Simama imara ni mapito tu, usijichanganye

Simama imara ni mapito tu, usijichanganye

Mshana jr nimekuwa msomaji wa thread zako kwa muda kidogo sasa.NAOMBA JIBU SWALI HAPO JUU
 
Yaani nimekuelewa sana mkuu nina pito Moja hapa najiuliza peke yangu hivi litapita kweli but uzi wako umenifanya nipate hope some how.
 
Hivi mungu yupo??

Mshana jr nimekuwa msomaji wa thread zako kwa muda kidogo sasa.NAOMBA JIBU SWALI HAPO JUU

Mungu yupo na miungu pia ipo... Ni mada moja pana saana na imezua mijadala na tafiti nyingi sana ulimwenguni, hata hapa jukwaani tulishawahi kuwa ni mijadala ya namna hii na kila wakati inaibuka
Mungu yupo kwakuwa hata kwenye vitabu vya historia ya kidunia vinakiri uwepo wa mitume yake kama Yesu kristo na wengine, sasa huwezi kukiri uwepo wa Yesu kisha ukakataa uwepo wa Mungu
Mungu yupo kwakuwa hata hao wanaopinga uwepo wake wanakiri Maandiko yake kwenye misahafu Kama Bible, sasa unaikubali Bible lakini unakataa uwepo wa Mungu huu ni ujuha wa kiwango chake
 
Nahitaji maneno haya kwenye kipindi hiki kigumu ninachopitia.
Amen

Kuna wimbo mmoja mzuri sana wa dini usemao
Tazama wewe ni Bwana Mungu wa vyote vyenye mwili.. Je kuna gumu lolote usiloliweza...!!!
Hakika hakuna Mungu hashindwi na hajawahi kushindwa.. Alisema wazi kuwa hatatujaribu kuliko uwezo wetu, kwakuwa kuna wakati magumu tunayopitia ni kipimo tu cha imani kwake

Lakini Tukumbuke vilevile katika maisha kuwa, Mungu huwa hawahi wala hachelewi katika kujibu maombi bali hujibu katika wakati uliokubalika... Siku moja kwa Mungu ni sawa na siku elfu kwa mwanadamu

Kuna wakati tunasongwa na mambo na kudhani kuwa Mungu katuacha kabisa lakini hebu jaribu kutembelea sehemu Kama muhimbili segerea gerezani utatoka na picha tofauti.... Haya ni mapito tu jipe moyo utayashinda yana mwisho vumilia kitu kimoja cha muhimu sana Usikate tamaa
 
Yaani nimekuelewa sana mkuu nina pito Moja hapa najiuliza peke yangu hivi litapita kweli but uzi wako umenifanya nipate hope some how.

Simama imara na Mungu wako usiyumbishwe na yeyote yule wala usiogope lipe muda litapita na kuisha Kama barafu iyeyukavyo juani.. Kwani umepitia mangapi???? Hili nalo litapita
 
mkuu umenipa faraja ya kutosha nipo katika kipindi kigumu sana kwenye maisha yangu
 
mkuu umenipa faraja ya kutosha nipo katika kipindi kigumu sana kwenye maisha yangu

1443923467962.jpg kibaa si wewe pekeyako kila mmoja ana magumu yake popote pale... Hata hapa jukwaani kuna kipindi members wenzetu hutoweka kwa muda... Kumbe huko waliko wanayopitia Mungu pekee ndie ajuaye... Lakini hatimaye husimama tena na kurejea jukwaani....!!magumu unayopitia ni sehemu ya maisha yatapita, jitahidi tu kuwa imara na kusimama na Mungu tuu
 
Last edited by a moderator:
mshana you are full of logic and wisdom iko siku nitakutafuta nifanye kazi na wewe ya kuinua watu waliokata tamaa ya maisha hapa duniani,endapo Mungu atanibariki ni mwakani tu,kazi tutakayofanya itainua taifa lote na hata mataifa jirani,kwa sasa sitakuambia ni ipi.
 
