimi Nina miezi mitano sina kazi na ninaishi na mdogo wangu wa kike, Mke wangu na mtoto wangu mwenye wiki tatu, Kilichonifanya nikabaki bila kazi ni aliyekuwa rafiki yangu alinidhulumu haki yangu kwenye biashara tuliyoanzisha wawili ambayo tulianza kwa mtaji Wa milioni moja laki mbili mwaka Jana mwezi Wa pili, mpaka ananidhulumu ni kuibinafsisha biashara na kuifanya yake tulikuwa tushaikuza na kufikia mtaji Wa Milioni ishirini na mbili(22). Ila mwezi Wa nne alinitumia ujumbe Wa msg nikiwa nyumbani mgonjwa ya kwamba me niendelee na mambo yangu nimwachie biashara yake na nimwambie nahitaji bei gani anitumie kama haki yangu, nakwambia nilipona gafla ila ndo hivyo akaniambia ndo msimamo wake na nikizidi mfuatilia atanimaliza kwa kuondoa uhai wangu, ilibidi niitikie kinyonge na akanitumia laki nne na elfu thelathin (430000) ndo kama haki yangu, sikuweza kumjibu bali nilizidi kuchanganyikiwa na sikuweza kumshitaki kwani hatukuandikiana. Nilikaa ndani kama wiki moja nikilia tu, akatokea mtu mmoja akanishauri anipeleke kwa mtaalamu(mganga) ili afanye mambo yake niweze rudishiwa haki yangu kamili japo nilikuwa siaminigi mambo hayo na ikawa Mara ya kwanza kwenda kwa mganga wa kienyeji, ila Huyo mganga alifanya mambo yake na akaanza kuniambia huyu rafiki yako ameshaingia kwenye ushirikina tena mkubwa sana na aliupatia huko anakoagiza bidhaa, na pia anatumia nyota yangu kwenye mambo yake, Alinichaji 2000 tu na kuniambia atajaribu kupambana nae ila arudishe haki yangu japo ni ngumu kwani rafiki yangu yupo vizuri kishirikina na atakapofanikiwa kumuweza ndo nitamlipa ujira wake, nilikaa kama miezi miwili bila kuona mafanikio ikabidi nirudie huko tena na kuuliza kulikoni na alijibu ngoma ni ngumu kwani jamaa kashagundua kuwa nimegundua umafia wake nami namzunguka, akanipa dawa ya kuogea na akaniambia niwe makini kwani jamaa kazidisha vita na Mimi, ndo mwanzo nilianza kupata maswahibu makali mengi, mke wangu aliyekuwa mjanzito nae akapata matatizo makubwa ya tumbo mimba ikiwa na miezi nane, nilipambana haikusaidia ila mke wangu ni mtu Wa maombi sana hakukubali kwenda kwa mganga Wa kienyeji, mimba ilipitiliza hadi miezi 10 na nusu akiwa anateseka nami nikiwa nimefulia sina kitu, Akajifungua salama ila mtoto akulia akahamishiwa Muhimbili, nakuambia mtoto aliwekwa ICU na mashine ya oksijen wiki mbili hajitambui, Mimi na mke wangu tulichanganyikiwa sana na kukata tamaa, Siku moja ya ijumaa mtoto akanyonya gafla kwani alikuwa hawezi nyonya tukasema kapona kumbe ndo mwanzo wa kuzidiwa zaidi, Jumamosi asubu nikamfuata Daktari Wa zamu nikamuomba aniambie kama mtoto wangu atapona au ndo napoteza muda, Daktari akamuita mke wangu akatuambia hivi nyie mnasali kweli tukamuambia ndio, akatuambia hebu angalieni na mambo ya wazee huko isije kuta ndo dawa kwani tatizo la mtoto wenu halionekani, nakwambia nilitoka pale kama chizi na kwenda kuomba ushauri kwa mama mmoja, alinipa namba ya baba mmoja nikampigia nikamweleza tatizo zima akaomba jina la mke wangu ili atumie nyota yake kuangalia tatizo, me nikamuambia anisaidie kwani sitoweza kwenda kwake siku hiyo kwani nashughulika na chakula cha mzazi tutawasiliana baadae na ikiwa poa nitamuomba huyo mama anipeleke kwake kesho yake. Mchana nilipofika hospitali nilishangaa kumkuta mke wangu ana furaha sana nikamuuliza kulikoni akaniambia mtoto anaendelea vizuri na ananyonya mwenyewe na ameshatolewa ICU na kukabidhiwa. Nilienda nyumban kwa furaha ila nilipompigia yule mganga kienyeji ili anipe majibu hakupatikana. Kesho yake asubuhi Mimi na yule mama tukaenda tukamkuta, aliniambi cha kwanza Jana uliona matokeo gani? Nikamueleza akaniambia tena ilikuwa kidogo nichelewe na kupoteza uhai Wa mwanangu, akaniambia matatizo yalianzia tumboni kwa mke wangu na ilikuwa kusudio afe yeye na mtoto ila ni Mungu tu, mbaya zaidi akasema aneyefanya haya ni mtu niliyegombana nae kwenye biashara na anataka kumtoa mwanangu kafara baada ya kunishindwa Mimi, akaniambia siku hiyo hawezi fanya kazi ila kuna dawa atanipa ya kumsaidia mama mtoto ili kuua ule uchafu mwilini kwa mama. Nilipeka ile dawa kesho yake kwa mshangao tukaruhusiwa kurudi nyumbani na mtoto wetu, Nikarudia kwa yule bwana akamalizia tiba na mpaka sasa ananidai kwani nilimlipa 22000 tu, Japo mpaka sasa nipo kwenye shida kwani sina kazi ila Nina Amani mwanangu anaendelea poa. Sijui kama nilifanya kosa kwenda kwa mtaalamu ila nitakwenda Kutubu. Ila naamini uchawi upo. Na nilipanga kumfanyia jambo baya huyo rafiki yangu ila baada ha kusoma hapa nimejikuta nikisema namsamehe bure. Story ya kweli inanihusu Mimi