Usikate tamaa, usichanganyikiwe, usipoteze tumaini ni mapito yatapita na utakuwa imara zaidi... Mungu kamwe hawezi kufunga milango yote hata siku moja... Wanasema in the darkest moment there is always a twinkle in of light to lead you through

Changamoto Zipo katika maisha na huwa unakutana na magumu kuzidi ustahimilivu wetu, inafika mahali mtu hukata tamaa na kuamua kuchukua njia za mkato mojawapo ikiwa ni kufupisha maisha yake.
Njia nyingine ni kujaribu tiba mbadala, kuacha kumtegemea Mungu na kutafuta mambo ya giza ambayo hata hivyo ni mabaya Sana na humfanya mhusika kujenga maagano ya milele na kuzimu.. Mambo ya kutolewa nuksi kusafishwa nyota, kupewa kinga na ngekewa ni maagano ambayo kila yakiisha nguvu itabidi ukakoleze tena... Hayafai Simama na Mungu wako

Kuna changamoto za ndoa na familia.. Hili jambo halina maelezo ya kueleweka kuwa kwanini huwa hivi, lakini wanandoa wengi wanepitia kipindi cha changamoto za ugomvi kutoelewana, magonjwa kipato na hata mambo kuharibika tu bila sababu ya msingi. Usijaribu kutafuta waganga wa kienyeji wataharibu badala ya kutengeneza. Kwakuwa utaingia kwenye maagano mabaya
Kumbuka kuwa mnakutana watu wawili tofauti, huu ni muungano wa kimwili, muungano wa kiroho huja na mengi sio kitu rahisi na hilo ndio huleta changamoto zote hizi... Mkiweza kupita kipindi hiki salama mtashinda zaidi ya kushinda na mtakuja imara zaidi
Nawatakia jumamosi njema

Mkuu umenitoa machozi! Asante sana.
 
mshana you are full of logic and wisdom iko siku nitakutafuta nifanye kazi na wewe ya kuinua watu waliokata tamaa ya maisha hapa duniani,endapo Mungu atanibariki ni mwakani tu,kazi tutakayofanya itainua taifa lote na hata mataifa jirani,kwa sasa sitakuambia ni ipi.

Nashukuru ndugu Kikubwa tuombeane Afya njema na uzima
 
Ubarikiwe mkuu tena mno...Moyo wangu wakuonea fahari kwenye malango ya ROHONI..Ni salam nzuri saana kwa timu yote ya kuzimu iliyopo hapa JF...bila kumsahau KIRANGA chairman mkuu.
 
Yaani nimekuelewa sana mkuu nina pito Moja hapa najiuliza peke yangu hivi litapita kweli but uzi wako umenifanya nipate hope some how.

Rafiki km ni Mkristo na msomaji wa Biblia soma Yeremia 32:27 Weka TUMAINI kwa MUNGU wa kweli kila kitu kitakuwa sawa
 
Rafiki km ni Mkristo na msomaji wa Biblia soma Yeremia 32:27 Weka TUMAINI kwa MUNGU wa kweli kila kitu kitakuwa sawa
dolevaby pls siku ingine ukiweza weka mstari kamili kuwasaidia wale wavivu wa kusoma Bible
 
Last edited by a moderator:
Barikiwa sana mshana,umenitia moyo hasa kipindi hiki nilipo ktk pito hili. Maneno yako yamenipa nguvu sana. Barikiwa.
 
Mipango yangu nimeighaili;
1.Nilikuwa nimepanga kulipa kisasi
(a)kuua
(b)kutumia watu wambake kotekote
(c)kumchizisha
Ngoja niendelee kutafakari
 
Mipango yangu nimeighaili;
1.Nilikuwa nimepanga kulipa kisasi
(a)kuua
(b)kutumia watu wambake kotekote
(c)kumchizisha
Ngoja niendelee kutafakari

Mungu akutie nguvu usifanye lolote katika hayo mwachie yeye atakulipia
 
Back
Top Bottom